Jack Daniel
JF-Expert Member
- Sep 23, 2021
- 4,042
- 16,872
- Thread starter
- #1,021
SEHEMU YA TISINI NA NANE
Hakuna aliyekuwa na furaha na amani kwa wakati ule, si mama yake Samson, wala Samson mwenyewe,
Hata Sarah na Rahma walionesha unyonge fulani, kwani waliogombana walikuwa Top leaders kwenye ile familia, hivyo Kila mmoja alimuomba MUNGU hali ile ipite.
Mzee Mgaya alitoka ndani akiwa na hasira sana huku akimpita mama yake Samson kama hamuoni vile, akaja usawa wa gari lake akafungua mlango wa siti za nyuma na kutoka na makaratasi fulani lengo aingie nayo ndani kwa mkewe, lakini mama Kulwa tayari alikuwa nje, huku akionesha ana hasira zisizo za kawaida.
Weeeee baba, usinitanie, tena nataka unyooshe maelezo vizuri, sihitaji makaratasi, bali nahitaji pesa.
Huwezi kunizuga wala kunifanya mjinga, ili amani ipatikane nahitaji unioneshe kiasi cha pesa nilichokutajia, kisha tutamaliza kesi yetu, hakuna haja ya kuzungushana.mwaka unaisha huu na kumbuka uliniahidi mwenyewe kuwa mwisho wa mwaka utaweka kile kilichopatikana kwa msimu mzima, umepata tenda za kutengeneza vitu kwenye taasisi kubwa tu, hivyo sihitaji senti nahitaji pesa.
aliweka kituo mama Kulwa akionesha anahitaji pesa toka kwa mumewe japo haikujulikana ni kiasi gani.
Mzee Mgaya aliwaangalia mama Samson na mwanaye, namna walivyoonesha kusononeka, ilimuwia vigumu kuendeleza ugomvi japo uso wake ulionesha hasira za wazi, alirudisha makaratasi yale kwenye gari huku akipiga ngumi nzito kwenye moja ya siti, ni hasira ambapo alishindwa cha kufanya haswa mbele ya mgeni mama yake Samson.
Sasa unapiga hilo gari ili iweje, wewe nipige Mimi Wala usijizuie maana hoja zangu, matakwa yangu hayana maana ndiyo maana nimefikia hatua ya kukuudhi , Mimi sijachukia wewe kufanya mambo yako na Tausi, unaweza hata kumjengea Jumba la kifalme (kasri)Mimi sitauliza wala kuonesha hisia mbaya Bali ni pale utakaponitimizia ulichoniahidi basi. Nataka unioneshe kiasi cha pesa taslimu iwe Cash, usiniambie zipo wapi mara wapi.
mama Kulwa aliongea kwa kujiamini kiasi cha kumtisha mama yake Samson maana tangu amfahamu hajawahi kumuona akiwa kwenye hali ile.
Mzee Mgaya alicheka sana, tena sana siyo kicheko cha kawaida, Bali kicheko cha majonzi na huruma kwa maisha anayopitia. Kisha akawasha gari na kumuashiria Samson apande Kisha wakaondoka huku wakiacha maneno mengi aliyoongea mama Kulwa japokuwa hawakuyasikia vizuri.
Mzee Mgaya aliendesha gari taratibu huku akiwa hajui anaenda wapi huku muda mwingine gari likihama njia yote ni hali aliyokuwa anapitia, hatimaye wakapark gari kwenye Pub moja ambayo haikuwa na watu wengi, wakaamua kukaa nje karibu na maua fulani mazuri huku Samson akiwa na shauku ya kutaka kumuuliza Mzee Mgaya maswali kadhaa.
Waliita vinywaji visivyolewesha kisha Samson akaanza kujimiminia ile soda huku Mzee Mgaya akiwa katulia tu, huku akicheka peke yake kila mara.
Samahani baba pengine sipaswi kujua habari zako nyingi lakini kwakuwa mmekwazana na mama mkubwa pale najikuta napenda nifahamu kwani mama Kulwa kakwazika na nini?
aliuliza Samson.
Mwanangu wakati mwingine napenda sana maisha wanayoishi wazazi wako, yaani wanaheshimiana kiasi cha Mimi kuwaonea wivu, yaani juu ya kuwa hawana kitu lakini , sijawahi kushuhudia wala kusikia habari kuwa labda wamegombana, ni ngumu, sisemi kuwa hawagombani lakini Mimi na mke wangu tumezidi na si Mimi Bali ni huyu mama yako asiyekua yaani sijui anajionaje ila yote namuachia MUNGU.
aliongea Mzee Mgaya akiwa hata soda hajaifungua kwani huenda aliagiza kwa kutimiza masharti ya eneo husika.
Hivi kumbe mama Kulwa mlienda naye kwa mama yako mdogo Tausi siyo? aliuliza Mzee Mgaya.
Ndiyo ila aliondoka mapema sana kwani alisema anajisikia vibaya.
alijibu Samson.
Mzee Mgaya alicheka kidogo Kisha akaendelea..........
Mwanangu najua kuna vitu vingine sipaswi kukwambia lakini haina budi wewe ni kijana sasa, ni mtu unajua baya na zuri ni lazima nikwambie tu baadhi ya mambo, ni kwamba bila shaka unaukumbuka ugomvi wa mwaka jana Kati ya Mimi na mama yako mkubwa.mzee Mgaya aliongea huku akimwangalia Samson.
Sam akatingisha kichwa kuonesha anakumbuka.
Mwanangu na ndiyo maana huwa nakushauri usome kwa bidii zote yaani ujitoe nguvu na akili zako zote ziishie kwenye masomo, maana Kuna watu wanakuombea ushindwe ili wapate cha kuongelea, pia nataka ujue kuwa Kuna siku niliita wazee pale kwangu watusuluhishe, baada ya mama yako kusema hela natumia vibaya hususani wewe, akidai nasomesha mtu mwenye laana, na ambaye ni ngumu kuonesha matunda ya uwekezaji unaofanyika, unasahau Kuna siku ulifukuzwa, na bahati nzuri ndiyo siku narudi, Sasa kile kipindi ndicho mke wangu alitaka wewe ufukuzwe na baada ya wazee kumuuliza ili Aishi na Mimi kwa amani anataka nini , aliwajibu kuwa wewe uache shule siyo uhame nyumbani kwake, la hasha uhame yaani isitumike shilingi yoyote yenye kukuhusu wewe.
Hivyo Mimi na uzee huu nilitumia busara kuwa siwezi kumuacha mke wangu kwa mambo ya kipuuzi na pia siwezi kukufukuza wewe, kisa ujinga wa mtu mmoja, Imani yangu ni Moja juu ya wewe kutuonesha nidhamu mbovu mara kadhaa lakini najua una kitu kichwani kwako kipo kitu.
aliweka kituo mzee Mgaya.
Sasa baba niambie ulifanyaje ili nisifukuzwe, na pia wewe na mama maisha yenu yakiendelea vizuri. aliuliza Samson.
Samson umekua na hakika najivunia kwa Sasa , umeuliza swali zuri ambalo nililisahau,
Ni kwamba nilitumia mbinu ya kumuahidi kiasi fulani cha pesa hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu, na hiyo pesa ipo na ningemuonesha lakini tatizo ameuliza kwa njia ya dharau huku akishinikiza aione Leo leo na Mimi kama mwanaume siwezi kupelekwa kihivyo. Yaani kuona kile kibanda cha Tausi tayari akaona pesa itakuwa imepotea, badala ya kutulia aulize kwa heshima yeye ananiropokea na hata hivyo tarehe ambayo tulipanga haijafika. Pia hela hizo zipo kwenye account ambayo hata nikifa leo yeye ataziona tu kwani taarifa zangu zote anajua hakuna kitu nimemficha, kwani mama Jose ana nini lakini.
aliongea kwa sauti Kali Mzee Mgaya huku akigonga ile meza iliyodizainiwa
Kwa mtindo wa culture ikifanana natumbwi.
Oyaa wewe James vipi muda wote naona uso wako umesawajika nini kinakusibu, na shida yako ni hela tu hakuna namna yaani na tatizo lako wewe muoga, na utakufa masikini, au ndiyo umeshatidhika na maisha yako eeeh. aliongea kwa dharau yule jamaa ambaye umri unafanana na mzee Mgaya kwani wote walikuwa na mvi nyingi za uzee ili tofauti yao ni kwamba huyu mwingine alijiweka kiujana kwani alikuwa kavaa kaptura na vest huku shingoni kukiwa na cheni kadhaa Samson alimkumbuka kuwa ni bwana wake Cathy.
Sikia wewe nipo na mwanangu na sikuzote huwa nakuonya upunguze utani haswa ukinikuta na watoto wadogo kama hawa, aliongea Mzee Mgaya akionesha kukerwa na maneno ya jamaa.
Wewe James vipi bwana, Mimi nakwambia ukweli unadai nakutania ona sasa umepaki land cruiser hapa yaani gari za kwendea safari za mbali mikoani huko wewe unakuja nazo huku wewe vipi au nikuuzie hii yangu, kwanza hela zenyewe unazo. aliendelea na tambo yule jamaa.
Kufumba na kufumbua yule jamaa alipigwa ngumi kwenye paji la uso akaangukia kule, kwenye kokoto huku akivuja damu, Mzee Mgaya akataka kukimbia lakini akazuiwa na baadhi ya watu pale.
Weeee Mzee unaenda wapi nani unataka kumwachia kesi, yaani uuue halafu utuachie msala hebu tulia hapo. Mzee Mgaya alitii amri.
Mzee Mgaya kazua balaa kwenye pub alipoenda kupunguza mawazo,
Mama Kulwa anataka aoneshwe pesa na mumewe na haelewi chochote,
Muda wa Samson kuripoti shule unakaribia, itakuwaje?
Kumbuka Kuna mgeni mama yake Samson naye anatakiwa arudi kijijini.
Itaendelea...............................
Hakuna aliyekuwa na furaha na amani kwa wakati ule, si mama yake Samson, wala Samson mwenyewe,
Hata Sarah na Rahma walionesha unyonge fulani, kwani waliogombana walikuwa Top leaders kwenye ile familia, hivyo Kila mmoja alimuomba MUNGU hali ile ipite.
Mzee Mgaya alitoka ndani akiwa na hasira sana huku akimpita mama yake Samson kama hamuoni vile, akaja usawa wa gari lake akafungua mlango wa siti za nyuma na kutoka na makaratasi fulani lengo aingie nayo ndani kwa mkewe, lakini mama Kulwa tayari alikuwa nje, huku akionesha ana hasira zisizo za kawaida.
Weeeee baba, usinitanie, tena nataka unyooshe maelezo vizuri, sihitaji makaratasi, bali nahitaji pesa.
Huwezi kunizuga wala kunifanya mjinga, ili amani ipatikane nahitaji unioneshe kiasi cha pesa nilichokutajia, kisha tutamaliza kesi yetu, hakuna haja ya kuzungushana.mwaka unaisha huu na kumbuka uliniahidi mwenyewe kuwa mwisho wa mwaka utaweka kile kilichopatikana kwa msimu mzima, umepata tenda za kutengeneza vitu kwenye taasisi kubwa tu, hivyo sihitaji senti nahitaji pesa.
aliweka kituo mama Kulwa akionesha anahitaji pesa toka kwa mumewe japo haikujulikana ni kiasi gani.
Mzee Mgaya aliwaangalia mama Samson na mwanaye, namna walivyoonesha kusononeka, ilimuwia vigumu kuendeleza ugomvi japo uso wake ulionesha hasira za wazi, alirudisha makaratasi yale kwenye gari huku akipiga ngumi nzito kwenye moja ya siti, ni hasira ambapo alishindwa cha kufanya haswa mbele ya mgeni mama yake Samson.
Sasa unapiga hilo gari ili iweje, wewe nipige Mimi Wala usijizuie maana hoja zangu, matakwa yangu hayana maana ndiyo maana nimefikia hatua ya kukuudhi , Mimi sijachukia wewe kufanya mambo yako na Tausi, unaweza hata kumjengea Jumba la kifalme (kasri)Mimi sitauliza wala kuonesha hisia mbaya Bali ni pale utakaponitimizia ulichoniahidi basi. Nataka unioneshe kiasi cha pesa taslimu iwe Cash, usiniambie zipo wapi mara wapi.
mama Kulwa aliongea kwa kujiamini kiasi cha kumtisha mama yake Samson maana tangu amfahamu hajawahi kumuona akiwa kwenye hali ile.
Mzee Mgaya alicheka sana, tena sana siyo kicheko cha kawaida, Bali kicheko cha majonzi na huruma kwa maisha anayopitia. Kisha akawasha gari na kumuashiria Samson apande Kisha wakaondoka huku wakiacha maneno mengi aliyoongea mama Kulwa japokuwa hawakuyasikia vizuri.
Mzee Mgaya aliendesha gari taratibu huku akiwa hajui anaenda wapi huku muda mwingine gari likihama njia yote ni hali aliyokuwa anapitia, hatimaye wakapark gari kwenye Pub moja ambayo haikuwa na watu wengi, wakaamua kukaa nje karibu na maua fulani mazuri huku Samson akiwa na shauku ya kutaka kumuuliza Mzee Mgaya maswali kadhaa.
Waliita vinywaji visivyolewesha kisha Samson akaanza kujimiminia ile soda huku Mzee Mgaya akiwa katulia tu, huku akicheka peke yake kila mara.
Samahani baba pengine sipaswi kujua habari zako nyingi lakini kwakuwa mmekwazana na mama mkubwa pale najikuta napenda nifahamu kwani mama Kulwa kakwazika na nini?
aliuliza Samson.
Mwanangu wakati mwingine napenda sana maisha wanayoishi wazazi wako, yaani wanaheshimiana kiasi cha Mimi kuwaonea wivu, yaani juu ya kuwa hawana kitu lakini , sijawahi kushuhudia wala kusikia habari kuwa labda wamegombana, ni ngumu, sisemi kuwa hawagombani lakini Mimi na mke wangu tumezidi na si Mimi Bali ni huyu mama yako asiyekua yaani sijui anajionaje ila yote namuachia MUNGU.
aliongea Mzee Mgaya akiwa hata soda hajaifungua kwani huenda aliagiza kwa kutimiza masharti ya eneo husika.
Hivi kumbe mama Kulwa mlienda naye kwa mama yako mdogo Tausi siyo? aliuliza Mzee Mgaya.
Ndiyo ila aliondoka mapema sana kwani alisema anajisikia vibaya.
alijibu Samson.
Mzee Mgaya alicheka kidogo Kisha akaendelea..........
Mwanangu najua kuna vitu vingine sipaswi kukwambia lakini haina budi wewe ni kijana sasa, ni mtu unajua baya na zuri ni lazima nikwambie tu baadhi ya mambo, ni kwamba bila shaka unaukumbuka ugomvi wa mwaka jana Kati ya Mimi na mama yako mkubwa.mzee Mgaya aliongea huku akimwangalia Samson.
Sam akatingisha kichwa kuonesha anakumbuka.
Mwanangu na ndiyo maana huwa nakushauri usome kwa bidii zote yaani ujitoe nguvu na akili zako zote ziishie kwenye masomo, maana Kuna watu wanakuombea ushindwe ili wapate cha kuongelea, pia nataka ujue kuwa Kuna siku niliita wazee pale kwangu watusuluhishe, baada ya mama yako kusema hela natumia vibaya hususani wewe, akidai nasomesha mtu mwenye laana, na ambaye ni ngumu kuonesha matunda ya uwekezaji unaofanyika, unasahau Kuna siku ulifukuzwa, na bahati nzuri ndiyo siku narudi, Sasa kile kipindi ndicho mke wangu alitaka wewe ufukuzwe na baada ya wazee kumuuliza ili Aishi na Mimi kwa amani anataka nini , aliwajibu kuwa wewe uache shule siyo uhame nyumbani kwake, la hasha uhame yaani isitumike shilingi yoyote yenye kukuhusu wewe.
Hivyo Mimi na uzee huu nilitumia busara kuwa siwezi kumuacha mke wangu kwa mambo ya kipuuzi na pia siwezi kukufukuza wewe, kisa ujinga wa mtu mmoja, Imani yangu ni Moja juu ya wewe kutuonesha nidhamu mbovu mara kadhaa lakini najua una kitu kichwani kwako kipo kitu.
aliweka kituo mzee Mgaya.
Sasa baba niambie ulifanyaje ili nisifukuzwe, na pia wewe na mama maisha yenu yakiendelea vizuri. aliuliza Samson.
Samson umekua na hakika najivunia kwa Sasa , umeuliza swali zuri ambalo nililisahau,
Ni kwamba nilitumia mbinu ya kumuahidi kiasi fulani cha pesa hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu, na hiyo pesa ipo na ningemuonesha lakini tatizo ameuliza kwa njia ya dharau huku akishinikiza aione Leo leo na Mimi kama mwanaume siwezi kupelekwa kihivyo. Yaani kuona kile kibanda cha Tausi tayari akaona pesa itakuwa imepotea, badala ya kutulia aulize kwa heshima yeye ananiropokea na hata hivyo tarehe ambayo tulipanga haijafika. Pia hela hizo zipo kwenye account ambayo hata nikifa leo yeye ataziona tu kwani taarifa zangu zote anajua hakuna kitu nimemficha, kwani mama Jose ana nini lakini.
aliongea kwa sauti Kali Mzee Mgaya huku akigonga ile meza iliyodizainiwa
Kwa mtindo wa culture ikifanana natumbwi.
Oyaa wewe James vipi muda wote naona uso wako umesawajika nini kinakusibu, na shida yako ni hela tu hakuna namna yaani na tatizo lako wewe muoga, na utakufa masikini, au ndiyo umeshatidhika na maisha yako eeeh. aliongea kwa dharau yule jamaa ambaye umri unafanana na mzee Mgaya kwani wote walikuwa na mvi nyingi za uzee ili tofauti yao ni kwamba huyu mwingine alijiweka kiujana kwani alikuwa kavaa kaptura na vest huku shingoni kukiwa na cheni kadhaa Samson alimkumbuka kuwa ni bwana wake Cathy.
Sikia wewe nipo na mwanangu na sikuzote huwa nakuonya upunguze utani haswa ukinikuta na watoto wadogo kama hawa, aliongea Mzee Mgaya akionesha kukerwa na maneno ya jamaa.
Wewe James vipi bwana, Mimi nakwambia ukweli unadai nakutania ona sasa umepaki land cruiser hapa yaani gari za kwendea safari za mbali mikoani huko wewe unakuja nazo huku wewe vipi au nikuuzie hii yangu, kwanza hela zenyewe unazo. aliendelea na tambo yule jamaa.
Kufumba na kufumbua yule jamaa alipigwa ngumi kwenye paji la uso akaangukia kule, kwenye kokoto huku akivuja damu, Mzee Mgaya akataka kukimbia lakini akazuiwa na baadhi ya watu pale.
Weeee Mzee unaenda wapi nani unataka kumwachia kesi, yaani uuue halafu utuachie msala hebu tulia hapo. Mzee Mgaya alitii amri.
Mzee Mgaya kazua balaa kwenye pub alipoenda kupunguza mawazo,
Mama Kulwa anataka aoneshwe pesa na mumewe na haelewi chochote,
Muda wa Samson kuripoti shule unakaribia, itakuwaje?
Kumbuka Kuna mgeni mama yake Samson naye anatakiwa arudi kijijini.
Itaendelea...............................
