Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,170
- Thread starter
- #241
SEHEMU YA 61
Amina hakutaka kabisa kuwasiliana na Dickson kwa kuwa kile alichoambiwa na Linda akifanye alikifanya kwa mafanikio makubwa. Moyo wake ukaridhika na hivyo kuendelea na maisha yake.
Picha ya Dickson haikutoka kichwani mwake, alimpenda mwanaume huyo kwa moyo wa dhati, tabasamu lake lilikichanganya kichwa chake na muda mwingi alikuwa akipambana kumtoa kijana huyo asikisumbue kichwa chake lakini ilishindikana kabisa.
Kwa kitendo chake cha kuacha kuwasiliana na Dickson kilimuuma mno, kwake, mwanaume huyo alionekana kuwa kama malaika ambaye hakutakiwa kupotezwa na mwanamke yeyote yule.
Kuwa na Dickson, hakukuhitaji pesa kwani kumwangalia yeye tu kuliyafanya maisha yako kuonekana kukamilika, hata kama unamiliki baiskeli tu, lakini kuwa naye ilikuwa ni sawa na kujiona ukimiliki Prado.
Hata kama ulikuwa na njaa ndani ya nyumba na hakuna chakula, kuwa na Dickson pembeni ilikuwa ni sawa na kuliangalia sinia pembeni lililokuwa na pilau la kutosha.
Moyo wake ulimuuma mno kutokuwasiliana na mwanaume huyo kwani kwake japokuwa alitembea na wanaume wengi lakini kwa Dickson alionekana kufa na kuoza.
Baada ya siku kadhaa akaamua kuweka laini yake kwenye simu yake kwani aliamu kuachana nayo kwa kipindi fulani baada ya kuona akitafutwa sana na Dickson.
Alipoiweka tu, kitu cha kwanza kilikuwa ni kuingia kwa meseji nyingi za mabwana zake na huku wengine wakilalamika kuachwa na wakati walikuwa kwenye mapenzi ya dhati.
Hakutaka kujali kuhusu meseji hizo, haraka sana akaenda WhatsApp na kulitafuta jina la Dickson, alipolipata, macho yake yakatua katika picha ya msichana fulani aliyekuwa amelala kitandani huku dripu ikining’inia juu yake.
Moyo wake ukamshtuka, picha aliyokuwa akiiona ilimtisha sana, aliiangalia kwa sekunde thelathini kisha kuingia katika sehemu ya ‘status’.
Amina hakutaka kabisa kuwasiliana na Dickson kwa kuwa kile alichoambiwa na Linda akifanye alikifanya kwa mafanikio makubwa. Moyo wake ukaridhika na hivyo kuendelea na maisha yake.
Picha ya Dickson haikutoka kichwani mwake, alimpenda mwanaume huyo kwa moyo wa dhati, tabasamu lake lilikichanganya kichwa chake na muda mwingi alikuwa akipambana kumtoa kijana huyo asikisumbue kichwa chake lakini ilishindikana kabisa.
Kwa kitendo chake cha kuacha kuwasiliana na Dickson kilimuuma mno, kwake, mwanaume huyo alionekana kuwa kama malaika ambaye hakutakiwa kupotezwa na mwanamke yeyote yule.
Kuwa na Dickson, hakukuhitaji pesa kwani kumwangalia yeye tu kuliyafanya maisha yako kuonekana kukamilika, hata kama unamiliki baiskeli tu, lakini kuwa naye ilikuwa ni sawa na kujiona ukimiliki Prado.
Hata kama ulikuwa na njaa ndani ya nyumba na hakuna chakula, kuwa na Dickson pembeni ilikuwa ni sawa na kuliangalia sinia pembeni lililokuwa na pilau la kutosha.
Moyo wake ulimuuma mno kutokuwasiliana na mwanaume huyo kwani kwake japokuwa alitembea na wanaume wengi lakini kwa Dickson alionekana kufa na kuoza.
Baada ya siku kadhaa akaamua kuweka laini yake kwenye simu yake kwani aliamu kuachana nayo kwa kipindi fulani baada ya kuona akitafutwa sana na Dickson.
Alipoiweka tu, kitu cha kwanza kilikuwa ni kuingia kwa meseji nyingi za mabwana zake na huku wengine wakilalamika kuachwa na wakati walikuwa kwenye mapenzi ya dhati.
Hakutaka kujali kuhusu meseji hizo, haraka sana akaenda WhatsApp na kulitafuta jina la Dickson, alipolipata, macho yake yakatua katika picha ya msichana fulani aliyekuwa amelala kitandani huku dripu ikining’inia juu yake.
Moyo wake ukamshtuka, picha aliyokuwa akiiona ilimtisha sana, aliiangalia kwa sekunde thelathini kisha kuingia katika sehemu ya ‘status’.