Samuel jk_Euphoria
Member
- Apr 18, 2025
- 85
- 220
- Thread starter
- #121
SOLO KING: ANCIENT LEGACY
CHAPTER 30: Ugeni uliotarajiwa (expected visit)
Jimmy hisia zake zilikuwa ni sahihi kwani ndani ya sekunde kadhaa ulisikika mlio wa kengele ya mlango wa kuingia sebuleni kuashiria kwamba kuna ugeni muda huo
Aisha alinyanyuka na kwenda kufungua mlango na kuwaona watu wawili wamesimama mlangoni mmoja akwa ni mwanaume mwigine akiwa ni mwanamke. Mwanaume alionekana ni mkubwa kiumri huku mwanamke akiwa ni kijana zaidi
Wageni hao walikuwa wamevaa mavazi ya kawaida, mwanaume ambaye alikuwa ni kamanda Ramadhan alivalia t-shirt rangi ya zambsrau ambayo ilionekana kumbana kwa kiasi chake huku kifua chake na misuli ya mazoezi ikijichora, chini alivalia suruali nyeusi iliyombana na buti za kijeshi nyeusi zilizong'aa kana kwamba zimepakwa mafuta
Upande wa mwanamke alikuwa na asili ya kihabeshi na hakuwa mwingine bali ni Caren, naye alipendeza licha ya kuvalia kawaida kutokana na umbo lake matata. Chuchu saa sita za mrembo huyo zilionkana kusimama haswaa licha ya kuvalia shati kubwa la draft, rangi ya bluu lenye mikono mirefu, pia chini alivaa jinsi nyeusi iliyombana vyema na kuchora hipsi zake pamoja na mzigo wa wastani ulioko nyuma, bila kusahau buti nyeusi pia za doc matterns
"Karibuni ndani" Aisha aliwakaribisha na waliweza kuingia ndani.
"Msiishie kusimama tu hapo karibuni mpate kifungua kinywa haipendezi kwa wageni kula harufu ya misosi" aliongea Jimmy baada ya kuona wanaelekea kukaa sofani
Kama Rama na, Caren mara baada ya kusikia kauli hiyo kutoka kwa Jimmy walitabasamu na kuelekea mezani walikokaribishwa
"Ni wageni wako hawa?" Bianca aliumuuliza na Jimmy alitingisha jichwa kukubali
"Mbona hukutuambia kama una wageni asubuhi hii tuandae chakula cha kutosha" Bianca aliongea
"Usiwaze sana mummy watakunywa chai tu mimi mwenyewe sikutegemea ujio wao" Jimmy aliongea na alipomaliza kauli hiyo wageni waliweza kufika mezani na Bianca alinyanyuka kuwasalimia kwa heshima huku akiwapa tabasamu la kirafiki
"Miss lina sisi ndio tunapaswa kutoa heshima na kuomba radhi kwa ujio wa ghafla" aliongea Caren akimpa tabasamu
"Je haimpasi mke wangu kukaribisha wageni kwa heshima mahali pangu?" Jimmy aliongea
"Unanifahamu!" Bianca aliuliza kirafiki
"Kwa umaarufu ulio nao nani asikujue, mimi ni mmoja kati ya shabiki zako" alijibu Caren
"Haha! am humbled! Karibuni ten " Bianca aliwakaribisha kwa mara nyingine na walipokea ukaribisho
Aliwawekea juisi ya matunda kwenye glasi na vitafunwa baadhi kisha kwa kujiongeza yeye pamoja na vijakazi wa nyumba yake waliondoka kwa kisingizio cha kushiba kuwaachia 'privacy'
"Sikudhania kama utakuwa na mke mwenye kujiongeza haha" aliongea kamanda Rama huku akijichekesha
"Anyway sisi ni watu wazima haina haja ya kuzunguka nianze kujitambulisha mimi ni Ramadhan Suleiman Sudi na huyu hapa ni Caren nadhani mlishakutana"
"Ndio miaka mitanobiliyopita.. Hey long time no see!" aliongea Jimmy na kumpa ishara ya kirafiki Caren, naye Caren alirudisha kwa tabasamu la kirafiki
"Mimi ndiye mkuu wa kitengo cha Hidden Supremacy na lengo la kuja hapa ni kutaka....."
"Usiniambie unataka nijiunge kwenye hilo kundi lenu"
"Hilo lilikuwa ni kusudi langu la kwanza lakini nimebadili maamuzi"
"Ooh ni vizuri umebadili maamuzi maana hata kama usingebadili nisingekubali, unaonaje ukaniambia kilichokufanya ubadili maamuzi?"
"Mwanzoni nilidhani utakuwa ni mtaalamu uliyebobea kwenye mapigano kutokana na taarifa niliyopata kwa Caren na mimi huwa napenda kuendeleza vipaji kanma hivyo, na tulipofanya uchaguzi kuhusu wewe nikaja kugundua kwamba unafahamika sana katika ulimwengu wa kihalifu, of course ilikuwa ni taarifa nzuri sana kwa upande wetu na kupata sababu nzuri ya kukufanya uingie kundini hata kama hutaki" aliongea kamanda Rama na kunyanyua glasi yake ya juisi na kuigida yote kama maji
Jimmy alikuwa akimtazama tu huyo kamanda mweusi tii akisubiri muendelezo wa simulizi yake fupi, alijiambia hajawahi kukutana na binadsamu mweusi kama hiyo tangu azaliwe, aliwaza mbali na kudhani pengine wanawake aliokuwa nao wameondoka kwa sababu ya sura yake ngumu na weusi tii
"Lakini ulipotea kwa miaka mitano bila ya kujulikana ulikopotelea" alimalizia
"Kwahiyo kupotea kwangu ndio sababu ya wewe kubadili uamuzi?"
"Hapana"
"Sababu ni ipi?" Jimmy aliuliza akimkazia macho kusubiri jibu
"Tuachane na sababu lengo langu sio kuelezea sababu nimekuja hapa kuomba ushirikiano" aliongea kisha kunyamanza
"Ushirikiano wa nini kamanda mbona unaongea kwa mkato kwanini usitamke hotuba yote kuliko kuniambia kidogo kidogo"
"Nadhani utakuwa unajua kuhusu hivi viumbe vya ajabu ajabu vinavyotesa raia"
"Ndio ni vichaa tu waliopoteza ubinadamu" aliongea Jimmy
"Vyovyote vile tunataka kuwaondoa iliraia waishi kwa amani"
"Sasa mimi nahusikaje kwenye mpango wenu wa kutaka kuwaondoa?"
"Tunataka ushirikiane nasi kwenye huu mpango"
""Nini kinawafanya mdhani labda nitakubali na ninaweza kusaidia? "
" Ukweli uwezo wa kusaidia unao kuhusu wewe kukubali ni ombi letu, chukulia unaweka akiba ya msaada kwetu ukikubali na kutusaidia kwenye huu mpango kama una lolote utakalo ambalo tunaweza kukusaidia tutafanya hivyo"
"Mkuu mbona unanifanya mbuzi wa kafara? mimi ni binadamu tu wa kawaida sasa kutaka mimi kwenda kupambana na hao mashetani ni sawa na kunitoa kafara maana hatujui nini kitajiri, vipi mpango ukishindikana?"
"Ukijiunga nasi hauwezi kusgindwa!"
"Hahaha! Inashangaza sana hatujuani lakini unaniamini kupitiliza, au kwasababu ya kunifuatilia?"
"Kwahiyo ulikuwa unajua nakufatilia lakini ukaamua kujifanya, kwanini?" aliongea kamanda Rama, sio kama hakujua ameshtukiwa bali alitaka sababu
Ukweli Jimmy tangu ile siku alipodili na wale wahuni waliotumwa kumvunja miguu aliweza kugundua anafuariliwa lakini aliamua kujifanya kutoshtukia
" Kwasababu haukuwa na nia mbaya juu yangu" alijibu
"Unajuaje kama hakuwa na nia mbaya, inawezekanaje mtu kujua nia ya mwenzake?" Caren aliuliza
"Aura!" Jimmy alimjibu na kumfanya Kamanda Rama kutabasamu
"Aura anayosambaza muhusika hiubadilika kutokana na hisia na matendo, ni kama harufu ya mvua kabla haijanyesha. Mfano, mtu anayetaka kukuua, husambaza hisia flani zisizo za kawaida. Mapigo ya moyo wako hubadilika, na hata hewa inayokuzunguka huhisi kuwa nzito… kama kiza kinachofunika mwanga taratibu" aliongea na kunyamanza kidogo
"It’s like a feeling of something brushing against your soul" aliendelea akimaanisha "ni kama hisia flani ya kitu kinachogusa nafsi yako"
"Sawa tuseme Aura lakini uliwezaje kujua ni Kamanda Rama na si mwingine?" Caren aliuliza swali jingine
"Unauliza swali ambalo jibu unalo, jibu ni msisimko wa nguvu za kiroho anaotoa, ukweli sikujua kama ni kamanda wako zaidi ya kujua tu kuna mtu ananifatilia nimejua ni kamanda wako sababu msisimko wake naouhisi hauna tofauti na yule aliyekuwa akinifuatiliwa" Jimmy aliongea na kumgeukia kamanda Rama
"Ulifanya makusudi nikugundue si ndio? Ili ukija nitembelea nikutambue?" alimuuliza
"Haha! Kijana inaonekana una akili sana na mtu makini" aliongea kamanda Rama na ghafla tu alizima ule msisimko wa nguvu zake za kichaw
"Kwahiyo unataka kusemaje kamanda?"
"Nachotaka ni kujua chaguo lako, Ndio au hapana"
Jimmy alipiga kimya cha dakika kadhaa akiwaza na kuwazua kisha kumtazama kamanda Rama na tabasamu flani hivi na kunyanyuka pale mezani
"Hata hivyo bila ya msaada wa watu wako kipindi kile pengine nisingekuwa hapa leo hii" kisha alianza kutembea kuelekea juu na alipofika katikati ya ngazi kamanda Rama aliongea
"Nitakutaarifu mambo yakiwa tayari"
Hakuitaji maelezo zaidi kuelewa kwamba Jimmy amekubali kushirikiana nao kwenye mpango ambao Hidden Supremacy walikuwa wakuandaa na taratibu alinyanyuka pamoja na Caren kuondoka mahali hapo
Walipoufikia mlango Caren alisimama ghafla na kugeuza shingo nyuma akiangalia upande wa ngazi juu ambako Jimmy alipotelea na kuangalia kwa, sekunde kadhaa kisha kugeuza shinho na kuzipiga hatua kuondoka.
Jimmy aliweza kumuona Biancalina akiwa amesimama mlangoni mwa chumba chake akimsubiri na mkono wa kulia alikuwa ameshikilia nguo mpya kabisa, haikueleweka alinunua lini
"Mummy usiniambie ulikuwa unanisubiria muda wote huo" aliongea kiutani
"Shika hizi nguo ukabadili sasahivi" aliongea Bianca akimpatia nguo hizo
"Mummy kuna ulazima wakuvaa hizi nguo? mbona hata hapa nimependeza tu" aliongea Jimmy
"Darling bhana nishakwambia sipendi tabia yako ya kunikatalia vitu vidogo vidogo" aliongea huku akinuna na kumnyooshea nguo
Jimmy hakuwa jinsi aliona ni bora tu akubali kuliko kumkasirisha bila sababu za msingi maana ni jana tu hapo alitoka ku'confess alijiambia sasa kama alisema anampenda zaidi ya chocolate halafu amkasirishe si ataonekana muongo?
Baada ya Jimmy kuzipokea nguo hizo Bianca alifurahi moyoni na kumpiga busu la hatraka shavuni na kukimbilia chumbani kwake ambapo hakukuwa mbali na chumba cha Jimmy
Jimmy aliganda kwa sekunde kadhaa akiwa na tabasamu pana usoni huku akihisi mtekenyo kwenye moyo wake, hapana sio moyo tubali mwili mzima
"Sometimes, love surprises you when you least expect it… like now." alijiongelesha akimaanisha "muda mwingine upendo hukushangaza bila kutarajia.. Kama sasa hivi" na kuingia zake ndani
Dakika chache tu alitoka chumbani akiwa amebadili nguo na kuvaa zile alizopewa na mpenzi wake mpya
Alikuwa amevalia shati kubwa 'oversize' la mikono mifupi rangi ya urujuani(violet), design yake ilikuwa ni ya kipekee sana kama vile gwanda la juu la kijeshi maalum kwa jenerali, lakini halikuwa gwanda
Pia alivaa suruali nyeusi iliyokuwa stable, haikumbana sana wala haikuwa pana sana kifupi ilikuwa stable. Na miguuni alipigilia rubber safi nyeupe kama theluji kampuni ya Nike
Kwa staili hiyo ya mavazi Jimmy alitokelezea haswaa yaani alipendeza kinoma ukijumlisha na utanashati wake na mwili wake ndio kabisa hakuelezeka kwa maneno
Mdogo mdogo alishuka chini na kwenda zake sebuleni na kukaa kwenye sofa akimsubiri Bianca na kama mjuavyo tabia za wanawake kuchukua muda mrefu kujiandaa ilimbidi tu kuangalia Tv kusogeza muda
Baada ya kusubiri kwa dakika kadhaa hatimae aliweza kusikia hatua za miguu zikishuka na anageuza shingo yake kuangalia anakutana na bibie amepiga sare sawa na yake na alionekana kama tomboy fulani hivi
Itoshe kusema alipendeza kwelikweli, uzuri wake wa uso wake haukuhitaji make up kuupamba bali ulijidhihirisha wenyewe yaani ule uzuri wa asili
Kwenye macho ya Jimmy Biancalina alionekana kama vile mgeni kwake na muda wote alikuwa akimkodolea macho kama vile hakuwahi kumuona hapo kabla na mpaka Bianca anamkaribia ndio anashtuka kutoka kwenye kuzubaa. Kwa kizungu tunasema "he was in a daze"
"Mummy ni wewe kweli?" aliuliza kama vile haamini macho yake
"Nimependeza eeh!"
"Loh! For sure umependeza ni kama ndoto iliyosukwa kwa mkusanyiko wa nyota na mwezi ikawa halisi, yaani uzuri wako hauonekani tu, unahisiwa! Like a silent melody that plays in the soul." Jimmy alimwaga sifa kitaalamu sana akichanga kingereza na kiswahili
Bianca alisikia raha kusifiwa sio airi, japo hakuonyesha lakini alifurahi mno!
"Ni kama malkia asiyehitaji taji kujulikana. Na macho yako… ni kama galaksi mbili" aliendelea
"Inatosha" Bianca alianza kupatwa na aibu huku akiangalia chini
"Hehe mbona unanionea aibu? Lakini ndio unavyozidi kuvutia"
"Aah..." Bianca alitaka kuongea Jimmy akamuwahi
"Basi nitaacha..... My queen" aliongea akimpa ishara atangulie kama mfalme amfanyiavyo malkia
Bianca alitoa tabasamu kama la malaika na kutangulia kisha Jimmy akafuata na kumkaribia sawa na walipofika mlangoni Jimmy kama gentleman vile alimfungulia mlango na mrembo Bianca kupita
Walienda mpaka garage ya magari ambapo walimkuta Zuhura na walinzi wenzake wakimsubiri
"Zuhura leo hatutaongozana" Bianca alimtaarify mlinzi wake
"Lakini madam usalama wako ni muhimu isitoshe wewe ni celebrity utahitaji msaada paparazzi wanapojitokeza"
"Usiwe na wasiwasi nipo na Jimmy"
"Lakini madam huu ni wajibu wangu sio kwamba simuamini..."
"Nipo salama Zuhura leo sihitaji kuongozana na walinzi nahitaji uhuru na mume wangu"
Paah! Moyo wa Jimmy ulidunda na kuendelea kudunda mpaka ukadundika neno "mume wangu" hakulitegemea kulisikia mapema hivyo tena wakati kama huo mbele ya walinzi, ila hakujali sana kuhusu walinzi alipatwa na ile hisia ya kuitwa mume wangu kwa mara ya kwanza yaani jana love confession kesho yake ambayo ndio hiyo anaitwa mume wangu!
Hata hivyo alifurahi mnooo tena mno! Sura yake ilikuwa inang'aa kwa tabasamu kwa kuitwa mume, hata kama hawakufunga ndoa ila alifurahi sana kusikia hivyo
"Darling unajua kuendesha gari?" Bianca alimuuliza Jimmy ambaye alikuwa hajasikia, alikuwa mbali sana kimawazo akitabasamu bila ya kueleweka anawaza nini
"Hey.. Wewe.. Darling!" aliita na Jimmy alishtuka na kutoka kwenye mawazo na kumuangalia Bianca
"Naam mke wangu"
"Nimekuuliza unajua kuendesha gari"
"Ndio ndio mimi ni mtaalamu sana usiwaze" aliongea na Bianca aliingiza mkono kwenye suruali na kutoa funguo ya gari kisha kumpatia
Jimmy baada ya kupokea funguo alienda mfungulia mlango wa gari husika siti ya mbele ya abiria na baada ya Bianca kuingia alifumga na kumtolea tabasanu Zuhura
"Ondoa wasiwasi yuko salama" kisha alienda mlanfo wa dereva na kuingia. Dakika moja ilitosha kuliondoa gari hilo ndani ya nyumba na sasa lilikuwa barabarani likichanja mbuga kwa mwendo mtulivu
END OF SEASON ONE!.... THE RHYTHM CONTINUES.... 🔥
CHAPTER 30: Ugeni uliotarajiwa (expected visit)
Jimmy hisia zake zilikuwa ni sahihi kwani ndani ya sekunde kadhaa ulisikika mlio wa kengele ya mlango wa kuingia sebuleni kuashiria kwamba kuna ugeni muda huo
Aisha alinyanyuka na kwenda kufungua mlango na kuwaona watu wawili wamesimama mlangoni mmoja akwa ni mwanaume mwigine akiwa ni mwanamke. Mwanaume alionekana ni mkubwa kiumri huku mwanamke akiwa ni kijana zaidi
Wageni hao walikuwa wamevaa mavazi ya kawaida, mwanaume ambaye alikuwa ni kamanda Ramadhan alivalia t-shirt rangi ya zambsrau ambayo ilionekana kumbana kwa kiasi chake huku kifua chake na misuli ya mazoezi ikijichora, chini alivalia suruali nyeusi iliyombana na buti za kijeshi nyeusi zilizong'aa kana kwamba zimepakwa mafuta
Upande wa mwanamke alikuwa na asili ya kihabeshi na hakuwa mwingine bali ni Caren, naye alipendeza licha ya kuvalia kawaida kutokana na umbo lake matata. Chuchu saa sita za mrembo huyo zilionkana kusimama haswaa licha ya kuvalia shati kubwa la draft, rangi ya bluu lenye mikono mirefu, pia chini alivaa jinsi nyeusi iliyombana vyema na kuchora hipsi zake pamoja na mzigo wa wastani ulioko nyuma, bila kusahau buti nyeusi pia za doc matterns
"Karibuni ndani" Aisha aliwakaribisha na waliweza kuingia ndani.
"Msiishie kusimama tu hapo karibuni mpate kifungua kinywa haipendezi kwa wageni kula harufu ya misosi" aliongea Jimmy baada ya kuona wanaelekea kukaa sofani
Kama Rama na, Caren mara baada ya kusikia kauli hiyo kutoka kwa Jimmy walitabasamu na kuelekea mezani walikokaribishwa
"Ni wageni wako hawa?" Bianca aliumuuliza na Jimmy alitingisha jichwa kukubali
"Mbona hukutuambia kama una wageni asubuhi hii tuandae chakula cha kutosha" Bianca aliongea
"Usiwaze sana mummy watakunywa chai tu mimi mwenyewe sikutegemea ujio wao" Jimmy aliongea na alipomaliza kauli hiyo wageni waliweza kufika mezani na Bianca alinyanyuka kuwasalimia kwa heshima huku akiwapa tabasamu la kirafiki
"Miss lina sisi ndio tunapaswa kutoa heshima na kuomba radhi kwa ujio wa ghafla" aliongea Caren akimpa tabasamu
"Je haimpasi mke wangu kukaribisha wageni kwa heshima mahali pangu?" Jimmy aliongea
"Unanifahamu!" Bianca aliuliza kirafiki
"Kwa umaarufu ulio nao nani asikujue, mimi ni mmoja kati ya shabiki zako" alijibu Caren
"Haha! am humbled! Karibuni ten " Bianca aliwakaribisha kwa mara nyingine na walipokea ukaribisho
Aliwawekea juisi ya matunda kwenye glasi na vitafunwa baadhi kisha kwa kujiongeza yeye pamoja na vijakazi wa nyumba yake waliondoka kwa kisingizio cha kushiba kuwaachia 'privacy'
"Sikudhania kama utakuwa na mke mwenye kujiongeza haha" aliongea kamanda Rama huku akijichekesha
"Anyway sisi ni watu wazima haina haja ya kuzunguka nianze kujitambulisha mimi ni Ramadhan Suleiman Sudi na huyu hapa ni Caren nadhani mlishakutana"
"Ndio miaka mitanobiliyopita.. Hey long time no see!" aliongea Jimmy na kumpa ishara ya kirafiki Caren, naye Caren alirudisha kwa tabasamu la kirafiki
"Mimi ndiye mkuu wa kitengo cha Hidden Supremacy na lengo la kuja hapa ni kutaka....."
"Usiniambie unataka nijiunge kwenye hilo kundi lenu"
"Hilo lilikuwa ni kusudi langu la kwanza lakini nimebadili maamuzi"
"Ooh ni vizuri umebadili maamuzi maana hata kama usingebadili nisingekubali, unaonaje ukaniambia kilichokufanya ubadili maamuzi?"
"Mwanzoni nilidhani utakuwa ni mtaalamu uliyebobea kwenye mapigano kutokana na taarifa niliyopata kwa Caren na mimi huwa napenda kuendeleza vipaji kanma hivyo, na tulipofanya uchaguzi kuhusu wewe nikaja kugundua kwamba unafahamika sana katika ulimwengu wa kihalifu, of course ilikuwa ni taarifa nzuri sana kwa upande wetu na kupata sababu nzuri ya kukufanya uingie kundini hata kama hutaki" aliongea kamanda Rama na kunyanyua glasi yake ya juisi na kuigida yote kama maji
Jimmy alikuwa akimtazama tu huyo kamanda mweusi tii akisubiri muendelezo wa simulizi yake fupi, alijiambia hajawahi kukutana na binadsamu mweusi kama hiyo tangu azaliwe, aliwaza mbali na kudhani pengine wanawake aliokuwa nao wameondoka kwa sababu ya sura yake ngumu na weusi tii
"Lakini ulipotea kwa miaka mitano bila ya kujulikana ulikopotelea" alimalizia
"Kwahiyo kupotea kwangu ndio sababu ya wewe kubadili uamuzi?"
"Hapana"
"Sababu ni ipi?" Jimmy aliuliza akimkazia macho kusubiri jibu
"Tuachane na sababu lengo langu sio kuelezea sababu nimekuja hapa kuomba ushirikiano" aliongea kisha kunyamanza
"Ushirikiano wa nini kamanda mbona unaongea kwa mkato kwanini usitamke hotuba yote kuliko kuniambia kidogo kidogo"
"Nadhani utakuwa unajua kuhusu hivi viumbe vya ajabu ajabu vinavyotesa raia"
"Ndio ni vichaa tu waliopoteza ubinadamu" aliongea Jimmy
"Vyovyote vile tunataka kuwaondoa iliraia waishi kwa amani"
"Sasa mimi nahusikaje kwenye mpango wenu wa kutaka kuwaondoa?"
"Tunataka ushirikiane nasi kwenye huu mpango"
""Nini kinawafanya mdhani labda nitakubali na ninaweza kusaidia? "
" Ukweli uwezo wa kusaidia unao kuhusu wewe kukubali ni ombi letu, chukulia unaweka akiba ya msaada kwetu ukikubali na kutusaidia kwenye huu mpango kama una lolote utakalo ambalo tunaweza kukusaidia tutafanya hivyo"
"Mkuu mbona unanifanya mbuzi wa kafara? mimi ni binadamu tu wa kawaida sasa kutaka mimi kwenda kupambana na hao mashetani ni sawa na kunitoa kafara maana hatujui nini kitajiri, vipi mpango ukishindikana?"
"Ukijiunga nasi hauwezi kusgindwa!"
"Hahaha! Inashangaza sana hatujuani lakini unaniamini kupitiliza, au kwasababu ya kunifuatilia?"
"Kwahiyo ulikuwa unajua nakufatilia lakini ukaamua kujifanya, kwanini?" aliongea kamanda Rama, sio kama hakujua ameshtukiwa bali alitaka sababu
Ukweli Jimmy tangu ile siku alipodili na wale wahuni waliotumwa kumvunja miguu aliweza kugundua anafuariliwa lakini aliamua kujifanya kutoshtukia
" Kwasababu haukuwa na nia mbaya juu yangu" alijibu
"Unajuaje kama hakuwa na nia mbaya, inawezekanaje mtu kujua nia ya mwenzake?" Caren aliuliza
"Aura!" Jimmy alimjibu na kumfanya Kamanda Rama kutabasamu
"Aura anayosambaza muhusika hiubadilika kutokana na hisia na matendo, ni kama harufu ya mvua kabla haijanyesha. Mfano, mtu anayetaka kukuua, husambaza hisia flani zisizo za kawaida. Mapigo ya moyo wako hubadilika, na hata hewa inayokuzunguka huhisi kuwa nzito… kama kiza kinachofunika mwanga taratibu" aliongea na kunyamanza kidogo
"It’s like a feeling of something brushing against your soul" aliendelea akimaanisha "ni kama hisia flani ya kitu kinachogusa nafsi yako"
"Sawa tuseme Aura lakini uliwezaje kujua ni Kamanda Rama na si mwingine?" Caren aliuliza swali jingine
"Unauliza swali ambalo jibu unalo, jibu ni msisimko wa nguvu za kiroho anaotoa, ukweli sikujua kama ni kamanda wako zaidi ya kujua tu kuna mtu ananifatilia nimejua ni kamanda wako sababu msisimko wake naouhisi hauna tofauti na yule aliyekuwa akinifuatiliwa" Jimmy aliongea na kumgeukia kamanda Rama
"Ulifanya makusudi nikugundue si ndio? Ili ukija nitembelea nikutambue?" alimuuliza
"Haha! Kijana inaonekana una akili sana na mtu makini" aliongea kamanda Rama na ghafla tu alizima ule msisimko wa nguvu zake za kichaw
"Kwahiyo unataka kusemaje kamanda?"
"Nachotaka ni kujua chaguo lako, Ndio au hapana"
Jimmy alipiga kimya cha dakika kadhaa akiwaza na kuwazua kisha kumtazama kamanda Rama na tabasamu flani hivi na kunyanyuka pale mezani
"Hata hivyo bila ya msaada wa watu wako kipindi kile pengine nisingekuwa hapa leo hii" kisha alianza kutembea kuelekea juu na alipofika katikati ya ngazi kamanda Rama aliongea
"Nitakutaarifu mambo yakiwa tayari"
Hakuitaji maelezo zaidi kuelewa kwamba Jimmy amekubali kushirikiana nao kwenye mpango ambao Hidden Supremacy walikuwa wakuandaa na taratibu alinyanyuka pamoja na Caren kuondoka mahali hapo
Walipoufikia mlango Caren alisimama ghafla na kugeuza shingo nyuma akiangalia upande wa ngazi juu ambako Jimmy alipotelea na kuangalia kwa, sekunde kadhaa kisha kugeuza shinho na kuzipiga hatua kuondoka.
Jimmy aliweza kumuona Biancalina akiwa amesimama mlangoni mwa chumba chake akimsubiri na mkono wa kulia alikuwa ameshikilia nguo mpya kabisa, haikueleweka alinunua lini
"Mummy usiniambie ulikuwa unanisubiria muda wote huo" aliongea kiutani
"Shika hizi nguo ukabadili sasahivi" aliongea Bianca akimpatia nguo hizo
"Mummy kuna ulazima wakuvaa hizi nguo? mbona hata hapa nimependeza tu" aliongea Jimmy
"Darling bhana nishakwambia sipendi tabia yako ya kunikatalia vitu vidogo vidogo" aliongea huku akinuna na kumnyooshea nguo
Jimmy hakuwa jinsi aliona ni bora tu akubali kuliko kumkasirisha bila sababu za msingi maana ni jana tu hapo alitoka ku'confess alijiambia sasa kama alisema anampenda zaidi ya chocolate halafu amkasirishe si ataonekana muongo?
Baada ya Jimmy kuzipokea nguo hizo Bianca alifurahi moyoni na kumpiga busu la hatraka shavuni na kukimbilia chumbani kwake ambapo hakukuwa mbali na chumba cha Jimmy
Jimmy aliganda kwa sekunde kadhaa akiwa na tabasamu pana usoni huku akihisi mtekenyo kwenye moyo wake, hapana sio moyo tubali mwili mzima
"Sometimes, love surprises you when you least expect it… like now." alijiongelesha akimaanisha "muda mwingine upendo hukushangaza bila kutarajia.. Kama sasa hivi" na kuingia zake ndani
Dakika chache tu alitoka chumbani akiwa amebadili nguo na kuvaa zile alizopewa na mpenzi wake mpya
Alikuwa amevalia shati kubwa 'oversize' la mikono mifupi rangi ya urujuani(violet), design yake ilikuwa ni ya kipekee sana kama vile gwanda la juu la kijeshi maalum kwa jenerali, lakini halikuwa gwanda
Pia alivaa suruali nyeusi iliyokuwa stable, haikumbana sana wala haikuwa pana sana kifupi ilikuwa stable. Na miguuni alipigilia rubber safi nyeupe kama theluji kampuni ya Nike
Kwa staili hiyo ya mavazi Jimmy alitokelezea haswaa yaani alipendeza kinoma ukijumlisha na utanashati wake na mwili wake ndio kabisa hakuelezeka kwa maneno
Mdogo mdogo alishuka chini na kwenda zake sebuleni na kukaa kwenye sofa akimsubiri Bianca na kama mjuavyo tabia za wanawake kuchukua muda mrefu kujiandaa ilimbidi tu kuangalia Tv kusogeza muda
Baada ya kusubiri kwa dakika kadhaa hatimae aliweza kusikia hatua za miguu zikishuka na anageuza shingo yake kuangalia anakutana na bibie amepiga sare sawa na yake na alionekana kama tomboy fulani hivi
Itoshe kusema alipendeza kwelikweli, uzuri wake wa uso wake haukuhitaji make up kuupamba bali ulijidhihirisha wenyewe yaani ule uzuri wa asili
Kwenye macho ya Jimmy Biancalina alionekana kama vile mgeni kwake na muda wote alikuwa akimkodolea macho kama vile hakuwahi kumuona hapo kabla na mpaka Bianca anamkaribia ndio anashtuka kutoka kwenye kuzubaa. Kwa kizungu tunasema "he was in a daze"
"Mummy ni wewe kweli?" aliuliza kama vile haamini macho yake
"Nimependeza eeh!"
"Loh! For sure umependeza ni kama ndoto iliyosukwa kwa mkusanyiko wa nyota na mwezi ikawa halisi, yaani uzuri wako hauonekani tu, unahisiwa! Like a silent melody that plays in the soul." Jimmy alimwaga sifa kitaalamu sana akichanga kingereza na kiswahili
Bianca alisikia raha kusifiwa sio airi, japo hakuonyesha lakini alifurahi mno!
"Ni kama malkia asiyehitaji taji kujulikana. Na macho yako… ni kama galaksi mbili" aliendelea
"Inatosha" Bianca alianza kupatwa na aibu huku akiangalia chini
"Hehe mbona unanionea aibu? Lakini ndio unavyozidi kuvutia"
"Aah..." Bianca alitaka kuongea Jimmy akamuwahi
"Basi nitaacha..... My queen" aliongea akimpa ishara atangulie kama mfalme amfanyiavyo malkia
Bianca alitoa tabasamu kama la malaika na kutangulia kisha Jimmy akafuata na kumkaribia sawa na walipofika mlangoni Jimmy kama gentleman vile alimfungulia mlango na mrembo Bianca kupita
Walienda mpaka garage ya magari ambapo walimkuta Zuhura na walinzi wenzake wakimsubiri
"Zuhura leo hatutaongozana" Bianca alimtaarify mlinzi wake
"Lakini madam usalama wako ni muhimu isitoshe wewe ni celebrity utahitaji msaada paparazzi wanapojitokeza"
"Usiwe na wasiwasi nipo na Jimmy"
"Lakini madam huu ni wajibu wangu sio kwamba simuamini..."
"Nipo salama Zuhura leo sihitaji kuongozana na walinzi nahitaji uhuru na mume wangu"
Paah! Moyo wa Jimmy ulidunda na kuendelea kudunda mpaka ukadundika neno "mume wangu" hakulitegemea kulisikia mapema hivyo tena wakati kama huo mbele ya walinzi, ila hakujali sana kuhusu walinzi alipatwa na ile hisia ya kuitwa mume wangu kwa mara ya kwanza yaani jana love confession kesho yake ambayo ndio hiyo anaitwa mume wangu!
Hata hivyo alifurahi mnooo tena mno! Sura yake ilikuwa inang'aa kwa tabasamu kwa kuitwa mume, hata kama hawakufunga ndoa ila alifurahi sana kusikia hivyo
"Darling unajua kuendesha gari?" Bianca alimuuliza Jimmy ambaye alikuwa hajasikia, alikuwa mbali sana kimawazo akitabasamu bila ya kueleweka anawaza nini
"Hey.. Wewe.. Darling!" aliita na Jimmy alishtuka na kutoka kwenye mawazo na kumuangalia Bianca
"Naam mke wangu"
"Nimekuuliza unajua kuendesha gari"
"Ndio ndio mimi ni mtaalamu sana usiwaze" aliongea na Bianca aliingiza mkono kwenye suruali na kutoa funguo ya gari kisha kumpatia
Jimmy baada ya kupokea funguo alienda mfungulia mlango wa gari husika siti ya mbele ya abiria na baada ya Bianca kuingia alifumga na kumtolea tabasanu Zuhura
"Ondoa wasiwasi yuko salama" kisha alienda mlanfo wa dereva na kuingia. Dakika moja ilitosha kuliondoa gari hilo ndani ya nyumba na sasa lilikuwa barabarani likichanja mbuga kwa mwendo mtulivu
END OF SEASON ONE!.... THE RHYTHM CONTINUES.... 🔥