Watu ambao wangekutwa na hatia moja kwa moja ni yule aliyetoa amri na alitekeleza. hao wengine wangeshtakiwa kwa makosa ya kuficha mauaji, aliyetelezwa alitoroka na hadi leo hajapatikana, nao ni utata mtupu.
Hakika nimesononeka moyoni hii kesi nilikuaga naisikia nikiwa bado sijielewi kivile dah anyway Mungu tuhurumie wanadamu tumekua na roho mbaya kizidi hata ibilisi!!!
Yaaani hawa jamaa waliua na bado wakazidi kuua tena washiriki wenzi wao?Hatujui kwa kweli, inawezekana amefichwa, au aliuawa, mnakumbuka mmoja alikuwa anasema ukweli, jina lake Rashid Lema, ghafla akapatwa na ugonjwa wa ngozi kuputika hadi akafariki kabla hajatoa ushahidi wake
Hivi ni unyama? Au ni ushetani binadamu mwenye dhamana ya kulinda raia na mali zake kudiriki kukatiza uhai wa watu watatu wasio na hatia kwa mgawo wa sh m.5! Naomba kabla hajanyongwa mali zake ziuzwe wapewe ndugu tegemezi wa marehemu husika ndipo ashike njia ya kwenda huko alikoelekezwa na mahakama.Zombe!! Period na alipewa mgawo!
That's a million dollar question.Ukifuatilia huu ushahidi vizuri Bageni alihusika moja kwa moja kama mtekelezaji wa mauaji kwa kutoa amri. Yule aliyekuwa anaongea naye kwenye simu katika eneo la tukio bila shaka ni mkubwa wake wa kazi.
Kama Bageni ni Kamanda wa upelelezi Wilaya ya Kinondoni bila shaka mkubwa wake ni Kamanda wa upelelezi Mkoa au Taifa. Nani huyo?.........
Jibu hapo ni rushwa katika ubora wake,hao wakina Bageni wamechezewa na mkubwa wao ambaye network yake Ya kipolisi isingeweza kutoka hayo mawasiliano kuisaidia mahakama.Ukifuatilia huu ushahidi vizuri Bageni alihusika moja kwa moja kama mtekelezaji wa mauaji kwa kutoa amri. Yule aliyekuwa anaongea naye kwenye simu katika eneo la tukio bila shaka ni mkubwa wake wa kazi.
Kama Bageni ni Kamanda wa upelelezi Wilaya ya Kinondoni bila shaka mkubwa wake ni Kamanda wa upelelezi Mkoa au Taifa. Nani huyo?.........
Bageni asingepona maana ushahidi dhidi yake ulikuwa mzito sana...Kuliko kuachiwa huru Zombe bora Bageni naye aachiwe,hii hukumu haiingii akilini kabisa.
mke wa jenerali kombe nasikia alilipwa pesa mingi sana.... inatakiwa wamfuate awape a,b,cHivi kweli katika mazingira kama haya ambapo taasisi ya serikali kupitia watendaji wake sampuli ya akina Zombie na Bageni wanapokuwa wamesababisha mauaji ya watu wasio na hatia wanafamilia hawawezi kudai fidia kutoka serikalini? Wataalamu wa sheria hebu tupeni elimu hapa.
Ni moja ya mhimili unaoongoza kwa RUSHWA. Yah kesi ya msingi ni KUTUMIA MADARAKA HOVYO NA KUFICHA UHALIFU.