BY Samuel jk_Euphoria
SOLO KING: DARK MAJESTY
CHAPTER 35: One versus thousands
Jimmy alianza kutembea kuzunguka kijiji hiko maeneo mbalimbali pengine kutakuwa na raia waliojificha wakisubiri msaada.
Baada ya kuzunguka huku na huko katika kijiji hicho aliweza kufika sehemu yenye uwanja mkubwa wa nyasi zenye urefu wa inchi kumi na upande wa mbele ambapo uwanja huo unaishia umbali wa kama mita mia moja kulikuwa na miti mingi mirefu na bila shaka ukitokomea kwenye miti hiyo ni sawa na kuingia msituni
Alisimama kwenye uwanja huo akiangalia kulia na kushoto akijaribu kutafuta chochote kile cha kutilia shaka lakini hakukuwa na jipya zaidi ya hewa na harufu kali isiyoeleweka ni harufu ya nini, ilikuwa ni harufu mbaya zaidi ya uvundo ni kwavile tu mwamba alikuwa anaivumilia
Jimmy alikuwa na masikio yenye kusikia mbali kuliko kawaida na vilevile alikuwa na mafunzo ya hisia.
Aliweza kusikia hatua za miguu na alipoweka umakini zaidi aligundua ni hatua za mtu anaekimbia na kadri alivyozidi kuweka umakini aligundua sio mtu mmoja bali ni hatua za mamia ya watu
Kwakuwa sauti ilikuwa ikisikika kwa mbali hakuweza kugundua inatokea upi hivyo alichuchuma na kugusanisha kiganja chake na ardhi yenye nyasi kisha kufumba macho yake na kuruhusu hisia zake zitawale kujua uelekeo wa sauti hizo na kadri sekunde zinavyoenda ndivyo sauti za hatua zilizidi kuongezeka
"Msaada, jamani msaada!" ilisikika sauti ya mwanamke ikiomba msaada na ndipo Jimmy alipofumbua macho yake na kutazama mbele yake ambapo kulikuwa na msitu mnene lakini kwa bahati mbaya hakuweza kuona chochote kutokana na giza liliopo ndani ya msitu huo
Taratibu mawingu nayo yalianza kutanda angani na kuziba mwanga wa jua na kuonekana kama vile mvua ikitaka kunyesha, kifupi hali ya hewa ilibadilika ghafla
"Eyes of the darkness!" aliongea kwa sauti hafifu na palepale macho yake yalibadilika, rangi ya mboni za macho yake ilibadilika kutoka nyeusi kwenda bluu kisha kusimama
Mbinu hiyo ya jicho la gizani licha ya kwamba inasaidia kuona vizuri kwenye giza lakini vilevile iliwezesha muhusika kuweza kuona umbali mrefu kwa urahisi sana
Alielekeza macho yake mbele ya msitu uliokuwa mbele yake nakwa umbali wa mita chini ya mia na sabini na aliposimama, yaani ukijumlisha mita mia moja za urefu wa uwanja na mita chini ya sabini ya urefu kuanzia kwenye miti kuingia msituni aliweza kumuona mwanamke akikimbia nduki kama kichaa, ilikuwa akianguka anainuka tena na kuendelea kukimbia na hakujali majeraha atakayoyapata kifupi alijali uhai wake zaidi kuliko majeraha ambayo anaweza kupona iwapo atanusurika.
Pia nyuma ya mwanamke huyo umbali wa kama mita mia kulikuwa na kundi kubwa la binadamu wakikimbia kama vichaa waliorukwa na akili. Kibaya zaidi walikuwa ni wachafu kupita maelezo, walichafukwa na damu, wengine walikuwa uchi na hawakuonekana kujali, ni kama vile hawakuwa na akili. Ndugu msomaji iwapo ungepata fursa ya kuwashuhudia mamia ya viumbe hao wenye miili ya kibinadamu ungedhani ni wendawazimu waliotoroka mirenmbe dakika chache zilizopita.
Hivyo Jimmy aliweza kuona kwa urahisi umbali wa zaidi ya mita mia mbili bila shida yoyote
Jimmy hakutaka kuzama msituni bali alisimama palepaleakisikilizia makelele ya hatua mpaka pale yule mwanamke aliyekuwa akiomba msaada kutokelezea kwenye miti iliyokuwa mbele ya macho yake na alionekana amechoka vibaya sana na hata mwendo ulipungua lakini bado tu aliendelea kujivuta kibishi
Alikuwa ni msichana mzungu ambaye kwa kumuangalia tu ungejua ana umri wa miaka kati ya 18 hadi 20, alikuwa amevaa gauni zito lililochakaa na kuchafuka, pia alikuwa akiloa jasho kana kwamba ameibukia baharini, Jimmy alijiuliza huyo mzungu anafanya nini kijijini hapo? Lakini hakupata jibu
"Msaada!... Kaka nisaidie.." aliongea kwa sauti hafifu sana iliyokauka huku akipumua kwa tabu na hapohapo alipoteza fahamu na kutaka kuanguka lakini unadhani Jimmy angeruhusu litokee?
"Exsomnia Gravitus!" Jimmy alinena akimlenga msichana yule na kabla hata kichwa hakijagusa ardhi yenye nyasi aliganda hewani dizaini kama anaelea kwenye maji kisha alimfata na kumbeba msichana huyo na kwenda kumuweka mahali salama alipoona yeye kisha alirudi kwenye uwanja ule akijinyoosha viungo vyake, akiruka na kufanya squarts kadhaa
Dakika si nyingi jeshi la mazombi hatimae liliweza kutoka msituni na kuingia uwanjani ambao uwanja huo uligeuka kuwa uwanja wa vita. Jimmy ni kama vile alikuwa anajua watafika muda gani kwa kupiga mahesabu kulingana na mbio zao alizozipima kwa hisia.
Ni nusu tu ndio waliweza kukanyaga uwanjani na wengine wakiwa bado msituni na wote walikuwa wamesimama wakimuangalia Jimmy. Hiyo ni kutokana na msisimko wa ajabu waliokuwa wakiuhisi. Waliachana umbali wa mita hamsini
"Mnazubaa nini si mlikuwa mkifukuzia mwili mkitaka kuufanya kitoweo? Haya sasa ndio mimi nimegeuka kuwa mwanaume" aliongea Jimmy licha ya kujua kwamba hawatamuelewa
Mmoja wa mazombi walio mstari wa mbele ni kama vile ameelewa alichomaanisha Jimmy kwani alinguruma kama simba na huyooo! na wenzake wakamfuata nyjma. Ni kama vile askari wakisubiri Jenerali achukue hatua ndio wao wafuate
Zilikuwa ni mbio za mamia ya mazombi kuwahia kitowea ambapo kitoweo hiko nacho kilikuwa kikiwasogelea
Wa kwanza kukaribiana Jimmy alitandikwa ngumi moja takatifu yenye ujazo wa kutosha kichwani ambayo ilimpeleka moja kwa kuzimu kwani kichwa kilipasuka poof! Kama puto lichomwavyo na sindano
°°°°°°°°°°
NATIONAL SECURITY COUNCIL BRIEFING ROOM
Ndani ya chumba maalum cha usalama wa taifa kwenye meza kubwa ya mbao alionekana Jenerali John Merizesta akiwa katika gwanda zake safi amesimama, mbele ya macho yake walionekana viongozi wakubwa wa serikali wanne wameketi macho yao yakitazamana na ya Jenerali huyo
"Jenerali tumekuwa tukipokea taarifa—tata. Vifo vingi. Miili haina damu. Raia wananong’ona kuhusu… viumbe vya ajabu" aliongea kiongozi wa kwanza
"Je uvumi huu kuhusu wanywa damu ni kweli?" aliuliza kiongozi wa pili
"Mpaka mnapata taarifa kilichotokea Tanga na kinachotokea Tanga si uvumi tena huo ni ukweli? Kwa miaka mingi mmekuwa mkipuuza kuhusu hili ila nadhani madhara yake yamewafanya muamini sasa" aliongea Jenerali huyo
"Imewezekanaje kutokea chini ya uangalizi wetu? Na kwa kasi hii?" aliongea kiongozi wa tatu
"Tatizo linaanzia kwenu, zile kauli zenu za kukanusha licha ya dalili kuonekana. Jeshi lilitoa ishara na ushahidimkapuuza na kutokuamini" alimjibu
"Jenerali kwahiyo unatushumu sisi kupuza tishio la kitaifa?" aliongea wa nne
"Sio shutuma ni ukweli mlioukataa kwa muda mrefu, ni matumaini yangu mheshimiwa raisi ameliona hili na kulifanyia kazi" aliongea Jenerali huyo
"Kwahiyo tunalitatuaje hili?" aliuliza kiongozi wa kwanza
"Ukweli hakuna haja ya nyinyi kusumbua kichwa kuhusu hili tatizo" Jenerali aliwatuliza
"Elezea vizuri"
"Nimeshapeleka kikosi maalumu kazini, wamefundishwa kudili na hali kama hizi kwa utaalamu wa hali ya juu hivyo msiwaze sana. Sasa wako kimya ishara ya kuwa wako kazini"
"Bila kibali?"
"Mimi ni Mkuu wa majeshi, kibali kutoka kwa nani ilihali jeshi naliongoza mimi? Au mnataka kusema kwa muheshimiwa raisi ilihali ndiye mstafi wa kwanza kulipuuza?" aliongea Jenerali John na kuwafanya viongozi wale kuangaliana wenyewe kwa wenyewe
"Ni kikosi gani? Jeshi? Upelelezi?" aliuliza kiongozi wa kwanza
"They operate under a silent protocol independent, autonomous, and invisible by design. We call them Unit 9-H. But internally… they’re known as Hidden Supremacy." aliongea Jenerali akimaanisha "Wanafanya kazi chini ya itifaki ya kimya inayojitegemea, na isiyoonekana kwa muundo. Tunawaita Unit 9-H. ndani ya mfumo ... Lakini wanatambulika kama Hidden Supremacy."
"Kwahiyo hawa wanywa damu ni viumbe gani hasa?" aliuliza kiongozi wa nne
"wachukulie kama vichaa flani hivi wanaopandwa na mashetani kiasi cha kupoteza ubinadamu wao au kwa lugha nyepesi tuwaite mazombi" aliongea Jenerali huku akitabasamu tabasamu la ajabu kana kwamba anawatisha
°°°°°°°°°°
Ukisikia kukuru kakara basi ndio huku sasa kwani mamia ya miili ya viumbe hao isiyo na uhai ilizagaa kila kona ya uwanja na nyasi za uwanja huo kuchafukwa na damu, na waliobaki walikuwa si chini ya mia mbili. ukijumlisha na waliokufa kwa hesabu ya haraka haraka unapata idadi ya mazombi mia tatu na ushee na hapo ni mia tu ndio aliopoteza uhai kwa kutobolewa mioyo na kupasuliwa vichwa
Jimmy alionekana kuchafuka mnoo zile nguo alizovaa sare na mpenzi wake zilikuwa hazitamaniki tena
Viumbe wale licha ya kubakia mia mbili lakini walionekana kutotosha hivyo walianza kunguruma tena ishara ya kuwaita wenzao walioko msituni
"Pumbavu!" Jimmy alilaani baada ya kugundua wanawaita wenzao zaidi alijiambia hayo ndo madhara ya kuja kichwa kichwa pasipokuwa na mpango madgubuti na aliwaza wenzake aliokuja nao huko waliko wanafanya nini
Hazikupita dakika nyingi tu Jimmy allizingirwa na mamia ya wanywa damu na kukamilisha idadi ya zaidi ya wanywa damu elfu moja, vutavpicha mtucaliesimama katikati ya uwanja wa mpira halafu viti vya mashabiki vilivyomzunguka ndio walikuwa hao mazombi, kifupi kijiji kizima kilifunikwa na maelfu wanywa damu kana kwamba kuna mkutano wa kukisengenya chama cha siasa
"Ni muda sasa!" aliongea na kuangalia juu angani kwa sekunde kadhaa na kushusha kichwa chake chini akitoa na tabasamu la kikatilivkana kwamba amemnasa adui mtegoni
"Awaken!" alinena na ghafla upepo mkali ulianza kuvuma huku ukungu wa buluu usioeleweka umetokea wapi ulimfunika mwili mzima kuanzia kichwani mpaka miguuni na kutengeneza jmbo kama lake ni kama vile alikuwa na miili miwili mmoja wa nyama mwingine wa ukunhu
Macho yake ya bluh nayo yaliongezeka rangi na kukolea kiasi kwamba ungedhani ni tochi mbili zimulikazo. Ni dhahiri kwamba alikuwa katika uwezo wake wote katika levo aliyofikia
"Infinite gravity! Over a thousands let weight become wrath" alinena akimaanisha "Mvutano usio na kikomo! Juu ya maelfu na uzito uwe ghadhabu" na ghafla mkandamizo wa hewa wa hali ya juu ulitokea katika kijiji hicho kiasi kwamba nyumba kadhaa za makuti na tofali zilianza kubomoka. Pia maelfu wote ya wanywa damu walikandamizwa kisawasawa mpaka ardhini wakiugulia maumivu, ilionekana hata sauti walishindwa kutoa na kuonekana kama mabubu wanaotapatapa wakijaibu kunyanyuka, wengine kujiburuza lakini ilishindikana
"Oh shit!" Jimmy alimaks baada ya kugundua kitu na kufumba na kufumbua alipotea pale alipo na kutokelezea sehemu ambayo alimficha msichana yule wa kizungu ns kumkua ameshazinduka na alikuwa akiteseka na mkandamizo wa ghafla uliotokea na ni bahati tu nyumba hiyo aliyofichwa haikubomoka
"Ngao takatifu ya hewa na ikufunike!" Jimmy alinena kama vile anamuombea msichana huyo huku akimnuooshea koganja cha mkono wake wakulia na ghafla ngao ya hewa ilijitengeneza kimaajabu na kumfunika msichana yule na kisha kutoka ndani humo
Alifika nje na kuwashuhudia maviumbe hayo yanavyoteseka na kujiambia ngoja awawaishe kuzimu angalau kutawapunguzia kuteseka sana. Ni huruma ilioje!
"Shwii! Shaa! Fwuuuu! Shaa!" ilikuwa ni milio ya hewa kusuguana kutokana na spidi aliokuwa akitumia Jimmy na vichwa vya maelfu ya hao wanywa damu vilitenganishwa na miili yao na ndani ya nusu saa aliweza kuwashughulikia wote na kubaki peke yake na ile anamaliza tu ghafla alianza kuhisi maumivu ya viungo vya ndani na akili kutaka kumtawala
"pfft … pfft … pfft” Jimmy alitema damu mara tatu mfululizobkiasi cha kudondoka chini na kupiga magoti na ule ukungu uliomfunika ulipotea na macho yake yalirudi kawaida pamoja na mkandamizo wa hewa kuacha pia na hata ile ngao ya hewa iliyotumika kumkinga msichana yule wa kizungu ilipotea. Yaani vilipotea vyote kwa pamoja na sababu ya kupotea ni kukosa mawasiliano na chanzo kikuu ambacho ni nguvu za Jimmy zilizojizima
Jimmy alionekana kulegea sana, ilionekana nguvu alizotumia ni kubwa sana kiasi cha yeye kutohimili kwa muda mrefu na huyo mdogo mdogo alipoteza fahamu na kuanguka chini
°°°°°°°°°°
Anakuja kushtuka muda ukiwa umeenda sana, giza tayari lilikuwa limeshaingia na alikuwa amelala kwenda mkeka kifua wazi pamoja na boksa ndani ya nyumba mojawapo ya kijiji hiko iliyonusurika kubomoka. Pia alikuwa amesafishwa mwili wake
Pembeni yake mita tano na alipolala kulikuwa na moto ukiwa unawaka na bila shaka ulikuwa ukizuia baridi pamoja na kutoa mwanga ndani ya nyumba hiyo ndogo
Aliinuka taratibu na kukaa kitako na kujikagua na alishangaa kukuta yale makovu aliyokuwa nayo mwilini yamepotea na kuonekana imara kabisa isionekane kovu hata moja na kitendo hiko kilimuacha na maswali mengi yasiyo na majibu na aliona bora apotezee kwa muda kuliko kuumiza kichwa muda huo
Alipogeuka upande wake wa kushoto aliweza kuona nguo nyingine zimekunjwa pembeni yake na hakujiuliza mara mbili mbili alizivaa na zilionekana kumtosha
"Hawa wajeda wamepotelea wapi?" aliwaza Jimmy akimaanisha unit 9 H aliokuja nao
Wakati anazunguka zunguka ndani ya kijumba hiko yule msichana mzungu aliingia ndani humo akiwa amebeba ungo uliosheheni viazi na mihogo mibichi na ilionekana imetoka kuchimbwa muda si mrefu
"Umeamka!" aliongra msichana yule waa kizungu huku akitabasamu
Mara ghafla Jimmy alihisi msisimko wa nguvu unakaribia eneo hilo na haraka alimpa ishara msichana huyo anyamanze kisha kutega masikioyake kwa umakini akisikilizia.
Je wenzake Jimmy wako wapi?
Na ni nani anayesogelea mahali walipo Jimmy na msichana huyyo?
TO BE CONTINUED.....
SOLO KING: DARK MAJESTY
CHAPTER 36: Binadamu watatu
"Kuna nini kw.." kabla hata hajamaliza sentensi yake Jimmy alimsogelea haraka na kumuwekea mkono mdomoni huku kwa haraka akimvuta na kujificha nyuma ya mlango
"Sshhh" alinong'ona huku akimkazia macho msichana yule wa kizungu
Msichana yule pia alikuwa akimuangalia Jimmy usoni na alimtii huku akitulia tuli, ukweli mwanamke huyo alibarikiwa kuwa na sura nzuri sana na mashavu mamono pamoja na macho makubwa yenye kuvutia, kifupi alikuwa na sura kama ya kitoto fulani hivi. Umbile lake nalo lilikuwa si haba
Dakika moja si nyingi aliingia mwanaume ndani humo ambaye alionekana kujeruhiwa vibaya sana na alikuwa amejikaza na hakuwa mwingine bali ni Ben
Haikuwa na maana kwa Jimmy kujificha ilihali alikuwa akisambaza msisimko ambao unaweza kuhisiwa na mtu kama Ben hivyo alitoka mafichoni
"wenzako wako wapi?" Jimmy alimuuliza
"Hali si shwari wako hatarini" alijibu Ben huku akigugumia maumivu
"Kwahiyo umewaacha wateseke"
"Hakukuwa na namna zaidi ya mmoja wetu kutoka kuomba msaada, vifaa vya mawasiliano vimeharibiwa"
"kwahiyo unataka kuniambia wale vichaa wanauelewa na vifaa vya mawasiliano?"
"ukweli hatukutegemea kitu kama hicho kutokea" aliongea Ben kisha kumuangalia mwanamke aliyekuwa nyuma ya Jimmy
"Huyo ni nani?" aliuliza na Jimmy kugeuka na kumuangalia yule msichana ambaye muda huo alikuwa akiwatazama tu
"Naitwa Mia" alijitambulisha kwa ufupi kwa lugha ya kiswahili yenye lafudhi kama ya mzawa
Baada ya kujitambulisha aliweka ungo wake chini kisha kuwasogelea wanaume hao
"Vua vazi lako la juu" alimwambia Ben, Ben kusikia vile alimwangalia Jimmy kutaka kujua msichana huyo anataka kufanya nini mpaka kumwambia avue shati lakini Jimmy alikuwa akimwangalia tu asimwambie lolote
"Usiwaze sana unaonekana kuwa na majeraha ninachotaka ni kusaidia kuponya majeraha yako" aliongea Mia na kumfanya sasa, Jimmy aelewe, inaonekana aliyehusika na makovu yake mwilini alikuwa ni huyo msichana aitwaye Mia
"Unataka kusema unaweza kuniponya majeraha? Wewe ni nani?" Ben aliuliza
"Acha maswali mengi bro fanya kama unavyoambiwa" aliongea, Jimmy na Ben bila ubishi alivua vazi lake la juu na baada ya kuvua Mia alimpa ishara ya kukaa chini na alikaa
Mia alimsogelea Ben na kupiga magoti karibu yake na kugusa majeraha kwa viganja vya mikono yake miwili kisha kufumba macho na midomo yake kucheza kama vile anasali
Ghafla mwanga hafifu wa rangi ya kijani kibichi ulionekana kutoka kwenye mikono ya msichana huyo iliyogusanisha na majera na kadri sekunde zilivyozidi kusonga majeraha yalianza kupona taratibu bila kuacha hata kovu. Aliendelea hivyo hivyo kwenye majeraha mengine mpaka alipomaliza kumponya majeraha yote
"Ni miujiza ya uponyaji iliyoje" alijiambia Jimmy kichwani mwake baada ya kushudia maajabu hayo
Mia baada ya kumaliza alinyanyuka taratibu lakini ghafla alianza kuhisi kizunguzungu na kupoteza balansi ya kusimama lakini Jimmy alimuwahi asihanguke
"Nipo sawa" aliongea Mia akitaka kutoka mikononi mwa Jimmy lakini alishindwa kutokana na Jimmy kukaza
"Hauko sawa, umefanya kazi kubwa ya kutusaidia kuponya majeraha licha ya kwanza unaonekana na nguvu za upanyi lakini unapotumia nguvu za mwilini hupungua" aliongea Jimmy huku akimkazia macho
"Asante" Jimmy alimshukuru na kumfanya Mia akwepeshe macho yake
"Mimi pia" Ben naye alidakia
"Ni jambo dogo tu nilichotaka ni kulipa fadhila maana bila wewe wangeninyonya na mimi" aliongea, Mia baada ya kufanikiwa kujitoa mikononi mwa Jimmy huku akuibeba ungo wake wenye viazi na mihogo
"Hey bro ni wewe ndiye umedili na hiyo miili iliyozagaa uko nje?" aliongea Ben huku akionekana kutoamini lakini Jimmy alimpa ishara ya kwamba "uamini usiamini hilo ni juu yako"
"Pia Mia wewe ni nani? Inakuwaje unakuea na nguvu za ajabu namna hiyo? Kwanini uko hapa?" aliuliza Ben lakini Mia alionekana kutotaka kujibu
"Tuachane na maswali yako wenzako wako wapi?" Jimmy aliamua kuingilia baada ya kuona jamaa ana maswali mengi
FLASHBACK
Baada ya wanne hao kuzama msituni na kumuacha Jimmy akiwaangalia walianza kufuatili ute ute mwingi uliokuwa umepotelezea msituni huko
Baada ya mbio za dakika kadhaa hatimae waliweza kufika sehemu yenye uwazi na miti michache na mbele ya macbo yao kulikuwa kuna pango dogo la mawe yasiyojulikana nivya aina gani likiwa katika muundo wa pembe tatu kama vile Bermuda triangle
Ilishangaza kuona kuna pango katikati ya msitu huo, lilikuwa kama vile ni lango la kuingia ulimwengu mwingine na kwa wakati huo huo kuonekana kama pango dogo la kujikinga wakati wa baridi na mvua
"Ni maajabu yalioje" aliongea Joshua akivutiwa na mawe yaliyotumika kuunda pango hilo
"Kuna mengi sana ya kuvutia kwenye dunia hii ndugu yangu usishangazwe na hako kapango au sio bro.. " aliongea Ben huku akitabasamu huku neno bro akimlenga Jimmy lakini hakuweza kumuona
"Hey yule braza yuko wapi?" Ben alimuuliza Caren
"Jimmy?"
"Kumbe anaitwa Jimmy, ndio yuko wapi? Mbona sihisi uwepo wake eneo hili"
"Unamtaka? Unaweza kurudi tu kama unashida nae tumemuacha kijijini" aliongea Freya
"We manzi mzungu huu sio uungwana unajua? Unamchukulia poa sana au ni kwasababu ulimsaidia miaka ile mikononi mwa wale wanywa damu?" alimuuliza Ben
"Hata kama namchukulia poa unasemaje? Hakupaswa kushirikishwa kwenye hii misheni kisa tu amebahatika kuwa vijinguvu sawa na sisi... Inaonekana hata mkuu hatuamini vya kutosha." Freya alimjibu
"Hehe nishaelewa sasa, inaonekana kinachokuuma ni kwasababua l ya yeye kuweza kuwa na nguvu na hata kutufikia.. ooh sio kutufikia ni kukufikia ndani ya muda mfupi.. Imekuchukua miaka kumi na mbili mpaka kufika hapo ulipo lakini kwake ooh itapendeza nikisema "mtu uliyemuokoa" ame.. ..."
"Shut up you stupid imbasile!" Freya alimfokea kabla hata Ben hajamaliza sentensi yake
"Tafadhalini huu sio muda wenu wa kugombana, tumalizane kwanza na kile kilichotuleta ndio muendelee na ugomvi wenu na sitoingilia hata mkipigana" Caren aliingilia
Shida huyu mzungu wivu unamsumbua haiwezekani kila mtu ni wakumuonea wivu" aliongea Ben na kumfanya Cafen kukasirika kiasi kwamba alitaka kumshikisha adabu lakini Caren alimuwahi na kumpa ishara atulie
Freya aliishia kumkazia macho makali Ben huku Ben akimpa tabasamu flani hivi ni kama anamwambia "nimefurahi kukuona unakasirika"
Caren aliwapotezea na kisha kuangalia ardhini ambako kulikuwa ute mwingi umesambaa na moja kwa moja ulielekea kwenye lile pango dogo na bila shaka ilionekana ndiko walikotokea viumbe hao
"Tunaingia" aliongea Caren na kuwapa ishara wenzake kuwa tayari na kisha kuwa wa kwanza kuzama ndani akifuatiwa na Joshua kisha Freyya na mwisho Ben
°°°°°°°°°°
`Yule manzi licha ya kutokujali uwepo wako lakini ndiye aliyenitaka nije kukutafuta kuomba msaada na kufanikisha mpaka nikatoka mikononi mwa wale watu" aliongea Ben akimwelezea Jimmy
"Umesema baada ya kuingia ndani ya lile pango mlijikuta mko katika jangwa?" Jimmy alimuuliza
"Ndio, na pia kulikuwa na binadamu watatu wenye asili ya Asia" Ben alimjibu kwa urefu
"Nini kikafuata?" Jimmy alimuuliza
"we unadhani ni kitu gani kama sio kupigana? Inaonekana wao ndio walioko nyuma ya pazia kuhusiana na hawa wanywa damu" aliongea Ben na kumfanya Jimmy ashushe pumzi ndefu
"Kipi kinakufanya uamini kwamba wanahusika na hawa mazombi"
"Ni chungu, japokuwa sijui ni chungu cha nini lakini nilikuwa napata hisia ya ajabu ni kana kwamba kuna maelfu ya nafsi zimefungwa ndani ya chungu hiko"
"pango lenye muundo wa pembe tatu, binadamu wa tatu na chungu" Jimmy alikuwa akiwaza
"Pumbavu! Wale walozi wako mpaka huku!" alipayuka baada ya kukumbuka kitu
"Unawajua?" Ben alimuuliza Jimmy
"Nadhani hao binadamu watatu unaowazungumzia nimewaona pia" aliongea Mia
"Na ndio sababu ya wewe kukimbizwa na kundi la hao mashetani?" Jimmy aliuliza na Mia alitingisha kichwa kukubaliana nae
"Wakati wanavamia Kijiji mimi sikuwepo nilitoka kwenda msituni, huwa ni ratiba yangu kila saa sita natoka kijijini na kwenda mto saunyi na wakati wa kurudi nilipita njia nyingine na kukutana nao wamewateka baadhi ya watu kutoka vijiji vingine" Mia alieleza kwa ufupi sababu ya yeye kukimbia na kukimbizwa na wale mashetani
Ukweli sababu ya yeye kukimbia ni baada ya kushuhudia wakifanya utekaji na kukimbia baada ya kushtukiwa, hakujua kama atakimbizwa na yale mazombi na kwa bahati nzuri amenusurika baada ya kukutana na Jimmy
"Twende!" Jimmy alimwambia Ben na kabla ya kuondoka alikumbuka kitu
"Simu, simu yangu iko wapi?" Jimmy alimuuliza Mia
Uzuri Mia aliihifadhi mahali wakati anavivua nguo za Jimmy kumponya makovu hivyo alikwenda kuichukua na kimpatia
Simu yake ilikuwa imepasuka kioo kana kwamba ilipigwa ngumi na kusababisha nyufa nyingi. Licha ya hivyo bado ilikuwa ikifanya kazi na baada ya kuiwasha aliweza kuona saa ikisoma saa moja na dakika kumi pamoja na missed calls kumi na nne na jumba nyingi
Kati ya missed calls kumi na nne, nane zilikuwa kutoka kwa Biancalina, mbili kutoka kwa mama yake mzazi, mbili kutoka kwa Cid na mbili kutoka kwa dada yake Monica
Jimmy aliishia kumeza mate mengi tu na kujiambia inamaana alikuwa akitafutwa hivyo?
Kati ya missed calls ni namba ya Cid pekee ndiyo aliona inafaa kupiga kwa wakati huo
"Vipi shemeji" aliongea Jimmy baada ya simu kupokelewa
"Bro tuachane na ushemeji, hivi mbona hunitakii amani?" aliongea Ciid upande wa pili
"Kuna nini?
"Kwanza uko wapi?"
"Niko Tanga"
"Nini! Bro mbona hutulii? Kuangaika kwako kunanikosesha amani ujue. Uliondoka wapi sijui na baada ya miaka mitano unarudi lawama naangushiwa mimi, sasa hivi umerudi haijapita hata wiki ushaanza kuruka, napigiwa simu na Bianca kuulizia ulipo na nimewaambia sijui lakini haniamini ameenda mbali mpaka kunichongea kwa mke wangu kwamba nakataa kusema ulipo na hata mke wangu haniamini eti kisa nilihusika na wewe kuondoka kipindi kile, nina stress za kulea mtoto na bado unaletea stress zako huu sio uungwana kabisa" Cid alianza kutoa lawama
"vumilia bro fanya unikingie kifua we waambie tu soon narudi"
"Unatakiwa ufike kabla ya saa tatu"
"Saa tatu kuna nini?"
"Inaonekana Bianca hajakwambia"
"Sasa si unieleze"
"Iko hivi saa tatu Biancalina anatakiwa kuhudhuria mualiko wa Marriage anniversary ya thelathini ya msanii mkongwe nchini na siku hiyo pia kuwa siku ya kuzaliwa ya mtoto wao mpendwa"
"kumbe ndio sababu alikuwa anakomalia kwenda, shopping asubuhi asubuhi" Jimmy alijiwazia
"Asante kwa taarifa bro nitawasili kama muda unavyosema by the way unahudhuria?"
"Ningependa kuhudhuria maana nimesikia mzee ametumia ushawishi wake kwenye sanaa, pesa nyingi na koneksheni kuweza kuwaleta wasanii maarufu barani Asia na duniani kote kwa ujumla wajulikanao kwa jina la Four souls nchini ili kuja kutumbuiza kwenye siku hiyo, nimepata mualiko pia"
"Kwanini usiende sasa"
"Kaka najuta sana kuoa mapema yaani sina uhuru kabisa, unadhani dada yako angeniruhusu nikazurure usiku nimuache na mtoto peke yake?"
"Hehe! Pambania kujenga familia bro ujana ushakuishia sahivi we ni mzee, pambana kulea mtoto" aliongea Jimmy huku akicheka na kusababisha kukatiwa simu
Walitumia dakika saba tu kuweza kuzungumza kwenye simu na kumaliza
"Mia sisi tunatoka" aliongea Jimmy huku akivaa viatu vyake
"Subirini kwanza.." aliongea na kisha kuchukua viazi vitamu vibichi.na kuwarushia na walidaka
"Mtie chochote tumboni angalau mpate nguvu kidogo, isitoshe mmepoteza ngucu kudili na hawa viumbe" aliongea Mia kuwafanya wanaume hao kutabasamu tabasamu la shukrani
°°°°°°°°°°
Dakika kadhaa mbele Jimmy na Ben walikuwa wamesimama eneo la wazi msituni wakitazama pango la pembe tafu lililokuwa mbele yao
"Ndio hapa" aliongea Ben na kumfanya Jimmy alichunguze kwa dakika mbili bila kusema chochote
"Hili sio pango licha ya kuonekana kama pango" aliongea Jimmy
"Unataka kusema..."
"Ndio inaonekana hili ni lango la kuingia ulimwengu mwingine , ushawahi kusikia Bermuda Triangle? "
"Ndio inapatikana kusini mwa bahari ya antlantic na inasemekana meli zipitazo sehemu hiyo hupotea pasipo kuacha ushahidi wa aina yoyote pia inasemekana japo hakuna ushahidi wa moja kwa moja kwamba ni lango la kuingilia ulimwengu mwingine ulioko chini ya maji, lakini mimi siamini"
"Bado mpaka sasa huamini tu licha ya kushuhudia kwa macho yako"
"Unamaanisha nini"
"We si umesema baada ya kuingia humo mlitokezea jangwani?"
"Unataka kusema kwamba ni ulimwengu mwingine tumeingia?"
"Bro inaonekana akili yako inafanya kazi polepole... Mpo msituni mnaingia kwenye pango mnajikuta jangwani bado hujaelewa tu" aliongea Jimmy huku akitingisha kichwa kwa masikitiko
"Japokuwa sijawahi kushuhudia ila nimesoma kuhusu mambo ya aina hii. Kuna hadithi za kale zinazosema kuna maeneo duniani ambayo ni ‘miingilio’ ya dunia nyingine ambapo sheria za asili hazifanyi kazi kama tunavyozijua" aliendelea
Jimmy alivuta pumzi ndefu na kuzishusha kisha kupiga hatua na kuingia ndani ya pango hilo akifuatiwa na Ben
Baada ya kuingia tu walijikuta wametokezea upande mwingine, kukiwa jangwa tupu na majira kuonekana kama asubuhi ya saa kumi na mbili bila ya kujua chanzo cha mwanga hafifu ni nini maana angani hakukuwa hata na jua wala mwezi wala nyota. Pia baridi lilikuwa si la kitoto ni bahati tu walikuwa na mafunzo na nguvu zisizo za kawaida kuweza kuhimili
Jimmy alikuwa akishangaa eneo hilo na bila shaka ilikuwa nj mara yake ya kwanza kuingia kwenye ulimwengu usio na kitu chochote zaidi ya jangwa tu na mbele yake umbali wa kama mita thelathini na aliposimama aliweza kuwaona wenzake wakiwa katika kuelekea kukata tamaa kwenye pambano dhidi ya binadamu watatu, kwani walionekana kuchoka sana na kujeruhiwa na hata kusimama kwao kulikuwa ni kwa tabu sana
TO BE CONTINUED.....
SOLO KING: DARK MAJESTY
CHAPTER 37: It's Fury!
Pia ukiachana na hao kulikuwa na miili ikiwa imezagaa chini mchangani, ilikuwa ni miili ya wanywa damu si chini ya mia na ilionekana walitumia nguvu sana kuwashughulikia
Wale binadamu watatu na wakina, Caren waliweza kuhisi ongezeko la watu wawili na walipoangalia kupitia lango la kuingilia waliweza kumuona Jimmy na Ben
Kati ya wale watatu mmoja alibeba chungu cheusi cha wastani chenye michoro ya ajabu rangi ya dhahabu, wa pili alibeba kitu kama box la wastani ambalo limefunikwa na kitambaa kulisitiri, na wa tatu alikuwa mikono tupu
"J? Unafanya nini hapa? Na umefikaje huku?" aliongea mmoja wa wale binadamu watatu aliyekuwa mikono tupu akimtazama Jimmy
"Hilo swali nilipaswa kuwauliza nyinyi, mnafanya nini huku?" aliongea Jimmy
"Sisi kufanya nini huku kunakuhusu nini?" aliongea mwingine kwa kiburi aliyebeba chungu
"Nilidhani kuwasamehe kutawafanya muungame dhambi zenu ila inaoneka nilikosea kuwaonea huruma, na huruma yangu imewafanya muwe na kiburi na tamaa zaidi" aliongea Jimmy hukucakiwakazia macho
"Nasikia unaheshima sana freewill bwana J" aliongea aliyebeba boksi
"Mpo kwenye nchi yangu, mnaua mamia ya wanakijiji halafu mnaongelea kuhusu uhuru wa kuchagua? Mnaona mimi fala mwenzenu si ndio" aliongea Jimmy kikauzu
"Unakosea kusema nchi yako, hatupo tena kwenye nchi yako tupo ulimwengu mwingine" aliongea aliyebeba chungu
"Vyovyote vile nimesema mpo kwenye nchi yangu, lango mlilotumia kufika hapa ni la nchi yangu hivyo ni mali yangu pia, tukiachana na hilo mmesababisha machafuko na kuuwa raia wa nchi yangu"
"Tangu lini umekuwa raisi wa nchi mpaka kuimiliki?" aliongea aliyekuwa mikono tupu
"Inaonekana wewe ni empty set kabisa, hivi hujui kwamba nchi ni mali ya wananchi? Hata huyo raisi anateuliwa na wananchi wewe kunguni usiye na akili" aliongea Ben
"Bro kuongea nao ni sawa na kupoteza muda" Ben aliendelea kuongea huku akiwakazia macho watu wale
Ghafla Caren, Freya na, Joshua waliishiwa nguvu na kukosa udhibiti na kuanguka chini mchangani kwa magoti huku Caren ndiye aliyeonekana kutia huruma zaidi
" Hawa rafiki zako niseme tu ni wako imara sana lakini inasikitisha kwamba si ligi moja nasi"aliongea aliyekuwa mikono tupu
" Hio ni kwasababu nyinyi ni walozi hivyo ni sawa kusema si ligi yenu" aliongea, Jimmy
"Bro inaonekana unaonekana unawajua hawa watu, ni wakina nani?" aliuliza Joshua kwa sauti hafifu
"Soul shifters! Kuhusu majina yao hata sikumbuki ila huyo aliyebeba chungu tunaweza kumuita punguani, halafu huyo aliyebeba boksi ni pimbi na huyo mikono mitupu ni kunguni tu" Jimmy alijibu
"pumbavu! Unathubutu vipi kututukana?" aliyebeba boksi alifoka lakini Jimmy alimpotezea
"Nini? wabadili nafsi?" Ben aliuliza kwa mshangao
"Ndio hawa washenzi ni walozi wanaobadili nafsi za wengine. Mwanzoni nilijua hawa viumbe ni wachawi waliopoteza ubinadamu wao kutokana na kutumia sana mbinu ya damu inayobadilika lakini inaonekana nilikosea" aliongea, Jimmy
"Inamaana hao wanywa damu ni binadamu ambao nafsi zao zimebadilishwa?" alouliza Ben
"Ndio mi nilidhani hawa washenzi wanahusika kwenye kubadili nafsi za binadamu kwenda kwa binadamu wengine ila safari hii wameenda mbali sana mpaka kuingiza nafsi za mashetani kwenye miili ya binadamu huku nafsi za hao binadamu wakiziteka na kuzifungia ndani ya chungu" Jimmy alieleza
"Shabash! Hawastahili kuishi hawa washenzi" alimaka Freya kwa tabu kutokana na maumivu
"Hujakosea hawa walozi wanastahili kwenda kuzimu" alidakia Joshua
"Nyinyi vikaragosi bado mnathubutu kuongea tu, inaonekana kipigo bado hakijawaingia" aliongea aliyebeba chungu lakini walimpotezea na mkwara wake
"Hisia zangu zilikuwa na sahihi kuna nafsi zimefungwa kichawi ndani ya chungu" aliongea Ben
"Licha ya chungu hicho kutumika kuteka nafsi lakini vilevile kina nafsi za mashetani zikiishi ndani ya hiko chungu, ushawahi kusikia Tartarus?"
"Hapana" Alijibu Ben
"Itakuwa ngumu sana kukueleza ila kwa lugha nyepesi Tartarus ni neno la kigiriki lenye maana ya Gereza la nafsi ambako nafsi ovu za mashetani hufungiwa" alieleza kwa ufupi
"Kwahiyo hiko chungu ni gereza la nafsi!" Ben aliongea na Jimmy alitingisha kichwa kukubaliana nae
"Niwe mkweli huwa nakukubali sana upande wa maarifa, inaonekana unajua mengi sana" aliongea ambaye jimmy alimtambulisha kama punguani
"Aya sasa muda wa ngojera umekwisha ni wakati wenu wa kwenda kukutana na ndugu zenu walozi huko kuzimu" aliongea Jimmy kikauzu na ghafla aliziamsha nguvu zake za kichawi
"Awaken!" alitamka na upepo ukaanza kuvuma lakini ulikoma muda huo huo na Jimmy kuanza kutema damu
"pfft... Pfft.." alitema damu na mwili wake kuanza kulegea hata yeye mwenyewe alijishangaa
kitendo hiko kiliwafanya maadui kutabasamu na kumuangalia Jimmy kwa macho ya dharau na furaha ya kwenda kumshinda
"Nilikuwa na hofu ya bure tu, lakini nani angejua hofu yangu ingebadilika na kuwa ujasiri" aliongea mtu yule aliyebeba boksi
"Inaonekana bahati imetuangukia haha! Golden chance never comes twice lazima nihakikishe nawapeleka kuzimu" aliongea aliyekuwa mikono tupu
"Uzito wa tani millioni moja wa hewa!" aliongea yule bwana mwenye mikono mitupu na ghafla hali ya hewa ilibadilika na kuwa nzito kiasi kwamba ikawa tabu kupumua
Upande wa Caren na wenzake walionekana wanaelekea kukata tamaa kwani waliemtegemea kuwaokoa naye anapitia tabu kama wao
" Bro fanya kit..u" aliongea Ben kwa kujalizimisha kana kwamba amekabwa
"Caren! Caren!.. Car..en!" aliita Freya baada ya kumukna mwenzake akipitia mateso kuzidi wao na macho yake yalikuwa yakianza kupoteza uono, na bila shaka muda wowote angepoteza uhai kutokana na tabu ya kupumua
"Jimmy tafadhali fanya kitu tunakwenda kufa, Tunakwenda kumpoteza Caren" hakuwa Freya yule mwenye kiburi tena bali mwenye kuomba kusaidiwa ilionekana alikuwa na ukaribu sana na Caren
"Hahaha.. Hahahaha! Ni drama ilioje" aliongea bwana huyo kunguni
"Awaken... A. awak.en.. awaken! Aaa..." Jimmy alikuwa akijaribu kuziamsha nguvu zake lakini haikusaidia kitu na badala yake alipoteza nguvu na kutema damu mdomoni
Jimmy alimwangalia Ben anayehangaika kupumua kisha kuwaangalia na wengine na kupatwa hisia za ajabu zisizoeleweka
" Hakuna kukata tamaa...msiruhusu mioyo yenu ikubali..kushindwa, nimepigana vita vingi sana na unajua kwanini bado niko hai? ni kwasababu sikati tamaa...nyanyukeni mmpambane haijalishi ni nguvu kiasi gani mlizobaki nazi au mateso gani mnapitia mnatakiwa kupambana bila kukata tamaa" aliongea Jimmy kwa sauti hafifu lakini yenye kusikika vyema akijaribu kuwashawishi kuwa-motivate wasikate tamas huku akijinyanyua na kujikaza
"Sababu ya mimi kuwa hai sio kwasababu ya nguvu nilizonazo bali ni Hasira ya kutokata tamaa hasira kuu.. Its fury!
Ni hasira si chuki, si ghadhabu isiyo na mwelekeo, ni moto unaokataa kuzimika, hata pale kila kitu ndani yako unapohisi kama tayari kimekufa. Ni hasira ya kusimama tena wakati dunia inakukandamiza" aliendelea kuongea huku akisimama wima
"Ni kilio ndani ya kifua chako wakati hakuna anayesikiliza. ni nguvu inayochipuka kutoka kwa maumivu, hasara, kushindwa, yote hayo na kusema, ‘Sikubali kushindwa.’
Ni kukataa kuruhusu wewe mwenyewe kuharibiwa, ni kushikilia wakati miguu yako inatetemeka, wakati moyo wako unavunjika, wakati kila kitu kinacheka dhidi yako
Ni kuchagua kusonga mbele hata pale kila sehemu yako inaomba usimame. Mnadhani nguvu ni kushinda mapambano kirahisi? Kama ndivyo mnavyodhani basi mnakosea
Nguvu ni kupigwa, kuvunjwa, kuaibishwa na bado ukachagua kuinuka
Hasira ya kutokata tamaa ni sauti ndani yenu inayosema "najua maumivu, najua hofu, najua kukata tamaa lakini sitaruhusu kupiga magoti na kujikatia tamaa"
Ninawaka sio kwa sababu naichukia dunia, bali kwa sababu nakataa kuiruhusu dunia kunivunja. Na nyinyi... ndio nyinyi mnaofikiria kukata tamaa mna moto huo huo ndani yenu mnahitaji tu kuuruhusu upumue tena
Huitaji kuwa mkamilifu Unachohitaji ni kuwa na hasira kuu ya kutosha ili usiruhusu kukata tamaa" aliendea kwa sauti ya kawaidi lakini yenye kusambaza nguvu ya ajabu sana na taratibu Caren alijiinua kibishi na kusimama ni kama vile kuna nguvu ghafla imemuingia na uchovu kumpotea vivyo hivyo kwa wenzake
Watatu wale walishangaa kitendo hiko ni kama vile maneno ya Jimmy yamewapa nguvu tena na ghafla kwa pamoja waliweza kusimama wima na imara licha ya uzito wa hewa lakini hawakupata tabu kubwa kwenye kupumua ni kama vile uzito wa hewa ulipungua
"Inawezekanaje hii..? Aliongea aliyebeba boksi
"Sasa ni muda, shift phase one!" aliongea Freya na kutamka neno la kuiamsha damu yake na ghafla mabuja buja yalionekana kwenye ngozi yake kana kwamba damu iliyoko ndani yake ilikuwa ikichemka na kufumba na kufumbua aligeuka kuwa mbeha wa rangi ya chungwa
Shift!" Joshua naye alimtaka na kufumba na kufumbua naye pia alibadilika na kuwa simba dume mwenye manyoya meusi
" Blazing fist! blazing feet! "Joshua naye hakuwa mbali kwenye mabadiliko kwani baada ya kutamka tu hayo maneno moto wa njano uliwaka kwenye ngumi za mikono yake miwili na miguuni pia mpaka viatu kuungua na kubaki miguu peku iwakayo moto
Caren aliokota upanga wake uliokuwa chini ya mchanga na kukaa tayari kwa mpambano unaofuata na Jimmy naye alisimama imara bila kuweka staili yoyote ya kupigana zaidi ya kuwakazia macho, macho yao hayakuwa na utani hata kidogo.
"Kuweni makini" aliongea Jimmy akiwatahadharisha na kuchomoka ama mshale akisindikiza na shambulizi la teke la sarakasi moja matata sana akimlenga shingo bwana aliyeshika boksi
Ilikuwa ni spidi ndogo kutokana nguvu zake kichawi kutofanya kazi wakati huo bila ya kujua chanzo ni nini hivyo ilikuwa Rahisi kwa bwana yule kulikwepa na Jimmy alitegemea hilo kwani sekunde anayokwepa tu alimshtukiza na teke jingine la kifua lililo mrudisha nyuma
Jimmy hakutaka kumpa nafasi ya kupumua na kurusha mashambulizi yake ya kichawi kwani alirusha mashambulizi mengi ya haraka haraka kwa staili mbali mbali na utaalamu wa hali ya juu
Bwana yule alijikuta akiweka umakini wake kwenye kukwepa mashambulizi huku kwa wakati mmoja akijaribu kuhakikisha boksi alilolibeba haliguswi kwa namna yoyote ile.
Upande wa Freya na Caren walimshambulia adui as liyekuwa mikono tupu wakiwa na lengo sawa na Jimmy, kuhakikisha hawamruhusu kupata nafasi ya kushambulia vivyo hivyo kwa Ben na Joshua walikuwa wakipambana na Bwana aliyebeba chungu
Yalikuwa ni mapambano ya ana kwa ana bila kutumia uchawi wowote zaidi ya mbinu za mapigano na baada ya dakika kumi wote walisitisha pambano kuvuta hewa kidogo huku Frwya na Joshua wakirudi katika maumbo yao ya kibinadamu wakifuata kanuni ya uchawi wa damu inayobadilika ya kutotumia maumbo mengine zaidi ya dakika kumi
"Ben ondokeni!" Jimmy aliwaamuru na kuwafanya wote wamuangalie kwa macho ya kiulizo
"Haiwezekani tukuache peke yako ukihangaika kupambana na hawa mashetani, tumekuja wote tunaondoka wote" aliongea, Caren na wote walikubaliana nae
"Tukiendelea hivi mwisho tunachoka na kupoteza nguvu na kuwapa fursa ya kutumaliza, hivyo ondokeni" aliongea akiwa siriaz
"Nimesema ondokeni" alifoka baada ya kuona hawataki kumtii
"Never thought someone like you would want your fellas to choose a coward side" aliongea aliyeshikilia boksi akimaanisha "Sikudhani mtu kama wewe ungewataka wenzako wachague upande wa unyonge"
"Sometimes it's better being a coward you know? .. Better to live and fight another day than die chasing pride." aliongea Jimmy kwa utulivu akimaanisha "Wakati mwingine ni bora kuwa mwoga unajua? … Ni heri kuishi na kupigana siku nyingine kuliko kufa ukifukuza kiburi."
"Hivyo ndivyo unavyoita Tahadhari? Mbinu? Au ni woga tu" alicheka kwa dharau bwana yule
"Pengine huo woga utawafanya waendelee kuishi" aliongea Jimmy na kuwakazia macho senzako
"Ninachojaribu ni kuwaokoa kutoka kwenye kifo mbona hamuelewi? Msiwaze kuhusu mimi nishajua namna ya kudili nao na kutoka salama hivyo naomba msiniangushe kwa hili.."aliongea na kuwafanya wenzake waangaliane wao kwa wao kama vile wanashauriana wamsikilize ama wampuuze na mwisho wa siku walikubali kumsikiliza
Jimmy kwa kasi ya juu ya uwezo wake aliwashambulia mabwana wote watatu akiwapa nafasi ya kuondoka na kuhakikisha wanatoka na waliweza kutoka tu Jimmy alipoteza umakini na kupigwa teke moja takatifu lililomrusha umbali mrefu na kuanguka chini huku akitema damu nyingi mdomoni
Asingekubali kuonekana mnyonge kwani alijinyanyua kibishi na kusimama tena japo kwa tabu na ile anasimama tu alipokea shambulizi jingine lililomrusha na kuanguka chini lakini kiburi cha kusimama kilikuwa juu sana kwani alijivuta tena na kusimama huku akiyumbayumba kutokana na kukosa balansi na nguvu kumpungua
"Wewe ni mpumbavu sana, wenzako walikuwa tayari kupigana kufa kupona pamoja nawe lakini unawafukuza ona sasa unavyotia huruma" aliongea bwana aliyebeba Chungu na kumpiga ngumi nzito ya tumbo hali iliyomfanya Jimmy kujikunja mgongo huku akilegea na kuangukia chini kwa magoti huku damu zikimtoka mdomoni kama udenda
"Haha.. Hahaha.. Koh.. Kkk" Jimmy alianza kucheka kwa sauti hafifu huku akikohoa na kutema damu pasipo kueleweka nini kimemchekesha ni kama vile amekuwa chizi ghafla
Kitendo hiko kilimfanya bwana aliyebeba boksi kupandwa na hasira aliona ni dharau sana kuchekwa na mtu dhaifu ambaye muda wowote anakwenda kufa na palepale alifungua kitambaa na kuonekana boksi la kioo na kufumba macho yeye pamoja na wenzake, Jimmy baada ya kuona kilichopi ndani ya boksi alipiga makelele ya maumivu
"Aaarfhhh... Aaarghhh!" ulikuwa ni ukelele hafifu lakini wenye kuashiria maumivu. Jimmy aliposhuhudia na kupiga makelele hayo ya maumivu alifunika boksi lile
TO BE CONTINUED.....
SOLO KING: DARK MAJESTY
CHAPTER 38: I fight not to win, I fight not to lose
Katika hadithi za kale Baba yaga alisemekana kuwa mchawi wa kutisha, mzee mwanamke mwenye macho ya kutisha ambaye anaishi ndani ya msitu mnene
Nyumba yake aishiyo ilikuwa ni ya ajabu na inasemekana ilikuwa na miguu ya kuku na ina uwezo wa kutembea na kujificha popote msituni
anatajwa kuwa na macho ya laana yenye uwezo wa kupofusha unapomuangalia
Sasa katika boksi lile la kioo kilipatikana kichwa chake na haikueleweka bwana huyo alikipata wapi kichwa cha mchawi afahamikaye kwa jina la Baba yaga lakini jambo la uhakika kichwa hicho kilikuwa kinatoa msisimko wa ajabu ambao haukuelezeka na kitendo cha Jimmy kukutanisha macho yake na macho ya kichwa hicho chenye laana ya upofu ghafla alipiga kelele na kupatwa na upofu hapo hapo na hakutegemea hilo lakini ndio hivyo lishatokea
"Hahaha! unastahili kabisa kuwa kipofu mwanaharamu wewe!" aliongea bwana yule mwenye boksi na hakuishia kuongea tu, alimpiga teke lenye nguvu lililomrusha Jimmy na kubiringita mchangani kama tairi la gari umbali wa mita saba na kutulia tuli uso wake ukiwa umelalia mchanga
Alikuwa akipumua kwa tabu sana, alikuwa amelala chini kama mtu asiyekuwa na tumaini, alijigeuza na kulala chali akiangalia angani huku uso wake ukichafukwa na damu na michanga ya jangwa hilo
Hakuona akiona chochote, mbele yakealiona giza neno na taratibu alifumba macho, hata kama angeacha macho wazi isingekuwa na maana, kwa kipofu kufumba au kufumbua macho giza litabaki palepale
Alikuwa akivuta kumbukumbu mpaka alipokuwa mdogo akiongea na marehemu Baba yake
"kwenye maisha hutakiwi kukata tamaa ata kama unapitia changamoto pambana mpaka mwisho usikate tamaa sawa? " aliyakumbuka hayo maneno kwa ufasaha na kuanza kuwakumbuka ndugu zake, mama yake, rafiki zake na Biancalina pia na alijiambia vipi akifa nani atawalinda?
Alisema hapana hatakiwi kuruhusu hilo litokee
"Inasikitisha unakwenda kufa katika umri mdogo sana kijana" aliongea bwana aliyebeba chungu
"Wema ni akiba sana J kwakuwa ulituacha tukaishi kipindi kile nasi tunaeeza kusamehe uhai wako iwapo utatupa hazina unayobeba" aliongea yule bwana asiyebeba chochote
"Natumai utafanya maamuzi ya busara na kutupatia hiyo hazina" aliongea aliyebeba boksi
"Nilijua tu lazima mtaleta upumbavu wenu, nimekuja mikono tupu hazina naitolea wapi? Hata kama ningekuwa na hiyo hazina nisingekubali itue mikononi mwa mashetani kama nyinyi" aliongea Jimmy akiwa bado amelala ardhini
"Hiyo hazina ina thamani gani kiasi cha kujitoa na kuwa tayari kufa? Ina maana uhai wako hauna thamani?"
"Swali zurii...." alijibu Jimmy huku akijikakamua kuinuka na kusimama japo si wima ila alisimama kwa kulegea sana
"Kwangu mimi uhai una thamani sana kuliko kitu chochote katika dunia hii, si uhai wangu tu bali na raia wema wasio na hatia nyinyi was*ng* kazi yenu ni kuwateka binadamu na kuzifunga nafsi zao kisha kuingiza nafsi za mashetani kwenye miili yao ambapo matokea yake wanakwenda kuua binadamu wengine wasio na hatia, kuwapa ninyi hiyo hazina ni sawa na kuchoma kisu kidonda kibichi na kusababisha madhara makubwa" aliendelea
"Oh ni shujaa ulioje! Lakini kwa bahati mbaya shujaa unakwenda kufa"
"Kufa? Unakosea kusema hivyo, kwenye maisha yangu nina sheria nyingi nilizojiwekea na moja katika hizo ni" I fight not to win, I fight not to lose"* aliongea Jimmy na kufanya watu wale kutoelewa anamaanisha nini
"Najua hamjaelewa na haishangazi maana watu waliobahatika kusikia hii kauli walikuwa na nyuso kama zenu tu hiyo ni kwasababu hawataki kuelewa nachomaanisha bali wanaelewa maneno...."
".... The reason why I survive in battles is because I try my best not to lose my life, not to chase victory. You see, when you fight to win, you become less careful you get blinded by desire, by ambition, by the thirst to be on top. And when that happens, your guard lowers... your weakness gets exposed." aliongea akimaanisha" Sababu ya mimi kuendelea kuishi kwenye mapambano ni kwa sababu hujitahidi kadri ya uwezo wangu nisipoteze maisha yangu, na siyo kwa ajili ya kutafuta ushindi. Ona, unapopigana ili kushinda, unakuwa mzembe unatawaliwa na tamaa, na kiu ya kuwa juu. Na hali hiyo ikitokea, umakini unapungua… na udhaifu wako unaonekana wazi."
"You understimated me just cause I was powerless and now you think you could kill me just because you made me blind, you're wrong!" aliongea uso wake ukiangalia chini huku akinyanyua mkono kizembe na kufuta damu mdomoni akimaanisha "mmenichukulia poa kwa sababu sina nguvu, na sasa mnafikiri mnaweza kuniua kwa sababu umenifanya kipofu, mnakosea!"
"Asee J katika sifa zako moja ya sifa kuu ni unabwabwaja sana yaani unahubiri kinoma na kuwageuza mashetani kuwa malaika ila usidhani maneno yako yatatuyumbisha" aliongea bwana asiyebeba kitu
"Ndio unavyodhani?" aliongea Jimmy huku taratibu akitoa tabasamu la ajabu usoni, alikuwa ni kama shetani katika sura ya malaika
"Pumbavu! Kufa mwanaharamu wewe!" alimaka na palepale kufumbua na kufumbua aliibukia mbele ya Jimmy kama jini akitanguliza mkono kwenye shingo yake akidhamiria kumvunja na kuyakatisha maisha yake papohapo
Jimmy mwanzo mwisho amesimama vilevile kama sanamu lakini sasa ile mkono unakaribia kukamata shingo yake bwana yule asiyebeba kitu alishtukia tu anakamata hewa, Jimmy hakuwa mbele yake na alishangaa tu yuko pembeni upande wa kushoto wa mkono wake
Ilikuwa ni spidi kubwa ya kukwepa, ilikuwa ni kana kwamba anaona licha ya upofu alioupata
"Inawezekanaje hii?" alijiuliza bwana yule akiwa haamini macho yake, spidi aliyotumia Jimmy kusogea ilikuwa ni kubwa mara tano na ya kwake kibaya zaidi hakuwa anatoa msisimko wowote kuashiriia kama nguvu zake za kichawi zimerudi bali ni Jimmy kama Jimmy bila nguvunguvu zozote za ziada na hakika iliwashangaza na hata Jimmy uwezo huo ulimshangaza pia na kujiambia aliuchukulia poa sana
"Suprised?" Jimmy alimuuliza na bwana yule alishtukia ngumi ya uso iliyomrusha kama mpira na kwenda kumuangukia bwana mwenzake aliyebeba chungu na wote kuanguka kiasi cha chungu kupasuka kwani msukumo ulikuwa ni mkubwa sana
Chungu kupasuka ni kama amefungulia gereza la nafsi kwani maelfu ya nafsi zilianza kuzagaa angani huku na huko zikipiga makelele ya ajabu
Jalokuwa Jimmy hakuweza kuwaona lakini aliweza kuwahisi na kuwasikia wakipiga kelele za ajabu
"What the
JamiiForums' Community Engagement Guidelines | Mwongozo wa Ushiriki kwenye Mijadala" Bwana aliyebeba boksi alimaka kwa mshangao
"Ni nguvu ya aina gani hii?" aliuliza na swali hilo lilimuacha Jimmy na tabasamu
Ukweli kitabu alichorithi kwa mtawala wa uchawi mzee Salazar Soledad si tu kilikuwa na mbinu za kujifunza uchawi, kilikuwa pia na mbinu nyingine nyingi tu za kuweza kujifunza na kuwa na nguvu za ajabu na nyingi katizo hizo ni Instinict(mzio wa asili) na power of intuition(hisia za ndani)
Jimmy kabla ya kuanza kujifunza kuvuna nguo za kichawi alikuwa akijifunza mbinu mbalimbali kutoka kitabu na ndio hizo mbili na aliweza kuzimaster kikamilifu, nguvu hizo hazikuhitaji maswali ya kupanda levo bali ni kuziamsha mwilini kwakuwa ni nguvu za asili ambazo kila binadamu kuzaliwa nazo. Licha ya kufanikiwa kuziamsha hakumalizia hatua ya mwisho ya kuzipa utawala mwilini zaidi ya kuziweka kiporo
Hiyo ni kutokana na tamaa kubwa ya kutaka kujifunza uchawi lakini kwa wakati huo uchawi wake ulikuwa haufanyi kazi bila ya kueleweka sababu ni nini, na wakati kama huo aliona zina umuhimu mkubwa
Japo ni mbinu mbili ila ni uwili katika umoja yaani hufanya kazi pamoja, ni sawa na kusema sisi binadamu ili tuitwe binadamu ni ni lazima tuwe na mwili wa nyama, nafsi na roho. Licha ya hivyo vitatu ila tunakua binadamu mmoja aliye hai na pasipo kimoja wapo kati ya hivyo tunakuwa hatujakamilika, maana pasipo roho mwili unakuwa mfu sawa na maiti na pasipo nafsi hatuna utambuzi wa kiakili na kihisia na pasipo mwili wa nyama tunakuwa si binadamu kamili
Vivyo hivyo zichukulie hizo mbinu mbili yaani pasipo zote mbili nguvu inakuwa haina maana
Sasa wakati huo Jimmy aliweza kukamilisha hatua ya mwisho ya kuzipa hizo nguvu utawala kwenye mwili wake na automatically kuwa on muda wote
Chukulia kuzipa utawala ni sawa na kuzipa uhai na zinakuwa nguvu ambazo muda wote zinafanya kazi pasipo kukoma kama vile moyo wa mtu udundavyo bila kuacha mpaka pale atakapokufa
Kitabu kinaeleza kwamba Instinict ni nguvu ya ajabu ambayo mwili hufanya kitu au kujibu pasipo hiari yako ni kama programmu ya asili a.mbayo binadamu huzaliwa nayo.
Ni ule msukumo wa ndani wa kiasili ambao unakuongoza kulinda maisha yako au kushughulikia hatari bila kutumia akili ya kawaida yaani ukiwa kwenye hatari huna haja ya kufikiria bali mwili hujibu papo hapo automatically
Nikupe mfano rahisi, ushawahi kuona mtu ambaye hawezi kuruka ukuta hata ajaribu vipi anashindwa lakini baada ya kumuona simba ghafla tu anajikuta ameweza kuruka ukuta mpaka mwenye anajishangaa na baadae akijaribu tena anashindwa, unajua ni kwanini?
Hiyo ni kwasababu ile hatari na hofu imeweza kuishtua instinict ambayo imemuwezesha kufanikisha hilo jambo. ni mfumo wa "fight or flight" (pigana au kimbia) ambao uko ndani ya mwili tangu kuzaliwa Hio ndiyo nguvu ya instinict au kwa kiswahili tunasema "mzio wa asili"
Sasa kuipa kukamilisha hatua ya kuipa utawala ni kuipa uhai na mwili kuwa kama na ufahamu wake binafsi na macho yake ya kuona
Na pia tukija na nguvu ya hisia za ndani(power of intuition) ni ile nguvu ya hisia ya kuweza kuhisi nguvu hasi na chanyi na kuhisi vituvyote vilivyopo ndani ya dunia hii, ni kama kila kitu kinatambulika kwa hisia yake binafsi
Ni kama mwanga usioonekana unaowashwa ndani ya ubongo wako, ukikupa taarifa kabla macho, masikio au akili ya kawaida haijachakata. Wataalamu wa saikolojia huuita subconscious pattern recognition lakini kitabu cha Salazar kinaenda mbali zaidi: kinaeleza kwamba kila kitu kilicho hai au kisicho hai kinatoa “muungurumo” fulani wa nishati. Intuition ni kipokezi chako cha kuzisoma sauti hizo zisizo sikika. Mara tu nguvu hii inapopewa utawala, mwili wako unaongeza “kiungo cha sita” (sixth sense) kinachoendelea kufanya kazi 24/7 kana kwamba umepachikwa rada ndogo kifuani
Kama ulivyosema, hizi nguvu mbili ni kama “nafsi na roho” ndani ya binadamu mmoja. Instinict hukusukuma kutenda (fight or flight) bila kupoteza muda; Intuition hukupa taarifa ili ujue ni nini hasa kinakuja. Bila Intuition, Instinict inaweza kukukimbiza ovyo; bila Instinict, Intuition inaweza kukujaza hofu bila mwitikio. Pamoja, zinaunda mtandao kamili wa kujilinda na kufanya maamuzi katika sekunde sifuri.
Kwa lugha nyepesi ni kama vile Jimmy alikuwa akiisikiliza dunia, alikuwa akipata hisia ya kila kitu kilichopo ndani ya ulimwengu huo
"Mnakumbuka mara ya mwisho niliwaambia nini? Jimmy aliwauliza na alijua hawatojibu hivyo aliwasaidia kujibu
"Niliwaambia ninyi ni kunguni tu haijalishi mna nguvu kiasi gani lakini kunguni siku zote ni kunguni tu na stabaki kuwa kunguni" aliongea na kuwafanya kukunja nyiso zao kana kwamba wamenusu harufu ya yai lililooza
Walilipukwa na hasira kiasi kwamba hawakuwa hata na neno la kusema zaidi ya nyuso zao kuonyesha ni kwa namna gani wamechukia na kukasirika
"Bwana mdogo naona unavuka mipaka sasa hata kama una nguvu hivyo hupaswi kuvuka mstari wa maneno"
"Mipaka?" aliongea huku akianza kucheka kana kwamba amesikia kituko na kisha kutulia na kusimama kikakamavu huku sura yake ikibadilika nakuwa ya kuogopesha kwa jinsi alivyo kauzu
"Ngoja niwaambie kuhusu sheria yangu na nataka msikilize kwa makini sababu nataka pambano la haki, nataka mpambane mkiwa mnajitambua ili muone ukweli ya kwamba ninyi ni kunguni" aliongea na kunyamanza kidogo kisha akaanza kueleza
"Adui mkubwa tunayekabiliana naye si yule aliye mbele yetu, bali ni uwanja wa vita ulioko ndani ya mioyo yetu wenyewe. Hisia zetu wenyewe hutusaliti: tamaa, hasira, furaha kupita kiasi, hofu, kiburi, majivuno, huzuni, hata matumaini... Ndiyo, wakati mwingine.
Kila mojawapo ya hisia hizi zinaweza kutuangamiza ikiwa tutaziruhusu zitutawale.
Unapokasirika kupita kiasi, unashambulia bila kufikiri. Unapojivuna sana, unamdharau adui yako. Unapofurahi kupita kiasi, unasahau kujilinda. Unapohofia sana, unagandia mahali, na kifo kinakupata., Hata matumaini... hata matumaini, yakishikiliwa kwa nguvu kupita kiasi, yanaweza kukufanya kuwa mzembe.
Unaona... kuishi ni suala la usawa.
Ni kuhusu kupumua wakati mapafu yako yanapolia kwa hewa, kusimama imara wakati miguu yako inatetemeka, na kufikiri kwa uwazi wakati moyo wako unataka kuzama katika machafuko.
Kupigana ili usipoteze maana yake ni kupigana kwa akili, kwa unyenyekevu, kwa ufahamu daima ukijua kuwa kosa moja tu linaweza kugharimu kila kitu.
Sipigani kwa ajili ya utukufu. Sipigani kuthibitisha chochote. Napigana kwa sababu maisha yangu ni muhimu, kwa sababu wale wanaoningojea ni muhimu.
Napigana kwa tahadhari. Napigana kwa subira. Napigana kwa heshima ya maisha yangu na hata ya adui yangu."
Wakati Jimmy anaongea anga lote lilikuwa kimya kana kwamba lilikuwa likimsikiliza pia na sauti yake kusikika hata kwa umbali wa kilomita tatu
Alikuwa ni kama mfalme anayeng'aa ambaye anaingia vitani kuokoa raia wa himaya yake, kutokana na mwanga hafifa wa rangi ya dhahabu iliyofifia kummulika alionekana aking'aa kama ana utukufu fulani hivi hasa ukizingatia ni mweupe wa ngozi, ule weupe wa njano wa kibongobongo
Alipomaliza tu kuongea ghafla hali ya hewa ilianza kubadilika na wale watu watatu walianza mtafaruku wa kihisia na msisimko wa nguvu za ajabu na Taratibu walimshuhudia Jimmy akipitia mabadiliko
TO BE CONTINUED..........
SOLO KING: DARK MAJESTY
CHAPTER 39: Breakthrough(Kiini cha mabadiliko)
Upande mwingine ndani ya ofisi kubwa yenye mwanga hafifu alionekana mwanaume mweusi aliyevalia gwanda nyeusi na mwanaume huyo hakuwa mwingine bali kamanda Rama, mkuu wa Unit 9-H au Hidden Supremacy
Alikuwa amesimama huku mkono mmoja ukiwa sikioni kuashiria kwamba alikuwa katika maongezi kwenye simu
"Mkuu hali ni mbaya zaidi kuliko tulivyofikiria. Tunahitaji msaada wa haraka sasa hivi" ilisikika sauti upande wapili
""Nipe ripoti Freya kuna nini kinaendelea?" aliongea Kamanda huyo
"Tumeweza kudili na kundi la wanywa damu lakini tumekutana na adui wengine wenye nguvu, tumefanikiwa kutoka kwenye hatari ya kifo lakini Jimmy yuko kwenye hatari ya kupoteza uhai tukiendelea kuzubaa" Freya alijibu
"Sawa nitakuja mimi na wengine, niambie kuhusu raia, wangapi wamesalimika?"
"Kuhusu raia mara baada ya sisi kufika hatukuweza kuwaona lakini baadae tukaaja kugundua kwamba miili ya wanywa damu tuliyoikuwa ni ya wanakijiji"
"Nini! Ebu eleza ukaeleweka"
"Kamanda hatuna muda wa kupoteza, si kitu ambacho naweza kueleza kwenye simu kikaeleweka ni muhimu ukatuma kikosi mengine yafuate"
"Sasahivi nafika na kikosi" aliongea kamanda huyo kisha kukata simu
°°°°°°°°°°
Upande mwingine ndani ndani wenye nyumba nyingi za kifahari na mazingira safi, taa za rangi nyeupe zikimulika kila kona ya mtaa huo na kufanya kuonekana kama vile mchana
Katika moja nyumba nzuri ndani yake alionekana mwanamke ameketi sebuleni na bila shaka alionekana kukaa hapo muda mrefu akisubiri, pembeni ya sofa alilokuwa ameketi kulikuwa na simu janja na kila muda alikuwa akiiangalia
Mwanamke huyo hakuwa mwingine bali ni Biancalina, mpaka muda huo wa saa tatu kasoro alikuwa bado hajaondoka nyumbani kwake kuhudhuria mualiko wa sherehe ya msanii mkongwe nchini katika siku ya miaka thelathini ya ndoa yake na vilevile siku ya kuzaliwa ya mwanawe
Alikuwa akimsubiri Jimmy mpaka muda huo, mwanzoni alijiaminisha lazima atarudi kabla ya saa tatu, na pia kupokea simu kutoka kwa Cid kwamba Jimmy atarudi ndani ya muda lakini alionekana alikuwa akijifariji bure tu na pia kutumainia ahadi hewa
Muda ulikuwa ni saa mbili na dakika hamsini na kitu kupitia saa ya ukutani. Mwanamke huyo alionekana kuwa mnyonge sana kiasi cha kutia huruma.
Mwanamama Mary alikuwa amesimama mahali akimtazama mkwe wake mtarajiwa alivyokuwa akitia huruma na hakuwa na mpango wa kumuingilia na badala yake alimtazama huku moyoni akimtupia lawama za kila aina mwanae na alikusa akijiuliza huyo mtoto yuko wapi muda huo? Na anafanya nini? Hajui kama anasubiriwa na mke wake mtarajiwa?
Simu ya Bianca ilianza kuunguruma mlio wa alarm kuashiria ni saa tatu kamili na baada ya kuona alinyanyuka zake sofani na kupandisha juu na alikuwa ameghairi kabisa kuhudhuria sherehe hiyo. Alienda moja kwa moja mpaka chumbani kwake na kujifungia
°°°°°°°°°°
Kwanini wasipatwe na hofu kwa mfano? Kwa mabadiliko hayo ya kushtukiza na kutotegemea lazima hofu iliwavaa.
Upepo mkali ulikuwa ukivuma kutoka pande zote kuu nne za dunia na kana kwamba upepo huo mkali ulikuwa ukishangilia kwa shangwe baada ya kuhisi uwepo wa mfalme wao na kwenda kumlaki
Msisimko wa nguvu zake za kichawi uliongezeka mara ttatu zaidi ya mwanzo, nafsi zilizokuwa zikitangatanga angani zilikuwa zikipiga kelele za ajabu kana kwamba msisimko huo ulikuwa ukiwaathiri kwa kiasi fulani
Upande wa wale mabwana watatu walihisi ni kama nafsi zao zilikuwa zikivutwa na nguvu ya ajabu kama sumaku na walishindwa kuelewa ni nguvu ya aina gani hiyo lakini jambo la hakika walifahamu kwamba Jimmy amepiga hatua yani ni sawa na kusema amepanda levo
Mara taratibu Jimmy alianza kuelea hewani kana kwamba anavutwa na kamba kwenda juu mpaki kufikia urefu wa mita kumi kutoka hewani mpaka ardhini
Aliweza kuhisi hisia mchanganyiko za ajabu zikisambaa mwili mzima, kulikuwa na hisia za ubaridi, joto, shoti kusambaa mwilini na hisia nyingine nyingi, vuguvugu hilo la hisia lilimfanya ajishangae na kuishangaa nguvu hiyo. Alihisi pia ufahamu wake ukipanuka na kuongezeka kupita kawaida ni kama alikuwa akipokea funuo/ufunuo mbalimbali akilini mwake
Alikuwa akielea juu kama unyoya ueleavyo kwenye hewa, akiwa katikati ya nguvu isiyoelezeka alikuwa akisikilizia hisia alizokuwa akizipata na taratibu ukungu ulianza kujitokeza ukianzia chini ya miguu na kupanda juu taratibu na hatimae kumfunika mwili wake mzima
Mwili wake uliofunikwa, na ukungu ule haukuwa wa kawaida. Ulikuwa ni kama mvuke wa moto na baridi kwa wakati mmoja
Nywele zake ni kama vile zilikuwa zikichemka kana kwamba zilikuwa zinaishi; zikitetemeka kana kwamba zilikuwa zikipigwa na shoti
Haukuwa ule ukungu wa bluu tena bali mwekundu, ieleweke ukungu umtokao Jimmy ni ile nguvu ya kiroho aliyonayo ambayo msingi wake ni kutokana na nguvu za kichawi alizonazo. Kwa jinsi ukungu ule uliokithiri kumzingira alikuwa ni kama kivuli ndani ya moto wa ajabu, kila pumzi aliyovuta ilionekana kuongeza kasi ya mtiririko wa nguvu ile
Ilikuwa ni nguvu ya kipekee na scenerio ya ajabu iliyowaacha kwenye mshangao mabwana wale na hawakuwa na la kufanya zaidi kuendelea kustaajabu, sio kama walikuwa na hofu kubwa kiasi cha kutofanya chochote, walichohofia ni nini kitawakuta iwapo watakurupuka kushambulia
Naam mwamba alikuwa katika levo ya tatu ya uchawi, hatua ya kiini cha mabadiliko!(Breakthrough)
Licha ya hivyo Jimmy alishindwa kuelewa imekuwaje akapanda levo? au ni kwasababu ya mateso aliyokuwa akipitia? na kwanini ghafla tu nguvu zake za kichawi zinatenda kazi ilihali mwanzoni ziligoma?
Maswali yote hayo hkuweza kupata jibu hivyo kupotezea na kutua chini taratibu na ukungu kumpotea
Baada ya kutua tu alielekeza uso wake waliposimama mabwana wale usoni akiwa na tabasamu lenye nia ovu kisha kunyanyua mkono wake akiwanyooshea na kuwapa ishara ya wao kuanza kuchukua hatua
Maneno hayakuwa na maana wakati kama huo, haukuwa wakati wa ngojera bali vitendo kwani mabwana wale mara baada ya kupokea ishara walitazamana wao kwao kwa sekunde kadhaa
Kufumba na kufumbua hawa hapa mbele ya Jimmy kila mmoja akitanguliza shambulizi lenye nguvu
Spidi yao iliongezeka tofauti na mwanzo lakini licha ya hivyo kwa Jimmy ilionekana ni spidi ya kitoto sana mbele ya nguvu ya instinict aliyokuwa nayo, walishambulia mfululizo wa mashambulizi mengi tofauti lakini hakuna hata moja lililomgusa bwana mdogo Jimmy
Alikuwa akikwepa kitaalamu sana yaani kulia, kushoto, mbele, nyuma, juu, chini kwa utulivu wa hali ya juu kana kwamba alikuwa ni master aliyebobea kwenye kukwepa mashambulizi ya aina yoyote, licha ya upofu lakini kwa jinsi alivyokuwa akikwepa usingeamini kama ni kipofu
Ni kama vile alikuwa akifanya mazungumzo na hisia zake, alikuwa akijua kila ngumi, kila teke, kila shambulizi linatokea wapi na linakusudiwa kutua wapi na akwepe vipi, ukisikia mtaalamu basi alikuwa ni mtaalamu haswa!
Ni sauti za misuguano ya hewa pekee ilisikika na zilipita takribani dakika ishirini za kukuru kakara kati ya Jimmmy na mabwana wale.
"Pumbavu! Tukiendelea hivi tutaishia pabaya ni muda sasa wa kumuonyesha nguvu yetu halisi" alifoka mmojawao baada ya kuona wanavyosota kushambulia bila kufanikiwa kugusa hata unywele, na hakika jambo hilo lilimkasirisha sana yaani licha ya kumsababishia upofu hawakuweza kumgusa, na ilikuwa ni zaidi ya fedheha kiasi kwamba alipandwa na jazba na kutamani amkamate na kumkatakata viungo vyote vya mwili lakini sasa kumkamata ilikuwa ni ndoto ya mchana!
Baada ya mwenzao kutoa kauli hiyo walikubaliana nae bila ubishi waliona kuliko kujichosha na kupoteza muda ambapo mwisho wa siku wataishia kufa ni bora wkutumia nguvu zao zote kumaliza pambano kisha kuendelea na kile kilichowaleta ndani ya ulimwengu huo wa ajabu, kuendelea kujidhalilisha kwa mtu kipofu ni ushenzi uliopitiliza
Kwa pamoja walianza kutamka maneno ya ajabu kama vile wanasali na kadri muda unavyosonga hali ilianza kubadilika, Jimmy alipata hisia kwamba kuna kitu kibaya kinakwenda kutokea na hisia zake zilikuwa sahihi
Miili yao ilianza kutuna kana kwamba inataka kupasuka, urefu wao uliongezeka na makucha makali kujitokeza, nyuso zao zilibadilika na kuwa za kutisha, harufu nayo ilibadilika na kuwa mbaya zaidi kiasi kwamba Jimmy alijihisi kichefuchefu
Pamoja na kubadilika wote walikuwa vimo sawa, baada ya hatua hiyo walinyanyua mikono yao kuelekea angani kama vile wanaabudu na kuanza kutamka kwa pamoja
"Nafsi elfu, nguvu elfu eeh nafsi kwa damu na wimbo ingieni ndani yetu!"
Waliongea kwa kurudiarudia kana kwamba wanaimba na maelfu ya nafsi zilizokuwa zikitangatanga angani zilikuwa zikipiga kelele na ghafla zilijikusanya makundi matatu si kwa hiari bali kuna nguvu ya ajabu ilikuwa ikiwaendesha na kisha kama vile sumaku yenye nguvu kubwa walivutwa na kuingia ndani ya wale mabwana kupitia midomo yao mikubwa na kadri zilivyowaingia ndivyo walivyozidi kurefuka na kutuna
Ndani ya dakika mbili tu mabwana wale hawakuwa binadamu tena bali ni majitu makubwa yenye urefu wa futi nane na upana wa mita 2.3, walikuwa kama ma, hulk fulani hivi wenye sura kama fisi na pembe kama ng'ombe
Walikuwa wakitisha kwelikweli na nguvu zao ziliongezeka lakini hazikumuogopesha Jimmy, kwake neno woga halikuwepo kwenye dictionary yake. Zaidi tu aliweka uso wake siriaz
Bila hata kupoteza muda jitu la kwanza lenye sura kama fisi lilirusha ngumi yenye uzito wa kutosha akidhamiria kumkandamiza Jimmy kama chapati
"BOOM!" sauti ya ngumo kugongana ardhi ilisikika kiasi kwamba ni kama ardhi ilikuwa ikitetemeka na kusababisha shimo na vumbi kubwa
Jimmy aliweza kukwepa shambulizo hilo huku moyoni akitamka neno "Asee!"
Pengine ngumi ile ingempata angegeuka chapati kweli, aliweza kuhisi kabisa nguvu iliyotumika kurusha shambulizi ilikuwa ni kubwa sana
"Damu inayobadilika awamu ya pili, ngozi ya chuma!" alinena Jimmy akitumia mbinu ya damu inayobadilika
Baada ya kutamka taratibu cell za damu yake zilianza kuchemka na misshipa ya damu kuanza kutuna huku ngozi yake ikianza kubadilika kuanzia shingoni mpaka miguuni na kuwa ngumu kama chuma
Ni kama vile ngozi yake imebadilika na kuwa kama gamba la mgongo wa mamba, Kama jinsi ngozi ya mamba ilivyo ngumu na yake ilikuwa vivyo hivyo lakini ugumu ulikuwa mara tatu yake, hakuongezeka mwili wala kutuna ni ngozi yake pekee ndiyo iliyobadilika
Ngozi yake ilibadilika na kuwa kama mwangaza wa mwezi umulikao baharini na kung'aa. Yalikuwa mabadiliko ya kasi yaliyochukua nusu dakika pekee kukamilika
Ieleweke kwamba katika levo za uchawi wa mabadiliko mbinu zinazotumika ni zilezile tu hata ukipanda levo, kinachoongezeka ni makali na kina cha nguvu, mfano mtu aliyekatika levo ya kwanza na aliye katika levo ya pili wanatumia mbinu moja lakini aliye katika levo ya pili mbinu yake inakuwa na nguvu kubwa kuliko wa yule aliye katika levo ya kwanza
Hii ni kwa sababu kila unapopanda levo, damu na nafsi yako inakua ikitengeneza uhusiano wa ndani na chanzo cha uchawi. Hali hii inafanya mwili wako kuhimili mzigo mkubwa zaidi wa mabadiliko, bila kuvunjika au kuungua kwa ndani
Fikiria kama varnish(ni rangi ya kung’arisha mbao au kipako cha kung’arisha) inayowekwa kwenye mbao. Awali, mbao haina kinga kubwa inaweza kulowa na kuoza. Lakini unapoongeza varnish moja juu ya nyingine, mbao hiyo inakuwa ngumu, inang’aa na inastahimili mvua, jua na miale ya moto. Vivyo hivyo, kila levo mpya unayopanda kwenye uchawi wa mabadiliko ni kama kuweka varnish nyingine juu ya nafsi yako: unakuwa mgumu zaidi, wenye uthabiti na una uwezo wa kuhimili shinikizo kubwa la uchawi.
Kwa mfano, katika levo ya kwanza mtu anaweza kutumia mbinu za damu inayobadilika lakini anatumia kwa dakika chache mpaka kukosa udhibiti lakini kwa aliyekatika levo ya pili anatumia mbinu hiyohiyo kwa muda mrefu kuliko wa yule aliye katika levo ya kwanza
Ndiyo maana wachawi wengi wanaogopa wale walio katika levo za juu kwa sababu mbinu yao hiyo hiyo ya awali inakuwa ni kama dhoruba inayoangusha majumba
Mara baada ya mijitu ile kushuhudia mabadiliko hayo ilianza kunguruma na kupandwa na morali na wote kwa pamoja walianza kushambulia kama vichaa, pamoja na uzito wao lakini walikuwa wepesi kwenye kurusha mashambulizi
"BOOM! BAM! BAM! BOOM! BAM!"
Hatimae pambano lilichukua hatua nyingine, binadamu mmoja dhidi ya majitu matatu ni sauti za mipanguano ya ngumi kati ya majitu watatu na binadamu mmoja
Ulikuwa ni mpambano wa kibabe kwelikweli, kila ngumi, kila teke yaani kila shambulizi lilikuwa limebeba ujumbe maalumu, ni kama walikuwa wakizungumza kupitia mashambulizi, walikuwa wakidhihirisha ule msemo wa "Fighting is conversation" kwamba kupambana ni kuzungumza
Je wanazungumzaje? Kila shambulizi lilikuwa kama hoja yenye uzito wake. Kila teke lilikuwa kama nukta ya maelezo, na kila ngumi ilikuwa kama alama ya mshangao. Jimmy hakupigana tu kwa mikono na miguu, bali kwa moyo na roho, akitoa ujumbe kwa kila pigo alilolitoa
TO BE CONTINUED..........
SOLO KING: ANCIENT LEGACY
CHAPTER 40: The dance of survival
Majitu matatu pia hayakubaki nyuma, kila mmoja alionekana kutoa hoja zake kwa nguvu za ajabu. Vilio vyao vilikuwa kama sauti za giza, na kila pigo lililoachwa angani lilionekana kama dokezo la kifo.
Yote kwa yote Jimmy bado alibaki imara akisoma kila harakati zao, akijibu hoja kwa hoja, akigeuza kila shambulizi kuwa jibu. Halikuwa tu pambano la ana kwa ana ulikuwa pia kama mjadala wa maisha na kifo, na kila mmoja alikuwa na kitu cha kusema.
Kupitia kila ngumi na teke, Jimmy alionyesha kwamba nguvu pekee haishindi, bali akili na ujasiri vina nafasi yake. Majitu yalikuwa na nguvu, lakini Jimmy alikuwa na sababu na sababu hiyo ilimfanya awe imara kama mwamba.
Lilikuwa ni pambano la ujasiri dhidi ya nguvu, akili dhidi ya ukatili, mwanadamu dhidi ya majitu. Hakika walikuwa wanazichapa kwelikweli si lelemama, kasi yao haikuwa ya kawaida. Ukisikia pambano la haki ndiyo hilo sasa
Zilipita takribani dakika ishirini na tano kwenye uwanja vita bila mapumziko na hakuna aliyeonekana kuchoka na kama kawaida waliendelea kuzichapa, Jimmy alishangaa licha ya dakika zaidi ya ishirini kupita mbinu hiyo ya damu inayobadilika haikumletea madhara yoyote ni kama vile haina kikomo cha kutumia na jambo hilo lilimfurahisha
Upande wa lango la pembe tatu la kuingilia ulimwengu huo walionekana watu wakiingia ndani humo na aliye mbele kabisa alikuwa ni kamanda Rama, nyuma akifuatiwa na Freya, Caren, Ben Joshua na wengine waliokuwa katika kitengo cha unit-9 H, na Mia pia alionekana kuwepo kwenye kundi hilo, haikueleweka imekuwaje akawa pamoja nao lakini ilionekana amesaidia kuwaponya majeraha wakina Freya
Walikuwa wameingia jumla yao wakiwa kumi na wote mikono yao miwili walikuwa wamebeba masanduku makubwa meusi isipokuwa Mia pekee, Bila shaka yalikuwa ni yale masanduku ya kuhifadhia siraha za moto za kijeshi
Ile wanaingia tu kitu cha kwanza ni kuduwaa kwa mshangao mkubwa, hawakuamini macho yao kwa kile walichokuwa wakishuhudia mbele yao
"Damn! Oh dear mother Theresa!" aliongea Ben huku akimeza mate yake kwa shida sana
Wakina Freya pia hawakutegemea kukutana hali hiyo, Mkuu wao kamanda Rama naye kwa maelezo aliyopewa na anachoshuhudia ni sawa na mbingu na ardhi, aliambiwa watu lakini anakutana na majitu
Jimmy aliweza kuhisi ongezeko la watu ndani ya ulimwengu huo umbali wa mita sabini na alipo lakini alipotezea na kuweka umakini kwenye pambano na alionekana akilifurahia kwelikweli alijiambia ngoja kwanza apate uzoefu
Spidi na nguvu tu inayotumika kwenye pambano walijiambia hilo si levo zao kabisa ni bora kubaki shabiki kuliko kuingilia na kuishia kugeuzwa mlenda kwa shambulizi moja
"Nani ambaye hajipendi?" Ben alouliza na kufanya wote wamuangalie kwa macho ya ajabu, si kwamba hawakumuelewa anamaanisha nini bali walimuona anataka kuwageuza mbuzi wa kafara
"Kwanini usiende wewe Bwana Bernard kidoto?" Freya alimjibu akitaja majini yake mawili na bila shaka wote walikuwa wakisubiri kuona atasema nini, Ben ni kama vile hakusikia na kujifanya akiangalia pambano kwa umakini wa hali ya juu akitafuta upenyo wa kuingilia kutoa msaada
Kamanda Rama licha ya kuwa kiongozi wao lakini alikuwa levo sawa na wengine wote walikuwa katika levo ya pili ya damu inayobadilika, alichowazidi ni cheo tu lakini likija suala la nguvu ni walewale tu
"Anaonekana kama vile haoni bali anatumia hisia" aliongea Mia na kuwafanya wote wamuangalie ni kama vile hawakumuamini
"Unataka kusema ni kipofu? Mia acha utani basi, mimi na wewe wote tunajua Jimmy si kipofu" aliongea Ben
"Huwezi jua nini kilitokea baada ya kumuacha hapa!" Kamanda, Rama alidakia
"Japokuwa miondoko yake anaonekana kama anaona lakini ukweli ni kwamba haoni" Mia aliongea huku akitazama pambano kwa makini
"Wewe ni nani?" alouliza kamanda Rama alijiambia kama msichana huyo aliweza kugundua hilo bila wao kugundua ilitia mashaka
"Naitwa Mia" alijibu msichana huyo huku akitabasamu
"Hilo tayari ushaniambia nachotaka kujua ni asili yako na ni mtu wa aina gani?"
Mia alitabasamu kidogo, macho yake yakielekea kwenye pambano, kama vile hakutaka kutoa jibu kisha kusema "Some things are better unsaid" kwamba Baadhi ya mambo mengine ni bora kutosemwa na jibu hilo lilimfanya Kamanda huyo kukunja sura kwa kutoridhika
“Msichana, usinizungushe. Nimekuuliza swali wazi. Unatoka wapi na wewe ni nani haswa?”
"Wakati mwingine, majibu yapo kwenye vitendo, siyo maneno.” Mia liongea maneno yenye busara kama mzee licha ya kuonekana bado kijana
“Kama kweli unataka kujua mimi ni nani, labda ni muhimu kwanza uelewe kwa nini niko hapa. Hata bila kujua jina langu au historia yangu, unaweza kuelewa dhamira yangu kupitia kile ninachofanya.” Mia aliendelea kuongea
"Unazungumza kama mtu mwenye siri kubwa" aliongea kamanda huyo na Mia kutikisa kichwa taratibu na kufungua kinywa chake akinena
"Kila mtu ana siri zake, Kamanda. Lakini wakati mwingine, cha muhimu zaidi siyo siri yenyewe, bali ni jukumu unalochukua mbele ya wengine....."
"Tuangalieni namna ya kumsaidia mwenzetu kumalizana na hawa mashetani" Caren aliingilia kabla hata Mia hajamaliza sentensi yake, alifanya hivyo kwasababu aliona msichana huyo hakuwa akitaka kuelezea kuhusu yeye na kamanda anaonekana kufosi
"Heshimu siri za watu kamanda" aliongea Ben huku akimshika bega kamanda Rama na kuishia kupigwa jicho na kujikuta akitoa mkono bila kupenda
Walianza kuweka masanduku makubwa waliyokuja nayo chini ardhini moja baada ya jingine kisha kufungua na zilionekana siraha za moto aina tofauti
Kulikuwa na mabomu ya pini(granade) hamsini kwenye sanduku la kwanza na pili na kukamilisha idadi ya mabomu mia, magazine kubwa na ndogo si chini ya arobaini zilizojaa risasi kwenye sanduku la tatu na nne na kukamilisha idadi ya magazini zaidi ya Themanini, bastola ndogl kumi kwenye sanduku la tano na sita, Jegeja kumi kwenye sanduku la saba na nane, sanduku sita kila moja limebeba bazoka mbili na jumla ya bazoka kwenye sanduku zote sita zilikuwa kumi na mbili na sanduku nne zilizobaki zilikuwa zimebeba rocket za mabomu zitumiwazo na bazoka jumla zikiwa ishirini(tano kwenye kila sanduku)
"Asee nilidhani mtakuja kichwa kichwa tu kuja kujidhalilisha kwa kuchezea kichapo cha mbwa koko ila naona mmekuja na back up za kutosha sio mbaya, nfiyo maana unaitwa Kamanda" aliongea Ben huku akijivhekesha mwenyewe na kamanda Rama alimpuuzia alijiambia katika wagmtu anaowaongoza ni Ben pekee aliyekosa adabu
Ukweli kamanda huyo baada ya kupokea maelezo mafupi tu alijua lazima kutakuwa na jambo kubwa linakwenda kutokea hivyo kuandaa back-up plan mapema
Wanajeshi hao walianza maandalizi ya kuandaa siraha za kuingia nazo vitani, Mia aliishia kumeza mate mengi huku karoho kakitaka kumtoka kwa hofu ya kile kinachokwenda kutokea muda si mrefu
Upande wa pambano majitu yale yalifanikiwa kumzingira na kwa pamoja waliruka juu angani wakidhamiria kummaliza kwa kumkanyaga kwa kishindo
"BOOM!" mshindo kama kimondo kugongana na ardhi ulisikika na kusababisha wimbi kubwa la presha na vumbi, katika alipokuwa amesimama Jimmy kulikuwa na shimo kubwa lililosababishwa na majitu yale lakini Jimmy hakuonekana na hakukuwa na ishara yoyote kwamba shambulizi lile limempata
Alikuwa amepotea kimazingira, wakati wanajiuliza na kugeuka huku na huko kujua alipo Jimmy mara mmoja wa majitu yale alishtukia teke moja moja takatifu sana la mgongo lililomrusha kama furushi umbali mrefu sana huku akidunda dunda ardhini kama mpira
Mwingine ile anageuka upande ambao ambao shambulizi hilo linatoka naye alishtua ngumi nzito ya taya iliyomrusha hewani na kabla hajatua ardhini Jimmy aliweka miguu sawa kutafuta balansi kisha misuli ya miguu kutuna na kufyatuka kwenda kwenda hewa akisindikiza na shambulizi la "flying knee" ambapo goti lake humu kama vhuma lilimpiga tena kwenye taya kiasi kwamba ilisikika sauti ya migupa kuvunjika na baada ya shambulizi hilo alitua chini kwa ustadi wa hali ya juu kwa kuruka sarakasi
"BAM!" ilikuwa ni sauti ya jitu lile kutua ardhini vibaya sana, mashambulizi yote hayo yalifanyika ndani ya sekunde tatu pekee na kuwaacha kwenye bumbuwazi wenzake ambao walikuwa wakishuhudia
Jitu la mwisho mara baada ya kuona wenzake wamejeruhiwa vibaya sana alikasirika na kunguruma kilio cha maumivu na kwa hasira kama zote kufumba na kufumba alikuwa nyuma ya Jimmy, lakini unadhani Jimmy angeruhusu hilo?
"Exsomnia Gravitus!" hatimae alitumia uchawi wa maneno
Ile anadhamiria kumvunja Jimmy shingo anajishtukia ameganda hewani na kuwa katika slow motion! Kisha Jimmy alimgeukia akitanguliza na tabasamu la kishetani na alimtandika ngumi nyingi mfululizo
Ngumi zake zilikuwa na kasi kiasi kwamba ilikuwa ngumu kuhesabu na kujua idadi ya ngumi alizompiga, jitu lile mimacho ilitaka kumtoka kwa mauteso aliyokuwa akipata na hawakuwa na uwezo wa kufanya chochote zaidi ya kusikilizia maumivu
Ni kama vile alikuwa amefungwa na kamba zisizoonekana. Jimmy baada ya kumshushia ngumi mfululizo aliruka hewani huku akijizungusha kama feni na kumsindilia teke la kifua ambalo lilimtoa kwenye kifungo cha hewa na kumrusha kama furushi na kwenda kumuangukia mwenzake aliyekuwa anasimama "BAM!"
Jimmy alikuwa na uwezo wa kukwepa shambulizi lile ni vile tu aliona anapoteza muda baada ya kukumbuka anahitajika nyumbani
Tokea mwanzo alikuwa na uwezo wa kuwamaliza ndani ya dakika moja tu kwa uchawi wake wa maneno lakini hakufanya hivyo ni kwasababu alikuwa akipata uzoefu wa pambano la ana kwa ana na majitu hayo
Kingine majitu yale uchawi wao mkubwa ulikuwa ni kwenye kubadili nafsi na kusababisha uzito wa hewa, hawakuwa na jipya jingine hivyo aliona ni kama atakuwa anafanya uonevu ndiyo maana alichagua pambano la ana kwa ana angalau kuchangamsha mwili kidogo, isitoshe haikuwa mara ya kwanza kupambana nao, mara ya mwisho aliwashinda je awamu hiyo ambapo amepanda levo atashindwaje kwa mfano? Hata kama asingepanda levo bado angewashinda tu ni vile tu nguvu ziligoma kutenda kazi pasipo kujua sababu
Lakini kulikuwa na tofauti kwenye pambano hilo na mara ya mwisho anapambana na hao walozi, kipindi kile alikuwa akipambana yeye kama yeye akitumia mbinu hiyo hiyo ya ngozi ya chuma na hawakuwa na chungu cha nafsi wala boksi lenye kichwa cha Baba yaga
Kipindi hiko sasa kulikuwa na ugumu kidogo, ukiangalia amepatwa na upofu wa ghafla ambapo chanzo chake ni laana iliyokuwa kwenye kutazama macho ya mchawi wa kale aitwaye Baba yaga, kingine nguvu zake ziligoma kwa muda na pia mabwana hao kunyonya maelfu ya nafsi za mashetani na binadamu kwa ujumla na kubadilika kuwa viumbe vya kutisha.
Yule jitu aliyeharibiwa taya alisimama tena japo kwa shida na kukusanya pumzi nyingi na kupumua kama nyati aliye tayari kumtimua yeyote akatizaye mbele yake na taya kurudi sawa
Lakini sasa la haula! Rocket lililokatika kasi lilikwenda kumbamiza jitu hilo kwa nguvu na kusababisha mlipuko na kumtupilia mbali
"BOOM!!"
Na kwa mbali alionekana kamanda Rama amebeba bazoka begani akilenga upande huo na bila shaka ni yeye aliyefanya shambulizi hilo la kushtukiza
Jimmy aliyesimama umbali kidogo aliweza kulishtukia hilo mapema na ndiyo maana hakuwa na mpango wa kufanya chochote zaidi ya kutulia tuli
Jitu lile baada ya kushambuliwa na rovket alipatwa na majeraha madogo tu ilionekana alikuwa na ngozi ngumu pia lakini haikumaanisha hakupata maumivu!
"We strike!" aliongea kamanda Rama kwa amri akimaanisha sasa wanashambulia na baada ya kauli hiyo wote walijipanga kisawasawa wakiwa wamepakia siraha na magazine huku mikononi wakishikilia majegeja wengine bazoka isipokuwa Mia aliyekuwa amekwenda kukaa mbali nao kujilinda
"as usually we go the dance of survival!" aliongea Freya akimaanisha "kama kawaida tunakwenda mtindo wa ngoma ya kusalia hai"
Mara baada ya kumaliza kauli hiyo walianza kukimbia kwa pamoja wakijipanga kwa safu maalumu huku kila baada ya sekunde tatu wakibadilisha safu zao kwa ustadi sana ni kama vile walikuwa wakicheza mchezo wa kubadilisha nafasi zao
"Namba nne shambulia!" aliongea Kamanda Rama na wote kwa pamoja walisimama huku wakipiga goti la mguu mmoja na namba 4 ambaye alikuwa ni Joshua alikimbia na kuukanya goti la mmoja wapo na kuruka angani huku akielekeza shabaha yake kwa moja ya yale majitu mawili yaliyoanguka pamoja
Wakati akiwa hewani alifyatua rocketi na kutua ardhini kwa kujiviringisha sarakasi murua na kutua vizuri
"FwOOOOOSH.... BOOM!" roketi ilifyatuka na kwenda kumlenga kisawasawa lile jitu na kurushwa hukooo
"Namba sita" Ile Joshua anatua tu Rama alitamka tena na namba sita naye aliyepiga goti na kulenga shabaha yake alifyatua roketi
"FWOOOOSH...... BOOM!" shabaha ililenga palepale ilipokusudiwa na kwenda kumshambulia jitu la mwisho na kwenda mumbamiza na kumlipukia
"Safu ya mshale!" aliongea kamanda Rama na ghafla walibadili safu na kusimama kama ungekuwa angank ungeona wamesimama kama vile wamechora umbo la mshale
"Songa mbele!" na kama kawaida walianza kusonga mbele wakikimbia kuelekea kwa wale majitu. Na kama ilivyotegemewa hawakuweza kufa kirahisi kwani walisimama tena
"Namba, moja, tano na tisa" baada ya hiyo kauli wote walipiga magoti chini isipokuwa namba moja ambaye ni kamanda Rama aliyesimama kushoto kabisa, namba tano ambaye ni Ben aliyesimama kulia kabisa na namba tisa mwanamke aliyesimama mwisho kabisa na wote kwa pamoja walifyatua rocketi wakiwalenga majitu yale mawili
"FWOOOOSH...... BOOOOM... BOOOM. BOOOOM!!!"
TO BE CONTINUED........
SOLO KING: ANCIENT LEGACY
CHAPTER 41: Mtu anayepita tu
Makombora yote matatu kila moja lilikwenda kuwalipukia wale majitu watatu na kuishia kutoa ngurumo za maumivu iliyochanganyika na hasira lakini wangefanyaje? Wanajeshi wale hawakuwaachia hata nafasi ya kupumua walishambuliwa mfululizo na rocketi za mabomu, mabomu ya pini na kufyatuliwa bastola kana kwamba wapo vitani
"Tu tu tu tu tu tu!... Boom!.... Tu, tu, tu, tu... Boom! Boom!" zilikuwa ni sauti za risasi kufyatuliwa na mabomu kulipuka mfululizo
Miondoko yao ilikuwa ni ya kipekee sana, kama ni wataalamu basi walistahili kuitwa wataalamu haswa! Pngine kupewa hata tuzo za utaalamu wa matumizi ya siraha kijeshi. Kwa jinsi miondoko yao ilivyo na jinsi walivyokuwa wakishambulia kwa mpangilio maalumu hawakukosea kuiita mbinu hiyo "dance of survival"
Walikuwa wakishambulia na wakati huohuo kujilinda iwapo kutatokea la kutokea. Laiti Jimmy asingepatwa na upofu angevutiwa na jinsi walivyokuwa wakishambulia na mpaka wanakuja kumaliza risasi na mabomu ni vumbi pekee ndio lilikuwa likitamalaki eneo walilokuwepo kiasi kwamba ilikuwa ngumu kuona kwa macho kilicho mbele zaidi ya vumbi tu
Ni kana kwamba kulitokea dhoruba kubwa ya vumbi isababishwayo na upepo mkali na vumbi kufunika eneo lote walilokuwepo.
Kadri muda ulivyosonga vumbi lilianza kupotea na hatimae waliweza kuona vizuri, yale majitu yalikuwa chini hoi bin taaban. Ilionekana kabisa mapigo waliyopokea yalikuwa ni zaidi ya maumivu. Japokuwa hayakuweza kuwaua lakini yaliwajeruhi pakubwa sana na taratibu walianza kupungua vimo na kubadilika kutoka majitu kurudi kuwa binadamu wa kawaida huku wakitema damu nyingi mdomoni
Jimmy naye alionekana kurudi katika hali yake ya kawaida huku macho yake akiwa ameyafumba na sasa waliweza kugundua kwamba ilikuwa ni kweli jamaa hakuwa anaona, kwa maana hiyo Mia alikuwa sahihi
"Mnaonekana kukurupuka sana lakini sio mbaya kikubwa mmeweza kuwadhibiti hawa kunguni" aliongea Jimmy huku akitabasamu, ni kama vile kupatwa kwake kwa upofu lilikuwa jambo la kawaida
"Bro ni kweli huoni?" aliuliza Ben lakini Jimmy hakujibu zaidi ya kutoa tabasamu
"Acha kuuliza maswali ambayo majibu unayo" Freya alimwambia Ben
"Kwanza tumalizane na hawa kunguni mengine ndio yafuate" aliongea Jimmy na kuwasogelea wale watu kisha kuchuchumaa, yaani hata tembea yake haikuwa imebadilika ni kama vile hakuwa kipofu
"Hivi kweli haoni huyu?" aliuliza mzube mara baada ya kuona Jimmy ameweza kujua mahali walipo mabwana wale lakini hakuna aliyejibu zaidi ya kukaa kimya.
"Mna bahati sana nilitaka niwatoe utumbo lakini bahati mbaya wasamaria wema wameingilia hivyo chukulieni kama ukombozi kutoka mikononi mwa shetani" Jimmy aliongea na hakuwa anajali watamwamini au lah
"We.. wee mshe..n...zi usijion..e wa maana sana kisa tu umeweza kutud..hibit..i.. ni kwasababu u.." alikuwa akiongea kwa tabu sana, ilikuwa ni sauti ya yule bwana aliyebeba chungu hapo mwanzo lakini kabla hata hajamaliza kuongea aliishia kutoa mimacho na kupana mdomo lakini sauti haikuwa inamtoka
Jimmy alikuwa amemtoboa tumbo kwa mkono wake na kuuchomoa utumbo wake na kumuonyesha kabisa. Kilikuwa ni kitendo cha kikatili na kishetani kwelikweli.
"Sijakupa ruhusa ya kuongea wewe kunguni, siku zote kunguni ni kunguni tu, ni wadogo hawana cheo wala hadhi zaidi ya kuitwa kunguni tu. Nyinyi kunguni daima mnanyonya damu za wengine ili kuishi hamna thamani yoyote" aliongea na kuutupa ule utumbo pembeni
Bwana yule hakupata hata nafasi ya kumsikiliza mpaka mwisho kwani alikata roho palepale, damu nyingi zilikuwa zikimtoka kama bomba la maji, zilikuwa damu nyeusi zenye harufu mbaya kishenzi lakini Jimmy hakuonekana kujali sana harufu hiyo
Kamanda Rama na wengine pamoja na wale mabwana wawili waliobaki walihisi ubaridi ukisambaa kwenye uti wao wa mgongo na hogu kuwatawala bila kupenda. Hawakuelewa kwanini lakini walijikuta tu wakitawaliwa na hofu kiasi kwamba nywele ziliwasisimka na hakuna aliyedhubutu kufungua mdomo. Hakuwa yule Jimmy wa masaa kadhaa yaliyopita alikuwa mtu mwingine kabisa
"Mna kingine cha kuongea?" Jimmy aligeuza uso wake kwa wale wawili waliobaki na kuwauliza lakini hakuna hata aliyedhubutu kufungua kinywa chake, zaidi ya kutetemeka huku vijasho kuwatoka
"Hamna? sasa nisikie kunguni yeyote anaongea pumba na nataka mnijibu maswali yangu kwa ufasaha mmenisikia?" aliwauliza
Licha ya kwamba Jimmy alitoa kauli hiyo kwa mabwana wale lakini wenzake walihisi ni kama vile na wao kauli hiyo iliwahusu hasa ile sentensi ya" sasa nisikie kunguni yeyote anaongea pumba"
"Tutakwambia kila kitu lakini kwa mabadilishano ya kutuacha hai" aliongea mmoja kwa kutetemeka alikuwa ni yule ambaye hakubeba kitu hapo mwanzo
"Hahaha..hahahaha!!"Jimmy baada ya kusikia kauli hiyo alianza kucheka kwa sauti hafifu huku taratibu ikipanda na kuwa kubwa, alionekana ni kama kichaa fulani hivi
Sekunde ambayo anamaliza kuangua kicheko aliikamata shingo ya bwana yule kwa mkono uleule aliotumia kumchomoa utumbo mwenzao na kuibana koo kwa nguvu
Kutokana na maumivu makali yaliyosababishwa na mashambulizi ya siraha ya kijeshi hakuwa hata na nguvu ya kunyanyua mkono hivyo alibaki kuteseka ndani kwa ndani akikosa pumzi bila kufanya chochote zaidi ya macho kuwa mekundu na machozi kumtoka
"Nimekupa ruhusa ya kuongea? Nani kakwambia kwamba mimi ni mfanya biashara? Sikia we kunguni mimi sio mfanya biashara na sipo hapa kufanya barter trade, kwangu mimi sijali kama utakuwa hai au lah, uniambie au usiniambie mimi sitopungukiwa na kitu nadhani hujui mimi ni nani. Ngoja nikwambie" aliongea huku akiendelea kuibana shingo ya bwana yule
"I am a man of many indentities but my most honest indentity is 'a man passing by' I ain't a hero nor a devil, I am the wind that cuts through the night, the shadow that comes and goes I don't care whether you die or live because your fate is yours alone. I carry no burden of mercy, no chains of pity
You are nothing but a stepping stone on my path a speck of dust, just like every other man who crossed my way. Whether you beg or scream or curse me, I don’t care. I just pass by, I move on, and life goes on.” aliongea kwa sauti ya kawaida lakini iliyosikika vyema kwenye kila sikio lililoko eneo hilo akimaanisha
"Mimi ni mtu mwenye nyuso nyingi, lakini utambulisho wangu wa kweli ni mtu anayepita tu. Mimi sio shujaa, wala sio shetani, mimi ni upepo unaopita usiku, kivuli kinachokuja na kuondoka. Sijali kama utakufa au kuishi, kwa sababu hatima yako ni yako mwenyewe, sibebi mzigo wa huruma wala sina huruma.
Wewe si kitu zaidi ya jiwe nalokanyaga kwenye njia zangu, chembe za vumbi kama wengineo tu waliokatiza mbele yangu, omba sana, piga kelele, nilaani mimi sijali, mi napita tu, nasahau na maisha yanaendelea"
Itoshe kusema yalikuwa ni maneno yenye kuvuruga hisia za kila mmojawapo aliyeko mahali hapo na mpaka anamaliza kuongea bwana yule alikuwa ameshakata roho tayari na kumuacha shingo
""Nadhani wewe ndiye uliyenisababishia upofu huu si ndio?" aliongea lakini bwana yule aliyesalia hai hakuthubutu kufungua kinywa zaidi ya kutingisha kichwa, nguvu ya kuongea anaipata wapi kwa mfano? Licha ya Jimmy kuwa na sura ya kimalaika lakini vitendo alivyokuwa akifanya ni shetani mtupu
"Safi" jimmy alijibu baada ya bwana yule kutingisha kichwa ni kana kwamba amemuona akitingisha kichwa
"Sasa nataka kusikia ndio na hapana, tofauti na kauli hizo napasua pumbu" aliongea akiwa siriaz kiwango cha kimataifa
"Je miaka zaidi ya tano iliyopita ni nyinyi mliohusika na wanywa damu waliokuwa wakiua raia nchini?"
"Hapana"
"Unanidanganya?"
"Hapana?"
"Unataka kuniambia kwamba hamkuhusika?"
Ndio"
"Na kwamba wahusika ni wengine?"
"Ndio"
"Kwa maana hiyo mpo wengi si ndio?"
"Ndio"
"Je wenzako bado wako nchini?"
"Hapana"
Ulikuwa ni mwendo wa maswali na majibu ya ndio na hapana mpaka Jimmy ananyamanza kwa sekunde kadhaa
"Safi una adabu sana, nimependa! Aya nataka maelezo yaliyonyooka kuhusu wanywa damu"
"Kuhusu wanywa damu ni binadamu ambao tunawateka na kuzitoa nafsi zao kisha kuingiza nafsi za viumbe ambao hutegemea damu kuishi, ndio maana licha ya kuwa na maumbo ya binadamu lakini tabia ni tofauti na uhalisia wa binadamu ni rahisi kusema si binadamu tena bali ni mashetani waliovaa sura za binadamu." bwana yule alieleza kwa ufupi lakini yaliyonyooka
"Kuna namna yoyote ya kurudisha nafsi za binadamu kwenye miili yao?" aliuliza kamanda Rama
"Hapana kwasababu nafsi zao si hai tena" alijibu na Jimmy alishaelewa kwani nafsi zilizotekwa za binadamu zikinyonywa, umejuaje? Ni ile hisia ya ndani 'power of intuition'
'Hata kama zingekuwa hai bado isingewezekana chukulia mfano wa bastola na ili bastola ifanye kazi inahitajika magazini na risasi, chukulia magazini ni roho ya mwanadamu na risasi ni nafsi halafu bastola ni mwili. Risasi ikishafyatuliwa hakuna uwezekano wa kuirudisha tena labda uchukue risasi mpya ambayo haijatumika. Vivyo hivyo kwa nafsi, nafsi ikishatolewa kwenye mwili husika hakuna namna ya kuirudisha unajua kwanini?"aliongea Jimmy na kila mtu alitingisha kichwa kutokujua isipokuwa Mia ambaye alijibu
"Ni kwasababu nafsi si kitu kinachoweza kuhifadhiwa kwenye kopo au mfuko, haiwezi kushikika wala kuonekana kwa macho. Nafsi ni kiini cha maisha, ni mwanga wa uhai. Ikitoka mwilini, haikimbii tu kama ndege inafungamanishwa na kanuni za ulimwengu ambazo haziruhusu kurudi tena "
"Exactly Mia unaonekana kujua mengi ni kama kujaribu kuunganisha kioo kilichovunjika vipande elfu moja. Hata ukiviunganisha, hakitarudi kuwa kile kioo cha mwanzo kitakuwa kimepoteza thamani na kiini chake cha kwanza chukulia mfano wa moto, unapowasha moto na ukazima, moshi wake unapaa na kupeperushwa na upepo si ndio? . Unaweza kuupata tena? Hapana. moto unaweza kuwashwa tena, lakini moshi ule ule huwezi kuurudisha. Vivyo hivyo kwa nafsi, ikitolewa au kunyonywa, imepotea milele, no turning back!" aliendelea kuongea ni kama vile mwalimu anayewafundisha wanafunzi darasani
"Kwahiyo zile nafsi zilizotekwa zimenyonywa? Na ndio sababu ya hawa washenzi kubadilika na kuwa majitu?" aliuliza Caren
"Yeab, nafsi ya binadamu inaponyonywa na waseng* kama hawa hubadilishwa kuwa sehemu yao, wanaitumia kama nguvu yao ya kuishi na kuimarika. Kwa hivyo, nafsi hiyo huangukia chini ya nguvu za giza, kama kinyesi kilichogeuzwa mbolea. Nafsi hiyo haingekuwa tena safi au huru inakuwa imepoteza utu wake na heshima yake. hata kama tukijaribu kuirudisha, tungekuwa tunarudisha kitu ambacho hakina thamani tena. Nafsi hiyo inakuwa na sumu ya uovu, na mwili usingeweza kuipokea. Ingekuwa ni kama kutia sumu kwenye maji safi, kingine mikli yao imeshakufa na roho kuwatoka” Jimmy alimjibu kwa kirefu
"Kitu pekee ni kuziombea tu nafsi zilizopotea, be it buddha, Jesus or Allah whoever you believe in just pray for them folks" jimmy aliongea kisha kusimama
"Kamanda una swali lolote la kutaka kumuuliza huyu kunguni?"
"Nataka kujua hapa wapi?"
"Umesikia wewe kunguni toa maelezo!" Ben aliropoka
"Huu ni ulimwengu wa utupu, ulimwengu ambao ni jangwa tupu, hakuna mwezi, hakuna jua wala nyota kifupi hakuna chochote zaidi ya anga na mchanga" aliongea Bwana yule
"Kumbe ulimwengu wa utupu ndio uko hivi?" alijiwazia Jimmy, ni kama vile amewahi kuusikia au kuusoma mahali
"Agenda yenu ni ipi kuingia ndani ya huu ulimwengu?" Joshua aliuliza
"Ushasikia ni ulimwengu wa utupu sasa kuna agenda gani itakayofanyika sehemu ya utupu? Ukizunguka huku na kule hakuna utakachokutana nacho zaidi ya upepo unaosafiri kama mpumbavu asiye na malengo" Jimmy alijibu kisha kuchuchumaa tena chini uso wake ukitazamana na uso wa bwana yule aliyetawaliwa na hofu isiyo na kifani
"Hey usiniambie mlikuwa hapa kutafuta hazina" aliongea Jimmy
"Hazina? Kuna hazina humu? Ni ipi hiyo?" aliuliza Freya fululizo
"Inasemekana kuna hazina ambayo ina nguvu kubwa sana iliyofichwa kwenye ulimwengu huu hapo kale na mmiliki wake akihofia kuanguka kwenye mikono ya watu wabaya, well who believe this bullshit?" aliongea Jimmy
"Ninaamini" alijibu Mzube
"Kwahiyo kama unaamini ndo tuseme unataka kuitafuta na wewe?" Jimmy aliongea kwa masikitiko
"Hii dunia haitoishiwa na wapumbavu" alimalizia na kauli yake ilimtia hasira Mzube
"We dogo! kwasababu tulikusaidia kipindi kile sasahivi ndio unajikuta mjuaji sana, unadhani kama tusingefika kukusaidia kipindi kile leo hii ungekuwa hapa ukinitukana?" Mzube aliongea kwa hasira
"No hard feelings!" aliongea Jimmy
"Halafu sio kama nimekutukana na pia sijakosea bali ni ukweli kwamba hii dunia kuna wapumbavu wanaibuka kila siku" aliendelea kukazia
"Nikuulize swali labda, unajua hiyo hazina ni hazina gani?" aliuliza na Mzube aliishia kujing'atang:ata mdomo
“Unaona sasa! Hujui ni hazina gani na inapatikana wapi zaidi ya kuamini upuuzi wa mpumbavu mwenzio. Sasa unajiona una utofauti gani naye? Sikulaumu kwa kuamini, isitoshe imani ni suala la kuchagua, lakini kuamini kitu bila kufikiria mara mbili-mbili, huo ni upumbavu wa hali ya juu.
Halafu neno mpumbavu sio tusi bali ni utambulisho wa mtu yoyote ambaye kichwani mwake kumejaa pumba tu, kilichoongezwa ni neno "vu" ambacho ni kivumishi. kinachoashiria hali ya mtu huyo asiye na uelewa wala fikra timamu.
Mpumbavu hakosi kuwa na macho lakini haoni, ana masikio lakini hasikii, hana akili lakini hajui kwamba hana. Anaamini kila kitu kama vile mzizi wa ndizi unavyonyonya maji, bila hata kujua yupo wapi au anatoka wapi.
Wewe ni binadamu mwenye uwezo wa kufikiri, usikubali kuamini kila kitu kama punda anayeamini nyasi ni chakula bila kuhoji ubora wake. Fikiria, tafakari, jadili, halafu uchague. Usikubali upuuzi wa mpumbavu kuwa mwanga wako; kwani mwanga wa mpumbavu ni sawa na giza nene lisilo na mwisho. Ndio maana nikasema, imani ni jambo la kuchagua lakini kufikiri kabla ya kuamini ndilo linatofautisha mpumbavu na mwenye hekima"
TO BE CONTINUED..........
SOLO KING: ANCIENT LEGACY
CHAPTER 41: Mtu anayepita tu
Makombora yote matatu kila moja lilikwenda kuwalipukia wale majitu watatu na kuishia kutoa ngurumo za maumivu iliyochanganyika na hasira lakini wangefanyaje? Wanajeshi wale hawakuwaachia hata nafasi ya kupumua walishambuliwa mfululizo na rocketi za mabomu, mabomu ya pini na kufyatuliwa bastola kana kwamba wapo vitani
"Tu tu tu tu tu tu!... Boom!.... Tu, tu, tu, tu... Boom! Boom!" zilikuwa ni sauti za risasi kufyatuliwa na mabomu kulipuka mfululizo
Miondoko yao ilikuwa ni ya kipekee sana, kama ni wataalamu basi walistahili kuitwa wataalamu haswa! Pngine kupewa hata tuzo za utaalamu wa matumizi ya siraha kijeshi. Kwa jinsi miondoko yao ilivyo na jinsi walivyokuwa wakishambulia kwa mpangilio maalumu hawakukosea kuiita mbinu hiyo "dance of survival"
Walikuwa wakishambulia na wakati huohuo kujilinda iwapo kutatokea la kutokea. Laiti Jimmy asingepatwa na upofu angevutiwa na jinsi walivyokuwa wakishambulia na mpaka wanakuja kumaliza risasi na mabomu ni vumbi pekee ndio lilikuwa likitamalaki eneo walilokuwepo kiasi kwamba ilikuwa ngumu kuona kwa macho kilicho mbele zaidi ya vumbi tu
Ni kana kwamba kulitokea dhoruba kubwa ya vumbi isababishwayo na upepo mkali na vumbi kufunika eneo lote walilokuwepo.
Kadri muda ulivyosonga vumbi lilianza kupotea na hatimae waliweza kuona vizuri, yale majitu yalikuwa chini hoi bin taaban. Ilionekana kabisa mapigo waliyopokea yalikuwa ni zaidi ya maumivu. Japokuwa hayakuweza kuwaua lakini yaliwajeruhi pakubwa sana na taratibu walianza kupungua vimo na kubadilika kutoka majitu kurudi kuwa binadamu wa kawaida huku wakitema damu nyingi mdomoni
Jimmy naye alionekana kurudi katika hali yake ya kawaida huku macho yake akiwa ameyafumba na sasa waliweza kugundua kwamba ilikuwa ni kweli jamaa hakuwa anaona, kwa maana hiyo Mia alikuwa sahihi
"Mnaonekana kukurupuka sana lakini sio mbaya kikubwa mmeweza kuwadhibiti hawa kunguni" aliongea Jimmy huku akitabasamu, ni kama vile kupatwa kwake kwa upofu lilikuwa jambo la kawaida
"Bro ni kweli huoni?" aliuliza Ben lakini Jimmy hakujibu zaidi ya kutoa tabasamu
"Acha kuuliza maswali ambayo majibu unayo" Freya alimwambia Ben
"Kwanza tumalizane na hawa kunguni mengine ndio yafuate" aliongea Jimmy na kuwasogelea wale watu kisha kuchuchumaa, yaani hata tembea yake haikuwa imebadilika ni kama vile hakuwa kipofu
"Hivi kweli haoni huyu?" aliuliza mzube mara baada ya kuona Jimmy ameweza kujua mahali walipo mabwana wale lakini hakuna aliyejibu zaidi ya kukaa kimya.
"Mna bahati sana nilitaka niwatoe utumbo lakini bahati mbaya wasamaria wema wameingilia hivyo chukulieni kama ukombozi kutoka mikononi mwa shetani" Jimmy aliongea na hakuwa anajali watamwamini au lah
"We.. wee mshe..n...zi usijion..e wa maana sana kisa tu umeweza kutud..hibit..i.. ni kwasababu u.." alikuwa akiongea kwa tabu sana, ilikuwa ni sauti ya yule bwana aliyebeba chungu hapo mwanzo lakini kabla hata hajamaliza kuongea aliishia kutoa mimacho na kupana mdomo lakini sauti haikuwa inamtoka
Jimmy alikuwa amemtoboa tumbo kwa mkono wake na kuuchomoa utumbo wake na kumuonyesha kabisa. Kilikuwa ni kitendo cha kikatili na kishetani kwelikweli.
"Sijakupa ruhusa ya kuongea wewe kunguni, siku zote kunguni ni kunguni tu, ni wadogo hawana cheo wala hadhi zaidi ya kuitwa kunguni tu. Nyinyi kunguni daima mnanyonya damu za wengine ili kuishi hamna thamani yoyote" aliongea na kuutupa ule utumbo pembeni
Bwana yule hakupata hata nafasi ya kumsikiliza mpaka mwisho kwani alikata roho palepale, damu nyingi zilikuwa zikimtoka kama bomba la maji, zilikuwa damu nyeusi zenye harufu mbaya kishenzi lakini Jimmy hakuonekana kujali sana harufu hiyo
Kamanda Rama na wengine pamoja na wale mabwana wawili waliobaki walihisi ubaridi ukisambaa kwenye uti wao wa mgongo na hogu kuwatawala bila kupenda. Hawakuelewa kwanini lakini walijikuta tu wakitawaliwa na hofu kiasi kwamba nywele ziliwasisimka na hakuna aliyedhubutu kufungua mdomo. Hakuwa yule Jimmy wa masaa kadhaa yaliyopita alikuwa mtu mwingine kabisa
"Mna kingine cha kuongea?" Jimmy aligeuza uso wake kwa wale wawili waliobaki na kuwauliza lakini hakuna hata aliyedhubutu kufungua kinywa chake, zaidi ya kutetemeka huku vijasho kuwatoka
"Hamna? sasa nisikie kunguni yeyote anaongea pumba na nataka mnijibu maswali yangu kwa ufasaha mmenisikia?" aliwauliza
Licha ya kwamba Jimmy alitoa kauli hiyo kwa mabwana wale lakini wenzake walihisi ni kama vile na wao kauli hiyo iliwahusu hasa ile sentensi ya" sasa nisikie kunguni yeyote anaongea pumba"
"Tutakwambia kila kitu lakini kwa mabadilishano ya kutuacha hai" aliongea mmoja kwa kutetemeka alikuwa ni yule ambaye hakubeba kitu hapo mwanzo
"Hahaha..hahahaha!!"Jimmy baada ya kusikia kauli hiyo alianza kucheka kwa sauti hafifu huku taratibu ikipanda na kuwa kubwa, alionekana ni kama kichaa fulani hivi
Sekunde ambayo anamaliza kuangua kicheko aliikamata shingo ya bwana yule kwa mkono uleule aliotumia kumchomoa utumbo mwenzao na kuibana koo kwa nguvu
Kutokana na maumivu makali yaliyosababishwa na mashambulizi ya siraha ya kijeshi hakuwa hata na nguvu ya kunyanyua mkono hivyo alibaki kuteseka ndani kwa ndani akikosa pumzi bila kufanya chochote zaidi ya macho kuwa mekundu na machozi kumtoka
"Nimekupa ruhusa ya kuongea? Nani kakwambia kwamba mimi ni mfanya biashara? Sikia we kunguni mimi sio mfanya biashara na sipo hapa kufanya barter trade, kwangu mimi sijali kama utakuwa hai au lah, uniambie au usiniambie mimi sitopungukiwa na kitu nadhani hujui mimi ni nani. Ngoja nikwambie" aliongea huku akiendelea kuibana shingo ya bwana yule
"I am a man of many indentities but my most honest indentity is 'a man passing by' I ain't a hero nor a devil, I am the wind that cuts through the night, the shadow that comes and goes I don't care whether you die or live because your fate is yours alone. I carry no burden of mercy, no chains of pity
You are nothing but a stepping stone on my path a speck of dust, just like every other man who crossed my way. Whether you beg or scream or curse me, I don’t care. I just pass by, I move on, and life goes on.” aliongea kwa sauti ya kawaida lakini iliyosikika vyema kwenye kila sikio lililoko eneo hilo akimaanisha
"Mimi ni mtu mwenye nyuso nyingi, lakini utambulisho wangu wa kweli ni mtu anayepita tu. Mimi sio shujaa, wala sio shetani, mimi ni upepo unaopita usiku, kivuli kinachokuja na kuondoka. Sijali kama utakufa au kuishi, kwa sababu hatima yako ni yako mwenyewe, sibebi mzigo wa huruma wala sina huruma.
Wewe si kitu zaidi ya jiwe nalokanyaga kwenye njia zangu, chembe za vumbi kama wengineo tu waliokatiza mbele yangu, omba sana, piga kelele, nilaani mimi sijali, mi napita tu, nasahau na maisha yanaendelea"
Itoshe kusema yalikuwa ni maneno yenye kuvuruga hisia za kila mmojawapo aliyeko mahali hapo na mpaka anamaliza kuongea bwana yule alikuwa ameshakata roho tayari na kumuacha shingo
""Nadhani wewe ndiye uliyenisababishia upofu huu si ndio?" aliongea lakini bwana yule aliyesalia hai hakuthubutu kufungua kinywa zaidi ya kutingisha kichwa, nguvu ya kuongea anaipata wapi kwa mfano? Licha ya Jimmy kuwa na sura ya kimalaika lakini vitendo alivyokuwa akifanya ni shetani mtupu
"Safi" jimmy alijibu baada ya bwana yule kutingisha kichwa ni kana kwamba amemuona akitingisha kichwa
"Sasa nataka kusikia ndio na hapana, tofauti na kauli hizo napasua pumbu" aliongea akiwa siriaz kiwango cha kimataifa
"Je miaka zaidi ya tano iliyopita ni nyinyi mliohusika na wanywa damu waliokuwa wakiua raia nchini?"
"Hapana"
"Unanidanganya?"
"Hapana?"
"Unataka kuniambia kwamba hamkuhusika?"
Ndio"
"Na kwamba wahusika ni wengine?"
"Ndio"
"Kwa maana hiyo mpo wengi si ndio?"
"Ndio"
"Je wenzako bado wako nchini?"
"Hapana"
Ulikuwa ni mwendo wa maswali na majibu ya ndio na hapana mpaka Jimmy ananyamanza kwa sekunde kadhaa
"Safi una adabu sana, nimependa! Aya nataka maelezo yaliyonyooka kuhusu wanywa damu"
"Kuhusu wanywa damu ni binadamu ambao tunawateka na kuzitoa nafsi zao kisha kuingiza nafsi za viumbe ambao hutegemea damu kuishi, ndio maana licha ya kuwa na maumbo ya binadamu lakini tabia ni tofauti na uhalisia wa binadamu ni rahisi kusema si binadamu tena bali ni mashetani waliovaa sura za binadamu." bwana yule alieleza kwa ufupi lakini yaliyonyooka
"Kuna namna yoyote ya kurudisha nafsi za binadamu kwenye miili yao?" aliuliza kamanda Rama
"Hapana kwasababu nafsi zao si hai tena" alijibu na Jimmy alishaelewa kwani nafsi zilizotekwa za binadamu zikinyonywa, umejuaje? Ni ile hisia ya ndani 'power of intuition'
'Hata kama zingekuwa hai bado isingewezekana chukulia mfano wa bastola na ili bastola ifanye kazi inahitajika magazini na risasi, chukulia magazini ni roho ya mwanadamu na risasi ni nafsi halafu bastola ni mwili. Risasi ikishafyatuliwa hakuna uwezekano wa kuirudisha tena labda uchukue risasi mpya ambayo haijatumika. Vivyo hivyo kwa nafsi, nafsi ikishatolewa kwenye mwili husika hakuna namna ya kuirudisha unajua kwanini?"aliongea Jimmy na kila mtu alitingisha kichwa kutokujua isipokuwa Mia ambaye alijibu
"Ni kwasababu nafsi si kitu kinachoweza kuhifadhiwa kwenye kopo au mfuko, haiwezi kushikika wala kuonekana kwa macho. Nafsi ni kiini cha maisha, ni mwanga wa uhai. Ikitoka mwilini, haikimbii tu kama ndege inafungamanishwa na kanuni za ulimwengu ambazo haziruhusu kurudi tena "
"Exactly Mia unaonekana kujua mengi ni kama kujaribu kuunganisha kioo kilichovunjika vipande elfu moja. Hata ukiviunganisha, hakitarudi kuwa kile kioo cha mwanzo kitakuwa kimepoteza thamani na kiini chake cha kwanza chukulia mfano wa moto, unapowasha moto na ukazima, moshi wake unapaa na kupeperushwa na upepo si ndio? . Unaweza kuupata tena? Hapana. moto unaweza kuwashwa tena, lakini moshi ule ule huwezi kuurudisha. Vivyo hivyo kwa nafsi, ikitolewa au kunyonywa, imepotea milele, no turning back!" aliendelea kuongea ni kama vile mwalimu anayewafundisha wanafunzi darasani
"Kwahiyo zile nafsi zilizotekwa zimenyonywa? Na ndio sababu ya hawa washenzi kubadilika na kuwa majitu?" aliuliza Caren
"Yeab, nafsi ya binadamu inaponyonywa na waseng* kama hawa hubadilishwa kuwa sehemu yao, wanaitumia kama nguvu yao ya kuishi na kuimarika. Kwa hivyo, nafsi hiyo huangukia chini ya nguvu za giza, kama kinyesi kilichogeuzwa mbolea. Nafsi hiyo haingekuwa tena safi au huru inakuwa imepoteza utu wake na heshima yake. hata kama tukijaribu kuirudisha, tungekuwa tunarudisha kitu ambacho hakina thamani tena. Nafsi hiyo inakuwa na sumu ya uovu, na mwili usingeweza kuipokea. Ingekuwa ni kama kutia sumu kwenye maji safi, kingine mikli yao imeshakufa na roho kuwatoka” Jimmy alimjibu kwa kirefu
"Kitu pekee ni kuziombea tu nafsi zilizopotea, be it buddha, Jesus or Allah whoever you believe in just pray for them folks" jimmy aliongea kisha kusimama
"Kamanda una swali lolote la kutaka kumuuliza huyu kunguni?"
"Nataka kujua hapa wapi?"
"Umesikia wewe kunguni toa maelezo!" Ben aliropoka
"Huu ni ulimwengu wa utupu, ulimwengu ambao ni jangwa tupu, hakuna mwezi, hakuna jua wala nyota kifupi hakuna chochote zaidi ya anga na mchanga" aliongea Bwana yule
"Kumbe ulimwengu wa utupu ndio uko hivi?" alijiwazia Jimmy, ni kama vile amewahi kuusikia au kuusoma mahali
"Agenda yenu ni ipi kuingia ndani ya huu ulimwengu?" Joshua aliuliza
"Ushasikia ni ulimwengu wa utupu sasa kuna agenda gani itakayofanyika sehemu ya utupu? Ukizunguka huku na kule hakuna utakachokutana nacho zaidi ya upepo unaosafiri kama mpumbavu asiye na malengo" Jimmy alijibu kisha kuchuchumaa tena chini uso wake ukitazamana na uso wa bwana yule aliyetawaliwa na hofu isiyo na kifani
"Hey usiniambie mlikuwa hapa kutafuta hazina" aliongea Jimmy
"Hazina? Kuna hazina humu? Ni ipi hiyo?" aliuliza Freya fululizo
"Inasemekana kuna hazina ambayo ina nguvu kubwa sana iliyofichwa kwenye ulimwengu huu hapo kale na mmiliki wake akihofia kuanguka kwenye mikono ya watu wabaya, well who believe this bullshit?" aliongea Jimmy
"Ninaamini" alijibu Mzube
"Kwahiyo kama unaamini ndo tuseme unataka kuitafuta na wewe?" Jimmy aliongea kwa masikitiko
"Hii dunia haitoishiwa na wapumbavu" alimalizia na kauli yake ilimtia hasira Mzube
"We dogo! kwasababu tulikusaidia kipindi kile sasahivi ndio unajikuta mjuaji sana, unadhani kama tusingefika kukusaidia kipindi kile leo hii ungekuwa hapa ukinitukana?" Mzube aliongea kwa hasira
"No hard feelings!" aliongea Jimmy
"Halafu sio kama nimekutukana na pia sijakosea bali ni ukweli kwamba hii dunia kuna wapumbavu wanaibuka kila siku" aliendelea kukazia
"Nikuulize swali labda, unajua hiyo hazina ni hazina gani?" aliuliza na Mzube aliishia kujing'atang:ata mdomo
“Unaona sasa! Hujui ni hazina gani na inapatikana wapi zaidi ya kuamini upuuzi wa mpumbavu mwenzio. Sasa unajiona una utofauti gani naye? Sikulaumu kwa kuamini, isitoshe imani ni suala la kuchagua, lakini kuamini kitu bila kufikiria mara mbili-mbili, huo ni upumbavu wa hali ya juu.
Halafu neno mpumbavu sio tusi bali ni utambulisho wa mtu yoyote ambaye kichwani mwake kumejaa pumba tu, kilichoongezwa ni neno "vu" ambacho ni kivumishi. kinachoashiria hali ya mtu huyo asiye na uelewa wala fikra timamu.
Mpumbavu hakosi kuwa na macho lakini haoni, ana masikio lakini hasikii, hana akili lakini hajui kwamba hana. Anaamini kila kitu kama vile mzizi wa ndizi unavyonyonya maji, bila hata kujua yupo wapi au anatoka wapi.
Wewe ni binadamu mwenye uwezo wa kufikiri, usikubali kuamini kila kitu kama punda anayeamini nyasi ni chakula bila kuhoji ubora wake. Fikiria, tafakari, jadili, halafu uchague. Usikubali upuuzi wa mpumbavu kuwa mwanga wako; kwani mwanga wa mpumbavu ni sawa na giza nene lisilo na mwisho. Ndio maana nikasema, imani ni jambo la kuchagua lakini kufikiri kabla ya kuamini ndilo linatofautisha mpumbavu na mwenye hekima"
TO BE CONTINUED..........