Tabora iliyodidimia inahitaji kuinuliwa...

Sikonge umeona comments za Jamaa yetu Mjegwa? baada ya kutembelea kwetu, cha kushangaza hajasifia uoto wa asili hii ni pamoja na kimvuli vya miembe katika barabara kuu zote hasa ile inayoenda station, ngome kuu zamani, ofisi za mkoa hadi kitete hospital.

Ni kweli wananchi wa Tabora hawana utamaduni wa kupanda daladala sababu vitongoji vyake vipo jirani sana, kwa hiyo huhitaji kupanda gari kwa mfano toka Mjini kwenda kitete, kanyenye, ng'ambo, Tambukareli huhitaji daladala -- hata mie nikenda likizo natembea tu sababu kwanza hakuna joto kama hapa kwenu Dar. Hoja ya Umaskini na udhaifu wa kubuni miradi ya maendeleo isihusihwe na hili na kutembea kwa miguu na matumizi ya baskeli - huu ni utamaduni tu wa mkoa wetu kama ilivyo Tanga.

Ni kweli hali ya uchumi inazidi kudidimia hasa baada ya Reli ya kati kufa kifo kibaya, wengi tulisikitika kwani ndiyo ilirahisisha kukuza uchumi ukizingatia Tabora ilikuwa kiungo cha usafiri wa Reli toka Kigoma, Mwanza hadi Dar.

Pia kumbukani Tabora haijaunganishwa na mikoa mingine ambayo imepakana nayo kwa njia ya barabara, hii pia inachangia mkoa ukose nguvu ya kiuchumi na biashara kwa wakazi wa Tabora kuwa ndoto ya mchana. Kwa mfano Tabora ingeweza kuunganishwa na Mbeya, Kigoma via Mpanda (Kwa waziri Mkuu wetu), Nzega (Wilaya ambayo ina nguvu ya uchumi sababu ya madini na pia barabara kuu ya Dar Mwanza inapitia hapo), Siginda via Itigi na ile ya Tabara Kahama, Geita hadi mwanza, kama mnavyojua Kahama ni mji wenye madini na kilimo hasa cha mpunga na mahindi.

Mbali na kilimo cha zao la Tumbaku na Uvunaji wa mbao aina na Mninga kwa wingi zaidi Tanzania, Ikumbukwe pia Mkoa wa Tabora ni mkoa pekee unaotoa zao na Asali na Nta ambayo ina soko kubwa sana nchi ya arabuni na ulaya, kama kweli serikali ingelifufua kiwanda cha nyuki ili kuwafanya wananchi wa mkoa huu ambao 80% ni wakulima wadogo wadogo na wale wavunaji wa asali basi ingesaidia sana kukuza uchumi wa mkoa huu.

Mwandishi kapita Tabara mjini tu, lakini ningemshauri kama angekuwa na nafasi angesafiri katika wilaya ndani ya mkoa huu kuona fursa nyingi tu ambazo kama kweli tungezitilia mkazo kama Taifa basi zingeweza kuongeza pato la taifa na pia kuwafanya wenyeji wa Tabora kunyenyuka ki-uchumi.

Kwa kuanza ningeomba sana mwandishi tuwasiliane ili tuanze kulifanyika kazi hili la Zao la Asali - nina uhakika ni Tabora pekee inatoa Mamillion ya lita ila zinaishia mikononi kwa kina MO na wengine wenye mitaji wanaowalalia wananchi wa mkoa huu.

Pia viwanda vingi vinatakiwa kufufuliwa -- nakumbuka vichache tu ambavyo vimekufa kifo cha mende kama kiwanda cha nyuzi na SIDO ambapo vijana waliweza kupata ajira miaka hiyo. Pia kufufua vyuo ambavyo vimekufa au kama vipo basi ni mahututi kama chuo cha Nyuki; chuo cha ardhi; Reli na hata kile chuo cha kihistoria cha Uhazil.

Mwisho natoa wito kwa wasomi na wazawa wa Tabora ambao ni wengi sana wapo katika taasisi za elimu ya juu, waangalie ni namna gani wanaweza kusaidia kukuza uchumi wa mkoa wao wakisaidiana na sisi wazawa wengine tulioko huku, maana wengi kaka zangu wameloea huko pwani na kaskazini hawataki kurudi kabisa kusaidia mipango ya maendeleo katika sehemu walizotoka hasa katika sekta za kilimo, elimu na ufugaji ambazo ndizo pekee za kumkomboa mwananchi wa kipato cha chini kabisa
 
Sijakuelewa, una chuki na Maggid au.................
Hope amesema anachoona yeye na si aseme unachotaka wewe.


Wewe ndo una chuki na humtakii mema!!!nimesoma makala zake na blog yake kila siku iendayo kwa Mungu unless kuna udhuru lazima niipitie!!!nina zaid ya miaka 5 nasoma makala zake tangu RAI mpaka magazeti yote anayaandikia hapa na pale makala!ndugu yangu hujui dhana ya kukosoa(kupingana) bila kupigana.

Na kam ungekuwa na philosophy ndogo tu ya akili za watu ungegundua si mtu wa concern za watu!!MUDA WOTE NAMUONA YUPO HAPA HAJAJIBU,UNAJUA KUSUDI LAKE?

HAKIKA BINADAMU NI KIUMBE CHA PEKEE!!!!
 
Ndugu zangu,

Leo nimetembea kwa miguu kutoka mahali nilipofikia maeneo ya Ali Hassan Mwinyi Stadium hadi Chuo Cha Ualimu kunakofanyika mafunzo ya wanahabari. Umbali wa kilomita mbili hivi. Nimetembea nikiongea na wenyeji ambao wengi wanatembea kwa miguu. Kuna niliyojifunza njiani. Tabora si mji wa daladala, hazizidi nne mji mzima.

Baiskeli na pikipiki ndio daladala za Tabora Mjini. Na moja kubwa linalochangia Tabora kubaki nyuma ni miundo mbinu mibovu ikiwamo barabara na ukosefu wa usafiri wa uhakika wa treni umechangia kurudisha nyuma maendeleo ya Tabora.

Na lingine ni attitude ya umwinyi ya baadhi ya watu wa Tabora Mjini. Jana nimezunguka sana kutafuta vocha ya simu, naambiwa kuna wenyeji ambao hawataki kufanya biashara ya vocha ambayo faida yake yaweza kuwa shilingi elfu nne kwa vocha za laki moja! Tabora inahitaji muingiliano zaidi na watu wa mengine. Miundo mbinu itawezesha hilo.


Naam, Tabora iliyodidimia inahitaji kuinuliwa, na wenye jukumu la kwanza la kuifanya kazi hiyo ni Wana-Tabora wenyewe.
Maggid Mjengwa,
Tabora, Januari, 26, 2012
Mjengwa Blog::Habari,Picha,Matangazo
Tembelea pia; Tabora & Singida Press Clubs
CCM hoyeeeeee....! teh teh teh.
 
Ni kweli Tabora yaitaji spesho atensheni.

ILA UKWELI UNABAKI PALE PALE .........
1.ccm imekuwa ikielekeza maendeleo kwenye maeneo/majimbo/mikoa yenye mchanganyiko wa siasa.
2.Ikiwa Tabora wanataka kukumbukwa ni lazima waamke kisiasa (sio lazma wawachague wabunge wa upinzani) kwa kupunguza idadi ya kura wanazoimwagia CCM

my take:KAMA UNAPATA MAZIWA BURE YANINI UJISUMBUE KUFUGA NG'OMBE i.e kama ccm inapata maelfu ya kura bure tabora yanini iwaonge/iwalainishe wanainchi maendeleo??

Tabora ni zaidi ya pemba ambako kuna CUF since 1995,sijaona mantiki ya majimbo na ccm,vitu vingine mtawaonea bure wabunge wetu, huko kwetu,ilifika kipindi tuna waziri wa ulinzi,spika wa bunge na waziri wa elimu katika jimbo moja,sidhani kama ni vyepesi kupata bahati hiyo,sema sisi wanyamwezi ni umwinyi tu kama kaka maggid alivyosema,tunaweza kunywa kahawa tu,tuwekewe pesa mifukoni labda ,hata tuongozwe nani bado itakuwa vile vile tu
 
Tabora ni zaidi ya pemba ambako kuna CUF since 1995,sijaona mantiki ya majimbo na ccm,vitu vingine mtawaonea bure wabunge wetu, huko kwetu,ilifika kipindi tuna waziri wa ulinzi,spika wa bunge na waziri wa elimu katika jimbo moja,sidhani kama ni vyepesi kupata bahati hiyo,sema sisi wanyamwezi ni umwinyi tu kama kaka maggid alivyosema,tunaweza kunywa kahawa tu,tuwekewe pesa mifukoni labda ,hata tuongozwe nani bado itakuwa vile vile tu

wilaya moja
 
Jamani barabara za mkoa wetu wa Tabora zinatisha. Mpaka sasa hakuna barabara hata moja yenye rami ambayo inaingia mkoa wa Tabora. Chama changu cha Chadema mko wapi? Waamsheni wananchi wa Tabora kwani ni waelewa. Siku zote wanyamwezi na wasukuma ukiwaelimisha wakaelewa watakuunga mkono. Chadema nendeni Tabora kwani waanzilishi wa vyama hakina Fundikira, Mapalala na Kasela Bantu wote walikuwa ni wenyeji wa Tabora.
Wana JF muwe huru kuchangia kwenye thread ili mkoa wa Tabora uweze kuinuliwa. Kwasababu wanasiasa wenye maamuzi nao wanatembelea mtandao wetu wa JF. Nahisi kuna kitu kitafanyika.

kumbe barabara za lami zinazoingia mikoani zote zimewekwa na sisi,Big up Chadema
 
Elnino,
Asante sana.

Muda huu niko kwenye darasa la mafunzo kwa wanahabari wa Singida na Tabora. Inahusu Online Journalism. Nao wanafuatilia mjadala huu. Kuna wanaojifunza. Na miye pia najifunza mengi. Ahsanteni sana.

Maggid
,
Tabora Mjini

Sikonge umeona comments za Jamaa yetu Mjegwa? baada ya kutembelea kwetu, cha kushangaza hajasifia uoto wa asili hii ni pamoja na kimvuli vya miembe katika barabara kuu zote hasa ile inayoenda station, ngome kuu hadi kitete hospital.

Ni kweli wananchi wa Tabora hawana utamaduni wa kupanda daladala sababu vitongoji vyake vipo jirani sana, kwa hiyo huhitaji kupanda gari kwa mfano toka Mjini kwenda kitete, ng'ambo, Tambukareli huhitaji daladala -- hata mie nikenda likizo natembea tu sababu kwanza hakuna joto kama hapa kwenu Dar. Hoja ya Umaskini na udhaifu wa kubuni miradi ya maendeleo isihusihwe na hili na kutembea kwa miguu na matumizi ya baskeli - huu ni utamaduni tu wa mkoa wetu kama ilivyo Tanga.

Ni kweli hali ya uchumi inazidi kudidimia hasa baada ya Reli ya kati kufa kifo kibaya, wengi tulisikitika kwani ndiyo ilirahisisha kukuza uchumi ukizingatia Tabora ilikuwa kiungo cha usafiri wa Reli toka Kigoma, Mwanza hadi Dar.

Pia kumbuka Tabora haijaunganishwa na mikoa mingine ambayo imepakana nayo kwa njia ya barabara, hii pia inachangia mkoa ukose nguvu ya kiuchumi na biashara kwa wakazi wa Tabora kuwa ndoto ya mchana. Kwa mfano Tabora ingeweza kuunganishwa na Mbeya, Kigoma via Mpanda (Kwa waziri Mkuu wetu), Nzega (Wilaya ambayo ina nguvu ya uchumi sababu ya madini na pia barabara kuu ya Dar Mwanza inapitia hapo), Siginda via Itigi na ile ya Tabara Kahama, Geita hadi mwanza, kama mnavyojua Kahama ni mji wenye madini na kilimo hasa cha mpunga na mahindi.

Ikumbukwe pia Mkoa wa Tabora ni mkoa pekee unaotoa zao na Asali na Nta ambayo ina soko kubwa sana nchi ya arabuni na ulaya, kama kweli serikali ingelifufua kiwanda cha nyuki ili kuwafanya wananchi wa mkoa huu ambao 80% ni wakulima wadogo wadogo na wale wavunaji wa asali basi ingesaidia sana kukuza uchumi wa mkoa huu.

Mwandishi kapita Tabara mjini tu, lakini ningemshauri kama angekuwa na nafasi angesafiri katika kila wilaya kuona vitu gani ambayo kama kweli tungevitilia mkazo kama taifa vingeweza kuongeza pato la taifa na kuwafanya wenyeji wa Tabora kunyenyuka ki uchumi.

Kwa kuanza ningeomba sana mwandishi tuwasiliane ili tuanze kulifanyika kazi hili la Zao la Asali - nina uhakika ni Tabora pekee inatoa Mamillion ya lita ila zinaishia mikononi kwa kina MO na wengine wenye mitaji wanaowalalia wananchi wa mkoa huu.

Pia viwanda vingi vinatakiwa kufufuliwa -- nakumbuka vichache tu ambavyo vimekufa kifo cha mende kama kiwanda cha nyuzi na SIDO ambapo vijana waliweza kupata ajira miaka hiyo. Pia kufufua vyuo ambavyo vimekufa au kama vipo basi ni mahututi kama chuo cha Nyuki; Reli na hata kile chuo cha kihistoria cha Uhazil.

Mwisho natoa wito kwa wasomi na wazawa wa Tabora ambao ni wengi sana wapo katika taasisi za elimu ya juu, waangalie ni namna gani wanaweza kusaidia kukuza uchumi wa mkoa wao wakisaidiana na sisi wazawa wengine tulioko huku, maana wengi kaka zangu wameloea huko pwani na kaskazini hawataki kurudi kabisa kusaidia mipango ya maendeleo katika sehemu walizotoka hasa katika sekta za kilimo, elimu na ufugaji ambazo ndizo pekee za kumkomboa mwananchi wa kipato cha chini kabisa.
 
Tabora ni zaidi ya pemba ambako kuna CUF since 1995,sijaona mantiki ya majimbo na ccm,vitu vingine mtawaonea bure wabunge wetu, huko kwetu,ilifika kipindi tuna waziri wa ulinzi,spika wa bunge na waziri wa elimu katika jimbo moja,sidhani kama ni vyepesi kupata bahati hiyo,sema sisi wanyamwezi ni umwinyi tu kama kaka maggid alivyosema,tunaweza kunywa kahawa tu,tuwekewe pesa mifukoni labda ,hata tuongozwe nani bado itakuwa vile vile tu
tatizo la pemba ni full CUF tena bila hoja bali chuki dhidi ya unyerere
ingetakiwa pemba uwepo mchanganyiko wa CCM na CUF hapo ungeona maendeleo
 
Elnino,
Asante sana.

Muda huu niko kwenye darasa la mafunzo kwa wanahabari wa Singida na Tabora. Inahusu Online Journalism. Nao wanafuatilia mjadala huu. Kuna wanaojifunza. Na miye pia najifunza mengi. Ahsanteni sana.

Maggid
,
Tabora Mjini

Pia jifunze kuwa Tabora hawawezi endelea kwa kuongozwa na kiongozi mwizi wa mipira na jezi za FAT, Kitu kingine ambacho kinadumaza maendeleo yao ni kwamba wanyamwezi ni wanafiki na wabinafsi sana ktk jamii inayowazunguka, angalia Kapuya alivyokuwa waziri wa Ulinzi alivyokuwa anafuja Ndege za jeshi kwenda Tabora kula nchi na vijidada vya home kwao, angalia Six alivyotolea nje Richmond, Meremeta, Tangold etc lakini hivi sasa eti anajiita mpambanaji...to hell
 
Ngoja mwenyekiti wetu wa wekundu akusikie. Atakupeleka mahakamani, ooohhh
 
Na Mbunge nae ni tatizo kwa Tabora inayodidimia ambayo inahitaji kuinuliwa. Wanyamwezi ni watani zangu, ninadhubutu kuwaambia kwamba kichwani mwao wamebebe bweha na wala siyo akili, kweli wangekuwa na akili wangemchagua Aden Rage kuwa Mbunge wao? Hebu nyie wanyamwezi msiokuwa na akili niwarudisha nyuma kidogo, kabla ya kumpa mtu madaraka ya kukuongoza au kukufanyia jambo fulani inabidi kwanza uangalie background yake.

Kwa mfano' Jeshi la Israel chini ya kamanda wao LT.COL Jonathan Netashahu waliomba kwenda Entebe Kijeshi kuwaokoa mateka wa ki.Esrael waliokuwa wamehifadhiwa huko huko enzi za utawala wa Idd Amin mwaka 1976. Bunge la Israel (knesset ) halikukubali ombi hilo kichwa kichwa waliwauliza kwanza waeleze waliisha fanikiwa mission ngapi kama hizo huko nyuma? kabla ya ombi lao hilo? Jibu lilikuwa rahisi sana , shirika lao la ujasusi (MOSSAD) ambalo wote ni wanajeshi walijinasibu:-
1. Waliiiba RADA ya kirusi huko Bagdad wakaipeleke Kwao Israel wakaisomaaaaa kiundani na kisha kuirudisha Bagdad bila warabu kujua.
2. Waliangusha jengo la makao makuu ya PFLP huko Bairut Lebanon jengo la gorofa sita kwa dakika chache sana kidogo na Carlos Jambazi anaswe ndani. N.K
Ndipo Bunge la Israel likawaruhusu haya nendeni mkafanye kazi hiyo, kilichotokea ulimwengu wote ulishuhudia, nakumbuka tarehe 4 July redio na TV zote duniani zilizungumzia tukio hilo tu la ki-historia.

Sasa nyie Wanyamwezi mlipompa Ubunge Rage mlikuwa mnafahamu background yake?
Ngoja niwasaidieni- MTU HUYU RAGE:-
1. Mwaka 1883 aiwa kwetu Dodoma kama muajiliwa wa CDA yeye na maafisa wenzake tisa walifukuzwa kazi na Nyerere kwa ubadhirifu japokwa yeye alikuwa stationed DSM kama clearing anf forwading Officer.
2. Miaka ya theminini au tisini akiwa ni katibu mkuu wa DRFA mafanikio aliyopata ni ugomvi tu na serikali wakigombea uwanja wa Kerume
3. Miaka iliyofuata akawa katibu mkuu wa Klabu ya Simba , mafanikio aliyopata ni Simba kutaka kushuka daraja shukrani kwa Yanga kukubali kufungwa 2 kwa 1.
3. Mtu huyu Rage akawa katibu mkuu wa FAT, mafanikio;
a. Ugomvi na serikali
b. kuzaliwa kwa sheria ya 18 ya FIFA,timu ya nyumbani lazima ishinde.
sheria hii ikapelekea Mpira wa Bongo ukashuka kabisa, kabisa hadi
Mzee Mwinyi kuiita timu ya Taifa kichwa cha mwenda wazimu.
C. Akitokea FAT alikuja huko Tabora kugombea Ubunge mwaka 1995
kwenye kura za maoni Rage aliongoza kwa kura nyingi lakini Kamati
kuu na Nyerere akiwepo walikata jina lake asubuhi subuhi kwa sababu
waliona Randlover 109 ikigawa ruswa akatuhumiwa mgombea aliyeku
wa anapenyeza mlungula ni yeye Rage( Usicheze na Nyerere);
D. Baadae akafungwa kwa wizi japokuwa aliweza kukata rufaa na baa
dae kutoka kwa rufaa hiyo akiwa teyari kamaliza kifungo.
Sasa mtu mwenye background kama hiyo ndo kweli wa kumpa dhamana ya Ubunge ili awe chachu ya maendeleo? Hamjifunzi kwa Israel tu? Halafu nyie wanayamwezi hivi unavyofuga fisi unategemea fisi huyo atatembelewa na swala? kama siyo fisi wenzake? Basi jitayarisheni kuvamiwa na Ma ELSHABABU. Kwa hili Tabora ididimie ife kabisa Mbwa nyie.

Blayi wa Mpwapwa.
 
Duh...Mboka Tabora...sio siri Tabora inahitaji mwamko...WANYA MOON ..acheni kulala..Nimesoma Tabora Boys ninaujua vzuri...pipo za Tabora ni kama wapwani..kutwa taarabu kazi hawataki ...
 
Wanyamweziiii! Pigeni kazi acheni soga, jifunzeni ka watanzania wenye asili ya kenya (wachaga)
 
Na Mbunge nae ni tatizo kwa Tabora inayodidimia ambayo inahitaji kuinuliwa. Wanyamwezi ni watani zangu, ninadhubutu kuwaambia kwamba kichwani mwao wamebebe bweha na wala siyo akili, kweli wangekuwa na akili wangemchagua Aden Rage kuwa Mbunge wao? Hebu nyie wanyamwezi msiokuwa na akili niwarudisha nyuma kidogo, kabla ya kumpa mtu madaraka ya kukuongoza au kukufanyia jambo fulani inabidi kwanza uangalie background yake.

Sasa mtu mwenye background kama hiyo ndo kweli wa kumpa dhamana ya Ubunge ili awe chachu ya maendeleo? Hamjifunzi kwa Israel tu? Halafu nyie wanayamwezi hivi unavyofuga fisi unategemea fisi huyo atatembelewa na swala? kama siyo fisi wenzake? Basi jitayarisheni kuvamiwa na Ma ELSHABABU. Kwa hili Tabora ididimie ife kabisa Mbwa nyie.

Blayi wa Mpwapwa.
kaka kama una ugomvi na Rage mtafute mmalizane naye si kuwatukana wanyawezi hata kama ni utani sasa huo wako umepita kiasi.

Wewe unajua jinsi uchaguzi wa CCM ulivyo; hata kama hutaki huyo mbunge wanaomtaka wao atakuwa tu; kwa hili kaka tunaomba utuombe radhi please na ufute kauli zako.
 
Na Mbunge nae ni tatizo kwa Tabora inayodidimia ambayo inahitaji kuinuliwa. Wanyamwezi ni watani zangu, ninadhubutu kuwaambia kwamba kichwani mwao wamebebe bweha na wala siyo akili, kweli wangekuwa na akili wangemchagua Aden Rage kuwa Mbunge wao? Hebu nyie wanyamwezi msiokuwa na akili niwarudisha nyuma kidogo, kabla ya kumpa mtu madaraka ya kukuongoza au kukufanyia jambo fulani inabidi kwanza uangalie background yake.

Kwa mfano' Jeshi la Israel chini ya kamanda wao LT.COL Jonathan Netashahu waliomba kwenda Entebe Kijeshi kuwaokoa mateka wa ki.Esrael waliokuwa wamehifadhiwa huko huko enzi za utawala wa Idd Amin mwaka 1976. Bunge la Israel (knesset ) halikukubali ombi hilo kichwa kichwa waliwauliza kwanza waeleze waliisha fanikiwa mission ngapi kama hizo huko nyuma? kabla ya ombi lao hilo? Jibu lilikuwa rahisi sana , shirika lao la ujasusi (MOSSAD) ambalo wote ni wanajeshi walijinasibu:-
1. Waliiiba RADA ya kirusi huko Bagdad wakaipeleke Kwao Israel wakaisomaaaaa kiundani na kisha kuirudisha Bagdad bila warabu kujua.
2. Waliangusha jengo la makao makuu ya PFLP huko Bairut Lebanon jengo la gorofa sita kwa dakika chache sana kidogo na Carlos Jambazi anaswe ndani. N.K
Ndipo Bunge la Israel likawaruhusu haya nendeni mkafanye kazi hiyo, kilichotokea ulimwengu wote ulishuhudia, nakumbuka tarehe 4 July redio na TV zote duniani zilizungumzia tukio hilo tu la ki-historia.

Sasa nyie Wanyamwezi mlipompa Ubunge Rage mlikuwa mnafahamu background yake?
Ngoja niwasaidieni- MTU HUYU RAGE:-
1. Mwaka 1883 aiwa kwetu Dodoma kama muajiliwa wa CDA yeye na maafisa wenzake tisa walifukuzwa kazi na Nyerere kwa ubadhirifu japokwa yeye alikuwa stationed DSM kama clearing anf forwading Officer.
2. Miaka ya theminini au tisini akiwa ni katibu mkuu wa DRFA mafanikio aliyopata ni ugomvi tu na serikali wakigombea uwanja wa Kerume
3. Miaka iliyofuata akawa katibu mkuu wa Klabu ya Simba , mafanikio aliyopata ni Simba kutaka kushuka daraja shukrani kwa Yanga kukubali kufungwa 2 kwa 1.
3. Mtu huyu Rage akawa katibu mkuu wa FAT, mafanikio;
a. Ugomvi na serikali
b. kuzaliwa kwa sheria ya 18 ya FIFA,timu ya nyumbani lazima ishinde.
sheria hii ikapelekea Mpira wa Bongo ukashuka kabisa, kabisa hadi
Mzee Mwinyi kuiita timu ya Taifa kichwa cha mwenda wazimu.
C. Akitokea FAT alikuja huko Tabora kugombea Ubunge mwaka 1995
kwenye kura za maoni Rage aliongoza kwa kura nyingi lakini Kamati
kuu na Nyerere akiwepo walikata jina lake asubuhi subuhi kwa sababu
waliona Randlover 109 ikigawa ruswa akatuhumiwa mgombea aliyeku
wa anapenyeza mlungula ni yeye Rage( Usicheze na Nyerere);
D. Baadae akafungwa kwa wizi japokuwa aliweza kukata rufaa na baa
dae kutoka kwa rufaa hiyo akiwa teyari kamaliza kifungo.
Sasa mtu mwenye background kama hiyo ndo kweli wa kumpa dhamana ya Ubunge ili awe chachu ya maendeleo? Hamjifunzi kwa Israel tu? Halafu nyie wanayamwezi hivi unavyofuga fisi unategemea fisi huyo atatembelewa na swala? kama siyo fisi wenzake? Basi jitayarisheni kuvamiwa na Ma ELSHABABU. Kwa hili Tabora ididimie ife kabisa Mbwa nyie.

Blayi wa Mpwapwa.

hata babake hajazaliwa,usituite mbwa tafadhari
 
Inasikitisha sana kwani mimi nilipita Dec 2011, kutoka Tabora mjini mpaka Urambo kwenye maziko. hakika hali ni mbaya sana.

 
Kwanza kabisa mtani MBWA MWENYEWE!!Mkoa wa Tabora tatizo lake kubwa ni kusahauliwa na serikali sikubaliani hata kidogo na nyie mnaosema tunaendekeza umwinyi hatutaki kufanyakazi wakati hata wakolono walikuwa wanachukuwa watumwa na manamba wa Nyanyembe Empire kuwafanyia kazi na mpaka ule usemi maarufu wa mzigo mzito mpe MNYAMWEZI ukuibuka!Wanyamwezi niwachapakazi sana lakini serikali ndiyo inatuangusha,serikali imekuwa unaudharau sana mkoa wa Tabora tangu enzi za nyerere tena bila kujali yule mzee pamoja na kusoma Tabora boys(Tabora school ) na baadae kufundisha Milambo Secondary zote za tabora laikni aliupa kisogo sana mkoa wetu!Tangu kipindi hicho Tumbaku ilikuwa ikilimwa kwa wingi Tabora lakini kiwanda kikajengwa morogoro!Mpaka leo hii huwezi amini Tabora hakuna lami tu ya kuunganisha wilaya moja na nyingine achilia mbali mkoa kama ndugu yangu ELNINO alivyosema hapo juu!Kijiografia njia fupi ya kusafirishia bidhaa zinazokwenda nchi jirani za Rwanda,Kongo DRC na burundi ni ile inayopita manyoni-itigi-tura-tabora-urambo mpaka kigoma laokini barabara hiyo ni vumbi mpaka leo!Mikoa tunayoiita ghala la chakula la taifa ya Rukwa na Kigoma mazao yao yatoke kwa urahisi kwenda mikoano ni lazima yapitie Tabora badala ya kuzungukia Mbeya!Achilia mbali mkoa wenyewe tu kuwa na resources nyingine nyingi kama Asali na mengineyo lakini hivi vitu vinatokaje wakati watu tupo kisiwani.Reli imashajifia,mabasi mvua ikinyesha imakula kwenu,ndege imerudi juzi tu Air Tz lakini gharama zake mkulima gani wa tumbaku ata-afford?Iambieni serikali yenu itufungulie mipaka muone kama hatupendi kufanyakazi sio mnalaumu tu kama mnatumia MASABURI!
Suala la kutembea kwa mguu kaka Mjengwa wala lisikuumize kchwa,Tabora mjini ni ndogo sana yaani ukitenga masaa ma3 kwa baskeli unaumaliza mkoa wote sasa Daladala ya kazi gani?hizo 4 ulizoziona zote zinatokea mjini kusaidia wanawake wanaokwenda kuhemea wasielemewe na mizigo wakitoka sokoni!Halafu nimeingia ktk globu yako naona picha ulizoweka za mkoa wa Tabora zote ni nyumba za tope tu hebu usiwe bias kaka utawatisha wasioijua Mboka manyema wasifike kabisa kujionea fursa mbalimbali zilizopo.Hebu weka basi na picha za uzunguni,cheyo,majengo nk,pia mahoteli town na baadhi ya maeneo Town pale!Naona kama mtoa hoja aliyesema una ujuaji sana kwa mbali anakaukweli kama utaendelea kuonyesha nyumba za tope tu kuuwakilisha mkoa wa Tabora!Maana hata mimi naweza kwenda dar nikapiga picha za Tandale,mtongani,kigogo then nikaandika Dar inakufa nikapeleka nje ya nchi sijui watakaoziona hizo picha watasemaje!Wewe ni muandishi makini basi hebu acha kuwa bias!Just be real brother!!
Halafu jamani nina swali hv kwanini ulaya na U.S.A watu wanapaita unyamwezini?au vijana wengine utawasikia wanasema mimi mnyamwezi bana?
(Ni mtazamo tu wadau msijenge chuki)!

By Mnyamwezi mkereketwa!!!
 
Ndugu zangu,

Leo nimetembea kwa miguu kutoka mahali nilipofikia maeneo ya Ali Hassan Mwinyi Stadium hadi Chuo Cha Ualimu kunakofanyika mafunzo ya wanahabari. Umbali wa kilomita mbili hivi. Nimetembea nikiongea na wenyeji ambao wengi wanatembea kwa miguu. Kuna niliyojifunza njiani. Tabora si mji wa daladala, hazizidi nne mji mzima.

Baiskeli na pikipiki ndio daladala za Tabora Mjini. Na moja kubwa linalochangia Tabora kubaki nyuma ni miundo mbinu mibovu ikiwamo barabara na ukosefu wa usafiri wa uhakika wa treni umechangia kurudisha nyuma maendeleo ya Tabora.

Na lingine ni attitude ya umwinyi ya baadhi ya watu wa Tabora Mjini. Jana nimezunguka sana kutafuta vocha ya simu, naambiwa kuna wenyeji ambao hawataki kufanya biashara ya vocha ambayo faida yake yaweza kuwa shilingi elfu nne kwa vocha za laki moja! Tabora inahitaji muingiliano zaidi na watu wa mengine. Miundo mbinu itawezesha hilo.


Naam, Tabora iliyodidimia inahitaji kuinuliwa, na wenye jukumu la kwanza la kuifanya kazi hiyo ni Wana-Tabora wenyewe.
Maggid Mjengwa,
Tabora, Januari, 26, 2012
Mjengwa Blog::Habari,Picha,Matangazo
Tembelea pia; Tabora & Singida Press Clubs

Jana Usiku hatukupata muda wa kuongea Vizuri tulipokutana pale Tabora Orion Hotel wakati napata chakula cha usiku, kwani hata mimi ndiyo nilikuwa nafika baada ya safari ndefu nikitokea Mbeya. Dar es salaam - Mbeya - Tabora.

Kama ulivyosema kuhusiana na Tabora ukiangalia maeneo uliyofikia pale maeneo ya Mwinyi, tuseme Franman Hotel, tembea mpaka stand kuu, katikati ya mji, fuata barabara ya Urambo maeneo ya Milambo Sec. Hadi Ipuli, utagundua si tu kuwa Tabora ipo nyuma, bali ni ngumu kabisa kwa mji ule kupata maendeleo.

Wana Tabora ni ngumu sana kujiletea maendeleo, labda mkakati wa sasa ambao unafanywa kwa nguvu kuhamishia shughuli nyingi pale zitakapoweza kutuletea mseto wa watu, na watu hao wakashawishika na kuamua kuifanya Tabora kuwa makazi yao, hapo tunaweza kushuhudia mabadiliko.
Hali hiyo ni tofauti kabisa na Shinyanga ambayo ina zidi kustawi kila uchao. Kuna kazi ngumu ya kufanyika Tabora
 
Kwanza kabisa mtani MBWA MWENYEWE!!Mkoa wa Tabora tatizo lake kubwa ni kusahauliwa na serikali sikubaliani hata kidogo na nyie mnaosema tunaendekeza umwinyi hatutaki kufanyakazi wakati hata wakolono walikuwa wanachukuwa watumwa na manamba wa Nyanyembe Empire kuwafanyia kazi na mpaka ule usemi maarufu wa mzigo mzito mpe MNYAMWEZI ukuibuka!Wanyamwezi niwachapakazi sana lakini serikali ndiyo inatuangusha,serikali imekuwa unaudharau sana mkoa wa Tabora tangu enzi za nyerere tena bila kujali yule mzee pamoja na kusoma Tabora boys(Tabora school ) na baadae kufundisha Milambo Secondary zote za tabora laikni aliupa kisogo sana mkoa wetu!Tangu kipindi hicho Tumbaku ilikuwa ikilimwa kwa wingi Tabora lakini kiwanda kikajengwa morogoro!Mpaka leo hii huwezi amini Tabora hakuna lami tu ya kuunganisha wilaya moja na nyingine achilia mbali mkoa kama ndugu yangu ELNINO alivyosema hapo juu!Kijiografia njia fupi ya kusafirishia bidhaa zinazokwenda nchi jirani za Rwanda,Kongo DRC na burundi ni ile inayopita manyoni-itigi-tura-tabora-urambo mpaka kigoma laokini barabara hiyo ni vumbi mpaka leo!Mikoa tunayoiita ghala la chakula la taifa ya Rukwa na Kigoma mazao yao yatoke kwa urahisi kwenda mikoano ni lazima yapitie Tabora badala ya kuzungukia Mbeya!Achilia mbali mkoa wenyewe tu kuwa na resources nyingine nyingi kama Asali na mengineyo lakini hivi vitu vinatokaje wakati watu tupo kisiwani.Reli imashajifia,mabasi mvua ikinyesha imakula kwenu,ndege imerudi juzi tu Air Tz lakini gharama zake mkulima gani wa tumbaku ata-afford?Iambieni serikali yenu itufungulie mipaka muone kama hatupendi kufanyakazi sio mnalaumu tu kama mnatumia MASABURI!
Suala la kutembea kwa mguu kaka Mjengwa wala lisikuumize kchwa,Tabora mjini ni ndogo sana yaani ukitenga masaa ma3 kwa baskeli unaumaliza mkoa wote sasa Daladala ya kazi gani?hizo 4 ulizoziona zote zinatokea mjini kusaidia wanawake wanaokwenda kuhemea wasielemewe na mizigo wakitoka sokoni!Halafu nimeingia ktk globu yako naona picha ulizoweka za mkoa wa Tabora zote ni nyumba za tope tu hebu usiwe bias kaka utawatisha wasioijua Mboka manyema wasifike kabisa kujionea fursa mbalimbali zilizopo.Hebu weka basi na picha za uzunguni,cheyo,majengo nk,pia mahoteli town na baadhi ya maeneo Town pale!Naona kama mtoa hoja aliyesema una ujuaji sana kwa mbali anakaukweli kama utaendelea kuonyesha nyumba za tope tu kuuwakilisha mkoa wa Tabora!Maana hata mimi naweza kwenda dar nikapiga picha za Tandale,mtongani,kigogo then nikaandika Dar inakufa nikapeleka nje ya nchi sijui watakaoziona hizo picha watasemaje!Wewe ni muandishi makini basi hebu acha kuwa bias!Just be real brother!!
Halafu jamani nina swali hv kwanini ulaya na U.S.A watu wanapaita unyamwezini?au vijana wengine utawasikia wanasema mimi mnyamwezi bana?
(Ni mtazamo tu wadau msijenge chuki)!

By Mnyamwezi mkereketwa!!!

wamesahau ule usemi mzigo mzito mpe Mnyamwezi
 
Back
Top Bottom