Sijazibwa Mdomo - Dr Ulimboka

Sijazibwa Mdomo - Dr Ulimboka

watanzania ni legelege tu.mangapi yamesemwa lakini hamjachukua hatua?
Kamanda Ulimboka pumzika bila wasiwasi kwani umefanya mengi kwenye sekta ya afya.daima tutakukumbuka na kukutolea mfano.

Kumbe we ni mchina ndo mana unaingilia mambo ya watz ambayo hayakuhusu mdau.
 
Kaambiwa asubiri mpaka harakati za uchaguzi zitapoanza, kwa sasa mshiko hakuna, kisha kula fedha za watu nyingi na kazi haikufanyika ilivyotarajiwa!
 
JANA mwenyekiti wa Jumuiya ya madaktari nchini, Dk. Steven Ulimboka aliibuka na kusema anajiandaa kumwaga mboga juu ya wale waliomteka. Aliwaambia maneno haya baadhi ya waandishi wa habari aliokutana nao:

"Bado niko imara. Sijanunuliwa. Walionichagua (madaktari wenzake) wanafahamu hivyo. Hata walioniteka wanajua kuwa hawawezi kuninyamazisha na kwamba katika kutetea maslahi ya taifa, mimi sina bei. Bali kimya changu kimetokana na kufuatilia kwa karibu masharti ya matibabu yake na katu si kwa kuwaogopa watesi wangu."

Dk. Ulimboka alitekwa, kuteswa kusukumizwa kwenye gari, kupigwa, kufungwa mikono na miguu, kunyofolewa kucha na kutolewa meno; na hatimaye kutupwa katika msitu wa Mabwepande, usiku wa 26 Juni 2012.
Amesema, "Watanzania na wapenda haki duniani kote, wanahaki ya kujua kwa kina yale yaliyonisibu pamoja na watu waliohusika katika kutekwa kwangu. Hivyo ninao wajibu mkubwa wa kueleza ukweli huo na bila kuuma maneno."

Amesema mapambano hayo ni muhimu kuendelezwa kwa kuwa ndiyo njia pekee itakayoifanya serikali kuboresha huduma za afya nchini, ambapo amesema ripoti mbalimbali zinaonyesha kuwa mamia ya wananchi wanakufa kwa kutokana na kukosa huduma bora za afya.

Kauli yake hiyo, inaiweka serikali ya Rais Jakaya Kikwete katika wakati mgumu hasa kutokana na ukweli kuwa iliamua kulifungia gazeti la kila wiki la Mwanahalisi ili lisiweze kuchapisha taarifa juu ya kutekwa kwa kiongozi huyo. Sasa Ulimboka anasema atasema kila neno na kutaja kila mmoja.

Ikiwa hili litafanyika, basi bila shaka kuwa Ulimboka atakuwa amemaliza kiu ya Watanzania. Atakuwa amesaidia sana taifa katika kufahamu ukweli wa kilichotokea. Lakini kikubwa zaidi atakuwa amewafanya seriakli waliofungia Mwanahalisi ili kumlinda mtekaji, Ramadhani Ighondu Abeid ionekane serikali ya wapuuzi.

Hatua hiyo, itamfanya pia Zoka Jack afiche sura yake kwa aibu.

 
Amesema mapambano hayo ni muhimu kuendelezwa kwa kuwa ndiyo njia pekee itakayoifanya serikali kuboresha huduma za afya nchini, ambapo amesema ripoti mbalimbali zinaonyesha kuwa mamia ya wananchi wanakufa kwa kutokana na kukosa huduma bora za afya.
 
Hayo yote ni endapo atafanya hayo aliyosema maana kuwaambia watu utasema ni kuwapa tahadhari wakuzime kabla ya kuwaumbua. Yetu macho.
 
Amesema mapambano hayo ni muhimu kuendelezwa kwa kuwa ndiyo njia pekee itakayoifanya serikali kuboresha huduma za afya nchini, ambapo amesema ripoti mbalimbali zinaonyesha kuwa mamia ya wananchi wanakufa kwa kutokana na kukosa huduma bora za afya.

ok.Ngoja tusubiri tupewe kilichotokea
 
Hivi ile tume iliyoundwa kwa ajili ya kuchunguza saga la Dr Ulimboka imeshaleta report gani?
 
Yale Yale ya Mwakyembe nikirudi kutoka India nitaeleza yote mpaka sasa kiko wapi.Zaidi ya kuwaambia Waandishi wamwache kumfuata fuata.
 
Kauli yake is inviting to the mafisadi waje wazungumze kabla hajasema, vinginevyo...atasema! Sioni umakini wa statements kama hizi. Mkubwa hatishiwi nyau...huletewa nyau wakapambana na si kumtishia nyau. Haoni kuwa anahatarisha maisha yake? Kuna wengine wengi waliahidi watasema, ilipofika wakati wa kusema wakawa wameshazibwa midomo.....yuko tayari kuzibwa midomo?
 
Kwanini ameamua kuhuahidi hadhani wala hafikirii kuwa walengwa wanaweza kutumia mbinu chafu za kuweza kumzima kabla hajafikisha kile alicho nacho kwa wananchi?
 
...........mtasubiri dr aseme mpaka mwisho wa dunia, achana na kitu mfumo bana!!!!!!!!!!!!
 
Kapewa sh mil mia tatu na ahadi ya kupewa cheo wizara ya afya ama kupelekwa India kusaidia watanzania wanaopelekwa India kwenye matibabu, hivyo atakuwa na ofisi ndani ya ubalozi wa Tanzania India. Chezea pesa weye.

Mil.3?? hivi mkuu unajua mshahara wa Dr. Ulimboka ulikuwa ni upi na anafanya kazi wapi?!..Usikurupuke kusema usichokijua mkuu.
 
aendelee kunyamaza tu!! kwani wao kumng'oa meno na kucha bila 2% Lidocaine walisubiri??
 
Kaambiwa asubiri mpaka harakati za uchaguzi zitapoanza, kwa sasa mshiko hakuna, kisha kula fedha za watu nyingi na kazi haikufanyika ilivyotarajiwa!

Penye udhia unapenyeza rupia eeeh! Kwangu mimi nashukuru afya yake imetengemaa. Hayo mengine anaweza kuyapima mwenyewe kama yanalipa au laaa.
 
Hapo tu ndipo watanzania wenzangu tusipoelewana.

1. Tunataka Dr.Ulimboka aseme nini?
2. Akishasema iweje?
3. Maelezo yaliyotolewa magazetini, Youtube video
havitoshi? Tulifanya juhudi ya kusoma hizo habari,
kutazama zile video?

-Kama hatukusoma, kuona n.k kwa nini tusifanye juhudi kufanya hivyo kabla ya kuchangia hapa JF?

- Kama tulisoma, kuona maelezo n.k tunataka na hatukifanyia chochote kile kilichosemwa tunataka Dr. Ulimboka aseme nini tena? Kama hatujafanyia kazi maelezo "madogo" yaliyosemwa, kutakuwa na tofauti gani akisema tena?

4. Kuna tume fulani iliundwa kuhusu mkasa wa Dr. Ulimboka, Je, iko wapi? Haikutumia fedha? majibu yalipatikana? Je, tume haijasahaulika akili mwetu?

-Kama TUME YA UCHUNGUZI iliyoundwana "RAIS" kupeleleza watuhumiwa (kujipeleleza wenyewe) na IKASAHAULIKA, Tutakumbuka chochote kile kitakachosemwa na Dr. Ulimboka?
 
Jamani msikilizeni Dr.anasemaje kuhusu ukimya wake yawezekana kweli kazbwa au la????????
 
we cant wait an mo!kama anafungua ....afunguke kama vipi apige kimya!Nimechoshwa na Michakato isiyo isha!
 
Huyu jamaa asitutanie, alitupa siku arobaini na hajafanya chochote.
Kuna ninibcha kufikiria ama anawaza cha kusema, ameshasahau alichofanyiwa hadi akae na kufijiria cha kusema?
Jamani mwenye access na Mlimani TV amwangalie Dr Ulimboka sasa hivi anazungumza

Updates:

Hii ni habari iliyoandikwa na Tanzania Daima JumatatuOktoba 8 2012
 
Back
Top Bottom