Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 573
- 2,553
Droo ya Ligi ya Mabingwa Afrika imepangwa, Simba itaanzia Raundi ya Pili kwa kucheza na mshindi wa mechi kati ya Power Dynamos (Zambia) dhidi ya African Stars (Namibia)
Yanga itaanzia Raundi ya Kwanza kwa kukipiga na ASAS ya Djibouti, timu itakayoshinda itaingia Raundi ya Pili na kukutana na timu itakayoshinda kati ya Otoho ya Congo dhidi ya Al Merrikh ya Sudan
KMKM ya Zanzibar itaanzia Raundi ya Kwanza kwa kukipiga na St. George ya Ethiopia, mshindi wa hapo atacheza dhidi ya Bingwa Mtetezi Al Ahly ya Misri.
Mechi za Raundi ya Kwanza zitachezwa Agosti 18–19 na marudio ni Agosti 25–26, 2023, Raundi ya Pili ni Septemba 15–16 na marudio ni Septemba 29–30, 2023, baada ya hapo inafuata Hatua ya Makundi.