Simulizi: Milango ya mafanikio

Simulizi: Milango ya mafanikio

Kwanini mkuu
Unachosha mkuu unakaa miongo unatuma kamoja ni kama umemuacha mke mwaka mzima umeenda masomoni unarudi unampa kamoja ka sekunde mia unalala sa si bora umuache na nye..zake tu mbona aliishi na hakufa
 
Unachosha mkuu unakaa miongo unatuma kamoja ni kama umemuacha mke mwaka mzima umeenda masomoni unarudi unampa kamoja ka sekunde mia unalala sa si bora umuache na nye..zake tu mbona aliishi na hakufa
Nimekupata mkuu, wiki hii ni kila saa tatu asubuhi
 
SEHEMU YA HAMSINI

Hivi kwanini unatufanyia hivi wewe mtoto eeh, kwanini lakini?
Yaani kwamba honi ya gari hamkuisikia? Karibu dakika tano nzima , mpaka baba yako anajaribu kupanda ukuta ili aje afungue, mpaka tumewaza vibaya tukajua labda mmekufa humu ndani, kwanini mnaleta dharau namna hii,
Na wewe Binti vipi ina maana kweli hukusikia honi hizo mfululizo?
Na hata baada ya mzee wenu kushuka kwenye gari, kagonga mlango kama anataka kuuvunja bado hamkusikia tu? loooooh leo mmetuweza sana. alilalamika mama Kulwa huku akiingia ndani kwa pupa nusura viatu vyake virefu vimuangushe.

Kwa upande wa mzee Mgaya yeye hakuongea jambo mbele ya Rahma badala yake alimuita Samson nje kabisa ya geti na kumuuliza Samson maswali kadhaa akiwa bado amekasirika lakini alijitahidi kujizuia vinginevyo angetandikwa mtu

Najaribu kuwaza vitu vingi juu ya usumbufu mliotupa dakika chache zilizopita , nakushangaa sana mwanangu kwanini unasahau haraka? Ina maana huyu mama yako umemsahau eeh?
Unajua fika alivyo na mdomo, au unataka yajirudie ya kipindi kile?
aliongea Mzee Mgaya kwa sauti ya chini lakini inayoeleweka.

Samson hakuwa na majibu ya maswali yale badala yake alizidi kuomba msamaha tu,
Samahani sana baba Mimi nilikuwa chumbani najisomea na Rahma alikuwa jikoni anapika Sasa binafsi nilikuwa mbali kweli ikawa vigumu kusikia na mwenzangu aliyekuwa karibu sijajua Nini kilimfanya asisikie.
alidanganya Samson akijaribu kuweka sawa mambo.

(Mzee Mgaya akacheka)
Hakuna uhuni utakaofanya Samson Mimi nisiujue na kuanzia leo Kuna uchunguzi nitaufanya naamini nitakuja kupata majibu siku si nyingi maana najua vipo vitu vikifanyika mtu hawezi kusikia sauti hata umbali wa mita moja. mzee Mgaya aliweka kituo.

Moyo ulimdunda Samson na hofu ikamwingia alielewa nini anamaanisha Mzee Mgaya,
Wote wawili walirudi ndani wakaelekea hadi kwenye meza ya Chakula huku wote wakiwa kimya hakuna aliyemuongelesha mwenzie ndipo Mzee Mgaya akavunja ukimya.,

Vipi mama yenu mmemuita, maana muda wote alikuwa alilalamika njaa, hebu mfateni maana ana asili ya lawama kwamba hamjamuita uzuri mnamjua vyema, halafu na wewe Binti sijui nani unaitwa, nakuomba ongeza umakini kwakuwa wewe upo hapa muda wote Sasa itakapotokea vitu vinaenda tofauti lazima mtakosana tu na huyu mama, halafu si anakulipa ? aliuliza mzee Mgaya

Rahma akatingisha kichwa kukubaliana na swali lile.

Eeenh Sasa kama unalipwa, ndiyo mkumbuke wajibu wenu sawasawa maana tayari umekuwa dada wa kazi humu ndani kwahiyo usiishi kindugu humu , ohooooh usije kulalamika unanyanyasika kumbe siyo.
mzee Mgaya alikuwa na busara za hali ya juu lakini pia alisifika kwa kusema ukweli.

Mama Kulwa alikuja pale sebuleni huku akionekana kanuna kuliko maelezo, akachukua kitabu fulani cha kiingereza ambacho kilikuwa kinahusisha masuala ya biashara na uchumi , ni kitabu huwa anakipenda sana .akawa anaingia nacho chumbani kwake.

Vipi mwenzetu Chakula vipi maana uliniambia una njaa, aliuliza Mzee Mgaya.

Njaa, njaa gani tena nakushangaa mwenzangu una nguvu hata ya kula , maana haya mateso waliyonipa Hawa watoto hata hamu ya kula sina kiukweli. aliongea Kwa kifupi mama Kulwa huku akiingia zake ndani.

Mzee Mgaya aliwaangalia wanaye wale kwa zamu huku akiwa hajasema chochote, wakagawana vyumba na kwenda kulala huku wakimuacha Rahma akiwa pale sebuleni akionekana mwenye mawazo kwani uso wake ulionesha hivyo

Samson aliingia chumbani kwake akiwa anakumbuka stori ambayo alisimuliwa na Rahma muda si mrefu hakika ilimgusa sana lakini pia ule wivu alikuwa anawaza asije kupokonywa Rahma na yule mwalimu angalau Presha ilipungua kwani Rahma alimthibitishia kuwa hawezi kuwa na mtu yeyote yule.

Asubuhi na mapema Samson alikuwa kwenye viunga vya shule yao huku baadhi wakimlaumu kwanini Jana hakuonesha uwezo wake wa kucheza mpira badala yake akasababisha timu kufungwa, Samson akajitetea kuwa alikuwa anaumwa ili kumaliza ule utata.

Wakati wakiwa wanapiga stori kule nyuma ya vyoo vya shule, Samson aliambiwa anaitwa kwenye ofisi ya walimu, akawaza anaitiwa nini asubuhi asubuhi, akaenda mpaka ofisini akawakuta walimu kadhaa kila mmoja akiwa kwenye meza yake,

Samson aliwaamkia huku akiwa hajajua kaitwa na nani,
Hakuna mwalimu aliyejibu salamu yake badala yake walianza kumsimanga ,

Wewe unaitwa nani, halafu mbona una nywele ndefu hivyo, na pili hujachomekea, kwanini?
walianza kumshambulia kwa maneno huku akiwa hajui kaitwa na nani.

Huyu ni Samson hamuwezi kumjua kirahisi kwasababu labda hakuna masomo mliyoshika kwenye darasa lake, na mnavyomuona hivyo jibaba Zima eti bado yupo form two, alisema yule mwalimu ambaye alikuwa anamtaka Rahma ile Jana yake.

Uuuuiiiiuwiiii mi nikajua yupo form four huko, alichelewa wapi huyu,mwalimu fulani wa kike alidakia na kufanya walimu wacheke.

Walimsimanga Kisha wakamuacha aende darasani huku akishindwa kujua ni mwalimu gani alimuita na kwanini hawajamwambia walichomuitia.
Wakati wa break yeye hakutoka alibaki na group lake wakijadili mambo fulani yanayokuhusu masomo yao.

Aisee Samson nimekutafuta huko nje sijakuona kumbe upo huku kweli upo serous na masomo, komaa kazana tena huu ndiyo muda wa nyinyi kupambana kumbukeni mwezi wa ngapi tu hapa necta inawahusu hivyo pigeni kitabu,
Aaaaah ila Samson nakuomba kwanza nina maagizo na wewe.

Wakatoka nje, mwalimu akaanza kujieleza,
Sasa Sam eeeh Jana uliniambia yule Binti hasomi siyo?
Samson akatikisa kichwa kukubaliana.

Sawa, Sasa nina shida naye yule nilikuwa nataka muda wa wewe kwenda nyumbani tuongozane , Mimi nitakuwa hapo nyuma tu karibu na mgahawa wa mwalimu mkuu halafu utamuita sawa. alisema yule mwalimu.

Hapana, haiwezekani kwasababu yule ni mfanyakazi wa pale nyumbani na haruhusiwi kutoka nje, labda kwasababu maalum kama kwenda sokoni na maeneo mengine ya muhimu. alijibu Samson.

Halafu wewe inaonekana ni mkorofi sana na taarifa zako ninazo usidhani sikufahamu, nakufahamu fika haiwezekani mwalimu wako anakutuma halafu unamuonesha jeuri, Mimi ni mwalimu wako lazima uwe na nidhamu, ukitumwa lazima ujue nani kakutuma sawasawa? aliongea mwalimu yule kwa ukali.

Sasa teacher utanionea bure, zipo sheria za shule lazima nizifuate na pia nyumbani kwa walezi wangu Kuna sheria wameweka lazima niziheshimu. alijibu Samson

Hebu wahi darasani maana nakuona kama kichaa tu usiyejielewa, nitakukomesha wewe subiri .
Aliongea yule ticha akionesha kukerwa na majibu ya Samson.

Samson siku haikumwendea vizuri sana kwani yule mwalimu alionesha Nia kubwa ya kumtaka Rahma hivyo tayari mambo yalikuwa mabaya kwa Samson. Lakini pia baadhi ya wanafunzi hata wamadarasa mengine Kila walimuona walikuwa wakimzomea kwa kushindwa kucheza mpira vizuri wapo waliofanya yale kiutani na wapo waliomaanisha kweli. lakini hili Wala halikumsumbua alijua ipo siku atawaziba midomo.

Muda wa kurudi nyumbani ulifika, kama kawaida ya group lao walipanga Kila mmoja akale na arudi pale shule kwaajili ya kujifua zaidi hasa ukizingatia ule mwaka kwao ulikuwa na vijitest vingi sana, aliingia ndani akashangaa kumkuta yule mwalimu yupo anaongea na wazazi wake huku wote wakiwa wana furaha sana.

Eeeeh msomi huyooo, karibu mwanafunzi wangu, yaani wazee nisiwe mnafiki Sina somo lolote ninalofundisha kule darasani kwao, lakini nawasikia walimu wanavyomsifia huyu dogo, yaani hongereni sana wazazi maana tunajua msingi mzuri huwa unaanzia kwenu kifupi dogo ana uelewa mkubwa sana tena isitoshe Wana kikundi Chao ambacho ni mfano mzuri sana kwa wenzao ndiyo maana nikasema lazima nifike nyumbani kwao nikawajue hata wazazi wake huyo dogo. alimwaga sifa kwa Samson huku wazazi wakiwa wanafurahi wasijue shida yake.

Kwanza mwalimu nikushukuru sana, sijui niseme nini, ni walimu wachache ambao wanaweza kuwa na moyo wa upendo kama huo, Yaani nyinyi walimu tukishirikiana kama hivi kwaajili ya maendeleo ya watoto wetu, itapendeza sana na hakika lazima mwanafunzi afanye vizuri yaani hongera kwa Hilo na karibu sana mwalimu. Mzee Mgaya alisema huku akionesha kafurahi sana.

Basi Mimi niwaage wazazi wangu, maana nilikaa ofisini nikasema hapana, lazima nifike nikawajue wazazi wa Samson, japo Sam naye Kuna muda ni mkorofiiiiii lakini hayo ni ya kawaida hakuna binadamu aliyekamilika. alisema yule mwalimu ambaye alikuwa ni mtanashati sana.

Yaani sijui hata nisemeje baba yangu, yaani ni shukurani zaidi ya shukrani, yaani karibu sana mwanangu na Samson ni mdogo wako tunaomba kuwa karibu naye na umkumbushe pale atakapojisahau , aliongea mama Kulwa huku wakiwa wanamsindikiza Hadi getini wote wawili yaani Mzee Mgaya na mkewe.

Yule ticha bishoo macho yalikuwa kwa Rahma huku Samson akiwa anaona Kila kitu kwani alijua wazi ujio wa yule mwalimu ni kuleta mazoea ili iwe rahisi kuja kuja pale, kitendo kile Rahma alikielewa na akaamua kugeukia sehemu nyingine huku akiwa bize na kufua.

Dada habari, yule mwalimu alisalimia.
Rahma hakuitikia ile salamu si kwamba hakuisikia ila alikuwa hataki.

Wewe Rahma unasalimiwa na huyu mgeni, ni mwalimu wa shuleni kwa akina Samson, mama Kulwa aliongea huku akimfinyia jicho Rahma kwanini anashindwa kuitikia salamu,
Wakamfikisha nje huku wakiagana kwa bashasha.

Waliporudi ndani wakaanza kumshambulia Samson,
Hivi wewe mtoto upoje, mwalimu wa shuleni kwako, wewe unamfahamu sisi hatumjui, amekuja kwaajili yako , lakini cha ajabu upo mbali nae hata kumsindikiza hukutaka mbona huna aibu ,Tena umepata bahati mtu anakutembelea nyumbani kwako huoni kama ni jambo zuri.
aliongea Kwa kulaumu mama Kulwa

Ni sahihi kabisa Samson wewe si mtoto Tena lazima baadhi ya vitu uwe unajiongeza mwenyewe, Mzee Mgaya alipigilia msumari.

Mimi sitaki mazoea na huyo mwalimu kwanza hana somo anapofundisha kwetu , pili Sina mazoea naye kwani ni mwalimu mpya hata miezi mitatu hajafikisha , halafu, hebu mjiulize kama angekuwa ni rafiki yangu Mimi ndiyo ningemleta hapa nyumbani na kumtambulisha,hivyo niseme tu kuwa sitaki mazoea naye kama anakuja hapa labda kwaajili yenu.
alijibu Kwa kujiamini Sam.
Na tangu wampokee akitoka kijijini hajawahi kujibu vile.

Mzee Mgaya na mkewe waliangaliana kwa muda wakishindwa kujua Samson ana maana gani.

Milango ya mafanikio itafunguka kwa Samson? Maana tayari ana mambo mengi.

Itaendelea.................
 
SEHEMU YA HAMSINI NA MOJA

Baada ya wiki kadhaa kupita Kuna siku ambayo ilikuwa ni weekend, Mzee Mgaya aliamka asubuhi na mapema na kumtaka Samson aamke kwani kulikuwa na ratiba nyingi siku hiyo

Najua una ratiba zako za kwenda kujisomea sasa nataka twende kwanza kule Karakana maana mafundi wameniambia niende sijui Kuna Nini lakini pia tutaenda Temeke maana ile gari nilimwambia anitafutie mteja, na inaonekana tayari kampata hivyo jiandae mpaka saa nane mchana tuwe tumesharudi.
aliongea Mzee Mgaya huku akipiga piga tairi za gari na buti zake.

Watu watatu, Mzee Mgaya, mama Kulwa na Samson waliingia kwenye gari lao jipya,
Sasa shoga yangu, nadhani tutarudi mchana hivyo masuala ya chai wewe jiandalie mwenyewe sisi tutarudi muda wa chakula cha mchana, hata hivyo naomba jambo moja uzingatie wageni usiowafahamu usiwafungulie geti waambie sisi hatupo. alisisitiza Mama Kulwa Kisha gari likaondoka.
Huku wakipiga stori za hapa na pale wakiwa njiani

Hivi baba Jose Kuna mtu nasikia jana mlikuwa mnagombana naye, tena nasikia nusura mpigane, vipi nini sababu maana mume wangu kuonekana umri huo ulitaka kupigana, inaleta picha mbaya halafu jua una heshima uliyojijengea siku nyingi kwenye jamii sasa inakuwaje tena? aliuliza mama Kulwa.

Dah kweli watu ni wanafiki, yaani tayari washakuletea hizi habari, duh japo ni kweli niligombana na huyo mtu , kwani kanitia hasara isiyoelezeka hela zangu kibao zimepotea kwasababu yake
Iko hivi yule aliniambia nimtengenezee milango miwili kwaajili ya kukamilisha nyumba yake, akatoa hela nusu kwaajili ya kununua mbao na materials mengine, Sasa kama kawaida Mimi nimenunua hivyo vitu, halafu yeye amekuja jana na kudai nimrudishie hela yake eti kabadili maamuzi, baada ya kumkatalia ndipo ugomvi ulipoanzia .
alifafanua mzee Mgaya.

Halafu kuna kitu ambacho nimegundua toka kwa yule bwana, kwasababu nilishangaa kumkuta nje ya geti la nyumbani akiongea na Rahma wewe ukiwa haupo , nadhani ulikuwa dukani kwako na Samson alikuwa shule, kwa namna nilivyowakuta ni dhahiri alikuwa anamtaka japo Binti yangu alionesha kama hataki vile, basi katika kumuhoji kwanini anamshikashika Binti yangu ndipo akasema alikuwa ananiulizia mimi akitaka nimtengenezee milango , akaingia kwenye gari akachukua hela akanipa na kunitaka nimuharakishe japo nikishangaa hata aina ya milango iweje hajanipa, Wala mchoro nikapanga nitamrudia ili nikaombe anipe design au namna milango itakavyo kuwa cha ajabu akasema hahitaji mlango wala Nini ila nimpe tu pesa yake. aliweka kituo mzee Mgaya.

Hili mbona lipo wazi inaonesha alitoa hela kwa kujinasua kwenye mtego, baada ya kumfuma na Binti yetu, kwani ni nani huyo mtu? Mama Kulwa aliuliza.

Si yule aliwahi kugombea udiwani kisa akapigwa chini na akipata kura zisizozidi ishirini. alijibu mzee Mgaya

Haaaaah Sasa yule mzee ndiyo wa kumtongoza Rahma kweli? aliuliza kwa mshangao mama Kulwa.

Ndiyo ushangae wewe maana Dunia haiishi visa na vituko, wanaume tumekuwa na tamaa mbaya sana, Nia yake nini, aje amuambukize tu magonjwa yule mtoto, unasahau mke wangu kwamba hata sifa zilizomfanya wananchi wamkatae awe kiongozi wao ni kwasababu ya skendo zake mbaya, kutembea na wake za watu n.k.alifafanua Mzee Mgaya.

Stori ziliendelea Kati ya mzee Mgaya na mkewe huku Samson akiwa makini akisikiliza huku akigundua jambo kuwa kumbe pindi akiwa shule Kuna watu huwa wanakuja nyumbani kwao, na mbaya zaidi wengine ni wazee kabisa, alijikuta anateswa na wivu uliochanganyika na uoga wa kuambukizwa magonjwa.

Hivi baba Kulwa huku Nako ulikupendea nini mbona Karakana hii umeijenga mbali sana, mwenzangu huku si porini kabisa, yaani bado kupo local sana mume wangu.

Wewe unaongea Ukiwa kwenye gari tu shuka kwanza, Kuna watu wanajenga kwa kasi sana huku lakini pia hili eneo nililopata ni kubwa sana zaidi ya ekari sita, najua ipo siku upande mwingine naweza kuuza, lakini pia huku Kuna wanakijiji wanaishi na baadhi ya miundombinu kama umeme vishafika na ndiyo maana nikafunga mashine zangu,bado maji tu hayajaanza kutoka japo mabomba yameshasambazwa kifupi huku Kila kitu kipo ok mama Jose, uliza kiwanja kinauzwa bei gani licha ya kuona ni porini huku, yaani Nina mpango wa kuja kujenga ili uzee wetu tumalizie huku Kwa huoni kulivyo tulia.aliongea Mzee Mgaya huku akionesha kaikubali sana ile sehemu.

Mama Kulwa hakujibu ila alibinua midomo yake kwa dharau huku akionesha hajapakubali hata kidogo , wakaingia ndani ya Karakana na kuona jinsi vijana wanavyopiga kazi bila kuamrishwa yaani Kila mmoja alionesha kujituma labda kwakuwa bosi alikuwepo , hapa mama Kulwa alifurahishwa sana na utenda kazi wa vijana, walimfuata mmoja mmoja wakimsalimia.

Baada ya muda Mzee Mgaya aliwaita vijana wake, akiwatambulisha kuwa yule wanaye muona ndiye mke wake na yule anayekujaga Mara kwa Mara {Tausi)ni mke mdogo.
Wapo ambao walikuwa wanamfahamu mama Kulwa kwani wameshafuata spair Mara kadhaa hivyo haikuwapa tabu.

Mzee naona huyu dogo unaongozana naye Kila ukija vipi mbona anakuwa bishoo hivyo mlete huku tumfundishe kazi, siyo mtoto wa kiume kupendeza asubuhi, alitania mmoja wa vijana wake akimtaka Samson ajiunge kupiga kazi pale.
Mzee Mgaya akaishia kucheka tu, Kisha akapanda gari na kuondoka.

Mke wangu, hili gari nimelipenda sana ni zuri sana wapo wanaodai inakula sana mafuta, lakini kwa safari kadhaa nilizozunguka nalo, nimeiona ipo vizuri tu, halafu inaonesha iliagizwa na hapa ndipo unaponichanganya maana hukunishirikisha. aliweka kituo mzee Mgaya

Hili gari kiukweli nimepata zali tu, yule mwanangu Cathy ana bwana wake ambaye alimzawadia hili gari siku ya birthday yake, hivyo kwakuwa yeye analo, akaniuzia kwa bei rahisi mno, na pia si unamjua Cathy alivyo na maringo anadai hawezi kuendesha gari toka Japan yeye anataka za mzungu.
Mama Kulwa aliongea wote wakacheka.

Yule msichana namuonaga kama ana dharau mno tena sana, sijui umewezaje kuwa na urafiki naye, aliuliza Mzee Mgaya.

Ni stori ndefu sana yule alitaka kuwa mkweo maana alitoka kumpenda sana Jose, hata hivyo Jose kama unavyomjua misimamo yake, hakutaka hata kumpa nafasi ya dakika moja ajieleze , hivyo Binti wa watu nikaishia kumpa moyo tu. alisema mama Kulwa huku akicheka.

Yaani my first born Jose, awe na yule kahaba wa mjini, weeeeeh kwanza Namuamini sana Jose ana akili zangu zote Tena kanipita asingeweza kuwa na aina ya mwanamke kama Cathy,
Mtu ana mabwana Kila kona loh.
tena wanawake sijui mpoje yule si kajengewa nyumba na jamaa huyu mnayesema alimpa zawadi ya gari hili Sasa mwanangu anamtaka wa Nini tena . aliongea Kwa masikitiko Mzee Mgaya.

Mume wangu Mimi njaa inaniuma huko sijui Temeke siendi naomba unipeleke nyumbani tukale, saa Saba hii ujue, alilalamika mama Kulwa,

Baada ya muda fulani walifika nyumbani, wakasukuma geti ambalo halikufungwa huku wakimlaumu Rahma kwanini hafungi geti wakati ndicho kitu wanachosisitiza Kila siku , waliingia ndani, na kumkuta Rahma akiwa peke yake analia kilio cha kwikwi huku Kila mmoja akishangaa Nini kimetokea. Mama Kulwa alikuwa kachelewa kidogo kushuka kwenye gari, hivyo Mzee Mgaya alimuita akiona ni mtu sahihi wa kumuhoji yule Binti Nini kimempata.

Itaendelea jioni hii............
 
SEHEMU YA HAMSINI NA MOJA

Baada ya wiki kadhaa kupita Kuna siku ambayo ilikuwa ni weekend, Mzee Mgaya aliamka asubuhi na mapema na kumtaka Samson aamke kwani kulikuwa na ratiba nyingi siku hiyo

Najua una ratiba zako za kwenda kujisomea sasa nataka twende kwanza kule Karakana maana mafundi wameniambia niende sijui Kuna Nini lakini pia tutaenda Temeke maana ile gari nilimwambia anitafutie mteja, na inaonekana tayari kampata hivyo jiandae mpaka saa nane mchana tuwe tumesharudi.
aliongea Mzee Mgaya huku akipiga piga tairi za gari na buti zake.

Watu watatu, Mzee Mgaya, mama Kulwa na Samson waliingia kwenye gari lao jipya,
Sasa shoga yangu, nadhani tutarudi mchana hivyo masuala ya chai wewe jiandalie mwenyewe sisi tutarudi muda wa chakula cha mchana, hata hivyo naomba jambo moja uzingatie wageni usiowafahamu usiwafungulie geti waambie sisi hatupo. alisisitiza Mama Kulwa Kisha gari likaondoka.
Huku wakipiga stori za hapa na pale wakiwa njiani

Hivi baba Jose Kuna mtu nasikia jana mlikuwa mnagombana naye, tena nasikia nusura mpigane, vipi nini sababu maana mume wangu kuonekana umri huo ulitaka kupigana, inaleta picha mbaya halafu jua una heshima uliyojijengea siku nyingi kwenye jamii sasa inakuwaje tena? aliuliza mama Kulwa.

Dah kweli watu ni wanafiki, yaani tayari washakuletea hizi habari, duh japo ni kweli niligombana na huyo mtu , kwani kanitia hasara isiyoelezeka hela zangu kibao zimepotea kwasababu yake
Iko hivi yule aliniambia nimtengenezee milango miwili kwaajili ya kukamilisha nyumba yake, akatoa hela nusu kwaajili ya kununua mbao na materials mengine, Sasa kama kawaida Mimi nimenunua hivyo vitu, halafu yeye amekuja jana na kudai nimrudishie hela yake eti kabadili maamuzi, baada ya kumkatalia ndipo ugomvi ulipoanzia .
alifafanua mzee Mgaya.

Halafu kuna kitu ambacho nimegundua toka kwa yule bwana, kwasababu nilishangaa kumkuta nje ya geti la nyumbani akiongea na Rahma wewe ukiwa haupo , nadhani ulikuwa dukani kwako na Samson alikuwa shule, kwa namna nilivyowakuta ni dhahiri alikuwa anamtaka japo Binti yangu alionesha kama hataki vile, basi katika kumuhoji kwanini anamshikashika Binti yangu ndipo akasema alikuwa ananiulizia mimi akitaka nimtengenezee milango , akaingia kwenye gari akachukua hela akanipa na kunitaka nimuharakishe japo nikishangaa hata aina ya milango iweje hajanipa, Wala mchoro nikapanga nitamrudia ili nikaombe anipe design au namna milango itakavyo kuwa cha ajabu akasema hahitaji mlango wala Nini ila nimpe tu pesa yake. aliweka kituo mzee Mgaya.

Hili mbona lipo wazi inaonesha alitoa hela kwa kujinasua kwenye mtego, baada ya kumfuma na Binti yetu, kwani ni nani huyo mtu? Mama Kulwa aliuliza.

Si yule aliwahi kugombea udiwani kisa akapigwa chini na akipata kura zisizozidi ishirini. alijibu mzee Mgaya

Haaaaah Sasa yule mzee ndiyo wa kumtongoza Rahma kweli? aliuliza kwa mshangao mama Kulwa.

Ndiyo ushangae wewe maana Dunia haiishi visa na vituko, wanaume tumekuwa na tamaa mbaya sana, Nia yake nini, aje amuambukize tu magonjwa yule mtoto, unasahau mke wangu kwamba hata sifa zilizomfanya wananchi wamkatae awe kiongozi wao ni kwasababu ya skendo zake mbaya, kutembea na wake za watu n.k.alifafanua Mzee Mgaya.

Stori ziliendelea Kati ya mzee Mgaya na mkewe huku Samson akiwa makini akisikiliza huku akigundua jambo kuwa kumbe pindi akiwa shule Kuna watu huwa wanakuja nyumbani kwao, na mbaya zaidi wengine ni wazee kabisa, alijikuta anateswa na wivu uliochanganyika na uoga wa kuambukizwa magonjwa.

Hivi baba Kulwa huku Nako ulikupendea nini mbona Karakana hii umeijenga mbali sana, mwenzangu huku si porini kabisa, yaani bado kupo local sana mume wangu.

Wewe unaongea Ukiwa kwenye gari tu shuka kwanza, Kuna watu wanajenga kwa kasi sana huku lakini pia hili eneo nililopata ni kubwa sana zaidi ya ekari sita, najua ipo siku upande mwingine naweza kuuza, lakini pia huku Kuna wanakijiji wanaishi na baadhi ya miundombinu kama umeme vishafika na ndiyo maana nikafunga mashine zangu,bado maji tu hayajaanza kutoka japo mabomba yameshasambazwa kifupi huku Kila kitu kipo ok mama Jose, uliza kiwanja kinauzwa bei gani licha ya kuona ni porini huku, yaani Nina mpango wa kuja kujenga ili uzee wetu tumalizie huku Kwa huoni kulivyo tulia.aliongea Mzee Mgaya huku akionesha kaikubali sana ile sehemu.

Mama Kulwa hakujibu ila alibinua midomo yake kwa dharau huku akionesha hajapakubali hata kidogo , wakaingia ndani ya Karakana na kuona jinsi vijana wanavyopiga kazi bila kuamrishwa yaani Kila mmoja alionesha kujituma labda kwakuwa bosi alikuwepo , hapa mama Kulwa alifurahishwa sana na utenda kazi wa vijana, walimfuata mmoja mmoja wakimsalimia.

Baada ya muda Mzee Mgaya aliwaita vijana wake, akiwatambulisha kuwa yule wanaye muona ndiye mke wake na yule anayekujaga Mara kwa Mara {Tausi)ni mke mdogo.
Wapo ambao walikuwa wanamfahamu mama Kulwa kwani wameshafuata spair Mara kadhaa hivyo haikuwapa tabu.

Mzee naona huyu dogo unaongozana naye Kila ukija vipi mbona anakuwa bishoo hivyo mlete huku tumfundishe kazi, siyo mtoto wa kiume kupendeza asubuhi, alitania mmoja wa vijana wake akimtaka Samson ajiunge kupiga kazi pale.
Mzee Mgaya akaishia kucheka tu, Kisha akapanda gari na kuondoka.

Mke wangu, hili gari nimelipenda sana ni zuri sana wapo wanaodai inakula sana mafuta, lakini kwa safari kadhaa nilizozunguka nalo, nimeiona ipo vizuri tu, halafu inaonesha iliagizwa na hapa ndipo unaponichanganya maana hukunishirikisha. aliweka kituo mzee Mgaya

Hili gari kiukweli nimepata zali tu, yule mwanangu Cathy ana bwana wake ambaye alimzawadia hili gari siku ya birthday yake, hivyo kwakuwa yeye analo, akaniuzia kwa bei rahisi mno, na pia si unamjua Cathy alivyo na maringo anadai hawezi kuendesha gari toka Japan yeye anataka za mzungu.
Mama Kulwa aliongea wote wakacheka.

Yule msichana namuonaga kama ana dharau mno tena sana, sijui umewezaje kuwa na urafiki naye, aliuliza Mzee Mgaya.

Ni stori ndefu sana yule alitaka kuwa mkweo maana alitoka kumpenda sana Jose, hata hivyo Jose kama unavyomjua misimamo yake, hakutaka hata kumpa nafasi ya dakika moja ajieleze , hivyo Binti wa watu nikaishia kumpa moyo tu. alisema mama Kulwa huku akicheka.

Yaani my first born Jose, awe na yule kahaba wa mjini, weeeeeh kwanza Namuamini sana Jose ana akili zangu zote Tena kanipita asingeweza kuwa na aina ya mwanamke kama Cathy,
Mtu ana mabwana Kila kona loh.
tena wanawake sijui mpoje yule si kajengewa nyumba na jamaa huyu mnayesema alimpa zawadi ya gari hili Sasa mwanangu anamtaka wa Nini tena . aliongea Kwa masikitiko Mzee Mgaya.

Mume wangu Mimi njaa inaniuma huko sijui Temeke siendi naomba unipeleke nyumbani tukale, saa Saba hii ujue, alilalamika mama Kulwa,

Baada ya muda fulani walifika nyumbani, wakasukuma geti ambalo halikufungwa huku wakimlaumu Rahma kwanini hafungi geti wakati ndicho kitu wanachosisitiza Kila siku , waliingia ndani, na kumkuta Rahma akiwa peke yake analia kilio cha kwikwi huku Kila mmoja akishangaa Nini kimetokea. Mama Kulwa alikuwa kachelewa kidogo kushuka kwenye gari, hivyo Mzee Mgaya alimuita akiona ni mtu sahihi wa kumuhoji yule Binti Nini kimempata.

Itaendelea jioni hii............
Rahma kabakwa nini??
 
SEHEMU YA HAMSINI NA MOJA

Baada ya wiki kadhaa kupita Kuna siku ambayo ilikuwa ni weekend, Mzee Mgaya aliamka asubuhi na mapema na kumtaka Samson aamke kwani kulikuwa na ratiba nyingi siku hiyo

Najua una ratiba zako za kwenda kujisomea sasa nataka twende kwanza kule Karakana maana mafundi wameniambia niende sijui Kuna Nini lakini pia tutaenda Temeke maana ile gari nilimwambia anitafutie mteja, na inaonekana tayari kampata hivyo jiandae mpaka saa nane mchana tuwe tumesharudi.
aliongea Mzee Mgaya huku akipiga piga tairi za gari na buti zake.

Watu watatu, Mzee Mgaya, mama Kulwa na Samson waliingia kwenye gari lao jipya,
Sasa shoga yangu, nadhani tutarudi mchana hivyo masuala ya chai wewe jiandalie mwenyewe sisi tutarudi muda wa chakula cha mchana, hata hivyo naomba jambo moja uzingatie wageni usiowafahamu usiwafungulie geti waambie sisi hatupo. alisisitiza Mama Kulwa Kisha gari likaondoka.
Huku wakipiga stori za hapa na pale wakiwa njiani

Hivi baba Jose Kuna mtu nasikia jana mlikuwa mnagombana naye, tena nasikia nusura mpigane, vipi nini sababu maana mume wangu kuonekana umri huo ulitaka kupigana, inaleta picha mbaya halafu jua una heshima uliyojijengea siku nyingi kwenye jamii sasa inakuwaje tena? aliuliza mama Kulwa.

Dah kweli watu ni wanafiki, yaani tayari washakuletea hizi habari, duh japo ni kweli niligombana na huyo mtu , kwani kanitia hasara isiyoelezeka hela zangu kibao zimepotea kwasababu yake
Iko hivi yule aliniambia nimtengenezee milango miwili kwaajili ya kukamilisha nyumba yake, akatoa hela nusu kwaajili ya kununua mbao na materials mengine, Sasa kama kawaida Mimi nimenunua hivyo vitu, halafu yeye amekuja jana na kudai nimrudishie hela yake eti kabadili maamuzi, baada ya kumkatalia ndipo ugomvi ulipoanzia .
alifafanua mzee Mgaya.

Halafu kuna kitu ambacho nimegundua toka kwa yule bwana, kwasababu nilishangaa kumkuta nje ya geti la nyumbani akiongea na Rahma wewe ukiwa haupo , nadhani ulikuwa dukani kwako na Samson alikuwa shule, kwa namna nilivyowakuta ni dhahiri alikuwa anamtaka japo Binti yangu alionesha kama hataki vile, basi katika kumuhoji kwanini anamshikashika Binti yangu ndipo akasema alikuwa ananiulizia mimi akitaka nimtengenezee milango , akaingia kwenye gari akachukua hela akanipa na kunitaka nimuharakishe japo nikishangaa hata aina ya milango iweje hajanipa, Wala mchoro nikapanga nitamrudia ili nikaombe anipe design au namna milango itakavyo kuwa cha ajabu akasema hahitaji mlango wala Nini ila nimpe tu pesa yake. aliweka kituo mzee Mgaya.

Hili mbona lipo wazi inaonesha alitoa hela kwa kujinasua kwenye mtego, baada ya kumfuma na Binti yetu, kwani ni nani huyo mtu? Mama Kulwa aliuliza.

Si yule aliwahi kugombea udiwani kisa akapigwa chini na akipata kura zisizozidi ishirini. alijibu mzee Mgaya

Haaaaah Sasa yule mzee ndiyo wa kumtongoza Rahma kweli? aliuliza kwa mshangao mama Kulwa.

Ndiyo ushangae wewe maana Dunia haiishi visa na vituko, wanaume tumekuwa na tamaa mbaya sana, Nia yake nini, aje amuambukize tu magonjwa yule mtoto, unasahau mke wangu kwamba hata sifa zilizomfanya wananchi wamkatae awe kiongozi wao ni kwasababu ya skendo zake mbaya, kutembea na wake za watu n.k.alifafanua Mzee Mgaya.

Stori ziliendelea Kati ya mzee Mgaya na mkewe huku Samson akiwa makini akisikiliza huku akigundua jambo kuwa kumbe pindi akiwa shule Kuna watu huwa wanakuja nyumbani kwao, na mbaya zaidi wengine ni wazee kabisa, alijikuta anateswa na wivu uliochanganyika na uoga wa kuambukizwa magonjwa.

Hivi baba Kulwa huku Nako ulikupendea nini mbona Karakana hii umeijenga mbali sana, mwenzangu huku si porini kabisa, yaani bado kupo local sana mume wangu.

Wewe unaongea Ukiwa kwenye gari tu shuka kwanza, Kuna watu wanajenga kwa kasi sana huku lakini pia hili eneo nililopata ni kubwa sana zaidi ya ekari sita, najua ipo siku upande mwingine naweza kuuza, lakini pia huku Kuna wanakijiji wanaishi na baadhi ya miundombinu kama umeme vishafika na ndiyo maana nikafunga mashine zangu,bado maji tu hayajaanza kutoka japo mabomba yameshasambazwa kifupi huku Kila kitu kipo ok mama Jose, uliza kiwanja kinauzwa bei gani licha ya kuona ni porini huku, yaani Nina mpango wa kuja kujenga ili uzee wetu tumalizie huku Kwa huoni kulivyo tulia.aliongea Mzee Mgaya huku akionesha kaikubali sana ile sehemu.

Mama Kulwa hakujibu ila alibinua midomo yake kwa dharau huku akionesha hajapakubali hata kidogo , wakaingia ndani ya Karakana na kuona jinsi vijana wanavyopiga kazi bila kuamrishwa yaani Kila mmoja alionesha kujituma labda kwakuwa bosi alikuwepo , hapa mama Kulwa alifurahishwa sana na utenda kazi wa vijana, walimfuata mmoja mmoja wakimsalimia.

Baada ya muda Mzee Mgaya aliwaita vijana wake, akiwatambulisha kuwa yule wanaye muona ndiye mke wake na yule anayekujaga Mara kwa Mara {Tausi)ni mke mdogo.
Wapo ambao walikuwa wanamfahamu mama Kulwa kwani wameshafuata spair Mara kadhaa hivyo haikuwapa tabu.

Mzee naona huyu dogo unaongozana naye Kila ukija vipi mbona anakuwa bishoo hivyo mlete huku tumfundishe kazi, siyo mtoto wa kiume kupendeza asubuhi, alitania mmoja wa vijana wake akimtaka Samson ajiunge kupiga kazi pale.
Mzee Mgaya akaishia kucheka tu, Kisha akapanda gari na kuondoka.

Mke wangu, hili gari nimelipenda sana ni zuri sana wapo wanaodai inakula sana mafuta, lakini kwa safari kadhaa nilizozunguka nalo, nimeiona ipo vizuri tu, halafu inaonesha iliagizwa na hapa ndipo unaponichanganya maana hukunishirikisha. aliweka kituo mzee Mgaya

Hili gari kiukweli nimepata zali tu, yule mwanangu Cathy ana bwana wake ambaye alimzawadia hili gari siku ya birthday yake, hivyo kwakuwa yeye analo, akaniuzia kwa bei rahisi mno, na pia si unamjua Cathy alivyo na maringo anadai hawezi kuendesha gari toka Japan yeye anataka za mzungu.
Mama Kulwa aliongea wote wakacheka.

Yule msichana namuonaga kama ana dharau mno tena sana, sijui umewezaje kuwa na urafiki naye, aliuliza Mzee Mgaya.

Ni stori ndefu sana yule alitaka kuwa mkweo maana alitoka kumpenda sana Jose, hata hivyo Jose kama unavyomjua misimamo yake, hakutaka hata kumpa nafasi ya dakika moja ajieleze , hivyo Binti wa watu nikaishia kumpa moyo tu. alisema mama Kulwa huku akicheka.

Yaani my first born Jose, awe na yule kahaba wa mjini, weeeeeh kwanza Namuamini sana Jose ana akili zangu zote Tena kanipita asingeweza kuwa na aina ya mwanamke kama Cathy,
Mtu ana mabwana Kila kona loh.
tena wanawake sijui mpoje yule si kajengewa nyumba na jamaa huyu mnayesema alimpa zawadi ya gari hili Sasa mwanangu anamtaka wa Nini tena . aliongea Kwa masikitiko Mzee Mgaya.

Mume wangu Mimi njaa inaniuma huko sijui Temeke siendi naomba unipeleke nyumbani tukale, saa Saba hii ujue, alilalamika mama Kulwa,

Baada ya muda fulani walifika nyumbani, wakasukuma geti ambalo halikufungwa huku wakimlaumu Rahma kwanini hafungi geti wakati ndicho kitu wanachosisitiza Kila siku , waliingia ndani, na kumkuta Rahma akiwa peke yake analia kilio cha kwikwi huku Kila mmoja akishangaa Nini kimetokea. Mama Kulwa alikuwa kachelewa kidogo kushuka kwenye gari, hivyo Mzee Mgaya alimuita akiona ni mtu sahihi wa kumuhoji yule Binti Nini kimempata.

Itaendelea jioni hii............
haya lini na saa ngapi tena?
 
Jifunze moyo wa shukrani ili uwe na furaha na mafanikio unaamrisha utadhani unamlipa mwandishi?
mkuu we unajua mi na jack tunafahamiana vp na tunaongeleshanaje? pita hata juu uone tunavosemezana basi...we una ujuaji sana mwana naamini ni mwanaume punguza kidogo nakuona kila mahali unadakia na kurukia rukia mambo usije rushiwa rungu ukadaka ikawa mengine em kaaga kimya sometimes unaboa acha umama unajiendekeza sana mdomo umekuzidi huwez acha jambo likupite sio maisha dada we kiila kitu umo vp unataka chapati za maji utafikwa shauri yako
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom