Tabora iliyodidimia inahitaji kuinuliwa...

Tabora iliyodidimia inahitaji kuinuliwa...

Nenda kamanda tupo nawe kwenye mapambano ya kuukomboa mkoa wetu wa tbr.. Inasikitisha sana, mkoa wenye historia lukuki, haujaunganishwa na lami kwenda mkoa wowote ule, maji tatizo, nenda kamanda...
 
Viva kaka ila mimi na bukene tu liwalo na liwe ccm mmekwisha tena naenda kuwapoteza
 
Nenda kamanda tupo nawe kwenye mapambano ya kuukomboa mkoa wetu wa tbr.. Inasikitisha sana, mkoa wenye historia lukuki, haujaunganishwa na lami kwenda mkoa wowote ule, maji tatizo, nenda kamanda...
Asante mkuu, nitakwenda haraka, nitakwenda na sintarudi nyuma, nitakaa na Tabora yangu niiliwaza na kuisaidia, nitakwenda kwa uchungu, na kama wenyeji wasiponielewa basi nitazusha ugomvi mkubwa, haiwezekani watu wanapigika halafu wajifanye hawana shida, sasa ukombozi ni lazima kwa Tabora, wapende wasipende, ninaikomboa Tabora yangu sio chama cha siasa.

Nakuja huko, mtake msitake nitawakomboa tu, nimechoka kuwaona malofa siku zote.

Pangu Pakavu
 
Mkuu umenena vema. Vijana wa tbr tuamke tuukomboe mkoa wetu. Tabora ilikuwa city center ya kanda ya magharibu lakin sasa imekwisha KIGOMA na SHY zinazidi kung'ara dawa ni kuweka ccm kando kama kigoma basi. Sasa na mimi natangaza nia SIKONGE. Nkumba jiandae kuachia jimbo.It is time 4change 2tabora peoples.
 
jamani sijui wenzangu kama mmepata kung'amua kitu hiki mkoa wa Tabora ni kama vile umekufa kwa jinsi nionavyo mimi licha ya wakazi wake kuwa na chakula pengine cha kutosha lakini miaka nenda rudi nikipita hapo sioni mabadiliko utafikiri vile hakuna wazawa waliokwenda shule mpaka leo mbavu za mbwa ziko katika mji tatizo liko wapi?
-kwa wazawa wenyewe?
-serikali?
kwa kuwa kama ni viongozi waliosoma na kuwepo katika sytem hii ya serikali wapo tangu kitambo mbona kunadorola yaani huwa napata maswali mengi kichwani?
hebu nisaidiane hasa ninyi wazawa wa tabora na wenye kuufahamu vizuri unastahili kuwa kama ilivyo? ukizingatia kuwa ni mkoa wa kihistoria katika harakati za uhuru wa nchi hii.
hayo ni malipo mazuri ya CCM.Mikoa mingi ambayo CCM imejikita sana na wadau wengi ni wa CCM wako nyuma sana kielimu na kiuchumi na pia huduma za jamii ni duni sana
 
Ifikie wakati sasa hata kipofu alazimishwe kuona mwezi, kiziwi asikie hata kwa viboko. Hivi wana tabora ukiziwi huu na kutokujifanya hatuoni madhira yanayowapata Watanzania tunaupata wapi. Kifupi, kama ingebidi kutoa shamba darasa la siasa basi huu mkoa wangu huu program ingetakiwa kuchukua hata karne. Inamaana wana Tabora hatuoni mizigo tuliyoipeleka Bungeni na hivyo kuwabebesha gunia la misumari watanzania wa Arusha na maeneo mengine yenye mwamko na kujitambua. Angalia Prof. Kapuya, toka bunge limeanza hata kukohoa tuu hamna, Sumari wa Uyui akisimama, ujue speech yote ni kusifia serikali kwa kuimalisha uchumi wa nchi. Tusizungumzie kina Said Nkumba na Kina Rage, hakuna kitu kabisa. Ni wakati sasa tutambue kuwa siyo kila badiliko lazima lianzie Arusha, hata Sisi tunaweza. Laana hii mpaka lini?. Hebu tujitahidi basi, chondechonde wasomi na wanaharakati wa Mkoa huu, 2015 uwe mwanzo wa CCM kuwa wapinzani ktk Mkoa wa Tabora. Tushirikiane kutema sumu kwa wenzetu na hatimaye kutengeneza sura mpya ya mkoa huu, M4C
 
Mbona sauti za wabunge wenu zinasikika! Lakini ni zile za ndiyoooooo! bila kusahau zomea zomea
 
jamani sijui wenzangu kama mmepata kung'amua kitu hiki mkoa wa Tabora ni kama vile umekufa kwa jinsi nionavyo mimi licha ya wakazi wake kuwa na chakula pengine cha kutosha lakini miaka nenda rudi nikipita hapo sioni mabadiliko utafikiri vile hakuna wazawa waliokwenda shule mpaka leo mbavu za mbwa ziko katika mji tatizo liko wapi?
-kwa wazawa wenyewe?
-serikali?
kwa kuwa kama ni viongozi waliosoma na kuwepo katika sytem hii ya serikali wapo tangu kitambo mbona kunadorola yaani huwa napata maswali mengi kichwani?
hebu nisaidiane hasa ninyi wazawa wa tabora na wenye kuufahamu vizuri unastahili kuwa kama ilivyo? ukizingatia kuwa ni mkoa wa kihistoria katika harakati za uhuru wa nchi hii.


Kwanza nikupe HONGERA kwa Mada nzuri uliyotuwekea Mezani...
HONGERA SANA,,ila nasikitishwa na hawa wenzangu na mimi ambao bila kutaja jina la mtu au mbunge flani au chama flani ... Mada hiyo kwao haijakuwa ya Kisiasa..

Tabora ni mkoa kama mikoa mingine tu katika Tanzania yetu masikini(najua wengi hamtaki hili neno ingawa ndo ukweli wa mambo)...
Maendeleo ya Taifa/sehemu yoyote utegemea mambo mbalimbali ikiwemo WATU WA JAMII USIKA..

Umezungumzia matatizo kadha wa kadha ya Tabora... Hakika yapo yanayoweza kutatuliwa na Serikali na mengine ni watu wa Eneo husika....

Wewe umesikia wapi katika miaka 10 iliyopita, nchi imewajengea wananchi makazi bora bila ya kuwa na tatizo la msingi kama ilivyotokea KENYA kwa wakazi wa KIBELA...

Ni ngumu sana ndugu yangu kumlazimisha mtu kulala ndani ya chandarua kabla ya kujua umuhimu wake,, mim nasema swala la makazi boro,,yani nyumba nzuri katika miji ya mikoa mingine ni Juhudi tu za wananchi wa Eneo husika na si vinginevyo..!!

Hakuna mkoa ambao wananch wake waliwai pewa ruzuku ya kujengea...
Hvyo ELIMU ya umuhimu wa makazi bora ni lazima itolewe kwa wanaTABORA na watu wajue umuhimu wake..
Naskia mtu anasema "sasa hyo si kazi ya Serikali"
Ndiyo lakini yapo mashirika Mengi yanayojitolea kutoa Elimu kama hzi katikati ya Jamii,,mkisubiri Serikali mpaka Itengee bajeti swala hilo,, mtasubiri sana na mpaka hzo nyumba zitawabomokea...!!

Wito wangu ni kwamba wananchi wa Tabora amkeni na mkatae kukaa kwenye vijumba vibovu kwa kujenga nyumba za Kisasa...!
Swala la Barabara nadhani niwaachie wenzangu waendelee..
 
Tabora utatalii nini? Matoborwa?

Dhahabu yenyewe wanauza akina Junius kwa kuipeleka Uarabuni.

Na kesho wanadai hawataki Muungano.......

Ngoja tubaki tu tunajilia ugali wa Nsansa na kuichagua CCM yetu. Kesho tunaamkia Kihembe ........
U
Umenikumbusha mbali sana uliposema Nsansa tena uipate ile ya karanga.

Hakika kuna mengi sana sana kuhusu Tabora ambayo yamekuwa kichocheo kikubwa sana cha kudumaa kimaendeleo. Lakin msingi mkubwa ni kukosekana na njia nzuri hususam miundombinu ya barabara kuingia na kuziunganisha wilaya zake kama sikonge, usoke, urambo,nzega na mjini.
Lakin vile vile kusuasua kwa Reli nako kumechangia sana kudumaza uchumi wa Tabora.

Lakin kubwa nchi ya Tz haijaweza kipa kipaumbele katika maendeleo Tabora ambako ndiko chimbuko karibu la mashujaa na hata Uzawa wa Tanu achilia CCM.

Inahitajika nguvu za ziada zitumike kuokoa tabora kiuchumi. Bila usafiri wa uhakika basi hakuna maendeleo. Bila nishati ya umeme ya uhakika vile vile hakuna maendeleo.

Wabeja sana

 
Huyu Rage msomali ali shabab ni lazima tumchomoe, jama wana kiloleni, ng'ambo, isevya, mwinyi, ipuli, mihogoni, cheo, itaga, tumbi, milambo nk plz tuamkeni jamni toka usingizni ili 2015 tufanye kweli kwa kuileta CDM hapo.

Mimi nanavyojua Rage ndie aliyeleta Town buses pale mjini kuunganisha na maeneo mengine. Ana mengi sana mazuri ambayo anapanga na ameanza kuyafanya pale town.
sijasema lolote kuhusu Radio n.k
Ameunganisha wote walio nje na ndani ya TZ wenye hata chembe ya asli ya tabora na kuna mwamko mzuri sana.

Tuombe mungu na kuzidi kuisisitiza Serikali itupie kwa jicho la tatu katika kurekebisha miundombinu ya barabara na maji kwa wananchi.

Tumpe hongera Rage.

 
TB waswahili wengi. waswahili=maendeleo duni..wale wanaofanya bidii katika kilimo kama karanga, tumbaku, asali nk nafikiri wanaangushwa na wenzao wa mjini ambao ingebidi wawe ni soko lao la kwanza au kiungo cha soko lao nchini kote, sasa wanaacha wageni wanakuja kuchuma na kuacha mji vile vile utafikiri enzi za Nyerere anafundisha Tb boys.

serikali nayo inachangia kwa kuua taratibu reli ya kati na kutounganisha miundo mbinu mingine sawia ambayo ingewafanya wale wanaojituma kujitoa kwa kilimo kwa kuunganishwa kirahisi na soko la bidhaa zao katika maeneo mengine ya miji mikubwa.
 
TB waswahili wengi. waswahili=maendeleo duni..wale wanaofanya bidii katika kilimo kama karanga, tumbaku, asali nk nafikiri wanaangushwa na wenzao wa mjini ambao ingebidi wawe ni soko lao la kwanza au kiungo cha soko lao nchini kote, sasa wanaacha wageni wanakuja kuchuma na kuacha mji vile vile utafikiri enzi za Nyerere anafundisha Tb boys.

serikali nayo inachangia kwa kuua taratibu reli ya kati na kutounganisha miundo mbinu mingine sawia ambayo ingewafanya wale wanaojituma kujitoa kwa kilimo kwa kuunganishwa kirahisi na soko la bidhaa zao katika maeneo mengine ya miji mikubwa.

Nilipo RED.

Unaposema waswahili ni nani?

Kwangu mie wote wenye ngozi nyeusi na nywele ngumu na wanaoongea na kutumia kiswhili kama lugha yao ya mawasiliano ndio WASWAHILI.

Sijue mwenzangu unasemaje?
 
Nilipo RED.

Unaposema waswahili ni nani?

Kwangu mie wote wenye ngozi nyeusi na nywele ngumu na wanaoongea na kutumia kiswhili kama lugha yao ya mawasiliano ndio WASWAHILI.

Sijue mwenzangu unasemaje?

uswahili ni tamaduni, na tamaduni iliyopo maeneo mengi yaliyokaliwa na waarabu na ,au yaliyofanya sana biashara na waarabu. Hawa hata lugha yao kuu ni kiswahili na hata kama wana lugha yao nyingine ina maneno ya kiswahili zaidi ya 50% mfano hawa wadengereko na waunguja. wote hupenda kunywa kahawa vijiweni, kucheza bao, kuoa wake wengi, kutojishughulisha sana na kilimo kama ndiyo shughuli kuu ya kimaisha hata kama wana ardhi kubwa watakuja kuiza, kile kidogo wanachokipata huchezea ngoma na shughuli nyingine kama hizo (wakwere, wazalamo na wadengereko), wengi huwa ni waumini wa mdhehebu ya kiislamu, na elimu rasmi huwa hawaoni sana kama ina tija, ila elimu ya dini ina umuhimu kwanza.
waswahili wengi wanapatikana maeneo kama Tabora, (mjini), Kigoma, (haswa ujiji), Tanga, Visiwani kote, Pwani, Lindi na Mtwara (haswa mjini) pamoja na kwamba hawa mahusiano yao na wageni wa kiarabu moja kwa moja yalikua ni madogo bado walipata ushawishi wa tamaduni hii toka kwa majirani zao wa Pwani

NB; siyo waislamu wote ni waswahili kuna waislamu wengi wanajishughulisha na kilimo na ni wafanya kazi wazuri sana pale Tabora vijijini, ila waswahili wengi ni waislamu (nahisi ungetaka nifafanue hili)
 
uswahili ni tamaduni, na tamaduni iliyopo maeneo mengi yaliyokaliwa na waarabu na ,au yaliyofanya sana biashara na waarabu. Hawa hata lugha yao kuu ni kiswahili na hata kama wana lugha yao nyingine ina maneno ya kiswahili zaidi ya 50% mfano hawa wadengereko na waunguja. wote hupenda kunywa kahawa vijiweni, kucheza bao, kuoa wake wengi, kutojishughulisha sana na kilimo kama ndiyo shughuli kuu ya kimaisha hata kama wana ardhi kubwa watakuja kuiza, kile kidogo wanachokipata huchezea ngoma na shughuli nyingine kama hizo (wakwere, wazalamo na wadengereko), wengi huwa ni waumini wa mdhehebu ya kiislamu, na elimu rasmi huwa hawaoni sana kama ina tija, ila elimu ya dini ina umuhimu kwanza.
waswahili wengi wanapatikana maeneo kama Tabora, (mjini), Kigoma, (haswa ujiji), Tanga, Visiwani kote, Pwani, Lindi na Mtwara (haswa mjini) pamoja na kwamba hawa mahusiano yao na wageni wa kiarabu moja kwa moja yalikua ni madogo bado walipata ushawishi wa tamaduni hii toka kwa majirani zao wa Pwani

NB; siyo waislamu wote ni waswahili kuna waislamu wengi wanajishughulisha na kilimo na ni wafanya kazi wazuri sana pale Tabora vijijini, ila waswahili wengi ni waislamu (nahisi ungetaka nifafanue hili)

Naona ahali yangu hapa umechanganya mambo mengi sana yaani umechanganya Imani, Kabira na Muonekano (mweusi, mweupe (kwa maana mbantu na mwarabu).Na kuzungumza mambo ambayo hayana tija katika maendeleo ya uchumi wa nchi yenu

Mimi sipendi kujikita katika hayo. Labda nilitaka tu kukuuliza kwanini kabla ya uhuru wenu huko Tanganyika, Sehemu hizo ulizozitaja zilikuwa juu sana kiuchumi na kimaendeleo kulinganisha na sehemu ambazo sasa zimeendelea. Sehemu hizo ndizo zilikuwa maarufu katika biashara mbalimbali na watu wake walikuwa wastaharabu sana na walijua hata namna ya kuvaa vizuri na kula vizuri ukilinganisha na sehemu zingine. Mkoloni aliliona hilo sasa jiulize kwanini limepotea na kuwa sehemu duni baada ya nchi yenu kupata uhuru wake. Je kulikoni.

Nafikiri ukitafakari kwa kina utaliona hilo. Kama kweli uko makini na unatazama maendeleo kwa mantiki ya kukuza uchumi nafikiri utagundua haiingii akilini hata kidogo mkoa wa Tanga au Mtwara kuwa na uchumi duni ukilinganisha na kilimanjaro, arusha au Mwanza. Jiulize mbona Mombasa ipo juu mpaka leo huko Kenya?

Mimi kwa mtazamo wangu kuna mengi ya kufikirika na kutafakari na sio mawazo kama yako. Tabora ina wasomi wengi sana tena waliobobea sana na kushika nafasi mbalimbali za uongozi toka dahali na dahali ukianzia na akina Chief Fundikira na wengine.

Kwa vile bibi yangu mzaa mama yangu Mzazi alikuwa mkaazi wa sikonge na hivyo nina ndugu wengi huko. Napenda kusema Serikali yenu iliisahau Tabora na mikoa ya kusini kwa kutoimarisha miundombinu ya reli na barabara na nishati ya umeme ili kuleta tija kubwa katika uwekezaji wa viwanda na biashara na kuinua hali za maisha ya watu wake kwa labda madhumuni maalum ima kwa kuamini mawazo kama yako.


Binafsi kama mchumi nasema kama Serikali ya Tanganyika ingewekeza sawa sawa kwa mikoa yake yote basi msingekuwa masikini kwa kiwango cha sasa. Kumbuka kusini kunalipa sana kuna Gas, bandari nzuri, vivutio vya wanyama na ardhi nzuri ya kilimo cha mazao ya chakula na biashara kama ufuta, korosho n.k.

Lakin la mwisho nilitaka nikudokeze ni kuwa Uchumi wa Tanganyika umemebwa sana na watu wenye asili ya kiarabu ambao ndio wafanyabiashara wakubwa. Pitia sekta zote kuanzia nishati ya mafuta, Transportation, viwanda na uwekezaji wa kati na mkubwa katika sekta zote na nyanja zote za kiuchumi. Chunguza hilo kisha kama ni mwenye kifikiri basi utanipa jibu kuwa ni kweli au Lah.

Kumbuka baguzi mbaya sana na Mola anawahukumu kwa hilo kiuchumi.
 
hivi ule uchaguzi wa juzijuzi wakagawiwa mahindi kwenye vibaba ilikuwa mkoa huu au mkoa gani? nyie mlioelimika na kutoka tongotongo mkawafundishe wenzenu vijijini. tatizo mkija mjini hamtaki kurudi kwenu. Mikoa yote yenye maendeleo yanaletwa na wenyeji wanaotoka kutafuta then wanarudi ndani kuinvest na kuwahabarisha jamii ilobaki pale, kujenga, mabadiliko ya kisiasa. Mnatutusha mzigo mkubwa sana nyie watu wa tbr, lindi mtwara etc kazi kuoa kila mavuno aagggh!!
 
mhanya kaunga na figher , kwapela igembe kwenuko?sasa mukova kusuve hangi? ila mwenugu nago muhayo wakutega hivanza leki kugeme! !!! guys pale mto wala way to sikonge hapafai kuanzisha shamba kubwa la kilimo cha mpunga kwa umwagiliaji just to set an example to others!!! basi tunaweza kuanza na hilo kwanza huku tukijadili hilo la kilimo cha maembe ya miaka mitano maana ardhi Tabora ni ya kumwaga.

Tabora for change --2015.

Yaga vakakuloge! Ila ni wazo zuri.
 
Yaga vakakuloge! Ila ni wazo zuri.

Hayo ni mawazo duni na yamepitwa na wakti . Mbona Rage hajarogwa kwa kuanzisha town bus na kufungua biashara nyingi nyingi pale town na viunga vyake vyote.

Zindukeni kiakili kuimarisha uchumi wenu.
 
Naona ahali yangu hapa umechanganya mambo mengi sana yaani umechanganya Imani, Kabira na Muonekano (mweusi, mweupe (kwa maana mbantu na mwarabu).Na kuzungumza mambo ambayo hayana tija katika maendeleo ya uchumi wa nchi yenu

Mimi sipendi kujikita katika hayo. Labda nilitaka tu kukuuliza kwanini kabla ya uhuru wenu huko Tanganyika, Sehemu hizo ulizozitaja zilikuwa juu sana kiuchumi na kimaendeleo kulinganisha na sehemu ambazo sasa zimeendelea. Sehemu hizo ndizo zilikuwa maarufu katika biashara mbalimbali na watu wake walikuwa wastaharabu sana na walijua hata namna ya kuvaa vizuri na kula vizuri ukilinganisha na sehemu zingine. Mkoloni aliliona hilo sasa jiulize kwanini limepotea na kuwa sehemu duni baada ya nchi yenu kupata uhuru wake. Je kulikoni.

Nafikiri ukitafakari kwa kina utaliona hilo. Kama kweli uko makini na unatazama maendeleo kwa mantiki ya kukuza uchumi nafikiri utagundua haiingii akilini hata kidogo mkoa wa Tanga au Mtwara kuwa na uchumi duni ukilinganisha na kilimanjaro, arusha au Mwanza. Jiulize mbona Mombasa ipo juu mpaka leo huko Kenya?

Mimi kwa mtazamo wangu kuna mengi ya kufikirika na kutafakari na sio mawazo kama yako. Tabora ina wasomi wengi sana tena waliobobea sana na kushika nafasi mbalimbali za uongozi toka dahali na dahali ukianzia na akina Chief Fundikira na wengine.

Kwa vile bibi yangu mzaa mama yangu Mzazi alikuwa mkaazi wa sikonge na hivyo nina ndugu wengi huko. Napenda kusema Serikali yenu iliisahau Tabora na mikoa ya kusini kwa kutoimarisha miundombinu ya reli na barabara na nishati ya umeme ili kuleta tija kubwa katika uwekezaji wa viwanda na biashara na kuinua hali za maisha ya watu wake kwa labda madhumuni maalum ima kwa kuamini mawazo kama yako.


Binafsi kama mchumi nasema kama Serikali ya Tanganyika ingewekeza sawa sawa kwa mikoa yake yote basi msingekuwa masikini kwa kiwango cha sasa. Kumbuka kusini kunalipa sana kuna Gas, bandari nzuri, vivutio vya wanyama na ardhi nzuri ya kilimo cha mazao ya chakula na biashara kama ufuta, korosho n.k.

Lakin la mwisho nilitaka nikudokeze ni kuwa Uchumi wa Tanganyika umemebwa sana na watu wenye asili ya kiarabu ambao ndio wafanyabiashara wakubwa. Pitia sekta zote kuanzia nishati ya mafuta, Transportation, viwanda na uwekezaji wa kati na mkubwa katika sekta zote na nyanja zote za kiuchumi. Chunguza hilo kisha kama ni mwenye kifikiri basi utanipa jibu kuwa ni kweli au Lah.

Kumbuka baguzi mbaya sana na Mola anawahukumu kwa hilo kiuchumi.

Kaka kwa heshima zote, ukisoma reply yangu kwenye main topic nilitaja haya mambo uliyaoyasema kuwa ni moja wapo ya mambo yaliyochangia kudumaa kwa maendeleo ya Tabora haswa pale mjini. Haya ya miundo mbinu. niliwahi kufanya utafiti kule wa kilimo cha tumbaku..watu wanafanya sana kazi wale, sema mvua zinawaangusha muda mwingine, na kibaya zaidi ni sera za serikali za kilimo kuwa wauzaji wako wengi na hawana haki na kile wanachokizalisha, wanatakiwa wauze kwa watu fulani fulani tu waliohalalishwa na serikali, kama vile karafuu kule znz mnunuzi ni mmoja..sasa hapo unawanyima hawa haki yao ya kutafuta mununuzi kwa bei nzuri ya muda huo ya soko...changamoto ni nyingi, ila waswahili wanachangia kutudai maendeleo yao kwa sababu wao kila kitu kimepangwa na mola.

Angalia Tanga barabara kuu imepita pale kuelekea Kaskazini na Kenya, ile barabara ingepita Ruvuma ungeona Ruvuma iko wapi muda huu,
 
Mombasa iko juu kwa sababu mombasa ni mji wa bandari yaani tuseme kama vile Dar imeendelea kila mtu anawekeza hapa (pamoja na kujaa waswahili), hata kama mji mkuu na mkubwa kuliko yote ungekua ni Dodoma, bado dar ingekua kwa kiasi fulani kwa sababu ya bandari kuu na hiyo inavutia mitaji na watu toka sehemu mbali mbali za nchi na nje ya nchi..vile vile Tanga, Mtwara, Ujiji serikali ingewekeza katika kupanua na kuongeza bandari zile pale, maendeleo yangekuja kwa sababu sisi wengine tusiokua waswahili tungewekeza huko au kuhamia kufanya kazi na biashara, ila waswahili kama kawaida yao wangeuza viwanja na kuhamia pembezoni mwa mji.
 
Back
Top Bottom