Share nasi matukio yako ya ukuaji

Share nasi matukio yako ya ukuaji

Ilikuwa mkesha wa mwaka mpya nipo na kaka yangu mtoto wa baba mkubwa wangu, mama akaenda kanisani usiku akasema fungenu mlango msitoke nje basi tukatukia ndani.

Kufika mishale ya saa 3 hivi zikapita ngoma balaa enzi hizo mikesha ina vibe ni ngoma za madumu na nyimbo si tukashwishika kaifwata. Tukazunguka na ngoma hadi saa 6 usiku kaka yangu akakutana na washikaji wake akaniacha na ngoma matokeo yake ngoma ikaisha watu wananza kurudi makwao najikuta nipo mtaa wa mbali kishenzi na home halafu kufika nyumbani lazima nipite msitu mkubwa wenye makaburi na ilisemekana kuna majini.

Nilileta kisa hiki mkesha wa mwaka mpya mwaka jana

 
Mkuu na wewe ulikaa seed farm pale igowole kwa mwalimu kauta aloooo wewe ni chuma kama mimi. Pia nimepita pale.

Kauta hoyee .. alinikimbiza na mlinzi nilitoroka kwenda kuiba mapindigesi
 
1. Kumtukana mwalimu Mbando kumbe alikuwa nyuma yangu sikumuona. Nikiwa shule ya Msingi kulikuwa na Mwalimu mmoja mkali na anachapa sana alikuwa anaitwa :Mbando". Sasa siku moja nikiwa na wenzake nikawa namtukana kuwa Mwalimu "Mbando ni Mpumbavu" sana kumbe alikuwa anakuja na yupo nyuma yangu. Wenzangu wala hawakunishtua. Hahaaaaaa, nilipigwa sana siku hiyo na nikaambiwa nije na wazazi shuleni.

2. Nimeanza Msingi 1991. Kulikuwa na Mwalimu mmoja anaitwa Mwalimu "Shilla" alikuwa mkali sana. Akanipiga kibao kwani nilikuwa napiga Kelele. Hahaaaaa nikatoka nje na kuokota mawe na kuanza kupiga juu ya bati la shule kwa hasira. Hapo ndipo niliacha shule rasmi. Mwaka 1992 nikaenda tena shule. Nikamkuta yule yule Mwalimu Shilla ndio mwalimu wa Darasa la kwanza. Akanifukuza nikaanza kumlilia na kuomba msamaha. Akajua sasa nimekuwa akaniruhusu kuanza rasmi darasa la kwanza.

3. Simu 1 na wenzangu tumetafuta yale matunda ya minyonyo. Tukachukua zile mbegu zake na kuzikaanga kwani tulisikia yanatoa mafuta ukiyakaanga. Tukawa tunayale yale mambengu pamoja na mafuta yake yaliyokuwa yaanza kutoka kwa kuyakaanfa kwenye moto. Sitasahau jinsi tulivyotapika siku ile.
 
Daaah nimekumbuka mbali sana. Enzi ya asante Mkapa, RIP Big Benji, nikiwa darasa la pili nilikua napenda sana kwenda vibanda umiza vile vilikuwa vinaonyesha movies. Sasa ratiba ilikua hivi asubuhi mpaka sa6 mchana ni picha za kihindi huwa ni ndefu hivyo huwa mbili tu, sa7 picha za kibongo hadi sa10 au kizungu inategemea, sa10 hadi sa1 usiku ya kihindi ya kumalizia siku. Baada ya hapo watu hutawanyika lakini kwenye ule ubao wa kuwekea makava ya muvi nilikua nasoma kwa chini kila siku wanaandika leo usiku kutakuwa na pilau. Sasa nafikiri ni curiosity na utoto wa kutojua pilau ni nini? Siku moja nikasema leo siondoki, baada ya picha ya kihindi ya jioni kuisha nitasubiri mpaka na mimi leo nile hilo pilau nikidhani ni msosi. Sasa binamu zangu ambao tulikuwa na umri sawa wakati wanaondoka bandani baada ya picha ya kihindi nikawa nawashawishi tubaki wote tule pilau wakasema watoto hawaruhusiwi sikukata tamaa, nyuma ya lile banda kuna matobo yalikuwepo ambayo unaweza kuona ndani, nikasema nitajibanza kwa nyuma ya banda hadi mda wa pilau ufike wakipakua nitaenda na hakuna atakayenifukuza(masikini ningejua ningeondoka na binamu zangu).
Basi muda ukafika nikastaajabu kuona wake kwa waume, wababa kwa wamama, na mabraza na masista du wa mtaani wanaingia bandani, hapo ishafika saa4 usiku, laahula VHS ikafunguliwa wakatia mkanda wa tofali daaah nilichokiona (ilikua siku yangu ya kwanza kucheki porno) na kwa kuwa nilikua nachungulia toka nyuma ya banda nikawa naona na wale waliokaa nyuma walichokuwa wanafanya ni laana.
Sasa bana msala ulianza pale lile zoezi la pilau lilipoisha nisijue ishakua sa6 usiku na nimeshatafutwa kinyama bila mafanikio, na binamu zangu walipoulizwa wakasema nilikua nasubiri pilau, wewe sikia tu kama sikuzimia siku hii kutokana na kipigo sitazimia tena mshua alinidunda kama anaua nyoka.
Sasa nilipokua naulizwa umekula wapi pilau? Mimi kimya. Hapa nyumbani hauli? Mimi kimya. Mama anadakia huyo jeuri unaona hajibu, asijue ni mambo ya ajabu nimetoka kutazama nashindwa hata kuyaelezea. Siwezi sahau hii siku asubuhi nilipelekwa hospitali baada ya kupata homa kali na vijipu sababu ya kipigo.
Naona Leejay49 amelike pilau...🤣🤣 Itakuwa anapenda pilau huyu lee
 
Niaje wadau

Leo nlipata muda wa kuzunguka zunguka town, nimekutana na Mwalimu mmoja alinifundisha shule ya msingi, amefanya nikumbuke baadhi ya matukio mengi sana ya nyuma.

1. Kipindi niko shule ya msingi baada ya kusoma nkawa naenda polini kutafuta maembe afu nnauza
Nikiuza ile hela ni kununua alizeti na gropu za tochi. Kwahyo ile asubuhi wenzangu wanavyoingia darasani mimi nazama porini, ikifika saa 4 muda wa mapumziko naenda kununua VITU, hapo mimi ndio boss.

Sasa siku moja nikawanyima jamaa zangu alizeti wakachukia na kwenda kumpa taarifa baba kuwa Nahman hasomi anauza maembe! Aloo nlikula kichapo ile siku sitokaa nisahau!

2. Kipindi cha balehe kimekolea pale, nikategea wazazi hawapo na mpangaji mmoja ameshaenda kazini nkaita pisi moja nyumba ya pili ije kule chumbani kwetu. Mtoto akaja na kanga na kachupi tu, ile nmeanza manjonjo nikasikia geti linesukumwa la nje!

Si nkatoka ile haraka nkakutana na mama! Akauliza mbona umetoka haraka au unachezea umeme (nilikua napenda kujaribu jaribu vitu) nikajibu hapana. Akasema wee ngoja nije, akaingia chumbani me nmebaki nje nasikilizia bomu linaloripuka.

Nakuta kaingia katoka kaenda zake ndani kuchukua alivyosahau then akaenda zake. Sasa kuingia kule ndani na mimi simuoni J. Kumbe aliingia kwenye box kubwa la nguo halafu akajilundika mule, nikamwita akainuka akaenda zake.

Hebu tupe kisa chako/mdogo wako kipindi cha makuzi yenu.
Du hii balaa aisee!
1. Je, alizeti ilikuwa ya kula hadi ukawanyima wenzako? Kuna mahali fulani niliona watoto walikuwa wanakaanga alizeti. Mlikuwa mnakaanga mnakula?

2. Pole kwa kukatishwa mgegedo. Ina maana mama alipoondoka hukupata tena genye za kuendelea kugegeda? Hahahaha!

Back to story sharing................
Kipindi nikiwa shule ya msingi, tulikuwa na ujinga wa kujificha juu ya miti. Tuliamini kwamba mtu ukipanda juu ya mti aliye chini hakuoni. Utoto bhana!

Sasa siku moja mimi na mwenzangu tukajificha juu ya mti ili kukwepa kuonekana kwa walimu. Kumbe mti tuliojificha upo mbali na mahali alipokuwa mwalimu mkuu akiwapa adhabu wanafunzi wenzetu (huku tumevaa mashati meupe). Eeh bwane ehh, kumbe mtu akiwa mbali na miti anakuona vizuri tu aisee!

Basi mwalimu alipotuona akamtuma mwanafunzi mmoja mkubwa atufuate. Ile kushtuka huyu hapa! Tukashuka harakaharaka tukataka kukimbia lakini tukajua hata tukimbie hatuwezi kufua dafu. Sanasana tutakuwa tunajiongezea idadi ya makosa. Na huyo mwalimu aliyemtuma kutushusha hana masikhara aisee. Tukaone isiwe taabu tukajisalimisha tukakamatwa mateka akatupeleka kwa mwalimu.

Siku hiyo tulikula fimbo kidogo nijikojolee. Tangu siku hiyo tukaona tena kupanda kwenye miti hakutusaidii. Tukawa wanafunzi watiifu hadi tulipohitimu shule.

Utoto raha sana aisee!
 
Daaah nimekumbuka mbali sana. Enzi ya asante Mkapa, RIP Big Benji, nikiwa darasa la pili nilikua napenda sana kwenda vibanda umiza vile vilikuwa vinaonyesha movies. Sasa ratiba ilikua hivi asubuhi mpaka sa6 mchana ni picha za kihindi huwa ni ndefu hivyo huwa mbili tu, sa7 picha za kibongo hadi sa10 au kizungu inategemea, sa10 hadi sa1 usiku ya kihindi ya kumalizia siku. Baada ya hapo watu hutawanyika lakini kwenye ule ubao wa kuwekea makava ya muvi nilikua nasoma kwa chini kila siku wanaandika leo usiku kutakuwa na pilau. Sasa nafikiri ni curiosity na utoto wa kutojua pilau ni nini? Siku moja nikasema leo siondoki, baada ya picha ya kihindi ya jioni kuisha nitasubiri mpaka na mimi leo nile hilo pilau nikidhani ni msosi. Sasa binamu zangu ambao tulikuwa na umri sawa wakati wanaondoka bandani baada ya picha ya kihindi nikawa nawashawishi tubaki wote tule pilau wakasema watoto hawaruhusiwi sikukata tamaa, nyuma ya lile banda kuna matobo yalikuwepo ambayo unaweza kuona ndani, nikasema nitajibanza kwa nyuma ya banda hadi mda wa pilau ufike wakipakua nitaenda na hakuna atakayenifukuza(masikini ningejua ningeondoka na binamu zangu).
Basi muda ukafika nikastaajabu kuona wake kwa waume, wababa kwa wamama, na mabraza na masista du wa mtaani wanaingia bandani, hapo ishafika saa4 usiku, laahula VHS ikafunguliwa wakatia mkanda wa tofali daaah nilichokiona (ilikua siku yangu ya kwanza kucheki porno) na kwa kuwa nilikua nachungulia toka nyuma ya banda nikawa naona na wale waliokaa nyuma walichokuwa wanafanya ni laana.
Sasa bana msala ulianza pale lile zoezi la pilau lilipoisha nisijue ishakua sa6 usiku na nimeshatafutwa kinyama bila mafanikio, na binamu zangu walipoulizwa wakasema nilikua nasubiri pilau, wewe sikia tu kama sikuzimia siku hii kutokana na kipigo sitazimia tena mshua alinidunda kama anaua nyoka.
Sasa nilipokua naulizwa umekula wapi pilau? Mimi kimya. Hapa nyumbani hauli? Mimi kimya. Mama anadakia huyo jeuri unaona hajibu, asijue ni mambo ya ajabu nimetoka kutazama nashindwa hata kuyaelezea. Siwezi sahau hii siku asubuhi nilipelekwa hospitali baada ya kupata homa kali na vijipu sababu ya kipigo.
Hahahaha! Pole sana mkuu. utoto raha sana. Ungesem ukweli wangekuua, bora ulipobakia kuwa jeuri. Hahahaha!
 
Mimi binafsi nilichelewa sana kuanza kujihusisha na mambo ya ngono katika ukuaji wangu, lakini nilipokuwa chalii flani hivi nilijaribiu kujihusisha na tabia hiyo mbaya na kwa bahati nzuri sikufanikiwa.

Mara zote nlipojaribu nilijikuta katika mikono ya wazazi na wana jamii wenye nia niema.

Katika majaribio yangu yote mawili niikamatwa, na hii ilinipa fedhea sana katika umri ndogo maana sasa ikaonekana kwamba mimi ni mtoto mshenzi na sipaswa kuaminiwa japo nilikuwa mpole sana.

Tulihama ule mtaa, na skuwahi tena kujihusisha na tabia hiyo chafu mpaka nilipokuwa na umri sahihi.

Jamii ilinichukulia kama mzaririshaji wa kingono na mbakaji, lakini cha ajabu washkaji zangu walikuwa wanafanikisha 😅
 
Wakati nikiwa chalii, kwa mtoto wa kiume kuwa na m.avuzi ilikuwa dili sana, ila Mimi na mdogo wangu hatukuwa nayo.

Sasa kwenye kupiga story kitaa, wadau wakawa wanasema ukikojoa kwenye jiko asubuhi utaamka na msitu wa kufa mtu. Usiku baada ya kula, tukavizia wengine wameenda kulala, Mimi na dogo tukaenda kukojolea jiko.

Asubuhi palivyokucha kabla hata hatujapata muda wa kujikagua m.avuzi kama yameota au la, tuliamshwa na Mshua. Ile ndio ilikuwa mara ya kwanza kuiona bad side ya Mshua.

Ofcourse alinipatia somo pia, kwamba m.avuzi yanaambatana na maumivu. Tokea yameota rasmi, shida haziishi, majukumu yanazidi n.k
 
1. Mwalimu alikuwa anakaa kwenye koti na kukihamisha na kudondoka chini pwaa. Darasa zima lika Cheka. Ila Mungu c athumani adhabu alipewa mwingine . Maana nisogeza kiti na kusogea mbele.
Ilipogundulika ni mimi. Nikaambiwa nije na mzazi. Nilishambuliwa na ofisi nzima ya walimu. Na kurudi nyumba kama season nyingine ya adhabu.

2. Tupo na Wana Huwa tunatabia yankuchokoza mbwa wa geti Kali, tunachungulia kwenye upenyo tunabweka wuuu,wuuu, mbwa anabweka hatari, siku hazigandi tunaona Raha wenzangu wakawa wanapanda kwenye geti na kumfanya mbwa afyatuke kwenye mnyororo wake akaukata. Aloooo, bwana Yesu saidia nilikimbia kimya kimya niliposimama nikaamza kulia.
Jamaa yetu alipigwa bite za kutosha akalazwa na kuchomwa sindao za mbwa kichaaa.
Wengine ikawa adhabu mkienda kumwona fimbo 12.

3. Mechi za ndondo kapu kati ya mtaa na mtaa, Kuna watoto wa mabibo jeshin wakaja kucheza kwetu , tukafungwa tukaleta uhuni kuwa tupo mtaani kwetu tukachomoa goli ilikuwa matawi ya mnazi lilikuwa upande wetu tukarusha kwenye nyumba mojawapo ikaingia ndani, ugomv8 ugomvi jamaa yetu mmoja mjukuu wa Mary chipungahelo akagungulia mbwa wake wahuni wakakimbia woote, tukajua tumemaliza
Saa mbili usiku wakaja tena na brothers zao wengine walikiwa sijui MP wale waliangusha kichapo, kwa watu wengine sisi kwenye ugomvi tukampiga dogo mmoja baba yake.mjeshi nahisi aliumia vibaya jichoni. Mpaka sasa nichongo. Ulikuwa mzozo mkubwa sana. Lakini kesi sijui iliishaje .
4. Kuiba /kupora kofia ya police, akiwa anacheza kamali. Aisee cjawahi kuona police anakuwa mpole kiasi kile l, hii kesi yake tulipona kwa sababu aloyekuwa kwenye kesi alikuwa mjukuu wa Mkubwa.
5. Kesi zilivyokuwa nyingi nikapelekwa kijijini kama adhabu. Shule moja inaitwa igowole ipo mufindi. Mkataba wa kwenda Kule nikifanya ujinga wowote, mzazi hayupo na hakuna wa kunitetea, Kule nikakutana na watoto wanatoka morogoro wamepinda balaa, tunakumbuka shule ilikuwa na miradi tofauti, walimu wetu ndo walikiwa wanafaidi direct na ile.miraid, gafla wanafunzi wakagoma na maandano na mgomo mimi nikawa moja ya VIONGOZi wagomaji kwa stand 1. Migomo ya zamani ni kupasua vioo vya madarasani shuleni, nyumba za walimu, kubomoa ghala za misosi na pamoja na kuchoma mifugo na kuharibu mazao.. mishale ya saa 6 kwenda saa 7 fujo zimekolea kumbe FFU WALIKUJA KIMYA KIMYA C GIZANI. GAFLA UNASHANGAA MTU KAVAA KIOO KAMA ANAENDA KUVUA KAMBALE mabomu wa machozi mawili tumedakwa kama kuku wote. Wengine tukalal porini kwenye magogo baridi inatupiga... Aisee nimechoka kuandika

Ila Mungu alikuwa anasikikiza sana Sala za Mama, maana Kuna siku alikuwa anasali sitting room anasema Mungu huyu mtoto nakukabidhi wewe, ikiwezekana kama sio mpango wako asiwe wangu mpeleke Sehemu sahihi kama Yusuph. Alooooo
Dah hatari sana .
Mpende sana mama lakini nahisi sasa umebadilika maana hamkawii nyie watu wa hivi tukikutana bar mnatutegeshea tunaenda maliwato mnakojolea kwenye vinywaji vyetu

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Darasa la nne lilikua na uhaba wa dawati, tukaitwa mbele wote, mwalimu akaanza kupanga moja moja mpaka dawati lijae, bahati mbaya mimi nikawa wa mwisho nikaambiwa nitafute dawati lolote nikae, hapo kila dawati lina wanafunzi wa tano, kila ninapoenda nakataliwa , niliumia sana ila kwa vile nilikua mnyonge tokea chekechea sikujali sana, mwalimu alilazimisha nikae kwenye dawati la wanafunzi wembamba hivyo rukwa sita ila mimi nilikua nakaa upande.

Wiki ile ikaisha nikapata wazo , mpaka darasa la nne liishe nitateseka sana , jumapili kanisa letu lilikua karibu na shule, ibada yetu watoto ilikua ibada ya pili , niliwahi asubuhi sana nikaenda shuleni, nikaenda kuchukua dawati darasa la kwanza nikaleta darasa la nne nikaliweka nyuma kabisa.

Jumatatu ikafika japo nina wasi wasi lakini niko nafurahia kukaa dawati nzima peke yangu!
Sikuulizwa ila mpaka natoka darasa la nne nilikua nakaa kwa ku enjoy sana.
 
Kauta hoyee .. alinikimbiza na mlinzi nilitoroka kwenda kuiba mapindigesi
emoji1787.png
emoji1787.png
emoji1787.png
Ulipita
Kauta hoyee .. alinikimbiza na mlinzi nilitoroka kwenda kuiba mapindigesi
Kumbe na ww ulisoma pale. Ila nahisi ulisoma advanced level
 
Back
Top Bottom