Siasa za Mbeya 2005-2010

Siasa za Mbeya 2005-2010

FMES,

..lakini Engineer ametamka mara nyingi kwamba hajatumwa wala hamwakilishi Mwakalinga. mimi nadhani hiyo inatosha kwa hapa jamii forums.

..ila on the ground, kama Mwakalinga ana nia njema na Kyela, basi itabidi aachane na siasa za makundi na kukamiana kama inavyoonekana hapa jamii forums.
 
FMES,

..lakini Engineer ametamka mara nyingi kwamba hajatumwa wala hamwakilishi Mwakalinga. mimi nadhani hiyo inatosha kwa hapa jamii forums.

..ila on the ground, kama Mwakalinga ana nia njema na Kyela, basi itabidi aachane na siasa za makundi na kukamiana kama inavyoonekana hapa jamii forums.

- Mkuu vipi tena unataka kushindana na maneno ya Engineer mwenyewe hapo juu kuwa alionywa na Mwakalinga aache shari? Sasa kama alimuonya hayo, ni yapi mengine aliyowahi kumtuma?

Respect.

FMEs!
 
FMES,

..kwa mtizamo wangu haitakuwa busara kwa Mwakalinga kutokea hapa JF ktk mazingira ya sasa hivi.

..wewe mwenyewe umeona jinsi Zitto alivyosambaratika baada ya kujaribu kujibishana na watu ambao hawaoni na tena wanatumia majina bandia.

..kama in private Mwakalinga ameshamuonya Engineer, basi hilo linatosha kwetu sisi kuamini kwamba amem-disown na hahusiki na maneno na harakati za Engineer hapa JF.
 
FMES,

..kwa mtizamo wangu haitakuwa busara kwa Mwakalinga kutokea hapa JF ktk mazingira ya sasa hivi.

..wewe mwenyewe umeona jinsi Zitto alivyosambaratika baada ya kujaribu kujibishana na watu ambao hawaoni na tena wanatumia majina bandia.

..kama in private Mwakalinga ameshamuonya Engineer, basi hilo linatosha kwetu sisi kuamini kwamba amem-disown na hahusiki na maneno na harakati za Engineer hapa JF.[/QUOTE]

- Mkuu Jokakuu, katika kampeni za uchaguzi kuna ishu za private na ishus za public, sasa interest ya kampeni za Mwakalinga, ni kum-denounce huyu Engineer now na tena to the public hapa JF, kwamba hahusiki naye na anything to do with his ideas on him, yaani Mwakalinga,

- Bado ninasimamia hapo kutokana na experience kubwa niliyonayo na kampeni za uchaguzi wa siasa, hasa za jimbo na ubunge.

Na believe me ni ushauri wa bure tu!

FMEs!
 
Siasa za Kyela zinasikitisha sana maana sijaona mahali wapambe wa hao mafahari 2 wanaogombea uwakilishi wa wananchi kupitia CCM wakiongelea mikakati ya kupeleka maendeleo kwa wananchi zaidi ya siasa za kupakana matope na matusi ya reja reja.

Ukisoma baadhi ya wapambe hapa wanaonyesha wako kwenye ground, na kama wanayoyaandika hapa ndiyo wanayoyasema kwa wananchi basi hii ni hatari kubwa, wananchi wa Kyela wataishia kupandikiziwa mbegu ya chuki kitu ambacho ni sumu kwa maendeleo ya jimbo la Kyela.

Bwana Mwakalinga ninajua huwa unapita kusoma posts hapa JF, jiweke mbali sana na waliokuwa wapambe wa Mwakipesile 2005 na maadui wa Mwakyembe. Ukiwakubali wakusaidie watakusaidia kwa malengo ya kulipa kisasi, na siasa za visasi mara nyingi huwa hazijengi bali zinaweza kukubomoa hata wewe mwenyewe. Mara nyingi siasa za visasi huwa hazina hoja nzito, huwa zina hoja za chuki na kujenga uadui zaidi.

Bwana Mwakipesile ni mwana mtandao hilo halina ubishi, na mwana mtandao yeyote yule hawezi kukana connection na RA + EL. Kwa hiyo iwapo waliokuwa wapambe wa Mwakipesile 2005 utawapokea kama wapambe wako ama kuwaweka kwenye timu yako ya kampeni, itakuwa ni easy shot kwa Mwakyembe na timu yake kukupaka matope ya ufisadi. Ndiyo maana milioni 400 zinapigiwa kelele bado watu wako kazini kutafuta dots ili waweze kuziunganisha. Ninajua Mwakalinga huna uwezo wa kuwakataza wasikupigie debe, lakini una uwezo wa kugoma kuwaingiza kwenye inner circle yako ya timu ya kampeni na hivyo wao watabaki kuwa ma-'dei waka' wako ambao hutawajibika kwa lolote ama kauli zao, na unaweza kuwakana hata mbele ya wapiga kura, lakini kama wako kwenye timu huwezi kuwakana.

Watanzania wa leo japo hawasomi magazeti, lakini wameerevuka sana wanaweza kupima hoja nzito na nyepesi. Kuna memba mmoja kasema magazeti yanasomwa na wajanja wachache wa Kyela mjini, lakini hao wajanja wachache wa mjini ndiyo wanaokwenda huko vijijini kwa jina la upambe na kumwaga sumu mbaya ambayo wanaiokota kwenye magazeti uchwara ya Tanzania. Kwa hiyo hawa wapambe walio kwenye ground kama wanaenda kwa wapiga kura na hivi vioja wanavyoandika hapa unaweza kujikuta unapoteza kura kwa sababu ya wapambe wa namna hiyo.

Wagombea wa Kyela tusaidieni kutuletea maendeleo na siyo chuki. Wilaya ya Kyela ina mafuriko kila mwaka, mvua kidogo barabara hazipitiki kirahisi hata kwenda vijiji vya jirani tatizo, ongezeni juhudi kwenye mikakati ya maendeleo badala ya mikakati ya kupakana matope.
 
Last edited:
- Mkuu Jokakuu, katika kampeni za uchaguzi kuna ishu za private na ishus za public, sasa interest ya kampeni za Mwakalinga, ni kum-denounce huyu Engineer now na tena to the public hapa JF, kwamba hahusiki naye na anything to do with his ideas on him, yaani Mwakalinga,

- Bado ninasimamia hapo kutokana na experience kubwa niliyonayo na kampeni za uchaguzi wa siasa, hasa za jimbo na ubunge.

Na believe me ni ushauri wa bure tu!

FMEs!
FMES,

Mbona wewe Masha hakuku denounce ulipokuwa unamchafulia hapa? Wacha zako hizo. Watu kibao walikuambia acha na bado hukuacha, au tayari umeshasahau?

Mimi niliingia kumtetea Mwakalinga baada ya kuona wapuzi kama akina Shalom, Masanilo, Malafyale, magezi na wengine wameamua kumchafua mwenzao bila sababu. Nimepambana nao mpaka sasa wamepotea na wengine wamekuwa marafiki kama mzee wangu Malafyale.

Hata Mwakalinga akileta upuuzi hapa mimi nitamlipua tu. Mimi sio askari wa kukodiwa, ninajitegemea.

Hapa Kyela nampigia kampeni Mwakalinga bila kulipwa hata senti tano. Mimi sio mpambe njaa, nina kazi yangu hata kama silipwi mamilioni lakini inatosha kuishi na kutanua niwezavyo huku vijijini.

Sisi ndio tulimbeba Mwakyembe 2005, tukawaambia na wajumbe wakimchagua Mwakipesile hawatatoka pale ndani. Baadhi ya wapenzi wa Mwakipesile wakaogopa hata kupiga kura. Tulifanya hivyo kwasababu lile zee lilituchosha kwa wivu na kukwamisha maendeleo. Sina mapenzi hata tone kwa huyo Mwakipesile.

Bahati mbaya kumbe tulimweka msanii ambaye yuko tayari kuongea lolote. Miaka minne hii imekuwa ni balaa na ugomvi kila sehemu. Ikabidi baadhi yetu tumgeuke na kuanza kutafuta mtu mwingine. Alivyokuja Mwakalinga tukaona ni bahati maana angalau yeye kuna mambo mengi anaweza akasema ameonyesha kwa matendo kwamba anaipenda Kyela. Tunatumia pesa zetu kumnadi Mwakalinga, kwasababu tunataka maendeleo na sio ugomvi.

Mwakalinga anaungwa mkono na jumuia zote za chama hapa. Hao sio watu wa Mwakipesile. Mwenyekiti wa vijana hakuwa mtu wa Mwakipesile lakini Dr. Mwakyembe aliondoa jina lake ili asiwe mwenyekiti kwasababu tu alikuwa rafiki yake Mwanjala, akakata rufaa na jina lake likarudishwa. Juzi kakwamisha harambee yake kwa visingizio kwamba mtoto wa JK anakuja kumpigia kampeni Mwakalinga. Matokeo yake huyo mwenyekiti sasa anahamasisha vijana bila hata kuombwa na mtu.

Mwenyekiti wa UWT wilaya alipingwa na mbunge na badala yake mbunge alimuunga mkono mtu wa kutoka kwao huko Rungwe. Huyo mama mpaka leo hawaongei na mbunge. Unafikiri mama kama huyo anahitaji hata kuombwa na Mwakalinga? Yeye pia hakuwa mtu wa Mwakipesile huko nyuma.

Mwenyekiti wa Wazazi ni diwani wa Kyela mjini, huyu alikuwa mpambe wa Mwakipesile tokea zamani. Mbunge aliweka mtu wake na kumwaga pesa adondoshwe lakini diwani akashinda. Huyu ana kauwezo kake na yuko tayari kutumia pesa zake kumnadi Mwakalinga.

Team ya Mwakalinga ina watu wengi sana mchanganyiko na hata yeye alisisitiza team iwe na wale watu ambao mwaka 2005 walimwunga mkono Mwakyembe.

Pia kwenye mizunguko yake alikataa kabisa kuongelea ya Mwakyembe na muda wote alikuwa anaongelea hasa elimu, afya na kilimo. Ni tofauti na mwakyembe ambaye kwa aslimia 100 haongelei maendeleo bali ufisadi, na vijembe juu ya Mwakalinga. Akiulizwa ataje majina anakwepa.

Kuanzia sasa nitapunguza kuandika hapa maana naona JF inanipotezea muda wangu wa kufanya mambo mengine.
 
FMES,

Mbona wewe Masha hakuku denounce ulipokuwa unamchafulia hapa? Wacha zako hizo. Watu kibao walikuambia acha na bado hukuacha, au tayari umeshasahau?

- Sijawahi kumchafulia Masha kama kuchafua amechafua mwenyewe akiwa waziri, mimi nimemtetea sana watu walipojaribu kuchafua his background ambayo ninaijua vizuri sana, Masha na familia yake wanajua fika kwamba hata siku moja siwezi kumharibia yeye wala anybody kwenye familia yake, lakini siwezi kumsaidia anyone pia kama amejichafulia mwenyewe, Masha made some mistep nikamwambia one on one kwamba stop it na slow down, he did ndio maana ya friendship!

- Eti nilikuwa ninamchafulia Masha, ilikuwa on what? Yaani una maana Masha alikuwa ni msafi mimi ndio ninajaribu kumchafulia, huoni kwamba ni hoja mufilisi? Kwa taarifa yako na wenzako ni kwamba kuna watu waliotaka nimchafue Masha wakani-offer Millions of money nikaawanbia huwa sio tabia yangu kuwa-betray friends.

- Mwakalinga toka anaondoka UK na kutua Dar na safari zake zote bongo, nilikuwa ninaongea naye kila siku, na ndio maana nilikuja kumtetea sana hapa na uongo mwingi uliokuwa unatungwa na wasiomtakia mema, lakini aliporudi tu UK nikaamua kumuachia mwenyewe kujibu maswali.

Otherwise, ninasema hivi hebu achana na ishu ya Mwakalinga kwa muda hapa JF, maana ni mapema mno kuanza kampeni sasa. Halafu ishu za Masha mbunge na waziri tayari, haziwezi kulingana na Mwakalinga ambaye ndio kwanza anatafuta ubunge tena kwa kura za maoni ni makosa makubwa sana kuzilinganisha!

Respect.

FMEs!
 
FMES,

Mbona wewe Masha hakuku denounce ulipokuwa unamchafulia hapa? Wacha zako hizo. Watu kibao walikuambia acha na bado hukuacha, au tayari umeshasahau?

Mimi niliingia kumtetea Mwakalinga baada ya kuona wapuzi kama akina Shalom, Masanilo, Malafyale, magezi na wengine wameamua kumchafua mwenzao bila sababu. Nimepambana nao mpaka sasa wamepotea na wengine wamekuwa marafiki kama mzee wangu Malafyale.

Hata Mwakalinga akileta upuuzi hapa mimi nitamlipua tu. Mimi sio askari wa kukodiwa, ninajitegemea.

Hapa Kyela nampigia kampeni Mwakalinga bila kulipwa hata senti tano. Mimi sio mpambe njaa, nina kazi yangu hata kama silipwi mamilioni lakini inatosha kuishi na kutanua niwezavyo huku vijijini.

Sisi ndio tulimbeba Mwakyembe 2005, tukawaambia na wajumbe wakimchagua Mwakipesile hawatatoka pale ndani. Baadhi ya wapenzi wa Mwakipesile wakaogopa hata kupiga kura. Tulifanya hivyo kwasababu lile zee lilituchosha kwa wivu na kukwamisha maendeleo. Sina mapenzi hata tone kwa huyo Mwakipesile.

Bahati mbaya kumbe tulimweka msanii ambaye yuko tayari kuongea lolote. Miaka minne hii imekuwa ni balaa na ugomvi kila sehemu. Ikabidi baadhi yetu tumgeuke na kuanza kutafuta mtu mwingine. Alivyokuja Mwakalinga tukaona ni bahati maana angalau yeye kuna mambo mengi anaweza akasema ameonyesha kwa matendo kwamba anaipenda Kyela. Tunatumia pesa zetu kumnadi Mwakalinga, kwasababu tunataka maendeleo na sio ugomvi.

Mwakalinga anaungwa mkono na jumuia zote za chama hapa. Hao sio watu wa Mwakipesile. Mwenyekiti wa vijana hakuwa mtu wa Mwakipesile lakini Dr. Mwakyembe aliondoa jina lake ili asiwe mwenyekiti kwasababu tu alikuwa rafiki yake Mwanjala, akakata rufaa na jina lake likarudishwa. Juzi kakwamisha harambee yake kwa visingizio kwamba mtoto wa JK anakuja kumpigia kampeni Mwakalinga. Matokeo yake huyo mwenyekiti sasa anahamasisha vijana bila hata kuombwa na mtu.

Mwenyekiti wa UWT wilaya alipingwa na mbunge na badala yake mbunge alimuunga mkono mtu wa kutoka kwao huko Rungwe. Huyo mama mpaka leo hawaongei na mbunge. Unafikiri mama kama huyo anahitaji hata kuombwa na Mwakalinga? Yeye pia hakuwa mtu wa Mwakipesile huko nyuma.

Mwenyekiti wa Wazazi ni diwani wa Kyela mjini, huyu alikuwa mpambe wa Mwakipesile tokea zamani. Mbunge aliweka mtu wake na kumwaga pesa adondoshwe lakini diwani akashinda. Huyu ana kauwezo kake na yuko tayari kutumia pesa zake kumnadi Mwakalinga.

Team ya Mwakalinga ina watu wengi sana mchanganyiko na hata yeye alisisitiza team iwe na wale watu ambao mwaka 2005 walimwunga mkono Mwakyembe.

Pia kwenye mizunguko yake alikataa kabisa kuongelea ya Mwakyembe na muda wote alikuwa anaongelea hasa elimu, afya na kilimo. Ni tofauti na mwakyembe ambaye kwa aslimia 100 haongelei maendeleo bali ufisadi, na vijembe juu ya Mwakalinga. Akiulizwa ataje majina anakwepa.

Kuanzia sasa nitapunguza kuandika hapa maana naona JF inanipotezea muda wangu wa kufanya mambo mengine.

Naomba nieleze unafikiri Mwakalinga atafanya nini zaidi ambacho Mwakyembe hajafanya ama atashindwa kufanya?. Mwakyembe kupita na kuongelea ufisadi wewe linakukera nini na kivipi?. Na wewe ni moja kati ya mafisadi?. Matatizo yote yaliyopo Kyela na Tanzania nzima kwa 99.99% yanatokana na ufisadi unaofanywa, Mwakyembe kuukemea na kuuchukia ufisadi ni sababu anayachukia matatizo na umasikini wa wana Kyela na watanzania wote, sasa wewe ulitaka aongelee nini zaidi?. Viongozi wa dini zote, mabalozi wa nchi za nje walio Tanzania, Vyama vya upinzani, kila kona ndani ya Tanzania watu wanalia na ufisadi kwani ndiyo chanzo cha matatizo na umasikini uliopo Tanzania, sasa wewe mwenzetu ni mtu wa namna gani na ni wa wapi ambaye hujaguswa na ufisadi?.

Mwaka 2005 ulikuwa kwenye kambi ya Mwakyembe na sasa umehama na kwenda kwenye kambi inayompinga Mwakyembe, bila shaka una matatizo ya ubongo ama una tamaa ya pesa. Umeona wazi kwamba Mwakyembe hatoi rushwa ili kuchaguliwa sasa umehamia kambi ambayo unajua kwamba utapata mshiko. Umasikini utakuua pamoja na familia yako, usikubali kuiiza kura yako, bali tumia kura yako vyema kuleta maendeleo Kyela na Tanzania.

VOTE FOR MWAKYEMBE
 
Naomba nieleze unafikiri Mwakalinga atafanya nini zaidi ambacho Mwakyembe hajafanya ama atashindwa kufanya?. Mwakyembe kupita na kuongelea ufisadi wewe linakukera nini na kivipi?. Na wewe ni moja kati ya mafisadi?. Matatizo yote yaliyopo Kyela na Tanzania nzima kwa 99.99% yanatokana na ufisadi unaofanywa, Mwakyembe kuukemea na kuuchukia ufisadi ni sababu anayachukia matatizo na umasikini wa wana Kyela na watanzania wote, sasa wewe ulitaka aongelee nini zaidi?. Viongozi wa dini zote, mabalozi wa nchi za nje walio Tanzania, Vyama vya upinzani, kila kona ndani ya Tanzania watu wanalia na ufisadi kwani ndiyo chanzo cha matatizo na umasikini uliopo Tanzania, sasa wewe mwenzetu ni mtu wa namna gani na ni wa wapi ambaye hujaguswa na ufisadi?.

Mwaka 2005 ulikuwa kwenye kambi ya Mwakyembe na sasa umehama na kwenda kwenye kambi inayompinga Mwakyembe, bila shaka una matatizo ya ubongo ama una tamaa ya pesa. Umeona wazi kwamba Mwakyembe hatoi rushwa ili kuchaguliwa sasa umehamia kambi ambayo unajua kwamba utapata mshiko. Umasikini utakuua pamoja na familia yako, usikubali kuiiza kura yako, bali tumia kura yako vyema kuleta maendeleo Kyela na Tanzania.

VOTE FOR MWAKYEMBE

- Kidatu mkuu heshima mbele sana, this is what I am talking about hoja nzito, taifa na wananchi wa Kyela, sio kutuletea blah! blah! zisizokwisha hapa ambazo hazina anything to do na masilahi ya taifa wala wananchi,

- Saafi hizi zako ni hoja, tena nzito sana sasa zijibiwe kwa hoja sio viroja.

Respect.

FMEs!
 
Naomba nieleze unafikiri Mwakalinga atafanya nini zaidi ambacho Mwakyembe hajafanya ama atashindwa kufanya?. Mwakyembe kupita na kuongelea ufisadi wewe linakukera nini na kivipi?. Na wewe ni moja kati ya mafisadi?. Matatizo yote yaliyopo Kyela na Tanzania nzima kwa 99.99% yanatokana na ufisadi unaofanywa, Mwakyembe kuukemea na kuuchukia ufisadi ni sababu anayachukia matatizo na umasikini wa wana Kyela na watanzania wote, sasa wewe ulitaka aongelee nini zaidi?. Viongozi wa dini zote, mabalozi wa nchi za nje walio Tanzania, Vyama vya upinzani, kila kona ndani ya Tanzania watu wanalia na ufisadi kwani ndiyo chanzo cha matatizo na umasikini uliopo Tanzania, sasa wewe mwenzetu ni mtu wa namna gani na ni wa wapi ambaye hujaguswa na ufisadi?.

Mwaka 2005 ulikuwa kwenye kambi ya Mwakyembe na sasa umehama na kwenda kwenye kambi inayompinga Mwakyembe, bila shaka una matatizo ya ubongo ama una tamaa ya pesa. Umeona wazi kwamba Mwakyembe hatoi rushwa ili kuchaguliwa sasa umehamia kambi ambayo unajua kwamba utapata mshiko. Umasikini utakuua pamoja na familia yako, usikubali kuiiza kura yako, bali tumia kura yako vyema kuleta maendeleo Kyela na Tanzania.

VOTE FOR MWAKYEMBE

Naomba kupingana na wewe.
Naomba uniambie kipindi cha Nyerere na cha sasa ni kipi kilikuwa na ufisadi zaidi.?

Na kwa vipindi hivyo ni kipindi gani kina unafuu wa maisha?.

Majumuisho : Ufisadi ni tatizo lakini si chanzo cha umasikini wetu, ufisadi ni tatizo dogo ambalo linawezekana kurekebika ndani ya mwezi mmoja ,lakini tatizo la umasikini litatuchukuwa milongo na milongo.

Mimi nafikiri tusijaribu kukimbia wajibu wetu na makosa yetu kuyarundika kwa ufisadi ,hii itakuwa technical mistake.

Hii ya fanana kabisa na kila kosa analofanya mwanadamu kujaribu kumrushia SHETANI kwa ufupi wa mwanadamu akifikiri atasafishika kosa lake kwa sababu kamupa shetani kosa lake.

kwanini umeiba unajuwa shetani alinipitia kidogo ,kwanini umezini unajuwa shetani, teh teh teh teh teh.

Tatizo la umasikini ni tatizo la sisi wala si mafisadi AKILI zetu walio wengi bado hatujakubali kuwa matajiri.
 
Jamani, ifike wakati waandishi na hata wahariri wao wakaona umuhimu wa kupima habari zao kabla ya kuzichapisha, inavyoonekana hapa kwenye habari hii, uongo ni mwingi. Inawezekana namna gani 'muuaji' wa kweli akamwendea mwanasiasa jukwaani na kisu ili kummaliza? Nimependa Saidhorizons alivyoeleza kuwa huyo jamaa atakuwa na matatizo ya akili kama ni kweli hiyo ilitokea, apelekwe Hospitali ya Magonjwa ya Akili, hasa Mirembe na wala siyo Polisi kusumbuka naye
 
Naomba nieleze unafikiri Mwakalinga atafanya nini zaidi ambacho Mwakyembe hajafanya ama atashindwa kufanya?. Mwakyembe kupita na kuongelea ufisadi wewe linakukera nini na kivipi?. Na wewe ni moja kati ya mafisadi?. Matatizo yote yaliyopo Kyela na Tanzania nzima kwa 99.99% yanatokana na ufisadi unaofanywa, Mwakyembe kuukemea na kuuchukia ufisadi ni sababu anayachukia matatizo na umasikini wa wana Kyela na watanzania wote, sasa wewe ulitaka aongelee nini zaidi?. Viongozi wa dini zote, mabalozi wa nchi za nje walio Tanzania, Vyama vya upinzani, kila kona ndani ya Tanzania watu wanalia na ufisadi kwani ndiyo chanzo cha matatizo na umasikini uliopo Tanzania, sasa wewe mwenzetu ni mtu wa namna gani na ni wa wapi ambaye hujaguswa na ufisadi?.

Mwaka 2005 ulikuwa kwenye kambi ya Mwakyembe na sasa umehama na kwenda kwenye kambi inayompinga Mwakyembe, bila shaka una matatizo ya ubongo ama una tamaa ya pesa. Umeona wazi kwamba Mwakyembe hatoi rushwa ili kuchaguliwa sasa umehamia kambi ambayo unajua kwamba utapata mshiko. Umasikini utakuua pamoja na familia yako, usikubali kuiiza kura yako, bali tumia kura yako vyema kuleta maendeleo Kyela na Tanzania.

VOTE FOR MWAKYEMBE
Kidatu,
Hapo unaongea kweli toka moyoni au ni ushabiki tu?

Hata ufisadi ukikomeshwa kwa asilimia 100 bado Tanzania itaendelea kuwa maskini tena kwa muda mrefu tu.

Ufisadi ni tatizo lakini sio the tatizo. Matatizo ya ujinga, maradhi na uzalishaji duni yataendelea kutuandama hata kama hakutakuwa na ufisadi.

Tanzania ya Nyerere hasa miaka ya 60 na 70 haikuwa na ufisadi na bado Watanzania walikuwa maskini mno.

Wanasiasa wengi wanashikilia bango la ufisadi kwasababu ni rahisi kuongea kuliko kutenda. Kinachotakiwa ni kuongelea ufisadi pamoja na mipango mingine ya maendeleo.

Vinginevyo kwa mtindo huu tusahau hayo maendeleo kwa wote tunayoyasema.
 
Jamani, ifike wakati waandishi na hata wahariri wao wakaona umuhimu wa kupima habari zao kabla ya kuzichapisha, inavyoonekana hapa kwenye habari hii, uongo ni mwingi. Inawezekana namna gani 'muuaji' wa kweli akamwendea mwanasiasa jukwaani na kisu ili kummaliza? Nimependa Saidhorizons alivyoeleza kuwa huyo jamaa atakuwa na matatizo ya akili kama ni kweli hiyo ilitokea, apelekwe Hospitali ya Magonjwa ya Akili, hasa Mirembe na wala siyo Polisi kusumbuka naye

Kamanda,

Hiyo habari ilipikwa na hata polisi wamethibitisha hivyo. Hata mheshimiwa mwenyewe nimesikia sasa anasema tukio halikuwepo na ni vijana wake tu walizua bila yeye kujua. Lakini anacho sahau ni kwamba alishampigia simu hata IGP na pia spika Sitta kumwambia kaponea chupu chupu kuuawa kwa kisu.

Subirini report ya polisi na itawaumbua wanasiasa na vyombo vya habari ambavyo vinakurupuka bila kufanya uchunguzi.
 
SIKU moja baada ya Mkuu wa Mkoa (RC) wa Mbeya, John Mwakipesile, kuwatuhumu baadhi ya wabunge kwamba wanatumia vita dhidi ya ufisadi kuficha maovu yao, wabunge wawili wanaoaminika kuwa miongoni mwa wabunge waliolengwa na kauli hiyo wamepinga madai hayo, huku mmoja wao akimuelezea RC huyo kuwa amechanganyikiwa.

Wabunge hao, James Lembeli, wa Jimbo la Kahama, na mwenzake, Lucas Selelii, wa Nzega, walitoa maoni yao jana kwa nyakati tofauti kuhusiana na matamshi ya RC huyo walipozungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu.

Lembeli alisema RC huyo wa Mbeya hajui anachokisema na ni dhahiri kuwa amechanganyikiwa, kwani kauli aliyoitoa ya kutuhumu wabunge wanaopambana na ufisadi, inapingana na kile alichokisema Rais Jakaya Kikwete hivi karibuni wakati akizungumza na wananchi kupitia redio na televisheni kwa staili mpya ya kujibu maswali ya papo hapo.

Akizungumza na wananchi kupitia utaratibu huo mpya, Rais Kikwete aliwataka wabunge wanaoendelea na vita ya ufisadi waachwe waendeele na kazi hiyo kwani hata serikali haipendi vitendo vya ufisadi viendelee kushamiri nchini.

“Huyo RC hajui anachokisema, ni dhahiri kuwa amechanganyikiwa, maana ameamua kupingana na kile alichokisema Mheshimiwa Rais alipozungumza na wananchi wiki iliyopita. Rais alisema tuachwe tupambane na ufisadi, yeye anakuja anatoa kauli za kukebehi jitihada tunazofanya kupambana na ufisadi.

“Kama ana ushahidi auseme lakini si kuongea kutoka hewani tu. Mimi hanijui wala simjui, sasa anasemaje kuwa wabunge wanaopambana na ufisadi ni mafisadi?” alisema Lembeli.

Kwa upande wake, Selelii alisema kauli zilizotolewa na RC huyo si za kushangaza sana, kwani jambo lolote linalofanywa haliwezi kuungwa mkono na watu wote hata kama jambo hilo linafanywa kwa nia njema kiasi gani.

Alisema haishangazi kuona leo kunaibuka watu kama Mwakipesile wanaotoa kauli za kupinga na kubeza wanaopiga vita ufisadi kwani hata Mtume alipokuja wapo waliojitokeza kumpinga.

Alisema kauli ya Mwakipesile ni kielelezo tu kwamba katika vita yoyote inayopiganwa kwa nia njema, hakukosekani vikwazo, lakini alisisitiza kuwa kile kinachodaiwa kuwa ni uongo baadaye ukweli wake utadhihirika.

“Mimi si fisadi, matendo yangu si yanaonekana…lakini siwezi kukasirika kwa kuitwa fisadi. Hata Yesu alifanya kazi kubwa ya kuwatoa watu mapepo lakini bado kulijitokeza watu waliomtuhumu Yesu kuwa ndiye mkuu wa mapepo, lakini hakukasirika. Kwa hiyo hata mimi sina sababu ya kukasirika,” alisema Selelii.

Akizungumza mwishoni mwa wiki, Mwakipesile alisema wabunge wanaojifanya kupambana na ufisadi wanatumia njia hiyo kama kichaka cha kuficha ufisadi wao na kusema kwamba mambo mengi ya wanasiasa hao yanafahamika.

Mkuu huyo wa mkoa, alitoa kauli hiyo baada ya waandishi wa habari kuwasilisha hoja ya kutaka kujua sababu za ofisi yake kuwabagua baadhi ya wanahabari katika ziara mbalimbali za maendeleo zinazofanywa na viongozi wa mkoa.

Ingawa Mwakipesile hakuwataja kwa majina wanasiasa hao, lakini kauli zake hizo zilionekana kuwalenga wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao wamekuwa mstari wa mbele kupinga vitendo vya ufisadi vinavyofanywa na baadhi ya vigogo serikalini.

Miongoni mwa wabunge hao ni Dk. Harrison Mwakyembe (Kyela), Lucas Selelii (Nzega), James Lembeli (Kahama) na Fred Mpendazoe (Kishapu), ambao siku za hivi karibuni walifanya ziara katika Jimbo la Nzega na Kishapu, huku wakiwashambulia mafisadi.

Tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu mwaka 2005, Mwakipesile amekuwa katika mgogoro wa kutoelewana na baadhi ya wabunge wa mkoani Mbeya, hususan Dk. Mwakyembe, ambaye alimwangusha katika kinyang’anyiro cha ubunge kwenye Jimbo la Kyela.

Mgogoro huo umedaiwa kukiathiri chama hicho tawala mkoani Mbeya na serikali ya mkoa huo kwa ujumla, ambapo wabunge wakati mwingine wamekuwa wakikataa hata kuhudhuria vikao vya halmashauri kuu ya mkoa, kwa sababu baadhi ya wajumbe ni viongozi wa serikali


Source: Tanzania Daima sept 15

huyu ni mkuu wa mkoa ua mkuu wa ufisadi?
 
Taarifa ninazozipata toka kyela ni kwamba baada ya kushindwa kutekeleza ahadi alizowapa wanakyela mwakyembe ameanza kutapatapa mara mkuu wa mkoa mara mwakalinga na sikia wafuasi wake huko kyela wanatumia nguvu kunyanyasa mtu yeyote wanayedhani anampinga au hamuungi mkoo mwakyembe.mimi niliyembali sina uhakika na hili tuambieni wanakyela ni kweli?
 
RC Mwakipesile azungumzia kujiuzulu

Na Mwandishi wetu NIPASHE
16th September 2009

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, John Mwakipesile ameomba wazee wa jiji la Mbeya kufanya uchunguzi wa ugomvi baina yake na Mbunge wa Kyela wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe na kusisitiza kuwa atajiuzulu iwapo hatotekeleza watakayomuonya iwapo atabainika kuwa ni chanzo.

Mwakipesile alitoa kauli hiyo juzi wakati akizunguza na wazee hao katika mkutano uliofanyika Ukumbi wa Mkapa uliopo Halmashauri ya Jiji la Mbeya kwa ajili ya kuzindua Chama chao cha Akiba na Mikopo (Saccos) ambacho alichangia Sh milioni moja.

Aliwaambia wazee hao ikiwa atabaini yeye ndiye ana makosa wamuonye na asipotekeleza maonyo yao yuko radhi kumwandikia barua Rais Jakaya Kikwete kuomba ajiuzulu.

Alisema wazee hao wanapaswa kubeba jukumu la kumkutanisha yeye RC na Dk. Mwakyembe ili kurudisha hali ya utulivu mkoani hapa na kusaidia kuleta maendeleo ambayo yamekuwa yakiwama kutokana na mgogoro huo.

Kauli hiyo ya Mkuu wa Mkoa imekuja siku moja baada ya wabunge ambao ni wapambanaji wa vita ya ufisadi kumjibu asikurupuke kwa kutoa kauli ambazo hajazifanyia utafiti.

Hivi karibuni wakati wa mkutano wa kujadili mpango wa Kilimo kwanza, Mwakipesile aliwatupia lawama wabunge hao akisemawanatumia ufisadi kama kichaka cha kuficha maovu yao.

Alisema anakerwa na hali ilivyo sasa mkoani hapa na kwamba wakati umefika sasa kwa wazee hao kuingilia kati mgogoro huo ikiwa ni pamoja na kuwakutanisha na mbunge huyo ili wayajadili yaishe.

Mwakipesile alijitetea kuwa kimsingi yeye hana tatizo na Dk. Mwakyembe na kwambva jitihada kadhaa za viongozi wa juu wa chama na serikali wamejaribu kuwasuluhisha bila mafanikio na sasa ni zamu ya wazee kuchukua jukumu hilo.

Mwenyekiti wa wazee hao, Isakwisa Mwambulukutu, kwa niaba ya wazee wenzake walikubali kuifanya kazi hiyo ya usuluhishi.
 
Mwandishi wa Nipashe apigwa

Na Mwandishi wetu NIPASHE
16th September 2009


Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Mbeya, Henry Nguvumali, amemshambulia kwa kipigo kisha kumweka rumande Mwandishi wa Habari wa gazeti hili mkoani hapa, Thobias Mwanakatwe, kwa madai ya kupinga kukamatwa kwa gari walilokuwa wakisafiria waandishi wa habari wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

Mwanakatwe alikamatwa jana majira ya saa 7 :10 mchana katika eneo la Uwanja wa Maonyesho ya Kilimo maarufu kama Nanenane wa John Mwakangale, uliopo barabara kuu ya Iringa – Mbeya.

Tukio hilo lilitokea wakati waandishi hao wa mikoa ya Ruvuma, Iringa, Mbeya na Rukwa wakitoka kwenye mafunzo ya mazingira kwenye msitu wa Ikoho yaliyoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari za Mazingira (JET) katika msitu wa Ikoho.

Baada ya kufika katika maeneo hayo yaliyopo Uyole nje kidogo ya Halmshauri ya Jiji la Mbeya, gari walilokuwa wakisafiria waandishi hao aina ya Toyota Hiace likiendeshwa na Elias Mwampamba, lilikamatwa baada ya kusimamishwa na askari wa kikosi hicho mwenye namba WP 5233.

Baada ya kuhojiwa, walimweleza juu ya ziara yao hiyo na kuwataka kumuonyesha kibali cha Mamlaka ya Usafirishaji Majini na Nchi kavu (Sumatra) kinachowaruhusu kupita njia hiyo.

Katika hali ya kushangaza mkuu huyo ambaye alikuwa ametoa maagizo kwa njia ya simu kwa askari wake, alifika katika eneo hilo kwa daladala na kumtaka dereva wa gari hilo kulipeleka kituoni bila ya kupewa maelezo yoyote . Wakati akitoa maagizo hayo, waandishi wa habari waliteremka na kumweleza bila mafanikio kabla ya kuanza kumpa kipigo Mwanakatwe na kumlazimisha kuingia katika gari la polisi ili afikishwe kituo cha polisi kwa madai ya kuingilia kazi za askari hao.

Waandishi wa habari walipinga vikali gari hilo kukamatwa kwa Mwanakatwe na kupelekwa kituo cha polisi kwa zaidi ya dakika 45 bila mafanikio ndipo mkuu huyo alipiga simu na kuitia gari la polisi lenye namba PT 00675 na kumpakia kwa nguvu mwandishi huyo huku akimpa kipigo. Baada ya kukamatwa Mwanakatwe, waandishi wa habari wakiongozwa na Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya, Nico Mwaibale, waliandamana hadi kituo cha polisi kupinga hatua hiyo.

Akizungumza baada ya kuachiwa kwa dhamana, Mwanakatwe, alisema mkuu huyo amechukua note book yake yenye mambo nyeti.
 
Bado tume ya uchunguzi mpaka sasa haijatangaza ripoti.
Mbeya kazi kwelikweli.
 
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, John Mwakipesile ameomba wazee wa jiji la Mbeya kufanya uchunguzi wa ugomvi baina yake na Mbunge wa Kyela wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe na kusisitiza kuwa atajiuzulu iwapo hatotekeleza watakayomuonya iwapo atabainika kuwa ni chanzo.

Upuuzi mtupu. Give me a break!!
 
Back
Top Bottom