Samuel jk_Euphoria
Member
- Apr 18, 2025
- 85
- 220
- Thread starter
- #21
By Samuel jk_Euphoria
SOLO KING: ANCIENT LEGACY
CHAPTER 10: Salazar Solren Soledad
Upande wa Jenerali hakuwa na mabadiliko yoyote zaidi ya kutoa tabasamu tu maana alishaizoea hali hiyo kutoka kwa mwanae.
"Wewe mtukutu ifike muda uonyeshe heshima kwa wakubwa zako" aliongea Jenerali huyo na kumpotezea
Aliwaangalia wengine walioko lakini zaidi macho yake yalitua kwa Jimmy ambaye pia alikuwa akimuangalia
"Samahanini kwa ujio wangu wa ghafla mahali hapa sijaja kwa kutibua amani bali nimekuja kwa nia njema kabisa mimi ni Jenerali Johnson Merizesta mkuu wa majeshi ya ulinzi wa nchi, nina muda mchache kuwepo hapa, lengo ni kuzungumza na Jimmy Julian Jairo" alijitambulisha na kusema dhumuni la kuja mahali hapo
"Kuweni na amani sitochukua muda mrefu sana kwa mgonjwa" aliendelea kuongea na kuwaomba wawapishe kidogo, maongezi mengine ni siri. Nani wa kumpinga Jenerali kwa mfano? Kila mmoja alitoka nje wakibaki watano tu, Jenerali, walinzi wake pamoja na jimmy
Jenerali alivuta kiti na kwenda kukaa pembeni kidogo akikunja nne
"Upo unajiuliza kwanini mkuu wa majeshi amekutembelea si ndio?" aliuliza
"Najiulizaje ilihali umeshasema unahitaji mazungumzo na mimi mzee Jenerali" aliongea Jimmy na kumfanya Jenerali aachie tabasamu
"Unajua maongezi gani ambayo yamenitoa makao makuu mpaka kuja hapa hospitalini kwa raia wa kawaida kama wewe?"
"Mkuu nitajuaje bila ya wewe mwenyewe kuniambia isitoshe mimi sio malaika mpaka kujua kila kitu"
"Hahaha! Napenda vijana jasiri kama wewe, mara nyingi nikiongea na watu huwaga waoga sana na kuchagua maneno ya kuongea lakini kwako wewe ni tofauti.... just like your father"
"Unamjua baba yangu?" Jimmy aliuliza akiwa amekunja sura yake
"Ndio alikuwa rafiki yangu jeshini, niseme tu baba yako alikuwa ni mtu muhimu sana ya jeshi lakini inasikitisha ha......." aliacha sentensi yake ieleee hewani
"Anyway hilo sio lengo langu la kuja hapa"
"Lengo lililokuleta ni lipi?" Jimmy aliuliza na Jenerali alitoa ishara na mmoja wa walinzi alitoa faili na kumpatia
"Unamfahamu huyo?" Jenerali alimuuliza baada ya kumpatia faili na Jimmy alikubaliana naye
"Ndio huyu ni mzee wangu nilikuja kujua Jina lake halisi ni Momochi Saizo juzi-juzi" alijibu na Jenerali alimpatia faili jingine tena
"Unamfahamu huyo?" aliuliza tena na Jimmy baada ya kulitazama faili alikataa
"Hapana simfahamu huyu"
"Angalia vizuri usiangalie sura angalia majina"
"Unataka kusema?" Jimmy alipatwa na mshangao kidogo baada yakugundua kitu
"Nadhani ushaelewa sasa hao wote ni mtu mmoja"
"Kama ni mtu mmoja ipi ni sura yake halisi?"
"Kuhusu sura yake halisi hilo nalo ni shaka jingine amekuwa akiishi nchi tofauti tofauti kwa sura tofauti, tumeweza kupata taarifa hiyo kwa msaada wa Uingereza kwamba yupo nchini" aliongea Jenerali
"Sawa, lakini nini maana ya kuniambia hizi siri za jeshi? Jimmy aliuliza
" Inashangaza eeh? Huyo ni "Former ninja assasin" yaani alikuwa na alitekeleza mauaji mengi sana kutoka mataifa tofauti na katika kustaafu kwake alipotea kusikojulikana na hivi karibuni aliweza kugundulika nchini humu baada ya msako wa muda mrefu. Umekuwa ukiishi na mtu hatari kwa muda mrefu"
"Mzee ana siri sana yule Mkuu sishangai"
"Kingine ameuawa na kundi lake la kininja alilokuwa akilihudumu kwa muda mrefu cha kushangaza uliweza kudili nao na kuwamaliza kwa maana hiyo umefanya kazi ambayo kitengo chetu kilipaswa kufanya"
"Kidogo nipoteze uhai wangu, niseme ni bahati tu"
"Ni kundi daraja B lijulikanalo kama Yami no Senshi lenye maana ya Warriors of Darkness ni kundi lenye maninja wasomi wanaojificha kwenye vivuli/giza" alieleza kwa kifupi
"Kwahiyo unataka kusemaje Mkuu?" Jimmy aliuliza na kumfanya anyanyuke na kusimama akiachia tabasamu
"Ninakukaribisha kujiunga na Jeshi letu ninaamini kwa uwezo wako ulionao tukikuongezea ujuzi utalisaidia taifa kwa namna nyingi sana"
"Asante lakini sivutiwi na kuwa mwanajeshi" alijibu Jimmy
"Usiwe na haraka ya kutoa jibu haraka je hutaki kuwa na heshima kama ya baba yako? hutaki kujua nini sababu ya baba yako kutangulia mbele za haki?"
"Kwasababu ya baba yangu kuwa mwanajeshi haimaanishi na mimi nitataka kuwa kama yeye kingine nachojua ni kwamba baba yangu alikufa kwa ajali, hata kama isingekuwa ajali bado kazi yake ni ngumu kutoka salama... Asante sana kwa ofa hiyo mkuu lakini jibu langu ni hapana"
"Kijana acha kukurupuka ni ngumu sana Mkuu wa majeshi kumualika raia ndani ya jeshi bila utaratibu" aliongea mmoja aa walinzi lakini jimmy alitingisha kichwa kukataa
"Sawa sitokulazimisha kijana kuheshimu uamuzi wa mtu ni jambo muhimu sana" aliongea Jenerali na kuzipiga hatua zake kuondoka alipoukaribia mlango alisita
"Ooh nimekumbuka" aliongea Jenerali na kumgeukia Jimmy "Una sbukrani zangu za dhati kijana umeiokoa familia yangu, hilo nashukuru" aliongea na kuondoka zake akimuacha Jimmy katika hali ya kutafakari
Ndugu zake waliingia mara baada ya Jenerali na jeshi lake kuondoka, wa kwanza kutangulia alikuwa ni Cid akifuatwa na Monica, Bianca na Mamaye
"Bro huyo mzee alikuwa anakwambia nini?" Cid aliuliza na kila mtu alitega masikio kusikiliza na Jimmy alitoa kicheko na kuwaangalia mmoja baada ya mwingine
"Amekuja kunipa pole tu na kutoa shukrani" alijibu
"Shukrani za nini?" Cid aliuliza na wengine kutingisha kichwa kukubaliana na swali lake
"Nenda kamuulize si mzee wako yule halafu kumbe ni mkuu wa majeshi asee"
"Kuhusu hilo hapana kwakweli bro fanya ututonye ndugu zako basi" aliendelea kumtaka amuelezee lakini Jimmy aliendelea kukomalia kwamba akamuulize mwenyewe na mpaka kufika jioni saa kumi na mbili walizungumza mengi na waliaga kwakuwa muda wa kutembelea wagonjwa umeisha
Kama kawaida baada ya wote kuondoka wakikwishakumuaga aliuchapa usingizi kama maiti vile.
°°°°°°°°°°
Jimmy alijikuta yuko mahali pasipojulikana ni wapi akiwa peke yake
Mahali hapo kulikuwa ni patupu kupita maelezo, ardhi yake ilikuwa ni tambarare yenye mchanga mweupe kama wa baharini, anga nalo lilikuwa ni la buluu safi lisionekane wingu hata moja
Wakati anajiuliza yuko wapi mara alisikia sauti kama mwangwi ikinena
"Welcome to my world young man" ilikuwa ni sauti yenye kusikika vyema masikioni mwa mtu yeyoteikimaanisha karibu katika ulimwengu wangu kijana
"Where am I and who are you?" aliuliza kwa lugha sawasawa na aliyoisikia akimaanisha Niko wapi na wewe ni nani
"I am Salazar Solren Soledad, Sovereign of the Arcane, The Forbidden Monarch of ancient knowledge, The Sorcerer, The Enchanter, Spellweaver, The Ancient legacy" sauti ilijitambulisha ikimaanisha "Mimi ni Salazar Solren Soledad, mtawala wa uchawi wote, Mfalme wa maarifa ya kale, Sorcer(mchawi), Enchanter(mchawi), spellweaver(mchawi wa spells), Uridhi wa kale"
Upande wa Jimmy licha ya utambulisho huo hakuelewa chochote licha ya kujua kingereza, aliishia tu kukaa chini akijikuna kichwa chake
"Unaonekana hujanielewa bado kijana" ilisikika tena sauti hiyo
"Unajua kuzumgumza kiswahili?" jimmy aliuliza
"Ninafahamu lugha nyingi sana kuliko unavyofikiria"
"Kumbe! Unaweza kuniambia kwanini niko hapa"
"upo hapa kwasababu unakwenda kuwa mrithi wangu"
"Mrithi? Usinitanie we mzee kwanza kwanini unajificha" aliongea jimmy na sekunde anamaliza kauli yake alihisi kuna mtu yuko nyuma yake na aligeuka haraka lakini hakumuona mtu na ile anarudisha kichwa chake tu anakutana na sura ambayo ilimshtua kiasi cha kuruka kama wadada wanavyorukia juu ya kochi baada ya kumuonda mende akiwakaribia
Alikuwa ni mzee mwenye sura iliyojikunja kiasi cha sura yake kumtisha yeyote atakaye muangalia kwa mara ya kwanza, meno yake nayo yalikuwa ni ya njano yenye mapengo yasiyo na idadi ya kueleweka, sasa vuta picha ndugu msomaji jinsi mzee huyo alivyo, kibaya zaidi alikuwa akitabasamu
"Sikujificha, sijajificha na sijawahi kujificha" aliongea mzee Salazar akivalia joho jeusi refu lililofunika mikono yake na miguu yake
Jimmy alivuta pumzi ndefu na kuzishusha akimtazama mzee huyo aliyekuwa akimtazama pia
" Unaweza kuniambia kwanini nipo hapa?" jimmy aliuliza
"Unataka kujua kwanini?"
"Ndio"
"Kaa chini kwanza" alimwambia aketi chini na Jimmy alikaa pamoja na huyo mzee
"Umekiona hiki kitabu" aliongea mzee Salazar baada ya kunyanyua mkono kumuonyesha na ghafla kitabu kilijitokeza kichawi hali iliyomfanya Jimmy kushangaa na kukunja ndita
"Kilitaka kunitoa uhai wangu na kusababishia familia yangu kutekwa bila kusahau mzee wangu Momochi ametangulia mbele za haki kwa sababu ya hako kakitabu ka kipuuzi"
"Hapana hiki kitabu sio upuuzi umepitia yote hayo ni kwasababu ya kile kilichomo humu"
"kilichomo my foot! Unataka kuniambia bizo kurasa tupu zilizomo humo ndio zilikuwa zikitafutwa" Jimmy aliongea kwa hasira alitamani jata kutukana lakini alikuwa akiogopa hata yeye mwenyewe alijishangaa kwanini anaogopa
"Fungua" aliongea mzee Salazar akimpatia kitabu na kutaka akifungue.
Jimmy alikipokea na kukifungua na alishangaa kukikuta kimeandikwa lugha zisizoeleweka tofauti na mwanzo ambapo hakukuta maandishi yoyote
Jimmy alimwangalia mzee huyo kwa sura yenye maswali na kutaka maelezo
"Hizo ni lugha za kale ambazo zimesahaulika katika dunia hii sababu ya wewe kutokuta maandishi ni kwasababu niliyaficha na kwasababu ya agano nililoliweka nilipokaribia kufa"
"kwamba damu ya awaye yote itakayomwagika katika kitabu hiki huyo ndiye atakayekuwa mrithi wangu atake asitake ndipo roho yangu ipumzike kwa amani..... "
"Umesema ulipokaribia kufa sasa mbona mpaka sasa hujafa" Jimmy alimkatisha
"Tulia kijana, subiri nimalize ndiyo uulize maswali yako ila ngoja nikujibu hilo kabla ya kuendelea. Mimi nilikwisha kufa kitambo mimi ni roho iliyokataa kwenda mahali pake kwasababu ya kudhulumiwa uhai wangu" aliongea mzee Salazar na Jimmy kufunga mdomo wake
"Hapo zamani nilikuwa ni mchawi mwenye nguvu sana na mwenye maarifa mengi ambayo ambayo mpaka kwenye dunia ya sasa hayapo"
"Unasema ni mchawi mwenye nguvu ilikuwaje sasa ukafa lakini sasa upo hai"
"Watu tunakufa kwa njia nyingi sana, inaweza kuwa ajali, magonjwa, kuuawa. na vifo vingine vinatokea bila sababu yoyote si ajali, si ugonjwa wala chochote kilichosababisha unajikuta tu unakufa, ila unajua ni kifo gani kinaumiza?" alimuuliza jimmy
"Sijui"
"Ni kile kifo cha kuuawa hasa kwa mtu ambaye hukutegemea atakuja kufanya hivyo, na mtu huyo ni mwenye kujua siri zako na udhaifu wako na kuzitumia kukuondosha kwenye uso wa dunia. Na mara nyingi mtu huyo ni mtu wa karibu sana kwako anaseza kuwa mpenzi wako unayemuamini, rafiki yako wa karibu na hata mwanafamilia wako." aliongea mzee Salazar na kunyamanza kidogo akimeza mate kisha kuendelea
"Yote hayo huanzia kwenye wivu, kijana unapaswa kujua wivu ni mbaya sana, Wivu husababisha tamaa na chuki na kwasababu ya chuki na tamaa za kijinga ndiyo husababisha kuuana"
Jimmy alikuwa kimya tu akimsikiliza mzee huyo kana kwamba yupo kanisani akipata mahubiri.
"Nimeuawa na mtu ambaye sikumtegemea, mtu ambaye nilikuwa nikimjali sana na kuhakikisha hapati tabu lakini ndiyo hivyo shukrani ya punda ni mateke, alinilipa wema kwa kuondoa uhai kwa tamaa ya kuwa na nguvu lakini hakufanikiwa kuzipata hizo nguvu, ni kwasababu nilizificha kanuni zake"
"Ooh ni hadithi ya kuhuzunisha iliyoje!" aliongea Jimmy huku akionyesha sura ya masikitiko
"Kijana unadhani nakwambia haya yote ili unisikitikie?"
"Hapana nakuhurumia tu mzee hakuna cha ziada, hata hivyo nimejifunza kitu kupitia maneno yako"
"kwamba?"
"No one can claim something truly precious without sacrifice. The greater the treasure, the higher the price" aliongea jimmy akimaanisha "Hakuna anayeweza kupata kitu cha thamani bila ya sadaka/kafara. Kadiri hazina inavyokuwa kuu, ndivyo gharama inavyokuwa kubwa"
"Safi sana kijana inaonekana una akili sana nadhani unafaa kuwa mrithi wangu"
" Sitaki kuwa mchawi mimi mzee" aliongea jimmy na kumfanya mzee acheke
"Watu mnatafsiri uchawi kwa namna tofauti sana ila kwa tasfiri yangi namaanisha nguvu zisizo za kawaida simaanishi kurogana na kuwangiana usiku uchi kijana"
"Mimi sioni tofauti yoyote uchawi ni uchawi tu kama uchawi mwingine" jimmy alikazia na mzee huyo alitabasamu na kusimama
"Unafanya nini?" Jimmy aliuliza naye akisimama
"Nakuonesha nguvu halisi niliyo nayo" aliongea yule mzee na kusogea umbali wa mita kumi na alipo jimmy
"Gravitas Inversus!" alinena kilugha na palepale gravity iliongezeka upande aliosimama jimmy ni kama kuna nguvu inamkandamiza kwenda chini na alianguka akipiga magoti, kila akijaribu kunyanyukka anashindwa, alifanya kila awezalo lakini wapii
"We mzee ndo nini sasa kunisababishia ha...." aliongea kwa tabu
"Gravitas Relinquere!" alinena tena yule mzee na kufanya ile hali kusitisha
"Vipi bado unakataa kurithi nguvu zangu?" alimuuliza Jimmy
Upande wa jimmy ambaye alikuwa amechoka na mwili kumlegea alikubali na kutamani sana kuijua nguvu hiyo na kumfanya mzee Salazar acheke
Alijiambia kuwa na nguvu ya ajabu kama hiyo kutamfanya aweze kuwalinda awapendao hakutaka lile kosa kujirudia kiasi cha kutaka kuondolewa uhai
"Unaweza kujifunza na kurithi nguvu zote lakini ni kwa sharti moja"
"Masharti tena mbona umegeuka kuwa mganga ghafla!"
"Nimesema sharti sio masharti"
"Lipi hilo"
"Unapaswa kunisujudia" aliongea mzee Salazar na kumfanya Jimmy acheke kama chizi mpaka kupaaliwa na mate
TO BE CONTINUED............
JIMMY YUPO KWENYE ULIMWENGU MWINGINE KUPITIA NDOTO BAADA YA KUSINZIA😁😁
ENDELEA KUFATILIA SIMULIZI HII TARATIBU NDUGU MSOMAJI, SIMULIZI BADO YA MOTO SANA🔥🔥
SOLO KING: ANCIENT LEGACY
CHAPTER 10: Salazar Solren Soledad
Upande wa Jenerali hakuwa na mabadiliko yoyote zaidi ya kutoa tabasamu tu maana alishaizoea hali hiyo kutoka kwa mwanae.
"Wewe mtukutu ifike muda uonyeshe heshima kwa wakubwa zako" aliongea Jenerali huyo na kumpotezea
Aliwaangalia wengine walioko lakini zaidi macho yake yalitua kwa Jimmy ambaye pia alikuwa akimuangalia
"Samahanini kwa ujio wangu wa ghafla mahali hapa sijaja kwa kutibua amani bali nimekuja kwa nia njema kabisa mimi ni Jenerali Johnson Merizesta mkuu wa majeshi ya ulinzi wa nchi, nina muda mchache kuwepo hapa, lengo ni kuzungumza na Jimmy Julian Jairo" alijitambulisha na kusema dhumuni la kuja mahali hapo
"Kuweni na amani sitochukua muda mrefu sana kwa mgonjwa" aliendelea kuongea na kuwaomba wawapishe kidogo, maongezi mengine ni siri. Nani wa kumpinga Jenerali kwa mfano? Kila mmoja alitoka nje wakibaki watano tu, Jenerali, walinzi wake pamoja na jimmy
Jenerali alivuta kiti na kwenda kukaa pembeni kidogo akikunja nne
"Upo unajiuliza kwanini mkuu wa majeshi amekutembelea si ndio?" aliuliza
"Najiulizaje ilihali umeshasema unahitaji mazungumzo na mimi mzee Jenerali" aliongea Jimmy na kumfanya Jenerali aachie tabasamu
"Unajua maongezi gani ambayo yamenitoa makao makuu mpaka kuja hapa hospitalini kwa raia wa kawaida kama wewe?"
"Mkuu nitajuaje bila ya wewe mwenyewe kuniambia isitoshe mimi sio malaika mpaka kujua kila kitu"
"Hahaha! Napenda vijana jasiri kama wewe, mara nyingi nikiongea na watu huwaga waoga sana na kuchagua maneno ya kuongea lakini kwako wewe ni tofauti.... just like your father"
"Unamjua baba yangu?" Jimmy aliuliza akiwa amekunja sura yake
"Ndio alikuwa rafiki yangu jeshini, niseme tu baba yako alikuwa ni mtu muhimu sana ya jeshi lakini inasikitisha ha......." aliacha sentensi yake ieleee hewani
"Anyway hilo sio lengo langu la kuja hapa"
"Lengo lililokuleta ni lipi?" Jimmy aliuliza na Jenerali alitoa ishara na mmoja wa walinzi alitoa faili na kumpatia
"Unamfahamu huyo?" Jenerali alimuuliza baada ya kumpatia faili na Jimmy alikubaliana naye
"Ndio huyu ni mzee wangu nilikuja kujua Jina lake halisi ni Momochi Saizo juzi-juzi" alijibu na Jenerali alimpatia faili jingine tena
"Unamfahamu huyo?" aliuliza tena na Jimmy baada ya kulitazama faili alikataa
"Hapana simfahamu huyu"
"Angalia vizuri usiangalie sura angalia majina"
"Unataka kusema?" Jimmy alipatwa na mshangao kidogo baada yakugundua kitu
"Nadhani ushaelewa sasa hao wote ni mtu mmoja"
"Kama ni mtu mmoja ipi ni sura yake halisi?"
"Kuhusu sura yake halisi hilo nalo ni shaka jingine amekuwa akiishi nchi tofauti tofauti kwa sura tofauti, tumeweza kupata taarifa hiyo kwa msaada wa Uingereza kwamba yupo nchini" aliongea Jenerali
"Sawa, lakini nini maana ya kuniambia hizi siri za jeshi? Jimmy aliuliza
" Inashangaza eeh? Huyo ni "Former ninja assasin" yaani alikuwa na alitekeleza mauaji mengi sana kutoka mataifa tofauti na katika kustaafu kwake alipotea kusikojulikana na hivi karibuni aliweza kugundulika nchini humu baada ya msako wa muda mrefu. Umekuwa ukiishi na mtu hatari kwa muda mrefu"
"Mzee ana siri sana yule Mkuu sishangai"
"Kingine ameuawa na kundi lake la kininja alilokuwa akilihudumu kwa muda mrefu cha kushangaza uliweza kudili nao na kuwamaliza kwa maana hiyo umefanya kazi ambayo kitengo chetu kilipaswa kufanya"
"Kidogo nipoteze uhai wangu, niseme ni bahati tu"
"Ni kundi daraja B lijulikanalo kama Yami no Senshi lenye maana ya Warriors of Darkness ni kundi lenye maninja wasomi wanaojificha kwenye vivuli/giza" alieleza kwa kifupi
"Kwahiyo unataka kusemaje Mkuu?" Jimmy aliuliza na kumfanya anyanyuke na kusimama akiachia tabasamu
"Ninakukaribisha kujiunga na Jeshi letu ninaamini kwa uwezo wako ulionao tukikuongezea ujuzi utalisaidia taifa kwa namna nyingi sana"
"Asante lakini sivutiwi na kuwa mwanajeshi" alijibu Jimmy
"Usiwe na haraka ya kutoa jibu haraka je hutaki kuwa na heshima kama ya baba yako? hutaki kujua nini sababu ya baba yako kutangulia mbele za haki?"
"Kwasababu ya baba yangu kuwa mwanajeshi haimaanishi na mimi nitataka kuwa kama yeye kingine nachojua ni kwamba baba yangu alikufa kwa ajali, hata kama isingekuwa ajali bado kazi yake ni ngumu kutoka salama... Asante sana kwa ofa hiyo mkuu lakini jibu langu ni hapana"
"Kijana acha kukurupuka ni ngumu sana Mkuu wa majeshi kumualika raia ndani ya jeshi bila utaratibu" aliongea mmoja aa walinzi lakini jimmy alitingisha kichwa kukataa
"Sawa sitokulazimisha kijana kuheshimu uamuzi wa mtu ni jambo muhimu sana" aliongea Jenerali na kuzipiga hatua zake kuondoka alipoukaribia mlango alisita
"Ooh nimekumbuka" aliongea Jenerali na kumgeukia Jimmy "Una sbukrani zangu za dhati kijana umeiokoa familia yangu, hilo nashukuru" aliongea na kuondoka zake akimuacha Jimmy katika hali ya kutafakari
Ndugu zake waliingia mara baada ya Jenerali na jeshi lake kuondoka, wa kwanza kutangulia alikuwa ni Cid akifuatwa na Monica, Bianca na Mamaye
"Bro huyo mzee alikuwa anakwambia nini?" Cid aliuliza na kila mtu alitega masikio kusikiliza na Jimmy alitoa kicheko na kuwaangalia mmoja baada ya mwingine
"Amekuja kunipa pole tu na kutoa shukrani" alijibu
"Shukrani za nini?" Cid aliuliza na wengine kutingisha kichwa kukubaliana na swali lake
"Nenda kamuulize si mzee wako yule halafu kumbe ni mkuu wa majeshi asee"
"Kuhusu hilo hapana kwakweli bro fanya ututonye ndugu zako basi" aliendelea kumtaka amuelezee lakini Jimmy aliendelea kukomalia kwamba akamuulize mwenyewe na mpaka kufika jioni saa kumi na mbili walizungumza mengi na waliaga kwakuwa muda wa kutembelea wagonjwa umeisha
Kama kawaida baada ya wote kuondoka wakikwishakumuaga aliuchapa usingizi kama maiti vile.
°°°°°°°°°°
Jimmy alijikuta yuko mahali pasipojulikana ni wapi akiwa peke yake
Mahali hapo kulikuwa ni patupu kupita maelezo, ardhi yake ilikuwa ni tambarare yenye mchanga mweupe kama wa baharini, anga nalo lilikuwa ni la buluu safi lisionekane wingu hata moja
Wakati anajiuliza yuko wapi mara alisikia sauti kama mwangwi ikinena
"Welcome to my world young man" ilikuwa ni sauti yenye kusikika vyema masikioni mwa mtu yeyoteikimaanisha karibu katika ulimwengu wangu kijana
"Where am I and who are you?" aliuliza kwa lugha sawasawa na aliyoisikia akimaanisha Niko wapi na wewe ni nani
"I am Salazar Solren Soledad, Sovereign of the Arcane, The Forbidden Monarch of ancient knowledge, The Sorcerer, The Enchanter, Spellweaver, The Ancient legacy" sauti ilijitambulisha ikimaanisha "Mimi ni Salazar Solren Soledad, mtawala wa uchawi wote, Mfalme wa maarifa ya kale, Sorcer(mchawi), Enchanter(mchawi), spellweaver(mchawi wa spells), Uridhi wa kale"
Upande wa Jimmy licha ya utambulisho huo hakuelewa chochote licha ya kujua kingereza, aliishia tu kukaa chini akijikuna kichwa chake
"Unaonekana hujanielewa bado kijana" ilisikika tena sauti hiyo
"Unajua kuzumgumza kiswahili?" jimmy aliuliza
"Ninafahamu lugha nyingi sana kuliko unavyofikiria"
"Kumbe! Unaweza kuniambia kwanini niko hapa"
"upo hapa kwasababu unakwenda kuwa mrithi wangu"
"Mrithi? Usinitanie we mzee kwanza kwanini unajificha" aliongea jimmy na sekunde anamaliza kauli yake alihisi kuna mtu yuko nyuma yake na aligeuka haraka lakini hakumuona mtu na ile anarudisha kichwa chake tu anakutana na sura ambayo ilimshtua kiasi cha kuruka kama wadada wanavyorukia juu ya kochi baada ya kumuonda mende akiwakaribia
Alikuwa ni mzee mwenye sura iliyojikunja kiasi cha sura yake kumtisha yeyote atakaye muangalia kwa mara ya kwanza, meno yake nayo yalikuwa ni ya njano yenye mapengo yasiyo na idadi ya kueleweka, sasa vuta picha ndugu msomaji jinsi mzee huyo alivyo, kibaya zaidi alikuwa akitabasamu
"Sikujificha, sijajificha na sijawahi kujificha" aliongea mzee Salazar akivalia joho jeusi refu lililofunika mikono yake na miguu yake
Jimmy alivuta pumzi ndefu na kuzishusha akimtazama mzee huyo aliyekuwa akimtazama pia
" Unaweza kuniambia kwanini nipo hapa?" jimmy aliuliza
"Unataka kujua kwanini?"
"Ndio"
"Kaa chini kwanza" alimwambia aketi chini na Jimmy alikaa pamoja na huyo mzee
"Umekiona hiki kitabu" aliongea mzee Salazar baada ya kunyanyua mkono kumuonyesha na ghafla kitabu kilijitokeza kichawi hali iliyomfanya Jimmy kushangaa na kukunja ndita
"Kilitaka kunitoa uhai wangu na kusababishia familia yangu kutekwa bila kusahau mzee wangu Momochi ametangulia mbele za haki kwa sababu ya hako kakitabu ka kipuuzi"
"Hapana hiki kitabu sio upuuzi umepitia yote hayo ni kwasababu ya kile kilichomo humu"
"kilichomo my foot! Unataka kuniambia bizo kurasa tupu zilizomo humo ndio zilikuwa zikitafutwa" Jimmy aliongea kwa hasira alitamani jata kutukana lakini alikuwa akiogopa hata yeye mwenyewe alijishangaa kwanini anaogopa
"Fungua" aliongea mzee Salazar akimpatia kitabu na kutaka akifungue.
Jimmy alikipokea na kukifungua na alishangaa kukikuta kimeandikwa lugha zisizoeleweka tofauti na mwanzo ambapo hakukuta maandishi yoyote
Jimmy alimwangalia mzee huyo kwa sura yenye maswali na kutaka maelezo
"Hizo ni lugha za kale ambazo zimesahaulika katika dunia hii sababu ya wewe kutokuta maandishi ni kwasababu niliyaficha na kwasababu ya agano nililoliweka nilipokaribia kufa"
"kwamba damu ya awaye yote itakayomwagika katika kitabu hiki huyo ndiye atakayekuwa mrithi wangu atake asitake ndipo roho yangu ipumzike kwa amani..... "
"Umesema ulipokaribia kufa sasa mbona mpaka sasa hujafa" Jimmy alimkatisha
"Tulia kijana, subiri nimalize ndiyo uulize maswali yako ila ngoja nikujibu hilo kabla ya kuendelea. Mimi nilikwisha kufa kitambo mimi ni roho iliyokataa kwenda mahali pake kwasababu ya kudhulumiwa uhai wangu" aliongea mzee Salazar na Jimmy kufunga mdomo wake
"Hapo zamani nilikuwa ni mchawi mwenye nguvu sana na mwenye maarifa mengi ambayo ambayo mpaka kwenye dunia ya sasa hayapo"
"Unasema ni mchawi mwenye nguvu ilikuwaje sasa ukafa lakini sasa upo hai"
"Watu tunakufa kwa njia nyingi sana, inaweza kuwa ajali, magonjwa, kuuawa. na vifo vingine vinatokea bila sababu yoyote si ajali, si ugonjwa wala chochote kilichosababisha unajikuta tu unakufa, ila unajua ni kifo gani kinaumiza?" alimuuliza jimmy
"Sijui"
"Ni kile kifo cha kuuawa hasa kwa mtu ambaye hukutegemea atakuja kufanya hivyo, na mtu huyo ni mwenye kujua siri zako na udhaifu wako na kuzitumia kukuondosha kwenye uso wa dunia. Na mara nyingi mtu huyo ni mtu wa karibu sana kwako anaseza kuwa mpenzi wako unayemuamini, rafiki yako wa karibu na hata mwanafamilia wako." aliongea mzee Salazar na kunyamanza kidogo akimeza mate kisha kuendelea
"Yote hayo huanzia kwenye wivu, kijana unapaswa kujua wivu ni mbaya sana, Wivu husababisha tamaa na chuki na kwasababu ya chuki na tamaa za kijinga ndiyo husababisha kuuana"
Jimmy alikuwa kimya tu akimsikiliza mzee huyo kana kwamba yupo kanisani akipata mahubiri.
"Nimeuawa na mtu ambaye sikumtegemea, mtu ambaye nilikuwa nikimjali sana na kuhakikisha hapati tabu lakini ndiyo hivyo shukrani ya punda ni mateke, alinilipa wema kwa kuondoa uhai kwa tamaa ya kuwa na nguvu lakini hakufanikiwa kuzipata hizo nguvu, ni kwasababu nilizificha kanuni zake"
"Ooh ni hadithi ya kuhuzunisha iliyoje!" aliongea Jimmy huku akionyesha sura ya masikitiko
"Kijana unadhani nakwambia haya yote ili unisikitikie?"
"Hapana nakuhurumia tu mzee hakuna cha ziada, hata hivyo nimejifunza kitu kupitia maneno yako"
"kwamba?"
"No one can claim something truly precious without sacrifice. The greater the treasure, the higher the price" aliongea jimmy akimaanisha "Hakuna anayeweza kupata kitu cha thamani bila ya sadaka/kafara. Kadiri hazina inavyokuwa kuu, ndivyo gharama inavyokuwa kubwa"
"Safi sana kijana inaonekana una akili sana nadhani unafaa kuwa mrithi wangu"
" Sitaki kuwa mchawi mimi mzee" aliongea jimmy na kumfanya mzee acheke
"Watu mnatafsiri uchawi kwa namna tofauti sana ila kwa tasfiri yangi namaanisha nguvu zisizo za kawaida simaanishi kurogana na kuwangiana usiku uchi kijana"
"Mimi sioni tofauti yoyote uchawi ni uchawi tu kama uchawi mwingine" jimmy alikazia na mzee huyo alitabasamu na kusimama
"Unafanya nini?" Jimmy aliuliza naye akisimama
"Nakuonesha nguvu halisi niliyo nayo" aliongea yule mzee na kusogea umbali wa mita kumi na alipo jimmy
"Gravitas Inversus!" alinena kilugha na palepale gravity iliongezeka upande aliosimama jimmy ni kama kuna nguvu inamkandamiza kwenda chini na alianguka akipiga magoti, kila akijaribu kunyanyukka anashindwa, alifanya kila awezalo lakini wapii
"We mzee ndo nini sasa kunisababishia ha...." aliongea kwa tabu
"Gravitas Relinquere!" alinena tena yule mzee na kufanya ile hali kusitisha
"Vipi bado unakataa kurithi nguvu zangu?" alimuuliza Jimmy
Upande wa jimmy ambaye alikuwa amechoka na mwili kumlegea alikubali na kutamani sana kuijua nguvu hiyo na kumfanya mzee Salazar acheke
Alijiambia kuwa na nguvu ya ajabu kama hiyo kutamfanya aweze kuwalinda awapendao hakutaka lile kosa kujirudia kiasi cha kutaka kuondolewa uhai
"Unaweza kujifunza na kurithi nguvu zote lakini ni kwa sharti moja"
"Masharti tena mbona umegeuka kuwa mganga ghafla!"
"Nimesema sharti sio masharti"
"Lipi hilo"
"Unapaswa kunisujudia" aliongea mzee Salazar na kumfanya Jimmy acheke kama chizi mpaka kupaaliwa na mate
TO BE CONTINUED............
JIMMY YUPO KWENYE ULIMWENGU MWINGINE KUPITIA NDOTO BAADA YA KUSINZIA😁😁
ENDELEA KUFATILIA SIMULIZI HII TARATIBU NDUGU MSOMAJI, SIMULIZI BADO YA MOTO SANA🔥🔥