Simulizi ya kifantasia: Solo king: ancient legacy

Simulizi ya kifantasia: Solo king: ancient legacy

By Samuel jk_Euphoria

SOLO KING: ANCIENT LEGACY

CHAPTER 22: Nakupa namba kumi


"Ningekuwa najua nisingeuliza mzee wangu" Jimmy alimjibu mlinzi huyo



"Huyo ni msanii maarufu wa hapa bongo, anaitwa Bakari Juma almaarufu kama Beka"



"Oh sasa msanii anakuja kufanya nini huku muda ambao anatakiwa studio?"



"Kijana inaonekana hujui mengi licha ya kumiliki simu janja, mimi na huu uzee wangu lazima nizame mtandaoni kujua nini kinaendelea nchini na suala la huyo dogo kuja hapa iko hivi, kuna tetesi kwamba jamaa anampenda madam mdogo na ndiio yupo kwenye mchakato wa kummiliki na hii ni mara ya tatu kuja hapa"aliongea mlinzi huyo na kumfanya Jimmy akunje sura bila kupenda



"Hahaha... Hahaha.. Haha" ghafla tu Jimmy alianza kucheka bila ya kueleweka anacheka nini



"Vipi kijana mbona unacheka?" aliuliza mlinzi



"Huyu Beka anafurahisha sana mzee wangu, kitendo cha kuja mpaka nyumbani kwa madam mdogo maana yake ni kwamba madam anakaza si ndio?" aliongea Jimmy



"Yrah inaonekana ila kijana bado hajakata tamaa na ni mwaka wa pili anamfukuzia madam pemgine juhudi zake zitazaa matunda" aliongea mlinzi



"Kuna muda ni bora kukubali matokeo yalivyo l kuliko kulazimisha yawe tofauti, kwa maelezo yako inaonekana hapendwi ila anafosi kupendwa" aliongea Jimmy huku akifurahi moyoni



"Ndio vijana wa siku hizi walivyo halafu utasikia ndiyo nguvukazi ya taifa letu"



"Unaonaje mzee wangu kwa busara ukimfundisha kwamba kama moyo wa mtu hauko kwako, hata ujitume vipi, ni kupoteza muda tu."



"Haha kijana unataka kunitafutia matatizo sio"



Jimmy na mlinzi wa geti walijikuta wakipiga story mbili tatu kwa zaidi ya masaa matatu na bado Beka hakuwa ametoka ilionekana alikuwa akimsubiri Bianca na kweli muda huo wa saa tisa Jimmy na mlinzi waliweza kusikia honi kutoka nje ya geti na bila shaka alikuwa ndiye madam mdogo aliyekuwa akisubiriwa



Mlinzi alikwenda kufungua geti na gari jeusi liliingia na kwenda kujiegesha mahali pake kisha mlango ukafungulia na Zuhura aliweza kutoka na walinzi wawili ndani ya gari na kisha Bianca



"Amekuja tena" aliongea Bianca mara baada ya kuliona gari analolitambua mmiliki wake



"Je nimwambie aondoke?" aliuliza Zuhura



"Haina haja twende ndani" Bianca aliongea kikauzu



Ile wanataka kupiga hatua kuelekea ndani walisikia sauti ya mtu ikiongea



"Hatimae malkia umwrudi" aliongea Jimmy akiwasogelea mikono akiweka mfukoni mwa suruali na uso uliopambwa na tabasamu



"Tafadhali Jimmy"



"Aw sio mbaya angalau umeniita jina langu kwa mara ya kwanza zio mbaya ila usikasirike nimekuja tu kukupa hi na pole ya kazi"



"Inaonekana una muda mwingi sana wa kupoteza si ndio?" aliongea Zuhura huku amekunja sura ni wazi hakumpenda



"Ndio ndio lakini pia kutazama watu muhimu wakifika kwa kuchelewa ni mojawapo ya mambo yangu mapya ya kujifurahisha. Hasa wakati kama huu ambao kuna drama nakwenda kushuhudia" alijibu huku akitabasamu



"Drama?"



"oh tena ni pale mtu mashuhuri anapomtembelea mtu mashuhuri mwenzake bila taarifa" aliongea Jimmy



"Isn’t it though? He’s been showing up here thrird time now in two years, and you keep playing ice queen. You dont love him do you?" aliendelea akimaanisha kwamba Beka amekuwa akija hapo ni mara ya tatu sasa kwa miaka miwili na humpendi si ndio?



"Zuhura twende ndani" aliongea Bianca kisha kutangulia akifuatwa na Zuhura na walinzi wawili



"Haha very cute!" aliongea jimmy huku akicheka na kuunga trela kuingia ndani akiwaacha wale mabaunsa wa Beka wakimuangalia na macho yao yasiyo na utani lakini hakujali



Picha linaanza baada ya wote kuingia ndani Beka alikuwa sebuleni amekaa akinywa juisi ya matunda na mara baada ya kumuona Bianca alisimama



"Hatimae subira yangu imezaa matunda" aliongea Beka



"Beka kwanini upo hapa?" Bianca aliuliza



"Nimekuja kuzungumza kuhusu sisi"



"Hilo tu?"



"Pia kuhusu ile hafla ya hisani itakayofanyika wiki ijayo, wanataka sisi wawili kuwa sura ya kampeni hiyo"



"Wanataka au unataka?"



"Vyote"



"Oh sawa si ungempigia tu simu meneja wangu kulikuwa na haja gani ya kuja huku bila taarifa?"



"Pia nilikuwa nataka nije kukuona tuzungumze"



"Kuzungumza kuhusu nini?" aliongea na Beka alisita akimwangalia Jimmy ambaye muda wote alikuwa akisikiliza maongezi



"Ni jambo la faragha hivyo sio jambo la busara kuongea mbele za watu"



"Mbele za watu? Kijana yaani uvamie nyumba ya mpenzi wangu na bado tu haitoshi na unataka kwenda naye faragha? Hata kama wewe ni maarufu angalau kuwa na heshima kijana" Hatimae Jimmy aliongea



Kauli hiyo kutoka kwa Jimmy ilimfanya gBeka kukunja sura bila kupenda ilionekana hakutegemea hilo licha ya kujipanga vyema kabla ya kuja, upande wa Bianca hakubadilika muonekana wake alikuwa katika pozi lilelile la kikauzu Beka alimwangalia Jimmy kwa macho makali kisha kumpotezea na kumgeukia Bianca



"Bianca kwanini unashindwa kuuelewa moyo wangu, ninakupenda sana tena zaidi ya sana lakini kwanini hutaki kunielewa? Juhudi zangu zote kwako unazichukulia poa, unataka nifanye nini ili uniamini nakupenda kwa dhati? Niambie nina mapungufu gani ili nijirekebishe" Beka aliongea bila kujali uwepo wa Zuhura na Jimmy sebuleni humo



"Nishakwambia mara nyingi kwamba sipo interesyed kuanzisha mahusiano na mwanaume yoyote hivyo ulitakiwa unielewe wewe na sio mimi nikuelewe wewe" aliongea Bianca



"Lakini mbona huyu dogo anadai wewe.ni mpenzi wake"



"Hey usiniite dogo mbele ya mpenzi wangu, in case hujui jina langu, naitwa Jimmy halafu acha kufosi mambo pia kama mwanaume unatakiwa kujiongeza. Sababu ya kukwambia hataki kuanzisha mahusiano ni kwasababu tayari alikuwa na mtu anayempenda moyoni na huyo mtu ni mimi" aliongea Jimmy kibabe



Japo Bianca alitaka kuongea neno lakini alichagua kukaa kimya na kuona mwisho wake kati ya hao wanaume



"Tafadhali dogo naomba ukae kimya kwenye mambo yasiyokuhusu" aliongea Beka kwa hasira



Jimmy alitabasamu na kutoa mikono yake mfukoni kisha kuongea



"Hujakaribishwa, hupendwi lakini bado unajikuta mwamba sana, sikia we pimbi nani sijui ili kufanya mambo yasiwe magumu kwako nadhani unajua mlango ulipo" aliongea Jimmy



"Jimmy!" Bianca aliita ilionekana hakupenda kauli aliyoitumia hususani "pimbi"



"Hahaha unpaswa kufikiria mara mbili kati yangu mimi na wewe nani atakuwa wa kwanza kuusogelea mlango" aliongea Beka na alipiga kelele kuwaita mabaunsa wake na punde mabaunsa hawa hapa ndani!



"Tafadharini ndani kwangu sio uwanja wa fujo" Bianca aliongea na Zuhura alitaka kuchukua hatua lakini alipewa ishara ya macho na Jimmy akimtaka atulie na alijikuta tu anatii tu bila kupenda ni kama macho yake yalikuwa yakiogopesha kwa wakati huo hadi alijishangaa kulikoni anatii?



"Nilidhani utakuwa na akili ila inaonekana wewe ni mpumbavu na siku zote wapumbavu hujidhihirisha kupitia upumbavu wao yaani pamoja na kushobokea nyumba za watu lakini unataka kuanzisha na vurugu pia...Asee katika wapumbavu niliokutana nao nakupa namba kumi" Jimmy aliongea



"Wewe mshenzi nyamanza, Abuu mshikisheni adabu huyu punguani hakikisheni mnamvunja na mguu tuone kama ataendelea kuongea pumba" alimaka Beka na palepale baunsa aitwaye Abuu akiongozana wenzake walimsogelea Jimmy wakidhamiria kutekeleza kile walichoambiwa



Jimmy hakusogea alisimama palepale na Abuu baada ya kumsogelea alinyanyua mikono yake akitaka kumkunja vest yake na kumtandika utosi na kichwa chake kigumu kama jiwe



Lakini kabla hata mikono yake haijatua alishtukia kofi la uso kama wahindi wanavyowatandikaga maadui kwenye muvi na hata hakuelewa limemfikiaje

Halikuwa kofi la kitoto hata kidogo, lilisikika nyumba nzima, kofi lile lilimyumbisha Abuu na kurudi nyuma hatua nne na kutema mate yalichanganyika na damu pamoja na meno mawili



Mabaunsa wenzake wawili baada ya kushuhudia kitendo kile walipigwa na butwaa na kusita kidogo, walijiambia inawezekanaje mtu mwenye mwili wa kawaida tu wa mazoezi na kuonekana mwepesi kuweza kumpiga baunsa kofi lenye madhara kama yale, tena jitu lizito lililotuna na kukomaa mwili na mifupa. Hakika ilishangaza hata Beka macho yalimtoka pia bila kumsahau Zuhura na wenzake



"Pumbavu unathubutu vipi kunipiga kofi!" Abuu alimaka kwa hasira



"Nikufahamishe mapema nikishamaliza kudili na nyinyi pamoja na boss wenu unasafisha huo uchafu wako hapo chini" aliongea Jimmy bila ya kujali hasira ya baunsa huyo



"Mnazubaa nini mshambuliani kwa pamoja huyo" Beka alifoka



Mabaunsa mara baada ya kumsikia boss wao akifoka wote kwa pamoja walichomoa fimbo flani hivi ndogo za chuma zijulikanazo kwa kingereza kama batons ambazo hutumiwa na walinzi(security guards/bodyguards). Walibonyeza kitufe kilicho karibu na sehemu ya kushikia na urefu kuongezeka mpaka inchi ishirini na nne(24 inches)



Palepale kwa kasi kulingana na uzito wa miili yao walimsogelea Jimmy wakimshambulia kwa pamoja kutumia fimbo zile



Jimmy alizikwepa kwa ustadi wa hali ya juu bila kusogea sana pale aliposimama, alikuwa akikwepa na kupiga kupiga hatua mbili kusini, hatua mbili mashariki, harua mbili magharibi, hatua mbili kazini. Alikuwa akikwepa kwa mtindo huo huku akiuchezesha na kuuzungusha mwili wake kwa ustadi wa hali ya juu sana na kama vile alikuwa akicheza mchanganyiko wa Tango na rhumba



Walishambulia mpaka walichoka lakini hakuna hata fimbo moja iliyomgusa na sasa Jimmy alichukulia fursa ya wao kuchoka kufanya mashumbulizi yake



"Crack! Crack! Crack!" ilikuwa ni sauti ya kuvunjika kwa mifupa



Wale mabaunsa walipige makelele ya maumivu wakiwa chini na kila mmoja alikuwa ameshika mguu wake na bila shaka Jimmy aliwavunja, ile kauli ya "hakikisheni mnamvunja mguu" kutoka kwa boss wao imegeuka kuwa jukumu la Jimmy.

Upande wa Zuhuru alikuwa ni "wow! What a style!" hakutegemea mwanaume huyo kuwa mtaalamu kwenye suala hilo pia hata hivyo hakuonyesha waziwazi



"Wanaume kupiga kelele mbele ya wanawake haipendezi" aliongea Jimmy na kisha kumgeukia Beka



"Bado unataka kubaki au nikusindikize mlangoni? " aliuliza huku akitabasamu



Tabasamu lile lilitosha kumtoa Beka kijasho cha woga na mdomo wake ulianza kutetema



"Nitaondoka" alijibu na haraka haraka alipiga hatua kutaka kuondoka lakini Jimmy alimzuia kwa mbele wakiangaliana uso kwa uso



"Hey sijasema uondoke nimeuliza kama unataka kubaki au nikusindikize mlangoni ila unaonekana unataka nikusindikize basi sawa nitakusindikiza" aliongea, Jimmy



"Hapana... Unajua... aarggh" kabla hata hajamaliza kuongea alichotwa mtama matata sana na kuanguka chini akijipigiza upande wa kushoto wa komwe lake chini na kuishia kutoa ukelele wa maumivu. Hazikupita hata sekunde tano nundu lilitokelezea tayari



"Tafadhari Jimmy acha unachokifanya inatosha" aliongea Bianca akiwa na wasiwasi



"Unajua mimi ni nani eeh... Aargggh mamaaa!" aliongea Beka na sauti yake ya kuugulia maumivu na Jimmy alimuongezea teke lililomvunja goti lake na kutoa ukelele wa maumivu



"Mama? Hakuna mama hapa we pimbi"



"Jimmy acha!" Bianca aliongea kwa sauti ya juu



"Oh sawa nitaacha" aliongea



"Yaani tangu urudi umekuwa ni wa kunitia hasira tu na ona sasa haijapita hata siku tumeanza kuishi lakini ushanisababishia matatizo unajua Beka ni mtoto wa nani?" aliongea Bianca akilipukwa na hasira



"Si huyu hapa alikuwa anataka kuleta vurugu ndio nimechukua jukumu la kuzuia"



"kuzuia? Kuwavunja miguu ndio kuzuia? Hivi unajua hata baba yake ni nani?"



"Baba yake mimi simjui na sitataka kumjua" aliongea Jimmy



"Baba yake ni waziri wa sanaa na michezo we mkorofi" aliongea huku mishipa ikionekana kwenye paji lake



"Oh lumbe!" Jimmy hakushtuka



"Unapata wapi ujasiri wa kusema "oh kumbe" yaani unataka niletewe vikwazo kwenye kazi yangu kwa makosa yako?"



"Madam tafadhali usikasirike" aliongea Zuhura huku akimwangalia Jimmy kwa macho ya ajabu kweli, alitamani kumshushia kichapo kwa kumkasirisha boss wake lakini alichoshuhudia hakuthubutu hata kumsogelea kwa kuhofia kutolewa meno, Ingekuwa ni jana yake angekuwa na ujasiri huo kwasababu ya kutokujua lakini hapo tayari ashajua sasa kwamba ana mafunzo na kama aliweza kudili na mabaunsa kirahisi tu yeye ni nani?



"Usiwaze sana babe nitajua jinsi ya kufanya ikitokea au ushasahau mimi ni mwanasheria?" aliongea Jimmy na Bianca aliposikia kauli hiyo kutoka kwa Jimmy hakujua hata afanye nini alijiambia yaani bado tu huyu mkorofi anapata muda wa kumuita babe?



Aliona kuendelea kubaki hapo ataishia kukasirishwa zaidi na zaidi hivyo aliondoka akipandisha zake juu



"Haya ninyi pimbi safisheni huo uchafu wenu na muondoke hapa haraka iwezekanavyo vinginevyo msinilaumu kwa luwavunja mguu mwingine



Abuu harakaharaka alienda kufuta mate yake kwa shati lake jeusi na kuokota meno yake kisha yeye, wenzake na boss wake Beka kwa kuburuza miguu yao iliyovunjwa walitoka humo ndani lakini Beka kabla hajapotelea mlangoni aligeuka na kuongea



"Utajutia sana kwa hiki kitendo ulichokifanya" aliongea na Jimmy aliishia tu kumpa tabasamu na kumtishia kwa ishara kuwa anakuja kumvunja mguu mwingine akiendelea kusimama hapo mlangoni



Beka alishtuka na haraka japo kwa tabu alijivuta na kuondoka na sekundechache zilisikika ngurumo za gari kuondoka na Jimmy alijinyoosha mikono yake na kutulia lidogo akisimama pale sebuleni



Wakati amesimama alihissi kuangaliwa sana na ni kweli Zuhura alikuwa akimuangalia kana kwamba anataka kummeza



TO BE CONTINUED........
 
By Samuel jk_Euphoria

SOLO KING: ANCIENT LEGACY

CHAPTER 23: Mimi sio mtu mbaya


Upande mwingine ndani ya chumba kwenye kitanda kikubwa chenye inchi themanini na nne urefu na upana Bianca alikuwa amekaa kitandani akiwa katika hali ya mawazo


Chumba chake kilikuwa ni kikubwa kilichosambaa harufu nzuri ya kike, kulikuwa na shelve la vitabu mbalimbali, kulikuwa pia na masofa ya bei ghali, upande wa dirishani kulikuwa na piano kubwa ya mbao, japokuwa hakukuwa na viyu vingi sana licha ya ukubwa wa chumba lakini kilipambwa kikike zaidi na kupambika.


Bianca alikuwa amekaa akitulia tuli akitazama dhini, kwa jinsi alivyoonekana alikuwa ni mpweke sana na alitia huruma haswaa


Alinyanyua kichwa chake na kutazama upande wa dirisha kubwa la kioo kama ukuta, macho yake yalikazia ile piano kubwa ya mbao. Taratibu alinyanyuka na kutembea kuisogelea piano ile na kisha kukaa kwenye kistuli mfano wa benchi dog


Aliipitisha mikono yake juu ya kinanda kile cha mbao kwa mtindo kama wa kuburuza ni kama vile ameimisi sana na alisitisha mara baada ya macho yake kutua kwenye sehemu ambayo "sheet music" iliyojaa alama za muziki hupatikana, ni ile sehemu ya juu katikati ya kinanda


Lakini sehemu hiyo hakukuwa "sheet music" bali kulikuwa na karatasi nyingine ngumu na katika karatasi hiyo kulikuwa na sanaa ya uchoraji ikidhihirika, ilichorwa mwanaume na mwanamke kwa ustadi wa hali ya juu sana, ulikuwa ni mchoro wa viwango vya kimataifa kiasi kwamba ilionekana ni kama vile picha imepigwa


Mwanaume aliyexhorwa alikuwa ni Jimmy na hakika mchoraji hakukosea alimpatia haswaa na hakukuwa na kasoro yoyote vivyo hivyo kwa mwanamke aliyechorwa ambaye ni Bianca


Walikuwa katika pozi la kirafiki sana pengine ungedhania labda ni wapenzi, walikuwa wamesimama Bianca akimgeukia Jimmy na kumkumbatia ubavu huku mguu moja akiunyanyua na kuukunja, mkono wake akiwa ameunyanyua na kuusogeza karibo na uso wake uliopendezeshwa na tabasamu akiweka ishara ya amani, yaani vidole viwili(shahada na cha kati) vikisimama na vingine vikiwa vimekunjwa na mkono mwingine alkiupitisha kwenye bega la jimmy ambaye naye alikuwa katika tabasamu na pozi linaloendana vizuri na pozi la Bianca, vichwa vyap vilikuwa karibu kiasi cha mashavu yao kugusana.


Huo ndio ulikuwa mwonekana wa mchoro uliokuwa kwenye karatasi ambalo Bianca alikuwa akilitazama.
Aliupeleka mkono wake na kuishika ile karatasi upande wa mwaume na kuachia tabasamu la upole sana.


Mchoro huo ulikuwa ni picha waliyoipiga miaka mitano nyuma kabla ya kuondoka kwenda masomoni nchini Uingereza. Na alipokuwa uingereza alikutana na rafiki ambaye kazi yake ilikuwa ni kuchora na kumuomba amvhoree picha hiyo na kumlipa kabisa.


"Unaona mmh" aliongea kwa sauti ya upole akiangalia mchoro huo


"Upendo wamgu kwako ulikuwa na wa kunishangaza sana, sikuelewa ulitokana na nini nilipenda ghafla tu kama cheche itokezayo kwenye giza totoro pasipo kujua chanzo, moyo wangu ulikupenda siku ya kwanza mukuona kwa macho, na nilikupenda zaidi nilipokuona ukicheza moonlight sonata na nilizidi kukupenda mara kumi yake uliponiokoa mimi na kaka yangu katika tukio. Ni kama vile nafsi yangu ilikutambua bila hata mimi kujua" aliongea kwa utulivu kisha kunyamanza akiendelea kukazia macho mchoro


"Like a song I’d never heard before, but somehow knew all the lyrics. Like waking up one morning and the sky just felt bluer, the air so sweeter, But why?" aliendesha akimaanisha "Ni kama wimbo ambao sikuwahi kuusikia hapo kabla lakini kwa namna fulani nilijua maneno yake. Kama vile kuamka asubuhi moja na kuhisi anga kuwa safi, hewa tamu, lakini kwanini?"


"Kwanini uliondoka? Kwanini? Kwanini hukuitimiza ahadi? Au kwasababu ulishaijua siri yangu kabla sijakwambia? Mmmh?" alikuwa akiuliza maswali mfululizo kana kwamba huo mchoro ndio Jimmy halisi


Baada ya kuongea hivyo aliutoa mkono wake kwenye karatasi na kunyanyua mkono mwingine kisha yote aliielekeza kwenye keys za piano hiyo


Taratibu alianza kuibonyeza bonyeza kwa utulivu na kwa ustadi sana, haikuwa haraka haraka bali ni polepole na mpangalio wa sauti nzuri sana ulisikika, japokuwa hakubobea sana kwenye kucheza piano lakini mziki huo ulikuwa na ubora


Uzuri chumba hiko kilikuwa ni sound proof hivyo sauti ziliishia humohumo. Baada ya kama dakika tano za sauti kusambaa chumba kizima hatimae alisitisha kucheza na chozi lilianza kumdondoka na haraka haraka alifuta


°°°°°°°°°°°


Jimmy alikuwa akijiambia "kuna nini kwani mbona ananiangalia sana huyu manzi" huku akipeleka mkono wake wa kulia nyuma ya kisogo na kukikuna


"Kuwa na amani bibie, pia manzi kama wewe kumkata jicho mtu bila sababu haipendezi unaonaje ukitabasamu


" Koma kuniita kuniita bibie na leo ni mwanzo na mwisho kuniita hivyo, tumeelewana?"


"Nimekuelewa bibie" aliongea Jimmy huku akimtolea tabasamu


"Yaani wewe.... Laiti ungejua nini kinakwenda kutokea kutokea baadae usingethubutu kufanya ukatili" aliongea huku amekunja sura yake kana kwamba amemeza dawa chungu


"Ukatili gani kwani mi nilichofanya ni kuwafunza jinsi ya kuwa na heshima kwenye nyumba za watu anyway nina njaa sana" aliongea na kumpotezea Zuhura na kwenda zake uelekeo wa jikonina kuwakuta Sandra na Aisha wakimalizia kuandaa cha kula


Zuhura aliishia kumsindikiza na macho mwanaume huyo mpaka anapotelea jikoni na kutingisha kichwa kwa masikitiko, kisha aliwapa ishara wenzake waondoke, wale walinzi wawili kufafa maagizo tu pengine utadhani ni mabubu maana muda wote ni kimya tu hata kupiga chafya hakuna! Ni kimyaaaa.


"Kuna kitu unataka Sir?" aliongea Sandra kwa wasiwasi alipomuona Jimmy ameingia Jikoni


Ukweli ni kwamba Sandra na Aisha walishuhudia kila kitu kilichotokea sebuleni na vile tu hawakuwa na ujasiri wa kujitokeza na kuangaliza ni vile vitabia vya wadada kupenda umbea ndio viliwafikisha huko, waliposikia sauti ya kofi tu iliwashtua na kutaka kujua kulikoni.


Kitendo cha kushuhudia, Jimmy akiwavunja wageni miguu bila wasiwasi wala hati ilihali na yeye ni mgeni kiliwafannya wamuogope. Ni jana tu hapo alikuja na ni mtoto wa boss wao mkubwa(mwanamama Mary) lakini waliweza kushudia upande wake mwingine. Walijiuliza itakuwaje huko mbeleni wakimkasirisha? Je atawavunja miguu? Kufikiria hivyo ilikuwa ni haki yao kuwa na hofu


Jimmy aliweza kujua wasiwasi wake unatokana nini na alitaka kumtoa wasiwasi maana uwepo wake utawafanya wasiwe na amani kila siku na hakutaka iwe hivyo


"Nina hamu tu ya kula matunda" aliongea Jimmy kirafiki


"Una njaa? Bado kidogo tu tunamalizia utuvumilie kidogo" aliongea Sandra kwawasiwasiwasi na kufanya vitu haraka haraka


"Aisha muandalie bwana mdogo matunda" Sandra alimwambia mwenzake huku akiendelea na shughuli ya kuandaa msosi haraka haraka


Naye Aisha haraka haraka alisogelea friji na kulifungua na kutoa matufaa manne na kisha kuyaosha na kuanza kuyakatata


Jimmy alikuwa hajui nini cha kufanya, alitamani kucheka lakini hakuthubutu kufanya hivyo na alisubiri mpaka Aisha alipomaliza kumuandalia na kumpatia sahani iliyojaa vipande vya matufaa na alipokea kisha taratibu alianza kuondoka


Alipoufikia mlango wa jikoni alisimama na kuwageukia vijakazi wale nao walimwangalia wakijua anataka kuwaambia kitu


Jimmy alitoa tabasamu la kirafiki na kuongea


"Kuweni na amani, mimi sio mtu mbaya" kisha alichukua kipande cha tufaa na kukipeleka mdomoni na kugauka kuondoka zake


Upande wa Sandra na Aisha waliishia kumuangalia akiondoka na angalau nafsi zao zilitulia ni kama sauti ya Jimmy yalikuwa na nguvu flani hivi ya amani ndani yake na ilipowafikia masikioni walitulia na ule uharakishaji wa mambo wakaacha na kuendelea na kumalizia kuandaa bila wasiwasi


Jimmy alikwenda kukaa zake sebuleni kwenye sofa na kula vipande vya tufaa huku akitazama runinga kubwa iliyoko mbele ya macho yake na muda huo ilikuwa ikionyeshwa taarifa ya habari.


Kichwa cha habari kwenye runinga kilikuwa kikisomeka VIFO VYA KUTATANISHA NA UPOTEVU WA RAIA MKOANI TANGA


Na katika skrini alionekana mwanamke mtu mzima mweusi wa ngozi akivalia miwani ya macho


"Habari za mchana. Tunakatiza matangazo ya kawaida kuwaletea taarifa ya dharura kutoka mkoa wa Tanga. Ripoti zinaeleza juu ya matukio ya kutoweka kwa watu na vifo vya ajabu katika kijiji kidogo kilichopo ndani kabisa ya msitu, katika Wilaya ya Tanga" aliongea na sauti yake yenye kusikika vyema


"Kulingana na vyanzo vya ndani, ndani ya saa arobaini na nane zilizopita, watu zaidi ya kumi na wawili wametoweka. Mamlaka zimethibitisha kuwa miili mitano imepatikana yote bila majeraha ya wazi, lakini ikiwa imetokwa damu yote." aliendelea na kisha kuonyeshwa raia mbalimbali wakitoa maoni


" Hawana majeraha… lakini wanakufa ghafla… kama wamekamatwa na pepo" aliongea mkazi mmoja kwa sauti ya kutetemeka


"Kila siku usiku watu wanapotea. Tunahisi kuna kitu kinaishi gizani.” aliongea mwingine na kisha mtangazaji alionyeshwa tena


" Jeshi la Polisi limeanzisha uchunguzi, lakini hadi sasa wameshindwa kuelewa kilichotokea. Wengine wanaamini huenda ni kazi ya kundi la ibada haramu au virusi visivyojulikana. Lakini wengine wana hofu… ya kitu kibaya zaidi.”


"Wakazi wanashauriwa kukaa ndani baada ya jua kutua, na kuripoti matukio yoyote ya ajabu. Kwa sasa, eneo hilo limewekwa chini ya uangalizi mkali. Tutaendelea kuwaletea taarifa zaidi kuhusu tukio hili kadri linavyoendelea. Tanga pamekuwa mahali pa utulivu kwa muda mrefu… lakini hivi karibuni kumekuwa na hofu .”


Kisha taarifa ya habari ikatoweka na kurudishwa kipindi kilichokuwa kikionyeshwa hapo kabla.


Jimmy alikuwa akila vipande mpaka vikaisha na baada ya habari kutoweka alianza kutafakari juu ya suala na palepale alikumbuka kuhusu wale viumba wanywa damu aliowashuhudia miaka tano iliyopita na palepale alipata majibu juu ya utata wa vifo


"Ina maana wale mashetani bado wapo wanaranda ramda wapendavyo" alijiwazia Jimmy kisha kupotezea


Harufu ya chakula kitamu ambacho maandalizi yake yalikamilika na kuwekwa mezani tayari kwa kula ililisumbua tumbo lake ambalo halikuridhika na matunda


Hakutaka kuendelea kuteseka na njaa na aliachana na kutazama runimga na kusimama kuelekea kwenye "dining table" lakini kabla hajafika aliweza kumuona mrembo Bianca akishuka chini kwenye ngazi


Alikuwa amebadili nguo na kuvaa kinyumbani zaidi alikuwa amevaa t-sheti kubwa oversize rangi nyeupe na kikaptula kifupi kilichoacha mapaja yake meupe wazi, pia alikuwa akinukia harufu nzur sana, haikueleweka ni marashi ya aina gani lakini yaliifurahisha pua ya kila mwenye kuinusa


Kama mwanaume alianza kupatwa na hisia na mawazo ya ajabu ajabu kichwani mwake kiasi cha kusahau kama alikuwa ana njaa muda huo


"Unazubaa nini?" ilikuwa ni sauti kutoka kwa Bianca na kumtoa Jimmy kwenye mawazo ya kikuda


"Nashangaa uumbaji wa Mungu na ujuzi wake katika hakika hakukosea ni alitumia muda mwingi na kwa umakini mkubwa kukuumba" aliongea Jimmy bila aibu


"Unafiki tu unadhani sijui unachokiwaza kichwani mwako? Halafu sio kama hujawahi kuona mwanamke"


"Hata kama nimeona lakini kwako nikikutazama ni kama ndiyo mara yangu ya kwanza" aliongea huku akitabasamu


"Sitaki kusikia ujinga wako" aliongea Bianca na kumpita. Jimmy alifumba macho kuisikilizia harufu nzuri ya mwanamke huyo alipompita karibu yake na kujiambia "Asee kwa staili hii sidhani kama nitaweza kuvumilia kadri siku zitakavyosonga" na kuelekeza macho yake chini mpaka katika ya mapaja na mwanajeshi wake alikuwa tayari ameshajipanga kwa vita lakini kwa bahati mbaya hakukuwa na vita


Uzuri singlendi yake ilikuwa kubwa na kusitiri hali ile na kufanya iwe ngumu kugundilika na hilo alishukuru alijiambia ingekuwaje kama angevaa shati na kuchomekea? Si angeonekana ni kitombi?


Basi naye alikwenda mezani kwa ajili ya kula, alipoketi vijakazi Sandra na Aisha walichukua jukumu la kuwapakulia maboss wao
Sandra kwa Jimmy na Aisha kwa Bianca na walipomaliza walitaka kuondoka lakini Jimmy aliwazuia


"Mmekula?" aliwauliza


"Hapana ndio tunaenda kula" Aisha alijibu


"Wapi, jikoni? Kwanini msiungane na sisi, chakula huwa ni kitamu zaidi kinapoliwa na wsmgi" Jimmy aliwakaribisha mezani na bila ubishi walikubaliana nae na kupakua chakula chao kisha kuka


"Vipi kuhusu walinzi hawali?" Jimmy aliuliza


"Wameshakula" alijibu Bianca bila ya kumuangalia, umakini wake ulikuwa kwenye chakula


"Ooh bila shaka itakuwa wana na ratiba yao ya kula wanapokuwa kazini lakini vipi kuhusu yule mzee pale getini" aliongea Jimmy


"Yule hana ratiba maalumu ya kula, ni muda wowote tu anakula hivyo tunamwekea chakula jikoni akiwa na njaa anapitia mlangovwa pili na kuingia jikoni kupakua chakula" Sandra alieleza na Jimmy alitingisha kichwa kumuelewa na sasa alianza kula


Ulikuwa ni wali, samaki mboga za majani na matunda mchanganyiko


Alichota kijiko kimoja cha wali na kukipeleka mdomoni na alipomeza tu ghafla kundi la watu watatu waliovalia sare za polisi waliingia ndani na kumfanya Jimmy akunje ndita na kulaani ndani kwa ndani


"Samahani kwa ujio wetu wa ghafla lakini tupo hapa kwa mtu anayeitwa jimmy" aliongea Inspecta kolo


"Ni mimi afande kuna shida kwani?" aliongea Jimmy


"Tafadhali ongozana na sisi mpaka kituo cha polisi una kosa la kumshambulia raia pasipo sababu pili ni unyanyasaji" aliongea inspekta kolo na kumpa ishara wa pembeni yakre kwenda kumpiga pingu Jimmy


"Hey kwanini msisubiri nimalize kula kwanza nina njaa ujue" aliongea Jimmy huku akipeleka kijiko kuchota wali mwingine na kuupeleka mdomoni


TO BE CONTINUED........
 
Kauli ya kibabe kutoka kwa Jimmy 😂😂👇

Screenshot_20250609-190446_1.jpg
 
By Samuel jk_Euphoria

SOLO KING: ANCIENT LEGACY

CHAPTER 24: Uoga hufanya watu kuwa dhaifu


Bianca alionekana kutegemea ujio wa polisi kutokana na kile Jimmy aliwafanya Beka na walinzi wake lakini hakudhani ingekuwa ni mapema hivyo

"Tafadhari naomba utoe ushirikiano vinginevyo tutatumia nguvu" aliongea askari alipomsogelea Jimmy

Jimmy alishusha pumzi nyingi kisha kusimama na kumnyooshea mikono na askari bila kuchelewa alimfunga pingu

"Sawa sikatai kuhusu kushambulia maana walistahili lakini kuhusu unyanyasaji unakosea, hivi unajua kuhusu unyanyasaji afande?" Jimmy aliuliza akimwangalia Inspekta kolo

"Kuhusu hilo tutajua tukishafika kituoni" aliongea Inspekta kolo na kumgeukia Bianca

"Samahani sana madam kwa kuvamia muda kama huu lakini sisi kama wanausalama tunafanya ni kufata maagizo kutoka juu natumai umeelewa" aliongea Inspketa kolo, alikuwa akimjua Bianca sio kwasababu ya kuwa maarufu kwa usanii bali ni kwasababu ni mtoto wa Boss lady nchini. Hakunaasiyemjua mwanamama Velora, ni Tajiri anayeshika nafasi ya kwanza kwenye jinsia ke nchini na nafasi ya tatu tukimjulisha jinsia zote, bila kusahau connection alizokuwa nazo

Alikuwa na ukaribu na hadi raisi wa nchi, sasa Bianca akiamua kumpia bimkubwa na kumwambia anataka Jimmy aachiwe ni ndani ya chache tu inspekta kolo kupewa amri kwa mkubwa wake wa kazi amuachie.

Bianca alitabasamu tu na kumwangalia Jimmy kisha kumgeukia Inspekta na kutaka kuongea lakini Jimmy aliingilia kati

"Umesema kuvamia sasa una tofaiti gani na wale kunguni waliovamia na bado wakataka kuanzisha vurugu?" alimulliza, Kauli hiyo ilitosha kabisa kumkasirisha Inspekta kolo

"Pumbavu! Kaa kimya wewe" Inspekta kolo alifoka

"You dare Insult me infront of my woman?" Jimmy aliongea huku amekunja ndita akimaanisha unarhubitu kunitukana mbele ya mwanamke wangu

Upande wa askari aliyemfunga pingu alitaka kuchukua hatua ya kumtoa pale alipo kwa nguvu, alitaka kumshika Jimmy Tanganyika jeki lakini hata hajanyanyua mkono Jimmy alimkata jicho la uovu ni kama vile alikuwa anamwambia "Usijaribu huo ujinga" ilionekana kama vile alikuwa kwenye mawazo ya huyo

Lakini siku zote asiyesikia la mkuu huvunjika guu askari licha ya kupewa onyo hilo alijikuta mbishi sana na mjuaji na palepale aliupeleka mkono wake kutaka kushika suruali ya Jimmy lakini kabla hata mkono haujafika Jimmy aliudaka na kuuweka begani kwa ustadi kisha kama vile anavuta kamba iliyofungwa mtini alimnyanyua na kumbwaga kwenyw meza ya chakula na kutoa sauti ya mwili kugongana na meza

Kilikuwa ni kitendo cha sekunde moja pekee, askari huyo alikuwa ana bahati sana Jimmy hakutumia nguvu nyingi vinginevyo angevunja uti wake wa mgongo na meza kukatika nusu

Askari alikuwa akiugulia maumivu makali hata sauti isiweze kumtoka ni mikunjo ya sura yake ilitosha kueleza ni maumivu kiasi gani anayohisi, upande wa Inspekta kolo, Bianca na wengine wote walishtuka maana hawakutegemea Jimmy kwenda mbali hivyo

Uzuri sehemu ya meza aliyombwaga askari yule haikuwa na chakula na ni mtikisiko uliofanya chakula kimwage kiasi juu ya meza

Bianca, Sandra na Aisha waliokuwa wamekaa walisimama nyuso zao, zikiwa na wasiwasi

Inspekta kolo haraka haraka alichomoa bastola iliyokuwa kiunoni mwake na kumnyooshea vivyo hivyo kwa askari mwingine

"Uko chini ya ulinzi ukidhubutu kufanya ujinga natoboa miguu yako hiyo" aliongea Inspekta kolo akiwa Siriaz

"Tafadharini sitaki vurugu kwenye nyumba yangu" Bianca aliongea japo kwa wasiwasi na kumgeukia Jimmy

"Nakuomba Jimmy toa ushirikiano nitaangalia namna ya kukutoa" aliongea huku akimwangalia kwa macho yenye wasuwasi

Jimmy alifarijika kuona kwamba Bianca anamjali licha ya kumsusia na alishusha pumzi nyingi na kumpa ishara Inspekta kolo kwamba anatoa ushirikiano, naye inspekta alimpa ishara askari wake mwingine

Yule askari slimsogelea, Jimmy na kumpa ishara aongoze njia ni wazi hakutaka kukurupuka kama mwenzaka, baada ya kumpa ishara Jimmy alitembea kuelekea mlangoni huku nyuma akifuatwa na askari wawili mmoja akitembea kwa tabu sana

Inspekta kolo baada ya kuona mambo yamekuwa maraisi naye aligeuka kuondoka, Jimmy na wale askari kabla hawajavuka mlango, Bianca aliongea

"Subiri...." aliongea na Jimmy pamoja na askari walisimama na kumuangalia

"Nitaongozana nanyi" aliendelea

"Babe usisumbuke kuja mpaka kituoni we ni subiri nitarudi sawa" aliongea Jimmy akimwita Bianca babe bila aibu

"Nimetumia muda mrefu sana kujifanya sijali. Lakini najali. We mjinga, najali sana mpaka inauma, uliwahi kuondoka na kuchukua muda mrefu kurudi sitaruhusu itokee tena, nakuja",Bianca aliongea huku macho yake yakijawa na maji maji

"Lakini si umesema unaangalia namna ya kunitoa?" aliuliza

"Usiwe na wasiwasi nitarudi niamini awamu hii sawa? Unachotakiwa ni kunisaidia kitu kimoja tu" Jimmy aliendelea kuongea

"Ni nini?" aliuliza

"Just a little prayer" Jimmy aliongea huku akitabasamu

"Usiporudi siku nikikuona naapa nitakuua Jimmy" Bianca aliongea huku akifuta chozi ambalo lilikuwa linakaribia kumtoka

Baada ya kumaliza kuongea hivyo Inspekta kolo Jimmy na, askari wawili waliondoma na kuingia kwenye difenda waliyokuja nayo

Upande wa Bianca baada ya Jimmy kukamatwa na polisi alichukua simu yake iliyokuwa mfukoni kwenye kikaptura chake kisha kupiga simu na kuiweka sikioni

°°°°°°°°°°

Upande mwingine barabarani difenda ilikuwa kwenye mwendo wa wastani huku nyuma sehemu ya kupakia wahalifu Jimmy alikuwa amekaa kwa kutulia pembeni yake alikaa askari mmoja na mbele yake alikaa Inspekta kolo huku dereva wa gari hilo akiwa ni yule askari alichezea kipigo

Dakika zilizidi kwenda na gari kukata kona kadha wa kadha lakini bado hawakufika kituoni na ilionekana hawatafija kituoni hivi karibuni na Jimmy palepale alitabasamu baada ya kuwashtukia

"Kiasi gani umelipwa?" Jimmy alimuuliza

"Sisi ni watu wazima haina haja ya kufichana ilihali ajenda yenu nishaigundua" aliendesha kuongea

"Haha sio mbaya nikafunguka maana sidhani kama utaliona jua la asubuhi" aliongea inspekta kolo

"Ooh niambie adande"

"Kifupi ni kwamba umechokoza mtu ambaye si sahihi kuchokozwa"

"Ndo naniliu.. ooh beka?"

"Hukutakiwa kumchokoza kabisa"

"Sawa ni kiasi gani umelipwa kufanya uhalifu?"

"Uhalifu? acha kuongea upuuzi kijana mimi ninachofanya ni kufata maagizo ya kukukabithi kwa mabosi zangu"

"Huo ni sawa na utekaji afande, kibaya zaidi utekaji unsfanywa na inspekta asee hii ina wapumbavu wengi sana wanaoendeshwa na tamaa badala ya kulitumikia taifa ipasavyo"

"paah" ilikuwa ni sauti ya kofi lkutua kwenye shavu la Jimmy na aligeuka upande wa kushoto kusikilizia maumivu

Sio kama hakuliona hilo ni kwamba tu aliacha kofi litue kwenye shavu lake

"Ni muda mrefu sana sijachezea vibao, mara ya mwisho ilikuwa ni miaka mitatu iliyopita asante sana afande" aliongea Jimmy

"paah" alikuwa kibao kingine kilichomgeuza aangalie upande wa kulia na kukutana macho kwa macho na askari mwingine aliishia kumpa tabasamu kisha akamgeukia inspekta

"Unajua nini afande? Nakupa namba tano" aliongea Jimmy

"Namba tano ya nini we mpuuzi?" aliuliza akiwa bado hajamuelewa

"Ya wapumbavu niliowahi kukutana nao" aliongea, Inspekta kolo alipandwa na hasira kiasi cha kumchomoa bastola yake na kumyooshea kwenye paji la uso wa jimmy na kugusana kabisa

"Kaa kimya we mshenzi nitakufyatua ubongo wako kuwarihisishia kazi mabosa mabosi wangu" aliongea huku aking'ata meno kwa hasira

"kwahiyo unanitisha si ndio? Unajua nini kinafanya watu wawe dhaifu afande? " aliongea Jimmy akiwa hana wasiwasi wowote ni kama vile kunyooshewa bastola kwake ni jambo la kawaida

"Ni uoga afande, it's fear! Uoga hufanya watu kuwa dhaifu, Hofu ni pingu zisizoonekana ambazo huwafunga wenye nguvu, humgeuza simba kuwa kondoo. Hununua uongo, huzika tumaini, na hula ndani kwa ndani hadi mtu asahau yeye ni nani ila sio mimi, kuhusu mimi ni nani tutajua huko mbeleni

Hofu ndiyo adui halisi. Sio risasi kwenye bastola, wala kisu shingoni la hasha. Ni sauti ndani ya kichwa chako. Ile inayokuambia huwezi, Tulia utakufa, hauna nguvu. ni sawa na wadudu wanaokula imani yako, wakimea ukimya, na kukuau taratibu kama unadhani kuninyooshea bastola kutanitisha basi unakosea."

"Kwangu mimi neno hofu na hisia za uoga hazipo ndani yangu nilishazizika miaka mitano nyuma" Jimmy aliongea kwa ujasiri mno mpaka Inspekta alishangas na kujiamnia huo ujasiri ameupata wapi

Taratibu Inspekta kolo alitoa bastola yake kwenye paji la uso na kuirudisha mahali pake

"Ni ujasiri ulioje ulionao! Ngoja tuone utafikisha wapi huo ujasiri" aliongea Inspekta kolo na mara alipomaliza kauli hiyo gari lilisimama

"Tumefika!" aliongea Inspekta kolo na kuwa wa kwanza kushuka akafata askari kisha Jimmy

Lilikuwa ni eneo lenye uwazi mkubwa na vumbi jingi lisababishwalo na upepo kulikuwa pia na majengo mawili ya ghorofa ambao ujenzi wao haukukamilika

Waliposhuka walikuja watu wawili karibu na difenda hiyo, wanaume wawili wenye sura mbaya zenye makovu mengi usoni, walikuwa weusi tii Jummy alijiambia Jini kabula ana afadhali maana sio kwa sura hizo

"Yule mshenzi ndiyo huyu?" aliuliza mmoja wa wale wanaume wawili na Inspekta kolo alikubaliana naye

Yule mwingine alichomoa bahasha na kumrushia Inspekta kolo naye alilidaka na kufungua kisha kuchungulia na kutoa tabasamu la kuridhika

Baada ya tabasamu yeye na askari wake waliingia kwenye difenda na kuondoka wakimuacha Jimmy akiangaliana na wale watu wawili

"Tembea we fala!" aliongea mmoja kwa sauti ya kuamrisha yenye mkwaruzo iliyoadhiriwa na bangi

Jimmy alijiambia ngoja atii na kuona mwisho wake na alianza kutembea kwenda mbele akisukumwa sukumwa mpaka jengo moja wapo na baada ya kuingia ndani ya jengo hilo floor ya chini kabisa aliweza kuona kundi la wanaume wasiopungua kumi, kila mmoja akisimama kwenye angle yake na katikati kabisa kulikuwa kuna kiti na bila shaka kilikuwa ni kwaajili yake kukaa

"Sio mbaya huduma yenu ni nzuri, hadi kiti mmeniandalia" aliongea kama utani vile na kukaa kwenye kile kiti kisha kuwaangalia wale wanaume wawili waliokuja nao

"Mnaonaje kabla ya kuanza shughuli zenu mkinipatia chakula kwanza nina njaa sana" aliongea kana kwamba yeye ndiye boss wa hao majambazi

"We fala kama sio boss kutupa maagizo kutokukufanya chochote kabla hajafika ningekwishakuvunja miguu yako"

"kumbe!, inaonekana boss wenu ana akili sana sio mbaya. Wakati tunamsubiri boss wenu kwanini msininunulie msosi kwanza nikala? Isitoshe kwa mtu mnayekwenda kumtesa sio mbaya akafurahia nyakati zake za mwisho za uhuru" aliongea huku akiwaangalia mmoja

"We unaonaje ukienda hapo nje ukanichumie maembe manne mtini, nimeuona muembe hapo" aliongea akimnyooshea mikono yake iliyofungwa na pingu akimtuma

Upande wa yule mtu aliyeambiwa hivyo alitabasamu na kumsogelea karibu zaidi

"Mimi?" aliuliza huku akijinyooshea kidole kana kwamba hakuwa na uhakika kama ni yeye anayetumwa

"Ndio, wewe" alimjibu huku akitabasamu

"Hahaha.. Hahaha!" ghafla alianza kucheka kama kichaaisieleweke nini kimchekeshacho, naye Jimmy aliungana nae kucheka na kuonekana vichaa wawili wanacheka

Hali hiyo ya wao kucheka bila sababu iliwafanya na wengine pia kuungana kwenye kicheko hicho bila kupenda

"Hahaha! Unafurahisha sana haha!"

"Ndio ndio nafurahisha sana haha" Jimmy alijibu huku akiendelea kucheka, Baada ya dakika mbili za kucheka ghafla tu kukawa kimya

"Ata sasa kanichumie maembe" aliongea Jimmy na kumfanya yule mtu kukunja ndita na kwa hasira alinyanyua mguu wake nakutaka kumtandika Jimmy teke la kifua

Lakini ile mguu unakaribia kutua eneo la kifua Jimmy kwa kasi aliudaka ule mguu na kumtupia kushoto huko kama anatupa kiroba cha mchanga na kumrusha mita nne na alipokaa na alisimama haraka kisha kunyanyua kiti na kumpiga mwingine aliyekuwa karibu yake kichwani na alipoteza fahamu palepale kilikuwa ni kitendo cha sekunde mbili tu kwa watu wawili

Licha ya Jimmy kufungwa pingu haikuwa shida kwake kudaka mguu na kunyanyua kitu lilikuwa ni jambo jepesi tu. Jimmy alichokuwa akitaka ni kutaka wao waanze kuchukua hatua na njia rahisi ni kumchokoza aliyekuwa kiongozi wao na alifanikiwa

"Mdundeni huyo mshenzi!" alifoka kwa hasira na wote walitii amri, palepale walianza kumsogelea wakidhamiria kumdunda

Jimmy aliyekuwa amesimama alinyoosha shingo kwa kuligeuza upande wa kulia na kushoto

"Sasahivi ningekuwa nimeshamaliza kula na kushiba ila nyinyi wapumbavu mmenileta huku na bado mnaninyima kula njoeni niwashikishe adabu" alijiongelesha

Wa kwanza kumsogeelea na mbio zake za kiherehere akiwa ameshika rungu mkononi aliishia kupigwa teke aina ya brazilian kick almaarufu kama "question mark kick (?)" na kuangua chini puuh! na kutulia tuli bila mtikisiko wowote mwilini

Ni teke flani hivi kama unachora alama ya kiulizo ndivyo alivyotandikwa huyo bwana kiherehere ni kama vile alikuwa anautiliza mpira uliokuwa unakuja kwa kasi hewani

Wemgine kuona hivyo walipunguza spidi na kuwa makini zaidi lakini waliishia kuchezea kichapo kitakatifu kutoka kwa mtaalamu Jimmy Jairo na kuisoma namba.

Dakika moja tu ilimtosha kuwashughulikia wale viherehere na kuwaacha chini wakiugulia maumivu wengine wakipoteza fahamu

Yule kiongozi alipoona hivyo alichomoa bastola na kufyatua akimlenga Jimmy mguu wa kulia



TO BE CONTINUED.........
 
By Samuel jk_Euphoria

SOLO KING: ANCIENT LEGACY

CHAPTER 25: Triple strikes


Jimmy alikuwa ni wa tahadhari mno, ukweli alishamuona tangu anachomoa bastola na ile risasi inafyatuliwa kumlenga mguu sehemu ya paja alichofanya ni kuweka pingu sehemu ambayo risasi inalenga kwa ustadi na haraka

"Ting!" mlio wa mnyororo mdogo unaounganisha pingu kugongana na risasi ulisikia na risasi kudondokea upande mwingine

Pingu aliyofungwa Jimmy ilikuwa ni imara sanaa, chuma chake kilikuwa ni kigumu hivyo hata mnyororo wake ulikuwa ni imara pia na si rahisi kukatika kwa risasi moja

Yalikuwa ni mahesabu makali sana ya harakaharaka ambayo mtu mwenye akili za kawaida hawezi. Jimmy alikuwa akijua kabisa mnyororo huo wa pingu hauwezi kukatika kwa risasi moja na aliutumia kukinga risasi. Ukiangalia kwenye muvi utaona steringi anakatwa mnyororo wa pingu kwa risasi moja ila kwenye uhalisia ni tofauti kabisa kuna uwezekano mkubwa kuishia kwenye majeraha au kushindwa au vyote kwa pamoja

Kwa lugha nyepesi ni kwamba ilikuwa ni "risky move" iliyofanikiwa, na ni mtu mwenye ujasiri wa hali ya juu na kutohofia pekee ndiye anaweza fanya hivyo akiweka mwili wake rehani kudhuriwa maana kosa kidogo tu risasi inatua kwenye mwili na kama sio kwenye mapumbu basi ni jambo la kushukuru

Upande wa yule kiongozi hakutegemea hilo lakini hakuwa na muda wa kushangaa alifyatua risasi nyingine awamu hii alikuwa akifyatua mfululizo kama kichaa

"Paah! Paah! Paah! Paah!" zilikuwa ni sauti za risasi kufyatuliwa

Jimmy alikuwa na macho yenye kuona mpaka risasi inavyo safiri na ustadi wa hali ya juu alizikwepa risasi zote kwa kuruka sarakasi na kujiviringisha hewani kama mtaalamu

Spidi yake ilikuwa imeongezeka mara tatu ya miaka mitano iliyopita, alikuwa ni mwepesi kama karatasi hivyo kukwepa haikuwa ngumu kwake

"Click! Click!" risasi zilikuwa zimeisha na hakuna hata moja iliyomgusa Jimmy kibaya zaidi hakuwa na magazini nyingine

"Hapana.. Haiwezekani! Binadamu kukwepa risasi haiwezekani.. Wewe ni nani?" aliongea huku akitetemeka na kurudi nyuma kwa woga

"Mimi ni binadamu kama wewe" Jimmy alimjibu huku akitabasamu na kuanza kumsogelea

Mwanaume yule spidi yake ya kurudi nyuma iliongezeka na kugeuka kuanza kukimbia maana hakuwa na jinsi, kwa kichapo alichoshuhudia wenzake wakipewa aliona kabisa hana namna nyingine zaidi ya kukimbis

Hata kama alikuwa ni jasiri ujasiri nao unakikomo kwake kupigana na Jimmy ni sawa na swala kujipeleeka kwa simba mwenye njaa na matokeo yake aliyajua

Jimmy hakujisumbua hata kumfukuzia na chini kwenye sakafu ya simenti aliona rungu, na hakuwa na haja ya kujiuliza afanyie kwani palepale alilipiga teke kama mpira na rungu lile lilifyatuka kwa spidi kubwa na kwenda kumpiga kisogoni na kuanguka ksenda mbele kama vile amejikwaa na kuisgia kubweka kwa maumivu na kushika kisogo chake

Jimmy alimsogelea karibu na kumkanyaga mguu wake na mlio wa cravk! kuashiria mfupa kuvunjika ulisikika

"Aaargh! mama!" alipiga kelele yule mwanaume na Jimmy alichuchuma akimkazia macho

"Ndiyo unamkumbuka mama sasahivi?" Jimmy alimuuliza

"Tafadhari niache usiniue.. Na.. na.. nakuomba" aliongea kwa sauti yenye maumivu na macho yake kuzidi kuwa mekundu akitaka kulia

"Kwanini? Kwasababu umeshindwa kuniua na sasa kibao kimegeukia kwako?"

"Tafadhari" aliomba aachiwe yaani ghafla tu ametoka kuwa jamnazi na sasa alikuwa akiomba kuhurumiwa na Jimmy alitamani kucheka

"Ukweli mimi sipendi kuua sababu naheshimu na najua thamani halisi ya uhai wa mtu, it's priceless ila kuna watu huwa wanaidharau thamani ya uhai wa wenzao lakini ikifikia wakati wao wa kutaka kupoteza uhai wao ndio wanaanza kuona thamani ya uhai na kutaka kuhurumiwa ilihali wao hawakuwahurumia wale waliowatoa uhai na watu kama hao dawa yao ni kuwaua tu na wewe ni mmoja wao" aliongea kwa sauti yenye ubaridi na kumuogopesha mwanaume yule

"Nilikuwa nafata maagizo tu kutoka kwa boss wangu" alianza kujitetea

"Lakini si ulisema boss wako amesema msinishughulikie mpaka atakapokuja?" alimuuliza na mwanaume yule aliishia kubaki kimya mdomo ukimtetema asijue cha kuongea

"Hata hivyo sikulaumu kwa kutotii maagizo ya boss wako maana binadamu tuna machaguzi aidha kutii ama kutotii, kukubali ama kukataa, kuelewa ama kutoelewa, kuamii ama kutoamini yote hayo ni machaguzi yetu, it's choices lakini kupitia hayohayo machaguzi kuna muda yanatugharimu sana na kuna muda yanatunufaisha, kutufaidisha na hata kutuokoa

Boss wako anaweza kukupa amri umsubiri mahali mpaka atakaporudi na katika kusuburi ghafla wanatokea simba je utaendelea kusubiri? Jibu ni hapana hapo unakuwa na machaguzi aidha kuendelea kutii amri ya boss na ufe kwa kuliwa na simba ama kutoendelea kutii na kukimbia kuokoa maisha yako, si unaona mwisho wa yote ni hiari ya kuchagua" Jimmy aliongea kana kwamba anamuhubiria na yule mwanaume hakuthubutu kufungua mdomo na kubaki kuwa msikilizaji

"kwahiyo hata wewe ulikuwa na machaguzi, aidha kwenda kunichumia maembe nile uendelee kutii amri ya boss wako au kinyume chake lakini matokeo yake ukaenda kinyume maana yake umemuasi boss wako" aliendelea

"your boss understood loyalty but failed to understand about freewill..." aliongea kidogo kisha kunyamanza na kukaa chini na kukunja miguu yake kama vile anaongea na rafiki yake aliyelala akimaanisha boss wake alielewa uaminifu lakini akashindwa kuelewa kuhusi hiari

"Anaamini kuwa uaminifu ndio sarafu ya mwisho katika uongozi. Kwamba ikiwa watu wanasimama nawe bila kuuliza maswali basi hao ndio watu bora kuwa nao karibu. Na kwa kiwango fulani, hakuwa na makosa. Uaminifu unaweza kujenga himaya. Unaweza kuleta imani, ufanisi, na mshikamano. Wanajeshi hupigana kwa bidii zaidi wanapokuwa waaminifu. Wafanyakazi hufanya kazi kwa bidii zaidi kwa kampuni wanayoiamini. Familia hukaa pamoja panapokuwa na uaminifu.

Lakini hapa ndipo ukweli ambao viongozi wengi husahau na boss wako ni mmoja wapo ni kwamba uaminifu bila hiari ya kuchagua si kujitolea bali ni utumwa. bosi wako anajua namna ya kuamrisha na kutaka utiifu, lakini hakuwahi kuuliza kwa wale wanaomfuata kama walichagua kufanya hivyo au lah. Hakuelewa kuwa mtu mwaminifu anayechagua kubaki, akijua yuko huru kuondoka muda wowote ni mwenye nguvu zaidi kuliko yule anayebaki kwasababu ya hofu, tamaa na kadhalika yaanianawachukulia kama maroboti yanayopokea maagizo na nyinyi mlivyo wa pumbavu mkiendeshwa na tamaa mnakubali"

"Anyway boss wako ni nani?" alimuuliza na yule mwanaume alianza kujing'atang'ata mdomo akijishauri atoe siri ama aendelee kufunga mdomo na Jimmy kuona hivyo alitabasamu

"Yaani kuhubiri kote huko bado huelewi tu? Ninachokupa ni uchaguzi aidha uniambie boss wako ni nani na nikuache ama upigee imya nikuue"

"Nasema, nasema!" aliongea mwanaumd yule akionekana hayuko tayari kufa

"Boss wangu anajulkana kwa jina la Don mswahili" iongea na kumfanya Jimmy kukunja sura kidogo baada ya kusikia hilo jina na kisha kuwa kawaida

"Ina maana huyu jamaa wa kujiita don mswahili bado yupo tu" alijiongelesha huku akitingisha kimasikitiko na kutabasamu

Katika ulimwengu wa underworld, ulimwengu usiotawaliwa na sheria bali hofu, nguvu na faida tunauita underworld yaani ulimwengu wa wahalifu watu hutumia majina feki.

Kulikuwa na wahalifu wa kila aina yaani kuanzi wauza sembe, magenge ya kihalifu(mafia's), wahalifu wanaosakwa, wauaji wa kulipwa, mafisadi wa nchi n.k wote humo wamo lakini huweza kuta hata mmoja akitumia jina lake halisi zaidi utasikia Don naniliu na majina mengi ungaunga mradi kuficha utambulisho wao. Huu ulimwengu wa siri hufanyika popote pale, iwe ni jirani na unakoishi, nchi fulani au bara fulani, ni kwamba umesambaa kila mahali.

Jimmy aliishia kumuangalia mwanaume yule jambazi ambaye alionekana kutaka kuachwa hai alikuwa ni sawa na kuku aombaye kuhurumiwa na mwewe na kwa bahati nzuri mwewe akasikia kilio chake.

Ukweli Jimmy hakuwa na mpango wa kumuua zaidi alitaka kumpiga mkwara tu lakini nani angejua ngojera zake zingemfanya shetani atubu? Maneno yake yalionekana kumuingia kisawasawa bwana yule kiasi cha kutaka kububujikwa na machozi

Jimmy alinyanyuka kutoka chini na kusimama kisha akawaangalia wale wengine aliowakung'uta na kukuta bado wako chini wakiugulia maumivu ilionekana kipigo walichopata ni cha kiwango cha lami kisha akamgeuka yule bwana

"Sayonara!" aliongea akimaanisha kwaherini na hakujisumbua kujua kama ameeleweka au lah na alizipiga hatua kuondoka eneo hilo

Alipofika nje aliuangalia muembe uliokuwa mbele yake na aliukazia macho kwa sekunde kadhaa na ghafla maembe matatu yalianguka na alikwenda kuyaokota hakujali sana kuhusu kuosha maana hata angetaka kuosha maji hayakuwepo alichojali kwa wakati huo ni kupooza njaa yake

Uzuri yote yalikuwa yameiva kabisa na aliyaokota, mawili akishika mkono wa kushoto na jingine mkono wa kulia na alikuwa akilipeleka mmdomoni huku akitembea

Ghafla mbele yake ilionekana gari aina ya V8 ikiwasili maeneo hayo na baada ya kusimama dereva alishuka kwenda kufungua mlango wa nyuma wa abiria na alishuka mwanaume mrefu mwenye mwili wa mazoezi, kichwani alinyoa mtindo wa kawaida nywele zake zikiwa fupi pia ndevu za mviringo, alikuwa amevalia t-sheti jekundu la mikono mirefu lililoubana mwili wake vyema kiasi cha kifua chake kujichora pia alivalia suruali nyeusi na biti nyeusi. na kwa kumuangalia umri wake ulikuwa kwenye miaka thelathini ya mwanzo(early 30s)

Na bila shaka Jimmy alijiambia huyo ndio Don mswahili, Don mswahili baada ya kushuka na kumuona mwanaume aliyekuwa mbele yake aliishia kukunja sura na kumtazama kwa makini sana kana kwamba aliwahi kuiona hio sura

Upande wa Jimmy baada ya kuona anakaziwa macho aliishia kutabasamu na kumalizia kulamba kokwa kisha kulitupa na kuchukua embe jingine

"Vipi Don ushawahi kuiona hii sura mahali" Jimmy aliongea huku akilipeka embe jingine mdomoni

"Triple ni wewe kweli?" aliuliza Don mswahili akitaka kama ni kweli anayemdhania ndio huyo

"Haha! Inaonekana unakumbukumbu sana, za miaka mingi"

"Aah nasahauje sura yako kwa mfano? Ukweli hujabadilika kabisa yani sura yako ni ileile ya miaka kumi na tano iliyopita na unazidi kuwa kijana tu" aliongea Don mswahili kwa bashasha na kumsogelea Jimmy kisha kukumbatiana kishkaji bila kujali kama atachafuliwa na mikono ya Jimmy iliyojaa michirizi ya embe

"Ni kitambo sana ila sahivi naona umekuwa boss wa genge la kihalifu" aliongea Jimmy huku akitabasamu

"Ni story ndefu sana Triple ila inakuwaje upo hapa?" aliuliza

"Kwahiyo unajifanya hujui si ndio?" Jimmy aliongea huku akimkazia macho

"Nitajuaje sasa bila ya wewe kuniambia" aliongea Don mswahili na alionekana hakuwa akidanganya na Jimmy alimuelezea

"Ishu ni kwamba watu wako wameniteka na kunileta hapa wakipokea maagizo kutoka kwako" aliongea

"Nini? Unasema?" aliongea akiwa haamini anachoambiwa

"Ila usiwaze sijawaua kwa maana hiyo sijakutia hasara" aliongea Jimmy akimalizia kulamba kokwa jingine na kulitupa

"Wewe ndio Jimmy?" Don mswahili alimuuliza na Jimmy alitingisha kichwa kukubaliana naye

Ishu ni ile ile katika ulimwengu wa kihalifu hakuna anayejua jina halisi la mwenzie isipokuwa wakifungukiana majina yao wao kwa wao na ni wachache sana wanaojulikana majina yao halisi hasa viongozi wa serikali kwasababu wanawakilisha pande mbili.
Don mswahili alikutana na Jimmy kwenye ulimwengu huo miaka kumi na tano iliyopita

Katika miaka zaidi ya kumi ya Jimmy kujuana na mzee Momochi Saizo yule myahudi aliyeishi naye kwa miaka mingi bila kujua ni ninja mstaafu kutoka kundi la kininja nchini japani lifahamikalo kwa jina la "Yami no Senshi" na kukubali kufunzwa mbinu nyingi za kimapigano na mambo mengine ya kawaida ndipo alipotambulishwa katika ulimwengu huo wa siri ulioko nchini Tanzania

Alikutana na Momochi Saizo alipokuwa na umri wa miaka saba na kuwa mwanafunzi wake na alipofikisha miaka kumi na mbili alitambulishwa kwenye huo ulimwengu yaani miaka mitano baada ya kuwa mwanafunzi wa mzee huyo na kusota kwenye mafunzo

Alimtambulisha katika yale mapambano haramu lengo ni kutaka kumpatia uzoefu wa kupigana na adui na sio kuishia kumaster mbinu tu. Yalikuwa ni mapambano yanayohusisha vijana wadogo kuanzia miaka kumi na mbili mpaka kumi na saba na huko ndipo alipoweza kuona kwamba kumbe kuna vijana rika lake ambao wanajua kupigana pia

Yalikuwa ni mapambano haramu na ikitokea umekufa ulingoni ndio basi tu unatupwa baharini na wengi wa watoto hao walikuwa ni yatima na wapo hapo kupambana kwaajili ya pesa kuweza kutimiza mahitaji yao. Walichukuliwa na madon mtaani na kuwagharamia mafunzo ili baadae kujipatia maokoto kupitia mapambano na hawakujali kuhusu uhai wa watoto hao ili mradi muamala unasoma kupitia akaunti ya blockchain mengine hayana umuhimu

Na huko ndiko Jimmy aliweza kushuhudia watoto wenzake wakipoteza uhai live bila chenga yaani ilionekana lengo jingine la mzee Momochi ni kutaka kumuonyesha kwamba dunia haipo kama tunavyoidhania, kuna mengi sana ya ajabu na kusikitisha yanayofanyika sirini.

Na katika hayo mapambano Jimmy aliweza kukutana na mvulana mwenzake aliyemzidi umri wa miaka mitano naye si mwingine ni Don mswahili.
Ukweli Jimmy katika mapambano hakuwa akipigana kuua kama wenzake bali alikuwa akipigana kushinda na alikuwa akishangaza sana mbinu zake za kimapagano alikuwa akimshinda mshindani wake kwa mapigo matatu tu ya krav-maga na ikitokea mshindani wake ni mgumu basi atamshinda kwenye mzunguko wa tatu wa pambano na kubatizwa jina la Triple strikes yaani mapigo matatu.

TO BE CONTINUED..........
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom