Tabia ya kutopokea namba ngeni/namba mpya

Tabia ya kutopokea namba ngeni/namba mpya

Kweli namba mpya kupokea huwa mtihani kidogo .
Ila mie nae nina tatizo la kusave namba. Phonebook yangu ina majina 14 tu kwaiyo inawezekana kabisa nikawa nakujua ila nisipokee mpaka simu ikatike niangalie call history nikukumbuke au niwe nimekariri namba yako
 
Mimi hii ndio principle yangu namba ngeni huwa sipokei kabisa.
Huu utaratibu naupenda na siuachi kamwe.

Najiambiaga kama una la muhimu sana kuniambia utanitumia message.
Na kama hujatuma message najua huyu hakuwa na jambo la msingi ndio maana hajanitumia message.

Ila kwa ujumla kabisa sipendi kupokea simu kabisa, kuna siku ntapokea na tutaongea vizuri ila kuna siku sipendi kupokea kabisa hata kama naijua namba yako.

Cha ajabu ukituma texts tutachati kabisa na nitaanza kutunga sababu za kukwambia kwanini sikupokea simu yako.

Japo ni tabia ya ajabu kabisa yaani unaona kabisa simu inaita na jina unaliona lakini badala ya kupokea unaanza kutunga uongo wa kudanganya kwanini hukupokea.
Na ikinilazimu sana nitakupigia huku nikiomba kimoyomoyo usipokeee yaani ikiita tu mara 2 nakata, kuweka ushahidi kuwa hata mimi nilikupigia[emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1].

Ila kuna watu wanaudhi sana wanaweza kukupigia simu saa 12 asubuhi alafu hawana hata cha maana kukwambia.
Mimi naanza kupokea simu kuanzia saa tatu asubuhi (9:00AM) kwa siku za kazi na saa tano(11:00AM)siku za WeekEnd na Public Holiday.

Sio dharau wala kiburi ila ndio Principle yangu tu japo najua kuna wakati nakosea sana kufanya hivi, ila kwenye maisha lazima uwe na Principle zako na uweze kuzisimamia.
Kuna siku ubapigiwa siku na Wateja asa mteja apige simu usipokee ahangaike kutuma SMS tena
 
Kwa kweli tunatofautiana, mimi naweza nisipokee mtu ninayemfahahamu ila hakuna namba napokea haraka kama namba mpya. Huwa nakuwa na shauku sana nijue ni nani?? Kapiga kwa sababu gani?
Aisee tuko sawa kabisa
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mpak utumiwe ujumbe kwanza Mkuu.. Unachoogopa ni nini hasa? Kama ni mtu asiyefaa si unamsikiliza tu kisha unaachana nae?
Fear of unknown inaumuhimu wake pia kwenye maisha mkuu
 
ni utaratibu binafsi tu kila mtu anawake
hata angepokea mwanzoni kaka asingepona

mimi simu ya mawasiliano nawasha saa 4 asubuhi nazima saa 2

watu wangu wote washazoea.
Hahaha safi sana upo pamoja nami ,Mimi naviendesha vitu,system inafanya kazi,uzuri tu umekubali Faida na hasara
 
Mmoja alipigiwa kuitwa kwa interview akaringa kupokea. Siku wamemaliza interview woote wakatumiwa ujumbe kuwashukuru kwa walioweza kuhudhuria. Akawapigia kuuliza mbona yeye hakuwa na taarifa. Wakamjibu aangalie missed calls5 alizopigiwa tarehe x kati ya saa 4 asub mpaka saa10 jioni.
 
Nami nimo hapa ,sipendi kuongea na simu ,Mara hello sikusikii vizuri ,lakin SMS as long zainafika uhakika wa anakiandika kuwa ndicho ,,,imagine unatajiwa jina LA swhemu
Tupo wengi mkuu!
 
Kwan kupokea simu ukamsikiliza MTU kama ataongea kitu usiafiki si unaacha tu
Tatizo nyakati hizi,kupokea ponea simu,si salama,,mfano mimi nina kinokia 210 cha mwaka 2012,siku moja napigiwa simu eti,"hiyo simu ni yangu,,imepotea uko wapi?",
Nimeinunua dukani,na imechoka hata button zimefutika namba,
Kwa maana ingine unaweza kuwa na bifu na mtu hata humu jf,,akakuhack na kupata imei yako na kukuripoti umemwibia simu
 
Siwezi kupokea no ngeni, sikati ila itaita had ikate enyewe afu nakaa mda kidogo natuma text kuuliza "sorry nani". Baaaas
 
Aisee tuko sawa kabisa
[emoji1787][emoji1787] kuna taahira pale juu kasema kwa sababu ya umaskini...kwa sehemu nakubaliana nae. Mtu ambaye hapokei namba ngeni ni yule aliyeridhika, hana shida hata kama ni simu ya dili haimpi presha kama lipo lipo tu na kama halipo atapata wakati mwingine. Akina sie wasaka tonge ni ngumu sana kuwa na misimamo ya hivyo maana unawaza labda ni simu ya interview, au mteja wa maparachichi, au watu wa vicoba wanadai deni mradi tafrani[emoji1787][emoji1787]. Lakini mtu anajua akipigiwa simu ni kuombwa hela, kuombwa kazi, kukopwa, mara afisa mikopo wa benki anamshawishi achukue mkopo, mara ofisini kuna wageni ni halali akwepe namba ngeni...ila mimi hapa hata kama babe yuko kifuani ikiingia simu namba ngeni namwambia tu-pause kwanza nipokee simu (hapa nimetania tu jamani[emoji16][emoji16])
 
[emoji1787][emoji1787] kuna taahira pale juu kasema kwa sababu ya umaskini...kwa sehemu nakubaliana nae. Mtu ambaye hapokei namba ngeni ni yule aliyeridhika, hana shida hata kama ni simu ya dili haimpi presha kama lipo lipo tu na kama halipo atapata wakati mwingine. Akina sie wasaka tonge ni ngumu sana kuwa na misimamo ya hivyo maana unawaza labda ni simu ya interview, au mteja wa maparachichi, au watu wa vicoba wanadai deni mradi tafrani[emoji1787][emoji1787]. Lakini mtu anajua akipigiwa simu ni kuombwa hela, kuombwa kazi, kukopwa, mara afisa mikopo wa benki anamshawishi achukue mkopo, mara ofisini kuna wageni ni halali akwepe namba ngeni...ila mimi hapa hata kama babe yuko kifuani ikiingia simu namba ngeni namwambia tu-pause kwanza nipokee simu (hapa nimetania tu jamani[emoji16][emoji16])
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] duuuuh mam umetishaaaaaaah sanaah lol
 
Back
Top Bottom