Tabia ya kutopokea namba ngeni/namba mpya

Tabia ya kutopokea namba ngeni/namba mpya

Haaaaaaaa mkuu bilashaka wewe Ni mwana-SUASO, dark city nomaa Sana kule, Mauki, barakuda
Hapana mkuu, ila nilitakiwa nisome pale nikaona noma, ndio nikaingia kusaka noti kisha nikaenda kusomea ubaharia.

Wana Sua walikuwa wanangu sana, kipindi cha sup na probation tulikuwa tunashinda magetoni.

Naikumbuka mitaa ya unit 1,2,3 Dark City,Maziwa,Bazizane,Kabla ya reli,Mauki,FK,Kitimoto,Kanisani,Modeco
 
mimi hua napokea ila niko makini sana kusikiliza point kwa point ili nijua kua nachekechwa au la ... maana mi mwenyewe mzee wa vimeo
 
Wengine hawana muda wa kutuma ujumbe. Si vizuri kupuuza simu unazapigiwa. Nyingine zina umuhimu kwako. Mimi Ukipuuza kupokea wakati ni kwa faida yako, na mimi nakupotezea, sina haja ya kupoteza muda kujitambulisha kwa sms.
Nadhani badala ya kumpigia tu mtu na namba mpya, mtumie ujumbe jitambulishe. Sasa mtu unapiga kama vile hasira
 
Kwenye maisha kila mtu kajiwekea principles zake na utaratibu wa Maisha.. Ni sahihi sana lakini Kuna vingine vinahitaji Utashi wa kibinadamu kung'amua Hasara na Faida zake.

Kuna watu wamejiwekea utaratibu kwamba Hata iweje, Basi Namba ngeni itapiga sana na kamwe hatopokea.. Sijui ni madeni au basi tu hataki lakini ndo alivyoniwekea.. Hii iko pande zote kwa Baadhi ya wanaume na Wanawake.. Wanawake wengi wanasema wao huepuka Usumbufu kwani mara nyingi huwa ni wanaume wakware wanaotaka penzi lao.

Dhana hii kwa upande mmoja ni sahihi.. Lakini Je, huoni haja ya kumsikia anayekupigia ni nani kabla huja ignore? Na unakuta wewe ni mfanyabishara, mfanyakazi na pengine Mtafutaji wa kazi ume apply huko na huko.. Sasa umepigiwa simu ya interview na hupokei unataka uje kumlaum nani?

Juzi Mtu wangu wa karibu Kapigiwa sana simu Kwa namba mpya na hakuipokea maksudi kabisa zaidi ya mara nne.. Huku akibetua mdomo "Wanaume bana huyu nae anataka kunisumbua tu" Lakini baadae kupitia Namba hyo hiyo akatumiwa Msg Kwamba Kaka yake kafariki kwa Ajali.. Ndo akaanza kutoa vilio kama punda mwenye Njaa

Wakati mwingine tuangalie misimamo yetu kama ina tija kwenye Maisha.
[/QUO
 
Kwenye maisha kila mtu kajiwekea principles zake na utaratibu wa Maisha.. Ni sahihi sana lakini Kuna vingine vinahitaji Utashi wa kibinadamu kung'amua Hasara na Faida zake.

Kuna watu wamejiwekea utaratibu kwamba Hata iweje, Basi Namba ngeni itapiga sana na kamwe hatopokea.. Sijui ni madeni au basi tu hataki lakini ndo alivyoniwekea.. Hii iko pande zote kwa Baadhi ya wanaume na Wanawake.. Wanawake wengi wanasema wao huepuka Usumbufu kwani mara nyingi huwa ni wanaume wakware wanaotaka penzi lao.

Dhana hii kwa upande mmoja ni sahihi.. Lakini Je, huoni haja ya kumsikia anayekupigia ni nani kabla huja ignore? Na unakuta wewe ni mfanyabishara, mfanyakazi na pengine Mtafutaji wa kazi ume apply huko na huko.. Sasa umepigiwa simu ya interview na hupokei unataka uje kumlaum nani?

Juzi Mtu wangu wa karibu Kapigiwa sana simu Kwa namba mpya na hakuipokea maksudi kabisa zaidi ya mara nne.. Huku akibetua mdomo "Wanaume bana huyu nae anataka kunisumbua tu" Lakini baadae kupitia Namba hyo hiyo akatumiwa Msg Kwamba Kaka yake kafariki kwa Ajali.. Ndo akaanza kutoa vilio kama punda mwenye Njaa

Wakati mwingine tuangalie misimamo yetu kama ina tija kwenye Maisha.
na yeye apipiga ili kutaka kuujua undani asipokelewe
 
Kama hutatuma SMS kujitambulisha sitapokea ataupige miaka 5 mfululizo, simu ni yangu ntakavyoamua nisawa
 
Hili swala huwa nawaambia sana watu hawaelewi. Na kama kuna mtu anakusumbua kwenye simu yako una kila haki ya kumkataza asikusumbue tena na ikibidi unamblock.

Ila tabia ya watu kujifanya wao wanajeuri huwa ndio inawagharimu. Imagine sasa mtu unaweza ukapigiwa simu pengine ni mteja wa biashara mpya, au pengine ni interview unapigiwa upangiwe appointment au pengine unakuwa unatakiwa kupewa taarifa nyeti. Sasa why haupokei.....?!
 
Mimi hii ndio principle yangu namba ngeni huwa sipokei kabisa.
Huu utaratibu naupenda na siuachi kamwe.

Najiambiaga kama una la muhimu sana kuniambia utanitumia message.
Na kama hujatuma message najua huyu hakuwa na jambo la msingi ndio maana hajanitumia message.

Ila kwa ujumla kabisa sipendi kupokea simu kabisa, kuna siku ntapokea na tutaongea vizuri ila kuna siku sipendi kupokea kabisa hata kama naijua namba yako.

Cha ajabu ukituma texts tutachati kabisa na nitaanza kutunga sababu za kukwambia kwanini sikupokea simu yako.

Japo ni tabia ya ajabu kabisa yaani unaona kabisa simu inaita na jina unaliona lakini badala ya kupokea unaanza kutunga uongo wa kudanganya kwanini hukupokea.
Na ikinilazimu sana nitakupigia huku nikiomba kimoyomoyo usipokeee yaani ikiita tu mara 2 nakata, kuweka ushahidi kuwa hata mimi nilikupigia[emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1].

Ila kuna watu wanaudhi sana wanaweza kukupigia simu saa 12 asubuhi alafu hawana hata cha maana kukwambia.
Mimi naanza kupokea simu kuanzia saa tatu asubuhi (9:00AM) kwa siku za kazi na saa tano(11:00AM)siku za WeekEnd na Public Holiday.

Sio dharau wala kiburi ila ndio Principle yangu tu japo najua kuna wakati nakosea sana kufanya hivi, ila kwenye maisha lazima uwe na Principle zako na uweze kuzisimamia.
Mkuu ndio maana juzi hukupokea simu zangu ? Sawa bana.
 
Back
Top Bottom