Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,501
- 9,280
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai ameitaka Serikali iache kutoa visingizio ambavyo havina msingi kuwa malori ya kampuni ya Dangote yanaharibu barabara za mikoa ya Lindi na Mtwara.
Amesema kinachotokea ni barabara hizo kujengwa chini ya kiwango, kwani ni jambo linalofahamika kwamba malori hayo yanapimwa uzito, hivyo kampuni ya Dangote haistahili lawama.
Kabla ya kauli hiyo ya Spika, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Sera na Watu Wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama alisema Serikali itapitia upya ujenzi wa barabara hizo ambazo zimekuwa zikiigharimu fedha nyingi.
Awali wabunge wa kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara walilalamikia jinsi Serikali inavyotumia fedha nyingi katika kuikarabati wa barabara hiyo ukarabati ambao hauna tija kwa kuwa imekuwa ikiharibika.
ITV
Amesema kinachotokea ni barabara hizo kujengwa chini ya kiwango, kwani ni jambo linalofahamika kwamba malori hayo yanapimwa uzito, hivyo kampuni ya Dangote haistahili lawama.
Kabla ya kauli hiyo ya Spika, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Sera na Watu Wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama alisema Serikali itapitia upya ujenzi wa barabara hizo ambazo zimekuwa zikiigharimu fedha nyingi.
Awali wabunge wa kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara walilalamikia jinsi Serikali inavyotumia fedha nyingi katika kuikarabati wa barabara hiyo ukarabati ambao hauna tija kwa kuwa imekuwa ikiharibika.
ITV