Tabora iliyodidimia inahitaji kuinuliwa...

Tabora iliyodidimia inahitaji kuinuliwa...

Duh! mji mzima daladala hazizidi nne! Kwa hiyo ajali nyingi ni za baiskeli,pikipiki,punda na mikokoteni?!
 
Sikonge umeona comments za Jamaa yetu Mjegwa? baada ya kutembelea kwetu, cha kushangaza hajasifia uoto wa asili hii ni pamoja na kimvuli vya miembe katika barabara kuu zote hasa ile inayoenda station, ngome kuu zamani, ofisi za mkoa hadi kitete hospital.

Ni kweli wananchi wa Tabora hawana utamaduni wa kupanda daladala sababu vitongoji vyake vipo jirani sana, kwa hiyo huhitaji kupanda gari kwa mfano toka Mjini kwenda kitete, kanyenye, ng'ambo, Tambukareli huhitaji daladala -- hata mie nikenda likizo natembea tu sababu kwanza hakuna joto kama hapa kwenu Dar. Hoja ya Umaskini na udhaifu wa kubuni miradi ya maendeleo isihusihwe na hili na kutembea kwa miguu na matumizi ya baskeli - huu ni utamaduni tu wa mkoa wetu kama ilivyo Tanga.

Ni kweli hali ya uchumi inazidi kudidimia hasa baada ya Reli ya kati kufa kifo kibaya, wengi tulisikitika kwani ndiyo ilirahisisha kukuza uchumi ukizingatia Tabora ilikuwa kiungo cha usafiri wa Reli toka Kigoma, Mwanza hadi Dar.

Pia kumbukani Tabora haijaunganishwa na mikoa mingine ambayo imepakana nayo kwa njia ya barabara, hii pia inachangia mkoa ukose nguvu ya kiuchumi na biashara kwa wakazi wa Tabora kuwa ndoto ya mchana. Kwa mfano Tabora ingeweza kuunganishwa na Mbeya, Kigoma via Mpanda (Kwa waziri Mkuu wetu), Nzega (Wilaya ambayo ina nguvu ya uchumi sababu ya madini na pia barabara kuu ya Dar Mwanza inapitia hapo), Siginda via Itigi na ile ya Tabara Kahama, Geita hadi mwanza, kama mnavyojua Kahama ni mji wenye madini na kilimo hasa cha mpunga na mahindi.

Mbali na kilimo cha zao la Tumbaku na Uvunaji wa mbao aina na Mninga kwa wingi zaidi Tanzania, Ikumbukwe pia Mkoa wa Tabora ni mkoa pekee unaotoa zao na Asali na Nta ambayo ina soko kubwa sana nchi ya arabuni na ulaya, kama kweli serikali ingelifufua kiwanda cha nyuki ili kuwafanya wananchi wa mkoa huu ambao 80% ni wakulima wadogo wadogo na wale wavunaji wa asali basi ingesaidia sana kukuza uchumi wa mkoa huu.

Mwandishi kapita Tabara mjini tu, lakini ningemshauri kama angekuwa na nafasi angesafiri katika wilaya ndani ya mkoa huu kuona fursa nyingi tu ambazo kama kweli tungezitilia mkazo kama Taifa basi zingeweza kuongeza pato la taifa na pia kuwafanya wenyeji wa Tabora kunyenyuka ki-uchumi.

Kwa kuanza ningeomba sana mwandishi tuwasiliane ili tuanze kulifanyika kazi hili la Zao la Asali - nina uhakika ni Tabora pekee inatoa Mamillion ya lita ila zinaishia mikononi kwa kina MO na wengine wenye mitaji wanaowalalia wananchi wa mkoa huu.

Pia viwanda vingi vinatakiwa kufufuliwa -- nakumbuka vichache tu ambavyo vimekufa kifo cha mende kama kiwanda cha nyuzi na SIDO ambapo vijana waliweza kupata ajira miaka hiyo. Pia kufufua vyuo ambavyo vimekufa au kama vipo basi ni mahututi kama chuo cha Nyuki; chuo cha ardhi; Reli na hata kile chuo cha kihistoria cha Uhazil.

Mwisho natoa wito kwa wasomi na wazawa wa Tabora ambao ni wengi sana wapo katika taasisi za elimu ya juu, waangalie ni namna gani wanaweza kusaidia kukuza uchumi wa mkoa wao wakisaidiana na sisi wazawa wengine tulioko huku, maana wengi kaka zangu wameloea huko pwani na kaskazini hawataki kurudi kabisa kusaidia mipango ya maendeleo katika sehemu walizotoka hasa katika sekta za kilimo, elimu na ufugaji ambazo ndizo pekee za kumkomboa mwananchi wa kipato cha chini kabisa

Mkuu lakini mimi nadhani Tabora inakaribia kufunguka kwa kuwa kuna hiyo miradi ya kuwekea lami barabara za kuingia na kutoka mkoa wa tabora (angalia post ya FF). Pia Tabora itakuwa kiungo muhimu kati ya Mpanda (Mbuga ya Katavi) na mikoa mingine. Jitahidini tu mhakikishe barabara ya Tabora - Ipole - Mpanda inawekewa lami pamoja na ile ya Tabora - Ipole- Rungwa - Mbeya.

Kuhusu asali nasikia wazungu siku hizi hawaipendi sana asali ya Tabora na Mpanda kwa kuwa inakuwa na vimelea vya nicotine. Naambiwa hiyo inatokana na kwamba nyuki huwa wanachavusha maua ya tumbaku na kwenda kutengenezea asali. Tumbaku ina nicotine hivyo asali itokanayo na na maua ya Tumbaku huwa ina nicotine. Ni afadhali Tabora ikaachana na kilimo cha tumbaku ili ijiimarishe kwenye asali kwa kuwa huenda sigara (tumbaku) ikapigwa marufuku kama bangi!

Kila la kheri Tabora.
 
04.jpg

Na huu ndio uwanja wa mpira wa mji ambao mbunge wake anadai mpira uko kwenye damu yake!.... Unafiki mkubwa.
 
Tabora ni ngome ya CCM, na CCM lazima iwe na ngome mahala palipojaa wajinga ( Tabora ) na kama hiyo haitoshi hata Ubunge wamempa Msomali wakati Watanzania wenzao wapo. hii ni mijtu ya hovyo kweli kweli!!

haya mambo ya usomali ya nini jamani?,kwani kuni mtu kajipangia kuzaliwa alivyozaliwa,unatuita wajinga mbona ilala kwenye kila kitu wamempa zungu?,hebu tuachieni mwenyekiti wetu wa simba jamani

 
Mkuu lakini mimi nadhani Tabora inakaribia kufunguka kwa kuwa kuna hiyo miradi ya kuwekea lami barabara za kuingia na kutoka mkoa wa tabora (angalia post ya FF). Pia Tabora itakuwa kiungo muhimu kati ya Mpanda (Mbuga ya Katavi) na mikoa mingine. Jitahidini tu mhakikishe barabara ya Tabora - Ipole - Mpanda inawekewa lami pamoja na ile ya Tabora - Ipole- Rungwa - Mbeya.

Kuhusu asali nasikia wazungu siku hizi hawaipendi sana asali ya Tabora na Mpanda kwa kuwa inakuwa na vimelea vya nicotine. Naambiwa hiyo inatokana na kwamba nyuki huwa wanachavusha maua ya tumbaku na kwenda kutengenezea asali. Tumbaku ina nicotine hivyo asali itokanayo na na maua ya Tumbaku huwa ina nicotine. Ni afadhali Tabora ikaachana na kilimo cha tumbaku ili ijiimarishe kwenye asali kwa kuwa huenda sigara (tumbaku) ikapigwa marufuku kama bangi!

Kila la kheri Tabora.

Asante mkuu karibu ujipatie MATOBOLWA NA NSANSA ZA NTWILI

 
Asante mkuu karibu ujipatie MATOBOLWA NA NSANSA ZA NTWILI

Mkuu nashukuru. Nilikuwa nimeenda kufanya uwindaji wa kitalii huko kwenye hifadhi ya Rungwa nikapita pale Sikonge nikapata hiyo chakula!

Nilisahau ya kwamba huko Tabora kuna mapori mengi ya hifadhi ya akiba pia kuna uwindaji kama nilioenda kuufanya.
 
Thanks FF najua umecopy na kupaste kwenye site fulani ama wewe unafanya wizara ya magufuri, ukweli ni kwamba kuna kambi zimejengwa njia ya kwenda urambo nadhani mpaka sasa ni takribani zaidi ya mwaka mmoja lakini sijaona kitu cha maana kilichofanyika pale zaidi ya idadi kubwa ya NYOKA na MIJUSI kupungua kutokana na idadi kubwa ya wachina waliopo kambini, Ninasubiri tarehe ya kukamilisha ujenzi huo..................................

Njia sahihi ya kuendelea kutawala watu walio na uelewa kidogo ni kuendelea kuwa MATUMAINI kwamba kesho au kesho kutwa hali itakuwa bora zaidi. Fikiria daraja limekuwa gumzo kwa muda wa miaka mingapi? (miaka 30). Umemsikia mkuu wa kaya akiwaaambia watu wa Kimara waendelee kununua magari kwani flyovers zinakuja pale Ubungo, Mwenge, TAZARA n.k. Umeona chochote kinachoendelea?

Hii ndiyo dhana wanayotumia watawala wetu, " To continue ruling keep them hoping while doing nothing".
 
View attachment 46152

Na huu ndio uwanja wa mpira wa mji ambao mbunge wake anadai mpira uko kwenye damu yake!.... Unafiki mkubwa.

Mkuu huo uwanja siyo wa CCM kweli? Niliwahi kuutembelea huo uwanja. structural drawings zake ni nzuri sana. Ni uwanja wa mpira kweli kwa kuwa siyo kama viwanja vyetu hivi ambayo vina maeneo ya kufanyia mashindano ya riadha. Katika uwanja huu ukikaa eneo lolote unawaona wachezaji vizuri sana. Tatizo uwanja haukuisha. Tafuteni mwekezaji aumalizie.
 
Jamani barabara za mkoa wetu wa Tabora zinatisha. Mpaka sasa hakuna barabara hata moja yenye rami ambayo inaingia mkoa wa Tabora. Chama changu cha Chadema mko wapi? Waamsheni wananchi wa Tabora kwani ni waelewa. Siku zote wanyamwezi na wasukuma ukiwaelimisha wakaelewa watakuunga mkono. Chadema nendeni Tabora kwani waanzilishi wa vyama hakina Fundikira, Mapalala na Kasela Bantu wote walikuwa ni wenyeji wa Tabora.
Wana JF muwe huru kuchangia kwenye thread ili mkoa wa Tabora uweze kuinuliwa. Kwasababu wanasiasa wenye maamuzi nao wanatembelea mtandao wetu wa JF. Nahisi kuna kitu kitafanyika.

Jamani mimi ni wa huko lakini mjadala huu hauna vigezo wala viashilia kuonyesha Tabora imedidimia mbali na kutoa hisia zetu. Faiza amejaribu kuonesha facts na wengine tuoneshe facts. kama ni barabara tulinganishe na mikoa mingine, kama ni regional GDP tulinganishe na mikoa mingine, kama ni mchango wake kwenye national GDP tulinganishe na mikoa mingine, n.k. Kwa kifupi tuwe na variables na indicators ambazo zitaonyesha kuwa kabla ulikuwa juu na sasa huko chini pia in comparison with other regions with similar comparative advantages!!! Otherwise na sisi tutakuwa tunajadili kama tuko pale kwa fundi viatu Manzese darajani!!!!!!

Kwa msaada soma kwanza Tabora region: socio-economic profile 2005 available at NBS library.
 
Jamani mimi ni wa huko lakini mjadala huu hauna vigezo wala viashilia kuonyesha Tabora imedidimia mbali na kutoa hisia zetu. Faiza amejaribu kuonesha facts na wengine tuoneshe facts. kama ni barabara tulinganishe na mikoa mingine, kama ni regional GDP tulinganishe na mikoa mingine, kama ni mchango wake kwenye national GDP tulinganishe na mikoa mingine, n.k. Kwa kifupi tuwe na variables na indicators ambazo zitaonyesha kuwa kabla ulikuwa juu na sasa huko chini pia in comparison with other regions with similar comparative advantages!!! Otherwise na sisi tutakuwa tunajadili kama tuko pale kwa fundi viatu Manzese darajani!!!!!!

Kwa msaada soma kwanza Tabora region: socio-economic profile 2005 available at NBS library.

Mkuu mbona unatunyanyapaa?
 
Kutwa nzima wanakunywa kahawa,kucheza bao,draft.wataendelea saa ngapi?hawa hawapishani na wazaramo!

Umejuaje? Kinachonifurahisha kwa hawa wanyamwezi wa Tabora ni kuwa na jambo moja only ambalo ni unform kwao si kwa watoto, vijana, wazee, au hata wale unaowaona machoni kwako kuwa ni vikongwe lakini ni balaa, jambo hilo wao ni jadi na lipo ndani ya damu bila kujali umri, wapi, lakini zaidi zaidi inapoingia giza Tabora ya mchana huwa si ile ya kagiza kanapoingia, utaona kama kumbi kumbi vile from no where wametapakaa kila kona ushindwe weye, Tabora ni mji wa kipato kidogo hivyo wewe Maggid kama kamchezo kale unakapenda sijui kama utarudi salama, kuanzia buku mpaka msimbazi tosha kabisa, si mtoto si mama si kikongwe ni balaa wote wanashindana nani kafungasha zigo kubwa na hapo ni wewe tu kwa raha zako, ukitaka kuthibitisha usiku nenda pale Orion Hotel au kwa sie tusio na uwezo wa kufika Tabora basi angalia tabia hizo toka kwa viongozi wanaotoka Tabora (maisha ya ndani) eg Kapuya mzee wa Ngwasuma au Mr 6 wote hao ni "formula one" kama walioko Tabora
 
Nafikiri Wa Tz mnahitaji mfikirie nje ya Box.

Hakuna hata chama kimoja chenye kuweza kuwajengea barabara wote ni walaji tu na waroho wa madaraka na uchu wa kutaka uongozi..
be careful. Heri mshike mlichonacho kwani kinauma na kupuliza kuliko kufikiria mbadala.

Kila la kheir.
 
Umejuaje? Kinachonifurahisha kwa hawa wanyamwezi wa Tabora ni kuwa na jambo moja only ambalo ni unform kwao si kwa watoto, vijana, wazee, au hata wale unaowaona machoni kwako kuwa ni vikongwe lakini ni balaa, jambo hilo wao ni jadi na lipo ndani ya damu bila kujali umri, wapi, lakini zaidi zaidi inapoingia giza Tabora ya mchana huwa si ile ya kagiza kanapoingia, utaona kama kumbi kumbi vile from no where wametapakaa kila kona ushindwe weye, Tabora ni mji wa kipato kidogo hivyo wewe Maggid kama kamchezo kale unakapenda sijui kama utarudi salama, kuanzia buku mpaka msimbazi tosha kabisa, si mtoto si mama si kikongwe ni balaa wote wanashindana nani kafungasha zigo kubwa na hapo ni wewe tu kwa raha zako, ukitaka kuthibitisha usiku nenda pale Orion Hotel au kwa sie tusio na uwezo wa kufika Tabora basi angalia tabia hizo toka kwa viongozi wanaotoka Tabora (maisha ya ndani) eg Kapuya mzee wa Ngwasuma au Mr 6 wote hao ni "formula one" kama walioko Tabora

Ako kamchezo also nakalike! leo tunajadili kuutoa mkoa
 
Mkuu kkitabu, unachokisema si kwa mkoa wa Tabora tu bali tatizo hili lipo ktk maeneo mengi sana ya hii nchi yetu ya Tanzania. Sababu kubwa ya hayo yote ni kutokuwepo kwa viongozi wenye nia ya dhati ya kuleta maendeleo ktk nchi hii, viongozi wetu waliowengi UBINAFSI & UMIMI au KWANGU KWANZA umetawala mioyoni mwao kitu ambacho kinapelekea kutokuwepo kwa mgawanyo linganifu wa rasilimali za nchi hii! Kinachotakiwa ni sisi wananchi wote kuwa na FIKIRA HURU na hasa ktk kufanya maamuzi!
 
kwa hiyo ulitaka ajenge kama wa taifa?,hebu tupe picha uwanja wa mpira wa karatu,bagamoyo,pemba na moshi mjini


Hizo sehemu ulizotaja hazina wabunge wenye mpira ndani ya damu yao.
Si lazima ajenge kama uwanja wa taifa. Kuripea hilo paa la jukwaa na kuhamasisha ukataji wa nyasi, sidhani kama inagharimu pesa nyingi. Point is ... Uwanja wa mpira umefikia kufanana na maeneo ya makaburini..!!! Lahaula...!!
 
Umejuaje? Kinachonifurahisha kwa hawa wanyamwezi wa Tabora ni kuwa na jambo moja only ambalo ni unform kwao si kwa watoto, vijana, wazee, au hata wale unaowaona machoni kwako kuwa ni vikongwe lakini ni balaa, jambo hilo wao ni jadi na lipo ndani ya damu bila kujali umri, wapi, lakini zaidi zaidi inapoingia giza Tabora ya mchana huwa si ile ya kagiza kanapoingia, utaona kama kumbi kumbi vile from no where wametapakaa kila kona ushindwe weye, Tabora ni mji wa kipato kidogo hivyo wewe Maggid kama kamchezo kale unakapenda sijui kama utarudi salama, kuanzia buku mpaka msimbazi tosha kabisa, si mtoto si mama si kikongwe ni balaa wote wanashindana nani kafungasha zigo kubwa na hapo ni wewe tu kwa raha zako, ukitaka kuthibitisha usiku nenda pale Orion Hotel au kwa sie tusio na uwezo wa kufika Tabora basi angalia tabia hizo toka kwa viongozi wanaotoka Tabora (maisha ya ndani) eg Kapuya mzee wa Ngwasuma au Mr 6 wote hao ni "formula one" kama walioko Tabora
Hii topic sasa imeamua kututukana,hivyo vimichezo ni vya kila mahara,sehemu gani hakuna?
Dar?,Arusha? au wapi ?,tafuta hata records wapi wanaongoza uone,tabora hatupo kabisa


 
Wapanga du, ni dada yako lkn! I am glad umeamua kitu cha maana; there is a lot to do in Tabora. Wasomi wengi wameukimbia mji, waliobaki ni waswahili tu unategemea nini?
mhanya kaunga na figher , kwapela igembe kwenuko?sasa mukova kusuve hangi? ila mwenugu nago muhayo wakutega hivanza leki kugeme! !!! guys pale mto wala way to sikonge hapafai kuanzisha shamba kubwa la kilimo cha mpunga kwa umwagiliaji just to set an example to others!!! basi tunaweza kuanza na hilo kwanza huku tukijadili hilo la kilimo cha maembe ya miaka mitano maana ardhi Tabora ni ya kumwaga.

Tabora for change --2015.
 
Unajua uzuri Tabora nayo ni sehemu ya Tanzania kwa maana hiyo ni ndani ya nchi yangu na kama nasema naipenda nchi yangu namaanisha naipenda Tabora pia

Sasa mie huu unakatika mwaka wa 3 niko hapa Tabora na baadhi naweza kuyasema ijapo Sikonge atasema mie siyo mzawa hivyo siyajuhi matatizo yao,ni kweli lakini ukikaa na watu unajaribu kudadisi na wao watakwambia tu,kwahiyo kuna mengine nimeyaona na kuna mengine nimeambiwa na wazawa wenyewe kwa kukiri

Tatizo kubwa linalowasumbua hawa wenzetu kusema kweli ni makuzi (malezi),kuna dalili za wazi kwamba vijana wengi wazawa wa hapa si shapu kujituma katika kufanya kazi,wanalala sana,wanapenda sana kamari,wanapenda sana vijiwe na kunywa kahawa

Nilipojaribu kulifuatilia hili nilimpata kijana mmoja akanambia tatizo ni wazee wa mjini pale Tabora,hawana kazi ila wanawatumia vijana kwenda kuiba na kisha kuleta hela kwa mabwana wao na hii inafanyika usiku alafu ikifika asubuhi kutwa nzima utakuta vijana hawa na wazee wako wanacheza bao na kunywa kahawa,mtu anatoka kwenda kula ama msikitini kisha anarudi baoni

Kwa hiyo kikubwa mkiweza kubadili haya makuzi ya vijana wenu naamini kabisa mtakuwa mmeweza kupiga hatua kubwa,naamini uvivu,umwinyi na kushinda vibarazani vitakwisha,pelekeni elimu sana kwa watu wa huko make pia bado kuna kasumba kama za pwani za kufikiria elimu ya madrasa ndo kila kitu na ile ya dunia inaonekana kana kwamba ni subsidiary kitu ambacho kinapelekea watoto wanaingia kwenye ndoa hata bado wakiwa shule ya msingi..niishie hapa ila tatueni matatizo yenu kwani hawatakuja watu wa kuwasaidia kama nyinyi mtaonekana bado mmelala.

Mkitaka mkoa wenu utoke hapa ulipo jaribuni kuwakomboa vijana wapende kujituma kufanya kazi make ndo nguvu kazi lakini kuendelea kuuza kahawa vijana badala ya kuenyesha miili yao wao wanauza kahawa ili ikupeleke wapi?wakomboe vijana wenu,sasa kama aliyemaliza bachelor anarudi kuimba kwaya vipi huyu wa fm6 na fm4 si watauza kahawa daima?
 
mhanya kaunga na figher , kwapela igembe kwenuko?sasa mukova kusuve hangi? ila mwenugu nago muhayo wakutega hivanza leki kugeme! !!! guys pale mto wala way to sikonge hapafai kuanzisha shamba kubwa la kilimo cha mpunga kwa umwagiliaji just to set an example to others!!! basi tunaweza kuanza na hilo kwanza huku tukijadili hilo la kilimo cha maembe ya miaka mitano maana ardhi Tabora ni ya kumwaga.

Tabora for change --2015.

Magambo genago Mhanya!! leka tugeme!
 
Back
Top Bottom