Siku Mwakyembe alipoomba radhi baada kuonekana malalamiko yake dhidi ya mkuu wa mkoa yalikuwa ya uongo.
Bambubile
Habari hii ni ya zamani(mwaka 2007) sana na haina ukweli wowote na ilikanushwa vikali na Mbunge Mwakyembe!
Kuhusu Kyela;Bambubile tuletee habari mpya motomoto sio hizi ambazo hadi Mzee Glasswell Mwakalukwa akiwa bado yupo kundini;Mwakalukwa aliangushwa na Mzee Mwakasumi ktk uchaguzi mgumu uliojaa kila aina ya hila za rushwa, na hivi sasa yupo kijijini kwake Kafundo akilima!
Naama tunataka tuzipate habari za Kyela,lkn sio kama hizi za kale.
Malafyale,
Nilitaka tu kuonyesha kwamba kuna mtu alimuomba msamaha mwingine kwa uzushi.
Bahati nzuri nilikuwa mjumbe kwenye hicho kikao na mheshimiwa aliomba msamaha. Hilo la kwamba alikanusha labda ni kwa nyie wapambe.
Kuna sehemu leo nimesikia mheshimiwa anakanusha kwamba jaribio la kutaka kumwua halikuwepo. Labda kama nimesikia vibaya, kuna waandishi walikuwa wanamhoji, huenda magazeti ya kesho yakaandika. Sitashangaa akiwaruka wale vijana wake, labda yeye anajua upelelezi wamegundua nini.
Anyways,leo nipo kijijini kwetu Ilopa,na week hii nitakuja Kyela mjini hasa pale ninapofikia Baling'onye;njoo pale Bambubile tuje badilishana mawazo hasa kuhusu mustakabali wa Wilaya yetu nzuri-Kyela!
Bambumbile
Pamoja na habari zzko nzuri unazotupa kuhusu Kyela hasa sakata hili la kijana wetu Dan Mwakalinga,lkn bado hamjatueleza lolote kinagaubaga ni vipi Mwakyembe kama Mbunge anahusika na huo utekaji nyara!Tafadhali tupeni ushahidi timilifu iweje Mwakyembe ahusishwe na kitu ambacho yeye binafsi hajafanya!
Maelezo yako na mwenzetu Engineer kuhusu sakata hili iwe kwa faida ya wana JF,mtueleze hasa ni nini kinamuunganisha Mwakyembe na jambo hili hata kufikia kuwa eti nafasi yake ya kushinda ubunge mwakani sasa ni finyu?
Anyways,leo nipo kijijini kwetu Ilopa,na week hii nitakuja Kyela mjini hasa pale ninapofikia Baling'onye;njoo pale Bambubile tuje badilishana mawazo hasa kuhusu mustakabali wa Wilaya yetu nzuri-Kyela!
Nimetimiza ahadi yangu ya jana, kazi kwenu wapambe wa Dr. Mwakyembe
Pole Dr. Mwkyembe, kama habari hii ni kweli basi we huwafai wananchi kabisa. Msomi mzima unafanya kampeni za kitoto, hatari na uonevu mkubwa. No way, you must pay for it.
Tunashukuru sana kwa habari hii nzuri na ya kufundisha Mkuu Engineer,na inatupa picha halisi sisi wana Kyela nini kilitokea ktk Mkutano huo!
Lkn kwenye habari hii kuna sehemu yeyote inayoeleza kuhusika kwa Dr Mwakyembe moja kw amoja na ujasusi huu?
Tupe zaidi maelezo kama yapo,yanayomsukuma Dr Mwakyembe kwenye sakata hili kama mtuhumiwa namba moja!
Malafyale,
Mbona iko wazi sana kwamba Dr. Mwakyembe alihusika? Labda hutaki kuelewa tu.
Alishapiga hata simu kwa IGP kulalamikia kwanini kijana Daniel kaachiwa wakati alitaka kumuua.
Kwa mtu anayemfahamu Dr. Mwakyembe kwa karibu hawezi kushangaa hili. Dr. pamoja na uwezo wake mkubwa pia ana matatizo makubwa sana kwenye baadhi ya maamuzi yake.
Hizo ndio siasa za Kyela; muda wote amekuwa akimlundikia kila aina ya upuzi mkuu wa mkoa. Sasa kahamishia uongo huo huo kwa Mwakalinga. Kitu ambacho ameshindwa kuelewa ni kwamba watu walimchoka Mwakipesile na hivyo uongo wowote wanauchukulia kama ukweli. Mwakalinga hajawafanyia Kyela ubaya wowote, sana sana ana mazuri mengi tu ambayo watu wengi wanamshukuru. Kumuundia scandals Mwakalinga ni lazima ziwe credible vinginevyo ataishia kujichafua mwenyewe.
Huyo kijana asingelikuwa na ndugu wenye uwezo huenda mpaka leo angekuwa bado yuko ndani.
Mheshimiwa Mwawado,
Baada ya ujumbe huu nitaacha kutumia lugha mbaya maana wewe ni katika waungwana na wenye busara kwenye ukumbi huu.
Mtu ukiambiwa uache na wahuni wenzako unaweza kudharau lakini wazee wa maana kama wewe wakisema ni kweli inabidi niache.
Kuhusu somo, hapa tunaelemisha sana watu. Tuna uhakika mwana Kyela wa 2010 atafanya uchaguzi wa maana.
Pia tunasubiri Kyela FM radio ianze, nasikia mwezi kesho ili tuwaelemisha wananchi ipasavyo.
Tatizo ninaloliona ni vurugu kutokea. Kuna watu wa upande mmoja wako tayari hata kutumia mapanga ili kubaki madarakani.
Mwakalinga ni muungwana kama wewe tu. Hata vijana hapa juzi tulitaka kuwashughulikia hawa akina Kilumbu na Kinanasi ambao ndio mwanzo wa hili jungu lakini Mwakalinga akatuonya na kutuomba tusiwaguse wala kuwatukana. Badala yake alitushauri mkondo wa sheria utafanya kazi yake na kwamba yeye atasimamia kuhakikisha haki ya kijana Dan hainyang'anywi. Vijana hawakufurahi lakini tunamheshimu ila itafika siku hata yeye hatutamsikiliza kama wataendeleza hizi siasa zao za chuki.
Baada ya hii vurugu hata CCM wilaya wameamua kuingilia kati na wanaita kikao ili Dr. Mwakyembe athibitishe nani katoa hizo milioni 400 na kampa nani? Hii ya kutunga mauaji kwa kisu imewaamsha wana Kyela wengi kujua ukweli juu ya uropokaji wa mbunge wao.
Mkuu FMES,- Ninaomba kumkumbusha Mkulu Mwakalinga, kwamba wakati ni huu akajitokeza mapema na kuwakataa wapambe wa namna hii, yaani kweli atapata ubunge wa Kyela na this kind of advisers? are you kidding me or what?
- Mwakalinga huyu mtu anakuongezea maadui wabure tu humu ndani, nenda uka-concetrate na jimbo, give JF a break mkuu watu washau kidogo kwanza! ni ushauri wa bure tu!
Respect.
FMEs!
- Ninaomba kumkumbusha Mkulu Mwakalinga, kwamba wakati ni huu akajitokeza mapema na kuwakataa wapambe wa namna hii, yaani kweli atapata ubunge wa Kyela na this kind of advisers? are you kidding me or what?
- Mwakalinga huyu mtu anakuongezea maadui wabure tu humu ndani, nenda uka-concetrate na jimbo, give JF a break mkuu watu washau kidogo kwanza! ni ushauri wa bure tu!
Respect.
FMEs!
Mkuu FMES,
1. Wewe una uzoefu na JF, kweli kuna mtu hapa ana uwezo wa kumkataza mtu mwingine kuandika atakacho?
2. Mimi mwenyewe nimewahi kumkataza engineer hapa na kuna siku anapunguza na siku anaongeza. Naamini hata Mwakalinga kesha fanya hivyo.
QUOTE]
1. Tatizo ninaloliona ni vurugu kutokea. Kuna watu wa upande mmoja wako tayari hata kutumia mapanga ili kubaki madarakani.
2. Mwakalinga ni muungwana kama wewe tu. Hata vijana hapa juzi tulitaka kuwashughulikia hawa akina Kilumbu na Kinanasi ambao ndio mwanzo wa hili jungu lakini Mwakalinga akatuonya na kutuomba tusiwaguse wala kuwatukana.
3. Badala yake alitushauri mkondo wa sheria utafanya kazi yake na kwamba yeye atasimamia kuhakikisha haki ya kijana Dan hainyang'anywi. Vijana hawakufurahi lakini tunamheshimu
.