Jack Daniel
JF-Expert Member
- Sep 23, 2021
- 2,146
- 10,380
SEHEMU YA KWANZA.(utangulizi)
Sam, saam , samsoniii, huko unakoenda hakikisha unakula huko huko, maana huwezi kunisumbua kila siku , kwanini husikii weee mtoto Sasa nikwambie tu kuwa leo hakuna kula hapa nyumbani. nakwambia rudi sam, rudiii au unataka nimwambie baba yako akija, umesahau alichokufanyia Mara ya mwisho
Wewe, weeeeeeeeeh.
Yalikuwa ni maneno ya mke wa mzee
Mgaya, au mama yake na Samson, akimtaka mwanaye arudi ili aendelee na kazi za pale nyumbani kwao kuliko kwenda kuchunga ng'ombe wa watu tu, wakati wao hawana hata ng'ombe mmoja.
Lakini maneno yale wala hayakuweza kusaidia chochote maana Samson alizidi kutokomea porini akifuata kundi kubwa la ng'ombe kutoka kaya tofauti tofauti.huku jambo pekee lililo kuwa linampeleka Samson kule ni sinema za bure, yaani ng'ombe wanapopigana.
Iko hivi , tukiacha wafugaji wakubwa kama wamasai,wamang'ati na wasukuma, wapo baadhi ya makabila wengi wanafuga ng'ombe, mbuzi, kondoo na hata kuku, ni kawaida tu kukuta karibu Kila kaya Ina mifugo, utakuta hapa Kuna ng'ombe ishirini, hapa kumi na tano sehemu nyingine hata ng'ombe zaidi ya hamsini.
Lakini pia wapo watu wanaoazima ng'ombe wa mtu kwa lengo la kujipatia mbolea(samadi) kwaajili ya kukuzia mazao mbalimbali,
Yaani mtu unakaa na ng'ombe zaidi ya ishirini wa mtu lengo ni maziwa na mbolea, japo hata hayo maziwa huwa siyo mengi kutokana na aina ya ufugaji, kwani si wa kisasa.
Basi wakati mifugo kama ng'ombe wanakutana malishoni(nyikani) huwa Kuna kutambiana kwa madume au mafahali kutoka vikundi tofauti tofauti huku kukiwa na wale mafahali wanaojulikana kabisa kuwa ni unbeaten yaani wanatisha kwa kupigana.
Ni mchezo mzuri na watoto wengi wa vijijini huwa wanaenjoy sana kuangalia mapambano ambayo kwa kweli huwa yanaburudisha japo ni hatari maana huwa Kuna ng'ombe wenye hasira pale anapopigwa au anaposhinda hivyo ule ushindi wake humfanya aone anamudu Kila kiumbe.
Wenye mchezo wao Wala huwa hawapati taabu yaani wakiona mpambano ushaanza wanapanda juu ya miti huku wakienjoy game Bila wasiwasi, huku yule mwenye ng'ombe aliyeshinda akiheshimika kana kwamba kapigana yeye na Kuna wakati mnamaindiana kiasi Cha kuzichapa wenyewe.
Ni mchezo mzuri sana hasa ukiwakutanisha mafahali wale ving'ang'anizi inachukua muda wa lisaa au masaa mawili huku wafuatiliaji wakichukua points ni fahali yupi anajua vichwa na yupi anajua kutumia pembe zake vizuri, hakika ni mchezo unaovutia watoto wa vijijini, lakini pia hata sare hutokea. Kivipi?
Ni pale ng'ombe wanapochoka na kubaki wanaangaliana na Lila mmoja kushika njia yake wakiendelea kula majani, au ni pale waangaliaji wanapochoka yaani burudani inatosha, mshindi hapatikani , au Giza linaingia wanaachanishwa huku mkipanga namna ya kukutana siku nyingine.
Ni mchezo mzuri sana, wakati waliozaliwa mjini wakiinjoi mapambano ya akina Evander na akina Tyson, M. Alli watoto wa kijijini Wana namna yao ya kufurahi.
Samsoni ni mtoto pekee wa kiume kwenye familia ya watoto wanne wa mama mgaya huku yeye akiwa watatu kuzaliwa, huku kwa baba yake wakiwa ni wengi maana mzee mgaya alikuwa na wake wawili.
Miaka ya 1996 alianza darasa la kwanza kijijini kwao akiwa na umri wa miaka kumi, umri ule haukuwa kikwazo sana maana Elimu ilipewa kipaumbele sana hasa maeneo ya vijijini huku sera ile ikichagizwa na serikali mpya ya hayati B. W. Mkapa.
Hivyo watendaji na wenyeviti walihimiza watoto wote waanze darasa la kwanza huku wengine wakiwa na umri mkubwa zaidi ya Samsoni, basi samsoni alijitahidi sana kusoma kwa mbinde na uvumilivu wa hali ya juu kwani changamoto kubwa ilikuwa ni umbali kutoka huko mashambani anakoishi Hadi kijijini ilipo shule yao.
Alijitahidi Hadi pale alipohitimu shule ya msingi akiwa na umri wa miaka kumi na Saba, alimaliza na umri huo ni baada ya kufeli darasa la nne akalazimika kurudia darasa.basi baada ya kumaliza Elimu ya msingi hakukuwa na matarajio yoyote kwa labda ataenda Sekondari, si wazazi wake Wala si yeye mwenyewe ambaye aliwaza hatima ya aendelee shule ya upili au awe na mishe zingine.
Miaka kumi na Saba kwa mtoto ambaye kakulia kijijini huwa haha mature bado tofauti na aliyekulia mjini, basi balehe ilimfanya Samsoni awe mbishi, kiburi, jeuri na asiyependa kazi za pale nyumbani kwao, badala yake ni kwenda kucheza mpira wa makaratasi, au kwenda kuangalia mapigano ya ng'ombe huko malishoni.
Kwakuwa baba yake alikuwa na nyumba mbili {wake wawili}basi mama Mgaya alijikuta anapata kazi kubwa ya kuhandle kijana wake ambaye alikuwa akimgomea kazi nyingi ikiwemo kutokujijali yeye mwenyewe, maana hata kuoga yaani usafi unaohusu mwili wake samsoni ilikuwa Hadi akumbushwe vinginevyo na baridi la mkoani inaweza kupita siku kibao hajaoga.
Basi siku moja baba yake Samson mzee Mgaya alirudi nyumbani akitokea kwa mke mdogo, alifika pale huku akiegesha baiskeli yake aina ya Avon ukutani, huku akisikia makelele ndani yaliyoashiria hakukuwa na amani. Sauti alizitambua ni Samson na mama yake.
Vipi jamani Kuna Nini? Enhhhee mama Jane Kuna Nini na mwanao?
Aliuliza mzee mgaya. (Huku akimdaka Samson ambaye alitaka kupenya pale mlangoni akimbie)
Kaa chini wewe. aliamrisha Mzee Mgaya.
Afadhali umekuja, Tena ni kama MUNGU kakuleta Mimi nimechoka baba nimechoka, hebu muangalie mwanao, mtazame mavazi na nguo zake, haogi, hafui hapo alipo ukiingia ndani kwake hakutamani , Wala huwezi amini kama analala binadamu. Naomba nisaidie mwanao anatia aibu, nasema Bora hata alivyokuwa shule kuliko anavyoshinda hapa maana anazidi kuniongezea mawazo nashindwa kujua kwani nilimzaa mtoto wa aina gani.
Alilalamika mama Mgaya huku akizidi kumpalia makaa Samson, maana alijua fika tabia ya mzee Mgaya, akianza kupiga mtoto haangalii wapi anachapa.
Inajulikana kuwa samsoni hasikii vizuri kutokana na Kofi alilowahi kupigwa na baba yake kwa tuhuma za kusababisha pancha kwenye baiskeli yake.
Kitendo hiki kilimuuma mama Mgaya kwamba kwanini ampige mtoto mdogo kama anapigana na mtu mzima, na kupelekea mtoto akawa hasikii vizuri.
Lakini siku hiyo Wala hakujali aliamua liwalo na liwe maana samsoni alizidi ukorofi.
Mzee Mgaya alivuta kiti akakaa, akamsogeza Samson karibu na alipokaa akamwangalia kama sekunde kadhaa hivi bila kusema chochote Kisha akajiinamia chini huku akicheka kwa kumuhurumia Samson.
Itaendelea......................
Sam, saam , samsoniii, huko unakoenda hakikisha unakula huko huko, maana huwezi kunisumbua kila siku , kwanini husikii weee mtoto Sasa nikwambie tu kuwa leo hakuna kula hapa nyumbani. nakwambia rudi sam, rudiii au unataka nimwambie baba yako akija, umesahau alichokufanyia Mara ya mwisho
Wewe, weeeeeeeeeh.
Yalikuwa ni maneno ya mke wa mzee
Mgaya, au mama yake na Samson, akimtaka mwanaye arudi ili aendelee na kazi za pale nyumbani kwao kuliko kwenda kuchunga ng'ombe wa watu tu, wakati wao hawana hata ng'ombe mmoja.
Lakini maneno yale wala hayakuweza kusaidia chochote maana Samson alizidi kutokomea porini akifuata kundi kubwa la ng'ombe kutoka kaya tofauti tofauti.huku jambo pekee lililo kuwa linampeleka Samson kule ni sinema za bure, yaani ng'ombe wanapopigana.
Iko hivi , tukiacha wafugaji wakubwa kama wamasai,wamang'ati na wasukuma, wapo baadhi ya makabila wengi wanafuga ng'ombe, mbuzi, kondoo na hata kuku, ni kawaida tu kukuta karibu Kila kaya Ina mifugo, utakuta hapa Kuna ng'ombe ishirini, hapa kumi na tano sehemu nyingine hata ng'ombe zaidi ya hamsini.
Lakini pia wapo watu wanaoazima ng'ombe wa mtu kwa lengo la kujipatia mbolea(samadi) kwaajili ya kukuzia mazao mbalimbali,
Yaani mtu unakaa na ng'ombe zaidi ya ishirini wa mtu lengo ni maziwa na mbolea, japo hata hayo maziwa huwa siyo mengi kutokana na aina ya ufugaji, kwani si wa kisasa.
Basi wakati mifugo kama ng'ombe wanakutana malishoni(nyikani) huwa Kuna kutambiana kwa madume au mafahali kutoka vikundi tofauti tofauti huku kukiwa na wale mafahali wanaojulikana kabisa kuwa ni unbeaten yaani wanatisha kwa kupigana.
Ni mchezo mzuri na watoto wengi wa vijijini huwa wanaenjoy sana kuangalia mapambano ambayo kwa kweli huwa yanaburudisha japo ni hatari maana huwa Kuna ng'ombe wenye hasira pale anapopigwa au anaposhinda hivyo ule ushindi wake humfanya aone anamudu Kila kiumbe.
Wenye mchezo wao Wala huwa hawapati taabu yaani wakiona mpambano ushaanza wanapanda juu ya miti huku wakienjoy game Bila wasiwasi, huku yule mwenye ng'ombe aliyeshinda akiheshimika kana kwamba kapigana yeye na Kuna wakati mnamaindiana kiasi Cha kuzichapa wenyewe.
Ni mchezo mzuri sana hasa ukiwakutanisha mafahali wale ving'ang'anizi inachukua muda wa lisaa au masaa mawili huku wafuatiliaji wakichukua points ni fahali yupi anajua vichwa na yupi anajua kutumia pembe zake vizuri, hakika ni mchezo unaovutia watoto wa vijijini, lakini pia hata sare hutokea. Kivipi?
Ni pale ng'ombe wanapochoka na kubaki wanaangaliana na Lila mmoja kushika njia yake wakiendelea kula majani, au ni pale waangaliaji wanapochoka yaani burudani inatosha, mshindi hapatikani , au Giza linaingia wanaachanishwa huku mkipanga namna ya kukutana siku nyingine.
Ni mchezo mzuri sana, wakati waliozaliwa mjini wakiinjoi mapambano ya akina Evander na akina Tyson, M. Alli watoto wa kijijini Wana namna yao ya kufurahi.
Samsoni ni mtoto pekee wa kiume kwenye familia ya watoto wanne wa mama mgaya huku yeye akiwa watatu kuzaliwa, huku kwa baba yake wakiwa ni wengi maana mzee mgaya alikuwa na wake wawili.
Miaka ya 1996 alianza darasa la kwanza kijijini kwao akiwa na umri wa miaka kumi, umri ule haukuwa kikwazo sana maana Elimu ilipewa kipaumbele sana hasa maeneo ya vijijini huku sera ile ikichagizwa na serikali mpya ya hayati B. W. Mkapa.
Hivyo watendaji na wenyeviti walihimiza watoto wote waanze darasa la kwanza huku wengine wakiwa na umri mkubwa zaidi ya Samsoni, basi samsoni alijitahidi sana kusoma kwa mbinde na uvumilivu wa hali ya juu kwani changamoto kubwa ilikuwa ni umbali kutoka huko mashambani anakoishi Hadi kijijini ilipo shule yao.
Alijitahidi Hadi pale alipohitimu shule ya msingi akiwa na umri wa miaka kumi na Saba, alimaliza na umri huo ni baada ya kufeli darasa la nne akalazimika kurudia darasa.basi baada ya kumaliza Elimu ya msingi hakukuwa na matarajio yoyote kwa labda ataenda Sekondari, si wazazi wake Wala si yeye mwenyewe ambaye aliwaza hatima ya aendelee shule ya upili au awe na mishe zingine.
Miaka kumi na Saba kwa mtoto ambaye kakulia kijijini huwa haha mature bado tofauti na aliyekulia mjini, basi balehe ilimfanya Samsoni awe mbishi, kiburi, jeuri na asiyependa kazi za pale nyumbani kwao, badala yake ni kwenda kucheza mpira wa makaratasi, au kwenda kuangalia mapigano ya ng'ombe huko malishoni.
Kwakuwa baba yake alikuwa na nyumba mbili {wake wawili}basi mama Mgaya alijikuta anapata kazi kubwa ya kuhandle kijana wake ambaye alikuwa akimgomea kazi nyingi ikiwemo kutokujijali yeye mwenyewe, maana hata kuoga yaani usafi unaohusu mwili wake samsoni ilikuwa Hadi akumbushwe vinginevyo na baridi la mkoani inaweza kupita siku kibao hajaoga.
Basi siku moja baba yake Samson mzee Mgaya alirudi nyumbani akitokea kwa mke mdogo, alifika pale huku akiegesha baiskeli yake aina ya Avon ukutani, huku akisikia makelele ndani yaliyoashiria hakukuwa na amani. Sauti alizitambua ni Samson na mama yake.
Vipi jamani Kuna Nini? Enhhhee mama Jane Kuna Nini na mwanao?
Aliuliza mzee mgaya. (Huku akimdaka Samson ambaye alitaka kupenya pale mlangoni akimbie)
Kaa chini wewe. aliamrisha Mzee Mgaya.
Afadhali umekuja, Tena ni kama MUNGU kakuleta Mimi nimechoka baba nimechoka, hebu muangalie mwanao, mtazame mavazi na nguo zake, haogi, hafui hapo alipo ukiingia ndani kwake hakutamani , Wala huwezi amini kama analala binadamu. Naomba nisaidie mwanao anatia aibu, nasema Bora hata alivyokuwa shule kuliko anavyoshinda hapa maana anazidi kuniongezea mawazo nashindwa kujua kwani nilimzaa mtoto wa aina gani.
Alilalamika mama Mgaya huku akizidi kumpalia makaa Samson, maana alijua fika tabia ya mzee Mgaya, akianza kupiga mtoto haangalii wapi anachapa.
Inajulikana kuwa samsoni hasikii vizuri kutokana na Kofi alilowahi kupigwa na baba yake kwa tuhuma za kusababisha pancha kwenye baiskeli yake.
Kitendo hiki kilimuuma mama Mgaya kwamba kwanini ampige mtoto mdogo kama anapigana na mtu mzima, na kupelekea mtoto akawa hasikii vizuri.
Lakini siku hiyo Wala hakujali aliamua liwalo na liwe maana samsoni alizidi ukorofi.
Mzee Mgaya alivuta kiti akakaa, akamsogeza Samson karibu na alipokaa akamwangalia kama sekunde kadhaa hivi bila kusema chochote Kisha akajiinamia chini huku akicheka kwa kumuhurumia Samson.
Itaendelea......................