Symbion Power acquires DOWANS Power plant

Symbion Power acquires DOWANS Power plant

Hii ndo kusema kuwa mali haramu iko kwenye mchakato wa kutakatishwa na kufanywa kuwa mali halali! Kazi kweli kweli!
 
sioni tofauti kati ya symbion na makampuni mengine yaliyoitapeli TANESCO. Kwanini mkataba huu unakwenda haraka kiasi hiki na kwanini serikali isitafakari mbinu nzuri ya kutatua swala la umeme, kila kukicha utasikia hiki na mwisho utasikia mkataba feki. Hili ni balaa lingine linainyemelea TANESCO
 
Kuna tofauti kubwa kama mwanga ulivyo na tofauti na giza. Maswali yaliyopo yanahitaji kujibiwa katika majadiliano. Hadi hivi sasa hili ni suala la Symbion na Dowans.. nasubiri litakapokuwa Symbion na Tanesco..

Unasubiri ili iweje? uanze ufataani?
 
Kampuni ya umeme nchini Tanesco imesema mazungumzo na kampuni ya kuzalisha umeme ya Symbion Power yamefikia hatua nzuri na wanatarajia kusaini mkataba wa kuuziana umeme na kampuni hiyo muda wowote ndani ya wiki mbili.
Hayo yalisemwa jana na Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO wakati wa kikao cha kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini.

Kampuni ya Symbion Power ndiyo iliyoinunua kampuni ya Dowans/Richmond ambayo iliingia kwenye utata wa kisheria na Serikali/Tanesco kutokana na kasoro nyingi za kisheria katika mkataba wa kuzalisha umeme kati yake na Tanesco/serikali.

May take: Mkataaba wa Dowans haukuwa halali kutokana na kuwa na kasoro zilizorithiwa kutoka Richmond. Je iweje uwe halali kwa Symbion Power?

:sick:
 
Wakuu Salaam,
Kampuni ya Umeme nchini (TANESCO) imesema kuwa zaidi ya 70% ya mapato yake inatumika kuilipa kampuni ya kufua umeme ya Songas na bado umeme unaozalishwa na kampuni hiyo hautoshelezi mahitaji ya nchi.

Hayo yalisemwa jana na Mkurugenzi mkuu wa kampuni hiyo Bw. William Mhando wakati akihojiwa na Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini.
Mhando alisema Serikali haitoa ruzuku kwa ajili ya kuendeshea kampuni hiyo na vilevile ni vigumu kwa kampuni hiyo kukopesheka kwa kuwa haiwezi kujiendesha kibiashara kutokana na mzigo huo mkubwa wa kuilipa kampuni ya Songas.

My take: Kama mambo haya ni kweli basi kazi tunayo.

Source: Mtanzania 25.02.2011

Sijui ujuha wa Watanzania utaisha lini? Huyo Mkurugenzi anajua kazi anayoifanya hapo TANESCO? Kwanini TANESCO isiwe mali ya Songas kama asilimia 70% ya mapato yake yanakwenda Songas? Hata hao wajumbe wa Kamati ya Madini ni wasanii kwasababu mikataba ya aina hiyo ya TANESCO wanaijua vizuri na hayo ni matokeo. Kama hawakuwa na muda wa kukabiliana na hali hiyo katika hatua za kuingia mkataba, leo wanapiga kelele za nini?
 
Hii ni sawa na kuwa na mke Chuma kisha njemba ikaopoa na kupiga mkeo kiulaini. Ukitaka kufungua mdomo unapigwa kiCorola na mshiko wa 10M Keshi. Baada ya hapo jamaa anaanza kupiga mkeo kama vile wake huku wewe umevunja kisambusa na kukenua kwa sana kwenye kikolola chako kikuukuu.
Serikali ya CCM inapigwa kiulaini mbele yakadamnasi ya wana CCM wote na Vidume wa Dowans. Viongozi wote wa CCM wameinama huku wameshika Mabampa ya VX na GX huku wakikenua.

Sijui Symbiosys sijui Dowans MMMH! Chama namba 1 kimeinamishwa.
 
Rais ana gundu period!
kama hatujalielewa hilo tutaendelea kumtafuta mchawi hatutampata.

Suluhisho liko mikononi mwa nguvu ya umma period
 
From Richmond to DOWANS TO Symbion...what next?
 
Inaonyeesha hapa kwenye Symbion pana maswali mengi kidogo!
Hata mimi nisichoelewa kuhusiana na kampuni hii ni: je baada ya kununua hii mitambo ya Dowans wataihamisha au itabaki palepale ilipo?
Lakini pia nadhani walishahakikishiwa soko la umeme na mtu fulani, vinginevyo wasingenunua mitambo mizito hivyo, ndio waanze kutafuta soko!
Halafu ni juniors sana hawa watu...kama wameanza mwaka 2005 yaonyesha wanaendelea kujifunzia vichwani mwetu!...anyway!
Bado kuna harufu fulani unpleasant hapa kwa symbion!

Of course kwenye biashara kuna kila mbinu, kila mtaji unapokuwa mkiubwa na ndio mbinu za kibiashara zinakuwa kubwa. Wafanya biashara wakubwa na waliofaulu vyema kwenye biashara zao, hutegemea sana intelijensia za kibiashara, mahusiano na watu aina na kada mbalimbali, kunusa harufu ya faida na hasara mapema, uwezo wa kufanya maamuzi ya haraka.

Hivi katika vigezo hivyo vyote, ni mfanya biashara yupi atatumbukiza kiwango kikubwa cha fedha bila kuwa na intelijensia zilizomfanya aamue kutumbukiza fedha yake? Leo hii hata ukitaka kwenda machungwa toka muheza, kama hujatazama bei ya soko, kama hujatazama usafiri wa uhakika, kama hujatazama ni nani au wapi ukiyafikisha yatanunuliwa kwa haraka na kwa faida nzuri, basi utakuwa unacheza mchezo wa pata potea na hufanyi biashara.

Kwa mantiki hiyo, Symbion, wameyafanya yote kabla na ndio maana wanaingia katika hii biashara. Na kama hawajafanya hivyo watakuwa si wafanya biashara.
 
Duh!!!,nilifikiri hili muvu lilishamalizika kumbe bado kinaendelea!!!?wakubwa endeleeni na kamchezo kenu wananchi wa Tanzania bado ni wajinga huwa wanaishia kupiga kelele weeeeeee!!!!bila vitendo na kiukweli ni wapole na shida ni sehemu ya maisha Yao ya kila siku hivyo wawekezaji karibuni na muendelee kuwateka viongozi wao akili na kujichukulia madini bila kelele.Hamuoni Serikali inavyowatetea nyie wawekezaji embu ona huko Nyamongo mmeshawaua wananchi wao na wao Serikali nao wameongeza idadi baada ya kuwaua watano,,,wawekezaji karibuni katika SHAMBA LA BIBI sababu WATANZANIA BADO WAMELALA USINGIZI MZITO.
 
Kuna tofauti kubwa kama mwanga ulivyo na tofauti na giza. Maswali yaliyopo yanahitaji kujibiwa katika majadiliano. Hadi hivi sasa hili ni suala la Symbion na Dowans.. nasubiri litakapokuwa Symbion na Tanesco..

Mkuu heshima mbele,
Itakapofikia suala hilo kuwa la Symbion na Tanesco na hapo ndo tutakuwa tayari tumeshaliwa.
Ashakum, ni sawa na kumuona binti yako anarukaruka mitaani unasema hiyo haina tatizo nasubiri atakapopata mimba ndo ntathibitisha kuwa ni kweli.
Kwa taarifa tu ni kuwa tayari Tanesco imesema mkataba kati yake na Symbion utasainiwa muda wowote ndani ya wiki mbili kuanzia jana.
 
Ndio wametambua kuwa serikali ya CCM ina mijitu mipuuzi,yenye mizaha, miroho ya pesa na isyo na chembe za uzalendo. Wakafanya simple logical analysis kwamba kama kikampuni uchwara hewa cha mfukoni kama Richmond kiliwahi kupata nafasi kuvuna pesa za watanzania kikachomoka, kikaja kingine nacho cha mfukoni na kitapeli, DOwans kikavuna weee,kikaingia mpaka chumbani ikulu; Logical table ikaonesha faida ni TAUTOLOGY. Kwanini wasije?
Mbaya zaidi ni kuwa kuna vijitu miongoni mwa hao wanaoliwa fedha zao, kwa kudanganywa na vipesa,na tuvyeo...wanayashangilia hawa majizi na kuyaita MAJASIRIAMALI!
Of course kwenye biashara kuna kila mbinu, kila mtaji unapokuwa mkiubwa na ndio mbinu za kibiashara zinakuwa kubwa. Wafanya biashara wakubwa na waliofaulu vyema kwenye biashara zao, hutegemea sana intelijensia za kibiashara, mahusiano na watu aina na kada mbalimbali, kunusa harufu ya faida na hasara mapema, uwezo wa kufanya maamuzi ya haraka.

Hivi katika vigezo hivyo vyote, ni mfanya biashara yupi atatumbukiza kiwango kikubwa cha fedha bila kuwa na intelijensia zilizomfanya aamue kutumbukiza fedha yake? Leo hii hata ukitaka kwenda machungwa toka muheza, kama hujatazama bei ya soko, kama hujatazama usafiri wa uhakika, kama hujatazama ni nani au wapi ukiyafikisha yatanunuliwa kwa haraka na kwa faida nzuri, basi utakuwa unacheza mchezo wa pata potea na hufanyi biashara.

Kwa mantiki hiyo, Symbion, wameyafanya yote kabla na ndio maana wanaingia katika hii biashara. Na kama hawajafanya hivyo watakuwa si wafanya biashara.
 
Asante sana Mwanakijiji ingawa hatujasikia kipengele cha Tarime
 
RICHOMD=<DOWANS=<SYMBION THE SHOW GOES ON -LUPE FIASCO
The Show Goes On"

[Chorus x2:]
Alright, already the show goes on
all night, till the morning we dream so long
anybody ever wonder, when they would see the sun up
just remember when you come up
the show goes on!
 
Of course kwenye biashara kuna kila mbinu, kila mtaji unapokuwa mkiubwa na ndio mbinu za kibiashara zinakuwa kubwa. Wafanya biashara wakubwa na waliofaulu vyema kwenye biashara zao, hutegemea sana intelijensia za kibiashara, mahusiano na watu aina na kada mbalimbali, kunusa harufu ya faida na hasara mapema, uwezo wa kufanya maamuzi ya haraka.

Hivi katika vigezo hivyo vyote, ni mfanya biashara yupi atatumbukiza kiwango kikubwa cha fedha bila kuwa na intelijensia zilizomfanya aamue kutumbukiza fedha yake? Leo hii hata ukitaka kwenda machungwa toka muheza, kama hujatazama bei ya soko, kama hujatazama usafiri wa uhakika, kama hujatazama ni nani au wapi ukiyafikisha yatanunuliwa kwa haraka na kwa faida nzuri, basi utakuwa unacheza mchezo wa pata potea na hufanyi biashara.

Kwa mantiki hiyo, Symbion, wameyafanya yote kabla na ndio maana wanaingia katika hii biashara. Na kama hawajafanya hivyo watakuwa si wafanya biashara.

hapo kwenye red ndo kwenye shughuli nzima......uhakika wa soko, faida, usalama wa biashara, insurance, mikopo ya fasta N.K
ila naomba kuuliza, hii mitambo si ilikuwa imewekwa collateral benki ya stanbic na barclays ambako dowans walivuta hela??? sasa Symbion wameingia kwa style gani hapo??? kwakweli maswali ni mengi na majibu ndo yanachanganya kabisa!
 
Tanesco wizi mtupu, au huyajui mashirika ya umma? kwani yote yamekufa kwa nini? si ufisadi wa wafanyakazi wa hayo mashirika.
Mashirika ya uma yako chini ya nani Fauzia??? sio serikali?? serikali ni mwajiriwa wa nani Fauzia??? sio wa wananchi???? wananchi ni akina nani sasa?? sio mimi na wewe na yule?? sasa lawama abebe nani kama sio sisi wenyewe tunaokaa kimya pamoja na kuona maovu yote haya?
 
Nakubaliana na katibu mkuu nishati alivyosema majuzi kwamba tunataka umeme, sio siasa alipokuwa anazungumzia suala la Symbion, lakini kisheria tupo wapi katika hili ili tusije pata vikwazo tena huko mbeleni yaifanye Symbion ibadilike tena and become Chameleon. Tumechoka na mgao ambao umekaa kisiasa zaidi kuliko kitaalam in my view.

Wanasheria, uelewa wangu kuhusu Symbion kisheria ni mdogo sana, ndio maana uwepo wenu ni muhimu sana. Nawaomba msaada katika hili. Ni nini tofauti kubwa kati ya Symbion na Dowans? Ile kesi ya kupinga dowans kulipwa fidia, imeishia wapi? Kama bado ipo, ikipatiwa hukumu, itaathiri vipi suala la Symbion? Inachanganya kwa kweli. Kwa uelewa wangu finyu sana, suala la Dowans lilishamalizika bungeni mwaka jana; Suala la fidia nalo nahisi limesimama; Na leo katika vyombo vya habari, Tanesco, kamati ya bunge nishati na madini na wizara ya nishati wameridhia biashara na Symbion na according to Tanesco, wapo katika mchakato wa kuingia mkataba na symbion kununua umeme; Baraza la mawaziri kazi kubwa ni kutunga na kutekeleza sera mbali mbali, au sio? Bunge nalo kazi yake ni kutunga sheria, among other things au sio? Suala la Symbion limepitishwa kisera zaidi au kisheria or both? Kama ni kisheria, uamuzi wa chombo cha kutunga sheria yaani bunge wa mwaka jana juu ya Dowans umekaa vipi katika symbion? Kama kisera, suala la symbion kama limepata Baraka ya baraza la mawaziri, kuna synergy gani kisheria na kisera katika suala hili?

Kunapochanganya zaidi, juzi afisa mawasiliano wa tanesco alipoulizwa TBC kwenye taarifa ya habari saa mbili usiku je wananchi waelewe nani mwenye kauli ya mwisho, kamati ya bunge nishati na madini? Tanesco? Au wizara nishati na madini? Akajibu kwamba tanesco na wizara wana msimamo mmoja, akakwepa suala la kamati ya bunge nishati na madini; Sasa katika suala la symbion, tuelewe kwamba uamuzi wa kuiridhia symbion kibunge umefanywa kwa niaba ya chombo cha kutunga sheria (bunge) na kamati ya nishati na madini kwa niaba ya bunge au bado kuna hatua ya suala hili suala kwenda pata Baraka bungeni? Na je, Bunge mwaka jana lilimaliza suala la Dowans kama kampuni? Dowans kama mitambo? Dowans kama mrithi wa richmon? Au dowans kama mchakato mzima wa kupata tender?kama lililomalizwa lilikuwa ni suala la kampuni, hali ya leo ipo vipi under symbion? Kama lililomalizwa ni suala la mitambo, hali ipo vipi? Kama lililomalizwa ni mchakato mzima wa tender, hilo nalo lipo vipi katika mazingira mapya ya symbion? Na pia je, nini tofauti kubwa kati ya mabadiliko from Zain to Airtel na Dowans to Symbion katika sheria zetu Tanzania? Na je, hapa pia kuna kodi tumezikosa kutokana na ubovu wa sheria zetu?

Mkuu,
Vua hilo shati, vaa gwanda la khaki halafu tafuta kadi yenye rangi tatu na alama ya vidole viwili vinavyojenga alama ya Vee shinani.
 
Mzee Mwanakijiji,
Shukran sana mkuu wangu na shukran zaidi zimfikie Dr.Slaa ambaye kaniacha najiuliza maswali mengi sana kuhusu Uongozi wa CCM..
Hivi kwa nini ni rahisi sana kuwapata viongozi wa juu wa Chadema ktk mahojiano kuliko viongozi wa CCM na hata kama wakijitokeza huongea kwa jazba na vitisho badala ya kuwaelimisha wananchi?..

Halafu ningewaomba sana kina Mnyika na Zitto ambao ni wachama wa JF toka miaka, warudi kijiweni maana toka dogo amekamata madaraka haonekaniki ila tu kwa matakwa ya kurusha habari zake. Na Uongozi wa Jf ujaribu kuwafikia zaidi viongozi wa ngazi za juu wa CCM wapate kushiriki kikamilifu kama wanachama ili nasi tujenge maandamano na mikutano ya kuelimishana/kufahamishana hapa JF..Nadhani Jf inaweza kupeleka mialiko kwa wabunge wote wa Jamhuri kupitia e-mail, Tweet au facebook..

Ningependa sana kuwasikia viongozi ngazi zote wakijumuika nasi hasa ktk maswala magumu ya Katiba, Muungano, Kilimo kwanza, Ajira, Miundombinu na hadi zote ambazo naweza ziweka ktk fungu la Uchumi na jinsi gani tunaweza kupambana na UFISADI..Na ningekomba sana swala la Ufisadi litangaziwe vita ya kitaifa.

Maadam JK amewapa nafasi CCM kuwataja Mafisadi wazi na kuahidi wanachama kulishughulikia basi inabidi Kitaifa nako wabunge wetu walifikishe bungeni na kudai sheria ya kupambana na adui huyu kitu kama - PATROIT ACT.. Uzalendo unatakiwa kupiga vita Ufisadi na sheria itungwe kama ile ya Bush kupambana na Magaidi (Terrorist).
 
Back
Top Bottom