FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 92,147
- 107,669
"Se non sta andando bene, chiama tua nonna." Hiyo ni methali maarufu ya Kitaliano ambayo nimepata tabu kidogo kutafuta ya Kiswahili inayofanana-nayo, sijafanikiwa kuipata. Kwa tafsiri isiyo rasmi inasema "ikiwa hakuna linalokwenda sawa, muone bibi".
Nafahamu Kitanzania ukisema "kumuona bibi" au "babu" wengi wengine huhusisha na kuwaona mabibi na mababu ili waongee na mizimu mambo yaende sawa. Wataliano kwa msemo wao huo hawamaanishi kama Watanzania, Wataliano wanamaanisha umuone bibi kwa hekima na busara zake. Labda niifananishe na methali yetu ya "uzee ni dawa".
Binafsi kama bibi, leo nimedhamiria kutoa tafakuri yangu kwenye zao la korosho na ufumbuzi wa "matatizo" ya zao hilo.
Kwanza napenda ku "declare interest" kuwa binafsi ni mdau wa korosho kwa kuwa na mikorosho, mingi tu, tiliyoirithi toka mashamba ya mabibi zetu ile mbegu ya asili ya kizamani mpaka tumejaribu kuiendeleza na kupanda ya kisasa na tunaliona tija nzuri tu.
Ushauri: Serikali ijitowe kimasomaso kuwakopesha bila riba wafanya biashara wakubwa wenye uzoefu wa viwanda kama vile akina Bakhresa na Mo kufunguwa viwanda vikubwa vya kisasa vya kubangua, kusindika na kufungasha korosho kwa kiwango cha Kimataifa na kuwasaidia kushindana na masoko ya Kimataifa.
Hiyo ni badala ya serikali kuingilia zao hilo.
Sababu kuu ni kuwa wafanya biashara hao tayari wana uzoefu mpana wa viwanda vya "food processing" na tayari wana mitaji katika nchi kadhaa za SADC na Afrika Mashariki.
Ni tafakuri tu ya FaizaFoxy .
Nafahamu Kitanzania ukisema "kumuona bibi" au "babu" wengi wengine huhusisha na kuwaona mabibi na mababu ili waongee na mizimu mambo yaende sawa. Wataliano kwa msemo wao huo hawamaanishi kama Watanzania, Wataliano wanamaanisha umuone bibi kwa hekima na busara zake. Labda niifananishe na methali yetu ya "uzee ni dawa".
Binafsi kama bibi, leo nimedhamiria kutoa tafakuri yangu kwenye zao la korosho na ufumbuzi wa "matatizo" ya zao hilo.
Kwanza napenda ku "declare interest" kuwa binafsi ni mdau wa korosho kwa kuwa na mikorosho, mingi tu, tiliyoirithi toka mashamba ya mabibi zetu ile mbegu ya asili ya kizamani mpaka tumejaribu kuiendeleza na kupanda ya kisasa na tunaliona tija nzuri tu.
Ushauri: Serikali ijitowe kimasomaso kuwakopesha bila riba wafanya biashara wakubwa wenye uzoefu wa viwanda kama vile akina Bakhresa na Mo kufunguwa viwanda vikubwa vya kisasa vya kubangua, kusindika na kufungasha korosho kwa kiwango cha Kimataifa na kuwasaidia kushindana na masoko ya Kimataifa.
Hiyo ni badala ya serikali kuingilia zao hilo.
Sababu kuu ni kuwa wafanya biashara hao tayari wana uzoefu mpana wa viwanda vya "food processing" na tayari wana mitaji katika nchi kadhaa za SADC na Afrika Mashariki.
Ni tafakuri tu ya FaizaFoxy .