Simulizi ya kifantasia: Solo king: ancient legacy

Simulizi ya kifantasia: Solo king: ancient legacy

namba ya malipo ya coin kule fasihi napataje?
Malipo ya moja kwa moja bado mkuu ila mmiliki aliahidi mwisho wa huu mwezi mambo yatakuwa tayari

Kwasasa unalipia kwenye namba ya singano kisha unamcheki inbox pamoja na ushahidi wa muamala

Screenshot_20250525-115821.png
 
By Samuel jk_Euphoria

SOLO KING: ANCIENT LEGACY

CHAPTER 17: unatuepuka


"Vipi kuhusu miili ya walinzi waliokufa?"

"Tunatoa taarifa kwa polisi kwamba wamekufa kwenye majukumu yao ya kulinda usiku na ni ukweli, kuhusu vifo vyao hatutasumbuliwa isitoshe kesi kama hizi za watu kufa usiku vifo vya ajabu hazijaanza leo wala jana"

Kesho yake baada ya kutoa taarifa ya vifo vya walinzi walianza mchakato wa kuwazika kwa heshima walinzi hao na baada ya kumaliza maisha yakaendelea

Siku zikakata, wiki kadhaa zikapita na hatimae mwezi mwingine ukaingia, katika siku hizo zote tangu tukio lile la kutisha hakukutokea kingine zaidi ya kuishi kwa amani na kuongeza umakini kwenye usalama, kifupi ni kwamba waliamua kusahau na kuendelea na maisha mengine

Na katika siku zote mpaka kufikia siku hiyo Jimmy aliishi kwa kujitenga sana, alikuwa akiamka asubuhi na mapema na kurudi siku, kesha yake tena hivyo hivyo mpaka siku hiyo, Tangu ashuhudie maajabu na kutaka kupoteza uhai kwa mara ya pili na kusaidiwa na kundi la watu asiowajua aliamua kuwekeza muda wake mwingi kwenye kuielewa nguvu halisi aliyorithishwa na mzee asiyemjua kwa undani zaidi ya utambulisho wake tu

Alikuwa akijifunza namna ya kuiamsha na kuicontrol, alikuwa akijiimarisha kimwili, kiakili, kihisia na kiroho pia kufuatia muongozo kitabuni na alizingatia umakini sana kwenye kujifunza

Alikuwa akilalamikiwa sana na nduguze kwamba amekuwa mtu wa kujitenga sana kibaya zaidi hakuwa na simu, tangu simu yake iharibike hakujisumbua kununua mpya kiufupi ni kwamba alikuwa akiwekeza muda wake kwenye kitu kimoja nacho ni nguvu. Alitaka kuwa na nguvu maana dunia ina mengi na hawezi jua nini kitawatokea huko mbeleni hivyo alihitaji kujiandaa ipasavyo ili kuweza kukabiliana na Changamoto zijazo

Sasa mwezi huo ulikuwa ni mwezi wa kuanza elimu ya chuo kikuu kwa upande wa Jimmy,licha ya ku-apply chuo na kufanikiwa lakini hakujiandaa kabisa ni kama vile hakujali sana kuhusu hilo

Ilikuwa ni siku ya mchana wa saa sita na siku hiyo jimmy hakutoka zaidi ya kujifungia chumbani kwake asirleweke anafanya nini

"We J unafanya nini huko chumbani?"aliita mams yake kwa kifupi lakini hakukuwa na jibu lolote

"We Jimmy si nakuuliza?" aliita tena na alipoona kimya aliingia chumbani kwa wasiwasi lakini aliishia kumkuta Jimmy ameketi chini ya sakafu amekunja miguu mbele yake kukiwa na kitabu kilichofunguliwa kurasa kadhaa

Alikuwa amefumba macho na mdomo wake kucheza ksma vile anasali kwa kurudia rudia maneno, alikuwa ametulia kama uso wa bahari usio na upepo

Kwa picha alilolishuhudia mama yake alibaki kushangaa tu na kujiuliza huyu mtoto anafanya nini?

"Wewe mtoto yaani mimi nakuita wewe upo umekaa hapo chini ukipiga kimya tu, kwanza unafanya nini?" aliongea na sauri yenye lawama lakini bado mwanaye alikuwa kimya tu

Alisogea karibu yake na kuchukua kitabu kilicho cbini lakini aliishia kukunja sura tu baada ya kukutana na maandishi ya ajabu

"Umeanza lini uganga? "

"We Jimmy... Jimmy, we Jimmy" alikasirika baada ya kuona bado yupo kimya, uzuri kabla ya kuja hapo alikuwa jikoni akiandaa vitu kwa ajili ya kupika cha mchana na alikuwa amebeba mwiko, Alinyanyua mwiko na kutaka kumpiga nao begani kumshtua kwenye kile anachokifanya lakini kabla hata mwiko haujatua kwenye bega Jimmy aliudaka na kisha kuvumbua macho

"Naam mama unasema?" aliongea akiachia tabasamu usoni

"Kwanza kwanini nakuita hunisikii?" aliuliza

"Hapana nilikusikia cyema tatizo nilikuwa nasali" alijitetea

"Sala gani hii unakaa chini na mkitabu wa ajabu ajabu kwanza hiki ni nini? Usiniambie umeanza uganga"aliongea mama yake akitaka maelezo kuhussu hiko kitabu

" Usiwaze sana mwanao siwezi kuwa mganga kuhusu hiko kitabu, hiko ni kitabu cha hadithi ni vile tu wswe ni mshamba wa lugha" aliongea

"Kwanza sitaki kusikiliza hizo ngojera zako, nilikuwa na wasiwasi nilipoona upo chumbani muda wote ila kumbe wasiwasi wangu ni wa bure tu"

"Halafu kaka yako amenipigia simu anakuja"

"Nani, Cid?"

"Tena anakuja na Bianca uwape maelezo kwanini hupatikani, umekuwa ukiwaepuka na hata kuwatembelea"

"Cid si nilimwambia sina simu? Halafu sio kama nawaepuka" aliongea Jimmy, ukweli ni kwamba alikuwa akijua Cid na Bianca walikuwa wakitaka awafundishe kutumia ala za muziki na yeye alikuwa akijikita kwenye kitu kingine ambacho aliona nj muhimu zaidi kukizingatia na sio kwamba alikuwa akiwaepuka ni kutoka kwake asubuhi na kurudi usiku asieleweke ametoka wapi ndio kulimfanya aonekane kama anawaepuka.

Walikuwa wakifika mara kadhaa hapo kwao kwaajkli yake kila mmoja kwa wakati wake na wasimkute na hata waliposubiri mpaka giza linaingia hakuwa amerudi hivyo ilikuwa ni haki yao kusema wanatengwa. Ilifika wakati mama yake alikuwa akimpigia makelele kwa kuchelewa kwake usiku na kuwasubirisha mpaka alichoka hata hivyo Jimmy alikuwa mtu mzima aliishia kumuacha aendelee na mambo yake huku akiombea kimoyomoyo awe salama

"Utajijua mwenyewe yaani mtu mwenyewe hujali wala nini, kwani kununua simu ni ghali?"

"Sioni umuhimu wa kununua simu"

"Unasemajr? Yaani unatuacha na presha kuhusu usalama wako na hatujui umeennda wapi hata kupiga simu tu nafsi itulie ni ndoto, na unasema huoni umuhimu akili zako ni kama za baba yako tu ebu nikuache mie mambo yako utayajua mwenyewe" aliongea mama yake na kuondoka, aliona ataishia kupoteza muda na kijana wake ambaye hata hajali kuhusu simu, alikuwa na kazi ngumu sana ya kuwalea watoto wake.

Jimmy aliishia kumtazama mama yake akitoka chumbani na tabasamu usomi na mara alisikia chafya ikipigwa nje ya chumba chake na aliishia kusema "Bless you mama"

°°°°°°°°°°

Upande mwingine makao makuu ya jeshi la nchi ndani ya ofisi ya mkuu wa majeshi alionekana Jenerali John ameketi kwenye kiti katika hali ya mawazo uso wake ukielekea dirishani

Ghafla mlango ulifunguliwa na aliingia Luteni Jenerali Mwachitete ndani ya ofisi hiyo na ujio wake haukumshtua Jenerali katika hali ile ya mawazo ilionekana alitegemea ujio wake

"Una uhakika ni yeye?"

"Ndio ni yeye na kuna haja ya kutengua na kuteua upya kila ngazi kwenye usalama wa taifa?"

"Kuna ulazima?"

"Ww unadhani kwanini wale wapuuzi wameingiaje nchini bila kushtukiwa? Ni kwasababh kuna pandikizi"

"Wakina nani? Wale maninja au unazungumzia wale wapumbavu waliotaka kuwaua watoto wako?"

"Na kakikundi ka wahuni kutoka somalia kuja kutibua amani nchini, na kwa uimara wa jesho letu na ulinzi wangenaswa kitambo sana lakimi ikawa tofauti, mpaka wanakuja kusababisha maafa ndio tunaamka kutoka usingizini kwa hili tumefeli sana"

"Hilo niachie mimi nitadili nalo upesi pia shukrani ziende kwa kijana vinginevyo ingekuwa ni habari nyingine"

"Vijana siku hizi hawajui hata ni nini kizuri kwao amekataa kabisa kujiunga na jeshi na ninaheshimu uamuzi wake"

"kwahiyo baada ya kutoa maelezo yote....." aliongea Luteni Jenerali lakini kabla hajamaliza Sentensi yake Jenerali alitoa ishara ya mkono kuelekea shingoni kwake akimaanisha kwamba amewaua ni kama alikuwa anajua mzee mwenzake alikuwa anataka kusema nini

"Washenzi kama wale hawafai hawafai kuwepo kwenye uso wa dunia" aliongea Jenerali John kwa ukauzu akimaanisha wale wahuni waliotaka kutelekeza mauaji ya wanawe

"Pia wale maninja wa yami no senshi wamefanikiwa kutoroka nchini bila kukamatwa" aliongea Luteni Jenerali Mwachitete

"Ndio maana nikasema kuna haja ya kupanga safu upya, kuna vijana wapo kule kulamba maokoto na sio kulitumikia taifa"

°°°°°°°°°°

Jimmy mara baada ya kumaliza ile alixhokuwa akikifanya alitoka zake chumbani na kwenda sebuleni, kama bossi alikaa kwenye kochi miguu yake akiinyosha kwenye meza iliyokaribu, mkononj akishika rimoti ya king'amuzi cha azam na kila baada ya sekunde kadhaa alikuwa akibadili channel

Hakukuwa na channel yenye kuonyesha kipindi cha maana na aliona bora kwenda kumsaidia mama yake aliyekuwa jikoni akikatakata mboga akiandaa vya kupikia chakula cha mchana

"Mama, unahitaji nikusaidie!?"

"Ooh ni nadra sana kukuona unakujza jikoni kusaidia kulikoni?"

"Kwani lazima nimsaidie mama yangu nikiwa na sababu? Hata hivyo nimeboreka ni bora angalau kufanya kitu kuliko kuzubaa tu"

"Hmm! Sio mbaya kata vitunguu" alimpa vitunguu na kisu na mdogo mdogo alianza kukata

"Aisee macho yashaanza kuwasha tayari, hivi unavumiliaje haya mateso kila siku?" aliongea Jimmy

"Nishazoea, wewe ni mwanaume tayari jikaze utazoea" "

"Nikija kupofuka lawama zije kwako" alitania akiendelea kukata vitunguu

"Lione kwanza ebu endelea kukata!" alitabasamu

"Kwahiyo tunapika nini leo?" Jimmy aliuliza

"Chakula chako pendwa, mchuzi wa nyama wenye viungo na wali"

Wakati maongezi kati ya mama na mwana yakiendelea huko jikoni mlango wa sebuleni ulisikika ukigongwa na Jimmy alisitisha msaada wake Jikoni na kwenda kuuufungua mlango

Uso kwa uso na sura anayoifahamu huku nyuma ya hoyo sura kukiwa na sura nyingine anayoifahamu, zote zikiwa hazina hisia zozote baada ya kumuona Jimmy
Jimmy aliishia kutoa tabasamu flani hivi na kuwakaribisha ndani

"Karibuni ndani wapendwa msiishie kusimama nje" aliwakaribisha na Cif aliishia kutoa tabasamu la uchungu na kuingia huku Bianca akiwa na sura ya ukauzu
Wote kimya kimya waliingia ndani na kwenda kuketi kwenye makochi.

"Jisikieni huru kabisa hapa ni nyumbani kwenu pia" aliongea Jimmy

"Mnakunywa kinywaji gani ndugu zangu? Kuna juisi mbili za matunda kwenye friji, kuna embe na passion, mtapendelea kunywa nkni" aliendelea, yaani kwa jinsi alivyokuwa akiongea ji kwa unyenyekevu kana kwamba ni mara yake ya kwanza kukutana nao
Upande wa jikoni mama yake aliishia kumsikitikia tu

"Haina haja ya kutusahaulisha bro ila mimi niletee juisi ya embe" aliongea Cid akishaudtukia mchezo wa Jimmy

"Vipi Bianca na wewe..." alimuuliza lakini aliishia kukutana sura yenye kutia huruma kana kwamba amemkosea na hakujibiwa chochote zaidi ya kuangaliwa

Alijiongeza tu na kwenda kuleta glasi mbili za juisi na kuwapatia na alipatwa na ahueni baada ya Bianca kupokea pia

" Yo ebu utuambie umekuwa ukitukwepa kwa wiki kadhaa sasa",aliongea Cid baada ya kunywa pafu moja la juisi

"Tumekukosea nini bro mbona unatuepuka?"

"Sio kuwaepuka ni vile tu nimekuwa na mambo mengi"

"Mambo mengi karibia mwezi mzima? Hata kwenye simu hupatikani*

"Bro si nilikwambia sina simu au umesahau?"

"Unazingua sana bro yani simu tu unashindwa kununua? Anyway mimi sina neno unapaswa kuhakikisha huyu binti anakwenda masomoni" aliongea Jimmy akimnyooshea mkono Bianca ambayr muda wote alikuwa akimtazama Jimmy na hakujisumbua kunywa juisi zaidi ya kuishika tu

"Hnamaanisha nini?"

"Sikia huyu amegoma katakata kwenda chuo kuanza masomo rasmi kwa kisingizio cga kutaka kukuona" alieleza na Jimmy aliishia kushangaa tu na kumuangalia Bianca, na alipokutanishamacho mrembo huyo alikwepesha na kuangalia pembeni

"Ilitakiwa mwezi uliopita mwishonu aanze safari ya kwenda Uingereza kuwasili chuoni ila ona sasa uliyoyasababisha" Cid alimlaumu kana kwamba Jimmy ndiye aliyemzuia asiende masomoni

Bianca alinyanyuka na kutoka nje akiwaacha wenzake kwenye mshangao wakiangaliana wao kwa wao, upande wa mama yake alikuwa anasikia kila kitu na alikuwa akitabasamu tu huku akiendelea na shughuli yake ya kuandaa msosi

Lakini mara baada ya kusikia hatua za mtu akiondoka haraka haraks alihisi itakuwa Bianca na alikuwa sahihi, alitoka jikoni na kwenda sebuleni na kukuts Vijana wawili wakiangaliana tj

"Wewe mtukutu ebu nenda ukayamalize na binti yangu" aliongea huku akimfukuza na mwiko na Jimmy hakuwa ns jinsi zaidi ya kumfuata Bianca guko nje

"Shikamoo bi mkubwa nilihisi utakuwa jikoni unapika maana si kwa harufjmu hii kumbe nilikuwa sahihi"

"Haha marahaba mwanangu, vipi huko nyumbani mnaendeleajd?"

"Kama kawaida majukumu yamezidi leo nduo tumepata nafasi nhingind kuja kuwasalimia"

"Karibuni tena jamani*

" Tumeshakaribia, leo usiwaze tumekuja na matumbo empty kabisa"

"Haha kwakweli, lazima nihakikishe mnakula na kunisifia mapishi yangu" aliongea huku akicheka

"Sio mbaya nikija kukusaidia?" aliuliza Cid huku akijiambia anapaswa kujenga mahusiano mazuri na mama mkwe ajaye maana alimwelewa sana Monica

Upande wa mama mkwe ajaye hakuwa mtu wa kufikiria sana na alomkaribisha kwa tabasamu, Cid aliishia kufurahi moyoni na kuvua koti lake akibaki na T-sheti jeupe, alijiambia anapaswa kutupia maneno ya ucheshi huko jikoni kumfurahisha mama mkwe wake ajaye

Upande wa nje Jimmy mara baada ya kutoka alikimbilia upande wa ngazi na kushuka chini mpaka kwenye uwanja kabisa wa Apartment yao

Na Bianca alikuwa amesimama karibu na gari akimpa mgongo

"Bianca..." Jimmy aliita na mara baada ya mrembo huyo kusikia sauti ya mwanaume huyo ikimuita aligeuka na kutazamana macho kwa macho

Sekunde mbili si nyingi mrembo huyo machozi yalianza kumtoka na kuangua kilio cha kwikwi kama mtoto mdogo aliyeachwa na mama yake, Jimmy alikuwa akijiuliza amemkosea nini lakini hakuwa na jibu na badala yake alimsogelea karibu na kumkumbatia



TO BE CONTINUED..........
 
By Samuel jk_Euphoria

SOLO KING: ANCIENT LEGACY

CHAPTER 17: unatuepuka


"Vipi kuhusu miili ya walinzi waliokufa?"

"Tunatoa taarifa kwa polisi kwamba wamekufa kwenye majukumu yao ya kulinda usiku na ni ukweli, kuhusu vifo vyao hatutasumbuliwa isitoshe kesi kama hizi za watu kufa usiku vifo vya ajabu hazijaanza leo wala jana"

Kesho yake baada ya kutoa taarifa ya vifo vya walinzi walianza mchakato wa kuwazika kwa heshima walinzi hao na baada ya kumaliza maisha yakaendelea

Siku zikakata, wiki kadhaa zikapita na hatimae mwezi mwingine ukaingia, katika siku hizo zote tangu tukio lile la kutisha hakukutokea kingine zaidi ya kuishi kwa amani na kuongeza umakini kwenye usalama, kifupi ni kwamba waliamua kusahau na kuendelea na maisha mengine

Na katika siku zote mpaka kufikia siku hiyo Jimmy aliishi kwa kujitenga sana, alikuwa akiamka asubuhi na mapema na kurudi siku, kesha yake tena hivyo hivyo mpaka siku hiyo, Tangu ashuhudie maajabu na kutaka kupoteza uhai kwa mara ya pili na kusaidiwa na kundi la watu asiowajua aliamua kuwekeza muda wake mwingi kwenye kuielewa nguvu halisi aliyorithishwa na mzee asiyemjua kwa undani zaidi ya utambulisho wake tu

Alikuwa akijifunza namna ya kuiamsha na kuicontrol, alikuwa akijiimarisha kimwili, kiakili, kihisia na kiroho pia kufuatia muongozo kitabuni na alizingatia umakini sana kwenye kujifunza

Alikuwa akilalamikiwa sana na nduguze kwamba amekuwa mtu wa kujitenga sana kibaya zaidi hakuwa na simu, tangu simu yake iharibike hakujisumbua kununua mpya kiufupi ni kwamba alikuwa akiwekeza muda wake kwenye kitu kimoja nacho ni nguvu. Alitaka kuwa na nguvu maana dunia ina mengi na hawezi jua nini kitawatokea huko mbeleni hivyo alihitaji kujiandaa ipasavyo ili kuweza kukabiliana na Changamoto zijazo

Sasa mwezi huo ulikuwa ni mwezi wa kuanza elimu ya chuo kikuu kwa upande wa Jimmy,licha ya ku-apply chuo na kufanikiwa lakini hakujiandaa kabisa ni kama vile hakujali sana kuhusu hilo

Ilikuwa ni siku ya mchana wa saa sita na siku hiyo jimmy hakutoka zaidi ya kujifungia chumbani kwake asirleweke anafanya nini

"We J unafanya nini huko chumbani?"aliita mams yake kwa kifupi lakini hakukuwa na jibu lolote

"We Jimmy si nakuuliza?" aliita tena na alipoona kimya aliingia chumbani kwa wasiwasi lakini aliishia kumkuta Jimmy ameketi chini ya sakafu amekunja miguu mbele yake kukiwa na kitabu kilichofunguliwa kurasa kadhaa

Alikuwa amefumba macho na mdomo wake kucheza ksma vile anasali kwa kurudia rudia maneno, alikuwa ametulia kama uso wa bahari usio na upepo

Kwa picha alilolishuhudia mama yake alibaki kushangaa tu na kujiuliza huyu mtoto anafanya nini?

"Wewe mtoto yaani mimi nakuita wewe upo umekaa hapo chini ukipiga kimya tu, kwanza unafanya nini?" aliongea na sauri yenye lawama lakini bado mwanaye alikuwa kimya tu

Alisogea karibu yake na kuchukua kitabu kilicho cbini lakini aliishia kukunja sura tu baada ya kukutana na maandishi ya ajabu

"Umeanza lini uganga? "

"We Jimmy... Jimmy, we Jimmy" alikasirika baada ya kuona bado yupo kimya, uzuri kabla ya kuja hapo alikuwa jikoni akiandaa vitu kwa ajili ya kupika cha mchana na alikuwa amebeba mwiko, Alinyanyua mwiko na kutaka kumpiga nao begani kumshtua kwenye kile anachokifanya lakini kabla hata mwiko haujatua kwenye bega Jimmy aliudaka na kisha kuvumbua macho

"Naam mama unasema?" aliongea akiachia tabasamu usoni

"Kwanza kwanini nakuita hunisikii?" aliuliza

"Hapana nilikusikia cyema tatizo nilikuwa nasali" alijitetea

"Sala gani hii unakaa chini na mkitabu wa ajabu ajabu kwanza hiki ni nini? Usiniambie umeanza uganga"aliongea mama yake akitaka maelezo kuhussu hiko kitabu

" Usiwaze sana mwanao siwezi kuwa mganga kuhusu hiko kitabu, hiko ni kitabu cha hadithi ni vile tu wswe ni mshamba wa lugha" aliongea

"Kwanza sitaki kusikiliza hizo ngojera zako, nilikuwa na wasiwasi nilipoona upo chumbani muda wote ila kumbe wasiwasi wangu ni wa bure tu"

"Halafu kaka yako amenipigia simu anakuja"

"Nani, Cid?"

"Tena anakuja na Bianca uwape maelezo kwanini hupatikani, umekuwa ukiwaepuka na hata kuwatembelea"

"Cid si nilimwambia sina simu? Halafu sio kama nawaepuka" aliongea Jimmy, ukweli ni kwamba alikuwa akijua Cid na Bianca walikuwa wakitaka awafundishe kutumia ala za muziki na yeye alikuwa akijikita kwenye kitu kingine ambacho aliona nj muhimu zaidi kukizingatia na sio kwamba alikuwa akiwaepuka ni kutoka kwake asubuhi na kurudi usiku asieleweke ametoka wapi ndio kulimfanya aonekane kama anawaepuka.

Walikuwa wakifika mara kadhaa hapo kwao kwaajkli yake kila mmoja kwa wakati wake na wasimkute na hata waliposubiri mpaka giza linaingia hakuwa amerudi hivyo ilikuwa ni haki yao kusema wanatengwa. Ilifika wakati mama yake alikuwa akimpigia makelele kwa kuchelewa kwake usiku na kuwasubirisha mpaka alichoka hata hivyo Jimmy alikuwa mtu mzima aliishia kumuacha aendelee na mambo yake huku akiombea kimoyomoyo awe salama

"Utajijua mwenyewe yaani mtu mwenyewe hujali wala nini, kwani kununua simu ni ghali?"

"Sioni umuhimu wa kununua simu"

"Unasemajr? Yaani unatuacha na presha kuhusu usalama wako na hatujui umeennda wapi hata kupiga simu tu nafsi itulie ni ndoto, na unasema huoni umuhimu akili zako ni kama za baba yako tu ebu nikuache mie mambo yako utayajua mwenyewe" aliongea mama yake na kuondoka, aliona ataishia kupoteza muda na kijana wake ambaye hata hajali kuhusu simu, alikuwa na kazi ngumu sana ya kuwalea watoto wake.

Jimmy aliishia kumtazama mama yake akitoka chumbani na tabasamu usomi na mara alisikia chafya ikipigwa nje ya chumba chake na aliishia kusema "Bless you mama"

°°°°°°°°°°

Upande mwingine makao makuu ya jeshi la nchi ndani ya ofisi ya mkuu wa majeshi alionekana Jenerali John ameketi kwenye kiti katika hali ya mawazo uso wake ukielekea dirishani

Ghafla mlango ulifunguliwa na aliingia Luteni Jenerali Mwachitete ndani ya ofisi hiyo na ujio wake haukumshtua Jenerali katika hali ile ya mawazo ilionekana alitegemea ujio wake

"Una uhakika ni yeye?"

"Ndio ni yeye na kuna haja ya kutengua na kuteua upya kila ngazi kwenye usalama wa taifa?"

"Kuna ulazima?"

"Ww unadhani kwanini wale wapuuzi wameingiaje nchini bila kushtukiwa? Ni kwasababh kuna pandikizi"

"Wakina nani? Wale maninja au unazungumzia wale wapumbavu waliotaka kuwaua watoto wako?"

"Na kakikundi ka wahuni kutoka somalia kuja kutibua amani nchini, na kwa uimara wa jesho letu na ulinzi wangenaswa kitambo sana lakimi ikawa tofauti, mpaka wanakuja kusababisha maafa ndio tunaamka kutoka usingizini kwa hili tumefeli sana"

"Hilo niachie mimi nitadili nalo upesi pia shukrani ziende kwa kijana vinginevyo ingekuwa ni habari nyingine"

"Vijana siku hizi hawajui hata ni nini kizuri kwao amekataa kabisa kujiunga na jeshi na ninaheshimu uamuzi wake"

"kwahiyo baada ya kutoa maelezo yote....." aliongea Luteni Jenerali lakini kabla hajamaliza Sentensi yake Jenerali alitoa ishara ya mkono kuelekea shingoni kwake akimaanisha kwamba amewaua ni kama alikuwa anajua mzee mwenzake alikuwa anataka kusema nini

"Washenzi kama wale hawafai hawafai kuwepo kwenye uso wa dunia" aliongea Jenerali John kwa ukauzu akimaanisha wale wahuni waliotaka kutelekeza mauaji ya wanawe

"Pia wale maninja wa yami no senshi wamefanikiwa kutoroka nchini bila kukamatwa" aliongea Luteni Jenerali Mwachitete

"Ndio maana nikasema kuna haja ya kupanga safu upya, kuna vijana wapo kule kulamba maokoto na sio kulitumikia taifa"

°°°°°°°°°°

Jimmy mara baada ya kumaliza ile alixhokuwa akikifanya alitoka zake chumbani na kwenda sebuleni, kama bossi alikaa kwenye kochi miguu yake akiinyosha kwenye meza iliyokaribu, mkononj akishika rimoti ya king'amuzi cha azam na kila baada ya sekunde kadhaa alikuwa akibadili channel

Hakukuwa na channel yenye kuonyesha kipindi cha maana na aliona bora kwenda kumsaidia mama yake aliyekuwa jikoni akikatakata mboga akiandaa vya kupikia chakula cha mchana

"Mama, unahitaji nikusaidie!?"

"Ooh ni nadra sana kukuona unakujza jikoni kusaidia kulikoni?"

"Kwani lazima nimsaidie mama yangu nikiwa na sababu? Hata hivyo nimeboreka ni bora angalau kufanya kitu kuliko kuzubaa tu"

"Hmm! Sio mbaya kata vitunguu" alimpa vitunguu na kisu na mdogo mdogo alianza kukata

"Aisee macho yashaanza kuwasha tayari, hivi unavumiliaje haya mateso kila siku?" aliongea Jimmy

"Nishazoea, wewe ni mwanaume tayari jikaze utazoea" "

"Nikija kupofuka lawama zije kwako" alitania akiendelea kukata vitunguu

"Lione kwanza ebu endelea kukata!" alitabasamu

"Kwahiyo tunapika nini leo?" Jimmy aliuliza

"Chakula chako pendwa, mchuzi wa nyama wenye viungo na wali"

Wakati maongezi kati ya mama na mwana yakiendelea huko jikoni mlango wa sebuleni ulisikika ukigongwa na Jimmy alisitisha msaada wake Jikoni na kwenda kuuufungua mlango

Uso kwa uso na sura anayoifahamu huku nyuma ya hoyo sura kukiwa na sura nyingine anayoifahamu, zote zikiwa hazina hisia zozote baada ya kumuona Jimmy
Jimmy aliishia kutoa tabasamu flani hivi na kuwakaribisha ndani

"Karibuni ndani wapendwa msiishie kusimama nje" aliwakaribisha na Cif aliishia kutoa tabasamu la uchungu na kuingia huku Bianca akiwa na sura ya ukauzu
Wote kimya kimya waliingia ndani na kwenda kuketi kwenye makochi.

"Jisikieni huru kabisa hapa ni nyumbani kwenu pia" aliongea Jimmy

"Mnakunywa kinywaji gani ndugu zangu? Kuna juisi mbili za matunda kwenye friji, kuna embe na passion, mtapendelea kunywa nkni" aliendelea, yaani kwa jinsi alivyokuwa akiongea ji kwa unyenyekevu kana kwamba ni mara yake ya kwanza kukutana nao
Upande wa jikoni mama yake aliishia kumsikitikia tu

"Haina haja ya kutusahaulisha bro ila mimi niletee juisi ya embe" aliongea Cid akishaudtukia mchezo wa Jimmy

"Vipi Bianca na wewe..." alimuuliza lakini aliishia kukutana sura yenye kutia huruma kana kwamba amemkosea na hakujibiwa chochote zaidi ya kuangaliwa

Alijiongeza tu na kwenda kuleta glasi mbili za juisi na kuwapatia na alipatwa na ahueni baada ya Bianca kupokea pia

" Yo ebu utuambie umekuwa ukitukwepa kwa wiki kadhaa sasa",aliongea Cid baada ya kunywa pafu moja la juisi

"Tumekukosea nini bro mbona unatuepuka?"

"Sio kuwaepuka ni vile tu nimekuwa na mambo mengi"

"Mambo mengi karibia mwezi mzima? Hata kwenye simu hupatikani*

"Bro si nilikwambia sina simu au umesahau?"

"Unazingua sana bro yani simu tu unashindwa kununua? Anyway mimi sina neno unapaswa kuhakikisha huyu binti anakwenda masomoni" aliongea Jimmy akimnyooshea mkono Bianca ambayr muda wote alikuwa akimtazama Jimmy na hakujisumbua kunywa juisi zaidi ya kuishika tu

"Hnamaanisha nini?"

"Sikia huyu amegoma katakata kwenda chuo kuanza masomo rasmi kwa kisingizio cga kutaka kukuona" alieleza na Jimmy aliishia kushangaa tu na kumuangalia Bianca, na alipokutanishamacho mrembo huyo alikwepesha na kuangalia pembeni

"Ilitakiwa mwezi uliopita mwishonu aanze safari ya kwenda Uingereza kuwasili chuoni ila ona sasa uliyoyasababisha" Cid alimlaumu kana kwamba Jimmy ndiye aliyemzuia asiende masomoni

Bianca alinyanyuka na kutoka nje akiwaacha wenzake kwenye mshangao wakiangaliana wao kwa wao, upande wa mama yake alikuwa anasikia kila kitu na alikuwa akitabasamu tu huku akiendelea na shughuli yake ya kuandaa msosi

Lakini mara baada ya kusikia hatua za mtu akiondoka haraka haraks alihisi itakuwa Bianca na alikuwa sahihi, alitoka jikoni na kwenda sebuleni na kukuts Vijana wawili wakiangaliana tj

"Wewe mtukutu ebu nenda ukayamalize na binti yangu" aliongea huku akimfukuza na mwiko na Jimmy hakuwa ns jinsi zaidi ya kumfuata Bianca guko nje

"Shikamoo bi mkubwa nilihisi utakuwa jikoni unapika maana si kwa harufjmu hii kumbe nilikuwa sahihi"

"Haha marahaba mwanangu, vipi huko nyumbani mnaendeleajd?"

"Kama kawaida majukumu yamezidi leo nduo tumepata nafasi nhingind kuja kuwasalimia"

"Karibuni tena jamani*

" Tumeshakaribia, leo usiwaze tumekuja na matumbo empty kabisa"

"Haha kwakweli, lazima nihakikishe mnakula na kunisifia mapishi yangu" aliongea huku akicheka

"Sio mbaya nikija kukusaidia?" aliuliza Cid huku akijiambia anapaswa kujenga mahusiano mazuri na mama mkwe ajaye maana alimwelewa sana Monica

Upande wa mama mkwe ajaye hakuwa mtu wa kufikiria sana na alomkaribisha kwa tabasamu, Cid aliishia kufurahi moyoni na kuvua koti lake akibaki na T-sheti jeupe, alijiambia anapaswa kutupia maneno ya ucheshi huko jikoni kumfurahisha mama mkwe wake ajaye

Upande wa nje Jimmy mara baada ya kutoka alikimbilia upande wa ngazi na kushuka chini mpaka kwenye uwanja kabisa wa Apartment yao

Na Bianca alikuwa amesimama karibu na gari akimpa mgongo

"Bianca..." Jimmy aliita na mara baada ya mrembo huyo kusikia sauti ya mwanaume huyo ikimuita aligeuka na kutazamana macho kwa macho

Sekunde mbili si nyingi mrembo huyo machozi yalianza kumtoka na kuangua kilio cha kwikwi kama mtoto mdogo aliyeachwa na mama yake, Jimmy alikuwa akijiuliza amemkosea nini lakini hakuwa na jibu na badala yake alimsogelea karibu na kumkumbatia



TO BE CONTINUED..........
Kali sana, ila naomba angalau uwe unapost chapter 2 itapendeza mtaalam
 
Nimeula wa chuya nilizani kuna epsode 2. Ni tamu mpaka nimeiona fupi
Simulizi bado ndefu ina season nne hii

Season 1 ina 30 chapters
Season 2 ambayo ndo naandika itatakiwa iwe na 50 chapters
Season 3 nayo bado itakuwa na 70 chapters
Season 4 tutajua uko mbeleni

Season 1 inaitwa Ancient legacy, 2 inaitwa Dark majesty, 3 inaitwa Two realms halafu 4 inaitwa Last man standing

Ni simulizi kali sana kikubwa uzima tu ili niweze kuikamilisha
 
Simulizi bado ndefu ina season nne hii

Season 1 ina 30 chapters
Season 2 ambayo ndo naandika itatakiwa iwe na 50 chapters
Season 3 bayo bado itakuwa na 70 chapters
Season 4 tutajua uko mbeleni

Season 1 inaitwa Ancient legacy, 2 inaitwa Dark majesty, 3 inaitwa Two realms halafu 4 inaitwa Last man standing

Ni simulizi kali sana kikubwa uzima tu ili niweze kuikamilisha
NAAM kwenye hiyo MTU WA MWISHO KUSIMA
 
By Samuel jk_Euphoria

SOLO KING: ANCIENT LEGACY

CHAPTER 18: long time no see fam


MIAKA MITANO BAADAE



Kwenye uwanja wa ndege wa taifa, JNIA ilionekana ndege kubwa ikitua kwa kasi na hatimae kasi kupungua na kusimamia sehemu ya kushuka abira na mlango ulifunguliwa pia ngazi ikiwa tayari kwa abiria kuteremka



Waliteremka raia jinsia tofauti, rangi tofauti, wakubwa na kwa watoto na mwisho kabisa kushuka alikuwa ni mwanaume mrefu wa wastani, mweupe wa ngozi na jua la saa kumi na moja jioni hiyo lilimmulika na kung'aa kama mfalme aliyetoka kushinda vita vya muda mrefu



Juu kichwani alikuwa na nywele za wastani nyeusi zilizokolea akinyoa mtindo uliendana na kichwa chake na kupendeza, alivalia miwani nyeusi ya jua, shati kubwa jepesi lenye mauaua rangi tofauti chini alivalia pensi nyeusi iliyofikia magotini na miguuni alivalia raba nyeupe



Kwa jinsi alivyoonekana ni kama vile ametoka beach nchini hawali na sasa anarudi nchini uso ukiwa na tabasamu pana



Alishuka na kutembea kwa mwendo wa taratibu lakini tembea yake haikuwa ya kawaida, ilikuwa ni tembea ya kijasiri mno licha kasi ndogo kama bwana harusi, mkononi alikuwa ameshikilia begi kubwa la mkono mfano wa vriefvase flani hivi lakini halikuwa briefcase(nadhani nimeeleweka)

Lilikuwa ni begi la kuhifadhia nguo na vitu vingine umbo la mstatili



Upande wa ndani ya terminal 2 kulikuwa na kundi la watu lililokuwa likiwasubiri abiria na kuwapokea na mpaka abiria wote wanaisha na watu kupungua na kubaki mmoja tu



Alikuwa ni mwanaume mwenye ndevu zilizonyolewa mtindo wa "anchor" alikuwa amevalia kikawaida, T-sheti jeupe, suruali ya kitambaa pamoja na sendo mguuni, alikuwa amesimama mikono yote akiweka mfukoni na baasa ya kama sekunde ishirini aliachia tabasamu alipomuona aliyekuwa akimsubiri akitokelezea



Mwanaume huyo alikuwa ni Cidian na aliyekuwa akimsubiri hakuwa mwingine bali ni Jimmy



"Long time no see, fam" aliongea, Cid akiachia tabasamu baada ya Jimmy kumkaribia na walikumbatiana kishikaji akimaanisha ni mda mrwfu hawajaonana



"Too long kiasi cha kuota ndevu" aliongea Jimmy akimtazama Cid na ndevu zake



"Vyovyote vile karibu nyumbani bro" Cid alimkaribisha Jimmy kwa kurudi nchini alikozaliwa baada ya kuondoka na ni miako tano imepita



"Yeah nimeshakaribia kabla ya mengine kufata unaonaje tukale ice ceeam nimemisi sana hizi ice cream" aliongea jimmy huku akishika koo yake



"Usiniambie huko ulikokuwa hakukuwa na Ice cream"



"Ziwepo zisiwepo miminimemisi za huku nyumbani" aliongea Jimmy na kuanza kupika hatua kuelekea nje ya uwanja huo akifuatana Cid na mbele yao kulikuwa na Cadillac Escalade jeusi limepark kwenye maegesho ya muda mfupi na waliingia kisha gari liliondoka maeneo hayo



Masa kadhaa mbele Cadillac hilo lilionekana limesimama karibu na ufukwe wa bahari na juu kabisa ya gari(paa) Jimmy na Cid walikuwa wamekaa wakila ice cream wakitazama bahari



"Inanikumbusha kipindi kile tunakuwa marafiki rasmi" aliongea Jimmy huku akilamba Ice cream yake ladha ya black raspberry



Upande wa Cid alitingisha kichwa na kusema "yeah" na kimya kutawala wakiendelea kula wakisikilizia utamu wa Ice cream zao



"Utaenda kumwambia nini?" Cid alivunja ukimya baada ya kumaliza kula ice cream



"Nani?"



"Kwahiyo unajisahaulisha sio?" aliongea Cid huku akitingisha kichwa kwa masikitiko



"Ijapokuwa sijui mliongea nini kipindi kile mara ya mwisho kuonana na kupeana ahadi gani ila niseme tu amekuwa mpweke sana" aliongea Cid na Jimmy sio kama hakujua ni makusudi tuya kujifanya kutokujua



"Nilimwambia kwamba nitamsubiri arudi na kuniambia siri aliyoniahidi"



"Na aliporudi hakukuta na amekutafuta kwa miaka miwili bila mafanikio huoni kama huo ni ukatili bro?"



°°°°°°°°°°



FLASHBACK (MIAKA MITANO NYUMA)



Uzuri nje ya Apartment hiyo hakukuwa na mtu yoyote nje zaidi ya wao wawili. Jimmy alimwangalia Bianca aliyekuwa analia kwa kwikwi na kumsogelea karibu na kumkumbatia na kuchezea nywele taratibu akijaribu kumtuliza



Na sasa mrembo huyo alikuwa akilia kifuani mwa mwamba na picha kuonekana kama tamthilia flani ya kikorea ya mapenzi motomoto pale mwanamke anapomkumbatia na kulia kifuani mwa bwana wake akidhani alikufa kumbe yupo hai



Dakika tatu za kilio zilipita na Jimmy alifanikiwa kumtuliza mrembo huyo na kumkalisha kwenye boneti ya gori huku yeye akiwa amesimama mbele yake akimtazama



"Hey" Jimmy alimuita kwa sauti ya taratibu akimtazama machoni lakini Bianca alikuwa akitazama pembeni uso ukiwa na mnuno wa hali ya juu



"Unalia nini mummy nipo hapa kukusikiliza nielezee" alimsihi kwa upole na kilee kilio kilichokata kikaanza upya safari hii akitoa sauti hafifu



Jimmy aliishia kujikuna kichwa chake na kujiambia kweli kazi anayo alijiambia mbona huyu binti anamfanya kujisikia hatia ilihali hajui kosa lake



"Wewe.. Mkaka yaani.... Unapotea karibia mwezi... Mzima Unavunja ahadi... Yako halafu.. Kwanza hunipendi, hutaki urafiki na mimi" Bianca aliongea kwa hasira huku neno akilisindikiza na vingumi vyake dhaifu akimpiga kifuani Jimmy na kidume aliishia kutulia tu hata hivyo hazikuuma zaidi aliona kama vile anapapaswa



"Mimi? Kwanini nikukatae rafiki mzuri kama wewe? , unawaza mbali sana Bianca"



"Kama kweli kwanini hupatikani? Umezima simu makusudi sio? "



"Sina simu jamani" aliongea kwa.lawama huku akimlaumu Cid kwa kutomwambia dada yake



"Vipi kuhusu ahadi yako?"



"Ahadi?" Jimmy alijikuna kichwa na kujiuliza ni lini alitoa ahadi kwa huyo mrembo



"Si unaona sasa ushasahau kwanza nipishe niondoke sitaki kukuona" alinuna huku akijaribu kushuka kwenye boneti alilokalishwa lakini aliishia kuhangaika bila mafanikio kwani Jimmy hakumpa nafasi hio, aliishia kumuangalia kwa tabasamu mrembo huyo anavyohangaika na sura yake ya kununa. Alivutiwa sana kumuona hivyo ni vile tu hakuwa muwazi



"Unaonaje ukanikumbusha nimekuwa bize sana ndio maana pia unisamehe bure mummy"



"Nani mummy?"



"Wewe hapo"



"Mimi sio mummy wako"



"Haya basi mrembo nikumbushe"



"Uliniambia utanifundisha kucheza piano ila ukanikimbia"



"Sio hivyo basi unaonaje kesho nakufundisha nitakuwa na wewe muda wote sitokukimbia"



"Haina maana biyo kesho"



"Kwanini?"



"Naondoka kwenda masomoni?"



"Mbona mapema hivyo?"



"Mapema? Nilitakiwa kuwasili mwezi uliopita ni wewe ulienichelewesha" Jimmy aliishia kukaa kimya asije kumkaribisha na kununiwa tena.



"Jimmy" aliita kwa sauti yake nyororo



"Naam" aliitika



"Nina siri"



"Siri? Siri gani"



"Nataka nikuambie Siri yangu lakini si sasa mpaka nitakaporudi" aliongea mrembo huyo kisha kunyamanza kwa sekunde kisha kuendelea



"Utanisubiri?" Jimmy aliishia kumeza mate mengi na kujiambia ni siri gani hiyo ya kumfanya asubiri miaka kadhaa



"Niahidi utanisubiri okay?"



"Okay nakuahidi nitakusubiri uniambie hiyo siri" aliongea Jimmy na kumfanya mrembo Bianca kutabasamu kwa mara ya kwanza siku hiyo



°°°°°°°°°°



PRESENT DAY



Jimmy alikuwa akikumbuka walichoongea na Bianca kabla hajaondoka kwenda uingereza kuanza elimu ta chuo kikuu



"Kuna muda unapanga mambo nakudhani yataenda sawa kama ulivyopanga lakini unakuja kukuta yanaenda ndivyo sivyo" aliongea Jimmy



"Hata kama bro ndio uondoke bila kujulikana unaenda wapi? Japokuwa nimekusaidia kupata passport na mahitaji mengine ya usafiri lakini hukuniambia unakoenda zaidi ya kusema unaenda kusoma, aya sawa tuseme umeenda kusoma lakini hujaniambia unaenda kusoma nini, uliniambia tu ni miaka miwili unarudi, miaka miwili my foot! Ni mwaka wa tano huu ndio unarudi" Cid aliongea kwa lawama na Jimmy hakutaka kujielezea zaidi ya kutabasamu



"umewadanganya ndugu zako kwamba umeapply chuo mkoani na ukanisihi nifiche siri yako, kuna muda nahisi hatia kwa kuwakalia kimya na kuwaangali wanavyokuwa na wasiwasi juu yako kwa miaka yote hiyo, kibaya zaidi baada ya kuondoka nchini ukakata mawasiliano halafu juzi ndio unanitafuta nikupokee uwanjani baada ya miaka mitano ya kutususa" aliendelea kulalamika



"Kuna mambo mengine si vyema kuyaongea ila kuhusu kusoma ni kweli nimeenda kusoma" aliongea Jimmy



"Kama hutaki kuniambia sikulazimishi ila unapaswa kujiandaa kutoa maelezo yaliyonyooka kwa wanafamilia wako"



"Anyway umeenda kusomea nini?" Cid aliuliza



Kabla Jimmy hajajibu hilo swali alihisi kitu na kumwambia Cid aangalia mfukoni na alipotoa hicho kilicho mfukoni ilikuwa ni simu ya Cid ikiita, ilikuwa kwenye "silence mode" lakini aliweza kugundua inaita



"Bro umejuaje kama simu inaita ilihali iko silence?" aliuliza huku akishangaa kidogo



"Hata kama uliweka silence simu ikiita lazima iwake mimi nilichoona ni mwanga" Jimmy aliongea na kumfanya Cid kuona kweli ni sahihi lakini alivyoangalia suruali yake ilivyo nyeusi hata mwanga usionekane kirahisi aliishia kumsifia ana macho



Cid alipoangalia mpigaji kwenye simu yake alitabasamu na kuipokea



"Wewe mtoto kwanini hupokei simu zangu" ilisikika sauti upande wa pili na, Cid alitoa simu masikiani na kuangalia notification bar na kukuta missed calls tatu na bila shaka hiyo ni ya nne na kama sio Jimmy pengine asingeipokea



"Aah mama nilikuwa nilikuwa na maongezi na mtu muhimu hivyo niliweka silence" Cid alianza kujitetea



"Ksahiyo huyo mtu ni muhimu sana kuzidi mke wako?" aliongea upande wa pili



"Kuna nini kwani?"



"Yaani nyinyi wanaume na tabia zenu za kusahausahau mambo muhimu mnatia hasira"



"Niambie kuna nini kimempata mke wangu"



"Yaani mke wako ana mimba na huna habari kabisa"



"Usiniambie...."



"Ndii anajifungua na anapiga makelele anataka kumuona mume wake halafu wewe...." kabla hata upande wa pili kumaliza Cid alikata simu na haraka haraka alishuka kwenye kutoka juu ya gari



"Bro shuka chini tunakwenda hospitalini" aliongea Cid lakini Jimmy alikwishashuka muda sana na hawakupoteza muda waliingia ndani ya gari na Cid aliliondoa kwa kasi eneo hilo



Barabarani Cid alikuwa akikwepa magari kwa kasi huku akipiga honi kila mara apishwe kana kwamba yeye ndiye mmiliki wa barabara hiyo



"Bro kuwa na amani mkeo atajifungua salama si tayari yupo hospitalini" Jimmy aliongea, ilionekana alisikia kila kitu kwenye, simu



"Shida sio kujifungua sitaki kununiwa na mke wangu kwa vitu vidogo vidogo" aliongea Cid akiweka umakini barabarani



"Ooh sawa mkubwa" Jimmy aliitikia



"Hivi unajua hata mke wangu ni nani?" Cid alimuuliza



"Si uongee sasa kuliko kuniuliza maswali ambayo sina hata majibu yake"



"Kifupi ni kwamba mimi ni shemeji yako bro"



"Unasema!" Jimmy aliongea kwa sauti kama vile hakusikia vizuri



"Yeah I married your sister dude!" aliongea Cid kwa kingereza akimaanisha amemua dada yake Jimmy



Jimmy aliishia kumeza mate yake kwa tabu na kujiambia kweli amepitwa na mambo mengi sana. Alivuta picha dada alivyo na ujauzito aliishia kutoa tabasamu la uchungu



" Damn! Hii nchi ni ya kifala sana!" Cid alifoka baada ya kukutana na foleni na hakuwa na jinsi zaidi ya kusimamisha gari lake



Mara simu yake ikaanza kuita safari hii kwa sauti, ilionekana aliitoa ile silence mode na alipoona mpigaji aliishia tu kuiangalia kwa sura yenye hatia na hofu kidogo na aliipokea



"Wewe mpuuzi huko wapi?... Baba gani hataki kushuhudia mtoto wake akizaliwa" ilikuwa ni sauti ya kike yenye hasira na uchungu wa kujifungua ilionekana alikuwa kwenye shughuli ya kujifungua na bado akapata ujasiri wa kupiga simu bila ya madaktari kumzuia Cid aliishia kujiambia kweli huyo ndiyo mke wake amjuaye



Upande wa Jimmy aliposikiasauti ya dada yake na sura ya, Cid ilivyo aliishia kugeuza shingo yake dirishani na kucheka kisiri siri



"Hapana mke wangu usiwe na jazba nilitamani sana siku hii niwe karibu yako lakini si unajua mumeo ana mambo mengi" Cid aliongea kwa kujitia huruma



"Acha unachofanya na haraka uje huku vinginevyo...."



"Ndio ndio mke wangu nipo njiani naelekea huko ila kwasasa unapaswa kuzingatia kujifungua sitaki mwanetu apatwe na matatizo"



"Ndio unajali kuhusu mtoto sasa...Aarrghhhh!" mke wake aliongea na kutoa kelele ya kusukuma



"Sukuma mke wangu, sukuma, push! Nakuaminia mke wangu unaweza, sukumaaa" Cid alikuwa akiongea huku kijasho kikimtoka na mke wake alikuwa akisukuma bila shaka mpaka kufanikiwa kujifungua mtoto na Cid aliishia kupiga makelele ya shangwe na furaha



"Ni wa kiume ama wa kike?" Cid aliuliza



"Ni wa kiume" sauti upande wa pili ilisikika na, Cid almanusura ajigonge kichwa chake ndani ya gari kwa furaha aliyokuwa nayo



"Nakupenda sana mke wangu nakuletea zawadi nzuri ya kwako na mzaliwa weru wa kwanza" aliongea



"Namsubiri mume wangu mpenzi uje tumpatie jina zuri mtoto wetu, njoo haraka mtoto anataka kumuona baba yake"



"Dakika sifuri nitakuwa nimefika mke wangu mwaah!" aliongea Cid na simu kukatwa na sasa foleni ilianza kusonga mbele na hakutaka hata kuzubaa alikanyaga pedeli na gari hilooooo



"Hongera sana shemeji" Jimmy alitoa pongezi



Dakika kadhaa mbele Cadillac Escalade lilikuja kusimama nje ya jengo kubwa la hospitali binafsi na walishuka wanaume wawili, Cid na Jimmy

Cid akiwa amebeba "b onquet la maua mekundu(rose flowers) mkono wa kulia huku wa kushoto amebeba mdoli mdogo wa manypya rangi nyeupe, upande wa Jimmy naye alimsaidia kubeba mfuko ambao ndani yake haukujulikana kuna nini



Cid hakutaka kupoteza muda alitembea haraka haraka akifuatwa na Jimmy mpaka kwenye lift na kubonyeza kitufe na mlango wa lift kufunguka na kuingia kisha kubonyeza kitufe cha kuwapeleka floor husika.



TO BE CONTINUED..........
 
Bt Samuel jk_Euphoria

SOLO KING: ANCIENT LEGACY

CHAPTER 19: Mwanasheria na mshauri wa kisheria


Ndani ya dakika moja lift ilikuja kufunguka kwenye floor ya nne ya ghorofa la hospitali hiyo na Cid alitoka haraka haraka akikimbilia kwenye chumba alichokuwepo mke wake



Jimmy baada ya lift kufunguka na kutoka hakuwa na haraka kama ilivyo kwa Cid, yeye alitembea tu polepole na hakuingia kwenye chumba alichoingia Cid, alikwenda kukaa kwenye benchi nje ya chumba kile



"Mke wangu mumeo nimefika" aliongea Cid baada ya kuingia na kumkuta mkewe amembeba mwanaye kwenye mikono yake akimnyonyesha pembeni wakiwa wanawake watatu wamesimama na nyuso zilizojaa tabasamu



Alikwenda kukaa karibu na mke wake akiweka maua pembeni na kumbusu yeye pamoja na mtoto wake akitoa tabasamu macho yake yakiwa na majimaji akitaka kulia kwa furaha



"Umefanana nae" aliongea, Monica mke wake akimwangalia usoni Cid na wote wakitabasamu



"Yeah... ni copy yangu halisi lakini hayo macho amechukua kwa mama yake" aliongea Cid na monica are muangalia mtoto wao tena machonk na kucheka kidogo



"So beautiful and handsome" aliongea monica na Cid alikubaliana naye bila ubishi



"Kwa hiyo unakwenda kuzubaa tu bila kumbariki jina mwanao?



" kama tulivyokubaliana akiwa ni kidume kama baba yake nampa jina mimi na kama akiwa mrembo kama mama yakd basi ni haki yako ila naona ushindi umeangukia kwangu haha! "



" Lione kwanza, ole wako umpatie jina baya"



"Nawezaje kumpatia jina baya mrithi wa utanashati wangu? Ukweli nilishajiandaa muda, sana"



"Enhee nataka kulisikia"



"Alexander, ni jina zuri sana hili lenye maana ya shujaa, mtetezi wa wanadamu kama mfalme wa macedonia Alexander the great"



"Ni jina zuri lakini bado sioni linamfaa unaonaje tukimwita Freddie ni zuri linaashiria amani"



"Hey little boy unaonaje jina alilokupa mama yako kipenzi" Cid aliongea na mwanaye huku akichezea pua lake kwa na mtoto aliitikia kwa tabasamu la kitoto



"Hehe siovmbaya kama umelipenda najua asingeniruhusu nikupe jina maana mama yako hakubali kushindwa" aliongea Cid akimuomba ambebe mtoto na alipewa



Upande wa wanawake watatu walioko pembeni walikuwa ni mama yake monica ambaye ni mama mkwe kwa Jimmy, jina lake sikuwaambia aliitwa Mary, mwingine alikuwa ni mama yake Cid na mwingine alikuwa ni Sophia na hakuwa yule mwanamke kauzu, alikuwa amelegeza safari hii.



"Mke wangu nina suprise yako" aliongea Cid na kugeukia mlangoni na alionekana Jimmy akiingia ndani ya chumba hicho na aliziba mdomo wake kumuona mdogo wake ambaye hakumuona kwa muda mrefu



Na hata wakwe zake na mama yake waligeukia mlangoni na waliishia kushangaa nyuso zao zikiwa hazielezeki ni hisia gani walijisikia wakati huo



"Jimmy aliishia kuwaangalia kwa tabasamu kana kwamba halikuwa jambo kubwa sana



" Hello family"aliongea kwa sauti ya upole



Mwanamama Mary alimsogelea Jimmy uso wake ukibubujikwa na machozi na alimkumbatia mwanaye kwa nguvu kana kwamba angepotea muda wowote na hakutaka hilo litokee



" Mwanangu ni wewe kweli?" aliongea mwanamama huyo baada ya kutoka kwenye kumbatio



"Ni mimi mama nimerudi" alijibu na mwanamama mary alishusha pumzi ya ahueni



"Ni jambo zuri umeongezeko mwili na kimo umezidi kuwa mtanashati" aliongea mwanamama mary akimpapasa mashavu yake na kumchunguza



"Ulienda wapi?" mwanamama huyo aliuliza na Jimmy alijikuna kichwa chake.



"Ma mkwe ndio amerudi nchini leo hajapumzika baada ya safari ndefu unaonaje akapumzika kwanza halafu ndio tumuulize maswali"



"Nje ya nchi? Miaka mitano nje ya nchi? Si ulisema unaenda Chuo mkoani dodoma, Bro umevuka mipaka" aliongea monica akimgeukia Cid



"Na wewe kwanini ulitukalia kimya miaka yote hiyo"



"Mke wangu usiniangalie hivyo sikujua kama alienda nje ya nchi ni juzi tu hapo alinitafuta kwenye simu akiniambia nije kumpokea uwanja wa ndege, tangu aondoke sikuwasiliana nae wala, sikujua alikoenda" Cid alianza kujiteyea



"Na kwanini hukututaarifu hiyo juzi" Cid alojifanya kama vile hajasikia na kuweka umakini wake kwa mtoyo



"Monica usimlaumu mumeo sio kosa lake ni mimi niliemwambia asiwataarifu"



"Kumbe! Ulitegemea labda tutafurahi ukujitokeza baada ya miaka mitano, si ndio" aliongea monica sauti yake ikibadilika kutoka ya hasira hadi uchungu



"Hivi unajua ni wasiwasi kiasi gani tuliokuwa nao tukitegemea urudi nyumbani baada ya miaka mitatu ya masomo lakinj hukurudi?"



"Monica inatosha sasa, mdogo wako amerudi salama hilo ni jambo la kushukuru" aliongeza mwanamama mary na Monica alinyamanza



"Umerudi sasa mwanangu sitokuuliza ulikuwa wapi isitoshe wewe ni mtu mzima tayari, karibu nyumbani" alimkaribisha



"Kijana karibu nyumbani kwa mara nyingine tena" aliongea mwanamama velora kwa tabasamu

Upande wa, Sophia aliishia kumtolea tavasamu bila ya kuongea neno



"Ni nini hiyo umebeba?" Monica aliuliza



"Ooh hii ni zawadi kutoka kwa mumeo ni vitabu vyenye picha picha za kuvutia kwa watoto wachanga kutazama" aliongea Jimmy



"Usiishie kusimama hapo tu njoo umsalimie na umbebe mpwa wako" aliongea Cid na Jimmy aliweka ule mfuko chini na kwenda karibu na Cid na taratibu alikabidhiwa freddie mdogo



Mara baada ya freddie kutua mikononi mwa Jimmy alizidi kuachia tabasamu lake la kitoto



"Inaonekana tayari ameshakukubali mjomba wake" aliongea mwanamama Mary na wote humo ndani ya chumba walitabasamu



Kwakuwa Monica alionekana yuko sawa na afya tele licha ya shughuli pevu ya kujifungua hakuona haja ya kuendelea kubaki hapo, aliomba ruhusa kwa daktari kama anaweza kuondoka na aliruhusiwa baada ya vipimo na kukuta yuko



Walipumzika kwa masaa mawili na baadae ya masaa hayo kupita walianza kufanya mchakato wa kuondoka na ndani ya dakika kadhaa magari mawili yalikwenda kusimama kwenye geti lenye uzio mrefu na baada ya honi getu lilifunguliwa na magari hayoyaliingia ndani na kwenda kupark kwenye gereji lenye magari si chini ya tano na hayo mawili yaliongeza idadi na bila shaka jumba hilo lilikuwa kubwa na la kifahari



Walishuka na kuingia ndani, wakati wanafika hapo Jimmy alikuwa anashangaa mazingira ya eneo hilo na kulikuwa na walinzi wakilinda nyumba hiyo, aliwaona nane lakini hisia zake zilimwambia hio sio idadi yao kamili kuna wengine zaidi labda hao wengine wako upande wa nyuma wakilinda



"Bro welcome home!" Cid alimkaribisha Jimmy



"Mmehama huku sio?" aliuliza



"Ndio baada ya lile tukio miska ile hatukukaa sana tukihofia wale mashetani watarudi hivyo tulihamia huku na kuimarisha ulinzi na haya ndio makazi yangu mpaka sasa" Cid alimweleza Jimmy



"Kwahiyo hili jumba lote ni wewe na mke wako tu ndiyo mnaishi"



"Ndio ninaishi na mke wangu masuala ya kuishi familia nzima kwenye nyumba moja ni kunyimana uhuru tu ni vile tu wapo hapa kututembelea " aliongea Cid



"Sema walikuwa wanahakikisha mjukuu wao anazaliwa salama" aliongea Jimmy



"Vyovyote vile kila mtu ana makazi yake"



"Vipi mama anakaa wapi, usiniambie anaishi peke yake" aliongea Jimmy



"Haha usiwe na wasiwasi mama yako ni mama yangu pia nisingemwacha aishi maisha kipweke, nimemnunulia nyumba na kuwaweka wasaidizi wa kumuangalia pia....."



"Pia nini?"



"Aishi na wafanya kazi tu kuna mwingine"



"Mwingine nani huyo ebu acha kuzunguka zumguka bro"



"Kama unataka kumjua kwanini usiende kumtembelea kwake umjue" Cid aliongea hakutaka kuendelea kuzungushwa, zungushwa aliamua kupotezea



"Vipi hakuna kilichotokea chochote kile cha kutishia usalama?" alouliza swali jingine



"Hamna bro tangu siku ile mpaka leo tumeishi kwa amani pia mzee baada ya kupata taarifa aliwaweka watu wake kwaajili ya usalama, hao walinzi unaowaona si wa kawaida ni kutoka jeshini wamepitia mafunzo ya hali ya juu" aliongea Cid na Jimmy hakushangaa sana maana mzee wao ni Mkuu wa majeshi ya usalama wa nchi kuweka vijana kutoka jeshini kulinda familia yake lilikuwa ni suala dogo kwake



Walipokelewa na vijakazi wawili baada ya kuingia ndani l, Cid na Monica walipandisha ngazi kwenda juu wakiwaacha wengine huko chini



"Mwanangu utakuwa na njaa sana si ndio? " aliongea mwanamama Mary na Jimmy alitingisha kichwa kukubali



"Sawa ngoja niingie jikoni kuwaandalia chakula" aliongea mwanamama Mary



"Haina haja ya kujisumbua kuna vijakazi wataandaa vizuri tu" aliongea mwanamama Velora lakini Mama Jimmy hakutaka kuzubaa tu akasema huyo ni mwanae na ni jukuma lake kumuandalia. Nani angempinga? Isitoshe walielewa mapenzi ya mama kwa mtoto wake na ni miaka mitano imepita hajamuona mtoto wake.



Baada ya mwanamama Mary kwenda Jikoni pamoja na vijakazi kuandaa chakula walibaki watatu. Jimmy, Sophia na mwanamama Velora



"Hey Jimmy tunaweza kuzungumza mawili matatu kupoteza muda kama hutojali" aliongea mwanamama velora



"Sio mbaya tunaweza kuzungumza" hakuona haja kukataa na walikaa sofani wote watatu



"Niambie kuhusu taaluma uliyosomea huko nje naamini hukwenda nje kuzurura"



"Oh kwakuwa umeuliza nitakujibu nimesomea sheria, mimi ni mwanasheria na vilevile ni mshauri wa kisheria"



"A lawyer and a legal advisor what a talent" aliongea Sophia kwa kiingereza akimaanisha mwanasheria na mshauri wa kosheria ni kipaji



"Hiyo ndiyo ndoto uliyokuwa unaniambia unaifukuzia mpaka kukataa ofa yangu?" aliuliza Sophia



Jimmy alitabasamu na kuongea "Hapana ni hobbt yangu"



"Oh kumbe sikujua una hobby nyingi hivyo" aliongea, Sophia



"Kweli wewe ni mwanasheria na vilevile mshauri wa sheria?" aliuliza mwanamama Velora akiwa kama haamini vile



"Huniamini?" Jimmy alimuuliza



"Hapana ni vile hio kazi inahotaji kichwa kisicho na mambo mengi ili kukijaza sheria nyingi"



"Kwa maana hiyo bado unaonyesha huniamini au sio bi mkubwa?



" kutokumuamini mtu sio kosa unaonaje ukaniaminisha maana bwana mdogo kama wewe ni ngumu kuwa taaluma zote mbili"



"Nimeambiwa hivyo mara nyingi nilipojitambulisha lakini ni kweli nimekuwa nikisomea taaluma ya uanasheria na kubahatika kufanya kazi huko nje na pia ushauri wa kisheria ni sehemu muhimu pia ya kazi kwa mwanasheria"



"Unapaswa kunishawishi. Unafanya nini hasa katika majukumu haya mawili? Tofauti zao zikoje na usinitupie maneno magumu nielezee kwa maneno simple yanayoeleweka"



"Tuanze na mwanasheria. Mwanasheria ni mtu aliyesomea sheria, akafaulu mtihani wa uwakili, na akapewa ruhusa ya kisheria kumwakilisha mteja wake mahakamani. anawatetea watu, anashtaki wahalifu, anashughulikia kesi za madai, anatengeneza nyaraka za kisheria kimsingi, anahakikisha sheria inafuatwa na kutekelezwa ipasavyo na tukija mshauri wa kisheria yeye si lazima aende mahakamani. Badala yake, anatoa mwongozo wa kisheria kwa watu binafsi, biashara, au mashirika. Anawasaidia kuelewa sheria, kuepuka matatizo ya kisheria kabla hayajatokea, na kuhakikisha wanazingatia kanuni na taratibu"



"Hilo nalijua nipo mfano mwingine"



"Chukulia mwanasheria kama askari anayepigana mahakamani, na mshauri wa kisheria kama jenerali anayepanga vita kabla haijaanza"



"Oh na unafanya vyote"



"Ndio"



"Lakini wanasheria si tayari wanatoa ushauri?" Sophia aliulizwa



"Ndio, lakini kuna tofauti. Mwanasheria anatoa ushauri ndani ya muktadha wa migogoro ya kisheria au kesi mahakamani. Mshauri wa kisheria, kwa upande wake anajikita zaidi katika kuzuia matatizo ya kisheria kabla hayajatokea na kuhakikisha ufuataji wa sheria.simple like that"



"Sawa, hebu tuseme mimi ni mmiliki wa kampuni. Nikiamua kukuajiri kama mwanasheria wangu, utanifanyia nini?" Mwanamama Velora alitaka kumpima kwa swali



"Mbona kila kitu kipo wazi kwenye maelezo yangu" Jimmy hakutaka kutumia nguvu sana kumshawishi



"Tuseme nimekuamini, swali je utawezaje nisaidia kwenye kampuni yangu kuepuki kulipa kodi nyingi, nielezee japo kwa ufupi"



"Hahaha sawa nitakupa dodoso tu twende kwenye kodi, kofi kwa lugha rahisi tuseme ni kikapu cha serikali, serikali inakwambia "UBi mkubwa umepata pesa? Weka sehemu yake kwenye kikapu chetu. Kwaajili ya kuiendesha nchi" Lakini pia inakwambia "Ukifanya mambo fulani, unaweza kuchukua pesa fulani ndani ya kikapu kabla hatujazichukua." Hayo 'mambo fulani' ni makato na mikopo ya serikali"



"Bado sijakuelewa nipe mfano rahisi" mwanamama Velora alionekana kutokuelewa



"Tuseme unatoa mchango kwa shirika la hisani. Serikali inakushukuru kwa hilo kwa kiasi ulichotoa kwenye mapato yako yanayotozwa kodi. Ikiwa ulipata $50,000 mwaka huu na ulichangia $5,000 kwa hisani, unatozwa kodi kwenye $45,000 na sio $5000"



"kwa hiyo kutoa si tu kwa ajili ya kusaidia bali pia ni ujanja wa kifedha?"



"Hehe inshort serikali ni wahuni sana nadhani hata wewe unajua hilo" Jimmy aliongea na kumfanya mwanamama Velo kutabasamu



"Okay nieleze namna ya kuepuka kulipa kodi nyingi"



"Hapo ni sawa na kuuza siri za kambi"



"Hahaha inaonekana unajua vizuri kuhusu taaluma yako unaonaje nikikuajiri kama wakili na mshauri wa kisheria kwenye kampuni yangu" aliongea mwanamama Velora



"Not interested" alikataa bila kusita



"Name the price" aliongea Sophia



"Hey wewe Sophia nishamuwahi huyu ni wangu tafuta wako" aliongea mwanamama Velora



"Sijali siku zote biashara ni vita tu na atakaeshinda ndiyo mwenye kubeba kinachoggombaniwa" aliongea Sophia



Na saaa ikawa ni kumgombania Jimmy kama mwanasheria kati ya mama na mwana lakini mgombaniwa wala hakujali alinyanyuka baada ya kusikia harufu ya chakula mezani



"Mnaonaje tukale chakula nina njaa sana" aliongea Jimmy na wote waliishia kumwangalia tu na kujiambia kijana anaringa sana



Wakati wanamuangalia mara mlango wa kuingilia ndani ukafunguliwa na aliingia mwanamke mrembo, mzuri wa sura, ule uzuri wa asili alikuwa amevalia Shirt la mikono mirefu lenye draft viboksi vyeusi na jinsi ya bluu pamoja na rubber nyeupe na kuangaliana uso kwa uso na Jimmy aliyesimama sebuleni



TO BE CONTINUED...................
 
By Samuel jk_Euphoria

SOLO KING: ANCIENT LEGACY

CHAPTER 20: Nimesema usinisogelee


Bianca alikuwa amezidi kuwa mrembo maradufu na umbo lake lilizidi kuvutia, nyuma yake kulikuwa na walinzi wakike watatu wote wakiwa wamevaa suti nyeusi wakitoa ulinzi



Jimmy alikuwa akitazamana naye uso kwa uso kwa hisia zisizoelezeka walitazamana kwa sekunde kadhaa bila kutoa neno ni kama vile macho yao ndiyo yalikuwa yakizungumza na walishtuliwa kutoka kwenye kuzubaa na sauti ya mama yake



"Hatimae supa staa wetu amefika, karibu ndani" aliongea mwanamama Mary alipomsogelea na kumkumbatia



"Mnisamehe nilikuwa bize sana na kukosa nafasi ya kuja kwa wakati" aliongea, Biancalina



"Usijali tunaakuelewa pia wifi yako amejifungua salama"



"Bila shaka katakuwa ni kazuri kama mama yake"



"Dogo amerithi sura ya baba yake wewe" aliongea Cid akishuka chini kwenye ngazi



"Hey Jimmy amerudi umemuona? " aliongea, Cid kwa makusudi kama vile Bianca hakumuona



"Nataka nimuone mpwa wangu basi yuko wapi" alibadili mada ilionekana hakutaka kuliongelea hilo swala na alimuelewa



"Yuko juu na mama yake ila usiwaze utamuona kesho sasahivi amelala na sitaki damu yangu isumbuliwe" aliongea Cid kibabe



"Mbona unakuwa mchoyo hivyo bro, kwani kumtazama nitamuasha ebu acha unoko" aliongea Blandina



"Kweli ni mnoko huyo ebu njoo kipenzi chetu ukamuone mpwa wako" aliongea Monica aliyekuwa juu ya ngazi na Blandina alifurahi na kupandisha juu akiwaacha walinzi wake sebuleni, alienda na Monica kumuona freddie katoto.



Cid hakuwa neno aliishia tu kuwatazama wakipotelea juu na alienda mpaka karibu na, Jimmy na kumpiga piga bega ni kama vile alikuwa akimwambia "It's alright bro"



"Chakula tayari msiishie kuzubaa tu hapo ebu njoeni mezani mpate kula" aliongea mwanamama Mary na wote walikubali na kwenda kuketi "Dining table" isipokuwa wale walinzi wanawake waliokuja na Bianca

Mwanamama Mary aliwasihi nao wajiunge kupata chakula cha usiku lakini waliweka ngumu wakidai kwamba wapo kwaajili ya kutoa ulinzi na hawanisikii kula



"Haina haja ya kuwa siriaz hivyo ebu legezeni kidogo basi isitoshe sio kama walinzi mpo peke yenu kuna wengine wako nje hivyo msiwaze sana kuhusu usalama" aliongea Cid na wale walinzi waliangaliana wao kwa wao na walikubali kishingo upande



Dining table ilikuwa na viti kumi na mbili hivyo viliwatosha wote na nafasi zilibaki na haukupita muda Monica na, Bianca nao walishuka na kuungana kukamilisha idadi ya watu kumi kwenye meza ya kulia chakula



Kwenye meza kubwa umbo la mstatili lenye pande nne, upande wa urefu kulia na kushoto vilikuwa vitano na upande wa upana kilipatikana kiti kimoja kila pande, sasa katika upande wa kulia wa urefu waliketi Sophia, mwanamama Velora, Mary, na walinzi wawili wa kike, na upande mwingine wa urefu wa meza waliketi Jimmy, mlinzi mmoja wa kike, Cid, Monica na Biancalina



Chakula kilikuwa ni cha kutosha hivyo kila mtu alipakuwa kiasi chake na kabla ya kuanza kula mwanamama mary aliingilia kati



"Hakuna kula bila ya sala, lazima sala kwanza" kila mmoja aliangaliana na mwenzake, ilikuwa ni wazi hakuna aliyetaka kusali



"Jimmy unaonaje ukisali ni muda sana hatujaisikia sauti yako" Cid aliamua kumtupia mzigo mwenzake



"Kwahiyo umeona unitupie mzigo bro ila sio mbaya" Jimmy alijiwazia na kila mtu alikuwa akimuangalia wakisubiri sala Isipokuwa Bianca ambaye hakujisumbua kumuangalia



"Sawa nitasali, fumbeni macho" alitoa muongozo na walifumba



"Mungu mpendwa, asante kwa chakula hiki. Naomba ukibariki tukila tunenepe ila sio kwa mwili wangu maana sipohitaji unenr. Tafadhali kifanye kifanye chakula hiki kiwe kitamu zaidi ya kinavyoonekana, na kwa aliyepika, mpe baraka za nyota tatu za Michelin. Pia, kama kuna mtu anawaza kuiba chakula changu, fanya mikono yake itetemeke kidogo ili ajute. Amina!" alimaliza kuomba



" Bro sikujua unajua kusali hivi haha hongera! " Cid aliongea huku akicheka baada ya kufumbua macho



" Sio mbaya lakini mnaweza kuanza kula"aliongea mwanamama Mary na kila mtu alikula



Ulikuwa ni mlo wa kimya kimya ni sauti za mitafuno na vinjwaji kupita kooni ndizo zilisikika na baada ya zaidi ya nusu saa walikuwa wamemaliza kula na walikuwa bado wameketi mezani lakini idadi yao ilipungua, wale walinzi watatu waliondoka mahali hapo, pia meza ilikuwa imeondolea vyombo na kusafishwa



"Taja bei yoyote unayoitaka nami nitaongeza mara mbili yake" Sophia alivunja ukimya akimlenga Jimmy



"Kuna nini kwani?" mwanamama Mary aliuliza



"Mwanao ni wakili na mshauri wa sheria vilevile shida hataki kuajiriwa" mwanamama Velora alimtoa gizani



"Ooh kumbe, bila shaka ndiyo taaluma uliyokuwa unasomea?" aliongea mwanamama Mary



"Jimmy kwanini usikiubali tu kuajiriwa isitoshe tumeshakuwa familia" aliendelea



"Hapana mama sio kama sitaki, mimi ni wakili wa kujitegemea sitaki maswala kuajiriwa kwangu mimi naona ni kama vereza tu, unasaini mkataba wa miaka kadhaa na kwenye mkataba unakuta kuna vipengele vinavyokuzuia kufanya vitu kadhaa, naona ni sawa na kunyimwa uhuru hivyo sipo interested" Jimmy aliongea



"Nilidhani labda utabadilika kumbe bado ni yule yule tu hata hivyo ni uamuzi wako sitolazimisha" aliongea mwanamama Mary na alionekana kumjua vizuri mwanae, kifupi Jimmy kama hataki kitu ndio hataki hata umuahidi pesa kama amegoma ndiyo amegoma, alikumbuka jinsi jimmy alivyokuwa mbishi kwenda kanisani tangia utoto wake mpaka anakuwa mkubwa alitumia kila mbinu kumshawishi lakini wapii.



"Ulinikatalia ofa yangu kipindi kile na bado leo pia unakataa inaonekana unaringa sana" aliongea Sophia



"Vyovyote unavyoona wewe sawa tu ila kama utataka tufanye biashara sawa tutakubaliana malipo na baada ya kazi kuisha kila mtu anashika njia,najua kama boss unayemiliki lebo kubwa ya muziki lazima kuwe na kesi za wasanii mbalimbali ila kuhusu suala la kuniajiri sahau" aliongea Jimmy huku akitabasamu



"Hehehe huyu ndo Jimmy nimjuaye mimi" aliongea Monica akicheka



"Anyway tumejumuika kama familia hivyo masuala ya biashara wekeni pembeni" aliongea Cid na walikubaliana



"Jimmy unamuona supa staa wetu hapa?" aliongea Monica akiweka mkono begani mwa Bianca aliyekuwa pembeni yakw kirafiki



"Supa staa?" aliongea kwa kuuliza huku akimwangalia Bianca ambaye naye alikuwa akimwangalia pia kikauzu



"Unaonekana hujui hata hivyo sikulaumu maana ulipotea" aliongea Monica



"Bianca ni super star wa bongo anayetamba na kibao cha SIO MBAYA, na nyinginezo lakini SIO MBAYA ndio inashika namba moja kwa kusikilizwa na mashabiki wake, alianza safari yake ya muziki wa R&B(Rythm n blues) miaka miwili iliyopita japo wabongo tunaita bongofleva lakini zaidi ya hivyo" Cid alichukua nafasi ya Monica ya kumuelezea Bianca, alikuwa akiongea kwa kujivunia kuwa na dada ambaye ni maarufu kwenye tasnia ya muziki



"Bro nakwambia nimeisave kabisa hiyo nyimbo inahuzunisha sana na kutia moyo pia ni songi moja matata sana la taratibu la kiswainglishi" Cid aliendelea na kufanya wote watabasamu



"Unavyoongea utadhani ni wewe ndiye uliyeimba kumbe" aliongea mwanamama Veloea mama yake Cid



"Kwani kuna ubaya kuwa shabiki yake" Cid alionfea



"Shida umepitiliza sana kwenye sifa huo ni uchawa" aliongea Sophia



"Mradi sifa ni za kweli mi sijali mkiniita nachawa" aliongea na kutoa simu yake iliyokuwa mfukoni na kuanza kubonyeza bonyeza kioo cha simu nsa baada ya sekunde kadhaa aliiweka simu yake kwenye meza



Watu walikuwa wakimuangalia anachofanya na walielewa baada ya kusikia sauti ya mdundo wa muziki, ilionekana aliidownload kabisa hiyo nyimbo na ilikuwa ni original kabisa



🎶Huanzaga hivi na hivi na hiviii🎶

🎶Moja, mbili, tatu mpaka tamatiii🎶

🎶Mwisho huwaga ni maumivu moyoniii🎶

🎶Mawazo usiku kuchaaa🎶

🎶Ila sio mbaya (sio mbayaaa) 🎶

🎶Nimejifunza kitu kipya, dunia haiko sawaaa🎶

🎶People ain't fair nor do they care🎶





🎶 But it’s alright, I’ll be just fine 🎶

🎶 No regrets, just lessons in time 🎶.........



Walisikiliza mpaka inaisha, Ilikuwa ni nyimbo ya taratibu yenye huzuni na kutia moyo, sauti pia ilikuwa ni zaidi ya neno "tamu" yenye kugusa mioyo ya wengi



"Bro unaionaje hiyo?" Cid alimuuliza Jimmy



"Perfect, nyimbo nzuri sana, utunzi mzuri unaoelezea hisia za kutelekezwa, maumivu, na uvumilivu. Mashairi yake yanatiririka kwa urahisi, yakitengeneza simulizi ambalo ni la kibinafsi lakini linagusa mioyo ya wengi. Bila kusahau mchanganyiko wa Kiswahili na Kiingereza unaipa nyimbo mvuto wa kipekee,".alijibu akitoa na ishara ya kidole gumba huku akitabasamu



"Hey Biancalina that's a beautiful song out there! "Jimmy alimsifia



Bianca baada ya kusikia sifa hizo kutoka kwa Jimmy alisimama



" Muda umeenda hivyo napaswa kuwahi kesho nina shughuli nyingi za kufanya" aliongea na na bila kusubiri jibu alipiga hatua kuondoka na walinzi wake walimfata nyuma



"Bila shaka Sophia alitaka kumsainisha mkataba ila inasikitisha kwamba ulikataliwa bila kujali undugu" aliongea, Cid huku akimsikitikia Sophia na alipigwa jicho kali na mke wake mpaka alihisi nafsi ikitaka kumtoka na aliacha mara moja kile alichokuwa anafanya(kusikitika)



Ukweli ni kwamba Bianca alikuwa ni mwanamuziki chipukizi wa kujitegemea ambaye kazi yake hiyo ya uimbaji imewagusa na kukubalika na wengi sana na kufikia hata mabosi wa label kubwa za muziki kutaka kumsainisha mkataba lakini aliwagomea katakata sembuse dada yake Sophia akiwa na sababu zake binafsi



Jimmy naye alinyanyuka akielekea mlango kisha kuufungua na kutoka nje na aliwezs kumuona Bianca amesimama akiangalia mbalamwezi iliyokuwa iking'aa angani usiku huo lilikuwa limekamilika umbo la mduara kamili



Alitembea kumsogelea Bianca na alipokuwa umbali wa kama mita kumi Bianca alimzuia asimsogelee



"Usinisogelee" aliongea bila kugeuka lakini Jimmy alikuwa ni kama vile hasikii kwani aliendelea kusogea tu



"Nimesema usinisogelee" aliongea tena kwa sauti aliposikia hatua za miguu zikizidi kumkaribia



"Tafadhari bwana mdogo madam amesema usimsogelee ishia hapo hapo" aliongea mlinzi wa kike na ndiye mwenye mamlaka kwa wenzak lakini Jimmy hakuja kauli yake na alizidi tu kusogea



"Kijana usifanye mambo kuwa magumu" aliongea mlinzi yule akimsogelea asizidi kumkaribia Bianca na Jimmy aliishia kusimama



"Una uhakika hutaki nikusogelee" aliongea Jimmy akimwambia Bianca



"Sitaki unisogelee" alikazia maneno yake bila kugeuka nyuma ila sauti yake ilibadilika kidogo



"Mbona nahisi kama sauti yako haiko sawa" aliongea Jimmy



"Damn it! Nyamanza wewe mzimu" aliongea kwa hasira akimgeukia na macho yalikuwa na maji maji alikuwa akijizuia na Jimmy alinyamanza



"Unatoweka tu kama mzimu kwa miaka kadhaa bila hata kutujulisha ulikuwa wapi na sasa unajitokeza kama vile hakuna kinachotokea" aliongea kwa kufoka



"Lakini nimerudi" aliongea kwa upole



"Na kuhusu ile ahadi uliyoweka kwamba utanisubiria? Umeitimiza?" alimuuliza na Jimmy alibaki kimya



"See now, you took me for granted all the times"



"Hapana sio hivyo ni.... "



"Sio hivyo? Ni nini?" alimkatisha kabla hata hajamaliza kujielezea



"Kwanza sitaki kusikia maelezo yake" Bianca aliongea na kuingia ndani ya gari



"Usifikirie kabisa" mlinzi alimuwahi Jimmy aliyekuwa akitaka kumfuata Bianca na aliishia kusimama vilevile hakutaka kuwapa wakati mgumu walinzi hao pia hakutaka kumkasirisha zaidi Bianca



Aliishia kuamgalia Alphard nyeusi waliyokuja nayo ikiondoka ndani ya jumba hilo bila kufanya chochote, alibaki akisimama vilevile akitoa tabasamu la uchungu na aliweka mikono yake mfukoni na kurudi zake ndani



"Bro leo unalala hapa sawa? Kuna vyumba vya kutosha ni wewe tu uchague unalalia kipi" aliongea Cid mara baada ya Jimmy kuingia



"Hapana huyu nakwenda naye nyumbani nimemmisi mwanangu" aliongea mwanamama Mary ambaye alikuwa anataka kuondoka pia



"Lakini..."



"Hapana hakuna cha lakini huyu naondoka naye kwaherini tunaonana kesho" aliongea mwanamama mary na bila kusubiri jibu alimshika Jimmy mkono na kutoka naye nje na waliishia kuwasindikiza na macho tu



Sophia naye alishusha pumzi nyingi kuashiria amechoka na aliwaaga na hata kabla ya kujibiwa kwaheri yake huyoo nje na alibaki mwanamama Velora ambaye aliwaaga kwa kumkumbatia mwanae na mkwe wake pia akiwapiga mabusu ya shavuni kama zilivyo tabia za wakishua walio wengi, wahuni tunasema uzungu mwingi!



Baada ya kama lisaa limoja ya safari kutokana na foleni ya husika waliweza kutoka osterbay yalipo makazi ya, Cid na mkewe na kuingia mtaa wa mbweni na baada ya gari kukatiza kona mbili tatu za hapa na pale walikuja kusimama kwenye geti kubwa jeusi na baada ya honi kupigwa geti lilifunguliwa na gari liliingia ndani



Lilikuwa ni jumba la kisasa na la kifahari lenye ghorofa moja, halikuwa kubwa sana wala dogo lilikuwani la wastani, lilikuwa ni umbo la box fulani hivi(nadhani mmenipata) halikuwa na bati kifupi ilikuwa na roof juu yake, nisielezee sana kuhusu jumba hilo hilo ila ieleweka lilikuwa ni la kifahari



Licha kuwa usiku taa za teknolojia ya hali ya juu zilizoko kila upande zilimulika jumba hilo na mazingira kuonekana vizuri kwa macho



Gari lilikwenda kupaki na dereva ambaye alikuwa ni mama yake Jimmy alishuka na Jimmy pia alishuka akitazama mazingira ya jumba hilo lakini macho yake yalitua kwenye gari moja lililoegeshwa pembeni ya gari walilofika nalo



Lilikuwa ni lilelile Alphard waliloondoka nalo Bianca na walinzi wake na palepale alielewa yule "mtu mwingine" Cid alimzungumzia kumbe ni Bianca bhana!



Aliishia kufurahi tu moyoni na kujiambia kumfukuza kote kule lakini nani angejua baada ya lisaa limoja watakutana tena



"Karibu nyumbani Jimmy" aliongea mwanamama Mary akimkaribisha mwanae na kuongoza njia huku Jimmy akimfuata nyuma yake mkononi akishika begi lake la nguo



TO BE CONTINUED.........
 
By Samuel jk_Euphoria

SOLO KING: ANCIENT LEGACY

CHAPTER 21: Sioni tatizo, anaweza kuishi nasi


Uzuri hakukuwa na ulinzi mkali kama walikotoka, zaidi kulikuwa na kamera kila kona na ilionekana kuna walinzi wana nyumba yao pia na Jimmy alikuwa sahihi kwani upande wa kushoto wa jumba hilo kulikuwa na nyumba nyingine ndogo na alijiambia watakuwa humo wakilinda kupitia kamera zionyeshwazo kwenye Tv ndogo ndogo

Mwanamama Mary alikwenda mpaka mlangoni na ile kufungua tu tu anakutana mlinzi wa kike akiwa anatoka

"Ndio umefika madam karibu ndani.... Wewe unafanya nini?" aliongea mlinzi huyo alipomuona Jimmy

"Zuhura nadhani ushajua huyu ni mwanangu hivyo haina haja ya kuwa serious hivyo na kuanzia leo ataishi na sisi" aliongea mwanamama Mary na kiongozi huyo wa walinzi aitwaye zuhura alikubali kwa kutingisha kichwa huku akimwangalia Jimmy kwa namna flani hivi, ilionekana hakumpenda na Jimmy alimpa tabasamu tu na sura yake ya kitanashati huku akitingisha nyusi makusudi kumchokoza na kuingia ndani akimuacha zuhuru akimsindikiza na jicho baya

Jimmy hakujali huyo mlinzi anamfikiriaje lakini ilionekana zuhura hakuwa haba, japo sura ya kibaba lakini umbo alikuwa ni "very sexy"

Basi baada ya kuingia ndani Jimmy alikuwa akishangaa shangaa jinsi kulivyopendeza, hakukuwa na samani nyingi sana ni zile muhimu tu, mwanga wa ndani ulikuwa hafifu kama jua la jioni licha ya taa kuwa nyeupe, ndani palitafsiri aina ya watu waishio humo ni watulivu wasio na mambo mengi.

"Utakuwa umechoka subiri nikakuandalie chumba" aliongea mwanamama Mary na kuchukua begi mikononi mwa Jimmy na kupandisha juu

Jimmy alikuwa akichunguza chunguza ndani humo kwa kama dakika tatu na hatimae mama yake alishuka chini ikionekana maandalizi yalikuwa tayari

"Twende nikakuonyeshe chumba chako" aliongea

"Mama" Jimmy aliita

"Naam mwanangu" aliitika

"Unachukia kwa mimi kuondoka na kutowasiliana nanyi kwa miaka yote hiyo?" aliuliza na kumfanya mama yake atabasamu

"Namchukiaje mwanangu japokuwa sijui kwanini uliondoka bila kututaarifu lakini utakuwa sababu iliyokufanya hivyo pia umekuwa mtu mzima usiwaze sana" aliongea

"Kweli hujakasirika?"

"Ebu acha kufikiria sana kuhusu yaliyopita, muhimu ni kwamba umerudi salama na sitotaka kujua nini ulifanya huko ulikokuwa ila kama utataka kuyaongelea mimi nipo kukusikiliza sawa?" aliongea na Jimmy alitingisha kichwa kumuelewa

"Aya nenda ukaoge ulale maana hujapumzika toka urudi" aliongea mwanamama Mary na aliongoza njia na Jimmy alimfata mpaka kupelekwa kwenye mlango wa chumba chake

"Usiku mwema" aliaga mwanamama Mary na kuondoka

Jimmy aliufungua mlango wa chumba na kuingia, kilikuwa chumba kipana chenye hadhi flani ya kiuanaume, kulikuwa na Runinga ya flat screen, masofa mawili ya kupumzikia na bila kusahau bafu, ni kama walijua atarudi na kumwandalia chumba.

Kitu cha kwanza kufanya baada ya kuingia alikwenda kuoga kuondoa uchomvu kisha kuvaa nguo nyepesi na kujitupa kitandani kama mzigo na kufumba macho na ndani ya dakika tatu usingizi ulimchukua.

Saa kumi na moja asubuhi Jimmy alionekana nje ya nyumba hiyo kwenye bustani ameketi chini ya ardhi na kuikunja mjuu yake, ulikuwa ni ule mkao wa tahajudi na bila shaka alikuwa amefumba macho yake akivuta pumzi ndani na kuzitoa nje

Mpaka jua linachomoza na mwanga hafigu wa rangi ya dhahabu kummulika uso wake ndipo alifumbua macho na kutabasamu, alinyanyuka na kunyoosha viungo vyake vya mwili na kuingia ndani

Upande wa juu ndani ya nyumba Bianca alionekana akishuka na sura iliyochoka henye usingizi, ilionekana ndiyo anaamka muda huo. Alikuwa amevalia t-shati tupu kubwa jeupe liloacha mapaja yake yaliyonona wazi

Alikwenda moja kwa moja mpaka jikoni na kulisogelea friji kisha kulifungua na kutoa chupa yenye maziwa nusu na kulifungua na kugida yote, mara alipomaliza alihisi kuna mtu akimwangalia na alikuwa sahihi na alipogeuza shingo yake uelekeo aliohisi alikutana sura ambayo hakuitegemea na kushtuka

"Aaaah!!" alishtuka na kumrushia kopo mtu yule, na mtu yule hakuwa mwingine bali ni Jimmy, alikuwa amesimama pembeni ya uwazi wa kuingilia jikoni akishikilia glass ya maji akimkodolea macho lakini kabla kopo halijamfikia usoni alilidaka na mkono mwingine

"Habari za asubuhi mpenzi, umeamkaje?" Jimmy alisalimia kwa tabasamu mwanana

"Mpenzi? Yaani unavamia nyumbani kwangu halafu unaniita mpenzi?" aliongea kwa hasira na hasira yake iliongezeka baada ya kugundua Jimmy anakodolea mapaja yake

"You pervert!" alimaka na hakuwa na hamu ya kubaki pale na nduki alitimka kwenda juu. Jimmy aliishia lujichekesha na kugida maji yaliyobakia kwenye glasi aliyoishika na kuondoka kuelekea juu pia akisindikizwa na macho ya vijakazi wawili waliokuwa wakifanya usafi sebuleni

"Yule ndio mtoto wa madam mkubwa inaonekana amefanana sana na mama yake mkaka handsome" aliongea kijakazi mmoja aitwaye sandra

"Amemfanya nini madam mdogo mpaka kukimbilia juu vile" aliendelea kuongea kijakazi Sandra

"Acha umbea na wewe fanya kazi yako hayo mengine hayakuhusu shauri yako" aliongea mwenzake Aisha

Walijikuta wakiacha kuongea na kuendelea na kazi zao baada ya kusikia hatua za mtu kushuka kwenye ngazi na alikuwa ni mwanamama Mary na mara baada ya kumuona walisalimia na kuendelea na kazi

"Da sandra niandalie kifungua kinywa baadae kidogo nitatoka"

"Sawa madam" Sandra alijibu na kumuachia Aisha jukumu la usafi amalizie na kuingia jikoni kuandaa kifungua kinywa, pia mwanamama Mary alitoka nje kidogo kupigwa na jua la asubuhi lenye vitamin D na kutembea tembea kunyoosha viungo na baada ya dakika kumi alirudi ndani

Jimmy mara baada ya kuingia chumbani kwake alikwenda kuoga na alipomaliza alikwenda kwenye begi lake la nguo na kuzitoa zote na kuziamishia kwenye kabati la nguo na alichukua singlendi kubwa zile za wacheza mpira wa kikapu na kuvaa, ilikuwa ni singlendi rangi ya kijani na mbele ilikuwa na maandishi makubwa yasomekayo "LEGENDS" pia chini alivaa suruali jinsi nyeusi na mara baada ya kupulizia unyunyu alitoka

Ile anafungua mlango na kutoka upande wa kushoto wa Korido kama mita saba nao mlango ulifunguliwa pia na alitoka mrembo Bianca akiwa tayari amejiandaa na aliangaliana uso kwa uso na Jimmy

"Unafanya nini hapa?" Bianca alimuuliza

"Nani mimi?" Jimmy alijinyooshea kidole na kuangalia kulia, kushoto na nyuma yake kana kwamba hakuwa peke yake na kuzidi kumtia hasira mrembo huyo

"Naomba uondoke sitaki kukuona" aliongea Bianca akimfukuza mbele ya macho yake

"Kweli hutaki kuniona?" Jimmy alimuuliza na hakuonyesha dalili ya kutaka kuondoka na alipomaliza kutamka kauli hiyo mama yake alionekana akimsogelea

"Umeamkaje mwanangu?" mwanamama Mary alimjulia hali Jimmy

"Salama shikamoo mama" alijibu na kusalimia

"Marahaba ni vizuri kusikia hivyo, vipi na wewe Bianca umeamkaje?" aliitikia salamu kisha kumgeukia Bianca na kumjulia pia

"Salama mama hofu kwako?" Bianca aliitikia

"Mimi salama kabisa kipenzi, pia kuanzia leo tutakuwa tunaishi na Jimmy kama hujapenda unaweza niambia mwanangu" aliongea mwanamama Mary

"Sioni tatizo anaweza kuishi nasi" alijibu huku akitabasamu na Jimmy aliyekuwa pembeni ya mama yake alikuwa akijizuia asicheke, alijiambia kukasirika kote huko kumbe una moyo mwepesi

Bianca alikuwa wa kwanza kushuka chini akifuatiwa na Jimmy na walikwenda mpaka mezani ambapo kifungua kinywa kilikuwa tayari kimeandalia

Kulikuwa na chai ya maziwa, chapati, keki za kuoka, mikate yenye peanut butter na matunda kadhaa

Wa kwanza kukaa alikuwa ni Jimmy na Bianca alikwenda kukaa upande mwingine wa meza mbali na mwanaume huyo na Jimmy wala hakujali zaidi aliweka umakini wake kwenye msosi, haukupita muda mwanamama Mary naye alishuka na kuungana nao kwenye meza akiwa tayari amejiandaa akivalia kikawaida kama ilivyo kwa wamama wasio na mambo mengi, ni gauni safi la kitenge na viatu pamoja na mkoba basi, hakuwa na haja ya kujisumbua na make up ilihali ni mzee tayari

"Mimi natoka naenda kumsaidia dada yako kulea mjukuu wangu maana hana uzoefu kwaherini" aliaga mara baada ya kumaliza kifungua kinywa

Na walibaki wawili hao na haikupita hata dakika moja Zuhura mlinzi wa Bianca alifika ndani humo akitembea kijasiri na kwenda kusimama pembeni ya Bianca

"Madam maandalizi tayari tunaweza kwenda" aliongea Zuhura na Bianca alisimama akitaka kuondoka

"Hey ndiyo nini kutaka kuondoka bila kumuaga mpenzi wako unapaswa kunipiga busu kwanza kabla ya kuondoka" aliongea Jimmy kauli yenye utata

Zuhura aliishia kukunja ndita baada ya kusikia kauli hiyo kutoka kwa Jimmy, upande wa Bianca uso wake ulkkuwa na hisia mchanganyiko kulikuwa na ile hali ya hasira, hali ya kutotegemea kauli hiyo na hali ya mshangao pia lakini aliamua kupotezea na kumwambia Zuhura aachane naye na waliondoka

°°°°°°°°°°

Upande mwingine kwenye eneo lisilojulikana ni wapi jijini dar es salaam, ndani ya chumba cha mkutano walionekana viongozi watatu waliovalia gwanda, wawili wakiwa na gwanda zenye vyeo vingi kuashiria viongozi wa juu wa jeshi, na mmoja akiwa na gwanda jeusi lisilo na cheo wala alama yoyote, na ilionekana kuna kikao kikiendelea

Mbele yao ilionekana skrini(screen) kubwa ukutani ya teknolojia ya hali ya juu na katika skrini hiyo ilionyeshwa ramani nzima ya mkoa wa Tanga

"Hapo. Sehemu ya E-17. Hapo ndipo palipotokea mlipuko wa nishati usiku uliopita... tena. Ni mara ya nne mwezi huu" aliongea aliyevaa gwanda jeusi na ngozi yake ilivyo nyeusi tii

"Unamaanisha wamejificha kwenye pango la amboni? Eneo lile ni hatari kupita maelezo. pango la asili na ufuatiliaji mdogo wa satelaiti... pia ni hatari." aliongea Luteni Jenerali Mwachitete

" Who cares? . Angalia hizi alama za joto. Ziko sawa kila wakati. Zimesambazwa kwa mpangilio. Hawa si vichaa waliotawanyika hii ni ngome kamili. Huenda hata ikawa ndio makao yao makuu" aliongea Jenerali John

"Hiki ndio kinachonitia wasiwasi sasa wamepotea baada ya lile tukio miaka mitano na ghafla tu wanaibuka tena mkoa mwingine, hapa tunazungu vichaa Jenerali"

"Bado haieleweki wanajipatiaje mahitaji yao. Kama wako pangoni, watapata wapi damu ya kutosha? Ni mbali sana na miji mikuu" aliendesha Luteni Jenerali Mwachitete

"Hawatumii tena miji. Angalia njia hii nyembamba hapa."
(anaonyesha kwenye ramani)
"Vijiji vidogo vimekuwa kimya. Hakuna harakati. Tulikosea kwa kuelekeza macho mijini pekee. Wanakula kimya... kwa ufanisi." aliongea kamanda mweusi tii

"Kamanda Rama na imani utalishughulikia hili upesi pasipo kuleta taharuki kupitia vijana wako" aliongea Jenerali John

"Vijana wako likizo mkuu" aliongea kamanda Rama kiongozi wa Hidden Supremacy

"Nataka ndani ya masaa arobaini na nane wawe wamekusanyika wote hatuna muda wa kupoteza hawa mashetani kidogo tu waipoteze familia yangu hivyo nahitaji wakusanyikekuanza mkakati wa kuwazima mapema" aliongea Jenerali John

"Vipi kuhusu huyu" aliongea kamanda Rama akiangalia kwenye skrini na picha ya ramani ilibadilika na ilionekana picha ya mwanaume

"Huyo kijana mlimchukulia poa sana nimesikia kutoka kwa Caren inaonekana ana ujuzi wa kutosha alichokosa ni mafunzo yetu tu" aliongea kama Rama

"Unataka kusema?" alkuliza Jenerali John

"Ndio nataka kumuingiza kwenye kikosi kipaji kama kile hakitakiwi kuachwa" alijibu kamanda

"Sidhani kama atakubali" aliongea Jenerali huku akitabasamu

"Hilo niachie mimi mkuu" aliongea kamanda Rama huku akiiangalia picha iliyoko kwenye skrini

°°°°°°°°°

Jimmy hakuwa na pa kwenda popote siku hiyo na alibaki akiangalia runinga sebuleni mpaka aliona kero kuiangalia. Na mara akapata wazo alichomoa simu yake na kwenda kupakua nyimbo za msanii chipukizi anaeishi nae nyumba moja na kuanza kuzisikiliza na alionekana kuzikubali

Baada ya kuchoka kuka ndani alitoka nje ya nyumba na kwenda kukaa bustanini karibu na mti uliompa kivuli cha kujikinga na jua kali a saa sita

Wakati akiwa amekaa hana hili wala lile ghafa alisikia honi ya gari ikipiga na geti likafunguliwa Ikaingia Rolls royce cullinan blue metalic nyumba ilifuatwa na land rover defender nyeusi

Gari mbili zilikwenda kupaki sehemu ya kuegesha na dereva wa Rolls royce alishuka na kwenda kufungua mlango wa abiria na alishuka mwanaume mtanashati, bishoo mwenye marasta ya kuunga unga (rasta feki)

Kwenye ile land rover defender walishuka mabaunsa watatu wote wakivaa sare na kuongozana na boss wao lakini walipewa ishara wasimfate na walitii kisha yule marasta peke yake aliingia ndani, upande wa Jimmy alikuwa akiangalia mwanzo mwisho mpaka marasta anapotelea ndani na hakujisumbua kujua ni nani na amekuja kufanya nini. Zaidi alikuwa akihesabu maua yaliyoko bustanini kupoteza muda

Alipoona anaboreka alienda kukaa na mlinzi wa geti kupoteza muda

"Habari za mchana mzee" aliongea Jimmy baada ya kuona mlinzi ni mzee huku akimpa ishara ya kugonga tano

"Nzuri tu kijana niambie" alijibu yule mlinzi akigonga tano pia

"Vipi kazi inaendaje mzee?"

"Mambo ni yale yale kufungua geti kufunga geti hakuna jipya"

"Walinzi kama nyinyi mnapitia mengi sana mpo getini kila siku liwe jua au mvua"

"Ndio maisha yalivyo japo kazi ya kipweke ila ndiyo inatupatia mishahara ya kulisha familia, watu tunatafuta ridhiki kwa njia ngumu sana halafu inaonekana wewe ni mgeni hapa sijawahi kukuona"

"Ndio mi ni mgeni na naishi hapa"

"Oh sawa unataka kutoka?" mlinzi aliiliza

"Hapana nimeona tu nije hapa kuvunga vipi huyo marasta aliyekuja hapo unamjua?" Jimmy aliuliza

"Ina maana humjui mbona ni maarufu sana?" mlinzi aliuliza



TO BE CONTINUED.............
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom