Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

SEHEMU YA 54

Alishindwa kuyazuia machozi yake, moyo wake ulimuuma mno, akapata hasira kali dhidi ya Linda, japokuwa ilikuwa ni ajali tu lakini akahisi kama yeye ndiye aliyehusika katika ajali hiyo kwa kuwa tu hakumtakiwa kuwa na msichana huyo.
“Nandy!” aliita Dickson huku akimsogelea na kumwangalia vizuri.

Nandy hakuyafumbua macho yake, aliyafumba na kutulia, kwa jinsi alivyokuwa ametulia ilikuwa rahisi sana kusema kuwa msichana huyo alifariki dunia.
“Nandy...Nandy...Nandy! Forgive me,” (Nandy...Nandy...Nandy...nisamehe) alisema Dickson huku akitokwa na machozi.

Dokta hakutaka waendelee kubaki ndani ya chumba hicho, akawachukua na kutoka nao. Akaelekea nao ofisini na kuanza kuwaambia kuhusu mgonjwa wao.
Wote wawili walikuwa wakitokwa na machozi, waliumia, pamoja na kuwa katika hali ya huzuni lakini walitakiwa kuambiwa kitu kingine ambacho kingewatia huzuni zaidi.

“Kuna jambo jingine kuhusu mgonjwa wenu,” alisema Dk. Ndaki huku akiwaangalia kwa zamu.
“Tatizo gani?”
“Mgonjwa wenu....kwanza alipata ajali, donge la damu liliganda kwenye kichwa chake lakini tulifanikiwa kulitoa baada ya kumfanyia upasuaji wa kichwa. Ila kuna tatizo jingine ambalo mnatakiwa kulifahamu,” alisema dokta, hapo, akanyamaza, wote wakabaki wakimwangalia.

“Lipi?” aliuliza Dickson.
“Ni kwamba mgonjwa wenu amevunjika uti wa mgongo,” alisema dokta, wote wakabaki wakimwangalia.

“Uti wa mgongo kwa maana hatoweza.....”
“Kufanya lolote lile, atapooza, maisha yake yote yatakuwa kitandani tu,” alisema daktari, palepale kwenye kiti wote wawili wakaanza kulia kwa sauti kubwa kama watoto wadogo.

Je, nini kitaendelea?
 
Duh.... Nandy pole sana
Dick hayo ndio ulikuwa ukiyataka....bring back our Nandy akiwa anatembea
 
SEHEMU YA 55

“Eti uko wapi?” ilisikika sauti ya mwanamke kwenye simu.
“Kijiweni!”
“Upo na wenzako au?”
“Yeah! Kama kawaida yetu. Umeadimika sana, usharudi kutoka Uingereza?”
“Ndiyo! Kitambo fulani! Naomba tuonane kuna kitu nataka tuzungumze,” ilisikika sauti ya msichana huyo.
“Sawa.”

Aliyekuwa akiongea kwenye simu alikuwa msichana Linda. Moyo wake ulikuwa umewaka kwa hasira, hakutaka kukubali kuona kile ambacho kilitarajiwa kutokea kikitokea.
Alichokuwa akikifikiria ni kuupa moyo wake furaha ya milele, hakutaka kuona mtu yeyote anakuja na kuivuruga furaha aliyokuwanayo. Alijua kwamba alimpoteza Dickson kwa mara ya kwanza kabla ya kumrudia, hakutaka kuona akimpoteza kwa mara nyingine tena.

Alikuwa tayari kufanya kila kitu lakini mwisho wa siku kuwa na mwanaume huyo milele yote. Ili aishi kwa furaha, kulikuwa na mtu mmoja tu ambaye alitakiwa kuondoka duniani, huyo alikuwa Nandy.
Alikutana na kijana aliyekuwa amezungumza naye kwenye simu na kuanza kupanga mipango. Alichomwambia kijana huyo ni kwamba alitaka kumshuhudia Nandy akifa tu.

Alimwambia jinsi mipango ilivyotakiwa kufanyiwa kazi, yeye na wenzake walitakiwa kwenda mpaka chuoni na kumteka msichana huyo, waondoke naye na kwenda kumuua sehemu na mwili wake kuuweka kwenye kiroba.

Jamaa huyo aliyeitwa kwa jina la Hamisi akasikiliza maelezo ya Linda na kuona kabisa kungekuwa na ugumu wa kumuua msichana huyo kwa mauaji aliyokuwa ameyapanga, kama kweli walitaka kumuua basi wamuue kidigitali, kusiwe na mtu yeyote ambaye atagundua kama msichana huyo ameuawa.

“Kivipi?” aliuliza Linda.
“Tutengeneze ajali! Tumuue kwenye ajali, hilo tu,” alisema Hamisi.
Wazo hilo lkaingia kichwani mwa Linda na alichomwambia ni kwamba walitakiwa kulifanya jambo hilo haraka sana.

Akawapa picha ya Linda ambayo aliiba katika simu ya Dickson na hivyo Hamisi na wenzake kuanza kwenda chuoni kumtafuta msichana huyo.

Walipewa data zote kuhusu Nandy, hakukuwa na kitu kilichowachanganya, wakafanikiwa kumuona msichana huyo chuoni hapo na hivyo kuanza kujipanga kutekeleza adhima yao.
 
SEHEMU YA 56

Siku zikaendelea kukatika mpaka kufika siku ambayo walitakiwa kummaliza Nandy. Wakajigawa, kwa kuwa alikuwa akisoma chuo na kurudi nyumbani kwa usafiri wa bodaboda basi wangeweza kummaliza kwa kumgonga na gari.
Wakajipanga na magari yao, walitakiwa kufanya kila linalowezekana lakini mwisho wa siku majibu yatoke kwamba msichana huyo alikuwa amefariki dunia.

Walikuwa vijana sita, walijua kwamba msichana huyo alikuwa akiishi Kurasini hivyo kama alitakiwa kuondoka hapo ilikuwa ni lazima kutumia Barabara ya Mandela kuelekea nyumbani kwao.

Wakamweka mtu mmoja kwenye gari alilolipeleka mpaka Mabibo Hostel, mwingine akapelekwa mpaka Barabara ya Shekilango karibu kabisa na kuingia katika Barabara ya Morogoro, mwingine akawekwa katika Barabara ya Sam Nujoma, huyo alitakiwa kuwasiliana na wenzake kama gari lingekwenda Mbezi Beach au Makumbusho, lakini mbali na hao, pia kuna mwingine akawekwa Kimara, yote hiyo ilikuwa ni kumvizia msichana huyo katika barabara zote.

Wakati wao wakiwa wamejipanga, Hamisi alikuwa chuoni akimfuatilia msichana huyo. Alijifanya kuwa bize, mgongoni alikuwa na begi lake, alikuwa na muonekano kama mwanachuo.

Nandy alipotoka darasani, kama kawaida yake akaelekea sehemu ya bodaboda, akachukua na kuondoka mahali hapo. Hamisi hakujua mahali alipokuwa akienda, naye akachukua pikipiki yake aliyokwenda nayo na kuanza kuwafuatilia.

Ilipofika Barabara ya Sam Nujoma, bodaboda ile ikakata kushoto hali iliyoonyesha kwamba ilikuwa ikienda Makumbusho au Mbezi Beach.

Kichwa chake kilikuwa kinajiuliza sababu ya msichana huyo kwenda huko. Muda ulikuwa umekwenda na alitakiwa kurudi nyumbani lakini cha ajabu, alikuwa akielekea upande mwingine kabisa.
Alipofika Mwenge, bodaboda ikakata kona kulia, ikachukua Barabara ya Ali Hassan Mwinyi kuelekea Makumbusho.

“Anakuja upande wenu. Dereva kavaa fulana nyeusi, kampakiza dada mwenye blauzi ya pinki,” alisema Hamisi na hivyo dereva wa gari lililokuwa Bamaga akaliwasha na kuanza kuelekea Mwenge huku akiwa kwenye mwendo wa kasi.
 
SEHEMU YA 57

Kwa jinsi ajali ile ilivyotokea, hakukuwa na mtu aliyehisi kwamba ilikuwa imetengenezwa. Nandy aligongwa na gari lakini kitu cha ajabu dereva wa gari lile alikuwa amekimbia.

Baada ya nusu saa, Hamisi ambaye aliishuhudia ajali ile akampigia simu Linda na kumwambia kile kilichokuwa kimetokea, alimuelezea mazingira ya ajali hiyo na hata jinsi Nandy alivyokuwa ameumia vibaya.

“Linda...” aliita Hamisi.
“Niambie!”
“Yule dada akipona, naenda kuogelea baharini kule Morogoro,” alisema Hamisi huku akiwa na uhakika kwamba Nandy hawezi kupona.
“Kwani imekuwaje?”

“Ungebahatika kumuona, ungejiuliza kagongwa na treni au ajali ya gari na pikipiki,” alisema Hamisi huku akionekana kuwa na furaha kwani alikuwa na uhakika wa kulipwa malipo yao yaliyobaki kwa kazi kubwa waliyokuwa wameifanya.

*** Mzee Gwamaka hakukumbuka kuhusu ubaya wa Dickson, kitu pekee alichokuwa akikiangalia ni hali ya mtoto wake tu. Alikuwa kitandani, tangu siku ya kwanza alipokuwa amepelekwa hospitalini hapo mpaka siku ya tatu hakuwa amefumbua macho yake.

Nandy alikuwa kwenye hali mbaya, ingekuwa rahisi kusema kwamba tayari alikuwa amefariki dunia kwani hakuwa ametingishika tangu siku ya kwanza alipofika mahali hapo.

Dickson hakutaka kuondoka hospitalini, siku zote hizo tatu ambazo Nandy alikuwa hospitalini hapo alikuwa pembeni ya kitanda alicholalia. Muda wote alikuwa mtu wa kulia tu, macho yake yalikuwa mekundu kupita kawaida.

Linda alimpigia simu kwa lengo la kuzungumza naye lakini hakupokea, kwa wakati huo, alikuwa tayari kwa kitu chochote kile, alikuwa tayari kufungwa gerezani kwa kosa la kutaka kubaka lakini hakutaka kuona akimpoteza Nandy, msichana aliyekuwa akimpenda kwa moyo wa dhati.

Wazazi wa Dickson ndiyo waliokuwa wakigharamia kila kitu hospitalini hapo, walitamani kumuona kijana wao akiwa na furaha, kitendo cha kumuhudumia Nandy kwa kila kitu waliamini kwamba kingeweza kumfanya Dickson kuwa na furaha moyoni mwake.
 
SEHEMU YA 58

Washirika wa kanisa alilokuwa akisali walifika hospitalini hapo na kumuona Nandy, kila aliyemuona alisikitika, ilikuwa ni vigumu kuamini kile kilichokuwa kikionekana kitandani, Nandy yuleyule aliyekuwa na sauti kali ya kumuimbia Mungu leo hii alikuwa kimya kitandani.

Wachungaji kutoka katika makanisa mbalimbali nao walimiminika hospitalini, walimfahamu Nandy, alikuwa binti maarufu makanisani, alimsifu sana Mungu, kitendo cha kupata ajali ile kiliwashtua sana na hilo ndilo lililowapeleka hospitalini huko kumwangalia.

Japokuwa alikuwa amelazwa kwa siku tatu lakini hakukuwa na maendeleo yoyote yale, alikuwa vilevile kama alivyoletwa huku kila siku akila na kujisaidia kwa kutumia mipira iliyokuwa imefungwa mwilini mwake.

“Nandy mpenzi....” alisema Dickson huku akimwangalia Nandy kitandani pale.
“Najua nimekukosea, hukustahili kuumizwa kama nilivyokuumiza, najuta kwa kuchukua uamuzi wa kijinga namna ile. Mimi ni mwanaume ambaye nilitakiwa kuonyesha uanaume wangu hata kama ningeambiwa kwamba nafungwa gerezani milele.

“Nandy! Najua hii yote ni kwa sababu yangu! Kwa nini nimekuumiza? Kwa nini nilikubali kukuacha? Mimi ni mpumbavu, mimi ni shetani, sikutakiwa kukulipa wema kwa ubaya. Ulinionyesha mapenzi, yaani yote yale nimekuja kukuacha kwa sababu ya uoga? Yaani uoga wangu ndiyo ulinifanya nikuache na kukuumiza namna hii? Nandy! Ninakupenda, nipo hapa, sitoondoka hospitalini mpaka siku ambayo utafumbua macho yako na kuniangalia tena,” alisema Dickson huku akiwa pembeni ya kitanda alicholalia Nandy.

Kwa jinsi alivyokuwa akiongea ilikuwa ni rahisi kugundua kwamba alikuwa ameumizwa moyoni mwake. Machozi yalikuwa yakimtoka, yalitiririka mashavuni mwake na kulowanisha shati lake kifuani na kuonekana kama alimwagiwa maji.

Macho yake yalikuwa mekundu sababu ya kulia sana. Hakulia siku hiyo tu, kwa siku tatu mfululizo alikuwa akilia na hakutaka kuondoka hospitalini hapo, alikuwa tayari kupoteza kila kitu lakini si kumuacha Nandy akiendelea kuteseka.
 
Linda una roho mbaya kuliko hata shetani, Mungu atatulipia tu kwa Nandy wetu
 
SEHEMU YA 59

Marafiki zake walifika na kumpa pole, walimuonea huruma rafiki yao, kwa jinsi alivyokuwa akilia, alionekana kuumia kupita kawaida. Alitia huruma, alionekana kukata tamaa, hakuonekana kuwa na imani kwamba kuna siku Nandy angeweza kuamka kitandani hapo.

Siku zikaendelea kwenda mbele, mpaka mwezi unakatika bado Nandy aliendelea kuwa kitandani hapo huku akiwa kimya kabisa. Alikuwa akipumulia mashine ya gesi, mipira ikiwa imechomekwa mwilini mwake kwa ajili ya chakula na kwenda haja.

Baada ya kuona hakukuwa na maendeleo yoyote yale, wazazi wa Dickson wakaamua kwa pamoja kwamba msichana huyo alitakiwa kusafirishwa na kupelekwa nchini India kwa matibabu zaidi.
“Baba! Unadhani huko kunaweza kumrudisha mpenzi wangu?” aliuliza Dickson.

“Tuna imani hiyo! Atarudi na kuungana nawe kwa mara nyingine,” alisema baba yake huku naye akilengwa na machozi kwani kila alivyomwangalia Dickson kwa jinsi alivyokuwa ameumizwa, alijisikia uchungu moyoni mwake.

Wakakumbatiana! Waliendelea kubaki hospitalini hapo huku Nandy akiendelea kulala kitandani huku akiwa hajitambui.
Jopo la madaktari kila siku lilikuwa likikutana katika chumba cha mkutano na kujadili hali ya Nandy.

Hakukuwa na mabadiliko yoyote yale, uti wa mgongo ulikuwa vilevile, kichwani hakuwa amepata nafuu kama walivyokuwa wakitegemea.
 
SEHEMU YA 60

Baada ya kusikia kwamba wazazi walikubaliana kumsafirisha mgonjwa mpaka nchini India kwa matibabu zaidi, wakashukuru Mungu kwani walihisi kabisa kwamba hiyo kidogo ingewasaidia.

Haraka sana wakaanza kufanya mawasiliano na Hospitali ya Apollo iliyokuwa Chennai nchini India na baada ya wiki moja, harakati za safari zikaanza kufanyika, mgonjwa akaandaliwa na siku iliyofuata safari ya kuelekea nchini India ikaanza.

Bado Dickson alikuwa pembeni mwa Nandy, kulia ilikuwa sehemu ya maisha yake, pale alipokuwa hakuyatoa macho usoni mwa Nandy, alikuwa akimwangalia huku moyo wake ukiwa na mambo mengi mno.

Ili kuonyesha kwamba alikuwa ameumizwa sana na kile kilichokuwa kikiendelea, akawa anaweka posti katika mtandao wa WhatsApp kwa status na kuelezea hisia zake, jinsi alivyokuwa mpumbavu kuachana na msichana huyo, alivyokuwa akimuomba msamaha na mambo mengine mengi.

“Huyu mwanamke ni shetani! Nipo tayari kwa lolote sasa,” aliandika kwenye status moja WhatsApp huku akiwa ameweka picha ya msichana huyo.
Linda alipoiona tu, akajua sasa kwamba vita vilikuwa vimeanza na hakuwa na dalili za kuolewa na mwanaume huyo.

“Kama kamwaga ugali, namwaga mboga!” alisema Linda kwa hasira huku akiwa amevimba na uso kutawaliwa na ndita.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom