GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,690
- 109,104
GENTAMYCINE nimepitapita hapa JamiiForums na kuona baadhi ya Watu (Members) wakisema kuwa waliwahi Kumsikia nadhani Msemaji au huyu Kaimu Msemaji wa Jeshi akisema (tena kwa Kutamba kabisa) Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) hili hili ambalo Wiki iliyoisha tu baadhi ya Watendaji wake (hasa hasa MP wa Lugalo Makongo) waliovalia Kininja (Kuficha Sura zao) waliwakamata Raia 74 wasio na Hatia Kawe na kwenda nao Uwanja wa Mateso, Ukatili na Kipigo Mwenge na Kuwajeruhi vibaya wakiwatuhumu Kumuua Mwenzao Afande Muna (Lt. Col) kuwa linashika nafasi / namba Sita (6) kwa Ubora duniani.
Tafadhali naomba mwenye Orodha Kamili ya Viwango vya Ubora wa Majeshi duniani anipe au atuwekee hapa ili tuhakikishe na tusithibitishe kuwa JWTZ ni la Sita ( 6 ) kwa Ubora Kiutendaji ( hasa Kivita ) Ulimwenguni ili nami GENTAMYCINE nilipongeze na nijivunie nalo.
Nitashukuru.
Soma:
- JWTZ: Jeshi letu ni kati ya Majeshi 6 Bora duniani
Tafadhali naomba mwenye Orodha Kamili ya Viwango vya Ubora wa Majeshi duniani anipe au atuwekee hapa ili tuhakikishe na tusithibitishe kuwa JWTZ ni la Sita ( 6 ) kwa Ubora Kiutendaji ( hasa Kivita ) Ulimwenguni ili nami GENTAMYCINE nilipongeze na nijivunie nalo.
Nitashukuru.
Soma:
- JWTZ: Jeshi letu ni kati ya Majeshi 6 Bora duniani