Shukrani kwa Kikwete

Mimi sipo kati ya wale 1000 walioteuliwa. PIli kwa kukiri kwangu udhaifu ulioko na kuutambua bila kutoa sababu za kijinga kutetea udhaifu, huo ni mwanzo mzuri. Wanasemaga wenyewe kwanza acknowledge there is a problem, and clearly identify what is a problem.

Wala sijafika kuanza kutoa mapendekezo au kutoa solution, tuko kwenye early stage ya self identification and self examnation.

Kama ni hivyo, kwa nini usiwe mmoja kati ya waliochaguliwa, kama Kikwete vile, ili utuwekee hiyo mizani itakayo balance.
 
kazi gani?

kuanguka majukwaani na kupata sababu za kwenda kuzurura hospitali za ulaya na marekani nazo ni kazi?

watu wengine mna mawazo ya k*h*n*t** kweli.

Shule za sekondari kila kata ya Tanzania, zahanati kila kata ya Tanzania, mabarabara mikoa yote kaunganisha na sasa anaanza za wilaya, vyuo vikuu 11 kwa miaka 5, Zanzibar migogoro kwisha, Vibopar wizi wako mahakamani kibao, exemptions za kanisa zote kwisha funga. Jee niendelee na swali lako kazi gani?

Hayo matusi mimi sikujibu kwani wenye matusi hujulikana ni kina nani hapa kwetu Dar.
 
ww una hoja tangu lini? Viroja ndio kazi yako bcoz u have uncircumsized mind. na Viroja havijibiwi & let me tell u seriously hapa JF no one is EVER STUPID, arrogant, idiot as
you are, is not about right of expressions which you deserve.View attachment 19540 is about upuuzi u possess

Hahahaha, mwingine huyo, jazba za nini? Yote kuwa humpendi tu Kikwete?
 
Haya halafu utuwekee pumba zako kama kawaida, lakini angalia wenzako washaanza kukushtukia maana hivi juzi juzi tu niliona wanavyoku kandia! nikasema AlhamduliLllah yale niliyoyaona mimi zamaaani wao ndio kwanza wanayaona!

Wewe Dar es Salaam -mwanakijiji ni great thinker tunamkubali humu ndani na nje ya JF -ni potential figure kwa sauti ya umma. Siyo kibaraka kama wewe harafu eti kibaraka wa makamba.
 
Good food of thought for the beggining of the year Rev. Mambo bado ni magumu sana na uongozi uliopo haata kama hautakubali, ukweli ni kuwa hauna dawa ya kutibu matatizo yaliyopo maana hawana uwezo huo.
 
Wewe Dar es Salaam -mwanakijiji ni great thinker tunamkubali humu ndani na nje ya JF -ni potential figure kwa sauti ya umma. Siyo kibaraka kama wewe harafu eti kibaraka wa makamba.

Great Tinker I agree, Great thinker? No way!
 
Nchi yetu tumeifanya nchi ya wapiga story kuanzia top most mpaka sisi watu wa chini kabisa. Lakin lawama ni kwa jamaa wa juu kupenda mdaraka wakati hawajui wakipewa madaraka watayafanyia nini!
 
Hivyo Mzee Mwinyi alikuwa sahihi kusema sisi ni kichwa cha mwendawazimu au tunaruhusu kunyolewa na mwendawazimu?

Then wale walioko ndani ya CCM kwanini wanaridhika na udhaifu huu? Na tuwaeleweje wakidai eti wanasubiri 2015 ndio walete mapinduzi mapya ndani ya Chama chao ili kulijenga upya Taifa letu kwa umahiri?

Si ndio maana nika kwambia ni pumba! Mwinyi nani CCM nani? sasa fata hii link ukaone mambo ya Kikwete: https://www.jamiiforums.com/busines...ch-mortgage-financing-this-year-official.html
 
Haya halafu utuwekee pumba zako kama kawaida, lakini angalia wenzako washaanza kukushtukia maana hivi juzi juzi tu niliona wanavyoku kandia! nikasema AlhamduliLllah yale niliyoyaona mimi zamaaani wao ndio kwanza wanayaona!

tangu lini watu wanafunga safari kupanda vilima? kama huwezi kulipa gharama ya mabadiliko au misimamo yako usiiweke hadharani ujifungie chumbani tu. So wakandiaji wanakaribishwa - and you know me well to know that I can handle the punches as much as I can give mine. Its part of the same fight.
 
tangu lini watu wanafunga safari kupanda vilima? kama huwezi kulipa gharama ya mabadiliko au misimamo yako usiiweke hadharani ujifungie chumbani tu. So wakandiaji wanakaribishwa - and you know me well to know that I can handle the punches as much as I can give mine. Its part of the same fight.

Kwani usharudi Tanzania to take the punches?
 
Nimekuwa nikijiuliza kwa muda, hivi ni kweli kuwa Tanzania na watu wake wote ambao ni Milioni 39.999.999 tumekubali kwa urahisi kuongozwa na mtu mmoja na kwamba kila linalokwenda mrama ni yeye pekee apokee lawama?

Hata ukiweka mizani ukatusimamisha sisi Milioni 39,999,999 upande mmoja, na yeye upande mwingine, iweje mizani ielemee upande mmoja?

Sasa mwaka 2005, nilijisemea labda zile asilimia 80 zilitokana na Watanzania wenye tumaini, lakini baada ya miaka mitano ya ubangaizaji wa hali ya juu, bado hata kwa kuchakachua tumempa tena nafasi nyingine ya miaka mitano aendeleze libeneke!

Lakini najiuliza, labda nikianza kupunguza kundi la Watanzania kwenye hii mizani na labda tuseme ni Watanzania 1000 ambao ni Wanasiasa kwa mgawanyo wa kuwa Wabunge, Makatibu Wakuu, Mawaziri, Manaibu Waziri, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na Watendaji wengine ambao wameteuliwa kazi na Rais Kikwete. Je hata nanyi mmeshindwa kulazimisha mizani ikaangukia upande wenu?

Hakieleweki kama tutadai Kikwete ni Rais Mvivu, Mzembe, Mbangaizaji, Mfujaji, asiye Makini, asiye Wajibika, asiye Fanisi, asiye Jituma au si Mfuatiliaji na Msimamizi mzuri (angalia matumizi ya makusudi ya herufi kubwa katika hayo maneno) wa kazi hata tukamtuhumu kuwa ni Fisadi, Mla Rushwa na Mhujumu Uchumi, lakini wale walioko chini yake, hata mmoja wao asiwe maridadi na kutupa tumaini na taswira kuwa kuna tumaini.

Nikianzia na mawaziri, wengine wamerudi kwenye Uwaziri na hata wengine kuendelea na wizara zao. Leo sielewi ni vipi bado tunaendelea kuwa na tatizo la Chakula, Umeme, Afya, Maji, Elimu, Mifugo, Uhalifu na Uchumi mbovu na waliopewa majukumu ya kuongoza Taifa na hasa vitengo hivyo bado ni wale wale au wamepewa amjukumu mapya.

Ni kazi gani nzuri mno waliofanya mpaka wakastahili kupewa majukumu haya kwa mara nyingine?

Tuongelee Maji, najua lengo ni kuhakikisha Tanzania nzima ina maji ikifika mwaka 2025. Sasa ikiwa Mkoa wa Dar Es Salaam ambao ndio jiji kubw, bado lina shida kubwa ya maji, iweje tuendelee kuamini kuwa Waziri,naibu waziri na Katibu Mkuu wanafanya kazi nzuri kabisa? je ufanisi wao umefanikiwa vipi kuondoa tatizo la maji Dar? Je ni kweli hawa walioko kwenye hizi nafasi ni watu mahiri na wenye uwezo wa kielimu, tija na ufanisi kufanya kazi yao bila kujali udhaifu wa mwajiri wao? kwa nini basi wao hawang'ai na kutupa Watanzania tumaini kuwa labda ni Rais pekee ambaye hana uwezo wa kuchapa kazi?

Njoo kwenye umeme, huko nako ni vituko, kila siku umeme unakatika katika na tunasaini mikataba mipya kila tukiamka, lakini hata kuhakikisha Dar Es Salaam pekee ina umeme wa kutosha kuendesha viwanda na uzalishaji inakuwa ni vigumu, je tuna mtu mahiri na mwenye uwezo pale Wizara ya Nishati na hata Tanesco?

Turudi kwenye miundo mbinu. Wala hakuna haja ya kwenda nje ya Mbezi Luisi, anzia pale, njoo mpaka huku Bunju, nenda Pugu na kule Mbagala. Msongamano wa magari ni mkubwa, barabara ni finyu na mbovu, hakuna mifereji ya maji machafu, hakuna a, hakuna b, hakuna c na Waziri wa miundo mbinu, pale nje ya jengo la ofisi yake Tancot house, kuna mashimo barabrarani, hakuna miundombinu mizuri na ni kero tupu.

Je ilistahili nini huyu Waziri wa awamu ya nne sehemu ya kwanza kuteuliwa tena kuwa Waziri awamu ya nne sehemu ya pili?

Tuje kwenye masuala ya Uchumi, Waziri wa Fedha, Gavana wa Benki Kuu, Waziri wa Biashara, nao wameshindwa kabisa kulitutumua Taifa letu kiuchumi. Ile kauli yaAri, Kasi na Nguvu mpya imekuwa ni kichekesho huku matumizi yakiongezeka kila siku, thamani ya fedha ikishuka kila sekunde na ubadhirifu wa kodi ni kila nukta. Lakini hakuna hata mmoja wao aliyethubutu kujiwajibisha na kumwambia Rais, kazi hii imenishinda, siwezi kuwapa Watanzania matokeo nbora na kuamsha tumaini jipya.

Tuje Kilimo, Afya, Elimu, Mambo ya Ndani, Utawala Bora, Ardhi, Maliasili, Utumishi, Uwekezaji, TAMISEMI na hata Uwaziri Mkuu, je ni vipi tumerudishiwa watu ambao wameendelea kuonekana ni dhaifu na si fanisi hata chembe?

Haya uje kwenye wilaya, mikoa, Taasisi, Mashirika na hata Balozi zetu, bado matokeo ni yaleyale! Je tutaendelea kudai hii ni kutokana na Kikwete kuwa na Wasifu huo, basi kila aliyepewa jukumu haoni sababu za kujituma kama Bosi hajitumi?

Hata tukija kwenye Chama Tawala, iweje katika mchakato wao walikubali kuendelea kuteua na kuchagua Wagombea ambao i wachapa kazi? Je utamaduni umekolea sana kiasi kwamba leo watuhumiwa wa Uhujumu bado wanapewa nafasi kubwa na ya heshima ndani ya CCM ilhali inajulikana wazi kuwa wameelemewa na tuhuma za Uhujumu na Uzembe wa hali ya juu uliolitia Taifa hasara?

Je hili linaashiria nini kwetu sisi Wananchi? Je nasi tumeamua kuiga tembo midhali Rais wetu ni mdhaifu na mbangaizaji, nasi tunaendeleza libeneke kwa kufuata nyayo?

Sasa atakapoondoka madarakani Kikwete, ndipo tutaamka na kuanza kujituma na kutafuta Rais mpya katika kundi hilohilo la wale ambao wala hawajigusi kujitutumua na kuonyesha matunda ya kweli ay kazi na si porojo na mvuke wa mchemsho ambao hufifia makaa yanapopungua nguvu?

Ninampa Shukrani Kikwete kwa kutuonyesha wazi kuwa pamoja na udhaifu wake, ni wazi hakuna mtu ndani ya kundi lake analoliongoza na hasa Chama chake CCM ambaye mwenye uwezo, utashi na ari ya kuliongoza Taifa letu kuondokana na Umasikini, Ujinga na Maradhi.

Simlaumu Kikwete pekee ingawa yeye ndiye Alpha na Omega wa siasa na Uongozi, lakini wengine wanaojitia wanaweza kuwa Marais wa Tanzania, iweje hatuoni basi matunda bora ya kazi zenu leo hii?

Ina maana mnataka tusubiri mpewe Urais ndipo mtuthibitishie kuwa mna uwezo?

Kikwete alilaghai Watanzania kuwa alikuwa amejiandaa vyema kwa miaka 10 kuwa Rais, matokeo yake ni kuwa hadi leo hii inaelekea bado anajifunza kazi au haelewi nini wajibu wake.

Jee nanyi bado mnajifunza kazi na kubahatishabahatisha?

Haya ni malalamiko au mapendekezo hujaelewaka?

Unategemea kuna siku matatizo yatamalizwa kwenye nchi yeyote?

Kama ni hivyo tusingechagua wa kutoongoza kuyakabili matatizo?
 
nope na the TZ punchers are going to wait a little bit longer while I do my punches..

Wewe hauko kwenye realities (real politics) uko kwenye fantasy JF, Tanzania Daima and the like

Ukija siasa za majukwaani kwetu...you can deliver nothing
 
Na wewe majukumu yako ni pumba na fitna na chuki zisizo maana kwa Rais aliyefanya mengi mema kwa muda mfupi aliokuwepo katika uongozi kuliko ma Rais wote wa awamu zote ukijumlisha. Tutakwenda samba samba!
You keep saying rais aliyefanya mengi. Jana kule kwenye makala ya Maggid nimekuomba unipe mifano ya matatu tu makubwa aliyoyafanya Kikwete ambayo sisi Watanzania tunapaswa kujipiga vifua juu yake. Ukakimya. Umekuja huku badala ya kushambulia hoja unashambulia mtoa hoja. Haya, twende sambamba na utetezi wako wa mafisadi.
 
Rev: Your topic is certainly mind boggling.

Je, tumeweka msukumo mkubwa sana kwenye siasa kiasi cha kuamini na kuishi kwamba wanasiasa wakishindwa ndiyo hivyo tena kama nchi tumeshindwa? Hili swala la watz wengi kuanza kuamini kwamba mafanikio katika maisha hayapatikani kwa bidii isipokuwa kwa ujanja ujanja mnalionaje? Watu wanataka degree za uongo, wanajipachika ma PhD ambayo hawana, vijana wetu wanataka wafaulu hata kama hawakujiandaa kwa kusoma, wanatafuta mitihani ya kuiba badala ya kujisomea, mtu anagombea umeya huku akijia hawezi, anaongoza kwa ujanja ujanja,n.k. Je, falsafa kwamba viongozi ni kiwakilishi cha jamii husika ina-apply pia kwetu? Kwamba walivyo viongozi wetu kimsingi ndivyo na sisi wananchi wao tulivyo-kwamba tu wavivu, wapiga tanuri, wapenda maneno na misen'enyo, wababaishaji, mediocre, tunapiga vita watu wanaofanya kazi kwa bidii na wanaopenda unyoofu, tunawachukia wale wanaofuata taratibu na haki, n.k, ndivyo tulivyo kweli? Na kama ndivyo, je tunaweza kubadilika tukitaka? Na je, tuanze sisi kubadilika au tubadilishe kwanza viongozi?
 
Wote hao unaosema hawafanyi kazi vizuri wameteuliwa na rais mwenyewe. Hakuna kinachomzuia kuwafukuza na kuteua wengine. Kwa maneno mengine, ,mambo yakienda kombo wa kumlaumu ni rais mwenyewe. Hakuna mwingine zaidi. Mawaziri, makatibu wakuu, wakurugenzi na vyeo vingi sana wote wanateuliwa na rais na ndiye mwenye uwezo wa kuwaondoa kutoka kwenye nafasi hizo. Sisi wananchi wa kawaida hatuna amri wala hatuwezi kudiriki kuwaondoa. Sasa kwa nini tusimlaumu jk kwa madudu yanayoendelea hapa nchini??? Kumtetea jk ni propaganda tu. Hata wanaomtetea ukiingia mioyoni mwao utatambua kwamba nao wanaujua ukweli.
 
Rev: Your topic is certainly mind boggling.

Je, tumeweka msukumo mkubwa sana kwenye siasa kiasi cha kuamini na kuishi kwamba wanasiasa wakishindwa ndiyo hivyo tena kama nchi tumeshindwa? Hili swala la watz wengi kuanza kuamini kwamba mafanikio katika maisha hayapatikani kwa bidii isipokuwa kwa ujanja ujanja mnalionaje? Watu wanataka degree za uongo, wanajipachika ma PhD ambayo hawana, vijana wetu wanataka wafaulu hata kama hawakujiandaa kwa kusoma, wanatafuta mitihani ya kuiba badala ya kujisomea, mtu anagombea umeya huku akijia hawezi, anaongoza kwa ujanja ujanja,n.k. Je, falsafa kwamba viongozi ni kiwakilishi cha jamii husika ina-apply pia kwetu? Kwamba walivyo viongozi wetu kimsingi ndivyo na sisi wananchi wao tulivyo-kwamba tu wavivu, wapiga tanuri, wapenda maneno na misen'enyo, wababaishaji, mediocre, tunapiga vita watu wanaofanya kazi kwa bidii na wanaopenda unyoofu, tunawachukia wale wanaofuata taratibu na haki, n.k, ndivyo tulivyo kweli? Na kama ndivyo, je tunaweza kubadilika tukitaka? Na je, tuanze sisi kubadilika au tubadilishe kwanza viongozi?

Kitila,

It is frustrating kuona kuwa yani kila kona tunachechemea! Ukiangalia mfano wa BoT na Hazina, hawa jamaa wawili Mkulo na Ndulu wameshindwa kabisa kubadilisha dira ya Taifa ya uchumi. Mkulo haishi kushangilia misaada na kutamba kuhusu kusambaza bakuli, huku Ndulu anashindwa kutumia maarifa yake kumwambia bosi wake "funga mkanda, punguza matumizi, punguza ukubwa wa Serikali" na alichokifanya cha maana ni kila miezi mitatu kutoa takwimu bubu na sasa katuchaopishia noti mpya ambazo zimeshaibiwa kabla hata hazijawekwa kwenye mzunguko!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom