Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

Simulizi: Namtaka mpenzi wangu arudi

Tupia basi hata tatu, mkoloni katoka niutumie huu muda kuisoma... Plz shunie
 
Ukuje hapa kutembea tembea bhasiii huenda ukatufikiria hii lunch time
 
Sawa Sura ya 4
Aya ya 3 umeandika nbaada
Ilitakiwa iweje

Aya ya 5 umeandika pambi
Badala ya pambio
Ni hayo tuendelee Shunie
 
NAMTAKA MPENZI WANGU ARUDI-51

Alitakiwa kupasuliwa kichwa na donge lile litolewe kwani kwa jinsi hali ilivyokuwa ikionyesha, ilionekana kuwa mbaya sana kama tu wasingefanya kila liwezekanalo kuhakikisha donge lile la damu linatolewa.
Haraka sana daktari bingwa kwa upande wa upasuaji wa kichwa, Dk. Ezekiel Ndaki akapigiwa simu na kufika mahali hapo haraka sana. Nandy akachukuliwa na kupelekwa katika chumba maalumu cha upasuaji na kuanza kufanyiwa kazi.

“We have to perform Craniotomy very fast,” (ni lazima tumfanyie upasuaji wa kichwa haraka) alisema daktari huyo.
“Will she be okey?” (atapona kweli?) aliuliza nesi mmoja huku akionekana kuogopa.
“Is this your first time to help me?” ( hii ni mara yako ya kwanza kunisaidia?) aliuliza Dk. Ndaki.
“Yeah!”

“Are you scared?” (unaogopa?)
“A little bit!” (kidogo tu) alijibu, Dk. Ndaki akatabasamu kidogo.
Nandy alizungukwa na madaktari, manesi waliokuwa mahali hapo kwa ajili ya kumfanyia upasuaji, pale kitandani alikuwa kimya, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.

Upasuaji ukaanza, vifaa vyote vilivyokuwa vikihitajika vikawekwa tayari na kila mmoja kuwa makini katika kazi hiyo kwani kukifumua kichwa cha mgonjwa na kulitoa donge la damu lililokuwa kwenye ubongo haikuwa kazi ndogo kwani walitakiwa kuwa makini na kutokuichana mishipa iliyokuwa ikisafirisha damu kupeleka kichwani na kurudishwa katika moyo.

Kichwa kikachanwa na fuvu la kichwa kupasuliwa, kilichoonekana kilikuwa ni ubongo ambao ulikuwa na donge kubwa la damu.
Dk. Ndaki akaanza kuhangaika kulitoa donge hilo. Haikuwa kazi ndogo kwani kila alipokuwa akilisogelea, lilikwenda pembeni.

Lilimsumbua mno lakini mwisho wa siku akawa amefanikiwa kulikamata kwa kifaa maalumu na kulitoa huku tayari wakiwa wametumia muda wa saa tatu mpaka kumaliza.

Dk Ndaki akashusha pumzi nzito, alimshukuru Mungu na hivyo akatakiwa kurudishwa katika chumba kilichokuwa mashine ya MRI na kufanyiwa tena uchunguzi kwani waligundua kwamba mbali na kupasuka kichwa pia kulikuwa na uwezekano wa kuwa na tatizo jingine.
 
SEHEMU YA 52

Katika uchunguzi wao wa kina wakagundua kwamba Nandy alikuwa amevunjika uti wa mgongo na ndiyo maana hata alipokuwa amefikia katika barabara hakuweza kutingishika kwa kuwa uti huo haukuwa ukipeleka mawasiliano kichwani.

Madaktari wote hawakuamini, hakukuwa na kitu walichokuwa wakikiogopa kama kuvunjika kwa uti wa mgongo, kwa maana hiyo hata kama mgonjwa huyo angepona, bado kungekuwa na tatizo kubwa katika maisha yake, mwili wake usingeweza kufanya kazi tena, angepooza kitandani maisha yake yote na ni kichwa tu ndicho ambacho kingetingishika.

“Mungu wangu!” alisema daktari mmoja huku machozi yakimlenga, ripoti ya taarifa ya Nandy ilimuumiza mno kana kwamba alikuwa mtoto wake wa kumzaa.
Wakati madaktari wakiendelea kumshughulikia msichana huyo, huku upande wa pili baba yake, mzee Gwamaka alikuwa bize akimtafuta binti yake.

Alijaribu kumpigia simu lakini haikuwa ikipatikana, moyo wake ulikuwa na hofu, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, alichanganyikiwa, aliwapigia ndugu, jamaa na marafiki lakini kote huko walisema kwamba hawakujua mahali alipokuwa.

Haraka sana akampigia simu Dickson na kumuuliza kuhusu binti yake, alimwambia kwamba hakuwa amekutana naye kwa siku mbili hivyo hakujua kitu chochote kile.

“Kwani hajarudi nyumbani?” aliuliza Dickson.
“Ndiyo! Si kawaida yake, saa mbili sasa hivi lakini hajarudi,” alisema mzee Gwamaka.

Japokuwa hakuwa na Nandy kwa sababu ya Linda lakini taarifa hizo zilimshtua mno, hakutaka kubaki chuoni, akaondoka na moja kwa moja kuelekea nyumbani kwa kina Nandy, alipofika huko, hakumkuta mzee Gwamaka na alipouliza alijibiwa kwamba alikwenda nyumbani kwa mchungaji.

Akaelekezwa na kuelekea huko. Moyo wake ulimwambia kwamba kulikuwa na tatizo lililokuwa limetokea. Njiani, hakumfikiria Linda, akaanza kumfikiria Nandy ambaye kwake alionekana kuwa kila kitu japokuwa Linda aliingilia kati.

Alipofika huko, akamkuta mzee huyo akiwa amchanganyikiwa, simu ya msichana huyo haikuwa imepatikana hivyo kuunganisha nguvu kumtafuta msichana huyo.
 
SEHEMU YA 53

Mzee Gwamaka hakumpenda Dickson, alimchukia kwa kuwa alimuumiza binti yake lakini kwenye hali kama aliyokuwanayo, hakuwa na jinsi, akaungana naye na kuanza kwenda huku na kule kumtafuta msichana huyo.

Ilipofika majira ya saa sita usiku, wakaamua kuzunguka kwenye hospitali mbalimbali na kuulizia kama alifikishwa huko akiwa maiti. Wakaelekea katika mochwari za hospitali zote lakini hakukuwa na majibu.

“Twende Muhimbili,” alisema Dickson.
Wakaelekea huko, sehemu ya kwanza kabisa kufika ilikuwa ni mochwari ambapo huko wakaenda na kuanza kumtafut Nandy, walimkosa, hilo liliwachanganya sana na kwenda kuulizia kwa manesi ndipo wakapewa taarifa kuhusu wagonjwa walioletwa hospitalini hapo siku hiyo.

“Kuna msichana?” aliuliza mzee Gwamaka.
“Wapo sita hivi.”
“Majina?”
Akawatajia lakini akawaambia kwamba wawili hawakuwa wakijulikana. Wakataka kuwaona hao wawili, wakapelekwa kwa mmoja, walipomwangalia, hakuwa Nandy.
“Na huyo mwingine?”

“Huyo yupo mahututi, tangu aletwe hospitali hajanyanyuka, alipata ajali mbaya sana,” alisema.
“Ajali mbaya?”
“Ongeza sana.”
Wakataka kumuona msichana huyo. Hawakuruhusiwa kumuona kwa kipindi hicho mpaka baada ya daktari kufika kwa lengo la kumjulia hali.

Akawaambia kuhusu watu hao kwamba walitaka kumuona mgonjwa huyo kwani walikuwa wakimtafuta ndugu yao aliyekuwa amepotea na mpaka muda huo, saa nane usiku hawakujua mahali alipokuwa.

Kwa kuwa walikuwa wamechoka na walionekana kutaka kujua kuhusu ndugu yao, wakachukuliwa na kupelekwa katika chumba hicho.

Kwa mbele walimuona msichana akiwa kitandani, hakuwa akitingishika, aliwekewa dripu huku akipumua kwa kutumia mashine ya gesi. Kichwa chake kilizungushiwa bandeji, kwa kumwangalia pale alipokuwa ilikuwa rahisi sana kugundua kwamba mtu huyo alikuwa mahututi.

Wakaanza kumsogelea, walipomfikia na kumwangalia usini. Alikuwa Nandy. Mzee Gwamaka akahisi miguu yake ikipigwa ganzi, hakuweza kusimama, akajikuta akikaa chini na kuanza kulia.

Dickson, hakuamini alichokuwa akikiangalia, kwanza akahisi kwamba alikuwa akiota, Nandy, msichana aliyekuwa akimpenda kwa moyo wote hakuamini kama siku hiyo angekuwa katika hali aliyokuwanayo kipindi hicho.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom