SEHEMU YA 34
Wakati alipopigiwa simu kuonyesha kwamba tayari Dickson alifika, akaiwasha kamera hiyo na kuanza kurekodi. Mahali ilipokuwa, ilikuwa ni vigumu sana kwa mtu kuweza kuiona, baada ya dakika mbili, mlango ukaanza kugongwa, alipofungua macho yake yakatua kwa mwanaume huyo.
Kwa jinsi alivyokuwa amevaa taulo, Dickson alichanganyikiwa, alimwangalia kwa nyuma, wowowo lake lilikuwa likicheza na wakati mwingine kama lilitaka kudondoka.
Akamchukua na kumpeleka kitandani, pale, wakaanza kuongea, kichwa cha Dickson kilikuwa kikifikiria ngono tu, alitamani kumlalia Amina na kuanza kufanya naye mapenzi. Walizungumza kwa dakika chache, Dickson akashindwa kuvumilia, akaanza kumshika Amina huku na kule.
Kwa kuwa ulikuwa ni mchezo, akaanza kujikatalisha, kila alipoguswa, alikataa lakini Dickson akashindwa kumuacha. Amina alijua kuigiza, alikuwa akijifanya kukataa kataa lakini Dickson hakutaka kumuacha.
“Bebi! Nifikishe kileleni kwanza,” alisema Amina huku akimwangalia Dickson, mikono yake ni kama ilikuwa ikiendelea kukataa kufanya mapenzi na mwanaume huyo.
“Kivipi?” “Nipige vibao, nipige vibao shavuni, humo ndipo zilipokuwa,” Alisema Amina huku akiendelea kumzuia Dickson kumtoa taulo lile.
Hilo halikuwa geni kwa Dickson, aliwahi kukutana na wanawake ambao walikuwa na stimu kila kona, wengine videleni, wengine mikononi, wengine sikioni, hata alipoambiwa kwamba ampige vibao vya shavu akaanza kumpiga.
Amina aliumia lakini hakuwa na jinsi, hilo ndilo lilikuwa lengo lake, alipopigwa, akaacha kumzuia, akajilaza na kumwachia Dickson afanye lolote lile alilolitaka.
Walifanya huku Amina akiendelea kujifanya kama anakataa, siku hiyo hakuonyesha ushirikiano wowote ule kwa kuwa kamera ilikuwa ikiendelea kuchukua video.
Dickson alipomaliza, akaondoka na kwenda kuoga na huku nyuma Amina akaichukua kamera na kuizima.
Hiyo ilikuwa siku ya kwanza, akamfuata Linda na kumwambia kwamba alifanikiwa na hivyo kumpa ile kamera na kumuonyeshea jinsi ilivyokuwa.
“Safi sana! Chukua hii,” alisema Linda huku akimpa bahasha ya kaki iliyokuwa na pesa.