SEHEMU YA HAMSINI NA NANE
Hata muda wa kwenda nyumbani ulipofika Samson alikuwa mzito kwenda nyumbani alitamani angekaa tu darasani kwaajili ya kujisomea, lakini hata hivyo angeelewa nini?
Mawazo na hofu ya kuacha shule vilimsumbua sana.
Wanafunzi wenzake walitawanyika huku yeye akirudi darasani kwaajili ya kuzugazuga ili kupoteza muda ili afike nyumbani usiku,
Oyaa Sam mbona huoneshi kuondoka vipi, Mimi nadhani ni vyema ungeenda kula kabisa maana si tuliambizana turudi baada ya kula? Fanya hivyo mwanangu basi maana tunaweza kupishana, wewe unaenda sisi tunarudi tutakuwa tunafanya nini? aliongea mwanafunzi mmoja kutoka lile group la Samson kama walivyokubaliana warudi baada ya kula waje kujadili mambo yao.
Haina shida, Mimi mtanikuta humu humu, nyie nendeni tu. alijibu kifupi Samson.
Yule mwanafunzi alimwangalia Samson, kitambo kidogo Kisha akasema,
Unajua wee Sam tumegundua Leo huna furaha kabisa tatizo ni Nini, kwasababu hata muda wa mapumziko hukutoka, na hujala chochote muda ule, na saizi eti huendi nyumbani, kwani una Nini Sam. Unajua kundi letu Kuna baadhi wamedai tukupige chini na nafasi yako achukue mtu mwingine, lakini Mimi nimekutetea kuwa huenda hayupo sawa. aliweka kituo yule mwanafunzi huku akimwangalia Sam kwa umakini.
Watu bwana Sasa wanitenge kwenye kundi Mimi kosa langu nini, aliuliza Samson.
Wanakuona kama una kisirani sana, wewe mwenyewe jiangalie, Leo utakuja tutacheka tutafurahi tutasoma kwa pamoja, kesho utakuja Ukiwa tofauti ukionekana umenuna, nani umemnunia inakuwa haieleweki, na tulichogundua kutoka kwako Samson ni mademu, hususan yule msichana mnayekaa naye, Sasa nadhani kila anapokuzingua na wewe inapelekea kupoteza baadhi ya mambo fulani.demu kashakukataa ndiyo maana upo hivyo, na haya mambo ya kuchanganya mapenzi na masomo yatakugharimu.
Sam huo ndiyo ukweli, wapo wasiojua lakini baadhi kwenye kundi letu tushajua, na omba hizi taarifa zisifike kwa walimu nahisi utakuwa hatarini zaidi . alizidi kupigilia msumari yule mwanafunzi mwenzie.
Unasikia wewe Mimi sijawahi kuwaza wanawake, Mimi nimepokea taarifa mbaya, toka kijijini kwetu ndiyo maana unaona Niko hivi, sawa hakuna shida kama mmeamua kunizushia mnayoyajua nyinyi badala yangu Haina shida.
Samson alijifanya amekasirika huku yale aliyoambiwa yakimchoma kama mwiba maana kulikuwa na ukweli unaofanana
Aliinuka na kubeba begi lake, huku akipiga hatua kuelekea nje, alitamani angekuwa anakaa mbali ili achelewe kidogo maana hakutaka kufika mapema, lakini hakukuwa na jinsi tayari alikuwa anaangaliana na geti la nyumbani kwao muda mfupi tu.
Aligonga Kisha akasikia hatua za mtu kuja kufungua,
Rahma alifungua mlango Kisha akatabasamu baada ya kumuona Samson, lakini Samson hakutaka mazoea akasalimia kisha akawa anaenda ndani huku moyo Ukiwa bado unadunda dunda maana alijua kama wazee watakuwepo basi maada itazaliwa upya lakini hakuona dalili za uwepo wa mtu tofauti na Rahma, akamgeukia Rahma na kuuliza, vipi wazee wapo?
Hawapo, baba tangu alivyoondoka asubuhi, na mama naye kaenda mjini nadhani dukani kwake, alipita Cathy hapa wakachukuana wakaondoka, alijibu Rahma.
Lakini kaka Sam pole sana kwa mambo yaliyotokea jana, yaani nimewaza sana nakujikuta Mimi ndiye msababishaji, nilijisahau mwenzio, nikajikuta nimeweka komeo bila kujua kuwa utakuja, naomba nisamehe sana, lakini pia usijali Mimi nipo Kila kitu kitakuwa sawa, aliongea Rahma kwa hisia huku Samson akiwa anamwangalia kwa macho yanayoonesha hapendi anachoambiwa.
Akaingia ndani pitiliza hadi chumbani kwake, akawa anapanga vitu vyake huku akikumbuka kuwa aliambiwa aandike barua ya maelezo yanayoonesha hatarudia aliyoyafanya. Akatafuta karatasi nzuri huku akibuni maneno mazuri anayohisi yatawashawishi wazazi wake,
MUNGU nisaidie niokoe na hii hali nayopitia , nitaishije Sasa Ina maana narudi kijijini bila kutimiza ndoto zangu? na hili naliona lipo wazi muda wowote nitaanguka, ama kweli ng'ombe wa masikini hazai hata akizaa huzaa dume. lengo mambo mazuri yasiendelee, wakati akiwaza yale sauti ya Rahma ilisikika toka sebuleni.
Sasa kaka Sam ina maana huli Chakula leo, njoo basi Kuna mtu anakuita huku,
Samson alitoka huku akiwa na shauku ya kumjua huyo anayemuita lakini hakuona mtu,
Nani ananiita , aliuliza Samson.
Wewe kula kwanza Sam , hakuna anayekuita mimi nakuonea huruma mdogo wangu, nakuita mdogo wangu kwasababu Kwa umri wako Mimi nimekuzidi miaka saba, najua sura yangu hii inawafanya watu wanione mtoto, ila Mimi ni mkubwa,
Halafu Sam usijali Mimi mchana nimeongea na mama kuwa wewe huna tabia hizo na hujawahi kufanya mambo hayo ila ni shetani tu, na mama kaelewa. Rahma aliendelea kuongea huku akiwa hajibiwi lolote na Samson, hata baada ya kumaliza kula Samson alirudi chumbani kwake
Wewe Sam njoo kwanza mama aliacha maagizo hapa, kule jiko la umeme limeharibika sijui Kuna Nini, hivyo alisema ukirudi umfuate fundi aje arekebishe, nadhani angenituma Mimi lakini ana sababu ambazo zinapelekea asinitume.
Samson hakujibu kitu, yaani hakutaka kuongea na Rahma hata ule ukaribu hakutaka alifungua geti na kuingia mtaani akimfuata yule fundi ambaye alimkuta ofisini kwake akiwa anabishana mwanamke anayeonekana ni mkewe.
Sasa mke wanguuu, hali ni ngumu naomba unielewe , yaani huwezi amini tangu nafika hapa saa mbili asubuhi hakuna mteja aliyekuja hata mmoja eeh, hivyo Sina kitu mpaka saa kumi na mbili hii na ni Bora nifunge tu maana muda umeisha nimeshindwa kupokea wateja mchana watakuja usiku? alijitetea yule fundi kwa mkewe ambaye alionekana kafuata hela.
Wewe dogo vipi unasikiliza maongezi ya watu hebu Kaa pembeni basi , kwanza hata husalimii halafu unasogea hapa huna adabu nini wewe, aliongea yule fundi kwa ukali.
Hapana bro mimi nimeambiwa nikufuate,jiko letu limesumbua twende ukaliangalie, aliongea kivivu Samson.
Ahaaaaa basi sorry dogo ngoja nichukue vifaa,alijibu Kwa pupa yule fundi.
Unaona mke wanguu Mimi nilikwambia lazima uwe na Imani, MUNGU ndiye muweza na mpaji wa vyote, ona sasa riziki imekuja jiooooni kabisa, basi tangulia nyumbani kipenzi changu Mimi narudi Sasa hivi, aliongea yule fundi wakiangaliana na mkewe huku wote wakitabasamu.
Mmmh kweli hii ndiyo Dar es salaam, Ina maana bila Mimi kumtafuta wangeishije sasa, yaani maisha haya acha tu. Samson alijiwazia moyoni.
Walifika nyumbani fundi akaoneshwa kazi huku akiianza kwa mbwembwe zote Samson akiwa pembeni akimwangalia tu, ndani ya dakika kadhaa fundi alimaliza kazi huku, akisubiri malipo.
Da Rahma uko wapi, fundi amemaliza kazi yake huku njoo umlipe wewe si ndiye uliyeachiwa maagizo yote.aliita Samson
Rahma alikuja akamkabidhi pesa yule fundi ambaye uso wake ulionesha amefurahi sana, huenda malipo yalikuwa makubwa kuliko kazi.
Wakati Samson akimsindikiza fundi ili atoke na yeye afunge geti, fundi alianza mambo yake,
Aisee dogo hivi huyo dada unamuitaje, maana mwenyezi MUNGU anaumba jamani yupo vizuri sana Mashallah ,unaweza kuniitia niongee naye kidogo.
Fundi alianza kizidisha ufundi maana alianza kukimbilia mambo ambayo hayajamleta pale.
Oyaa bro eeeh, hebu wewe wahi bwana mkeo atakuwa anakusubiri, aliongea Samson huku akifunga geti.akarudi chumbani kwake na kuanza kuandika barua ya maelezo ili pindi Mzee Mgaya akirudi amkabidhi
Itaendelea...........................