Siri nzito ya Zombe na Bageni

Siri nzito ya Zombe na Bageni

Ila hapa binafsi sijaelewa, japo hii kesi imechukua muda mrefu sana, nini sababu hasa ya hawa jamaa kuuwawa? Ni kwamba polisi walijua wako na pesa nyingi wakaona njia ya kuzichukua ni kuuua na kusingizia majambazi ama kuna lingine?
A. Ndio jibu sahihi.
 
Kuna aliyekufa kimagumashi (ocean road) huyu yeye alikuwa Shahidi muhimu zaidi kwani alikuwa Gari moja na Kina Bageni Pamoja na wauaji, Kuna Wawili Walitoroshwa inasemwa hadi Leo hawajapatikana Nia ilikuwa ni ku neutralize situation kwamba Jumba lote bovu lidondoshwe kwao kwamba ndio wauaji. Zombe alicheza karata zake vizuri ila Mungu atampa Kifo kibaya Sana kamwe hatamuacha atambe.
 
Walikuwa Wamekuja Mjini kutokea huko Mkoani Morogoro Wilaya ya Ulanga so zile movement zao za kibiashara zilivuja as you know kuwa walikuwa na madini ya thamani Kubwa hivyo taarifa zilipowafikia Zombe na Bageni ndipo wakaamua kuwatengenezea tukio ili wawapoteze Kisha wachukue fedha zao madini waliyokuwa nayo. Waliporwa fedha na madini vyenye thamani karibu M300.

Walikuwa ni wenye kufahamika si unajua mjini Kuna madalali wa Kila Idara Hao kwa sehemu walichangia kuvujisha Habari zao. Zombe by then alikuwa ni kama Jambazi tu coz alikuwa na genge Lao wamepora Sana magari Kisha kubambikia Raia case haswaa ukutwe na Gari Yale ambayo yametoka South.
Niliambiwa kuwa walikuwa pia wafadhili wa vituo vya watoto yatima, na shughuli nyingine za kijamii huko kwao mpaka mbunge wa huko alikuwa anawafahamu. Ndiyo maana ilivyotangazwa kuwa ni majambazi jimbo lote likalalamika sana mpaka kuelekea kuundwa Tume.
 
Well, "mwenendo wa kesi upitiwe upya," ndio kesi kurudiwa mara mbili huko!



Ndio ilikuwa ni rufaa, lakini kuna wakati appeal on acquittal ni kama kesi kurudiwa upya.

Kwa kuelewa hilo, kuna msingi unaitwa double jeopardy kwenye nchi zilizopevuka kwenye haki za raia na misingi ya ki-katiba, ambapo serikali for the most part hairuhusiwi kukata rufaa wakishashindwa kesi.

India, Marekani, Afrika Kusini, kwa mfano, rufaa za serikali baada ya kushindwa kesi haziruhusiwi, isipokuwa for a few special exceptions. Hapa kwetu serikali ilishindwa na Shehe Ponda Morogoro, DPP akakata rufaa, mara ya pili Shehe Ponda akashindwa. Serikali imeshindwa kesi ya na kina Kamanda Zombe, DPP akakata rufaa, kesi ikarudiwa, kina Mageni wameshindwa.

Huku ni kuvunja misingi ya double jeopardy inayokataza serikali kuwa na nafasi ya kukushitaki mara mbili mbili mara tatu tatu kwa kosa lile lile.
Na wewe ni Wa kukufungulia mashitaka halafu ushinde... Then DPP akate rufaa ushindwe tukunyonge pale kariakoo mchana kweupe...
 
Hivi naweza kueleweshwa how kina Zombe came to know kuwa hao wafanyabiashara wana pesa nyingi cash?

Dreva tax alikua ni mtu wao wa Karibu sana kila wakati ja daresalaam kuuza Izo spinel walikua wakimchukua ...so anaweza kua alihusika... Nawajua kina jongo sana tu huko walipo nafsi zao zitakua zimetulia sasa
 
Hatimae leo Bageni kapata stahiki yake
Kutokana na hukumu hiyo polisi ndo wanapaswa kuikumbuka ile stori ya Mkw3re kuwa "za kuambiwa, changanya na za kwako" sio kila unaloelekezwa unalitekeleza bila ku reason, ona sasa ZOMBEH anaenda kula ugali kitaa while jamaa anaenda kunyongwa.............
 
Walikuwa Wamekuja Mjini kutokea huko Mkoani Morogoro Wilaya ya Ulanga so zile movement zao za kibiashara zilivuja as you know kuwa walikuwa na madini ya thamani Kubwa hivyo taarifa zilipowafikia Zombe na Bageni ndipo wakaamua kuwatengenezea tukio ili wawapoteze Kisha wachukue fedha zao madini waliyokuwa nayo. Waliporwa fedha na madini vyenye thamani karibu M300.

Walikuwa ni wenye kufahamika si unajua mjini Kuna madalali wa Kila Idara Hao kwa sehemu walichangia kuvujisha Habari zao. Zombe by then alikuwa ni kama Jambazi tu coz alikuwa na genge Lao wamepora Sana magari Kisha kubambikia Raia case haswaa ukutwe na Gari Yale ambayo yametoka South.

Hiyo sio sababu mimi niko kwenye Hii biashara mwaka wa 11 Sasa zinafanyika biashara za mamilioni na hamna anaeuliwa wala anaejua biashara inakua kati ya tajiri Na mkulima alieleta mawe na ni kila siku... Tatizo alikua dreva tax walizoeana nae sana kila wakija walikua wakimchukua alikua kama ndugu...na watu waliwatahadharisha ila ndio hivyo tena
 
Kuna aliyekufa kimagumashi (ocean road) huyu yeye alikuwa Shahidi muhimu zaidi kwani alikuwa Gari moja na Kina Bageni Pamoja na wauaji, Kuna Wawili Walitoroshwa inasemwa hadi Leo hawajapatikana Nia ilikuwa ni ku neutralize situation kwamba Jumba lote bovu lidondoshwe kwao kwamba ndio wauaji. Zombe alicheza karata zake vizuri ila Mungu atampa Kifo kibaya Sana kamwe hatamuacha atambe.

Uko sahihi kabisa, saad alawi na mwenzie ndio walikuwa mashahidi wazuri kummaliza zombe, kutopatikana kwao ndio kumemuacha huru zombe... Ila damu ya mtu haipotei bure..
 
Roho/damu za kina Chigumbi na dereva taxi hazitapumzika kwa amani na zitaendelea kuwasumbua wote walioshiriki kwa namna yote ile wakiingozwa mtuhumiwa 1 na familia zao.
 
Kuna nafasi kwa familia ya kufungua kesi ya madai dhidi ya tasisi husika pamoja na wahusika wote.
Hivi kweli katika mazingira kama haya ambapo taasisi ya serikali kupitia watendaji wake sampuli ya akina Zombie na Bageni wanapokuwa wamesababisha mauaji ya watu wasio na hatia wanafamilia hawawezi kudai fidia kutoka serikalini? Wataalamu wa sheria hebu tupeni elimu hapa.
 
Polisi kwa kutumika hawajambo mwisho wa siku wanaishia kuangushiwa jumba bovu....
 
Back
Top Bottom