Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

SEHEMU YA 67

Mgonjwa anapokuwa amevunjika katika sehemu hii ya kuanzia C1 hadi C4 inamaana kwamba katika mwili wake angepooza miguu, mikono, asingekuwa na uwezo wa kula au kuoga yeye mwenyewe na ilikuwa ni lazima atafutiwe mtu wa kumfanyia mambo hayo yote, asingekuwa na uwezo wa kuendesha gari, kwa kifupi alitakiwa kuwa chini ya uangalizi kwa saa ishirini na nne.

Mbali na hicho, pia kulikuwa na pingili nyingine walizoziwekea rangi ya kijani. Hizo ziliitwa Low-Cervical Nerves ambazo zilianzia C5 hadi C8.

Mgonjwa anapovunjika pingili hizo, kwake isingekuwa vigumu sana kufanya mambo mengine kwani angeweza kunyanyua mkono, kutembea na wakati mwingine hata kuzungumza kama kawaida lakini tatizo kubwa ambalo angekutana nalo ni kwenye mfumo wote wa upumuaji, asingeweza kupumua kwa kawaida, ilikuwa ni lazima kutumia mashine maalumu kupumua.

Kulikuwa na pingili nyingine walizozipa rangi nyekundu, hizi ziliitwa Thoracic Nerves walizozipa T1 hadi T5. Hizi nazo kama zingevunjika basi mgonjwa angepata matatizo katika kifua chake, miguu na mikono ingepooza ambapo kwa kitaalamu hujulikana kama paraplegia.

Walipitia kila kitu kwa umakini mkubwa na tatizo kubwa lililotokea kwa Nandy ni kwamba pingili nyingi zilikuwa zimevunjika hali iliyoonyesha hatari kubwa katika maisha yake.

Baada ya saa saba, kikao kikamalizika na hivyo kuanza kazi ya kumshughulikia mgonjwa huyo ambaye alipelekwa katika hospitali hiyo huku akiwa hajitambui.

Kila mtu aliyemwangalia pale kitandani alipokuwa, alimuonea huruma, alidhoofika mwili kwa siku chache tu, alipokuwa amelala, hakuweza kuyafumbua macho yake na ilikuwa ni rahisi kusema kwamba alikuwa amefariki dunia kutokana na ukimya wake.

Pale chumbani, Dickson alikuwa pembeni yake, moyo wake haukuacha kuuma, machozi hayakukatika mashavuni mwake, wakati mwingine alikuwa akijilaumu kwa kumuacha Nandy na kwenda kuwa na mwanamke mwingine ambaye aliamini kwamba hakuwa chaguo lake hata kidogo.
 
SEHEMU YA 69

Alimwangalia msichana huyo, wakati mwingine alihisi kwamba alifariki dunia pale kitandani kutokana na ukimya aliokuwanao, kitu pekee ambacho kilimpa uhakika kwamba Nandy hakuwa amefariki dunia ni mashine ya Medical EKG Heart Rate Monitor ambayo ilionyesha namba moyo wake ulivyokuwa ukifanya kazi kwa kupanda na kushuka.

“Mungu! Naomba uchukue kila kitu kwangu lakini naomba uniachie Nandy! Ni msichana mdogo mno, mwenye ndoto zake za kuwa muimbaji mkubwa wa injili, Mungu, kwa nini usininyang’anye kila kitu na kuniachia Nandy?” aliomba Dickson huku akimwangalia msichana huyo aliyekuwa kimya kitandani.

Maisha yaliendelea, kila siku Dickson na wazazi wao walikuwa wakielekea hotelini na kurudi hospitalini hapo. Hakukuwa na nafuu kwa msichana huyo, hali yake iliendelea vilevile kiasi kwamba kuna wakati wote walihisi kuwa msichana huyo alikuwa amefariki dunia lakini madaktari walishindwa kuwaambia ukweli.

Kila siku madaktari walikuwa wakimchukua na kumpeleka katika chumba maalumu cha matibabu na kuanza kumtibu humo. Zoezi kubwa walilokuwa wakilifanya lilikuwa ni kuunyoosha mgongo wake, zile pingili ambazo zilikuwa zimeachana zirudi na kuungana tena kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma.

Kuzinyoosha lilikuwa zoezi kubwa na gumu, madaktari walihangaika mpaka kufanikiwa kuzinyoosha na kitu pekee kilichobaki kilikuwa ni kuziacha ziungane na kuwa kama zamani zoezi ambalo lingeweza kuchukua hata zaidi ya miaka hamsini.

“Atapona?” lilikuwa swali alilouliza Dickson mara kwa mara.
“Ndiyo! Atapona japokuwa itamchukua muda mrefu sana!” alijibu daktari.
“Kama miezi mingapi?”
“Miezi kama mia sita!”
“Unasemaje?”

“Miezi mia sita. Hicho ni kipindi kifupi sana kwa mtu kama yeye lakini wengine wanaweza kuchukua miezi mingi zaidi ya hiyo,” alisema daktari.

Dickson akachoka, akahisi miguu yake ikinyong’onyea na kukaa chini. Kichwa chake kilifanya hesabu harakaharaka kwamba miezi hiyo mia sita aliyokuwa ameambiwa ilikuwa ni sawa na miaka hamsini.

Pale chini alipokuwa akaanza kulia, hakuona tumaini tena, alikata tamaa na kuhisi kabisa kuwa mpenzi wake huyo angekufa akiwa pale pale kitandani.
 
Jaman msishangae no hapo kama nimeruka ilirudiwa story ndio mana sijaiweka
 
SEHEMU YA 70

“Hawezi kufa akiwa kitandani, kuna siku atasimama na kutembea tena,” alisema Dickson huku akilia kwa sauti kubwa kiasi kwamba kila mmoja aliyekuwa hospitalini hapo akahisi kuwa mgonjwa wake alifariki dunia.

Siku zilikatika na baada ya miezi mitatu na nusu, hatimaye muujiza ukaonekana kwa Nandy, akayafumbua macho yake na kuanza kuangalia huku na kule.

Kitu pekee alichokuwa akikikumbuka ni kupata ajali mbaya akiwa kwenye pikipiki, baada ya hapo hakujua ni kitu gani kiliendelea.

Akaanza kuyapeleka macho yake huku na kule, mashine ya kupumulia ilikuwa puani na mdomoni mwake, kwa juu yake aliiona dripu ikiwa inaning’inia, hakutaka kujiuliza, kwa jinsi ajali ile ilivyokuwa imetokea, alijua kabisa kwamba hapo alipokuwa ilikuwa ni hospitalini.

Akajaribu kuinuka kitandani pale, akashindwa, mwili wake ulikuwa haufanyi kazi kabisa. Kiuno kilikataa kutingishika, alijaribu kuitingisha mikono yake, akashindwa kabisa, ilikuwa ni kama mtu aliyepigwa sindano ya ganzi.

Hakujua ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea, mwili wake ulikosa mawasiliano na ubongo na kitu pekee alichokuwa na uwezo wa kukitingisha kilikuwa ni kichwa chake tu.

“Nini kimetokea?” aliuliza kwa sauti kubwa iliyowafanya manesi wawili kuingia chumbani hapo.
Walipomuona Nandy amefumbua macho, mmoja akatoka na kwenda kumuita daktari. Ulikuwa ni mwezi wa tatu tangu afikishwe hospitalini hapo, alikuwa kimya, alipoteza fahamu na hatimaye siku hiyo aliyafumbua macho yake na kuangalia tena.

Daktari alipofika, akatoa tabasamu pana. Alishangaa, manesi waliokuwa mbele yake walikuwa Wahindi na hata daktari aliyekuwa ameingia ndani ya chuma hicho alikuwa Mhindi pia.

“Where Am I?” (nipo wapi?) aliuliza Nandy.
“In the hospital!” (hospitalini)
“Agha Khan?” “No! Apollo, India,” (Hapana! Apollo, India) alijibu daktari huyo.

“Doctor! What is wrong with me? I can’t move my legs, hands, what is wrong with me?” (Dokta! Nina tatizo gani? Siwezi kuisogeza miguu yangu, mikono, nina tatizo gani?) aliuliza Nandy huku akiwa kitandani pale.
 
SEHEMU YA 71

Daktari hakumjibu, alimwangalia, aliangalia mapigo ya moyo wake, mtungi wa gesi, alipoona kwamba ana uwezo wa kupumua pasipo mashine hiyo, akakitoa kifaa cha kupumulia na kisha kuandika maelezo machache na kutoka ndani ya chumba hicho.

Akaingia ofisini mwake na kuwaita wazazi wa binti huyo waliyekuwa wamemleta, wakaelekea huko wakiwa na Dickson na kuanza kuwaambia kuhusu hali ya mgonjwa.

Hakukuwa na aliyeamini waliposikia kwamba Nandy aliyafumbua macho yake na kuzungumza. Kila mmoja alihisi kama alikuwa kwenye ndoto moja ya kusisimua na baada ya dakika kadhaa angeamka kutoka kitandani.

Miezi mitatu yote walikuwa hospitalini hapo wakisubiria muujiza, walimuomba Mungu na mwisho wa siku akawajibu kwa kumrudishia pumzi msichana huyo huku akiwa kitandani.

Kila mmoja alikuwa na hamu ya kumuona Nandy ndani ya chumba kile, walizungumza na daktari lakini mawazo yao yote yalikuwa kwa msichana huyo tu.
Walipomaliza, daktari akawachukua na kuondoka nao kuelekea katika chumba kile. Moyo wa Dickson ulikuwa na shauku kubwa kumuona Nandy. Alimuomba sana Mungu, alihitaji kumuona akiyafumbua macho yake tena, kiu yake kubwa ilikuwa ni kusimama mbele ya msichana huyo na kuongea naye.

Walipoingia, moja kwa moja wakaanza kupiga hatua kumfuata huku nyuso zao zikiwa kwenye tabasamu pana. Nandy, alipomuona baba yake, akatabasamu lakini macho yake yalipohamia kwa Dickson, akaanza kupiga kelele huku akimtaka kijana huyo atoke haraka sana ndani ya chumba hicho.

“Dickson tokaaaaaaa.....sitaki kukuonaaaa...tokaaaaaaa....” alipiga kelele Nandy huku akimwangalia Dickson kwa hasira, machozi yakaanza kutiririka mashavuni mwake.

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 72

Dickson hakuamini alichokuwa akikisikia, alibaki akimwangalia Nandy kitandani pale ambapo aliendelea kumwambia kwamba ni lazima aondoke ndani ya chumba kile.

Moyo wake ulimuuma mno, machozi yakaanza kumtoka na kutiririka mashavuni mwake. Ni kweli alimkosea msichana huyo, alimuumiza mno lakini alimsaidia sana mpaka kufika nchini India na kuanza kupewa matibabu.

Nandy hakuwa akijua hilo, alipoteza fahamu kwa miezi mitatu hivyo hakujua ni kwa namna gani mwanaume huyo alikuwa amemsaidia kufika mahali hapo.
Hakutaka kubisha, huku akionekana kuumia sana akageuka na kuanza kutoka ndani ya chumba hicho tena kichwa chake akiwa amekiinamisha chini.

“Ninakuchukia, ninakuchukia Dickson,” alisema Nandy wakatik Dickson alipokuwa akitoka ndani ya chumba hicho.
Akaelekea nje na kukaa kwenye viti vilivyokuwa mahali hapo, aliumia moyoni mwake lakini baada ya kugundua kwamba msichana huyo alikuwa amefumbua macho yake baada ya miezi mitatu kupita, akaanza kumshukuru Mungu, akapiga magoti chini na kuinyoosha mikono yake juu.

Mule ndani, baba yake, mzee Gwamaka na wazazi wa Dickson wakaanza kumtuliza na kumtaka kunyamaza huku wakimwambia ni kwa jinsi gani Dickson alifanikisha kwa yeye kuwa mahali hapo.
Nandy hakutaka kukubali, hakuwaamini, alipoambiwa kwamba alikuwa kitandani hapo kwa muda wa miezi mitatu kwake aliona ni uzushi tu kwani kile kilichotokea kwenye ajali ile kilionekana kuwa kama siku iliyopita.

“Aliniacha, alinitesa, siwezi kuwa naye,” alisema Nandy huku akilia.
“Hutakiwi kusema hivyo! Mungu husamehe, kwa nini hutaki kusamehe binti yangu?” aliuliza mzee Gwamaka.
“Lakini aliniumiza sana!”

“Yesu aliumizwa, alichapwa mijeledi, alitemewa mate, alizomewa, aliitwa mwizi, alizihakiwa na kutundikwa msalabani Goligotha, lakini palepale msalabani alisema kwamba Mungu awasamehe, yaani alisamehe pamoja na kufanyiwa vyote hivyo, sisi ni nani mpaka tusisamehe?” aliuliza mzee Gwamaka huku akimwangalia binti yake.

Nandy alikuwa kimya, maneno aliyoongea baba yake yaliingia moyoni mwake na kumkumbusha maneno ya kwenye Biblia kwamba alitakiwa kusamehe saba mara sabini.
 
SEHEMU YA 73

Moyo wake ukalowa, hakuwa na ubishi tena, alijua kabisa kwamba hata kama alifanyiwa mambo gani alitakiwa kusamehe kwa kila kitu kilichotokea.
Akamwambia baba yake kwamba alikubali kumsamehe Dickson lakini hakutaka kuwa naye tena, yaani katika maisha yake, alitakiwa kubaki peke yake, bila kuwa na mwanaume mwingine mpaka kifo chake.

“Hakuna tatizo!” alisema mzee Gwamaka.
Hapohapo mzee huyo akatoka ndani na kwenda kumuita Dickson, alipofika kwenye korido, bado mwanaume huyo alikuwa amepiga magoti, alimshukuru Mungu kwa kile kilichokuwa kimetokea.
Kwake, kitendo cha Nandy kuyafumbua macho yake kilionekana kuwa muujiza mkubwa kama kuuhamisha mlima na kuupeleka baharini.

Hapohapo mzee Gwamaka akamfuata na kumshika bega na kumwambia kwamba alikuwa akihitajika na Nandy. Haraka sana akasimama, akaingia ndani ya chumba kile na kumfuata Nandy pale kitandani.

Kitu cha kwanza kabisa kukifanya ni kupiga magoti na kuanza kumuomba msamaha. Aliyajua makosa yake, kwa jinsi msichana huyo alivyokuwa akimpenda, hakutakiwa kumuacha kama alivyokuwa amefanya.

Aliomba sana msamaha huku akilia kama mtoto mdogo, alimwambia wazi kwamba katika maisha yake yote asingeweza kufanya ujinga kama aliokuwa ameufanya, alikuwa tayari kumfanyia kila kitu lakini si kumuacha tena.

“Nandy! Naomba unisamehe, najua nimekukosea, najua sistahili msamaha, nilikuumiza sana lakini naomba unisamehe mpenzi,” alisema Dickson huku akiwa amepiga magoti chini, macho yake yalikuwa mekundu mno.

“Dickson! Why did yo...” (Dickson! Kwa nini uli....) aliuliza Nandy lakini hata kabla hajamalizia sentensi yake, akaanza kulia.
Dickson akainuka na kuusogeza uso wake karibu na uso wa msichana huyo, akachukua fulana yake na kuanza kuyafuta machozi yake.

Moyo wake ulimumia mno, pale kitandani alipokuwa, Nandy alishindwa kufanya jambo lolote lile, machozi yale aliyokuwa akifutwa na Dickson yakaurudisha moyo wake na kuhisi kabisa kwamba ukianza kuanguka katika mapenzi mazito ya mwanaume huyo.
“Dickson! Nimepooza mpenzi,” alisema Nandy huku akimwangalia mwanaume huyo.
 
Maskini Nandy....
Wanaume muwe mnajitafakari kabla ya kufanya baadhi ya maamuzi.... Maamuzi ya kukurupuka ya Dick yamemfanya mdada wa watu apooze

Thanks Shunie
 
Maskini Nandy....
Wanaume muwe mnajitafakari kabla ya kufanya baadhi ya maamuzi.... Maamuzi ya kukurupuka ya Dick yamemfanya mdada wa watu apooze

Thanks Shunie
Anytime dear
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom