Mijitu yenye wivu wa kijinga utaiona tu, kazi yao kukimbilia failure moja katika mafanikio 100. Hata kama huyo Mwakalinga ange disco kama unavosema, je hapo alipo sasa amefikaje? Unajua watu wapenda maendeleo wanaangalia yule kafanikiwa vipi ili na wenyewe waige. Mijitu yenye wivu inaangalia yule aliwahi kuteleza wapi ili wacheke na kuridhisha nyoyo zao zilizojaa wivu.
kitu kinacho nisikitisha ni kuwa mzee unafikia kwenye conclusion kirahisi sana. Bila ya kufikiri kwa undani, unaonekana ni mvivu wa kufikiri. Sasa hilo ni tatizo kubwa kidogo najitahidi niwe mpole nikueleweshe atimaye naamini utaelewa tu. Unaposema wivu wa kijinga unamaanisha nini? Wewe mafanikio kwako ni nini? Halafu failure ni nini kwa definition yako? Mijitu ni nini?. Jaribu kuiga uone.
Je nyie ambao hamkudisco mafanikio yenu yako wapi? mmeifanyia nini Kyela na familia zenu zaidi ya kuishia kuogopa hata kurudi kuendeleza kwenu? Huu mji wenu ulikuwa umejaa Wakinga wenye nacho wakati wenyeji wanazagaa tu mjini. Akina Mwakalinga wameuchangamsha, nyie mnaanza kuona wivu.
Mzee kipimo cha mafanikio ni nini kwa mtazamo wako? Na mji kuchamshwa unamaanisha nini? Mimi mtazamo wangu upo mbali zaidi ya unavyofikiri wewe nitakueleza. Hivi wakinga sio watanzania. Hio tabia ya ukabila wa ajabu unautoa wapi tanzania hii? Umehesabu wakinyakyusa wangapi wako ukingani. Acha hizo sisi tumehama kwenye ukabila tupo kwenye utaifa zaidi. Sasa mtanzania anaeongelea ukabila leo hii inaonekana bado uko nyuma sana. Watanzania wengi wameachwa na dunia. Lakini mwenzangu inaonekana umeachwa na tanzania. Badili mtizamo hii si wakati wa ukabila.
Mbona huyo mbunge wako aliyekutuma uje ubwabwaje hapa alichemsha form six akaishia kwenda chuo cha uandishi wa habari badala ya UDSM? Je mafanikio yake ya elimu kwasasa tuyapuuze kwasababu tu hakufanya vizuri form six?
Tupe data katika hili hivi ni kweli kuwa Dr harison mwakyembe aliishia chuo cha uandishi wa habari badala ya UDSM? Hivi ndivyo mnavyodanganya watu huko, kwa kifupi mwakyembe amesoma chuo cha uandishi wa habari ambacho ni chuo kikuu cha dar es salaam, (IJMC). Sasa mzee hivi kuna haja ya kuendelea maana hapa inaonekana hujui hata IJMC kuwa ni sehemu ya UDSM. Uzuri wa jf ni pamoja na watu kupata elimu daka hilo halafu uwafundishe na wenzio.
Kama Mwakalinga ni msanii,basi nchi hii imejaa wasanii kwa asilimia 99.( usiconclude kirahisi hivi) Inaelekea hata Kyela hukai na nafikiri ndio wale wale mliosoma na kupata elimu nzuri kupitia Kyela na sasa mmekimbilia mijini na mnakuja kwenu kama watalii.
( hapa ndio ipo kazi).
Unaanza hata kuona Mwanjala kwenda na JK USA ni deal kubwa la kuliwekea jungu? Kama hujui kila mfanyabiashara anayeongozana na hawa viongozi huwa amepata hiyo nafasi kwasababu moja ama nyingine( zipi zitaje). Lazima umheshimu huyo Mwanjala, maana hajasoma kama nyie wengine lakini ana mafanikio kwenye biashara zake anazozifanya. Sisi huku wilayani tunawaona akina Mwanjala kama watu wa kuwaiga, watu waliohangaika kwa kuchapa kazi mpaka wakafika wlipofikia. ( usipende sana kuiga tumia akili yako kufiri)
Sasa wewe msomi mwenzetu una mafanikio gani hata kwenye kazi yako? Nyie ndio mmeua mashirika yetu na utendaji wenu hata serikalini mbovu kabisa. (hizi ni tuhuma ambazo inatakiwa uwe na usibitisho na si kulopoka tu)
Tunatamani kuiona kyela iliyonawili kwa maendeleo ya kila nyanja, ikiwamo elimu, afya, biashara, viwanda, miundo mbinu na kilimo. Haya yote ni mchakato wa muda mrefu ni si kitu cha miaka mitano. Sasa kwa mtu anayeweza kujaji kwa miaka mitano ni lazima ajiulize kuwa tumefika wapi? Na tumetoka wapi?
Na kufikiri njia zipi zitumike kujenga kyela yetu na kujenga taifa letu. Kwanza tuelewe kuendelea kwa tanzania ni kwendelea kwa kyela kwa kuwa kyela ni sehemu ya tanzania. Ikiwa kuna kikwazo cha maendeleo katika tanzania basi moja kwa moja kinaathiri kyela kama sehemu ya tanzania. Kwa hiyo mapambano dhidi ya mafisadi ni mapambano yanayowaunganisha watanzania wanaopenda tanzania yao bila kujali kabila na mahali mtu unapotoka. Sasa mapambano haya hata wewe kama unaipenda nchi yako yanakuhusu.
Maendeleo bado ni mchakato si suala la usiku mmoja. Sasa tunapofikiria maendeleo ya sehemu yoyote ile tutazame kwa upeo mkubwa na si kwa upande wa kuchangamsha mji.
Sasa kwa upande wa elimu hatua tuliyopo si mbaya sana. Tulikuwa na shule chache mno za sekondari lakini leo hii tuna shule nyingi (hapa ubora wa elimu ni tatizo la nchi nzima). Leo hii tunashuhudia wanafunzi wa darasa la saba wanafaulu wote kujiunga na sekondari. Zamani hali ilikuwa ni katika wilaya nzima wanaweza wakafaulu watu 30 tu kujiunga na sekondari, kuna shule zinaweza zisitoe hata mwanafunzi mmoja. Sasa leo hii kuna mikakati ya kuanzisha shule ya form six na five. Sijajua wewe na huyo mwakalinga mnashiriki vipi katika elimu maana hatuwaoni kabisa?
Katika kipindi hiki tunahitaji mtu aliyejasali kwa kuweza kuongoza mabadiliko haya, mtu mwenye elimu nzuri, ambaye anaweza akasimamia na kukemea ufisadi ambao umekithiri na umekuwa kikwazo cha maendeleo katika mji wetu. Pia tunahitaji mtu anayesikiliza watu, ninakumbuka mkutano mmoja wa mwakyembe sijawahi ona kyela ikiwa na uhuru kiasi kile. Watu walijieleza kwa mbunge wao akawasikiliza na kuwajibu na kuwalinda kuwa yeyote atakaewashughulia wananchi kwa kusema ukweli kwake atawapeleka mahakamani. Aliwalinda wananchi kwa kutumia uanasheria wake.( hapa muulize sata hapo kyela stendi atakupa story) Je mwakalinga atayaweza haya? Ni suala la kujiuliza kabla ujaingia na ushabiki badala ya hoja. Hapa usije na ishu eti mwakalinga kajenga ukumbi sasa eti hayo ndio maendeleo. Tatizo la wananchi si ukumbi bwana. Wananchi wanahamu na mabadiliko hususani kielimu, kiafya. N.k
Msije mkafikiri kyela haina wasomi wa kugombea, mkadhani eti watu hakuna ndio maana hawatokei kupingana na mwakyembe. Kwa sasa hakuna sababu ya kupambana na harrisoni, sasa ni muda wa kujenga kyela. Na ndio maana wote wemetulia tuli kuangalia na kusapoti jitihada za maendeleo baada ya kuleta upinzani. Sisi na watanzania wanayoitakia mema tanzania na kyela tunamuunga mkono mwakyembe na we will never fail.