Share nasi matukio yako ya ukuaji

Share nasi matukio yako ya ukuaji

Niaje wadau

Leo nlipata muda wa kuzunguka zunguka town, nimekutana na Mwalimu mmoja alinifundisha shule ya msingi, amefanya nikumbuke baadhi ya matukio mengi sana ya nyuma.

1. Kipindi niko shule ya msingi baada ya kusoma nkawa naenda polini kutafuta maembe afu nnauza
Nikiuza ile hela ni kununua alizeti na gropu za tochi. Kwahyo ile asubuhi wenzangu wanavyoingia darasani mimi nazama porini, ikifika saa 4 muda wa mapumziko naenda kununua VITU, hapo mimi ndio boss.

Sasa siku moja nikawanyima jamaa zangu alizeti wakachukia na kwenda kumpa taarifa baba kuwa Nahman hasomi anauza maembe! Aloo nlikula kichapo ile siku sitokaa nisahau!

2. Kipindi cha balehe kimekolea pale, nikategea wazazi hawapo na mpangaji mmoja ameshaenda kazini nkaita pisi moja nyumba ya pili ije kule chumbani kwetu. Mtoto akaja na kanga na kachupi tu, ile nmeanza manjonjo nikasikia geti linesukumwa la nje!

Si nkatoka ile haraka nkakutana na mama! Akauliza mbona umetoka haraka au unachezea umeme (nilikua napenda kujaribu jaribu vitu) nikajibu hapana. Akasema wee ngoja nije, akaingia chumbani me nmebaki nje nasikilizia bomu linaloripuka.

Nakuta kaingia katoka kaenda zake ndani kuchukua alivyosahau then akaenda zake. Sasa kuingia kule ndani na mimi simuoni J. Kumbe aliingia kwenye box kubwa la nguo halafu akajilundika mule, nikamwita akainuka akaenda zake.

Hebu tupe kisa chako/mdogo wako kipindi cha makuzi yenu.
We jamaa fala sana kwaiyo unasubiri upewe tuzo😂
 
Msanii Dully ndio katoka ni wimbo wake salome na ablam yake Historia ya kweli, nipo mkoa X shule boarding usiku tumetoroka tukaenda ukumbini, show imeisha tunatoka ukumbini tunakuta wahuni wanamzonga dada mmoja hivi kisa kavaa nusu uchi dada kujisalimisha akakimbilia kwa maskali waliokuwa lindo bank

Miye na jamaa tukapata wazo tukodi tax twende mchukua yule dada tuseme tunamjua ili tukampige mtungo,bwana wee sitosahau

Tax inapaki bank tu ile jamaa anashuka askari wakakoti bunduki mpo chini ya ulinzi lala chini jamaa akalala chini ikatolewa amri wote kwenye gari tushuke aisee tulicgezea kipigo kumbuka tumetoroka shule, tulipigwa nguo chanika magoti yamechubuka yani tupo hoi ndiotunambiwa ondokeni dereva wa tax alikimbia akasahau gari,

Tunarudi hostel tumeumia asubuhi kiongozi wa bwana akareport kwa uongozi wa shule, tukaitwa tunachezea kichapo tena, na suspension ikafuata mwezi mzima tukirudi tuje na wazazi

Hapo hapo shule mkoa huo huo imekuja imekuja timu ya Yanga kucheza si tukatoroka shule hao uwanjani vingilio hatuna ile kuzu guka zunguka uwanja tukakuta jamaa wamevunja eneo kwaiyo mnapita pale kwenye tundu mnaingia uwanjani bwana bwana acha tu

Kumbe ndani mule askari washatambua kwaiyo wamekaa ukiingia tu unaitwa kaa hapa so wazee hatujui tukaingia tukakuta watu kibao wamekamatwa tatizo siyo kukamatwa tatizo nimetoroka shule itakuwaje

Basi tumeingia hivi askari wakatuchukua kutupeleka kwenye karandinga tunapitishwa chini ya uwanja hivi jukwaani watu kibao hee kumbe walimu wapo umo na Head master si wakatuona wanafunzi wao, tupo kwenye karandika tukasikia wanafunzi wa shule X njooni tukatoka ebwana tukambiwa haraka sana rudini shule, tukarudi kesho yake sasa tulichezea fimbo na adhabu kali ikafuata


Ipo nyingine hiyo nipo form six na mwanangu mmoja kutoka Tanga uyo week end tunaenda club, tuna muhuri wetu kama wa club so tukifika tunakaa njee kingilio buku mbili tu enzi hizo kwaiyo siye tunagonga mhuri kwa buku buku tu unazama ndani ebwana kumbe wenye club wanafutilia inakuwaje watu ndani wengi arafu mapato madogo

bwana bwana si wakatuotea siku hiyo tuligongwa acha na polisi tukapelekwa uzuri form six nilikuwa day so nakaa gheto na wenzangu so wanafunzi we zangu wakajichanga wakaja nitoa

Hiyo ikapita club tunaenda ila deal hatuna ila tunaitaji bia inakuwaje tukaanza tabia za kishenzi ukijifanya unacheza mziki umeacha bia siye tunahamisha bia tunakunywa siku moja si tukahamisha bia kumbe mwenye bia katuona ebwana fujo zikaanza club ngumi ngumi, uongozi ukajuw wale wanfunzi tena aaah tukapigwa na marufuku kwenda hiyo club

Aisee story ni nyingi tunashukuru mungu utukutu wote tupo hai na maisha yana songa
 
Nikawa siadhibiwi kazi yangu ni kuleta fimbo nzuri kwa ajili ya kuadhibu wengine na kwa akili za kitoto na nilivyokuwa mtiifu kufuata maelekezo nilikuwa naleta fimbo nzuri kweli kweli. Nilikuwa na chimbo langu mtoni kwenye mti mmoja ulikuwa umenyooka haswa na fimbo zake hazivunjiki haraka.
Ulikuwa mnoko sana
 
Mimi kipindi cha ukuaji wakati wote nilikuwa mtu wa kusifiwa tu mkaka mzuri, handsome, kila mwanamke atatamani kuwa na ww utaleta sana shida lkn nimeishia kuwa mwanaume wa hovyo ndoto nyingi zikayeyuka nafikiri midomo ya sifa ikizidi wakati kutoka kwa watu wakati wa ukuaji wako hiyo ni sumu mbaya
 
Mimi bana TV ilikuwa inakaa chumbani kwa washua wakirudi kazini jioni wanaitoa tunatazama mpaka night kisha inarudishwa chumbani.Sasa mimi nikajiongeza niliiba funguo moja ya chumbani kwa washua ili wakienda kazini niwe naingia na kuangalia TV kwahiyo ndio ikawa mchezo wangu nikisikia gari wanarudi nazima fasta TV nafunga mlango wao kama hamna kilichotokea,house girl alikuwa analijua hili.Siku moja bwana kama kawaida walivyoondoka wazee kwenda kazini kama kawaida nikachukua funguo zangu nikafungua chumba chao nikaangalia sana TV ilipofika jioni mda ambao najua wanakaribia kurudi nikazima TV ila nikasahau kufunga mlango na funguo nikaiacha mlangoni.Mzee alivyorudi si akaikuta akamuuliza Housegirl nani ameingia mle chumbani na funguo kaipata wapi housegirl akanitaja duh katika siku nilizokula mikwaju ile ilikuwa miongoni mwa siku hizo na pia ndio ilikuwa mara ya mwisho kuchapwa na Mzee maana nilikuwa 16 au 17 hivi
Duh🤭 nikaju ulilala ukasinzia😂
 
Ila na wewe mchokozi aise! Kama hivi visa unafifikiliaje?

1. 200.....hapo nipo F5, boarding, nkatoloka. Maisha ya kuaa ndani huku ulikuwa dei,hayakuwa sawa. Kukawa na mshikaji nilisoma nae, kumbe kwao kuna rubisi,kali af tamu balaa. Nikanywa weeee,kumbe moshi unapanda mi sielewi. Njia ya kwenda kwao,kuepuka kukutana na mtu,ni sehemu ya kufugia ng'ombe wa maziwa,pamezinguushiwa senyenge.
Kukawa na maembe sasa. Ile narudi mida ya saa moja,mi naenda tu,nikasema niwapelekee washikaji hata maembe. Nkacuma,badhi yameiva,mengine mabichi na machanga humo humo.
Cha kubebea,hamna! Kuvua tu shati. Litafuliwa litakate,hapo sikuwa naelewa. Kuna mitalo ya maji humo balaa. Nikikanyaga, muguu huo,umezama. Hatua chache mbele,mzima mzima.
Naangalia sehemu ya kutokea,siioni. Maembe hapo yanamwagika na kupungua tu. Suruali na viatu,wewenyewe jiulize. Nilibahatika kukatiza barabara,nikaenda. Sikupita getini,nilipita njia za panya.
Mi sinajua naenda kwa majama,af ndo ilikuwa mara yangu ya kwanza kulewa sasa. Maembe yalobaki hayazidi hata 10.
Nimepita nkaingia darasani hapo ni mda wa kujisomea. Kumbe,kuna mwarimu hapo alikuwa amekuja kusaidia kurudia,kakaa kwenye viti vya wanafunzi. Naingia na maembe na suruali na viatu vimelowa, dah! Fedheha ya maisha nilopata nadhani ni ile tu. Nikatonywa,mi sielewi. Nadhani ile kutembea iliongeza wenge.
Maembe sikumpa mtu,nikaweka tu juu ya dawati.
Nashuka kuelekea bwenini, dah! Nkapoteza ramani mazima.
Kesho yake sasa, ndo naitwa na kupewa off siku 7,na kurudi na mzazi.
*****, naanzaje sasa! Khah!!!!!! Acha tu niishie hapa




2. Tukio la pili,nikiwa nasoma kama darasa la 2 au la tatu,acha niende kuiba asali🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣. Aiseee!
Nikatafuta mti mrefu,nkapata. Kuna mizinga ilikuwa karibu na kwetu ya jirani. Mi sijui asali ntapata au sipat. Na lengo likawa tu nitoe kifuniko cha mzinga(ile mikubwa ya zamani), kweli kikadondoka. Kuangalia,nkaona hapa ntashambuliwa. Akili za kitoto bwana. Nikajisemea ngoja tu nichovye na kile kijiti. Hata basi nililamba! Kilichonikuta sitokaa nisahau. Ila nachojua karibia mtaa mzima walisikia kilio na kuwahi. Kila sehemu ya mwili,nilidungwa. Baada ya mda sasa,mwili mzima unawaka moto, mdomo unapima kama kilo 10.
We misomisondo
Umepigaje apoo😅😂
 

Attachments

  • IMG_0468.jpeg
    IMG_0468.jpeg
    36.8 KB · Views: 12
Mimi kipindi cha ukuaji wakati wote nilikuwa mtu wa kusifiwa tu mkaka mzuri, handsome, kila mwanamke atatamani kuwa na ww utaleta sana shida lkn nimeishia kuwa mwanaume wa hovyo ndoto nyingi zikayeyuka nafikiri midomo ya sifa ikizidi wakati kutoka kwa watu wakati wa ukuaji wako hiyo ni sumu mbaya
Sikutambulishi wife😅
 
We misomisondo
Umepigaje apoo😅😂
Hapo hamna kitu mkuu. Hivi unaijua mizinga ya kienyeji wewe? We acha tu. Bora huyo jicho linaona moja. Mi yote yalivimba. Jiulize kwenye miaka kama 9 au 10. Kukimbia siwezi,acha tu
 
Hapo hamna kitu mkuu. Hivi unaijua mizinga ya kienyeji wewe? We acha tu. Bora huyo jicho linaona moja. Mi yote yalivimba. Jiulize kwenye miaka kama 9 au 10. Kukimbia siwezi,acha tu
Hahah pole mkuu
 
Hiyo ya pili!!

Kuna mdogo wangu wa kike ni mkorofi sana
Unajua ile kipindi cha nyuma tulikua tunanunuliwa nguo za skukuu
Mdog wangu alikua na gaunj jipyaaa zuri kishenzi
Sasa katika pitapita zake akavunja muwa kwenye nyumba ya watu
Wakaanza kufukuzia
Kimbe ki uzi kimenasa kwenye mchongoma
Yeye anakimbia gauni linafumuka hajui
Kafika home na muwa mreeefu
Ila makalio yako nje
Alikula fimbo sio poa
Hahaaaa, ukimkumbusha anasemaje sasa? Utoto Raha sana mkuu.
 
Nikiwa Darasa La Sita Wakati Nywele Sehemu Nyeti Zikianza Chipuka Nilianza Tabia Ya Uzururaji Nakumbuka Kuna Cku Nilitoka Nyumbani Saa 9 Mchana Mm Na Rafk Yangu.Aisee Tulizurura Sana Ikafka Saa 2 Ucku Nikaenda Kwa Rafk Yangu Mwngne Alikuwa Na Laptop Nikaanza Chezea Laptop Yake Mpaka Saa 5 Ucku Huku Nyumbani Hali Si Shwari Natafutwa Na Viboko Vimechumwa Viko Ndani Aisee Niliporud Nilifungiwa Ndani Niliisoma Namba Kwa Kirumi Hyo Tabia Ilifika Ukomo Siku Hyo
 
Kuna siku moja Mzee Alienda huko Akanunua Miche akaileta ili Aipande Basi Bana Akaipanda Ile Miche Asubuhi Yake Mimi na Upanga Wangu Hadi ilipo Ile Miche Nikaikata Kama Miwili hivi afu Nikaja Kushtuliwa na Mama Kua Ni Ya baba yako hiyo Miche.Daah Ile Siku Tumbo la ghafla Likanishika Mzee akarudi Akakuta ule Msala kuuliza Akaambiwa Ni Mimi Basi Bana Si Akaanza Kunikimbiza Akaja Akanishika Kwa bahati Nzurii Akawepo Mzee jirani Wanae heshimiana Akamwomba anisamehe!! Akawa ameniacha Sasa Usiku Wakati Wa chakula Kumbe Hasira Hazijaisha Kumtizama tu wakati Wa kula Nikala Bonge moja la Kofi eti Vibaya Kumtizama Wakti wa kula Nilienda na Kulala.
Hahaaaaa nimecheka kwa sauti. Wazee wetu walikuwa makauzu sana.
 
Mama alikuwa anasema roho za uharibifu... Unakula fimbo then anakuambia soma mithali ngapi ngapi' inasema usimnyime mtoto fimbo/mapigo maana hatayasahu hata atakapokuwa Mzee' ukimaliza kúsoma zinaanzia stick za maana
Daah!!!hyo na sisi pia tumepitia mda wa kichapo unapewa kwanza bible usome hicho kifungu
 
Back
Top Bottom