Nakubaliana na katibu mkuu nishati alivyosema majuzi kwamba tunataka umeme, sio siasa alipokuwa anazungumzia suala la Symbion, lakini kisheria tupo wapi katika hili ili tusije pata vikwazo tena huko mbeleni yaifanye Symbion ibadilike tena and become Chameleon. Tumechoka na mgao ambao umekaa kisiasa zaidi kuliko kitaalam in my view.
Wanasheria, uelewa wangu kuhusu Symbion kisheria ni mdogo sana, ndio maana uwepo wenu ni muhimu sana. Nawaomba msaada katika hili. Ni nini tofauti kubwa kati ya Symbion na Dowans? Ile kesi ya kupinga dowans kulipwa fidia, imeishia wapi? Kama bado ipo, ikipatiwa hukumu, itaathiri vipi suala la Symbion? Inachanganya kwa kweli. Kwa uelewa wangu finyu sana, suala la Dowans lilishamalizika bungeni mwaka jana; Suala la fidia nalo nahisi limesimama; Na leo katika vyombo vya habari, Tanesco, kamati ya bunge nishati na madini na wizara ya nishati wameridhia biashara na Symbion na according to Tanesco, wapo katika mchakato wa kuingia mkataba na symbion kununua umeme; Baraza la mawaziri kazi kubwa ni kutunga na kutekeleza sera mbali mbali, au sio? Bunge nalo kazi yake ni kutunga sheria, among other things au sio? Suala la Symbion limepitishwa kisera zaidi au kisheria or both? Kama ni kisheria, uamuzi wa chombo cha kutunga sheria yaani bunge wa mwaka jana juu ya Dowans umekaa vipi katika symbion? Kama kisera, suala la symbion kama limepata Baraka ya baraza la mawaziri, kuna synergy gani kisheria na kisera katika suala hili?
Kunapochanganya zaidi, juzi afisa mawasiliano wa tanesco alipoulizwa TBC kwenye taarifa ya habari saa mbili usiku je wananchi waelewe nani mwenye kauli ya mwisho, kamati ya bunge nishati na madini? Tanesco? Au wizara nishati na madini? Akajibu kwamba tanesco na wizara wana msimamo mmoja, akakwepa suala la kamati ya bunge nishati na madini; Sasa katika suala la symbion, tuelewe kwamba uamuzi wa kuiridhia symbion kibunge umefanywa kwa niaba ya chombo cha kutunga sheria (bunge) na kamati ya nishati na madini kwa niaba ya bunge au bado kuna hatua ya suala hili suala kwenda pata Baraka bungeni? Na je, Bunge mwaka jana lilimaliza suala la Dowans kama kampuni? Dowans kama mitambo? Dowans kama mrithi wa richmon? Au dowans kama mchakato mzima wa kupata tender?kama lililomalizwa lilikuwa ni suala la kampuni, hali ya leo ipo vipi under symbion? Kama lililomalizwa ni suala la mitambo, hali ipo vipi? Kama lililomalizwa ni mchakato mzima wa tender, hilo nalo lipo vipi katika mazingira mapya ya symbion? Na pia je, nini tofauti kubwa kati ya mabadiliko from Zain to Airtel na Dowans to Symbion katika sheria zetu Tanzania? Na je, hapa pia kuna kodi tumezikosa kutokana na ubovu wa sheria zetu?