Simulizi: Milango ya mafanikio

Simulizi: Milango ya mafanikio

SEHEMU YA HAMSINI NA TISA

Samson aliandika maelezo anayoyajua kwenye lile karatasi huku moyo unamuuma baada ya kurudia kile alichokiandika,
Ina maana katika hizi points nilizoandika nikikosea kidogo tu, tayari, nitakuwa nimetoa kuanzia shule hadi hapa ninapoishi. alijisemea Samson huku akijua fika hakuna binadamu akaishi kama malaika yaani asikosee jambo, akaona ni uongo,
Aliweka karatasi pembeni mahali panapoonekana, ili iwe rahisi kuliona.

Aliendelea kupekua pekua vitabu na madaftari yake huku siku hiyo akiwa hajafuata ratiba ya masomo kama alivyokuwa amejiandalia.
Wakati akiwa kwenye ubize ule, alimsikia mama Kulwa akiwa anaongeaongea sebuleni, akatoka wakasalimiana huku akimsoma mama Kulwa usoni kuona kama bado Wana zile habari zao.

Shoga yangu vipi kuna chochote kimeandaliwa hapa, maana leo nimejikuta Sina hata muda wa kutafuta chakula, maana kazi nazo zinabana sana, aliongea mama Kulwa akimwambia Rahma kama Kuna chochote kimeandaliwa.

Halafu huyu baba yenu hajarudi tu usiku wote huu, huyu ananitaka nini mimi, nimejikuta naenda kazini kwangu kwa kuomba msaada usafiri wakati gari langu ninalo, Sasa mtu kitu umeazimwa halafu mpaka saa tatu hii mtu haonekani, huyu Kuna kitu ananitafuta.

Wakati Rahma akiwa anaandaa chakula pale mezani, ilisikika honi getini, Samson akataka kwenda kufungua lakini akazuiwa, akiwa anatoka mama Kulwa huku akiongea maneno ambayo hayakusikika vizuri ila yakiwa ni ya shari, Mzee Mgaya akaingia na gari akalipark kwenye sehemu yake, kisha akaingia ndani akiwa mnyonge kiasi pengine kutokana na maneno aliyoambiwa na mkewe,

Baba Jose naomba ujitahidi upate usafiri wako, vinginevyo tutakuja kuambizana maneno yasiyofaa tukaja kuonana wabaya, gari langu mwisho leo, nakwambia sitaki kwanza nipe hizo funguo, hakuna siku nimepata shida kama leo, ni afadhali asubuhi yule Binti Cathy alinipa msaada kwenye gari lake, lakini huu muda wa kurudi nimekuja na Taxi! nikajiuliza kwani shida yote ni nini? aliendelea kubwata mama Kulwa huku akiwa hajibiwi chochote na mzee Mgaya.

Samson aliingia chumbani kwake akachukua lile karatasi ikiwa ni sehemu ya kutimiza maagizo aliyopewa, akamkabidhi baba yake mkubwa,

Mzee Mgaya aliipokea akaishikilia tu akiwa na hasira kutokana na maneno aliyoambiwa na mkewe muda mfupi uliopita,

Sikia mwanangu Samson, hili karatasi sina haja ya kusoma, ila zingatia kuishi hapa kwa kufuata sheria na kanuni za nyumba hii, Mimi nadhani yale tuliyokwambia yanatosha kama ni mtu mwenye akili timamu basi utakuwa umeelewa, aliongea Mzee Mgaya kiupole sana kiasi cha Samson kushangaa nini kimetokea, ila alifurahi sana kuona maelezo yake hayajasomwa akachana ile karatasi vipande vipande Kisha akarudi sebuleni, ambapo hakumkuta Mzee Mgaya tena, akajumuika pale mezani na kuendelea kupata dinner.

Vipi fundi alikuja kurekebisha jiko , maana na wewe kwa kusahau hujambo, aliongea mama Kulwa akimkazia macho Rahma.

Amekuja mama tena nilimfuata mwenyewe, alijibu Samson.

Hapo safi usione naulizia hivyo ukaniona mama mbona anaongea sana hapana! Mimi nakusaidia wewe mwenyewe, maana jiko la mkaa linakutesa ohooooh, aliongea mama Kulwa huku Sam na Rahma wakiangaliana na kutikisa vichwa vyao wakimshangaa mama alivyo na gubu lakini hawakuwa na namna ni mtu ambaye ukithubutu kumbishia hata jambo dogo basi yeye huja juu.

Samson alifurahi sana siku hiyo kuona angalau mambo yamepungua, kwani alikuwa kwenye mstari mwekundu ambapo aliona muda wowote anaweza kufukuzwa.

Siku iliyofuata alifika shule akiwa mchangamfu sana, hata wanafunzi wenzake wakaona Sasa yule ndiye Sam waliyemzoea, aliendelea na masomo yake kwa siku hiyo huku akiwa hana wasiwasi wowote, lakini ilipofikia ule muda wa kutoka na kwenda majumbani aliletewa bahasha fulani akiambiwa inatoka kwa mwalimu mkuu kwamba ampelekee baba yake.

Kama kawaida alifika nyumbani hakumkuta Mzee Mgaya Wala mama kulwa, aliiendea meza ya Chakula akajitetea kama inavyotakiwa kwaajili ya kuendelea kufaidi zawadi ya uhai, akatoka nje na kumuona Rahma akiwa bize na mambo yake, hakutaka kumstua wala kuleta mazoea naye, badala yake alitoa maagizo kuwa anaenda kwenye group discussion hivyo Kuna barua fulani ambayo inamuhusu Mzee Mgaya hivyo akirudi ampatie.

Rahma aligeuka huku akichovya mikono kwenye beseni lenye vyombo na kunawa zile sabuni,

Sasa Samuuuu kwani Mimi nimekukosea nini, umeingia hapa hujanisalimia si kwamba hukuniona?
Uliniona sana, na saizi najua hukutaka hata kuniongelesha sema tu kwakuwa una maagizo yako ya barua.alilalamika Rahma.

Samson hakujibu chochote zaidi ya kutoka na kuubamiza mlango mdogo wa geti na kutokomea alikokusudia,
alirudi kama mida ya saa moja akimkuta Mzee Mgaya akiwa na watu wawili na yeye pale nje wakiwa wamebeba makablasha huku wakiwa kwenye suti zilizowapendeza , licha ya kuwasalimia hakuna aliyejibu zaidi ya mzee Mgaya mwenyewe.

Walionekana waongeaji sana huku wakiwa wanapekua pekua, makaratasi fulani, na kumpa mzee Mgaya , baadaye akawakaribisha wakaingia ndani huku wakionekana wanafahamiana na mama Kulwa pia.

Aisee shemeji yaani hata huzeeki upo vile vile, nashangaa kuona ulistaafu, ni umri kweli au mambo mengine tu, aliuliza jamaa mmoja aliyeonekana ni mtu wa masihara mengi.

Kwanza wewe nani sijui nani unaitwa, naomba usiniite shemeji, wewe kipindi kile umemleta mkeo hospital kuja kujifungua si ulikuwa bado mtoto mdogo tu wewe, nakumbuka nilikuuliza huyo mwanao anayekuja ni wangapi, ukanijibu ndiyo. Huku Ukiwa umevurugwa kila ukiniona unaniamkia Mara mbili mbili nikawa nakuhurumia tu, yaani ulikuwa mtoto sana, lakini tangu uajiriwe na hilo shirika mambo si mabaya, unaleta dharau eeeeh.

Alitania mama Kulwa huku wote mle ndani wakicheka, Samson akibaki kuangalia kwani hakumtambua hata mmoja, huku wakiendelea na mazungumzo yao.

Mke wangu, hawa wanatokea kwenye shirika la (akitaja jina)
Sasa lile shirika linauza baadhi ya vifaa, yakiwemo magari madogo ya kutembelea, Sasa kwakuwa Mimi Nina shida ya gari nikapeleleza bei zao nikaona nazimudu hivyo wanifanyie mpango na hapa Wana kadi za magari kama nne hivi ndiyo najaribu kuchagua, aliweka kituo mzee Mgaya.

Unajua Baba Jose, nisikufiche sisemi naharibu biashara ya watu, ila naomba watupe muda kujadili, kwanza fanya upelelezi kama hilo shirika linauza magari, taasisi kibao magari huwa yanaoza tu kiasi cha kufunikwa na majani ila huwezi sikia wakiuza, pili sijawahi kuona shirika linatuma watu nyumbani kwa mtu, eti kufanya biashara hizo,
Kwani hilo shirika halina ofisi ambapo mteja angeenda kukamilisha taratibu zake hapohapo? Mimi naona watupe muda. alishauri Mama Kulwa huku Mzee Mgaya akionesha anamuunga mkono mkewe.

Sasa Mr Mgaya, mbona Sasa unamsikiliza mkeo wakati tumeshamalizana bado hatua za mwisho utoe hela upewe gari lako huoni kama umetupotezea muda.
alihoji mmoja wa wale wageni huku akionesha kukasirika.

Huyu ni mke wangu ushauri wake ni mzuri na nimekubali, kwani hoja na maswali yake yana mashiko, hivyo nyie nendeni nitawatafuta, si mmesema kuna zaidi ya gari hamsini na Mimi nataka moja tu hivyo vumilieni Kila kitu kitakaa sawa. aliwajibu mzee Mgaya.

Wale wageni waliangaliana Kisha wakaaga na kuondoka.

Mzee Mgaya alichukuwa barua iliyotoka kwa mwalimu mkuu wa shule anayosoma Samson, na kuanza kuisoma huku akionesha akikunja uso Kila aliposoma mstari kwa mstari, Kisha akaikunja na kuitupia mezani.

Mke wangu huyu mwalimu mkuu naona kama ananitafuta, maana anaonesha kuniita , cha ajabu bila hata heshima ananiamrisha kwani Kuna nini? aliongea Kwa hasira mzee Mgaya.

Kwani anasemaje jamani, hii nyumba haiishi vituko Mara matapeli wanataka wakuuzie gari Mara mwalimu mkuu kwani anasemaje?
aliuliza mama Kulwa huku akivuta karatasi ili ajisomee mwenyewe.

Mmmmh unajua Nini mume wangu, huyu ni haya masuala ya Rahma na yule mwalimu , wewe huoni Kuna sehemu kaandika,

"Hamuwezi kubuni na kuwasingizia vitu watu kwa maslahi yenu"

Kwa maana hiyo huyu Rahma aliongopa siyo, aliuliza mama Kulwa.

Kumbe ananiitia habari hizo, hata hivyo naenda sasahivi usiku huu huu , yaani wanifanyie fujo nyumbani kwangu halafu aanze kunitishia, wewe Samson vaa viatu vyako nataka nikamsikilize huyo mpumbavu anasemaje.

Itaendelea.................................
 
SEHEMU YA HAMSINI NA TISA

Samson aliandika maelezo anayoyajua kwenye lile karatasi huku moyo unamuuma baada ya kurudia kile alichokiandika,
Ina maana katika hizi points nilizoandika nikikosea kidogo tu, tayari, nitakuwa nimetoa kuanzia shule hadi hapa ninapoishi. alijisemea Samson huku akijua fika hakuna binadamu akaishi kama malaika yaani asikosee jambo, akaona ni uongo,
Aliweka karatasi pembeni mahali panapoonekana, ili iwe rahisi kuliona.

Aliendelea kupekua pekua vitabu na madaftari yake huku siku hiyo akiwa hajafuata ratiba ya masomo kama alivyokuwa amejiandalia.
Wakati akiwa kwenye ubize ule, alimsikia mama Kulwa akiwa anaongeaongea sebuleni, akatoka wakasalimiana huku akimsoma mama Kulwa usoni kuona kama bado Wana zile habari zao.

Shoga yangu vipi kuna chochote kimeandaliwa hapa, maana leo nimejikuta Sina hata muda wa kutafuta chakula, maana kazi nazo zinabana sana, aliongea mama Kulwa akimwambia Rahma kama Kuna chochote kimeandaliwa.

Halafu huyu baba yenu hajarudi tu usiku wote huu, huyu ananitaka nini mimi, nimejikuta naenda kazini kwangu kwa kuomba msaada usafiri wakati gari langu ninalo, Sasa mtu kitu umeazimwa halafu mpaka saa tatu hii mtu haonekani, huyu Kuna kitu ananitafuta.

Wakati Rahma akiwa anaandaa chakula pale mezani, ilisikika honi getini, Samson akataka kwenda kufungua lakini akazuiwa, akiwa anatoka mama Kulwa huku akiongea maneno ambayo hayakusikika vizuri ila yakiwa ni ya shari, Mzee Mgaya akaingia na gari akalipark kwenye sehemu yake, kisha akaingia ndani akiwa mnyonge kiasi pengine kutokana na maneno aliyoambiwa na mkewe,

Baba Jose naomba ujitahidi upate usafiri wako, vinginevyo tutakuja kuambizana maneno yasiyofaa tukaja kuonana wabaya, gari langu mwisho leo, nakwambia sitaki kwanza nipe hizo funguo, hakuna siku nimepata shida kama leo, ni afadhali asubuhi yule Binti Cathy alinipa msaada kwenye gari lake, lakini huu muda wa kurudi nimekuja na Taxi! nikajiuliza kwani shida yote ni nini? aliendelea kubwata mama Kulwa huku akiwa hajibiwi chochote na mzee Mgaya.

Samson aliingia chumbani kwake akachukua lile karatasi ikiwa ni sehemu ya kutimiza maagizo aliyopewa, akamkabidhi baba yake mkubwa,

Mzee Mgaya aliipokea akaishikilia tu akiwa na hasira kutokana na maneno aliyoambiwa na mkewe muda mfupi uliopita,

Sikia mwanangu Samson, hili karatasi sina haja ya kusoma, ila zingatia kuishi hapa kwa kufuata sheria na kanuni za nyumba hii, Mimi nadhani yale tuliyokwambia yanatosha kama ni mtu mwenye akili timamu basi utakuwa umeelewa, aliongea Mzee Mgaya kiupole sana kiasi cha Samson kushangaa nini kimetokea, ila alifurahi sana kuona maelezo yake hayajasomwa akachana ile karatasi vipande vipande Kisha akarudi sebuleni, ambapo hakumkuta Mzee Mgaya tena, akajumuika pale mezani na kuendelea kupata dinner.

Vipi fundi alikuja kurekebisha jiko , maana na wewe kwa kusahau hujambo, aliongea mama Kulwa akimkazia macho Rahma.

Amekuja mama tena nilimfuata mwenyewe, alijibu Samson.

Hapo safi usione naulizia hivyo ukaniona mama mbona anaongea sana hapana! Mimi nakusaidia wewe mwenyewe, maana jiko la mkaa linakutesa ohooooh, aliongea mama Kulwa huku Sam na Rahma wakiangaliana na kutikisa vichwa vyao wakimshangaa mama alivyo na gubu lakini hawakuwa na namna ni mtu ambaye ukithubutu kumbishia hata jambo dogo basi yeye huja juu.

Samson alifurahi sana siku hiyo kuona angalau mambo yamepungua, kwani alikuwa kwenye mstari mwekundu ambapo aliona muda wowote anaweza kufukuzwa.

Siku iliyofuata alifika shule akiwa mchangamfu sana, hata wanafunzi wenzake wakaona Sasa yule ndiye Sam waliyemzoea, aliendelea na masomo yake kwa siku hiyo huku akiwa hana wasiwasi wowote, lakini ilipofikia ule muda wa kutoka na kwenda majumbani aliletewa bahasha fulani akiambiwa inatoka kwa mwalimu mkuu kwamba ampelekee baba yake.

Kama kawaida alifika nyumbani hakumkuta Mzee Mgaya Wala mama kulwa, aliiendea meza ya Chakula akajitetea kama inavyotakiwa kwaajili ya kuendelea kufaidi zawadi ya uhai, akatoka nje na kumuona Rahma akiwa bize na mambo yake, hakutaka kumstua wala kuleta mazoea naye, badala yake alitoa maagizo kuwa anaenda kwenye group discussion hivyo Kuna barua fulani ambayo inamuhusu Mzee Mgaya hivyo akirudi ampatie.

Rahma aligeuka huku akichovya mikono kwenye beseni lenye vyombo na kunawa zile sabuni,

Sasa Samuuuu kwani Mimi nimekukosea nini, umeingia hapa hujanisalimia si kwamba hukuniona?
Uliniona sana, na saizi najua hukutaka hata kuniongelesha sema tu kwakuwa una maagizo yako ya barua.alilalamika Rahma.

Samson hakujibu chochote zaidi ya kutoka na kuubamiza mlango mdogo wa geti na kutokomea alikokusudia,
alirudi kama mida ya saa moja akimkuta Mzee Mgaya akiwa na watu wawili na yeye pale nje wakiwa wamebeba makablasha huku wakiwa kwenye suti zilizowapendeza , licha ya kuwasalimia hakuna aliyejibu zaidi ya mzee Mgaya mwenyewe.

Walionekana waongeaji sana huku wakiwa wanapekua pekua, makaratasi fulani, na kumpa mzee Mgaya , baadaye akawakaribisha wakaingia ndani huku wakionekana wanafahamiana na mama Kulwa pia.

Aisee shemeji yaani hata huzeeki upo vile vile, nashangaa kuona ulistaafu, ni umri kweli au mambo mengine tu, aliuliza jamaa mmoja aliyeonekana ni mtu wa masihara mengi.

Kwanza wewe nani sijui nani unaitwa, naomba usiniite shemeji, wewe kipindi kile umemleta mkeo hospital kuja kujifungua si ulikuwa bado mtoto mdogo tu wewe, nakumbuka nilikuuliza huyo mwanao anayekuja ni wangapi, ukanijibu ndiyo. Huku Ukiwa umevurugwa kila ukiniona unaniamkia Mara mbili mbili nikawa nakuhurumia tu, yaani ulikuwa mtoto sana, lakini tangu uajiriwe na hilo shirika mambo si mabaya, unaleta dharau eeeeh.

Alitania mama Kulwa huku wote mle ndani wakicheka, Samson akibaki kuangalia kwani hakumtambua hata mmoja, huku wakiendelea na mazungumzo yao.

Mke wangu, hawa wanatokea kwenye shirika la (akitaja jina)
Sasa lile shirika linauza baadhi ya vifaa, yakiwemo magari madogo ya kutembelea, Sasa kwakuwa Mimi Nina shida ya gari nikapeleleza bei zao nikaona nazimudu hivyo wanifanyie mpango na hapa Wana kadi za magari kama nne hivi ndiyo najaribu kuchagua, aliweka kituo mzee Mgaya.

Unajua Baba Jose, nisikufiche sisemi naharibu biashara ya watu, ila naomba watupe muda kujadili, kwanza fanya upelelezi kama hilo shirika linauza magari, taasisi kibao magari huwa yanaoza tu kiasi cha kufunikwa na majani ila huwezi sikia wakiuza, pili sijawahi kuona shirika linatuma watu nyumbani kwa mtu, eti kufanya biashara hizo,
Kwani hilo shirika halina ofisi ambapo mteja angeenda kukamilisha taratibu zake hapohapo? Mimi naona watupe muda. alishauri Mama Kulwa huku Mzee Mgaya akionesha anamuunga mkono mkewe.

Sasa Mr Mgaya, mbona Sasa unamsikiliza mkeo wakati tumeshamalizana bado hatua za mwisho utoe hela upewe gari lako huoni kama umetupotezea muda.
alihoji mmoja wa wale wageni huku akionesha kukasirika.

Huyu ni mke wangu ushauri wake ni mzuri na nimekubali, kwani hoja na maswali yake yana mashiko, hivyo nyie nendeni nitawatafuta, si mmesema kuna zaidi ya gari hamsini na Mimi nataka moja tu hivyo vumilieni Kila kitu kitakaa sawa. aliwajibu mzee Mgaya.

Wale wageni waliangaliana Kisha wakaaga na kuondoka.

Mzee Mgaya alichukuwa barua iliyotoka kwa mwalimu mkuu wa shule anayosoma Samson, na kuanza kuisoma huku akionesha akikunja uso Kila aliposoma mstari kwa mstari, Kisha akaikunja na kuitupia mezani.

Mke wangu huyu mwalimu mkuu naona kama ananitafuta, maana anaonesha kuniita , cha ajabu bila hata heshima ananiamrisha kwani Kuna nini? aliongea Kwa hasira mzee Mgaya.

Kwani anasemaje jamani, hii nyumba haiishi vituko Mara matapeli wanataka wakuuzie gari Mara mwalimu mkuu kwani anasemaje?
aliuliza mama Kulwa huku akivuta karatasi ili ajisomee mwenyewe.

Mmmmh unajua Nini mume wangu, huyu ni haya masuala ya Rahma na yule mwalimu , wewe huoni Kuna sehemu kaandika,

"Hamuwezi kubuni na kuwasingizia vitu watu kwa maslahi yenu"

Kwa maana hiyo huyu Rahma aliongopa siyo, aliuliza mama Kulwa.

Kumbe ananiitia habari hizo, hata hivyo naenda sasahivi usiku huu huu , yaani wanifanyie fujo nyumbani kwangu halafu aanze kunitishia, wewe Samson vaa viatu vyako nataka nikamsikilize huyo mpumbavu anasemaje.

Itaendelea.................................

mimi sio mtabiri ila jioni kutakua na episode
 
Huyu Mzee Mgaya inaonekana ana itikadi za Kizamani sana aisee 😂😂😂😂
 
SEHEMU YA SITINI

Mzee Mgaya na Samson walitoka huku Samson akiwa hajapenda kwenda sehemu kwa usiku ule ila angefanyaje, wanaomlisha ndiyo washasema, na hata hivyo bado alikuwa na jambo bichi hivyo ilibidi akubali kishingo upande.

Walianza kukatiza chochoro na kuivuka barabara na kuishika njia ya nyumbani kwa mwalimu mkuu, waligonga geti wakafunguliwa, na kukutana uso kwa uso na yule mwalimu mkuu,

Aiseee karibuni, karibu sana Mzee Mgaya, naona umeamua kuja kunitembelea, na una bahati nilikuwa nataka nitoke kina pub yangu Iko hapo nyuma huwa napenda kwenda kupoteza muda hapo.aliweka kituo yule mwalimu huku akionesha anamshangaa mzee Mgaya.

Siyo nimekuja kukutembelea Mzee mwenzangu, ila kuna ujumbe nimepata jioni hii nikaona nije nikusikilize maana sijaelewa vizuri.
aliongea mzee Mgaya huku akionesha Shari waziwazi.

Yule mwalimu akawakaribisha kwenye chumba fulani ambacho kilikuwa kizuri sana likiwa na viti karibu sita,
Karibuni huku hii ndiyo ofisi yangu nikiwa hapa nyumbani. aliongea yule mwalimu mkuu huku muda wote akishindwa kujizuia kumwangalia Mzee Mgaya.

Unajua Mzee Mgaya kwanza nimekuheshimu tu kukukaribisha hapa kwangu, kwasababu kwenye ile barua Kila kitu kipo wazi nilikwambia tukutane kesho, na siyo leo!
Ila siyo mbaya nilichokuitia ni kwamba,nimejaribu kuzungumza na mwalimu wangu ambaye nyinyi mnamtuhumu kuwa alileta fujo sijui alitaka kumfanyia vitendo vibaya Binti yako, lakini mwalimu Sadick amekataa na kwa mujibu wa maelezo aliyonipa nimemwelewa sana hivyo ukajaribu kuongea na Binti yako vizuri, huenda amezua haya mambo, au labda alimfananisha na wapo mashahidi kadhaa ambao kama ungekuja kesho kule shule basi ungejua jambo.

Na nikuombe kitu kimoja Mzee mwenzangu wewe tumesaidiana mambo mengi sana, mwisho ni siku ulipomleta huyu kijana, unajua fika taratibu za uhamisho hazikukamilika, lakini kwakuwa tumetoka mbali Mimi nilikusaidia sana hata kufikia kijana wenu anaendelea na masomo hadi Leo hii, Sasa wewe mbona unakuwa huna ubinadamu? aliweka kituo, mwalimu mkuu huku akionesha hajapenda kitendo cha Mzee Mgaya kwenda wake wakati barua ilimtaka wakutane shuleni.

Sawa Mimi nitafanya uchunguzi zaidi, kama yule Binti alitudanganya, itajulikana tu, alisema Mzee Mgaya huku akiinuka na kuondoka.

Wakiwa njiani Samson alimuuliza baba yake mkubwa maswali kadhaa...

Kwani baba hili suala la Rahma bado unalo tu? na kama bado lipo unaamua nini? Je, unataka kushtaki? Mimi nadhani tungeongeza ulinzi ikiwemo kumwambia Da Rahma kuwa asiwe anaruhusu au kumfungulia mtu mgeni. aliongea Samson kwa kujikaza huku akiwa anasubiri itakuwaje.

Wewe hujui kitu nyamaza, mambo yako yasiyo ya kinidhamu uliyoyafanya, ni sawa na aliyoyafanya huyu mwalimu wenu, na usione tumekukalia kimya Samson umetuudhi familia nzima, Tena hupaswi hata kuniuliza haya mambo wewe Kaa kimya sawa. alichimba mkwara Mzee Mgaya.

Walifika nyumbani kwao huku wenzao wakiwa washagawana vyumba na kuondoka, Samson aliingia bafuni akajiswafi na kuja kitandani kwake huku akijikuta ni kama mtumwa mle ndani,
Hivi huyu mzee hata wanae anaweza kuwazurulisha usiku namna hii, Ina maana hajui kuwa Mimi napaswa kupata muda wa ziada wa kujisomea? hakuwa na cha kufanya kwani alishazidiwa, asubuhi yake ilikuwa ni weekend kama kawaida alijihimu na kufanya kazi sawa na Rahma yote ikiwa ni kujitengenezea mazingira mazuri ili azidi kuaminika.

Wanangu leo tunaenda mjini naenda kucheki maendeleo ya biashara zangu, hivyo Kila mtu ajiandae, aliongea mama Kulwa kisha Mzee Mgaya akadakia.

Sasa watu wote muende mjini mkafanye nini, huyu Samson abaki alinde nyumba , sioni sababu ya kwenda huko. aliongea Kwa sauti ya kuamrisha Mzee Mgaya kitendo ambacho kilimuuma sana Samson ila hakuwa na jinsi.

Mama Kulwa , Mzee Mgaya mwenyewe pamoja na Rahma, waliingia kwenye gari na kutoka huku Mzee Mgaya akiwa hafiki mjini ila anaenda sehemu kwaajili ya kukutana na madalali wa magari, licha ya kushauriwa kuwa ni vyema angenunua gari jipya kwani uwezo alikuwa nao lakini yeye alipenda sana vitu vya bei rahisi.

Samson alirudi ndani huku asubuhi ile akishindwa cha kufanya, lakini akakubali hakuwa na jinsi, akaingia ndani na kuchukua kitabu fulani cha kiingereza na kukaa nje huku akijisomea.

Geti liligongwa Sam akainua macho na kutega masikio kama alichosikia ni kweli, geti likagongwa kwa nguvu akainuka na kwenda kufungua taratibu na kutizama ni nani,
Macho yaligongana na Cathy mwanamke fulani rika la mtoto wa kike wa mama Kulwa, ilikuwa ngumu, kusema Cathy na mama Kulwa ni marafiki lakini ndivyo ilivyokuwa,

Cathy alikuwa mtoto wa mjini sana , alijua vitu vingi vikubwa, huku akiwa na bwana nje ya nchi ndiye aliyekuwa akimpa kiburi cha kuishi mjini, Cathy hakuwa na kazi mjini ilikuwa ni kawaida kumkuta viwanja vya bata lakini akiwa anawezeshwa na bwana wake.

Mama yangu yuko wapi, aliuliza Cathy.

Katoka, kaenda mjini, kwani wewe hamjawasiliana naye? aliuliza Samson.

Hapana, mbona unaniuliza hivyo kwani kuja hapa Mimi hadi niwasiliane naye, maswali hayo muulize mtu mgeni Mimi hapa ni kama kwangu Mimi nimesoma chuo na Dr Glory mtoto wa huyu mama, nilikuwa nalala hapa hapa ,wewe kipindi hicho si ulikuwa shamba huko vijijini kwenu, kifupi hapa ni kama kwetu tu, aliongea Cathy kama anatania lakini ulikuwa ndiyo ukweli wenyewe.

Sawa , Mimi sikatai nilikuwa shamba na kule ni kijijini kwetu nilikozaliwa na hata ulivyonikumbusha tayari nimemiss mazingira ya nyumbani sana tu. alijibu Samson huku akicheka.

Kweli we mshamba yaani unafika maeneo ya mjini halafu unakumbuka habari za kijijini! alicheka sana Cathy huku akifunga mlango wa gari vizuri ili amsikilize Samson kwani stori zilikuwa zinanoga.
Kwa kifupi Cathy hajawahi kumkubali Samson, hata kipindi Sam akikwaruzana na Mama Kulwa, Cathy alikuwa mstari wa mbele akishadadia Samson afukuzwe.

Lakini pia Samson naye hakumpenda Cathy, alimuona kama kijipu uchungu mwilini mwake hasa kwa mdomo aliokuwa nao, lakini siku hiyo wakajikuta wanapiga stori.

Hivi wewe Samson kwahiyo unajisikiaje kukaa peke yako hivi, huoni kama wanakutenga? aliuliza swali la kimtego Cathy.

Wananitenga kivipi, yaani watu wameniamini na kuniachia nyumba na vyote vilivyomo halafu unasema watu wananitenga? wangekuwa wananituma kazi za nje wasinipe uhuru wa kukaa hapa ningekubaliana na wewe. alijibu Kwa kujiamini Samson.

Yaani Samuuuu umekuwa mjeuri, wewe si ulikuja na Sweta chafu mjini, Hadi nikija mama Kulwa ananikonyeza nikwangalie Sasa hivi umenenepa hapa kwa mzee Mgaya na unajua kuongea na wewe siyo?
Sema umekuwa bonge la baba saizi eeh.alitania Cathy.

Kwani hivi wewe dada unafanya kazi gani? aliuliza Samson

(Huku akicheka)
Heeee baba, unataka kunipa kazi mwenzangu? badala ya kujibu swali naye aliuliza huku akitoa macho yake makubwa na mazuri.

Hapana nataka siku unifundishe kuendesha gari, unajua shuleni kwetu vijana wengi wanaendesha magari, lakini Mimi sijui kabisa dada yangu .
safari hii aliongea kwa heshima Samson.

Wenzio ni born town mambo ya magari ni kitambo, usipende kuiga iga utakuja kuumia bure, haya kwa mfano nimekufundisha umejua utapata faida ikiwa huna gari lako? aliuliza kwa dharau Cathy.

Dada Cathy unapenda sana kwenda kanisani, ningekusaidia siku moja moja kuendesha au unasemaje. aliuliza Samson

Tausi hakujibu neno, zaidi ya kumwangalia Samson Kisha akatabasamu na kugonganisha viganja kwa mshangao kwani hakutarajia Samson aseme vile.

Sawa mwaya kesho naenda kanisani, nikirudi, nitakufundisha gari sawa aliongea huku akiingia zake ndani ya gari, huku Samson akimpungia mkono na Cathy akiwasha indicator kwa ishara ya kumkubalia.

Cathy Kuna namna kavutiwa na Samson, huku Samson naye akiwa hayuko nyuma, na ni mwepesi sana kusahau Nini kitatokea? Sehemu ijayo ina majibu.

Itaendelea.........................
 
SEHEMU YA SITINI

Mzee Mgaya na Samson walitoka huku Samson akiwa hajapenda kwenda sehemu kwa usiku ule ila angefanyaje, wanaomlisha ndiyo washasema, na hata hivyo bado alikuwa na jambo bichi hivyo ilibidi akubali kishingo upande.

Walianza kukatiza chochoro na kuivuka barabara na kuishika njia ya nyumbani kwa mwalimu mkuu, waligonga geti wakafunguliwa, na kukutana uso kwa uso na yule mwalimu mkuu,

Aiseee karibuni, karibu sana Mzee Mgaya, naona umeamua kuja kunitembelea, na una bahati nilikuwa nataka nitoke kina pub yangu Iko hapo nyuma huwa napenda kwenda kupoteza muda hapo.aliweka kituo yule mwalimu huku akionesha anamshangaa mzee Mgaya.

Siyo nimekuja kukutembelea Mzee mwenzangu, ila kuna ujumbe nimepata jioni hii nikaona nije nikusikilize maana sijaelewa vizuri.
aliongea mzee Mgaya huku akionesha Shari waziwazi.

Yule mwalimu akawakaribisha kwenye chumba fulani ambacho kilikuwa kizuri sana likiwa na viti karibu sita,
Karibuni huku hii ndiyo ofisi yangu nikiwa hapa nyumbani. aliongea yule mwalimu mkuu huku muda wote akishindwa kujizuia kumwangalia Mzee Mgaya.

Unajua Mzee Mgaya kwanza nimekuheshimu tu kukukaribisha hapa kwangu, kwasababu kwenye ile barua Kila kitu kipo wazi nilikwambia tukutane kesho, na siyo leo!
Ila siyo mbaya nilichokuitia ni kwamba,nimejaribu kuzungumza na mwalimu wangu ambaye nyinyi mnamtuhumu kuwa alileta fujo sijui alitaka kumfanyia vitendo vibaya Binti yako, lakini mwalimu Sadick amekataa na kwa mujibu wa maelezo aliyonipa nimemwelewa sana hivyo ukajaribu kuongea na Binti yako vizuri, huenda amezua haya mambo, au labda alimfananisha na wapo mashahidi kadhaa ambao kama ungekuja kesho kule shule basi ungejua jambo.

Na nikuombe kitu kimoja Mzee mwenzangu wewe tumesaidiana mambo mengi sana, mwisho ni siku ulipomleta huyu kijana, unajua fika taratibu za uhamisho hazikukamilika, lakini kwakuwa tumetoka mbali Mimi nilikusaidia sana hata kufikia kijana wenu anaendelea na masomo hadi Leo hii, Sasa wewe mbona unakuwa huna ubinadamu? aliweka kituo, mwalimu mkuu huku akionesha hajapenda kitendo cha Mzee Mgaya kwenda wake wakati barua ilimtaka wakutane shuleni.

Sawa Mimi nitafanya uchunguzi zaidi, kama yule Binti alitudanganya, itajulikana tu, alisema Mzee Mgaya huku akiinuka na kuondoka.

Wakiwa njiani Samson alimuuliza baba yake mkubwa maswali kadhaa...

Kwani baba hili suala la Rahma bado unalo tu? na kama bado lipo unaamua nini? Je, unataka kushtaki? Mimi nadhani tungeongeza ulinzi ikiwemo kumwambia Da Rahma kuwa asiwe anaruhusu au kumfungulia mtu mgeni. aliongea Samson kwa kujikaza huku akiwa anasubiri itakuwaje.

Wewe hujui kitu nyamaza, mambo yako yasiyo ya kinidhamu uliyoyafanya, ni sawa na aliyoyafanya huyu mwalimu wenu, na usione tumekukalia kimya Samson umetuudhi familia nzima, Tena hupaswi hata kuniuliza haya mambo wewe Kaa kimya sawa. alichimba mkwara Mzee Mgaya.

Walifika nyumbani kwao huku wenzao wakiwa washagawana vyumba na kuondoka, Samson aliingia bafuni akajiswafi na kuja kitandani kwake huku akijikuta ni kama mtumwa mle ndani,
Hivi huyu mzee hata wanae anaweza kuwazurulisha usiku namna hii, Ina maana hajui kuwa Mimi napaswa kupata muda wa ziada wa kujisomea? hakuwa na cha kufanya kwani alishazidiwa, asubuhi yake ilikuwa ni weekend kama kawaida alijihimu na kufanya kazi sawa na Rahma yote ikiwa ni kujitengenezea mazingira mazuri ili azidi kuaminika.

Wanangu leo tunaenda mjini naenda kucheki maendeleo ya biashara zangu, hivyo Kila mtu ajiandae, aliongea mama Kulwa kisha Mzee Mgaya akadakia.

Sasa watu wote muende mjini mkafanye nini, huyu Samson abaki alinde nyumba , sioni sababu ya kwenda huko. aliongea Kwa sauti ya kuamrisha Mzee Mgaya kitendo ambacho kilimuuma sana Samson ila hakuwa na jinsi.

Mama Kulwa , Mzee Mgaya mwenyewe pamoja na Rahma, waliingia kwenye gari na kutoka huku Mzee Mgaya akiwa hafiki mjini ila anaenda sehemu kwaajili ya kukutana na madalali wa magari, licha ya kushauriwa kuwa ni vyema angenunua gari jipya kwani uwezo alikuwa nao lakini yeye alipenda sana vitu vya bei rahisi.

Samson alirudi ndani huku asubuhi ile akishindwa cha kufanya, lakini akakubali hakuwa na jinsi, akaingia ndani na kuchukua kitabu fulani cha kiingereza na kukaa nje huku akijisomea.

Geti liligongwa Sam akainua macho na kutega masikio kama alichosikia ni kweli, geti likagongwa kwa nguvu akainuka na kwenda kufungua taratibu na kutizama ni nani,
Macho yaligongana na Cathy mwanamke fulani rika la mtoto wa kike wa mama Kulwa, ilikuwa ngumu, kusema Cathy na mama Kulwa ni marafiki lakini ndivyo ilivyokuwa,

Cathy alikuwa mtoto wa mjini sana , alijua vitu vingi vikubwa, huku akiwa na bwana nje ya nchi ndiye aliyekuwa akimpa kiburi cha kuishi mjini, Cathy hakuwa na kazi mjini ilikuwa ni kawaida kumkuta viwanja vya bata lakini akiwa anawezeshwa na bwana wake.

Mama yangu yuko wapi, aliuliza Cathy.

Katoka, kaenda mjini, kwani wewe hamjawasiliana naye? aliuliza Samson.

Hapana, mbona unaniuliza hivyo kwani kuja hapa Mimi hadi niwasiliane naye, maswali hayo muulize mtu mgeni Mimi hapa ni kama kwangu Mimi nimesoma chuo na Dr Glory mtoto wa huyu mama, nilikuwa nalala hapa hapa ,wewe kipindi hicho si ulikuwa shamba huko vijijini kwenu, kifupi hapa ni kama kwetu tu, aliongea Cathy kama anatania lakini ulikuwa ndiyo ukweli wenyewe.

Sawa , Mimi sikatai nilikuwa shamba na kule ni kijijini kwetu nilikozaliwa na hata ulivyonikumbusha tayari nimemiss mazingira ya nyumbani sana tu. alijibu Samson huku akicheka.

Kweli we mshamba yaani unafika maeneo ya mjini halafu unakumbuka habari za kijijini! alicheka sana Cathy huku akifunga mlango wa gari vizuri ili amsikilize Samson kwani stori zilikuwa zinanoga.
Kwa kifupi Cathy hajawahi kumkubali Samson, hata kipindi Sam akikwaruzana na Mama Kulwa, Cathy alikuwa mstari wa mbele akishadadia Samson afukuzwe.

Lakini pia Samson naye hakumpenda Cathy, alimuona kama kijipu uchungu mwilini mwake hasa kwa mdomo aliokuwa nao, lakini siku hiyo wakajikuta wanapiga stori.

Hivi wewe Samson kwahiyo unajisikiaje kukaa peke yako hivi, huoni kama wanakutenga? aliuliza swali la kimtego Cathy.

Wananitenga kivipi, yaani watu wameniamini na kuniachia nyumba na vyote vilivyomo halafu unasema watu wananitenga? wangekuwa wananituma kazi za nje wasinipe uhuru wa kukaa hapa ningekubaliana na wewe. alijibu Kwa kujiamini Samson.

Yaani Samuuuu umekuwa mjeuri, wewe si ulikuja na Sweta chafu mjini, Hadi nikija mama Kulwa ananikonyeza nikwangalie Sasa hivi umenenepa hapa kwa mzee Mgaya na unajua kuongea na wewe siyo?
Sema umekuwa bonge la baba saizi eeh.alitania Cathy.

Kwani hivi wewe dada unafanya kazi gani? aliuliza Samson

(Huku akicheka)
Heeee baba, unataka kunipa kazi mwenzangu? badala ya kujibu swali naye aliuliza huku akitoa macho yake makubwa na mazuri.

Hapana nataka siku unifundishe kuendesha gari, unajua shuleni kwetu vijana wengi wanaendesha magari, lakini Mimi sijui kabisa dada yangu .
safari hii aliongea kwa heshima Samson.

Wenzio ni born town mambo ya magari ni kitambo, usipende kuiga iga utakuja kuumia bure, haya kwa mfano nimekufundisha umejua utapata faida ikiwa huna gari lako? aliuliza kwa dharau Cathy.

Dada Cathy unapenda sana kwenda kanisani, ningekusaidia siku moja moja kuendesha au unasemaje. aliuliza Samson

Tausi hakujibu neno, zaidi ya kumwangalia Samson Kisha akatabasamu na kugonganisha viganja kwa mshangao kwani hakutarajia Samson aseme vile.

Sawa mwaya kesho naenda kanisani, nikirudi, nitakufundisha gari sawa aliongea huku akiingia zake ndani ya gari, huku Samson akimpungia mkono na Cathy akiwasha indicator kwa ishara ya kumkubalia.

Cathy Kuna namna kavutiwa na Samson, huku Samson naye akiwa hayuko nyuma, na ni mwepesi sana kusahau Nini kitatokea? Sehemu ijayo ina majibu.

Itaendelea.........................
Sam alkua handsome boy knoma eti
 

Cathy Kuna namna kavutiwa na Samson, huku Samson naye akiwa hayuko nyuma, na ni mwepesi sana kusahau Nini kitatokea? Sehemu ijayo ina majibu.

Itaendelea.........................
Samson Samson Samson Kijana huyu Machachari sana 🤣🤣🤣🤣
 
SEHEMU YA SITINI

Mzee Mgaya na Samson walitoka huku Samson akiwa hajapenda kwenda sehemu kwa usiku ule ila angefanyaje, wanaomlisha ndiyo washasema, na hata hivyo bado alikuwa na jambo bichi hivyo ilibidi akubali kishingo upande.

Walianza kukatiza chochoro na kuivuka barabara na kuishika njia ya nyumbani kwa mwalimu mkuu, waligonga geti wakafunguliwa, na kukutana uso kwa uso na yule mwalimu mkuu,

Aiseee karibuni, karibu sana Mzee Mgaya, naona umeamua kuja kunitembelea, na una bahati nilikuwa nataka nitoke kina pub yangu Iko hapo nyuma huwa napenda kwenda kupoteza muda hapo.aliweka kituo yule mwalimu huku akionesha anamshangaa mzee Mgaya.

Siyo nimekuja kukutembelea Mzee mwenzangu, ila kuna ujumbe nimepata jioni hii nikaona nije nikusikilize maana sijaelewa vizuri.
aliongea mzee Mgaya huku akionesha Shari waziwazi.

Yule mwalimu akawakaribisha kwenye chumba fulani ambacho kilikuwa kizuri sana likiwa na viti karibu sita,
Karibuni huku hii ndiyo ofisi yangu nikiwa hapa nyumbani. aliongea yule mwalimu mkuu huku muda wote akishindwa kujizuia kumwangalia Mzee Mgaya.

Unajua Mzee Mgaya kwanza nimekuheshimu tu kukukaribisha hapa kwangu, kwasababu kwenye ile barua Kila kitu kipo wazi nilikwambia tukutane kesho, na siyo leo!
Ila siyo mbaya nilichokuitia ni kwamba,nimejaribu kuzungumza na mwalimu wangu ambaye nyinyi mnamtuhumu kuwa alileta fujo sijui alitaka kumfanyia vitendo vibaya Binti yako, lakini mwalimu Sadick amekataa na kwa mujibu wa maelezo aliyonipa nimemwelewa sana hivyo ukajaribu kuongea na Binti yako vizuri, huenda amezua haya mambo, au labda alimfananisha na wapo mashahidi kadhaa ambao kama ungekuja kesho kule shule basi ungejua jambo.

Na nikuombe kitu kimoja Mzee mwenzangu wewe tumesaidiana mambo mengi sana, mwisho ni siku ulipomleta huyu kijana, unajua fika taratibu za uhamisho hazikukamilika, lakini kwakuwa tumetoka mbali Mimi nilikusaidia sana hata kufikia kijana wenu anaendelea na masomo hadi Leo hii, Sasa wewe mbona unakuwa huna ubinadamu? aliweka kituo, mwalimu mkuu huku akionesha hajapenda kitendo cha Mzee Mgaya kwenda wake wakati barua ilimtaka wakutane shuleni.

Sawa Mimi nitafanya uchunguzi zaidi, kama yule Binti alitudanganya, itajulikana tu, alisema Mzee Mgaya huku akiinuka na kuondoka.

Wakiwa njiani Samson alimuuliza baba yake mkubwa maswali kadhaa...

Kwani baba hili suala la Rahma bado unalo tu? na kama bado lipo unaamua nini? Je, unataka kushtaki? Mimi nadhani tungeongeza ulinzi ikiwemo kumwambia Da Rahma kuwa asiwe anaruhusu au kumfungulia mtu mgeni. aliongea Samson kwa kujikaza huku akiwa anasubiri itakuwaje.

Wewe hujui kitu nyamaza, mambo yako yasiyo ya kinidhamu uliyoyafanya, ni sawa na aliyoyafanya huyu mwalimu wenu, na usione tumekukalia kimya Samson umetuudhi familia nzima, Tena hupaswi hata kuniuliza haya mambo wewe Kaa kimya sawa. alichimba mkwara Mzee Mgaya.

Walifika nyumbani kwao huku wenzao wakiwa washagawana vyumba na kuondoka, Samson aliingia bafuni akajiswafi na kuja kitandani kwake huku akijikuta ni kama mtumwa mle ndani,
Hivi huyu mzee hata wanae anaweza kuwazurulisha usiku namna hii, Ina maana hajui kuwa Mimi napaswa kupata muda wa ziada wa kujisomea? hakuwa na cha kufanya kwani alishazidiwa, asubuhi yake ilikuwa ni weekend kama kawaida alijihimu na kufanya kazi sawa na Rahma yote ikiwa ni kujitengenezea mazingira mazuri ili azidi kuaminika.

Wanangu leo tunaenda mjini naenda kucheki maendeleo ya biashara zangu, hivyo Kila mtu ajiandae, aliongea mama Kulwa kisha Mzee Mgaya akadakia.

Sasa watu wote muende mjini mkafanye nini, huyu Samson abaki alinde nyumba , sioni sababu ya kwenda huko. aliongea Kwa sauti ya kuamrisha Mzee Mgaya kitendo ambacho kilimuuma sana Samson ila hakuwa na jinsi.

Mama Kulwa , Mzee Mgaya mwenyewe pamoja na Rahma, waliingia kwenye gari na kutoka huku Mzee Mgaya akiwa hafiki mjini ila anaenda sehemu kwaajili ya kukutana na madalali wa magari, licha ya kushauriwa kuwa ni vyema angenunua gari jipya kwani uwezo alikuwa nao lakini yeye alipenda sana vitu vya bei rahisi.

Samson alirudi ndani huku asubuhi ile akishindwa cha kufanya, lakini akakubali hakuwa na jinsi, akaingia ndani na kuchukua kitabu fulani cha kiingereza na kukaa nje huku akijisomea.

Geti liligongwa Sam akainua macho na kutega masikio kama alichosikia ni kweli, geti likagongwa kwa nguvu akainuka na kwenda kufungua taratibu na kutizama ni nani,
Macho yaligongana na Cathy mwanamke fulani rika la mtoto wa kike wa mama Kulwa, ilikuwa ngumu, kusema Cathy na mama Kulwa ni marafiki lakini ndivyo ilivyokuwa,

Cathy alikuwa mtoto wa mjini sana , alijua vitu vingi vikubwa, huku akiwa na bwana nje ya nchi ndiye aliyekuwa akimpa kiburi cha kuishi mjini, Cathy hakuwa na kazi mjini ilikuwa ni kawaida kumkuta viwanja vya bata lakini akiwa anawezeshwa na bwana wake.

Mama yangu yuko wapi, aliuliza Cathy.

Katoka, kaenda mjini, kwani wewe hamjawasiliana naye? aliuliza Samson.

Hapana, mbona unaniuliza hivyo kwani kuja hapa Mimi hadi niwasiliane naye, maswali hayo muulize mtu mgeni Mimi hapa ni kama kwangu Mimi nimesoma chuo na Dr Glory mtoto wa huyu mama, nilikuwa nalala hapa hapa ,wewe kipindi hicho si ulikuwa shamba huko vijijini kwenu, kifupi hapa ni kama kwetu tu, aliongea Cathy kama anatania lakini ulikuwa ndiyo ukweli wenyewe.

Sawa , Mimi sikatai nilikuwa shamba na kule ni kijijini kwetu nilikozaliwa na hata ulivyonikumbusha tayari nimemiss mazingira ya nyumbani sana tu. alijibu Samson huku akicheka.

Kweli we mshamba yaani unafika maeneo ya mjini halafu unakumbuka habari za kijijini! alicheka sana Cathy huku akifunga mlango wa gari vizuri ili amsikilize Samson kwani stori zilikuwa zinanoga.
Kwa kifupi Cathy hajawahi kumkubali Samson, hata kipindi Sam akikwaruzana na Mama Kulwa, Cathy alikuwa mstari wa mbele akishadadia Samson afukuzwe.

Lakini pia Samson naye hakumpenda Cathy, alimuona kama kijipu uchungu mwilini mwake hasa kwa mdomo aliokuwa nao, lakini siku hiyo wakajikuta wanapiga stori.

Hivi wewe Samson kwahiyo unajisikiaje kukaa peke yako hivi, huoni kama wanakutenga? aliuliza swali la kimtego Cathy.

Wananitenga kivipi, yaani watu wameniamini na kuniachia nyumba na vyote vilivyomo halafu unasema watu wananitenga? wangekuwa wananituma kazi za nje wasinipe uhuru wa kukaa hapa ningekubaliana na wewe. alijibu Kwa kujiamini Samson.

Yaani Samuuuu umekuwa mjeuri, wewe si ulikuja na Sweta chafu mjini, Hadi nikija mama Kulwa ananikonyeza nikwangalie Sasa hivi umenenepa hapa kwa mzee Mgaya na unajua kuongea na wewe siyo?
Sema umekuwa bonge la baba saizi eeh.alitania Cathy.

Kwani hivi wewe dada unafanya kazi gani? aliuliza Samson

(Huku akicheka)
Heeee baba, unataka kunipa kazi mwenzangu? badala ya kujibu swali naye aliuliza huku akitoa macho yake makubwa na mazuri.

Hapana nataka siku unifundishe kuendesha gari, unajua shuleni kwetu vijana wengi wanaendesha magari, lakini Mimi sijui kabisa dada yangu .
safari hii aliongea kwa heshima Samson.

Wenzio ni born town mambo ya magari ni kitambo, usipende kuiga iga utakuja kuumia bure, haya kwa mfano nimekufundisha umejua utapata faida ikiwa huna gari lako? aliuliza kwa dharau Cathy.

Dada Cathy unapenda sana kwenda kanisani, ningekusaidia siku moja moja kuendesha au unasemaje. aliuliza Samson

Tausi hakujibu neno, zaidi ya kumwangalia Samson Kisha akatabasamu na kugonganisha viganja kwa mshangao kwani hakutarajia Samson aseme vile.

Sawa mwaya kesho naenda kanisani, nikirudi, nitakufundisha gari sawa aliongea huku akiingia zake ndani ya gari, huku Samson akimpungia mkono na Cathy akiwasha indicator kwa ishara ya kumkubalia.

Cathy Kuna namna kavutiwa na Samson, huku Samson naye akiwa hayuko nyuma, na ni mwepesi sana kusahau Nini kitatokea? Sehemu ijayo ina majibu.

Itaendelea.........................
Sam anataka kujifunza kuendesha gari, Sam katisha sana
 
Yaani hii situation ya balehe ni hatari sana, kijana unasukumwa na hisia za kijinga sana.
 
SEHEMU YA SITINI

Mzee Mgaya na Samson walitoka huku Samson akiwa hajapenda kwenda sehemu kwa usiku ule ila angefanyaje, wanaomlisha ndiyo washasema, na hata hivyo bado alikuwa na jambo bichi hivyo ilibidi akubali kishingo upande.

Walianza kukatiza chochoro na kuivuka barabara na kuishika njia ya nyumbani kwa mwalimu mkuu, waligonga geti wakafunguliwa, na kukutana uso kwa uso na yule mwalimu mkuu,

Aiseee karibuni, karibu sana Mzee Mgaya, naona umeamua kuja kunitembelea, na una bahati nilikuwa nataka nitoke kina pub yangu Iko hapo nyuma huwa napenda kwenda kupoteza muda hapo.aliweka kituo yule mwalimu huku akionesha anamshangaa mzee Mgaya.

Siyo nimekuja kukutembelea Mzee mwenzangu, ila kuna ujumbe nimepata jioni hii nikaona nije nikusikilize maana sijaelewa vizuri.
aliongea mzee Mgaya huku akionesha Shari waziwazi.

Yule mwalimu akawakaribisha kwenye chumba fulani ambacho kilikuwa kizuri sana likiwa na viti karibu sita,
Karibuni huku hii ndiyo ofisi yangu nikiwa hapa nyumbani. aliongea yule mwalimu mkuu huku muda wote akishindwa kujizuia kumwangalia Mzee Mgaya.

Unajua Mzee Mgaya kwanza nimekuheshimu tu kukukaribisha hapa kwangu, kwasababu kwenye ile barua Kila kitu kipo wazi nilikwambia tukutane kesho, na siyo leo!
Ila siyo mbaya nilichokuitia ni kwamba,nimejaribu kuzungumza na mwalimu wangu ambaye nyinyi mnamtuhumu kuwa alileta fujo sijui alitaka kumfanyia vitendo vibaya Binti yako, lakini mwalimu Sadick amekataa na kwa mujibu wa maelezo aliyonipa nimemwelewa sana hivyo ukajaribu kuongea na Binti yako vizuri, huenda amezua haya mambo, au labda alimfananisha na wapo mashahidi kadhaa ambao kama ungekuja kesho kule shule basi ungejua jambo.

Na nikuombe kitu kimoja Mzee mwenzangu wewe tumesaidiana mambo mengi sana, mwisho ni siku ulipomleta huyu kijana, unajua fika taratibu za uhamisho hazikukamilika, lakini kwakuwa tumetoka mbali Mimi nilikusaidia sana hata kufikia kijana wenu anaendelea na masomo hadi Leo hii, Sasa wewe mbona unakuwa huna ubinadamu? aliweka kituo, mwalimu mkuu huku akionesha hajapenda kitendo cha Mzee Mgaya kwenda wake wakati barua ilimtaka wakutane shuleni.

Sawa Mimi nitafanya uchunguzi zaidi, kama yule Binti alitudanganya, itajulikana tu, alisema Mzee Mgaya huku akiinuka na kuondoka.

Wakiwa njiani Samson alimuuliza baba yake mkubwa maswali kadhaa...

Kwani baba hili suala la Rahma bado unalo tu? na kama bado lipo unaamua nini? Je, unataka kushtaki? Mimi nadhani tungeongeza ulinzi ikiwemo kumwambia Da Rahma kuwa asiwe anaruhusu au kumfungulia mtu mgeni. aliongea Samson kwa kujikaza huku akiwa anasubiri itakuwaje.

Wewe hujui kitu nyamaza, mambo yako yasiyo ya kinidhamu uliyoyafanya, ni sawa na aliyoyafanya huyu mwalimu wenu, na usione tumekukalia kimya Samson umetuudhi familia nzima, Tena hupaswi hata kuniuliza haya mambo wewe Kaa kimya sawa. alichimba mkwara Mzee Mgaya.

Walifika nyumbani kwao huku wenzao wakiwa washagawana vyumba na kuondoka, Samson aliingia bafuni akajiswafi na kuja kitandani kwake huku akijikuta ni kama mtumwa mle ndani,
Hivi huyu mzee hata wanae anaweza kuwazurulisha usiku namna hii, Ina maana hajui kuwa Mimi napaswa kupata muda wa ziada wa kujisomea? hakuwa na cha kufanya kwani alishazidiwa, asubuhi yake ilikuwa ni weekend kama kawaida alijihimu na kufanya kazi sawa na Rahma yote ikiwa ni kujitengenezea mazingira mazuri ili azidi kuaminika.

Wanangu leo tunaenda mjini naenda kucheki maendeleo ya biashara zangu, hivyo Kila mtu ajiandae, aliongea mama Kulwa kisha Mzee Mgaya akadakia.

Sasa watu wote muende mjini mkafanye nini, huyu Samson abaki alinde nyumba , sioni sababu ya kwenda huko. aliongea Kwa sauti ya kuamrisha Mzee Mgaya kitendo ambacho kilimuuma sana Samson ila hakuwa na jinsi.

Mama Kulwa , Mzee Mgaya mwenyewe pamoja na Rahma, waliingia kwenye gari na kutoka huku Mzee Mgaya akiwa hafiki mjini ila anaenda sehemu kwaajili ya kukutana na madalali wa magari, licha ya kushauriwa kuwa ni vyema angenunua gari jipya kwani uwezo alikuwa nao lakini yeye alipenda sana vitu vya bei rahisi.

Samson alirudi ndani huku asubuhi ile akishindwa cha kufanya, lakini akakubali hakuwa na jinsi, akaingia ndani na kuchukua kitabu fulani cha kiingereza na kukaa nje huku akijisomea.

Geti liligongwa Sam akainua macho na kutega masikio kama alichosikia ni kweli, geti likagongwa kwa nguvu akainuka na kwenda kufungua taratibu na kutizama ni nani,
Macho yaligongana na Cathy mwanamke fulani rika la mtoto wa kike wa mama Kulwa, ilikuwa ngumu, kusema Cathy na mama Kulwa ni marafiki lakini ndivyo ilivyokuwa,

Cathy alikuwa mtoto wa mjini sana , alijua vitu vingi vikubwa, huku akiwa na bwana nje ya nchi ndiye aliyekuwa akimpa kiburi cha kuishi mjini, Cathy hakuwa na kazi mjini ilikuwa ni kawaida kumkuta viwanja vya bata lakini akiwa anawezeshwa na bwana wake.

Mama yangu yuko wapi, aliuliza Cathy.

Katoka, kaenda mjini, kwani wewe hamjawasiliana naye? aliuliza Samson.

Hapana, mbona unaniuliza hivyo kwani kuja hapa Mimi hadi niwasiliane naye, maswali hayo muulize mtu mgeni Mimi hapa ni kama kwangu Mimi nimesoma chuo na Dr Glory mtoto wa huyu mama, nilikuwa nalala hapa hapa ,wewe kipindi hicho si ulikuwa shamba huko vijijini kwenu, kifupi hapa ni kama kwetu tu, aliongea Cathy kama anatania lakini ulikuwa ndiyo ukweli wenyewe.

Sawa , Mimi sikatai nilikuwa shamba na kule ni kijijini kwetu nilikozaliwa na hata ulivyonikumbusha tayari nimemiss mazingira ya nyumbani sana tu. alijibu Samson huku akicheka.

Kweli we mshamba yaani unafika maeneo ya mjini halafu unakumbuka habari za kijijini! alicheka sana Cathy huku akifunga mlango wa gari vizuri ili amsikilize Samson kwani stori zilikuwa zinanoga.
Kwa kifupi Cathy hajawahi kumkubali Samson, hata kipindi Sam akikwaruzana na Mama Kulwa, Cathy alikuwa mstari wa mbele akishadadia Samson afukuzwe.

Lakini pia Samson naye hakumpenda Cathy, alimuona kama kijipu uchungu mwilini mwake hasa kwa mdomo aliokuwa nao, lakini siku hiyo wakajikuta wanapiga stori.

Hivi wewe Samson kwahiyo unajisikiaje kukaa peke yako hivi, huoni kama wanakutenga? aliuliza swali la kimtego Cathy.

Wananitenga kivipi, yaani watu wameniamini na kuniachia nyumba na vyote vilivyomo halafu unasema watu wananitenga? wangekuwa wananituma kazi za nje wasinipe uhuru wa kukaa hapa ningekubaliana na wewe. alijibu Kwa kujiamini Samson.

Yaani Samuuuu umekuwa mjeuri, wewe si ulikuja na Sweta chafu mjini, Hadi nikija mama Kulwa ananikonyeza nikwangalie Sasa hivi umenenepa hapa kwa mzee Mgaya na unajua kuongea na wewe siyo?
Sema umekuwa bonge la baba saizi eeh.alitania Cathy.

Kwani hivi wewe dada unafanya kazi gani? aliuliza Samson

(Huku akicheka)
Heeee baba, unataka kunipa kazi mwenzangu? badala ya kujibu swali naye aliuliza huku akitoa macho yake makubwa na mazuri.

Hapana nataka siku unifundishe kuendesha gari, unajua shuleni kwetu vijana wengi wanaendesha magari, lakini Mimi sijui kabisa dada yangu .
safari hii aliongea kwa heshima Samson.

Wenzio ni born town mambo ya magari ni kitambo, usipende kuiga iga utakuja kuumia bure, haya kwa mfano nimekufundisha umejua utapata faida ikiwa huna gari lako? aliuliza kwa dharau Cathy.

Dada Cathy unapenda sana kwenda kanisani, ningekusaidia siku moja moja kuendesha au unasemaje. aliuliza Samson

Tausi hakujibu neno, zaidi ya kumwangalia Samson Kisha akatabasamu na kugonganisha viganja kwa mshangao kwani hakutarajia Samson aseme vile.

Sawa mwaya kesho naenda kanisani, nikirudi, nitakufundisha gari sawa aliongea huku akiingia zake ndani ya gari, huku Samson akimpungia mkono na Cathy akiwasha indicator kwa ishara ya kumkubalia.

Cathy Kuna namna kavutiwa na Samson, huku Samson naye akiwa hayuko nyuma, na ni mwepesi sana kusahau Nini kitatokea? Sehemu ijayo ina majibu.

Itaendelea.........................
umalaya utamuua samson
 
SEHEMU YA SITINI NA MOJA

Mzee Mgaya alirudi nyumbani huku akiwa anaonekana mwenye haraka sana, huku akimuomba dereva Taxi aliyemleta kuwa amsubiri kwani baada ya muda fulani wanaondoka.

Wewe umekula, maana ni saa tisa kasoro hii, huwezi kushinda na njaa hebu shika hii hela utaenda huko migahawani ukale. alisema mzee Mgaya huku akiangalia saa na kuondoka

Samson alichokifanya yeye ni kwenda kuiweka hela ndani kwake na kutoka nje akazugazuga pale nje, na kwenda kuoga Kisha akatoka kwenda kujisomea kwenye kundi lake.

Alirudi mida ya saa moja akimkuta mama Kulwa na Rahma wamerudi huku Rahma akiwa anaenda jikoni,

Wewe vipi tena mwenzetu unaachiwa nyumba na wewe unatoka maana yake nini,
Nini maana ya mzee Mgaya kukuzuia ubaki hapa, lengo lilikuwa nini ? Je tutabaini vipi wizi uliofanyika hapa, siku nyingine usifanye hivyo. alisema mama Kulwa.

Halafu ulikula wapi maana hatuoni dalili kama ulipika, aliuliza mama Kulwa.

Baba alirudi mchana, akanipa hela nikale mgahawani. alijibu Samson.

Sasa kuanzia leo ni marufuku kununua chakula, wewe unajua vyakula vipo ndani vimejaa, Kila kitu kipo unawezaje kwenda kununua chakula? Hiyo haifai na haitakiwi kabisa kwa kuanzia leo naomba uanze kushirikiana na dada yako kupika, hatua kwa hatua, nahitaji kuona siku ukipika chakula cha watu wote huku ndani. aliongea mama Kulwa huku akiwa zake ndani akifuatilia vipindi kwenye television.

Samson alikuwa anatumwatumwa vitu na Rahma, huku wakipiga stori za hapa na pale.

Unajua nini Samson, kumbe mama ana duka kubwa wewe acha tu, Kuna wauzaji zaidi ya wawili lakini pia inaonesha wale wafanyakazi wanamuogopa sana mama sijui ndiyo kumuheshimu, lakini safari hii nimeenjoy sana leo yaani natamani tungekuwa wote. aliweka kituo Rahma.

Mzee Mgaya anapenda sana kunionea mimi Kila nachofanya naonekana nakosea, muda ule asubuhi kanishusha kwenye gari eti nilinde nyumba, hapa aibe nani? Wazee Hawa Wana mambo ya kikoloni sana , yaani nimechukia sana ile asubuhi. alilalamika Samson.

Sasa nikusimulie, kwanza muda wa mchana mama akasema twende tukale, Mimi mawazo yangu labda kwenye hivi vimigahawa ya kawaida lakini nikashangaa kuona anaendesha gari hadi hotel fulani nzuriiiiiiii tukaingia humo na kukuta watu wengi maarufu wahindi, wazungu, na wengine wengi wanaonekana Wana maisha mazuri, tumekula chakula kitamu sana baada ya hapo , mama akasema inabidi tukanunue nguo zangu maana sina tukaelekea Hadi kwenye maduka ya wapemba ambako nguo zangu nazozipenda zinauzwa huko.

Yaani huyu mama MUNGU ambariki sana juu ya kuwa ana ukali na maneno fulani lakini hana roho mbaya ila yeye huwa hapendi utani ndiyo maana tunamuona hafai lakini yupo vizuri sana.

Sasa nikumalizie stori Sam, leo nimemuona Rais Mkapa live akiwa juu ya gari akiwapungia mikono wananchi, aliweka kituo Rahma.

Dah yaani hapa nimekosa vingi sana leo, kwani wewe umemuona akiwa wapi, kwani ni rahisi kiongozi mkubwa kuonekana hadharani hivyo? aliuliza Samson.

Hapanaaaa iko hivi, baada ya kutoka pale dukani kwa wapemba wakati tunataka kuingia kwenye gari mama alikutana na mwanamke mmoja wakasalimiana huku yule mwanamke akimshangaa mama kuwa kwanini hajaenda kwenye mapokezi ya Rais, ndipo alipokubali na kuniambia twende tukaone, tukalipita duka letu kama tunarudi nyumbani ndipo tulipokutana na msafara ule Ukiwa umesimama, tulishuka kwenye gari lakini hatukusogea sana kutokana na umati wa watu kuwa mkubwa sana. aliongea Rahma na kumfanya Samson ashike Tama huku wivu wa kitoto ukimsumbua kwa kukosa uhondo.

Mzee Mgaya aliingia na kumkuta Samson akiwa na Rahma jikoni,

Wewe Samson njoo kwanini upo huku wewe si nimekukatalia kuwa pamoja na huyo Binti? aliuliza mzee Mgaya lakini mama yao akaingilia......

Nataka ajifunze kupika, maana ipo siku atashinda na njaa wakati vyakula vipo, na si vizuri sana vile ulivyofanya maana nasikia umempa hela eti akanunue Chakula, Sasa lipi Bora ajifunze kupika au uwe unampa hela?
Utamlemaza huyu. alisema mama Kulwa.

Walijumuika mezani pamoja huku wakipiga stori zao,

Unajua nini mke wangu Sasa nimekwana naungana na wewe , nimekubali ushauri wako, nimezunguka kutwa nzima lakini sijaona gari la maana, lipo moja ni zuri sana ila ni gharama, halafu yaliyobaki ni kama kamari tu naweza kupoteza hela zangu bure tu. aliweka kituo mzee Mgaya

Mimi nilishakwambia agiza gari nje ya nchi, kubali kuingia gharama, lakini upate chombo ambacho utatumia muda mrefu sana, siyo service kila siku yaani mtu hulali Tena unawaza gari litaharibika lini, ila kama wewe mwenyewe umechunguza na kuona ushauri wangu una mashiko, fanya hivyo jua kuwa shughuli zako zinahitaji usafiri ohooooh, aliongea mama Kulwa.

Mke wangu nasikia Rais leo alikuwa anawashukuru wananchi wake kwa kumpa kura, ila huyu bwana Mimi hata sikuamini hata kidogo kama atapita basi tu, ila hongera zake kwa kweli maana changamoto kaipata
Augustino Mrema alimnyima sana usingizi huyu jamaa. aliongea Mzee Mgaya huku wakionesha wanajua wanachokizungumza.

Wewe baba Jose wewe sema tu kwakuwa si mwanasiasa na hukuzipenda siasa lakini Chama Cha mapinduzi ni dude kubwa sana kushindana nalo,naujue kuwa ili upate kunyoosha mambo yako kwenye nchi hii lazima ufungamane na hiki Chama. aliongea mama Kulwa huku akimwangalia mume wake usoni.

Kujiendekeza tu, ipo siku hata kama kizazi Cha mia moja, hakuna marefu yasiyokuwa na ncha Kila kitu kitakaa sawa tu wananchi wakishakijua wanachotaka basi Kila kitu kitakaa mahala pake. Alijibu mzee Mgaya

Stori zile zilimzuia Samson ambaye muda wote alisimama akionesha anataka kusema jambo, mama Kulwa alitambua Kisha akamuuliza,

Vipi baba yangu mbona kama unataka kusema kitu, sema Kuna nini?

Hakuna kitu ila nilikuwa nawaomba ruhusa kuwa kesho nataka kwenda kanisani, alisema Samson na kuwafanya Mzee Mgaya na mkewe waangaliane huku wakitabasamu.

Wewe tangu umefika hapa nilikuwa nakulazimisha tu kwenda kanisani, baadaye ukaanza kunikwepa na kufichama, leo hii unadai kwenda mwenyewe! Maajabu huenda siku za mwisho zimekaribia, alitania mama Kulwa huku akimwangalia mume wake na kucheka.

Kwani lazima zikaribie siku za mwisho, usipende kuwaza negative kwanini usiseme labda nyumba itabarikiwa, au tutapata neema?
Na ujue mke wangu haya mambo ya Imani haya yaone hivyo hivyo.
Hivyo usishangae mtu bila kushurutishwa akaanza kuwa karibu na MUNGU.
Samson Mimi nakutakie Kila la kheri na kesho ikifika wewe nenda mwanangu , napenda sana familia ya wachamungu Tena chukua na sadaka kabisa, aliongea Mzee Mgaya huku akiingiza mkono mfukoni na kutoka na sarafu na kumkabidhi Samson.

************************************

Misa kuu inaanza tayari Samson alikuwepo kuanzia masomo yote hadi injili ambayo ilisomwa na padre aliyeongoza Misa siku hiyo, lakini muda wote Sam alikuwa akiangaza macho hasa ule upande wa wanawake lakini hakumuona Cathy, aliwaza labda kachelewa tu, lakini dakika zilienda hakumuona mwili wake ulinyong'onyea sana, kwani hakwenda kanisani kumuomba MUNGU kama watu walivyodhani Bali ni kuonana na Cathy.

Wakati mahubiri yakiendelea padre alisoma kisa kinachoonesha Lazaro alikuwa mtu masikini, akila makombo yaliyoanguka chini ya meza ya tajiri huku akiwataka waumini wake haswa wenye uwezo kama wanamsaidia mtu basi watoe kwa moyo na so kutoa kitu kwakuwa eidha kimechakaa/oza au kimekinai.
Mfano ule ulionesha kuwachoma watu maana wengi walikuwa wakitikisa vichwa vyao.

Wakati wa kutoa matoleo au sadaka ulifika huku utaratibu ukiwa wanaanzia watu wa nyuma kabisa ili wasivuruge au kuleta mpangilio mbaya

Basi Binti machachari mwenye viatu vilivyokuwa na visigino virefu, huku vikisikika kanisa Zima alikuwa anaenda mbele ya kikapu kumtolea MUNGU sadaka kama shukurani.
Ndipo moyo wa Samson ulipopata amani baada ya kugundua uwepo wa Cathy mle ndani kanisani.

Baada ya Misa kuisha watu wote walitoka huku baadhi ya watu wakipiga stori kule nje wengine wakishika njia kuelekea majumbani mwao, Samson alimuona Cathy akiwa anaongea na baadhi ya wanawake wenzie pale nje, akaenda ili awasalimie, watu wote walishtuka na kushangaa yule kafata nini huku Cathy akionesha kuchukia,.

Wewe umekuja hapa kufuata nini, halafu usipende kunizoea hivyo sawa kwani hapa kanisani Kila mtu si kaja kivyake hebu potea nisikuone , aliongea Cathy kwa ukali na kuwafanya wenzake wamcheke Samson

Moyo wa Samson ulimuuma kama umepitishwa upanga wa moto, alijikuta kama mbele haoni, akamuomba MUNGU msamaha kwani aligundua kuwa huwenda ile ni laana kwenda kanisani kwaajili ya mtu kuliko kusudi la MUNGU.

Maana mtu aliyesababisha yeye aende huko ni Cathy na ndiye aliyemdharau, akajikuta anahuzunika sana, wakati akiwa yupo kama mita miambili akiwa analiacha kanisa alipigiwa honi , kugeuka lilikuwa gari la Cathy, akaambiwa aingie ndani. akawa dizaini kama anagoma ile sitaki nataka.

Ingia basi Samson au umekasirika , usiwe hivyo mwanaume huwa hayupo hivyo bwana, Samson akaingia na kufunga mlango.

Itaendelea..................
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom