Tabora iliyodidimia inahitaji kuinuliwa...

Kutoka Nzega kwenda tabora mjini, ile barabara haieleweki kama ni barabara au nini kinjia. Nilipita 2 years ago, sijui kama walishabadilisha hata hizo changarawe. Tabora wanakalia majungu na kunywa togwa. Wazinduke wananchi!
 
Tabora,
Tatizo lenu ni watu wa majungu, hamtaki kubadilika
Hizo barabara haziji kama mvua, ni mapambano ya kudai haki yenu ya msingi, kama mnauza tumbaku kodo inakwenda wapi?
Na hao wawakilishi wenu madiwani na wabunge wanawasaidiaje?
Kama mliowachagua mnaona hawana msaada, piga chini kwenye uchaguzi
 
Tabora,
Tatizo lenu ni watu wa majungu, hamtaki kubadilika
Hizo barabara haziji kama mvua, ni mapambano ya kudai haki yenu ya msingi, kama mnauza tumbaku kodo inakwenda wapi?
Na hao wawakilishi wenu madiwani na wabunge wanawasaidiaje?
Kama mliowachagua mnaona hawana msaada, piga chini kwenye uchaguzi

majungu ni ya viongozi?? au wananchi wote kwa ujumla??
 
a pity about tabora ni kwamba, tabora ni mji mkongwe kihistoria inashangaza hata barabara ya kuufikia mji wenyewe tu nishida from nzega, na ukifika town ndio kabisa hakuna barabara ya kiwango cha lami hata moja inayoenda kijiji chochote au town yoyote nje ya tabora, lami ni vibarabara vya pale mjini tu, its a very well planned town ila cjui kwa nini hauendelezwi na zao la tumbaku liko juu hata bei yake ktk soko la dunia ambalo linazalishwa kwa wingi tu tabora! lami ingeleta ukomboz mkubwa sana ktk mkoa wa tabora!
 
Sijaona ya Mbezi - Mabwe Pande watapoamia waathirika wa mafuriko ya Dar Es Salaam hadi Bunju
 
Tabora ni ngome ya CCM. Hata mfanyeje haitahamia CDM. Mmeona Igunga. Mtapoteza nguvu nyingi na pesa ambazo mngetumia kwingine. Ngome zingine za CCM ni Lindi, Mtwara, Unguja na Pwani.

Msipende kujua ni kwa nini iko hivyo. Inatokana na nchanganyiko wa vitu vingi na haviko systematic. Hata Marekani kuna Red States na Blue States.

CDM iwekeze zaidi kwenye maeneo yasiyo ngome za CCM. eg Mwanza, Shinyanga, Musoma, Mbeya, Arusha etc
 
Thanks FF najua umecopy na kupaste kwenye site fulani ama wewe unafanya wizara ya magufuri, ukweli ni kwamba kuna kambi zimejengwa njia ya kwenda urambo nadhani mpaka sasa ni takribani zaidi ya mwaka mmoja lakini sijaona kitu cha maana kilichofanyika pale zaidi ya idadi kubwa ya NYOKA na MIJUSI kupungua kutokana na idadi kubwa ya wachina waliopo kambini, Ninasubiri tarehe ya kukamilisha ujenzi huo..................................
 
Ni kweli nimekaa Tabora na nimejionea mwnywe kale ka mkoa ni kabaya kuanzia na barabara mpaka ujinga,ftina na majungu,hawa watu ni hatari sana kwa fitina na ubnafsi, na bado naamini ni miaka mingi itakayopita paspo Tabora kupata maendeleo

Uswahili mwingi TBR, ujuaji mwingi gossips n.k.
Tumaini Eli Kiwelu alipokuwa RC pale TBR, alikuta wenyeji wakicheza bao tangu asb hadi jioni, akawaambia wafanye kazi la sivyo atachukua hatua dhidi yao; kesho yake wazee wa mji wakamfuata pale Bomani ofisini wakidai kuwa wao wana umri mkubwa zaidi yake, kwanini anataka kuaribu atmosphere ya TBR! Kwamba kabla yeye Kiwelu kwenda pale walikuwa wanalala au kushinda na njaa!
Kiwelu akaamua kuachana nao. So kazi
ipo kukomboa wanamboka!
 
Na ndio maana mimi Pangu Pakavu najiandaa kuwakomboa wana Tabora kupitia chama mbadala, CDM.

Ni majuzi tu nilitoa salam kwa Mh Rage, mbunge wa Simba Sports Club, nikasema akae chonjo kwa kuwa umaskini na udhaifu wa Tabora hauvumiliki kamwe. Tabora haikupaswa kuwa hivyo ila ni dhahiri kwamba ama wanatabora hawakupewa elimu sahihi ya mageuzi ama elimu hiyo imechelewa kuwafikia.

Hakuna miujiza katika maendeleo, ni lazima kelele na juhudi zifanywe ili kuleta maendeleo hayo, ukisoma taarifa ya mkoa huu ya miaka 50 ya uhuru unaweza kulia bure, ofisi ya mkuu wa mkoa inaishia kusema eti kumekuwa na maendeleo ya kilimo hususan tumbaku na kwamba eti uvunaji wa asali umekua. Hivi tokea mwaka 1963 hiyo tumbaku na asali zimewafaidisha vipi wakulima wa Tabora, Mh Nkumba ataniunga mkono katika hili. Hiyo asalu ni ipi kama pale senta ya Nyuki kule airport imeishia kuchukuliwa na Mbola Project ile ya vijiji vya millenia, sembuse barabara???

Mabadiliko tutayahubiri na tutawaelimisha wanyamwezi na wasukuma ili twende sambamba, wakati wa ujinga umepita.

Ni mimi
Pangu Pakavu.
.

Unalosema ni kweli mwana JF, mimi nilienda mwezi Dec, 2011 kuna barabara ya kutoka Itigi to Tabora ni mbaya sana. Wanadai barabara ya rami wameanza lakini kinachofanyika hakionekani. Tunachoomba ni wabunge wa maeneo husika wasilale wafanye kazi ili mkoa wetu upate maendeleo kama mikoa mingine. Kama ilani ya CCM inavyosema kuwa barabara zote zinazounganisha mkoa kuwa na rami, inakuwaje mikoa mingine bado? Tafakari na chukua hatua!
 
Nawashukru sana wachangiaji wote, kwa kweli mmechangia kwa uchungu. CCM kwa miaka yote hiyo ambayo imekuwa madarakani imeshindwa kuendeleza mkoa wa Tabora. CHADEMA sasa ni wakati wenu kuingia Tabora ili maendeleo yaweze kuonekana kama mlivyofanya wilaya ya Karatu, Kigoma Kaskazini na kwingine ambako kuna wawakilishi wenu
 
Kutoka Nzega kwenda tabora mjini, ile barabara haieleweki kama ni barabara au nini kinjia. Nilipita 2 years ago, sijui kama walishabadilisha hata hizo changarawe. Tabora wanakalia majungu na kunywa togwa. Wazinduke wananchi!

Wa Ukenyenge! Du napakumbuka Ukenyenge bana! Niliwahi ishi huko! Vipi barabara ya kwenda Kishapu ina lami siku hizi?
 
Jamani barabara za mkoa wetu wa Tabora zinatisha. Mpaka sasa hakuna barabara hata moja yenye rami ambayo inaingia mkoa wa Tabora. Chama changu cha Chadema mko wapi? Waamsheni wananchi wa Tabora kwani ni waelewa. Siku zote wanyamwezi na wasukuma ukiwaelimisha wakaelewa watakuunga mkono. Chadema nendeni Tabora kwani waanzilishi wa vyama hakina Fundikira, Mapalala na Kasela Bantu wote walikuwa ni wenyeji wa Tabora.
Wana JF muwe huru kuchangia kwenye thread ili mkoa wa Tabora uweze kuinuliwa. Kwasababu wanasiasa wenye maamuzi nao wanatembelea mtandao wetu wa JF. Nahisi kuna kitu kitafanyika.
Hivi, ni lini mtaacha kuwapa magamba kura zenu, ndio faida zake hizo
 
Hodi! Hodi Hodiiiiii! Hata msipoitika mi nimo na mnachokisema wengi wenu ni ukweli usiotaka lamli ya mrithi wa Sheikh Yahaya! Tabora majungu, fitina, uvivu, wake wengi na mengineyo mengi ndo yanatuangamiza! Ni miezi 2 iliyopita tu wakati CHADEMA tawi la kata ya Ipuli Tabora walipotaka chumba cha kupanga kwa lengo la kufungua ofisi iliwachukua muda mpaka mwanachama mmoja aliposema najitolea mpange nyumbani kwangu, cha ajabu mwenyekiti wa mtaa ambaye ametokana na MAGAMBA alimfuata na kusema kwa nini unapangisha watu wa CHADEMA yule mmiliki akasema hata mimi ni wa-CHADEMA.Ninachotaka kusema hapa ni fikra mbovu walizonazo watu wa-MAGAMBA ya kuzani wanaweza kutoa miongozo hata nyumbani kwa watu wengine.Upande wa barabara; ukweli ni kwamba kuna matumizi mabaya ya fedha za miradi ya barabara, kwani fedha zilitumika katika kulikomboa jimbo la Igunga na hivyo barabara zikasimama! Kwa sasa tunachoambulia ni mabinti wanaoishi pembezoni mwa barabara hizo zinazotengenezwa na wachina kufaidi kupata penzi la kichina na kwa kuwa matumizi ya KONDOM hakuna basi baada ya miezi tisa tutegemee yaliyotokea jilani na uwanja wa Taifa - DSM.
 
kuna kipindi ujenzi wa barabara kutoka tbr mpaka nzega ilisimama kisa serikali iliwapa fedha kidogo wachina kujenga hiyo barabara.
Mkuu wa mkoa akaenda kufanya ziara huku na kuleta "cheap answers" kwamba wakandarasi wanakumbana na matatizo ya mawasiliano na wenyeji(lugha).
Cha kujiuliza je hawa wachina ni mara yao ya kwanza kufanya kazi tz? kama ni hivyo kwanini walikubali kuchukua tender hiyo while in first place they are unaware of our local languages?
Huu ulikuwa ni muda muafaka kwa mbunge wa tbr kuintervene issue na kuisimamia serikali kuhakikisha barabara inajengwa kwa wakati na kwa viwango viwango vinavyotakiwa.Unfortunately tunambuge wa Simba ambeye humkosi pala Msimbazi-Kariakoo,DSM kwenye ofisi za timu yao.
 
Ni majuzi tu nilitoa salam kwa Mh Rage, mbunge wa Simba Sports Club, nikasema akae chonjo kwa kuwa umaskini na udhaifu wa Tabora hauvumiliki kamwe. Tabora haikupaswa kuwa hivyo ila ni dhahiri kwamba ama wanatabora hawakupewa elimu sahihi ya mageuzi ama elimu hiyo imechelewa kuwafikia

Pia ni mbunge wa Rufita Club
 
pale amemchaguliwa mbunge wa Simba sio mbunge wa Tabora,kwa masuala ya maendeleo ya wanatabora hayamuhusu ndo maana kila siku kwenye tv akiangaikia mara kumpeleka contractor wa jengo lao mahakamani mara kakamata tani 1 ya jezi za Simba.Wacha tuipatepate wanatabora kwa kuendekeza magambaz.

Once a convict

rage270308.JPG


Always a law breaker

07ragekam.jpg
 
Tabora ni ngome ya CCM. Hata mfanyeje haitahamia CDM. Mmeona Igunga. Mtapoteza nguvu nyingi na pesa ambazo mngetumia kwingine. Ngome zingine za CCM ni Lindi, Mtwara, Unguja na Pwani.

Msipende kujua ni kwa nini iko hivyo. Inatokana na nchanganyiko wa vitu vingi na haviko systematic. Hata Marekani kuna Red States na Blue States.

CDM iwekeze zaidi kwenye maeneo yasiyo ngome za CCM. eg Mwanza, Shinyanga, Musoma, Mbeya, Arusha etc


Na kote huko kuna umaskini wa kutisha. Wakazi wa maeneo hayo ni wajinga bado na inakuwa rahisi magamba kuwadanganya miaka nenda rudi.
 
Jamani barabara za mkoa wetu wa Tabora zinatisha. Mpaka sasa hakuna barabara hata moja yenye rami ambayo inaingia mkoa wa Tabora. Chama changu cha Chadema mko wapi? Waamsheni wananchi wa Tabora kwani ni waelewa. Siku zote wanyamwezi na wasukuma ukiwaelimisha wakaelewa watakuunga mkono. Chadema nendeni Tabora kwani waanzilishi wa vyama hakina Fundikira, Mapalala na Kasela Bantu wote walikuwa ni wenyeji wa Tabora.
Wana JF muwe huru kuchangia kwenye thread ili mkoa wa Tabora uweze kuinuliwa. Kwasababu wanasiasa wenye maamuzi nao wanatembelea mtandao wetu wa JF. Nahisi kuna kitu kitafanyika.

Kwani Chadema wanajenga barabara?

Mbona hawajajenga Arusha town mpaka leo hakuna hata barabara moja japo ya nusu kilometa ya Lami? wao ni mabingwa wa malumbano tu.

 
Back
Top Bottom