Ahsante sana mkuuasante sana jack kwa simulizi nzuri yenye mafunzo na burudani ndani yake,pia tunashukuru kwa muda wako ulioutumia kuandika simulizi hii
Kwingine kule ulipaona kwa manuela nlikutagndo nafika babe,thnx
Mh sijapaona,siku hizi tag hazionekaniKwingine kule ulipaona kwa manuela nlikutag
Ahsante sana mkuuThanksmkuu
Ubarikiwe sana, hujatuambia mtoto wa Samson aliyezaa na rahma yuko wapiSEHEMU YA MWISHO
Masomo yaliendelea vizuri kwa Samson hata mwalimu mkuu ambaye alikuwa na wasiwasi na Samson akimtaka arudie darasa, alianza kuwa na Imani naye sana tu , Samson aliungana na ndugu zake wale mapacha ambao waliunda utatu fulani mzuri sana kiasi cha kuwashawishi na wengine.
Kitabu na wao, wao na kitabu.
Hii ilipekekea kuwa mfano wa kuigwa hata na wanafunzi wenzao ingawa kulikuwa na vichwa pale darasani kiasi cha Samson kushindwa kuelewa kwani wanafunzi wengine hutumia ubongo huuhuu au Kuna namna nyingine, lakini yote kwa yote Kila mtu alijikuna anapofikia.
Tabia ya mtu ni kama ngozi kuivua inakuwa haiwezekani,
Kuna siku moja Samson alipata kuvutiwa na msichana fulani pale shuleni, akaanza kutupa ndoano zake, Kila msichana wa watu akikataa yeye Samson akawa hakati tamaa, basi siku moja nyakati za usiku walikubaliana wakafanye tendo la kibiologia nyuma kabisa karibu na yalipo majiko ya kupikia ndipo walipofumwa na mwalimu aliyekuwa doria huku akiwatembezea bakora za kutosha. Kwakuwa neno lile Samson hakutaka lienee shuleni pale akaomba msamaha sana huku akitoa rushwa kidogo kwa yule mwalimu na kukubaliwa, lakini licha ya hivyo bado taarifa zilienea kwa baadhi ya wanafunzi ambao walimsema Samson na kumsimanga sana tu, ukawa mwisho wa tabia za kishenzi akaamua kudeal na masomo yake.
Baada ya shule kufunga mwezi wa sita wote watatu walirudi nyumbani na kukuta Kuna mabadiliko kidogo, kuanzia housemaid mpya, lakini pia Samson alishangaa kuona mtoto wake yupo na house girl Kila muda ikabidi aulize,
Mama vipi Rahma yuko wapi mbona simuoni? aliuliza Samson.
(Kwanza mama Kulwa aliguna kisha akaendelea)
Rahma katoroka,
Ilikuwa hivi Kwanza aunt yako Sarah aliaga kwakuwa mkataba wake uliisha kwani nilimchukua kwaajili ya uangalizi wa Rahma akiwa na mtoto mdogo, hivyo alidai anarudi nyumbani ambako Kuna mchumba wake na anaenda kuolewa. Hivyo nikamruhusu aondoke huku nikimkalisha kikao Rahma kuwa Sasa mtoto kakua hivyo anapaswa kufanya kazi zote hapa nyumbani ndipo alikubali huku nikigundua ni kwa shingo upande kwani tangu Samson uondoke alikuwa mnyonge. alifafanua mama Kulwa.
Lakiniiiiiii mmmmh yule mtoto basi tu, Kuna siku nilirudi toka mjini nikakuta hajaandaa chochote humu ndani, hata nilipomwambia Mzee wenu alidai kama nashindana naye basi naweza kumruhusu aondoke lakini kwa moyo wangu wa kibinadamu sikutaka kumfukuza Rahma wangu. mama Kulwa alifafanua Kisha akaendelea....
Baada ya miezi kadhaa kupita Rahma aliniambia kuwa anahitaji kubadili jina la mtoto wake, ikabidi nimuulize kwanini?
Akadai yeye tangu mtoto apewe jina lile hakuwa radhi kwani lipo jina linaloshabihiana na Dini yake ambalo mtoto anataka apewe.
Kiukweli sikumjibu kwani kuhusu yeye kuwa mdini natambua siku nyingi sana hivyo nilimwacha tu.
Baada ya siku mbili hivi wakati narudi toka mjini kwenye biashara zangu nilimkuta kijana fulani aliyevalia kanzu akiwa na muonekano wa kiustadhi,lakini yule kijana baada ya Mimi kuingia naye alitoka muda huo huo. Ikabidi nimuulize Rahma kwanini anaingiza watu ndani mwangu bila uoga Kuna kuibiwa , Kuna kupelelezwa na mengine mengi sana lakini Rahma alichukia na kuondoka usiku huohuo shahidi Mzee Mgaya ambaye alimuona anaburuza begi licha ya kumuita hakutaka kusimama basi Mzee Mgaya aliingia ndani kuja kuniambia hizi habari lakini tulipotoka hatukuiona sura ya Rahma hadi leo hii , akatuachia tu huyu mtoto ambaye nilipata naye taabu hivyo hivyo lakini MUNGU ni mwema mtoto anaendelea vizuri.
Mama Kulwa aliweka kituo.
Kitendo cha kuambiwa Rahma alitoroka kilimtingisha kidogo Samson kwani alimpenda sana lakini hakukuwa na namna ndiyo hivyo alikubaliana na hali.
Kuhusu wazazi wako tunawasiliana nao mara kwa mara, na wanakuombea sana. Na pia Tausi hatunaye mwanangu hivi una taarifa?
Maana Kuna siku Mzee Mgaya alikuja hakuwapa habari hii? aliuliza mama Kulwa.
Samson. Hakuwa na majibu akabaki anaangalia tu, ndipo mama kulwa akafafanua.
Tausi alifariki kwaajili ya gari, ambapo alikuwa anaendesha mwenyewe tena ikiwa ni siku ya kwanza tu tangu anunue akalivamia Lori lililokuwa limepaki pembeni mwa barabara ndipo ukawa mwisho wa uhai wake.
Lakini pia mwanangu Catherine (Cathy) yule sijui hela kapata wapi kwasasa anaishi maeneo wanakoishi watu wazito huko kiufupi hata hapa hajawaji kuja na mawasiliano yetu ni hafifu.alifafanua mama Kulwa ambaye anaonesha alimmiss Samson. Kuliko hata wanaye kwani walikuwa wanapiga stori akimsimulia mambo mbalimbali.
Na pia mwezi wa nane Kuna shughuli nzito hapa maana kaka yako Jose anaoa, japo huyo mchumba sijamuona ila sijapenda aina ya kazi yake nasikia ni mwanasheria kama alivyo kaka yako Sasa hofu yangu mwanangu asifunikwe maana Hawa mabinti wasomi haswa Hawa ma lawyer huwa Wana masharti sana kwenye ndoa, mama Kulwa alionesha hajapenda chaguo la mwanaye Jose.
Hapana mama Mimi nadhani kaka Jose anajua kikubwa heshima na uaminifu Kati Kati yao nadhani wenyewe wanajuana vizuri. alijibu Samson Kwa uelewa wake.
Mmmmh ngoja tuone na tatizo mwanangu hashauriki yule, alilaumu Mama Kulwa.
***************************************Baada ya Samson. Kuhitimu kidato cha nne alirudi nyumbani kama alivyoambiwa na wazazi wake kuwa arudi kijijini afanyiwe tambiko fulani ili kunyoosha mambo yake kama ilivyo kwa makabila mengi nchini. japokuwa hakuwa na Imani na mambo yale lakini aliheshimu wito na maamuzi ya wazazi wake, alikaa zaidi ya wiki kadhaa akiwa anasikilizia matokeo pia ndipo aliporudi mjini baada ya kusikia ataendelea na masomo yake ya kidato cha tano bila wasiwasi.
Cha ajabu wakati anafika nyumbani muda ya usiku kama saa tatu kwenda saa nne alishangaa uwepo wa magari mengi pamoja na wingi wa watu ndipo aliposikia kuwa Mzee wake aliyempa msaada, aliyemfutia ujinga japokuwa hakuwa amemaliza , yaani James Mgaya alikuwa amefariki huku majirani na marafiki wakidai walikuwa wanakunywa wote pombe hata alipodondoka walidhani ni pombe zimemzidia lakini ukweli ni kwamba Mzee Mgaya alikuwa kaaga Dunia.
Samson alilia, akalia na kulia mtu pekee mtetezi na mwenye misimamo yake alikuwa hayupo Tena Samson alijua mwisho wake ndiyo ule. Lakini baada ya taratibu za matanga na mengineyo Joseph James Mgaya alimuita Samson kwenye grocery moja iliyo karibu na nyumbani kwao mazungumzo yakawa hivi.
Samson mdogo wangu nimetambua ulivyolia na ulivyomnyonge mpaka muda huu kutokana na kuondoka kwa Mzee wetu, baba yetu Mzee Mgaya lakini nikutoe wasiwasi Mimi hapa ni mbadala wa mzee Mgaya nitajitahidi kusimamia miradi yake na mambo yake ikiwemo wewe kutimiza ndoto zako hivyo naomba usijisikie vibaya.
Kwa kuondoa shari na migongano ambayo itajitokeza wewe utasoma nje ya Dar es salaam jitahidi kuwa kwenye mstari mnyoofu na maadili mema. yalikuwa ni maneno ya Jose akimfariji Samson.
Kifupi Samson alisoma mpaka chuo kikuu akifanikiwa kupata Degree Moja ya uhandisi huku akipewa ushirikiano na kaka yake Jose,mengine alijiongeza mwenyewe kama ilivyo kwenye mbanga, mishe na habari za kujiongeza town, huku wenzake wakifeli haswa Dotto ambaye alichagua biashara mapema. Hujui Kulwa akiishia kuwa mwalimu wa sekondari.
Mama Kulwa alifariki kipindi Samson akiwa ana kazi, ameoa na ana mtoto mmoja.
Kuhusu wazazi kamili wa Samson wote wapo hai mpaka muda huu , MUNGU awalinde na awazidishie maisha marefu.
Stori ya kweli ya maisha ya Samson, huku majina yaliyotumika humu yakiwa fake ili kuwakwepa watu wa karibu kuunganisha matukio.
Huu ni mwisho wa simulizi yetu.
Hongera ndugu msomaji kwa kuifuatilia Hadi mwisho.
Pia niwaombe radhi kwa kushindwa kuileta muda na wakati sahihi. Tusameheane.
Nikipata muda na wakati wenye utulivu nitaleta simulizi nyingine lengo ni kuburudika na wanajamvi.
Alamsiki.
Sent using Jamii Forums mobile app
SEHEMU YA MWISHO
Masomo yaliendelea vizuri kwa Samson hata mwalimu mkuu ambaye alikuwa na wasiwasi na Samson akimtaka arudie darasa, alianza kuwa na Imani naye sana tu , Samson aliungana na ndugu zake wale mapacha ambao waliunda utatu fulani mzuri sana kiasi cha kuwashawishi na wengine.
Kitabu na wao, wao na kitabu.
Hii ilipekekea kuwa mfano wa kuigwa hata na wanafunzi wenzao ingawa kulikuwa na vichwa pale darasani kiasi cha Samson kushindwa kuelewa kwani wanafunzi wengine hutumia ubongo huuhuu au Kuna namna nyingine, lakini yote kwa yote Kila mtu alijikuna anapofikia.
Tabia ya mtu ni kama ngozi kuivua inakuwa haiwezekani,
Kuna siku moja Samson alipata kuvutiwa na msichana fulani pale shuleni, akaanza kutupa ndoano zake, Kila msichana wa watu akikataa yeye Samson akawa hakati tamaa, basi siku moja nyakati za usiku walikubaliana wakafanye tendo la kibiologia nyuma kabisa karibu na yalipo majiko ya kupikia ndipo walipofumwa na mwalimu aliyekuwa doria huku akiwatembezea bakora za kutosha. Kwakuwa neno lile Samson hakutaka lienee shuleni pale akaomba msamaha sana huku akitoa rushwa kidogo kwa yule mwalimu na kukubaliwa, lakini licha ya hivyo bado taarifa zilienea kwa baadhi ya wanafunzi ambao walimsema Samson na kumsimanga sana tu, ukawa mwisho wa tabia za kishenzi akaamua kudeal na masomo yake.
Baada ya shule kufunga mwezi wa sita wote watatu walirudi nyumbani na kukuta Kuna mabadiliko kidogo, kuanzia housemaid mpya, lakini pia Samson alishangaa kuona mtoto wake yupo na house girl Kila muda ikabidi aulize,
Mama vipi Rahma yuko wapi mbona simuoni? aliuliza Samson.
(Kwanza mama Kulwa aliguna kisha akaendelea)
Rahma katoroka,
Ilikuwa hivi Kwanza aunt yako Sarah aliaga kwakuwa mkataba wake uliisha kwani nilimchukua kwaajili ya uangalizi wa Rahma akiwa na mtoto mdogo, hivyo alidai anarudi nyumbani ambako Kuna mchumba wake na anaenda kuolewa. Hivyo nikamruhusu aondoke huku nikimkalisha kikao Rahma kuwa Sasa mtoto kakua hivyo anapaswa kufanya kazi zote hapa nyumbani ndipo alikubali huku nikigundua ni kwa shingo upande kwani tangu Samson uondoke alikuwa mnyonge. alifafanua mama Kulwa.
Lakiniiiiiii mmmmh yule mtoto basi tu, Kuna siku nilirudi toka mjini nikakuta hajaandaa chochote humu ndani, hata nilipomwambia Mzee wenu alidai kama nashindana naye basi naweza kumruhusu aondoke lakini kwa moyo wangu wa kibinadamu sikutaka kumfukuza Rahma wangu. mama Kulwa alifafanua Kisha akaendelea....
Baada ya miezi kadhaa kupita Rahma aliniambia kuwa anahitaji kubadili jina la mtoto wake, ikabidi nimuulize kwanini?
Akadai yeye tangu mtoto apewe jina lile hakuwa radhi kwani lipo jina linaloshabihiana na Dini yake ambalo mtoto anataka apewe.
Kiukweli sikumjibu kwani kuhusu yeye kuwa mdini natambua siku nyingi sana hivyo nilimwacha tu.
Baada ya siku mbili hivi wakati narudi toka mjini kwenye biashara zangu nilimkuta kijana fulani aliyevalia kanzu akiwa na muonekano wa kiustadhi,lakini yule kijana baada ya Mimi kuingia naye alitoka muda huo huo. Ikabidi nimuulize Rahma kwanini anaingiza watu ndani mwangu bila uoga Kuna kuibiwa , Kuna kupelelezwa na mengine mengi sana lakini Rahma alichukia na kuondoka usiku huohuo shahidi Mzee Mgaya ambaye alimuona anaburuza begi licha ya kumuita hakutaka kusimama basi Mzee Mgaya aliingia ndani kuja kuniambia hizi habari lakini tulipotoka hatukuiona sura ya Rahma hadi leo hii , akatuachia tu huyu mtoto ambaye nilipata naye taabu hivyo hivyo lakini MUNGU ni mwema mtoto anaendelea vizuri.
Mama Kulwa aliweka kituo.
Kitendo cha kuambiwa Rahma alitoroka kilimtingisha kidogo Samson kwani alimpenda sana lakini hakukuwa na namna ndiyo hivyo alikubaliana na hali.
Kuhusu wazazi wako tunawasiliana nao mara kwa mara, na wanakuombea sana. Na pia Tausi hatunaye mwanangu hivi una taarifa?
Maana Kuna siku Mzee Mgaya alikuja hakuwapa habari hii? aliuliza mama Kulwa.
Samson. Hakuwa na majibu akabaki anaangalia tu, ndipo mama kulwa akafafanua.
Tausi alifariki kwaajili ya gari, ambapo alikuwa anaendesha mwenyewe tena ikiwa ni siku ya kwanza tu tangu anunue akalivamia Lori lililokuwa limepaki pembeni mwa barabara ndipo ukawa mwisho wa uhai wake.
Lakini pia mwanangu Catherine (Cathy) yule sijui hela kapata wapi kwasasa anaishi maeneo wanakoishi watu wazito huko kiufupi hata hapa hajawaji kuja na mawasiliano yetu ni hafifu.alifafanua mama Kulwa ambaye anaonesha alimmiss Samson. Kuliko hata wanaye kwani walikuwa wanapiga stori akimsimulia mambo mbalimbali.
Na pia mwezi wa nane Kuna shughuli nzito hapa maana kaka yako Jose anaoa, japo huyo mchumba sijamuona ila sijapenda aina ya kazi yake nasikia ni mwanasheria kama alivyo kaka yako Sasa hofu yangu mwanangu asifunikwe maana Hawa mabinti wasomi haswa Hawa ma lawyer huwa Wana masharti sana kwenye ndoa, mama Kulwa alionesha hajapenda chaguo la mwanaye Jose.
Hapana mama Mimi nadhani kaka Jose anajua kikubwa heshima na uaminifu Kati Kati yao nadhani wenyewe wanajuana vizuri. alijibu Samson Kwa uelewa wake.
Mmmmh ngoja tuone na tatizo mwanangu hashauriki yule, alilaumu Mama Kulwa.
***************************************Baada ya Samson. Kuhitimu kidato cha nne alirudi nyumbani kama alivyoambiwa na wazazi wake kuwa arudi kijijini afanyiwe tambiko fulani ili kunyoosha mambo yake kama ilivyo kwa makabila mengi nchini. japokuwa hakuwa na Imani na mambo yale lakini aliheshimu wito na maamuzi ya wazazi wake, alikaa zaidi ya wiki kadhaa akiwa anasikilizia matokeo pia ndipo aliporudi mjini baada ya kusikia ataendelea na masomo yake ya kidato cha tano bila wasiwasi.
Cha ajabu wakati anafika nyumbani muda ya usiku kama saa tatu kwenda saa nne alishangaa uwepo wa magari mengi pamoja na wingi wa watu ndipo aliposikia kuwa Mzee wake aliyempa msaada, aliyemfutia ujinga japokuwa hakuwa amemaliza , yaani James Mgaya alikuwa amefariki huku majirani na marafiki wakidai walikuwa wanakunywa wote pombe hata alipodondoka walidhani ni pombe zimemzidia lakini ukweli ni kwamba Mzee Mgaya alikuwa kaaga Dunia.
Samson alilia, akalia na kulia mtu pekee mtetezi na mwenye misimamo yake alikuwa hayupo Tena Samson alijua mwisho wake ndiyo ule. Lakini baada ya taratibu za matanga na mengineyo Joseph James Mgaya alimuita Samson kwenye grocery moja iliyo karibu na nyumbani kwao mazungumzo yakawa hivi.
Samson mdogo wangu nimetambua ulivyolia na ulivyomnyonge mpaka muda huu kutokana na kuondoka kwa Mzee wetu, baba yetu Mzee Mgaya lakini nikutoe wasiwasi Mimi hapa ni mbadala wa mzee Mgaya nitajitahidi kusimamia miradi yake na mambo yake ikiwemo wewe kutimiza ndoto zako hivyo naomba usijisikie vibaya.
Kwa kuondoa shari na migongano ambayo itajitokeza wewe utasoma nje ya Dar es salaam jitahidi kuwa kwenye mstari mnyoofu na maadili mema. yalikuwa ni maneno ya Jose akimfariji Samson.
Kifupi Samson alisoma mpaka chuo kikuu akifanikiwa kupata Degree Moja ya uhandisi huku akipewa ushirikiano na kaka yake Jose,mengine alijiongeza mwenyewe kama ilivyo kwenye mbanga, mishe na habari za kujiongeza town, huku wenzake wakifeli haswa Dotto ambaye alichagua biashara mapema. Hujui Kulwa akiishia kuwa mwalimu wa sekondari.
Mama Kulwa alifariki kipindi Samson akiwa ana kazi, ameoa na ana mtoto mmoja.
Kuhusu wazazi kamili wa Samson wote wapo hai mpaka muda huu , MUNGU awalinde na awazidishie maisha marefu.
Stori ya kweli ya maisha ya Samson, huku majina yaliyotumika humu yakiwa fake ili kuwakwepa watu wa karibu kuunganisha matukio.
Huu ni mwisho wa simulizi yetu.
Hongera ndugu msomaji kwa kuifuatilia Hadi mwisho.
Pia niwaombe radhi kwa kushindwa kuileta muda na wakati sahihi. Tusameheane.
Nikipata muda na wakati wenye utulivu nitaleta simulizi nyingine lengo ni kuburudika na wanajamvi.
Alamsiki.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hongera kwa kusoma, ila siku nyingine usimkwaze Mr mkuuAsante J.D kwa simulizi yako,Jana sijalala nimekesha mpaka nagombana na mume wangu mwanga wa simu unamkera,Leo nimeamka nayo ndo nimeimaliza.




Sawa nasubiri ile nyingine ya bwana police Hussein wa madiniHongera kwa kusoma, ila siku nyingine usimkwaze Mr mkuu![]()
[emoji23![]()
AsanteSEHEMU YA PILI.
Mwanangu Samson, nakuonea huruma sana kwa aina ya maisha yako unayoenda nayo, nakuomba ubadilike mwanangu, unatambua fika hali halisi ya maisha yetu kwamba sisi wazazi wako ni masikini.
Sasa iweje umpe kazi mama yako Kila siku anaongea na wewe mtu mmoja, kwanini?
Hapo ulipo si mtoto tena ni mvulana mkubwa ambaye unategemewa, yaani naamini wewe ni msaada mkubwa pindi nikiwa sipo, lakini ya MUNGU mengi naweza kutangulia kufa hata leo nawaacha watoto wangu wengi tu lakini nyinyi wa kiume ndiyo nguzo pekee ya kuongoza hata hao dada zenu.
Badilika mwanangu, sitaki niwe nagombana na wewe kila wakati, ifike mahali nikuheshimu kama mwanangu na utuheshimu kama wazazi wako.
Yalikuwa ni naneno machache ya mzee Mgaya ambapo kwanza mama Mgaya mwenyewe alishangaa lakini pia hata Samson, maana kwa mkono mwepesi wa maamuzi wa mzee yule hakuna aliyefikiri kuwa ataongea maneno matupu bila makofi au viboko, ila kwa siku Ile alikuwa kawaida.
Siku ya pili kulikucha Samson akiwa anafanya kazi ya kuhamisha matofalu toka kwenye tanuri kuleta karibu na msingi uliochimbwa, karibu na nyumba yao kwaajili ya ujenzi, ni kazi ambayo alikuwa anafanya basi tu,labda kwakuwa baba yake alikuwepo.
Mara Kuna kijana jobless ambaye ni Rika la samson ila yeye aliacha shule kitambo sana, alipita karibu na anaposomba tofali Samson.
Oyaaaah Sam vipi, naona unapiga kazi mwanangu, dah sema Nini mi hata siwezi weee, we mitofali kama hiyo unajitwisha kichwani, kwanini usingetumia hata toroli Samuuuu?
We acha tu na hapa nilipo sijui Nina mkosi gani yaani tangu nimalize shule wananitumatuma tu, Mara fanya hiki Mara hili ili mradi wanione nafanya kazi, sijui haya mateso yataisha lini. alijisemea Samson.
(Hahaha) tatizo wewe Sam muoga sana, kwanza nikuulize, kwani hao mafundi ujenzi si wanalipwa? aliuliza yule kijana.
Wanalipwa ndiyo, na hapa nikifikia hatua fulani kwenye kusogeza tofali, nimeambiwa nijaze Yale mapipa ya maji Sasa jamaa yangu huu si uonevu kweli huu?yaani kulipwa walipwe wengine kazi nifanye Mimi kweli? alihoji Samson huku akionesha kukerwa sana na ile kazi.
Waliendelea kuongea mambo yao ya kipumbavu huku wakishawishiana mambo ya hovyo kulingana na umri wao, foolish age.
Mida ya saa kumi na mbili jioni familia nzima ilikuwa Barazani ikipunga upepo, mama Mgaya akavunja ukimya,
Hongera mwanangu Leo umefanya kazi kubwa na nzuri sana,
Weee kweli kabisa mama leo kaka Sam kafanya kazi nzuri wote tumeona jamani,. walidakia Dada zake Sam huku wakionesha kufurahi. Lakini Cha ajabu licha ya pongezi zote Sam alikuwa kakunja ndita kwa hasira akionesha hahitaji sifa wala pongezi zozote, uzuri hakujibu kitu .
Kwahiyo umekasirika, we mjinga nini, unadhani ukinikasirikia ndiyo hutatumwa Tena, muone kwanza sura yake, Mimi ni mama yako mpumbavu wewe na hapa ulipo kila kazi unayostahili utafanya, sijui unajiona nani humu ñdani, au kwakuwa Jana baba yako kaamua kukuacha hajakutia bakora? Naunajua Nini kingetokea . aliongea mama yake Samson kwa hasira huku samsoni mwenyewe akikimbilia ndani.
Usiku wa siku ile Samson aliwaza mambo mengi sana, alihisi ananyanyaswa, anaonewa.
Akawaza na kuwazua, akapata jibu kuwa njia pekee ya kuepukana na Yale yote ni kutoroka, ulikuwa ni msimu wa kuandaa Mashamba ya mpunga huko mbeya, kwahiyo maeneo ya Madibira, Rujewa ilikuwa ni moja ya sehemu ambazo angeelekea kwakuwa zinasifika kwa upatikanaji wa vibarua.
Aliwaza anatokaje nyumbani na nauli Hana, akapata wazo la kukamata kuku ili akauze apate nauli.
Asubuhi ilifika watu wote wakawa wanajiandaa kwaajili ya kuelekea kanisani, huku Samson akiachwa nyumbani.
Samson alifurahi sana kwakuwa ilikuwa ni opportunity nzuri ya yeye kubeba vitu vyake atoroke, akawaza sehemu rahisi ya kwenda na ni karibu ni Madibira, maana huko pia Kuna ndugu wanaishi huko hivyo akiulizia ulizia anaweza kuwapata, akachukua kibegi Chake akakibana mgongoni huku makwapani akiwa kabana kuku wawili .
Hakutembea sana,akakutana na mnunuzi wa kuku ambaye alikuwa na tenga lake kwenye baiskeli akiokoteza kuku kwa majirani , yule mnunuzi aliwachukua wale kuku kwa bei ya chini Sana labda kwasababu muuzaji alikuwa ni mtoto tena asiye mzoefu wa kuuza.
Sikia dogo Hawa kuku kwanza wanaumwa, na Mimi najua huu msimu wa kilimo wengi wanauza kuku hivyo kama huridhiki na bei niliyokutajia basi. aliongea kwa mbwembwe yule mnunuzi.
Samson kusikia vile hakuwa na ka kufanya kwasababu kwanza hawezi kurudisha kuku, akikuta wazazi wake wamerudi atasema alikuwa anawapeleka wapi, pia bei aliyoambiwa kwa kuku wote nauli ilitosha kumfikisha sehemu husika na chenji inabaki akauza hivyo hivyo kwa hasara.
Akasogea kwenye kituo akakwea gari kuelekea alikopanga.
Huku nyuma mama Mgaya na mabinti zake walirudi toka kanisani ila licha ya kutokumkuta Samson hawakushituka, kwakuwa ni kawaida yake kwenda kucheza mpira au kwenda kuangalia mapigano ya ng'ombe huko malishoni.
Hakuna aliyekundua upungufu wa kuku kwa haraka haraka, naana kila mtu alikuwa busy na Mambo yake, baada ya kazi za hapa na pale Dada yake Sam aitwaye Jane, alihoji.
Jamani wenzangu, hivi kaka Sam mpaka saizi mbona si kawaida?
Maana tayari Giza linaingia.aliuliza Jane
Wee Kaa kimya huyu Leo atanitambua maana sijui Mimi ananichukuliaje huyu bila kuchapwa haelewi Sasa Leo atanitambua. alidakia mzee Mgaya huku akizunguka nyuma ya nyumba yao kuchuma fimbo .
Dakika, Mara masaa yalikatika huku hofu, wasiwasi kwa Kila mmoja ukichukua nafasi yake. Mume wangu ni saa tano kasoro hii mwanangu hajarudi atakuwa wapi? Ni mtoto yule ujue mmmh mwenzangu Mimi hata sielewi. alianza kulalamika mama Mgaya
Atarudi tuu mke wangu, we unadhani awe wapi yule, usikute yupo kwa marafiki zake. alitoa jibu jepesi mzee Mgaya. japo hata yeye tayari alishaingiwa na wasiwasi, maana siyo kwa usiku ule.
Kwa marafiki zake? Marafiki gani, tangu lini mwanangu ukaona kalala kwa mtu?
aliongea kwa ukali na hasira mama Mgaya huku akitoka nje.
Itaendelea....................