Siri ya Kuuwawa Zitto - UWONGO

Siri ya Kuuwawa Zitto - UWONGO

Nilisema hapa huu ni uzushi sasa Mwandishi wa habari ile anasemaje? ndio maana baadhi ya wanandishi wanaitwa Makanjanja hawa watu njaa njaa sana...
 
tatizo lililopo ni kwamba,waandishi wanalazimisha swala hili lionekane ni lakweli,tangu awali Mh Zitto alishalisemea hili kuwa hajawahi onana na saanane na hata wakipishana barabarani watapishana,kwanini tunalazimisha mtu kumfahamu fukani?
watanzania tuache kuunganisha dots,tuache kulazimisha mambo,Zitto sio mjinga,anachokisema anamaanisha na tusilazimishe
 
hongera kwa kuweka hadharani msimamo wako dhidi ya propaganda chafu dhidi yako na chama chetu!...cdm nitofauti na jamaa wa magamba
 
Siku zote katika mapambano watu wakiona wanaelemewa wanatafuta njia mbalimbali za kujaribu kuonyesha mianya na mipasuko kwa wale wanaoelekea kupata ushindi. Ni vizuri wapenda mapinduzi ya kweli na maendeleo ya watanzania walio wengi tulielewe hili. Hizi hadithi za kutunga kuhusu mifarakano ndani ya CDM zimeanza kuwa nyingi baada ya ccm kujawa na hofu na mashaka kwa jinsi CDM inavyokubalika ndani na nje ya nchi. Tusikatishwe tamaa na hizi tamthiliya zao, na tuelewe ya kuwa hazitaishia hapa. Tukumbuke ya kuwa mti unaozaa matunda ndiyo unaotupiwa mawe!!!

Mungu Ibariki Tanzania na watu wake!
 
Pole sana ndugu Zitto.
Kuna vijana wanataka kupata umaarufu kwa kutumia jina lako, wanatumika na wanajua kuwa wanatumika! Wasamehe bure!
 
Last edited by a moderator:
"Kila nafsi itaonja mauti" asante Zitto kwa ujumbe! Na mkome wale wote mnaojidai kwamba mnamhurumia Zitto, na huwa mnaingia humu kumsemea kama vile amewatuma. Zitto ana uwezo wa kujisemea mwenyewe, wengine mnajidai kuwa na huruma naye kumbe mnataka kumharibia mahusiano na viongozi wenzake. Mnaojifanya vibaraka wa Zitto kuweni makini
 
Bravooo Zitto......ujumbe huu uwafikie wanasiasa na wale wote wafanyao siasa za majungu, fitina na visasi. Mungu ibariki Tanzania.
 
Safii Zitto.....
Hiyo ni hatua moja lakini ningeopa ufafanuzi uwe unatolewa mara pale shutuma zinapotoka. Hii maneno haijaanza jana naona kuna watu wanarudiarudia kitu hadi kinaonekana kama kweli.
Way forward ni kujenga chama
 
Last edited by a moderator:
Heshima ya Upande mmoja! Hapa Zitto utapongezwa kwakuwa tu 'umem-save' 'nabii' SLAA. Hawa hawa ndio wanaokuporomoshea matusi kila siku! Lengo lao wakutumie tu kama 'kile kifaa' kisha waku-dump! Sijui kama hulijui hili!
 
Mh.zitto haya magazeti yetu na vyombo mbalimbali vya serekali vinaendeshwa na skendo/mawazo ya watu humu jamii forums
1)TCRA ilivifungia vyombo kadhaa vya habari baada ya thread kuanzishwa humu
2)gazeti hilo la mtanzania na magazeti mengine yanaendeshwa na habari wanazoziona huku
3)hata kukamatwa kwa lwakatare walipata hiyo clip hukuhuku jamii forums
Kwaiyo nadhani wasikupe shida sana na pili washauri wabadilike kama nchi inaendeshwa na mawazo ya watu hapa jf inasikitisha

Kikubwa mheshimiwa zitto nakushauri hama chadema na utengeneze chama chenye malengo ya kumkomboa mtanzania
Chadema imeshaoza sana .........Take this from me
 
Asante kwa kuweka wazi mkuu. Somethings are simply to be ignored, and somethings must be addressed before they result in damage. Very important ni huu ujumbe umeweka hapa:
zitto said:
Nne, Nawashauri viongozi wenzangu wa CHADEMA na hasa wanachama tutumie muda wetu kujenga mshikamano ndani ya chama. Fitna, majungu, uongo, uzandiki nk kamwe havijengi chama. Chama chetu lazima kiwe mfano bora wa kuheshimu demokrasia na haki za binaadamu. Wananchi hawawezi kutoa dola kwa chama chenye mifarakano. Tusiruhusu kugawanywa kwa matakwa ya watu wachache. Tusimamie misingi ya kuanzishwa chama chetu.
 
Afadhali comrade umeonekana humu na kuwek kumbukumbu sawa maaana gazeti uchwara la makada waandamizi wa CCM wanataka kuleta siasa chafu na ujinga uliokataliwa siku nyingi na watu wanaofikiria mara mbili. upuuzi huu waliuanzisha FB ktk group la TANURU LA FIKRA wenye akili timamu wakawaambia ukweli juu ya SIASA zao chafu tena kabla hawajahama CHADEMA nashangaa leo mhariri kuifanya habari kuu wakati habari ilishatoka na kuchuja zaidi ya miezi miwili sasa
 
Tatu, nawashauri watu ambao wamehama CHADEMA na kuhamia vyama vingine watumie muda wao kujenga vyama vyao badala ya kila siku kuzungumzia masuala ya chama ambacho wao sio wanachama tena.
Kwanza ni very unprofessional kwa mtu kuhama kampuni/taasisi/shirika moja kwenda nyingine na kuanza kurusha vijembe ulikotoka au kutoa siri za kampuni ulikotoka, nii tanzania tu ambako bado tumelala sijui kama tuna sheria za waajiri/taasisi/mashikrika ili kulinda confidential informations zao. Only people who lack ethical conducts can do that. Ukifuatilia kwa makini utagundua kuwa watu wote wenye kufanya mambo ya ajabu ajabu hawajaiva katika taaluma zao na kuamua kufakamia taaluma zingine.
 
Mkuu Zitto asante kwa tamko.
Ila naomba ka uko serious kweli, uitishe press, huku umelishika hilo gazeti, ukemee na utishie kulipeleka mahakamani, lisipo kuomba radhi, ili usafishe chama chetu.
 
Last edited by a moderator:
Ze marcopolo, Ritz et al mko wp kuchangia uzi huu njoeni jamani tupate michango yenu
 
Kweli ZZK umepass out JKT. Very good.

Na kwa emotions nyingi sana...big up Mr Zitto must be singing this

Motherland cradle me​
Close my eyes​
Lullaby me to sleep​
Keep me safe​
Lie with me​
Stay beside me​
Don't go, don't you go​

2+(2).JPG
 
Jamani huyo ndio Zitto . Huyu ni miongoni mwa viongozi wa kuigwa duniani.Anaonekana ni kijana mkweli, mwaminifu asieuma maneno na anaejitahidi kuepuka fitna unafiki na siasa za kitoto.Nawasihi viongozi wote wa nchi hii waige mfano wake kwa kutolea ufafanuzi mambo yanayohitaji ufafanuzi kwa uwazi na mapema kama anavyofanya huyu ndugu yetu.Mungu ambariki Zitto.
 
Last edited by a moderator:
Viva Zitto Kabwe,
Obrigado, aluta continua
Tujenge chadema yetu
 
Back
Top Bottom