Sheikh Ponda akamatwa Dar!

Sheikh Ponda akamatwa Dar!

Tunachoshuhudia leo ni mavuno; mavuno ya miiba iliyoachwa iote, ichanue na kuzaa miiba mingine. Kukamata viongozi wa Kiislamu hakutatui tatizo la msingi lililopo - udini. Watawala hawa ndio wameupandikiza udini, kuupalilia na kuumwagilia maji kila wakipata nafasi. Leo yule mwanasimba waliyemlea na kumtendea kama paka nyumbani amekua na anaunguruma. Simba si paka na ukicheza naye hata kama ulimfuga anaweza kukugeuka na kukutafuna!

Utawala wa CCM umelea udini kwa kila namna; uchaguzi wa 2010 uligubikwa na udini uliokithiri - na ukavumiliwa, kauli za uchochezi wa kidini zimeendelea kutolewa na kuvumiliwa katika vyombo mbalimbali vya habari na zikichochea matukio ya visasi na kwa kufanya hivyo kuwageuza watu wasio na msimamo mkali wa kidini kuanza kuwa na msimamo huo.

Sasa leo chuki hii ya kidini ilikuwa inahitaji cheche tu kidogo kuweza kuiwasha kwani mafuta yake haramu yalikuwa tayari yametapakaa. Wamarekani wanasema "the chickens have come home to roost"! Wamepanda sasa wanavuna halafu wanakunja uso!!?
 
Jmushi1, nimeandika haya baada ya kuwasoma wachangiaji walokuwa wakitukana matusi mazito na kutangaza vita. Sikuanzisha mimi hoja au mada hii. Kosa langu ni kuuliza Sheikh Ponda amefanya kosa gani? watu wanataka niamini kwamba anahusika na mauaji ya Mbagala jambo ambalo halikuwepo hapa kijiweni isipokuwa maswala ya Redio Iman.

Nachojua mimi hii ni redio ya mtu ambaye kaisajili kwa kutumia jumuiya wa Waislaam huko Mrogoro. Hawa huenda na kurecord watu mbali mbali nchini ikiwa ni pamoja na huy Sheikh Ponda ktk propaganda zao za Kidini ambazo wananchi wameikemea serikali kwa muda mrefu lakini hadi leo ina operate..

Ponda sii mwanahisa wala mmiliki wa hiyo redio isipokuwa hawa jamaa hurekodi speach zake ambazo kusema kweli binafsi yangu sijazisikia isipokuwa moja inayohusu kuipinga serikali ktk swala la sensa, maswala ya MoU na hata NECTA ambayo kwa madai yake inatakiwa seirkali iyafanyie uchunguzi..I would..Kama mnayo hotuba yoyote ya Ponda inayoukashifu Ukristu ningeomba sana mniwekee ili nami nimjue huyu Sheikh ni mtu wa aina gani lakini anapotetea maslahi ya waislaam sioni tatizo ndio kazi yake aloapa kuifanya kama navyowasikia Mbowe, Dr.Slaa kuwatetea wananchi na Chadema, Wenyeviti wa Union iwe madaktari, walimu, watumishi wa serikali au Jumuiya ya Wanawake na watoto nchini wakilalamikia serikali. Hawa wote kama hukubaliani nao utawaona wanasababisha vurugu nchini..

Nitasema tena Wadanganyika mnapenda sana kuuchonga na kutangaza vita lakini hamuwezi vita na wala sii jambo la kuombea. Diplomacy inawezekana na tusiwe na jazba tuzungumze vitu kwa kituo tupate kujua kitu gani kinafanyika. Narudia tena kuuliza Ponda amefanya kosa gani? nambie halafu tutaendelea na mjadala..
Unaposema watanganyika hatuwezi vita una maana gani?Hawaviwezi vita dhidi ya nani?Waislam?Ni waislam ndo wenye kuweza vita?Naomba uwe specific hapo.

Kuhusu Ponda,hata wewe unamtetea bila kujuwa kwamba ni mashtaka gani atakayofunguliwa na kuona ushahidi utakaotolewa dhidi yake ndipo ujuwe kama kaonewa ama vipi.

Haya maneno ya wana JF humu haina maana kwamba wanafahamu ushahidi utakaotolewa na waendesha mashtaka,haya ni mambo ya hisia tu,hisia ambazo hata zimesababishwa na ukweli kwamba kuna chuki za kidini zinazosambazwa na vyombo hivyo vya habari,na ndiyo maana chuki inazidi kuenea.

Kama wewe ni muumini wa kusema kuna mfumo kristo,hilo tayari ni kupandikiza chuki.Kumbuka wakati wa sensa,chadema walizuiwa kufanya mkutano na hata ikasababisha kuuwawa kwa Mwangosi,lakini serikali ilifumbia macho waliowakataza waumini wao wasihesabiwe.

Sasa jiulize hapo kuhusu double standard.Nani mwenye kukwamisha zoezi la sensa hapo?mwenye kufanya mkutano ama mwenye kusema wakatae kuhesabiwa?

Narudia tena mkuu pia kwamba msichanganye dini na siasa,kwasababu unatolea mifano ya wanasiasa na kulinganisha na hayo ya Ponda kwa kudai ni haki za waislam,sasa ina maana hao kina Slaa na Mbowe wanapigania haki za "chadema wakristo"?si unaona ulivyokuwa twisted kwenye hiyo hoja?

Kama ni hivyo,basi si waislam muanzishe chama cha kiislam cha kisiasa kama bado hakipo?Kwasababu kamwe usidhani kuwa chama cha kisiasa kikijiingiza kwenye kuitetea imani moja ya dini basi kutakuwepo na usalama nchini mwetu.

Pia kwa kumalizia,sidhani hata kama hatua ya kumkamata Ponda inalengo la kutenda haki yoyote,kwasababu chini ya serikali hii,hilo ni msamiati.Serikali ingekuwa na nia ya kudhibiti uhuni huu,ingefanya hivyo toka kitambo sana.

Badala yake nadhani serikali ndiyo yenye nia mbaya kwenye hili.Subiri tuone mashtaka watakayomfungulia ndo utakuja kuniambia.Hakuna hata siku moja rais huyu tuliyenaye ameonyesha kuupinga udini.Na hili la kukamatwa pengine ni shinikizo flani,siwezi kujuwa limetoka wapi,lakini nina uhakika siyo hatua ambayo inaonyesha honesty ya rais kwenye kushughulikia hizi issue.

Na nilishawahi kuanzisha thread yenye kuelezea udini wa JK,lakini imefungwa kimyakimya,tena wakati watu wakiwa hawaichangii tena.Ukweli ni kwamba udini umeoteshwa,kupaliliwa na kukuzwa na serikali ya JK chini ya amiri jeshi mkuu mwenyewe!Hauhitaji kuwa akili ya astronaut kuona hilo.
Pengine kuna ushahidi ambao ni overwhelming,na ameshindwa kuifumbia issue hii macho.Kama unasema hujawahi kusikiliza hotuba za Ponda,basi usi conclude kwamba hajawahi kuziponda imani za wengine.
 
jana alikuwa anamlaumu kikwete kwanini ameenda kuangalia makanisa yaliyoharibiwa na kuacha msikiti uliovamiwa na polis. amesahau kwamba wale wez walikimbilia msikitin kujificha

Inawezekana amekamatwa kwasababu tu amemlaumu Kikwete na si nje ya hapo. Nyie subirini muone mwisho wa hii movie.
 
watamwachia
hana kosa ni yale yale ya Sheikh wetu Kassim bin Jumaa alikamatwa kwa shinikizo la kanisa
hatimaye mrema alimkamata na kumuua kwa sumu
waislam hawatakubali amani wao ndio waliitunza
wao ndio wamewwekwa nyuma katika kila sekta ya nchii hii
ni wao viongozi wao wanaposema na kuiomba serikali hata kwa jambo la msingi basi hawasikilizwi
ni wao viongozi wao wanapo takiwa police kutoa ushahidi huburuzwa kama majambazi ilhali mapadri polise huenda wao makanisani kuwahoji
madhali haki haipo, basi sasa ni wakati wake kuweka sawa mambo
waislam wamestahamili sana dhulam hawamo serikalini . wafanyakazi zaidi ya 90% ni wakristro
jeshi 90% ni wakristo
polisi 90% ni wakristo
bunge 90% ni wakristo
necta yote wakristo ambao kazi yao kubwa ni kuwafelisha watoto wa liislam
nchi kweli imeshaharibika
uonevu na dhulma ukivuka mpaka wananchi hawaogopi dola
lazima heshima ipatikane na Ponda watamtoa ama waislam watamtoa hii ni lazima
yaliyo tokea mbagala hayamhusu ponda
polisi wanafata maelekezo ya mapadri...na hawa mapadri kuwakumbusha tu ndio walio wachoma wahutu na watusi kule burundi na rwanda baaadae wakakimbia vatican na ulaya
kwa hiyo sio ponda wala waislam watakao haribu nchi hii
nchi hii tayari imeshaharibiwa na mapadri wanaondekeza uchoyo, dhulma na wizi kwani wao hawajali wana passport mbili..
wacheni kuchochea moto waislam hawana cha kupoteza
 
Sasa isiwe akamatwe kwa sababu wameamua kumtoa kafara; Ponda hajaanza leo kusema anayoyasema. Kama muda wote (miaka yote) wameweza kumvumilia imekuwaje leo waamke na kusema wanamkamata?

Kama kosa ni yale ya Mbagala au anayoyasema ukweli ni kuwa itakuwa ni kumuonea! Kosa ni la serikali inayotawala. Ukiacha mlango wazi kwenye zizi kila sikuw watu wanakuambia chui ataingia na kula mbuzi nawe ukapuuzia siku chui akiingia na kula utalaumu zizi kwanini halikufungwa?

inawezekana kama Thomaso, walitaka kujiridhisha kama kuna chui, hivyo kondoo wakafanywa kafara kuthibitisha kama yupo ama la.....madhara yake ni kama haya; ni lazima kondoo kadhaa watolewe kafara
 
Waislam kama wanaamini kuwa wanaonewa au wanatengwa katika maendeleo, wana haki ya kuilalamikia serikali na hata kuishinikiza lakini wanafanya kosa kubwa sana kuyashambulia makanisa na wakristo maana makanisa au wakristo hawahusiki na chochote katika uendeshaji wa serikali wala migawanyo ya rasilimali. Waislam kupeleka malalamiko yao serikalini kama kundi mojawapo la jamii yetu, haijalishi malalamiko yao kama yatakuwa ya kweli au ya uwongo siyo kosa. Ni jukumu la serikali kuyajibu na kuyafanyia kazi.

Lakini ikumbukwe kuwa kama waislam wanajiona kuwa ni kundi lililoachwa nyuma kimaendeleo kwa sababu zozote zile, wana haki ya kuiomba serikali iwape upendeleo maalum ili ifikie wakati ambao jamii yetu yote inaweza kwenda pamoja. Kwa bahati mbaya sana Waislam wamekosa uongozi wenye hekima, unaoweza kuwaongoza katika kuondoka mahali walipo na kuyafikia matarajio yao. Kwa haya yanayofanyika sasa, wale wanaojiita viongozi wa waislam wenye msimamo mkali hawawezi kumsaidia mtu yeyote, awe muislam au siyo muislam.

Tanzania ili iweze kusonga mbele inahitaji ushirikiano wa hali ya juu kati ya makundi mbalimbali ya jamii yetu. Ilikuwa rahisi sana enzi za mwalimu kutaifisha shule za Wakristo ili watanzania wote wasome kwa sababu ya mshikamano na upendo uliokuwepo kati ya wakristo na waislam. Lakini kwa hali inayojengwa sasa, sidhani kama hilo linaweza kutokea. Hata kuitoa mali ya serikali na kulipatia kundi moja la dini, ni lazima italeta chokochoko kubwa.h

Adui yetu CCM amefanikiwa. Mwaka 2010 aliegemea sana kwenye kampeni za udini. Alipoenda sehemu yenye wakristo wengi alisema wasiichague CUF kwa kuwa ni chama cha kidini, alipoenda sehemu yenye waislam wengi alisema wasiichague CDM kwa kuwa ni ya wakristo. Leo polisi wakiwasulubu waislam wakristo watafurahia na kuona kuwa sasa serikali inafanya kazi, na siku waislam wakichoma makanisa na serikali isichukue hatua zozote dhidi yao wanaona serikali inawapenda waislam. CCM inafurahia, maana katika kila hali ina watu wanaoiunga mkono.

Waislam na Wakristo, jikomboeni kutoka kwenye utumwa wa fikra. Shikamaneni, mwunganishe nguvu, muikabili CCM na serikali yake, na kisha mtengeneze mfumo rafiki unaozingatia namna bora ya kuijenga Tanzania yenye uwiano mzuri wa maendeleo. Haitawasaidia wakristo wala wapagani kuona jamii fulani ipo nyuma kimaendeleo, lakini hili haliwezi kutokea kama hakuna upendo wa kweli miongoni mwetu. HII NI RAI.


awawezi
Huna sababu yoyote ya kunitukana miye nmeuliza Sheikh Ponda amekamatwa kwa sababu gani?.. Hivi wewe umeona taabu gani kunambia anahusika na mauaji ya Mbagala? nimesema mimi nsijui sababu na ningeomab nielezwe tayari mnaona ni mshabiki kwa sababu tu mnajua Mkandara ni Muslaam. Ningekuwa nauliza kukamatwa kwa Dr.Slaa msingeyasema yote haya. Na kama ungesema unachokifahamu wewe kuhusu kukamatwa kwake ungepoteza nini? au unajua fika hujui sababu isipokuwa unajaribu kuaminisha watu hapa JF kuwa Sheikh Ponda anahusika na mauaji ya Mbagala? Ni swali dogo sana niliuliza niitaka nijue maana tayari nyie mmeisha anza kufanya kampeni za Kidini kuwafanya watu waamini jambo ambalo hamlijui wala hamna Uhakika.
 
Sasa isiwe akamatwe kwa sababu wameamua kumtoa kafara; Ponda hajaanza leo kusema anayoyasema. Kama muda wote (miaka yote) wameweza kumvumilia imekuwaje leo waamke na kusema wanamkamata?

Kama kosa ni yale ya Mbagala au anayoyasema ukweli ni kuwa itakuwa ni kumuonea! Kosa ni la serikali inayotawala. Ukiacha mlango wazi kwenye zizi kila sikuw watu wanakuambia chui ataingia na kula mbuzi nawe ukapuuzia siku chui akiingia na kula utalaumu zizi kwanini halikufungwa?

Mkuu,
kuvunja sheria hakusameheki.Ukivunja sheria usipokamatwa mara ya kwanza, au ukapewa onyo kama alivyokuwa anapewa maonyo huyu bwana haikupi hakikisho la kuendelea na uhalifu.Tuachie vyombo husika vifanye kazi yake.

Hili suala la UDINI ndio limeanza KUONEKANA NI "REAL PROBLEM". Wamechezea moto siku zote, sasa wataungua wajifunze kua moto unaunguza. Kwa muda mrefu watu kama hawa wamekuwa wanafanya vitendo vya uhalifu bila kuogopa maana ilijengeka dhana kuwa " WANAPENDELEWA AU KUOGOPWA".Wacha dola itunishe misuli sasa.
 
Makafiri mmefurahi kwa Sheikh Ponda kukamatwa, na mnalilia radio ya waislam(ifungwa). Kama kuna kosa amelifanya basi apelekwe mahakamani, asomewe mashatka yake kwa mujibu wa sheria za nchi, kama makosa yake ni ya kupewa dhamana lazima apewe dhamana! Huo ndo utawala washeria.

LAKINI kama ni makosa ya uchochezi basi wasiishie hapo tu, wamkamate haraka sana PADRI SLAA, kwani yeye ndo mchochezi namba moja, amesikika wazi wazi akisema nchi haitatawalika na amekuwa akitekeleza kwa vitendo, fujo na mauwaji. N akama ni kufungia radio Imaan, basi waanze na gazeti la Tanzania Daima na gazeti la Wakati,wasiishie hapo na waifungie haraka sana JAMIIFORUMS,kwani wajumbe wake wengi wamekuwa wakihubiri chuki dhidi ya watawala na kupandikiza uhasama hasa wakidini bila ya kuchukuliwa kwa hatua zozote na waratibu wa mtandao huu.
 
Hebu chekeni kidogo, naona mmenuna! Natamani kuwaona PINDA NA ANNA MAKINDA wanazaa, sijui mtoto afanane na nani kwenye unafuu, kwi kwi kwi kwi! Jioni njema!
 
Hapa ndipo mnapokosea sana wakristu kwa sababu wepesi sana kutukana matusi mazito mazito dini ....

Mkuu wangu Mkandara, hapo penye red naona umekosea sana. Kuna waislamu tena nawafahamu kabisa wanaompinga Ponda kwaajili ya tabia yake yakutumia jazba pasipo kufikiri. Nafikiri ni Ponda huyu huyu ambaye anahamasisha wafuasi wake wamkatae yule Sheikh wa Bakwata kwasababu anahubiri umoja/amani pamoja na sababu nyingine nyingi. Si kila muislamu anafurahia purukushani za huyu Ponda. Ukiwa mtu wakutafuta maugomvi kila siku ni lazima jamii yeyote iliyostaharabika ianze ku-question ajenda zako. Watu kwenye jamii iliyostaharabika huwa wanatafuta kuwa part of the solution ya tatizo lolote linalotokea na sio part of the problem? Sasa huyu Ponda naona kwenye huu umoja wetu ni part of the problem (just a personal thought).
 
Sawa kabisa, huwezi kujibu ujinga kwa ujinga. ikiwa mtoto kukojolea kurani ni dhambi mbaya kwani nini kuchanachana Biblia, kuchoma makanisa, kuahribu mali za kanisa na hata kusababisha uporaji wa mali za kanisa iwe sawa. Mtoto akililia wembe mpe. Kamanda Kova pull up your socks maana umechelewa. Namwomba rais hili asilifumbie macho maana kwa mwendo huu nchi inaenda pabaya.
Nasema tena, binafsi nasikitikia kwa kitendo cha yule mtoto kukjolea Kurani, lakini huwezi kulipa ujinga kwa ujinga. nampongeza sheikh mkuu wa Dar es salaam. Nasaha zake sahihi kabisa na Mungu amzidishie hekima na busara.
 
makafiri mmefurahi kwa sheikh ponda kukamatwa, na mnalilia radio ya waislam(ifungwa). Kama kuna kosa amelifanya basi apelekwe mahakamani, asomewe mashatka yake kwa mujibu wa sheria za nchi, kama makosa yake ni ya kupewa dhamana lazima apewe dhamana! Huo ndo utawala washeria.

Lakini kama ni makosa ya uchochezi basi wasiishie hapo tu, wamkamate haraka sana padri slaa, kwani yeye ndo mchochezi namba moja, amesikika wazi wazi akisema nchi haitatawalika na amekuwa akitekeleza kwa vitendo, fujo na mauwaji. N akama ni kufungia radio imaan, basi waanze na gazeti la tanzania daima na gazeti la wakati,wasiishie hapo na waifungie haraka sana jamiiforums,kwani wajumbe wake wengi wamekuwa wakihubiri chuki dhidi ya watawala na kupandikiza uhasama hasa wakidini bila ya kuchukuliwa kwa hatua zozote na waratibu wa mtandao huu.
kwi kwi kwi! Kwanza koma kutuita makafiri! Halafu jamii forums ikifungwa, jua hiyo ndiyo siku mwezi na jua vitakapoungana! Nendeni shule, nyie na vizazi vyenu, hamna ufikiri wala uthubutu lakini ni mabingwa wa kulalama! Shame on u pipo! Tusisitize upendo! Punguzeni kula urojo, kucheza bao, kuoa wake wengi na kuzaa watoto wengi wakati hamna uwezo wa kuwalea. Mwisho wanaishia kuwa watoto wa mitaani. Hebu tuirudishe tanzania ya zamani iliyokuwa na amani na upendo.
 
Nimefuatilia sana nimegundua Mkandara nae mdini mkubwa! Hivi ni mkandara yupi huyu?yule wa chuo kikuu cha DSM?
 
jini tumekaa nalo, limezaa watoto..watoto nao wamezaa wajukuu ..wajukuu nao wamezaa halafu leo eti ndo mnatambua kuwa jini hili linatakiwa kuondolewa?!!!!
 
Bablii hebu tulia na upate muda wa kufikiri zaidi, weye mwenyewe watumia JF, kisha wapendekeza ifungwe. Wewe vipi bwana?
 
Eti HAWATA MTOA MENO NA KOLEO KWELI..!? AKIFANYIWA HIVYO ATAHUBIRI PEACE & LOVE until the END... wallah....!!!
 
Back
Top Bottom