Siri ya Kuuwawa Zitto - UWONGO

Siri ya Kuuwawa Zitto - UWONGO

Zitto anapendwa sana na watu, akiwa mgombea wa kiti cha urais kwa kupitia CHADEMA, CCM tutakuwa na wakati mgumu sana.

UNAFIKI hautakusaidia ndugu yangu!Hata akigombea Shibuda, CCM wana hali ngumu mno!
 
siku zote utasimama na kuonyesha jinsi ulivyo wa KIPEKEE katika siasa za tanzania... acha CCM wakugwae,,,, acha VIONGOZI wenzio ndani ya CHADEMA wakuchukie, acha washabiki maandazi na vibaraka wa wanasiasa kama alivyo BEN SAANANE watokwe na povu kila wanapolitaja jina lako...... you are extra ordinary kaka and god bless you
 
Hongera kwa ufafanuzi zitto maana umeondoa wingu Lililotanda kuchafua chama chetu, aibu imewakuta wote walioshabikia.:rockon:
 
Hivi CCM wamekosa think tank ya kuestablish strategy ya kuiangamiza CHADEMA? mi nionavyo mbinu zao ni za low thinking. They should sit down and think again in a matured manner.
 
umesomeka mkuu poa sana viva cdm wale vilaza wa ccm hawana maana kazi yao umbea na uzushi hawana maana.
 
Aliongeza kuwa mara zote alizokutana na Zitto, hawajawahi kufika katika Hoteli ya Lunch Time wakiwa pamoja kama ilivyoelezwa katika gazeti hilo.

Hayo ndo majibu ya Mhe Zitto na Saanane kwa hiyo tafadhalini chambueni matatizo yenu badala ya kupoteza lengo la kumpata aliempiga Kibanda
Ebo! wamemmisquote nini?
 
Kaka Mtenda mabaya hutendwa the Zitto era has gone for ever ,hili linabebwa na mitandao yote watu tumeprint kama copy 200 kuzisambaza wamjue head wa masalia ,no more the great Zitto, kila kitu peupe Mtela Mwampamba kamvua nguo na kumuweka barabarani ameconfirm yale tulikuwa tunasema pole Zitto ulidhani kuwachanja chale za matakoni wangenyamaza kwisha dhambi za zitto ni nyingi Arusha kawafanya watu wanapigwa nyanya mpaka leo kwa kuwasaliti udiwani wakati yeye alikuwa anawakazania wasikubali ushauri
shukrani mkuu Lwesye kwa kutuwekea post ya Mwampamba...ila nimeshituka kauli za mwampamba kuwa umaarufu wa Zitto wameushikilia wao..hawa vijana kweli wamejeruhiwa,naona wanahisi kusalitiwa na mtu waliemwamini....tutasikia mengi.!!!
 
Last edited by a moderator:
Nimezisikia hizi habari zikishabikiwa na kiredio fulani kama sikosei ni clouds fm wameishabikia hii mada utadhani siyo professionals, as if ni wamama fulani wamekaa kibarazani wanajadiri umbea. Clouds FM inajipotezea sana status yake kushupalia uzushi tena kwa upendeleo, uzushi unaokichafua CCM wanakuwa kimya ila uzushi wa kuichafua CHADEMA utamsikia Geladi Hando, Kibonde na watu wa level hiyo jinsi wanavyo ishupalia kimbea,

Namshukuru Mungu kwa kuniepusha na aibu ya kutumika na wanasiasa.

hakuna watu professional pale Clouds Fm woooooote ni vimeo tu fuatilia utaamini nini ninachosema...hakuna mtangazaji hata mmoja wa clouds Fm anaweza kuwa kama wale wa BBC, CNN, VOA...wote wamejaa majungu, uzandiki na zaidi wanatumiwa kisiasa kueneza hayo...chukulia tu mfano KIBONDE....hivi huyu anaqualify kuwa mtangazaji ama mwimbaji mipasho?
 
Nikiwa katika upekuzi wangu ndani ya mitandao ya kijamii nimefanikiwa kupita katika facebook wall ya MTELA MWAMPAMBA na aliyoyaandika yamenistua na kuanza kunifanya kumuogopa. Katika kipindi cha nyuma pale ambapo alifanya makosa makubwa ya kukihujumu chama cha chadema akiwa na mwenzie Shonza, Mchange na baadhi ya vijana wengine, niliendelea kumdharau na kumuona ni mtu ambaye hana maana, lakini pia niliamini kuwa hana madhara yeyote kwa chama wala kiongozi wa chama.

Lakini sote tutakuwa mashahidi hapa kuwa tangu kutokea kwa sakata hilo mwishoni mwa mwaka jana, mambo yameanza kwenda kombo kwa kasi ya hali ya juu, hasa kwa siri mbalimbali kuvuja na kuondoka kwa staha ya chama mbele ya jamii. Hali iliyopelekea tahamaki kwa viongozi na wanachama pia.

Mtakubaliana na mimi kuwa yanayoendelea hivi sasa ndani ya chama yanatokana na kuondolewa kwa vijana hawa ambao kumbe walikuwa na siri nyingi na wameshiriki katika mambo mengi kiasi kwamba kila siku zinavyozidi kwenda yanaibuliwa mambo mapya na kuvuja kwa tuhuma mbalimbali.

Kilichonistua sasa ni juu ya Kijana huyo ambae mara ya kwanza niliamini kabisa kuwa ni masalia aliyekuwa anatumika na wanaCCM kuihujumu Chadema, na akiwa target yake kubwa ni Dr. Slaa alivyoanza kugeuza upepo kwa mtu ambae amedai kuwa ni rafiki yake wa karibu ndani ya chadema na kutoa maneno mazito juu yake.

Nitanukuu baadhi ya maneno hayo ambayo yapo katika wall ya mtela:

Kwa anayenifahamu na kuifahamu Chadema na Viongozi wake atakubaliana na ukweli kuwa MIMI, MTELA MWAMPAMBA nilikuwa karibu zaidi na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe.

Kwa kuwa LENGO langu si KUFITINISHA wala KUJIHUSISHA NA CHAMA CHAKE, Nitabainisha (kwa Ufupi) namna ninavyomfahamu ZITTO ZUBER KABWE, tena ikibidi nitabainisha kinagaubaga na wazi wazi (kama italazimu kufanya Hivyo) kiasi Umma ubaini ni nani ZITTO ZUBER KABWE ndani ya Chama: mjenzi, nguzo, mhimili ama mhujumu Chama. Nafanya hivyo kwa lengo la kutetea maslahi ya Kitaifa, maana watu hawa wanabeba nembo na sura ya Utaifa, na ni ubaya ulioje watu wasio na DHATI ya kiutawala kuaminiwa katika Utawala.

Ni kwa msukumo huo ninajikuta ninao wajibu wa kuwabainishia UMMA juu ya mambo hayo manne ambayo ZITTO ameyasema.(Kwa maana sitaeleza lini na wapi nimekutana na ZITTO.,sitaeleza tunafahamiana kiasi gani na tuliwahi kupanga lipi na wapi, sitasema tulifanikiwa mangapi na kushindwa mangapi, sitaeleza "sura halisi" ya ZITTO ninayoifahamu mimi kuliko mtu yeyote mwingine katika Chadema (ILA NASISITIZA KUWA NITAFANYA HIVYO TU PALE ITAKAPOBIDI)

Kwa maana yote yanayoendelea Chadema yanatokana na Mvutano na Kadhia ya CHUKI na VISASI baina ya Makatibu wawili wa Chama hiko, hata kuondoka kwangu na wengine ni kafara ya jambo hilo. Kuna mambo si sahihi kuyaeleza kiundani na hadharani kwa sababu tuliambizana na kupanga kwa Usiri na Kuaminiana, hatujafikia hatua hiyo ya kuuvunja hata Uaminifu tuliopeana kwa Viapo ila kama tutaendelea na maneno ya namna hii na UZANDIKI, ipo siku tutayasema.

. Ni wazi kuwa tumehojiwa katika vikao kadhaa ndani ya Chadema na kote hakuna ambako tulitaja jina lako wala kukuhusisha na chochote kuhusu sisi. Usijiachie sana katika mazungumzo yako, wakati mwingine neno huweza kuzaa yale usiyoyatarajia.
Karata yako ya mwisho inayo-determine maisha yako kama mwanachadema iko mikononi mwetu, Please brother, Don't mess with your last poker chip, u will lose the game.

Kauli yangu Moja ya Ushuhuda inamaliza Uhai wako ndani ya Chadema., I know you're smart brother, don't get crossed., straighten your words..!

Kuwa makini, AND THIS IS SERIOUS…!

Ni kwa maneno haya nimeanza kumuogopa mwampamba lakini kama haitoshi amedai anazo meseji mbalimbali kutoka kwa Slaa na Josephine ambazo zinaelezea taarifa nyeti juu ya kinachoendelea chadema na amenukuu moja ya sms ya JOSEPHINE aliyosema imetumwa tarehe 22/07/2012.

Mimi nimeanza kumuogopa kwa maana haya si tu yanatoa vitisho kwa mtu lakini ni hatari kwa afya ya chama ikiwa kila kukicha siri za vikao vya ndani vya chama vinaweza kutoka nje tena kwa mtu kama mwampamba, ambae anaropoka popote na kwa yeyote kama alivyosema katika wall yake kuwa,
ZITTO na viongozi wengine wanajua nini kimesemwa kuhusiana na Sakata letu ndani ya Kamati Kuu iliyopita na Jinsi hoja hiyo ilivyosababisha Kikao hiko kutahamaki pindi mwenyekiti alipoizima, lakini anafahamu kuwa Kikao Cha Kamati Kuu ijayo kitamjadili yeye (ZITTO) na SHIBUDA na BEN ni miongoni mwa watu watakao toa Ushuhuda wa aliyoyatenda ZITTO katika CHADEMA na juu ya anayoyasema yeye BEN katika mitandao ya Kijamii

WE ARE NO LONGER SAFE..,kuna mirija ya habari na upashikuna bado unaendelea ndani ya Chadema ukiongozwa na masalia walioondoka na baadhi waliobaki.,TUCHUKUE HATUA KWA UANGALIFU, na TUCHUKUA HATUA SASA.
 
hakuna watu professional pale Clouds Fm woooooote ni vimeo tu fuatilia utaamini nini ninachosema...hakuna mtangazaji hata mmoja wa clouds Fm anaweza kuwa kama wale wa BBC, CNN, VOA...wote wamejaa majungu, uzandiki na zaidi wanatumiwa kisiasa kueneza hayo...chukulia tu mfano KIBONDE....hivi huyu anaqualify kuwa mtangazaji ama mwimbaji mipasho?
Ila mwanangu anapenda sana kuwasikiliza jinsi wanavyochekacheka kama wanawake wa uswazi si unajua mambo ya watoto!!!!!!!!
 
wengine kumbe haturuhusiwi kuchangia?mbona commet yangu naambiwa topic imefungwa na wengine wanachangia?
 
hakuna watu professional pale Clouds Fm woooooote nini ninachosema...hakuna mtangazaji hata mmoja wa clouds Fm anaweza kuwa kama wale wa BBC, CNN, VOA...wote wamejaa majungu, uzandiki na zaidi wanatumiwa kisiasa kueneza hayo...chukulia tu mfano KIBONDE....hivi huyu anaqualify kuwa mtangazaji ama mwimbaji mipasho?
<br />
<br />
kimeo mwenyewe...abdul mohamed alikuwa anatangaza sports na news now anakula bata majuu landani bbc swahili....
 
Mmeona mafunzo ya JKT yalivyo na manufaa?<br />
<br />
Kijana fresh from JKT huyo...
<br />
<br />
character zako zafanana dizaini husein macheni quest wa cnn na anderson cooper.....
 
Nilijuaga JF wote ni ma Great Thinker kumbe tuna vilaza kibao sijui tutawasaidiaje ili tuwe tunajadili mambo kwa uhuru. hapa hatuko kuchambua ID tuko kuchambua maada acha ubongolala kama huna point jaribu nyingine mnachosha sana, haya kuanzia sasa nitalikana jina langu kisa ukiliona unaweweseka KILAZA - MBURULA wewe

Haya mama. You know better. Ujumbe wangu ulimlenga Josephine ambaye ni partner wa Dr. Slaa. If you are not the one, forgive me. And I was just saying. And I still think my message is valid. Wengine husema kwa nia njema. Vilevile, hukuwa na sababu ya kutukana. You are actually a great thinker. No?
 
Mh Zitto unachotakiwa kufanya ni kuita waandishi wa habari ukanushe na uwaamishe waTz wanaoamini kila wanachokisikia ktk tv zetu,
Nina maana gani
1. Si watz wote ambao wanaweza kuingia kwa net na ktk mitandao ya kijamii
2. Fanya hivyo wtz wote wakisikia maelezo kutoka ktk kinywa chako
hakoka aibu kubwa sana kwa waliokuwa wanashabikia hii mada especialy media!!

ni maoni yangu tu!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom