Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

NAMTAKA MPENZI WANGU ARUDI-50

Nandy alifikishwa katika Hospitali ya St. Magreth iliyokuwa Kijitonyama akiwa hajitambui, kila mtu aliyemwangalia hakuamini kama kungekuwa na mtu ambaye angeumia vibaya kama ilivyokuwa kwake.

Mwili ulijaa damu, kichwani ndiyo ilikuwa balaa kiasi kwamba hata sura yake haikuwa ikionekana kabisa, yote ilitapakaa damu.

Manesi wakamchukua na kumpeleka katika chumba cha wagonjwa mahututi ambapo huko akaoshwa na kupelekwa katika chumba cha upasuaji, ilikuwa ni lazima kuokoa maisha ya binti huyo kwani alikuwa kwenye hatari ya kuyapoteza maisha yake.

Watu waliokuwa wamempeleka mahali hapo walikuwa wakisubiri taarifa rasmi kwa madaktari kwani tayari walijua kwamba alikufa hivyo walisubiri uthibitisho kutoka kwa madaktari tu.

“Ni ndugu yenu huyu?’ aliuliza nesi mmoja huku akiwaangalia watu waliompeleka Nandy hospitalini hapo.
“Hapana! Tumemsaidia tu! Vipi? Amekufa?” aliuliza jamaa mmoja.
“Hapana ila hali yake ni mbaya sana!” alijibu nesi huyo.

Wale waliokuwa wakishughulika na Nandy ndani ya chumba kile walikuwa bize, kwa jinsi alivyokuwa ameumia ilikuwa ni lazima afanyiwe upasuaji wa kichwa ambao kwa kitaalamu uliitwa Craniotomy.

Kwa kuwa hospitali hiyo haikuwa kubwa, Nandy alitakiwa kuhamishwa na kupelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambapo huko wangemfanyia vipimo vyote ili hata kama upasuaji wa kichwa ungefanyika basi ingekuwa ni rahisi kujua ni kitu gani kilitakiwa kufanyiwa kazi.

Haraka sana simu ikapigwa kitengo cha usafirishaji, gari likaandaliwa na ndani ya dakika kadhaa kupandishwa garini na kupelekwa katika hospitali hiyo huku akiwa hajitambui.

Walipofika, akateremshwa na kupelekwa ndani ya hospitali hiyo. Akachukuliwa na moja kwa moja kuingizwa katika chumba ambacho alitakiwa kufanyika hatua ya kwanza ya kuangalia tatizo lililokuwa kichwani mwake.

Hapo, akachukuliwa na kuingizwa kwenye mashine ya MRI (Magnetic Resonance Imaging) na kugundulika kwamba kulikuwa na donge la damu katika ubongo wake, lilikuwa limeganda kiasi kwamba liliyahatarisha maisha yake.
 
NAMTAKA MPENZI WANGU ARUDI-50

Nandy alifikishwa katika Hospitali ya St. Magreth iliyokuwa Kijitonyama akiwa hajitambui, kila mtu aliyemwangalia hakuamini kama kungekuwa na mtu ambaye angeumia vibaya kama ilivyokuwa kwake.

Mwili ulijaa damu, kichwani ndiyo ilikuwa balaa kiasi kwamba hata sura yake haikuwa ikionekana kabisa, yote ilitapakaa damu.

Manesi wakamchukua na kumpeleka katika chumba cha wagonjwa mahututi ambapo huko akaoshwa na kupelekwa katika chumba cha upasuaji, ilikuwa ni lazima kuokoa maisha ya binti huyo kwani alikuwa kwenye hatari ya kuyapoteza maisha yake.

Watu waliokuwa wamempeleka mahali hapo walikuwa wakisubiri taarifa rasmi kwa madaktari kwani tayari walijua kwamba alikufa hivyo walisubiri uthibitisho kutoka kwa madaktari tu.

“Ni ndugu yenu huyu?’ aliuliza nesi mmoja huku akiwaangalia watu waliompeleka Nandy hospitalini hapo.
“Hapana! Tumemsaidia tu! Vipi? Amekufa?” aliuliza jamaa mmoja.
“Hapana ila hali yake ni mbaya sana!” alijibu nesi huyo.

Wale waliokuwa wakishughulika na Nandy ndani ya chumba kile walikuwa bize, kwa jinsi alivyokuwa ameumia ilikuwa ni lazima afanyiwe upasuaji wa kichwa ambao kwa kitaalamu uliitwa Craniotomy.

Kwa kuwa hospitali hiyo haikuwa kubwa, Nandy alitakiwa kuhamishwa na kupelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambapo huko wangemfanyia vipimo vyote ili hata kama upasuaji wa kichwa ungefanyika basi ingekuwa ni rahisi kujua ni kitu gani kilitakiwa kufanyiwa kazi.

Haraka sana simu ikapigwa kitengo cha usafirishaji, gari likaandaliwa na ndani ya dakika kadhaa kupandishwa garini na kupelekwa katika hospitali hiyo huku akiwa hajitambui.

Walipofika, akateremshwa na kupelekwa ndani ya hospitali hiyo. Akachukuliwa na moja kwa moja kuingizwa katika chumba ambacho alitakiwa kufanyika hatua ya kwanza ya kuangalia tatizo lililokuwa kichwani mwake.

Hapo, akachukuliwa na kuingizwa kwenye mashine ya MRI (Magnetic Resonance Imaging) na kugundulika kwamba kulikuwa na donge la damu katika ubongo wake, lilikuwa limeganda kiasi kwamba liliyahatarisha maisha yake.

Shualina...hizi hadithi huwa unatunga wewe?
 
Ahsanteee!!!!! Mkwe tunaendelea kuchunguliana au tuoge tulale?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom