mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,076
- 4,113
Shirika la ndege la taifa la Israel El Al litaacha kutoa safari za ndege kwenda Afrika Kusini kuanzia mwisho wa Machi, shirika hilo la ndege lilisema Ijumaa, likitaja kupungua kwa mahitaji ya wateja.
“Kutokana na hali ya usalama ilivyo sasa, kumekuwa na upungufu mkubwa wa mahitaji ya wasafiri wa Israel wanaokwenda maeneo mbalimbali, ikiwemo Johannesburg nchini Afrika Kusini,”El Al ilisema katika taarifa yake.
"Kwa kuzingatia hili, kuanzia mwishoni mwa Machi 2024, tutasimamisha shughuli kwenye njia ya Johannesburg-Tel Aviv."
Tangazo hilo linakuja muda mfupi kabla ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) kutoa uamuzi wa awali kuhusu iwapo itaiamuru Israel kusitisha operesheni zake za kijeshi huko Gaza.
Kesi hiyo katika mahakama ya ICJ ni sehemu ya kesi iliyoletwa na Afrika Kusini, ikiishutumu Israel kwa kufanya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina.
Israel inakanusha vikali shtaka hilo.
Afrika Kusini imekuwa muungaji mkono mkubwa wa Wapalestina katika mzozo unaoendelea, na kusababisha mvutano na Israel.
Chanzo: BBC
“Kutokana na hali ya usalama ilivyo sasa, kumekuwa na upungufu mkubwa wa mahitaji ya wasafiri wa Israel wanaokwenda maeneo mbalimbali, ikiwemo Johannesburg nchini Afrika Kusini,”El Al ilisema katika taarifa yake.
"Kwa kuzingatia hili, kuanzia mwishoni mwa Machi 2024, tutasimamisha shughuli kwenye njia ya Johannesburg-Tel Aviv."
Tangazo hilo linakuja muda mfupi kabla ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) kutoa uamuzi wa awali kuhusu iwapo itaiamuru Israel kusitisha operesheni zake za kijeshi huko Gaza.
Kesi hiyo katika mahakama ya ICJ ni sehemu ya kesi iliyoletwa na Afrika Kusini, ikiishutumu Israel kwa kufanya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina.
Israel inakanusha vikali shtaka hilo.
Afrika Kusini imekuwa muungaji mkono mkubwa wa Wapalestina katika mzozo unaoendelea, na kusababisha mvutano na Israel.
Chanzo: BBC