Swali kwa Ayubu Rioba: Siku hizi sera ya Taifa inaruhusu taasisi za kidini kunufaika na fedha za walipa kodi kupitia TBC?

Kuabudu ni uhuru wa mtu kama hutaki kuangalia wengine wakiabudu kupitia TBC wewe zima TV yako au badili channel.

Huo uwezo wetu wa kuvumilia na kuchukuliana kama tulivyo ndio umetuwezesha kufikisha miaka 60 ya uhuru msidhani ni jambo jepesi tu kama kwenda chooni asubuhi baada ya kuamka.

Nchi yetu haina dini ila kila mtu anayo dini yake na anao wajibu wa kuheshimu dini ya mwenzake.
 
Hata asiye na dini,vipi vipindi vinavyomuhusu,kuna vipindi vya dansi,mziki,ngoma,makala za biashara,kilimo,ujasiriamali,nk.Na hao wasio na dini,hawajazuia kuwakilisha vipindi vyao,wenzao wenye dini wanawasilisha vipindi vyao.

Sent from my TECNO KB8 using JamiiForums mobile app
Umekwenda nje ya hoja iliyo mezani. Tunajadili hoja hii:

1. Matakwa ya kikatiba ya kutenganisha dini na dola yanaweza kutekelezwa kwa njia kuu mbili: American style or Germany style.

2. German style inabagua baadhi ya dini na kulazimisha baadhi ya walipa kodi kubeba mzigo usiowahusu; wakati American style haina mapungufu hayo.

3. Kwa hiyo, twende na American style?

Kwa hiyo, utaona kuwa hayo mambo ya dansi,mziki,ngoma,makala za biashara,kilimo,ujasiriamali, sio sehemu ya hoja hii.

Kama nasahihisha karatasi ya majibu ya mtihani wa mwanafunzi ningekwambia: Jibu swali uliloulizwa.
 
Kuabudu ni uhuru wa mtu kama hutaki kuangalia wengine wakiabudu kupitia TBC wewe zima TV yako au badili channel.

Huo uwezo wetu wa kuvumilia na kuchukuliana kama tulivyo ndio umetuwezesha kufikisha miaka 60 ya uhuru msidhani ni jambo jepesi tu kama kwenda chooni asubuhi baada ya kuamka.

Nchi yetu haina dini ila kila mtu anayo dini yake na anao wajibu wa kuheshimu dini ya mwenzake.

Hapana. Habari ya "kuzima TV" haina nafasi katika hoja hii kwa kuwa TBC ni civi space.
Yaani TBC ni eneo ambalo linapaswa kuwa huru dhidi ya kanuni na mienendo ya kiparokia (particular phenomena), ambayo ni kinyume cha kanuni na mienendo mtambuka (universal phenomena).
 
Kwanza hizo sehemu zinazotumika kiarabu mbona ni sehemu chache sana nashangaa kwanini hii nayo ni hoja humu!
Hoja inayohusu lugha za kiarabu na kilatini kutumika kwenye TV ya Taifa sio tatizo dogo kwa sababu kuu tatu.

1. Jambo hilo linakula nafasi ya lugha ya Taifa ambayo ni nyenzo muhimu ya kujenga utaifa.

2. TBC wanao wajibu wa kukuza umoja wa Taifa kwa kutumia lugha ya Taifa, na ndio maana wametofautisga kati ya TBC1, TBC2, etc.

3. Ukoloni wa lugha ni tatizo lisilovumulika.
 
Serikali haina dini ila watu wake wana dini, huwezi kuwazuia kupata neno la Mungu kupitia chombo chao cha habari, na ndiyo maana utakuta utoaji wa huduma za jamii kama vile afya vina ushirika wa serikali na mashirika ya dini, kuna hospitali za mashirika ya dini zina watumishi wa serikali, kinachoangaliwa ni huduma kwa jamii.
Naona unachanganya mambo. Hebu nirekebishe hivi:

1. Chombo chao cha habaro: KIna nani? Katoliki wana Tumaini TV, KKKT wana Upendo TV, Waislamu wa Iman TV, Watanzania wote wana TBC. Kwa hiyo, masuala ya kisekta yanapaswa kuonyeshwa kwenye TV za kisekta, na masuala ya kitaifa kwenye TV ya kitaifa. Hiyo ndiyo maana ya civic space.

2. Utoaji wa huduma za jamii kama vile afya na elimu kupitia ushirika wa serikali na mashirika ya dini: Dini zinasajiliwa MOHA, shule zinasajiliwa Wizara ya Elimu, AZAKI zinasajiliwa Wizara ya Ustawi wa Jamii. Kwa hiyo, huduma za jamii kama vile afya na elimu sio kazi ya msingi ya taasisi za dini. Zinaweza kufutiwa leseni za shule na hospitali na kubakiza leseni ya MOHA.
 
Hoja inayohusu lugha za kiarabu na kilatini kutumika kwenye TV ya Taifa sio tatizo dogo kwa sababu kuu tatu.

1. Jambo hilo linakula nafasi ya lugha ya Taifa ambayo ni nyenzo muhimu ya kujenga utaifa.

2. TBC wanao wajibu wa kukuza umoja wa Taifa kwa kutumia lugha ya Taifa, na ndio maana wametofautisga kati ya TBC1, TBC2, etc.

3. Ukoloni wa lugha ni tatizo lisilovumulika.
Unajua lolote kuhusu ibada za kiisalamu? nakuuliza hivyo kwa sababu huko kutumia kiarabu kwenye ibada ni sehemu ya ibada yenyewe kwa maana inatakiwa yatamkwe hayo maneno kwa kiarabu na si kwa lugha nyengine hivyo si suala la ukooloni wa lugha kama unavyofikiri, na hizo sehemu zenye kulazimika kutamka maneno kwa kiarabu ni sehemu ndogo sana tena zengine hata huwasikii husoma kimoyo moyo sasa ndio maana nashangaa hili suala linakuaje ni hoja humu? labda ingekuwa wanatoa mawaidha kwa kiarabu tu hapo sawa tungejadili lakini sio ibada usifananishe ibada ya waislamu na wengine kuna tofauti ungezingatia hilo usingekuja kuleta hii hoja.
 
Na ndio imani ilivyo ila sio kushikilia imani et kisa ya mababu zako kipi spesho walichokuwa nacho hao mababu? wao waliamini imani zao kwa kipindi chao na ndio maana kuna imani zao zengine tunaita ni imani potofu sasa hivi, kwahiyo kama mtu anaamini hizo imani za mababu aamini kwa hiari kwa kuona ndio imani yenye kufaa na sio kwa sababu et ni za mababu zake.
Ila wewe kuwa mkristu au muislamu kwa kuwa wazazi wako wanatoka kwenye imani hizo ni fresh tu au sio
 
TBC haipaswi kuwa jukwaa la dini yoyote?
Umeenda mbali sana, inawezekana wakawa wanatumika bila wao kujua kama wanatumika.

Japo I highly doubt that kwani TBC ipo kwa ajili ya umma wa watanzania na Waislamu na Wakristu ni moja ya makundi makubwa yaliyopo.

Mfano. Siku kama ya leo Ijumaa Waislamu (kundi mojawapo) ndio huswali na lugha kuu inayotumika kwenye dini yao ni kiarabu, this is the reality we should face it is worldwide otherwise walazimishwe kubadili lugha which is not possible, coz watakuwa tofauti na wenzao duniani.

Same kwa wakristu siku ya jumapili nao hurushwa hewani bahati nzuri kwao lugha inayotumika ni kiswahili, I think this to you is not a problem.

Hicho kimekuwa intended kuwafikia walengwa pekee, ni kweli usemavyo Tanzania/serikali haina dini, lakini pia ukumbuke watu wake wana dini zao.

Hili naona tulikubali tu halikwepeki, au kama wataka kuondolewa vipindi vya dini TBC basi viondolewe vyote bila kujali lugha inayotumika.
 
Naona unachanganya mambo. Hebu nirekebishe hivi:

1. Chombo chao cha habaro: KIna nani? Katoliki wana Tumaini TV, KKKT wana Upendo TV, Waislamu wa Iman TV, Watanzania wote wana TBC. Kwa hiyo, masuala ya kisekta yanapaswa kuonyeshwa kwenye TV za kisekta, na masuala ya kitaifa kwenye TV ya kitaifa. Hiyo ndiyo maana ya civic space.

2. Utoaji wa huduma za jamii kama vile afya na elimu kupitia ushirika wa serikali na mashirika ya dini: Dini zinasajiliwa MOHA, shule zinasajiliwa Wizara ya Elimu, AZAKI zinasajiliwa Wizara ya Ustawi wa Jamii. Kwa hiyo, huduma za jamii kama vile afya na elimu sio kazi ya msingi ya taasisi za dini. Zinaweza kufutiwa leseni za shule na hospitali na kubakiza leseni ya MOHA.
Na vile vipindi vinavyoonesha tamaduni za makabila yetu navyo Tv yao ni ipi?
 
Wote tupinge kwa nguvu zote kuiingiza dini yoyote katika masuala ya serikali. Kuna faida kubwa zaidi serikali kutochanganywa na dini kuliko hasara itokanayo na dini kuunganika na serikali.
 
Siku zote nitapinga kuingiza mambo ya dini yoyote katika mifumo, taasisi na shughuli za serikali.
 
Nimekuwa nikipinga kuchanganya shughuli za kidini kwenye shughuli, mifumo na taasisi za serikali bila kujali mfalme ni nani.
MPUMBAF MJINGA MDINI
Kawaida yenu tunaijua mkisha ona Nchi inaongozwa na WAISLAM mtaanza kuhoji kila aina ya ujinga Madhebu za Kikristo kila siku zitatoa MATAMKO mkitawa na Wagalatia wenzenu hata wakivuruga Nchi namna gani mnaufyata kimyaaa
Tumesha wazioe Waatoliki mnataka Nchi iwe ktk mikono yenu tu pumbaf zenu!
 
Taasisi za serikali kutumika kama majukwaa ya dini ni matumizi mabaya sana ya pesa za walipakodi. Wote tupinge huu utaratibu.
View attachment 1792752
Rubish

Dini zote zinamhubiri Mwenyezi Mungu, hao walioko kwenye hilo taifa ni wacha Mungu, na hicho chombo ni chao kwakuwa kinaendeshwa kwa kodi zao

Mleta mada nenda kakate gogo kwanza kuna zigo linakusumbua
 
Vyombo vya serikali visitumike kama jukwaa la dini yoyote.
...na ukashangaa..maana ulifikiri hao waislam hawana haki ya kutumia hiyo stesheni ya Luninga..ila wakristo tu siku ya Jumapili? Nafikiri ungeyaacha kama yalivyo!
 
Ila wewe kuwa mkristu au muislamu kwa kuwa wazazi wako wanatoka kwenye imani hizo ni fresh tu au sio
Wapi nimesema mimi ni mkristo au muislamu kwa sababu tu wazazi wangu ni wakristo/waislamu? Mimi hadi hapa sasa nafuata imani niliyonayo kwa hiari yangu na sababu zangu na sio et kwa sababu ya kufuata wazazi wangu. Sasa nyie mnafuata imani kisa wazee wenu huko walikuwa na hizo imani sasa hapo mnafuata imani au hao wazee?
 
Tuache kupoteza muda na mambo ya kubalance. Taasisi, mifumo, idara na shughuli zote za serikali zisitumike kama jukwaa la dini YOYOTE.
Sikuwahi kulifuatilia hili,ila nadhani wanachofanya ni kutaka kubalance, yani siku ya ijumaa airtime kubwa inakuwa ni kwa dhehebu la kiislamu na siku ya jumapili airtine kubwa ni kwa wakristo.Kwahiyo kama wanapendelea upande mmoja zaidi hapo watakuwa wanakosea...
 
Sio sawa kabisa.Naunga hoja mkono.
Hapana, kosa linalofanyika TBC ndio linafanyika kwa msajili wa vyama vya siasa. Kodi ya watanzania wasio na vyama inatumika kulipa ruzuku kwa vyama.

Vivyo hivyo, kodi ya mtu asiye na dini inatumika kuendesha TBC kwa faida ya muumini wa dini Y, etc

Haya mambo sio sawa hata kidogo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom