By Samuel jk_Euphoria
SOLO KING: ANCIENT LEGACY
CHAPTER 14: Nina ndoto tofauti ya kutimiza, kuimba kutabaki kuwa hobby yangu
Macho yalikuwa ni mengi sana yakiangalia upande wa meza waliyokaa Jimmy na wanafamilia wake.
Jimmy aliupamba uso wake kwa tabasamu na kusimama akielekea mbele alikoitwa akisindikizwa na macho ya wengi kana kwamba ni supa staa kumbe ni mshikaji mmoja tu ambaye bahati humuangukia mara kwa mara
Mbeleni kulikuwa ni kijukwaa kidogo ambacho Cid alisimama, Jimmy alipomkaribia alikumbatiana nae kishkaji kwa bega moja na kabla hajaachia mkono alimnong'oneza
"Thatās a wonderful speech, but why me?" (Hio ni hotuba nzuri sana lakini kwanini mimi) alimnong'oneza na Cid aliishia kumtolea tabasamu tu na kumpatia Mic
Alikusanya ujasiri na kusafisha koo yake vizuri kisha kusogeza mic karibu na mdomo tayari kwa kuongea
" Sio mbaya nikiruka salamu na utambulisho maana tayari wote mnajua naitwa Jimmy kama nilivyotambulishwa, Pia ningependa kumshukuru rafiki yangu kwa maneno mazuri aliyosema kunihusu. Ukweli ni kwamba, sikufanya yote hayo kwa kutegemea shukrani au malipo nilifanya kwa sababu ilikuwa jambo sahihi kufanya.
But you know, life works in many mysterious ways, Back then, I had no idea that the person I helped would one day become a close friend, niwe mkweli tu kama rafiki sijaja na zawadi kwenye siku yake maalum kwa sababu ya kukosa maokoto haha" Jimmy aliongea kiswainglish akitoa na kicheko na kufanya baadhi yao kucheka wengine kutoa tabasamu kisha aliendelea
"Kwakuwa ameniomba na kunitaka hivyo sio mbaya nikachukulia kama zawadi yangu kwake naona haitakuwa haki kumkatalia"
Jimmy alirudishia mic Cid, uzuri maandalizi yalishafanyika kitambo kulikuwa na kinanda jukwaani pamoja na guitar na vifaa vingine vya muziki kwaajili ya band zilizoalikwa kutumbuiza
Alikwenda na kuchukua guitar(gitaa) moja rangi ya chungwa brand ya Corodoba C5, ni gitaa iliyoundwa kwa mtindo wa jadi wa Kihispania na lina bracing ya feni, inayosaidia kutoa sauti yenye nguvu na endelevu.
Alivuta stuli ndefu iliyojukwaani na kuketi juu yake akikunja nne kisha kuiweka gitaa vyema tayari kwa kuicheza, alikuwa katika utulivu wa hali ya juu sana
Na mdogo mdogo alianza kuchezesha vidole na sauti nyororo ilisikika vyema masikioni mwa watu huku akiimba wimbo aujuao yeye, alikuwa akicheza mtindo flani wa mziki wa gitaa uitwao "Cavatina"
Cavatina ni mtindo ulioundwa na mwana muziki wa filamu kutoka uingereza aitwaye Stanley myers miaka ya 1960s, ni mtindo wa muziki unaowakilisha hisia na kujieleza, ni mtindo wa taratibu wenye kuukonga moyo wa yeyote asikilizaye, hasa kama msikilizaji ni mpenda nyimbo za taratibu
Sababu ya Jimmy kuamua kucheza huo mtindo ni kwasababu ya wimbo aliokuwa akiimba, ni wimbo uliokuwa ni kama storytelling flani hivi, ni kama alikuwa akihadithia alivyokutana na Cid na hakutegemea kama wangekuja kuwa marafiki siku za mbeleni kwa njia ya kuimba, pia wimbo uliokuwa na shukrani ndani yake. Ukiniuliza ni shukrani gani mimi sijui.
Sauti nayo ilikuwa ni nzuri na yenye kuvutia sana, kwa jinsi alivyokuwa hapo jukwaani ni kama supa staa flani hivi akitumbuiza kwenye birthday ya Cid.
Upande wa Monica na mama yake walikuwa kwenye mshangao, ilikuwa ni mara yao ya kwanza kumshudia jimmy akiimba na kucheza gitaa kwa ustadi sana, upande wa Bianca naye alikuwa akimtazama Jimmy kwa hisia mchanganyiko isieleweke anahisi nini moyoni
Mpaka anakuja kumaliza kuimba watu walimpigia makofi wakionyesha kumkubali na Cid aliyekuwa pembeni yake alimsogelea na kumpongeza huku akimnong'oneza masikioni
"Leo lazima wadada wakugombanie bro yaani kwa staili hii sidhani kama umewaacha salama mioyoni mwao" alinong'ona Cid
Basi baada ya hapo sherehe ilianza kama kawaida, nisiongelee sana yaliyotokea ila kifupi sherehe hiyo ilikwenda vizuri, watu walikula wakashiba na blah blah blah
"Mdogo wangu sikujua kama una kipaji kiasi hiki" aliongea Monica baada ya kumaliza kula
Jimmy hakujisumbua kumjibu badala yake yeye alikuwa akibebe tonge la pilau na kulisindilia mdomoni hakuwa na haja ya kutumia kijiko, mkono wake wa kulia ulimtosha kabisa kushughulika na msosi
"Wewe Jimmy hivi ushibi? Ni sahani ya tano hio kama sikosei?" aliongea mama yake akimshangaa mwanae maana hakuwahi kumuona akila chakula kingi kiasi
"Na mchana alikula sahani tatu huyu" Monica alichomekea
"Hata mimi sielewi mama najikuta tu nina njaa" aliongea huku akiendelea kula chakula huku Bianca akimshangaa asitie neno lolote
Mara katika meza yao aliongezeka mtu mwingine, alikuwa ni Sophia na haikueleweka amekuja kufanya nini hapo.
"Samahanini nahitaji maongezi na huyu kijana" aliongea Sophia akimnyooshea kidole Jimmy
Jimmy sasa ndiyo alikuwa akimalizia tonge la mwisho la pilau na baada ya kumaliza alichukua maji ya chupa yaliyokuwa kwenye meza na kunywa yote mfululizo huku sauti ya maji kupita kooni ilisikika, alipomaliza alinyanyuka na kwenda kunawa kisha kurudi
"Oh mimi? Haina shida kwahiyo tunaongea wapi au ni hapahapa?" aliliza Jimmy na Sophia aliongoza njia
"Nitarudi" Jimmy aliwaambia wenzake na kumfuata Sophia nyuma
"Vijana wa siku hizi hawanaga muda wa kusalimia wakubwa zao" aliongea Mamaye kwa kutingisha kimasikitiko baada ya Jimmy na Sophia kuondoka, Monica na Bianca waliungana naye kusikitika
Watu walikuwa wakimuangalia Jimmy ambaye alikuwa akimfuata Sophia kwa nyuma, nadhani walikuwa wakijiuliza imekuwaje mpaka kijana huyu akiongozana mrembo Sophia ilihali wao hata ujasiri wa kumsogelea hawakuwa nao
Walienda mpaka ndani ya nyumba na kwenda sebuleni
"Unaonaje tukasahau yaliyopita.... Jimmy" Sophia aliongea baada ya kuketi kwenye sofa na kumpa Jimmy ishara aketi
"Usiwaze sana mimi huwa siwekagi vinyongo kwenye vitu vidogo" Jimmy aliongea baada ya kukaa
"Oh sawa... Sijui kama unanifahamu ila sio vibaya kujitambulisha, Naitwa Sophia Merizesta na ndiye dada mkubwa na mzaliwa wa kwanza kwenye hii familia" aliongea akijitambulisha
"Unajua lengo la mimi kukuleta mpaka hapa?" Sophia aloiliza
"Umesema unahitaji maongezi na mimi" aliongea Jimmy akijiambia huyu bibie ni kama baba yake tu kuzunguka zunguka tu badala ya kwenda kwenye point
"Yes nataka tuongee biashara, lakini kabla ya kuanza ningependa kutoa shukrani zangu kwa uliyoyafanya, sikudhani mtu yule tuliyekutana bar na kutofautiana angekuwa ndiye mwokozi wa ndugu zangu, I owe you one" aliongea Sophia
Japokuwa Sophia alikuwa ni mwanamke mwenye kujisikia sana lakini likija suala la familia yake alikuwa ni tofauti na yule mwenye nyodo, alikuwa akiwajali ndugu zake ni sawa na kusema kwa nje anaonekana mgumu sana ila ndani ni mwepesi hivyo aliguswa na wema wa Jimmy
"Nilishasema sikufanya yote nikitegemea shukrani au malipo yoyote hivyo suala la wewe kuwa na deni sahau isitoshe mtu yeyote angefanya vile"
"Kama nilivyosikia kuwa wewe ni mgumu sana kama kwa mama yangu ulikataa shukrani sidhani kama kwangu utakubali pia, anyway tuzungumze biashara"
"Nakusikiliza" Jimmy aliuliza
"It's an offer, just then I saw you perform on stage out there and I have to say you truly are a talent, A raw natural talent that my industry is always looking for. And I happen to be in a position to offer you an opportunity that most people would dream of.ā aliwasilisha Ofa yake kwa kingereza safi cha kwa mfalme Charles III akimaanisha "Ni ofa, mara tu nilikuona ukitumbuiza kwenye jukwaa huko nje na lazima niseme ukweli wewe ni talanta, Kipaji cha asili ambacho tasnia yangu inatafuta kila wakati. Na nimetokea kuwa katika nafasi ya kukupa fursa ambayo watu wengi wangeitamani.ā
"I hear you" Jimmy aliitikia akimaanisha anamsikia
"I run Sonic Bloom Records Weāre one of the biggest labels in the country, responsible for shaping some of the top artists in the industry. We provide the best producers, world-class management, and a platform that guarantees success." (Ninaendesha Sonic Bloom Records Sisi ni mojawapo ya lebo kubwa zaidi nchini, inayohusika na kuunda baadhi ya wasanii wa juu katika tasnia. Tunatoa watayarishaji bora zaidi, usimamizi wa kiwango cha kimataifa na jukwaa linalohakikisha mafanikio) aliisifia label yake na kuendelea
" I see potential in you. If you sign with us, weāll take your music to heights you never imagined. Your name, your voice it could be everywhere" akimaanisha Naona uwezo ndani yako. Ukijiunga nasi, tutaupeleka muziki wako katika kiwango ambacho hukuwahi kufikiria. Jina lako, sauti yako vitasikika kila mahali.
"āI appreciate the offer, But Iām not interested.ā alikataa kistaarabu
" Usiwe na haraka jipe muda wa kufikiria hii fursa adimu sana kwa vijana kwenye tasnia ya muziki" Sophia alijaribu kumshawishi tena
"Naelewa lakini nimeshafanya uamuzi sio kwamba sipendi hapana nina ndoto tofauti ya kutimiza, kuimba kutabaki kuwa hobby yangu" Jimmy aliongea
Sophia alitabasam na kuongea "Endapo utabadili mawazo mlango wetu upo waz" kisha alinyanyuka na kumpa mkono ishara ya "handshake" naye alinyanyuka na kuupokea
"Wewe kijana yaani unikatalie kote kule lakini leo unalegeza kwa mwingine au kwasababu mimi ni mzee" ilisikika sauti ya mwanamke na kweli alikuwa ni mwanamke ambaye kwa kumuangalia alikuwa kwenye miaka ya mid 60s
Alikuwa katika tabasamu pembeni yake kulikuwa pia na mwanamke mwenzake ambaye bila shaka alikuwa ni mwanamama Velora
"Haha kumbe upo huku?" Jimmy aliuliza huku akijichekesha
"Nilikuona mda sana tu ila si unajua mambo ya koneksheni kijana" aliongea mwanamke yule
"Oh Kumbe ila sio mbaya vipi hali yake bibi?" Jimmy alimjulia hali
"Sio mzima mimi umenikatalia ofa yangu halafu unamkubalia mshindani wangu" aliongea mwanamama yule
"Hamna msimamo wangu ni ule ule tu kupeana mikono kusipe presha sana bibi utazeeka vibaya mno"
"Ma Jack unamjua huyu?" Mwanamama velora aliuliza
"Ndio huyu mtoto ana vipaji vingi sana hata familia yake haijui nishambembeleza sana lakini wapi" aliongea Ma Jack akisikitika na kuwaeleza alivyomjua
Ma Eliasi ni mama yake Sara na ambapo Sara ni mtoto wa pili kwake, Sara ni rafiki yake na Monica na kupitia Sara aliweza kumfahamu Jimmy
Alikuwa ni mfanya biashara wa Real Estate na Music industry nchini Tanzania na biashara yake ya muziki mshindani wake mkuu ni Sophia na ofa aliyokuwa akijaribu kumshawishi Jimmy akubali ni kuwa Producer wa label yake huku akimuahidi mshahara mnono lakini bila mategemeo alikataliwa kwa kisingizio kilekile alichomwambia Sophia
Hata Jimmy kule hotelini alipocheza piano mualiko alioupata ulikuwa ni kutoka kwa Ma Jack ambaye jina lake halisi ni Mrs Rose bayeye na jina lake maarufu kwa kumiliki label ya muziki nchini lilifahamika kama Bibi machina hivyo haikushangaza kwa Jimmy kumuita Bibi, hata hivyo alikuwa ni Bibi kweli, ni kule kufosi tu kuonekana kama kijana kwa kupaka mavipodozi
"Sikutegemea ile siku ungetoroka bila kuaga" alilalama Bibi machina alikuwa akimaanisha ile siku hotelini ambapo aliondoka alipokutana na Cid lakini Jimmy aliishia kujichekesha tu na kumwambia kwamba alijisahau kutokana na njaa
Wakati wakiendelea kuzungumza kirafiki Cid, Bianca, Monica na Mamaye waliongezeka. Muda ulikuwa umeenda sana na ilikuwa ni saa sita wengi wa waliokuja kusheherekea walikuwa washaondoka
"Bro nilikuwa nakutafuta kumbe umejificha huku na wazee" Cid alitania na aliishia kukatwa jicho na Bi machina pamoja na mama yake
Mara walionekana walinzi watatu wakiingia taratibu wasije wakaiangusha piano kubwa ya mbao ambayo walikuwa wameibeba, walienda kuiweka sehemu ambayo walielekezwa na ilikuwa humohumo sebuleni
"Leo mnashinda hapa kwakuwa muda umeenda, kuna vyumba vingi vya wageni na nishaongea na wenzako na wamekubaliana nami" aliongea Cid akimuangalia Jimmy
"Lakini kabla ya kwenda kulala lazima utupigie songi moja matata sana ili tulale vizuri au sio ndugu zangu" aliongea Cid akiwageukia wakina Monica na Bianca nao walitingisha kichwa kukubaliana nae
Monica alitaka kushuhudia umahiri wa mdogo wake kwenye kucheza piano maana alishachoka na ngojera za Cid za kumsifia na ndio alitaka kuona kwa macho yake na sio kuishia kusikia tu
Alijiambia hata kama Jimmy aliweza kucheza gitaa haimaanishi na piano ataweza, kifupi Monica alikuwa ni kama mafarisayo tu yaani mgumu kukubali licha ya kushuhudia kipaji mojawapo cha ndugu yake. Kati ya gitaa na piano, gitaa ni ngumu sana hasa kwa wanaoanza kujifunza tofauti na wacheza piano, sasa kama kitu kigumu amekiweza kwanini kirahisi isiwezekane? Ni vile tu aliamua kuwa mgumu kukubali
"Bro ina maana zawadi yangu haikutosha?" aliongea Jimmy huku akikunja sura aliona huyu rafiki yake ni msumbufu sana
"Kwanini usituburudishe kidogo Jimmy nataka kujionea kipaji chako kwenye kucheza piano" aliongea mwanamama Velora na wote walitingisha kichwa kukubaliana naye isipokuwa Sophia tu na walinzi
Jimmy aliishia kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha, alianza kujilaumu kwanini hakuondoka mapema, kingine alikuwa ameshiba sana hivyo alihitaji kupumzika
Alikubali kishingo upande na kwenda kukaa kwenye piano, na wengine wote walikwenda kukaa kwenye sofa wakitega masikio yao
Ile Jimmy anataka kuanza tu zilisikika sauti za vishindo vizito vilivyomshtua kila mtu
"BAM! BAM! BOOM!
TO BE CONTINUED.............