Dilunga
JF-Expert Member
- Apr 8, 2009
- 679
- 52
nimesoma humu watu wengi wanasema watoto wa darasa la kwanza wanafanyiwa interview, mtoto wa darasa la kwanza hafai kufanyiwa interview this is wrong. kinachotakiwa kufanyika ni kithibitisho tu kama anaweza kuanza darasa la kwanza kutoka kwa walimu wake wa vidudu. nadhani hiyo interview inatumika kama ukiuliza kwa nini mwanangu hajapata nafasi utaambiwa kafeli iterview.
embu fikiria unaambiwa mwanao kafeli interview darasa la kwanza na wengine wamefaulu, eti hana hakili za kujiunga na shule hii???
wazazi wa JF kwa kuwaona watoto wao wana akili kabla hata hawajaanza real shule kiboko..
kuna mtu amesema mwanawe anajua kusoma kabla hajaanza la kwanza...
jamani a e i o u abcd et al sio kujua kusoma.....
ni vigumu sana kujua kama mwanafunzi atakuwaje au anaakili kiasi gani kwa ajili wengine wanachelewa kuonyesha dalili zao.....
mwalimu wa shule ya msingi kazi yake ni kumnoa mtoto na kuhakikisha ananawiri kielimu. madhumuni makubwa ya shule ya msingi ni kuhakikisha mwanafunzi anaweza kuyajua mambo mawili muhimu lugha na hisabati kwa ajili haya ndio mambo ambayo atakumbana nayo katika maisha yake yote. kwa mlio nje mtaelewa jinsi nchi za wenzetu hata form 6 bado wanataka uwe umefanya vizuri kwenye english na hisabati(uk).
kuhusiana na shule bwana max kuna mambo mengi ya kuzingatia wakati unamchagulia shule mwanao.....
1. ufundishaji kama watu wengi humu ndani walivyoongelea
2. mazingira ya shule ilipo ni muhimu sana
3. vitu vilivyopo shuleni je shule ina viwanja vya michezo hichi ni kitu muhimu sana kwa mtoto na watu wengi wanaki overlook. mtoto anapocheza ni vizuri kwa afya yake obesity ni hatari, anaweza akawa na talent nyingine ambayo sio masomo, pia mtoto anakuwa na furaha na hichi ni kitu muhimu ambacho kinamfanya mtoto apende kwenda shule. embu fikiria wewe ukicheza na mtoto wako anapata furaha kiasi gani.
4. tabia za wanafunzi mimi nilipata bahati ya kusoma shule hizi za private (nairobi) nikiwa secondary watoto wengi ambao wazazi wao wanazo huwa wanakuwa na kiburi cha kuzarau kusoma na kudhani kwamba hela kwao zitakuwepo milele. kama mkuu YE hapo juu anvyosema ni wizi wa pesa tu.
5. na kama ulivyosema ni bweni - uangalie menu ya shule ikoje ili kuepusha kuingia gharama za kununua vitu vya kula kula.
6. inabidi na wewe uwe unafatilia progress yake hichi ni kitu muhimu sana
Semilong,
Na mimi nimechoka akili kusikia wazazi wa JF wanashabikia kitoto cha vidudu kufanyiwa "interview" ya kujiunga na darasa la kwanza. Kama unavyosema, wengine wanachelewa kuonyesha uwezo wao. Albert Einstein hakuwa genius darasani. Alifanya dead end jobs kabla ya kutulia na kuja na Nadharia Maalum ya Uwiano. Eti unamfanyia mtoto wa vidudu "interview." "Interview" ya kutathmini kama anajua kusoma na kuandika?
Kuna kitu umesisitiza, Semilong, kuhusu kufuatilia maendeleo ya mtoto. Nilitaka nikwambie tu, usije ukamfundisha mwanao maneno "hichi kitu," "hana hakili," "embu fikiria."
Hiki, akili, hebu.