SEHEMU YA HAMSINI NA TATU
Kama kawaida kama ada, ikiwa ni mwendelezo wa kuisaka elimu kama njia ya kujitengenezea wepesi wa maisha ya baadaye au njia ya kujikomboa na maisha magumu,japokuwa hii si kanuni ya kuwa na maisha mazuri kwa Elimu siyo ndiyo Kila kitu, wapo wamefanikiwa kwenye maisha bila kupita darasani
Samson alikuwa smart akiwa kavaa begi lake kama ambapo jumatatu huwa ina vimbwanga vyake si kwa wafanyakazi tu, hata kwa wanafunzi.
Ni siku ambayo huweza kukupa picha ya mambo yatakavyoenda kwa wiki nzima japo si kwa wote wanaichukulia jumatatu kihivyo
Alifika shule muda sahihi huku siku hiyo akishangaa wanafunzi kuwa wachache tofauti na alivyozoea, hili halikumpa tabu akaingia darasani kwake huku akijiandaa na Somo la hesabu kama timetable, ilivyokuwa inaonesha akawa anafungua fungua kitabu fulani chenye Topic ya siku hiyo kwaajili ya kujikumbusha ,
Mwalimu wa somo husika aliingia, ambaye alikuwa ndiye mkuu wa shule ile,licha ya wanafunzi kusimama wamsalimie aliwaashiria wakae tu,
Huku akimuulizia monitor wa darasa.
Wewe ndiyo monitor, mbona mchafu hivyo halafu, nywele hizooooo! Hebu njoo mbele kwanza, haiwezekani monitor mzima unakuwa rafu na ni nani alikupa huu uongozi, eti class ni vigezo gani vilitumika kumpa umonitor huyu, aliongea yule mwalimu huku akimuinamisha ili amchape viboko.
Kuanzia leo huyu namvua hiki cheo, au hamjui maana ya uongozi,
Unapopewa uongozi maana yake wewe ni mfano kwa vitu vingi, kuanzia akili darasani, nidhamu, usafi na mengine mengi Sasa wewe hapana, Sasa nawataka mchague monitor wa darasa mwingine haraka vigezo awe na uwezo wa kuandika vizuri pamoja na kumudu baadhi ya masomo. lakini wanafunzi wote walikataa wakimtaka yule yule kwani wao walimwamini kwa uwezo wake mkubwa wakipewa test alikuwa di mchoyo anaweza kuwapa majibu darasa Zima na pia alijua alichokifanya kwani alikuwa na akili sana, jambo pekee lilimfanya aonekane mchafu ni kutokana na familia duni anayotoka, ikiwa haijiwezi, hivyo kuwa na maisha ya kuungaunga.
Baada ya wanafunzi kuonesha wote wanamtaka yule monitor wao waliyemzoea mwalimu alimpandisha na kumshusha huku akionesha hajamkubali .
Haya sawa kwakuwa wenyewe mnamkubali Mimi Sina neno ila nakuachieni test tu kwakuwa Leo Nina mambo mengi nipo kwenye msafara fulani wa mkuu wa mkoa na hata hivyo wiki hii Kuna mwalimu mpya wa somo la Mathematics atakuja kwakuwa Mimi nakuwa na ratiba nyingi mno.alisema yule mwalimu mkuu
Wanafunzi wote walihuzunika sana, waliamini hawawezi kupata mwalimu genius na mwenye kipaji cha kufundisha kama yule kwani hata wale vichwa ngumu kuelewa, ilikuwa rahisi kumuelewa yule mwalimu ambaye alikuwa ni mwalimu wa hesabu wa shule nzima.
Wakati anatoka, alikuja upande wa nyuma kule back benchers akakutana uso kwa uso na Samson,
Eheee wewe nilikuwa nakutafuta sana yaani pindi natoka ofisini mtu ambaye nilikuwa nataka nikuone ni wewe hebu nifuate ofisini, aliamrisha yule mwalimu mkuu
Samson moyo ulimlipuka akijaribu kuwaza kafanya kosa gani ila hakuelewa, maana walimu wale ilikuwa wakikuita lazima Kuna mistake umefanya.
Alifika ofisini akakuta kuna walimu wawili ambao walikuwa siyo wa shule yao ila aliwafahamu vyema,
Dah samahani ndugu zangu nimechelewa kiasi , majukumu nayo ni mengi kama nilivyomuomba Afisa Elimu na kamati yake waweze kutuongezea walimu wa masomo ya Sayansi pengine itanipunguzia majukumu. aliongea huku akijiweka kwenye kiti chake, Kisha akawapa wale walimu wenzake bahasha fulani na kuwaruhusu waondoke ,
Samahani kidogo naongea na huyu kijana ila ndani ya nusu saa nitakuwa nimefika kwani mheshimiwa atapita mida ya saa tano. aliwaambia wale walimu
Enhee Samson nimekuita hapa, nahitaji kuuliza jambo moja, naomba unijibu, kwa ufasaha na ukweli, kama Kuna kitu hukukiona kwa macho ila ulisikia usikitolee maelezo, nahitaji kile uliona na kusikia kwa macho yako, hebu niambie siku ya jumamosi kulitokea Nini kwenu Kati ya familia yenu Na mwalimu Sadick, aliuliza yule mwalimu mkuu.
Samson kwakuwa alishatahadharishwa asiseme jambo ambalo hakuliona, akili ilimcheza vizuri sana, akamjibu kuwa hakukutokea jambo lolote.
Nyumbani kwenu mnaishi watu wangapi? aliuliza mwalimu mkuu
Tunaishi watu wengi tu, ila kwasasa tunaishi watu wanne yaani , baba mkubwa Mzee Mgaya, Mama mkubwa, pamoja na dada wa kazi (akimaanisha Rahma)
kwahiyo huna unalolijua, mbona nimeambiwa mwalimu Sadick aliumizwa na mtu wa familia ya mzee Mgaya, japo yeye amenificha kaniambia kuwa anaumwa, lakini kwa taarifa na vyanzo visivyo rasmi sana, kwa shuhuda za majirani inaonesha mtu alitoka mbio huku akiugulia maumivu akiwa anatoka kwenye nyumba yenu bado Samson unataka kuniambia hujui kitu. aliongea mwalimu mkuu huku akijichekesha akilazimisha Samson aongee.
Mwalimu siku ya jumamosi tulisafiri mimi na wazazi wangu kwenda huku shamba kukagua miradi ya Mzee na tuliporudi tulikuta ni salama tu, Sasa hayo mengine Mimi sijayajua. alijibu Kwa kujifanya hajui ili kuepusha mlolongo wa maswali.
Haya wahi darasani, nitaongea na Mzee Mgaya mwenyewe, maana hili kinaleta picha mbaya kwa siye walimu, alisema mwalimu mkuu
Samson aliwaza kidogo huku wakati mwingine akicheka, ni nani aliyemuona mwalimu Sadick, akitoka ndani mwetu, na kwanini amdanganye mwalimu mkuu kuwa anaumwa wakati kaumizwa na Rahma? Watajijua wenyewe. alijisemea Samson huku akiendelea na masomo yake. Muda wa saa Saba mchana Samson aliambiwa anaitwa kwenye ofisi ya walimu wote, akaingia akakuta jopo la walimu karibu wote wakiwa na mwalimu mkuu wakiwa wanaongea kwa lawama kidogo.
Hii serikali basi tu, yaani watu hawazingatii itifaki kabisa yaani, haiwezekani safari inapangwa kwa muda wa wiki nzima halafu inaahirishwa kirahisi tu, Mimi hapa nimetumia gharama kibao nikiwa kama mratibu wa Elimu kwa kuchukua walimu kadhaa ambao tungekuwa kwenye msafara lakini , Cha ajabu safari hakuna , na hakuna sababu za msingi. Alilaumu mwalimu mkuu ambaye Samson aligundua kuwa pia ni mratibu wa Elimu cheo ambacho hakukijua kabla.
Sasa ndugu zanguni hayo tuyaache tu, Wala hatuna namna Hawa ndiyo viongozi wetu wa taifa hili, hata wakituambia muda huu Kuna safari tena, hatuna budi kutii mamlaka. alisema kwa masikitiko mwalimu mkuu.
Haya Mimi natoka kidogo naenda hapo kwa mzee Mgaya nina mazungumzo naye, aliwaaga wenzake huku akiongozana na Samson hadi nyumbani kwao. Wakimkuta Mzee Mgaya akishuka kwenye gari kuonesha Kuna sehemu anatoka muda si mrefu
Karibu sana Mzee mwenzangu, naona umekuja kunitembelea na wewe navyokujua huwa huji hapa kirahisi bila shaka , kuna matatizo, vipi kijana wetu anasumbua nini. aliuliza kiutani Mzee Mgaya.
Hapana, hakuna jambo baya kwa Samson yaani huyu tangu umenikabidhi mwaka ule, naishi naye vizuri sana shuleni kwangu, Tena kitaaluma yupo vizuri ana wastani mzuri, na pia ni bonge la football player, yaani hii ndiyo winga ya shuleni kwetu . aliongea mwalimu mkuu huku akimpigapiga Samson mgongoni.
Haya mwalimu karibu ndani, karibu sana, waliingia ndani wakakutana na watu wengi kidogo,
Akiwemo muuza nyama maarufu wa mtaa ule, mama Kulwa akiwa ndiye mazahausi, alikuwepo pia Tausi mke mdogo wa mzee Mgaya, alikuwepo pia Cathy msichana ambaye ni rafiki wa mama Kulwa, pamoja na Rahma.
Samson alishangaa uwepo wa watu wale, akagundua kuwa kumbe mwalimu mkuu hajakuja kwa bahati mbaya Bali, ameitwa.hivyo watu nane ndani ya familia ya mzee Mgaya wakaanza kwa kutambulishana ili kikao husika kiweze kuendelea.
Nini kinajadiliwa kwenye hicho kikao?
Ni nini kitajiri baada ya majadiliano?
Sehemu inayofuata ina majibu,
Itaendelea..........................