Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

SEHEMU YA 61

Amina hakutaka kabisa kuwasiliana na Dickson kwa kuwa kile alichoambiwa na Linda akifanye alikifanya kwa mafanikio makubwa. Moyo wake ukaridhika na hivyo kuendelea na maisha yake.

Picha ya Dickson haikutoka kichwani mwake, alimpenda mwanaume huyo kwa moyo wa dhati, tabasamu lake lilikichanganya kichwa chake na muda mwingi alikuwa akipambana kumtoa kijana huyo asikisumbue kichwa chake lakini ilishindikana kabisa.

Kwa kitendo chake cha kuacha kuwasiliana na Dickson kilimuuma mno, kwake, mwanaume huyo alionekana kuwa kama malaika ambaye hakutakiwa kupotezwa na mwanamke yeyote yule.

Kuwa na Dickson, hakukuhitaji pesa kwani kumwangalia yeye tu kuliyafanya maisha yako kuonekana kukamilika, hata kama unamiliki baiskeli tu, lakini kuwa naye ilikuwa ni sawa na kujiona ukimiliki Prado.

Hata kama ulikuwa na njaa ndani ya nyumba na hakuna chakula, kuwa na Dickson pembeni ilikuwa ni sawa na kuliangalia sinia pembeni lililokuwa na pilau la kutosha.

Moyo wake ulimuuma mno kutokuwasiliana na mwanaume huyo kwani kwake japokuwa alitembea na wanaume wengi lakini kwa Dickson alionekana kufa na kuoza.

Baada ya siku kadhaa akaamua kuweka laini yake kwenye simu yake kwani aliamu kuachana nayo kwa kipindi fulani baada ya kuona akitafutwa sana na Dickson.

Alipoiweka tu, kitu cha kwanza kilikuwa ni kuingia kwa meseji nyingi za mabwana zake na huku wengine wakilalamika kuachwa na wakati walikuwa kwenye mapenzi ya dhati.

Hakutaka kujali kuhusu meseji hizo, haraka sana akaenda WhatsApp na kulitafuta jina la Dickson, alipolipata, macho yake yakatua katika picha ya msichana fulani aliyekuwa amelala kitandani huku dripu ikining’inia juu yake.

Moyo wake ukamshtuka, picha aliyokuwa akiiona ilimtisha sana, aliiangalia kwa sekunde thelathini kisha kuingia katika sehemu ya ‘status’.
 
SEHEMU YA 62

Huko akakutana na picha za msichana mrembo aliyekuwa na sura yenye furaha huku kukiwa na ujumbe uliosindikizia picha hiyo uliosema ‘Nalikumbuka tabasamu lako’. Hakuishia hapo, picha zikaanza kubadilika na baada ya picha tatu, akamuona msichana huyo huyo akiwa amelala kitandani huku akiwa na dripu kwa juu yake.

Msichana huyo alikuwa Nandy. Alisikitisha pale alipokuwa, Amina mwenye hakuweza kuangalia kwa muda mrefu, akaitoa na kuangalia picha nyingine.

Huko ndipo akapata jibu ya kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Aliziona picha za Linda ambapo pia kulikuwa na ujumbe kuhusu msichana huyo, Dickson akimlalamikia kwa kulazimisha penzi na wakati hakuwa na mapenzi yake lakini mbaya zaidi, akaandika kwamba hakuogopa polisi hata kama alipanga kumfanyia jambo baya sana.

Hapo, akahisi kitu, akagundua kabisa kwamba inawezekana jambo baya alilokuwa akilizungumzia Dickson lilikuwa ni lile alilokuwa amemfanyia ambalo kwa kifupi walipokuwa chumbani wakifanya mapenzi ilionekana kama msichana huyo alikuwa akibakwa.

Moyo wa Amina ukamuuma kupita kawaida, hakuamini kama mipango ya msichana huyo ilikuwa hivyo. Hasira kali ikamkaba kooni, chuki ikajitokeza moyoni mwake dhidi ya Linda ambaye hakujua alikuwa mahali gani.

Ilipofika majira ya saa 2:06 usiku simu yake ikaanza kuita na alipoichukua na kuangalia jina, mpigaji alikuwa Linda. Kwanza akakunja sura yake, hakumpenda kwa kuwa alimfanya kushiriki katika jambo ambalo hakufahamu ni kwa namna gani video zile zingekwenda kutumia.

Akaamua kuipokea.
“Nini?” aliuliza Amina mara baada ya kupokea simu.
“Upo wapi?” lilikuwa swali kutoka kwa Linda.
“Nyumbani!”
“Nakwenda mahakamani kufungua kesi. Yule mshenzi amenibadilikia kwa sababu ya malaya wake,” alisema Linda huku sauti yake ikisikika kama mtu aliyekuwa na hasira mno.

“Mshenzi gani?”
“Dickson!”
“Weee! Dickson mshenzi! Mshenzi gani anakuwa na sura nzuri kama ile?” aliuliza Amina, yaani muda huo hakutaka kusikia lolote lile baya kuhusu Dickson.
 
SEHEMU YA 63

Linda akaanza kumuhadithia kila kitu kilichokuwa kimetokea. Alionekana kukasirika mno na moyo wake ulidhamiria kufanya jambo moja tu, kumfunga Dickson hata kama alikuwa na mapenzi makubwa kiasi gani juu yake.

Japokuwa Amina alishirikiana naye lakini katika jambo hilo hakutaka kushirikiana naye tena, moyo wake ulibadilika na kuhisi kabisa kwamba alihitajika kumsaidia Dickson hata kama Linda angepata mahakamani na kumshtaki mwanaume huyo.

Alichokisema Linda ndicho alichokifanya, siku iliyofuata akaamka asubuhi na mapema na kwenda katika Kituo cha Polisi cha Osterbay na kufungua jalada la kesi huku akimshutumu Dickson kwa kumbaka msichana ndani ya chumba cha hoteli.

Polisi hao wakataka kujiridhisha na hivyo kuangalia video ile. Kwa jinsi ilivyoonekana ilikuwa rahisi sana kujua kama Dickson alikuwa akimbaka Amina kitandani walipokuwa.

“Hii ni kesi kubwa sana! Huyu msichana yupo?” aliuliza polisi mmoja huku akimwangalia Linda.
“Amejaa tele!”

“Basi mlete kwanza tuzungumze naye.”
Hilo halikuwa tatizo kabisa kwa Linda, akawasiliana na Amina na kumwambia kilichokuwa kimetokea polisi na hivyo mtu aliyekuwa akihitajika alikuwa yeye tu.

Hakukuwa na tatizo lolote lile, kwa sababu tayari alikuwa amekula pesa za msichana huyo, hakuwa na jinsi kushirikiana naye. Siku hiyohiyo akaelekea katika kituo hicho cha polisi ambapo akawaambia polisi kwamba kweli alikuwa amebakwa na mwanaume huyo chumbani.

“Alikubaka hotelini?” aliuliza polisi mmoja.
“Ndiyo!”
“Duuh! Sasa wewe ulifuata nini kule?”
“Aliniita kwa ajili ya kuzungumza mambo ya biashara!”
“Mzungumzie chumbani?”
“Ndiyo!”
“Kitandani?”
“Ndiyo!”
“Hata akili yako haikuhisi chochote kile binti?”
“Hapana!”

“Basi kuna baadhi ya mishipa yako haifanyi kazi inavyotakiwa,” alisema polisi huyo kwa utani ulioonekana kuwa na shaka tele.
Haraka sana Amina akaandkika maelezo yake aliyoonyesha kwamba alibakwa na Dickson ambaye katika kipindi hicho hakuwa nchini Tanzania.
 
Huyu Dickson kanikumbusha mbaali sana!!!! Daaaah niliwahi kuokokaga kule kanusa tag msambweni tanga!! Kisa binti wa aliekuwa mchungaji hapo kanisan! Daah nkasikia sasa hiv huyo pastor Ni askofu!
 
Huyu Dickson kanikumbusha mbaali sana!!!! Daaaah niliwahi kuokokaga kule kanusa tag msambweni tanga!! Kisa binti wa aliekuwa mchungaji hapo kanisan! Daah nkasikia sasa hiv huyo pastor Ni askofu!
Mkuu kwahiyo sasa hivi umeachana na ulokole kabisa uliokoka sababu ya papuchi tu
 
[QUOTE="Shunie, post: 25794728, member:

“Mungu, naomba uniondolee jaribu hili, naomba by kijana huyu akilini mwangu,” aliomba Nandy kimoyomoyo.
“Mungu, huyu ndiye mwanamke sahihi, naomba unipe nafasi ya kuwa naye katika maisha yangu yote,” naye Dickson aliomba.

Kukawa kama na nguvu mbili zikawa zinashindana.

JE, nini kitaendelea?[/QUOTE]


acheni Mungu aitwe Mungu!! Huwa anasikia vitu vingi sana!!! Hapa angekuwa binadamu nadhani angechukua rushwa ili kukudhi takwa la mmojawapo!! Tuombe!!
 
SEHEMU YA 65

Moyo wake ulimuuma mno, hakuamini kama kweli yeye ndiye angethubutu kufanya kitendo kama kile, kwa sababu ya pesa, alikuwa tayari kufanya jambo lolote lile kumuangamiza mwanaume aliyekuwa akimpenda ambaye kwa kipindi hicho alikuwa kwenye hali mbaya baada ya mpenzi wake kupata ajali.

Alimuuliza maswali mengi Linda kuhusu Dickson lakini kwa wakati huo msichana huyo hakutaka kujibu chochote kile. Alishangaa kwani alihitaji kupata maelezo ya kina kabla hawajafika mpaka mahakamani lakini bado msichana huyo hakutaka kumpa ushirikiano.

“Linda...” aliita Amina.
“Naomba uniache kwanza. Nimechanganyikiwa mno,” alisema Linda huku akiendesha gari.
“Sawa. Hebu nijibu swali moja,” alisema Amina.
“Lipi?”
“Hivi kweli Dickson alikuwa mpenzi wako?”
“Ndiyo!”
“Na alikuwa akikupenda?”

“Ulisema swali moja, si ndiyo? Naomba nipumzishe kichwa changu,” alisema Linda na kutilia umakini katika uendeshaji wa gari lake.
Moyo wake uliwaka kwa hasira, hakuridhika japokuwa Nandy alikuwa kitandani akiteseka, alikuwa na uhakika kwamba msichana huyo angekufa kitandani pale lakini kwa kuwa Dickson alikuwa na msichana huyo, akakosa furaha mkabisa.

Alimfikisha Amina mpaka Manzese alipokuwa akiishi na yeye kuondoka zake. Njiani, hakuacha kumfikiria Dickson, alijua kwamba kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakiumia katika mapenzi lakini kwa maumivu aliyokuwa akiyasikia kipindi hicho, alijiona kuwa mwanamke wa kwanza aliyekuwa akiumia kuliko wote.

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 66

Ndege ikatua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Chennai uliokuwa nchini India. Haraka sana gari la wagonjwa kutoka katika Hospitali ya Apollo likasogezwa mahali husika na wazazi wa Dickson na mzee Gwamaka kuanza kuteremka.

Baada ya kufika chini, kitanda cha mgonjwa, Nandy kikaanza kuteremshwa kutoka ndani ya ndege huku Dickson akisaidiana na wahudumu wa ndege hiyo kumteremsha.

Baada ya kufikishwa chini, akaingizwa ndani ya gari la wagonjwa lililokuwa mahali hapo na safari ya kuelekea hospitalini kuanza.

Muda wote huo, Dickson alikuwa pembeni yake, moyo wake uliendelea kuwa kwenye majonzi tele, aliumia, hakukuwa na kitu ambacho kiliichanganya akili yake kama kuugua kwa mpenzi wake.

Hawakuchukua muda mrefu wakafika hospitalini, akateremshwa na kuanza kuingizwa ndani ya hospitali hiyo.
Kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kumpeleka katika chumba cha mapumziko kwa ajili ya madaktari kupitia ripoti yake ili kuangalia kwa undani tatizo lililokuwa likimkabili ambalo lilimfanya kuwa kitandani.

Baada ya nusu saa, jopo la madaktari kumi na mbili likakutana ndani ya chumba kimoja cha mkutano na kuanza kuijadili ripoti ya Nandy ambayo ilitumwa kutoka nchini Tanzania.

Kila daktari aliyeona ripoti ile alishtuka, hakukuwa na aliyeamini kama kungekuwa na mtu aliyepata majeraha makubwa ya uti wa mgongo kama ilivyokuwa kwa Nandy.

Uti wa mgongo ulivunjika hali iliyoonyesha kwamba ilikuwa ni lazima apooze kitandani pale alipokuwa. Kila mmoja alimsikitikia lakini hawakuwa na jinsi kwani kama uti wa mgongo ulivunjika vibaya namna ile, wasingeweza kuurudisha katika hali yake kwa kipindi kifupi, ingeweza kuchukua miaka zaidi ya hamsini mpaka kuwa sawa.

Uti wake wa mgongo ukagawanywa kwa sehemu kuu tatu. Sehemu ya kwanza ya juu ilikuwa ikianzia C1 hadi C4, sehemu hii waliiweka alama ya bluu na iliitwa High-Cervical Nerves iliyokuwa na pingili nne.
 
Hongera mtunzi, miongoni mwa story zenye kuvuta hisia na zenye mpangilio mzur sana wa matukio na yakifuatana kwa umakin.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom