Share nasi matukio yako ya ukuaji

Nahman

JF-Expert Member
Oct 4, 2023
521
1,521
Niaje wadau

Leo nlipata muda wa kuzunguka zunguka town, nimekutana na Mwalimu mmoja alinifundisha shule ya msingi, amefanya nikumbuke baadhi ya matukio mengi sana ya nyuma.

1. Kipindi niko shule ya msingi baada ya kusoma nkawa naenda polini kutafuta maembe afu nnauza
Nikiuza ile hela ni kununua alizeti na gropu za tochi. Kwahyo ile asubuhi wenzangu wanavyoingia darasani mimi nazama porini, ikifika saa 4 muda wa mapumziko naenda kununua VITU, hapo mimi ndio boss.

Sasa siku moja nikawanyima jamaa zangu alizeti wakachukia na kwenda kumpa taarifa baba kuwa Nahman hasomi anauza maembe! Aloo nlikula kichapo ile siku sitokaa nisahau!

2. Kipindi cha balehe kimekolea pale, nikategea wazazi hawapo na mpangaji mmoja ameshaenda kazini nkaita pisi moja nyumba ya pili ije kule chumbani kwetu. Mtoto akaja na kanga na kachupi tu, ile nmeanza manjonjo nikasikia geti linesukumwa la nje!

Si nkatoka ile haraka nkakutana na mama! Akauliza mbona umetoka haraka au unachezea umeme (nilikua napenda kujaribu jaribu vitu) nikajibu hapana. Akasema wee ngoja nije, akaingia chumbani me nmebaki nje nasikilizia bomu linaloripuka.

Nakuta kaingia katoka kaenda zake ndani kuchukua alivyosahau then akaenda zake. Sasa kuingia kule ndani na mimi simuoni J. Kumbe aliingia kwenye box kubwa la nguo halafu akajilundika mule, nikamwita akainuka akaenda zake.

Hebu tupe kisa chako/mdogo wako kipindi cha makuzi yenu.
 
Hiyo ya pili!!

Kuna mdogo wangu wa kike ni mkorofi sana
Unajua ile kipindi cha nyuma tulikua tunanunuliwa nguo za skukuu
Mdog wangu alikua na gaunj jipyaaa zuri kishenzi
Sasa katika pitapita zake akavunja muwa kwenye nyumba ya watu
Wakaanza kufukuzia
Kimbe ki uzi kimenasa kwenye mchongoma
Yeye anakimbia gauni linafumuka hajui
Kafika home na muwa mreeefu
Ila makalio yako nje
Alikula fimbo sio poa
 
Nikiwa primary school nilikuwa mpole na mkimya sana hali iliyopelekea kupendwa sana na baadhi ya walimu, ilifikia hatua nikawa miongoni mwa wanafunzi wanaoachwa kuadhibiwa hata likiadhibiwa darasa zima( wengine wanaachwa kwa sababu mbalimbali kama za kiafya). Darasa la 5 akahamia mwl mmoja wakike ana mwanae wakwanza wakiume mwenye jina kama langu, alikuwa mkali sana ila hakuwai kunipiga kabisa alikuwa ananipenda kwa sababu n mtulivu na nna jina kama la mwanae.

Nikawa siadhibiwi kazi yangu ni kuleta fimbo nzuri kwa ajili ya kuadhibu wengine na kwa akili za kitoto na nilivyokuwa mtiifu kufuata maelekezo nilikuwa naleta fimbo nzuri kweli kweli. Nilikuwa na chimbo langu mtoni kwenye mti mmoja ulikuwa umenyooka haswa na fimbo zake hazivunjiki haraka.

Hii ikanijengea chuki kwa baadhi ya wanafunzi wenzangu na ukizingatia mimi huwa siadhibiwi.
Usiku mmoja nimelala nikaota nimefuata fimbo kama kawaida, kabla sijafika kwenye ule mti nikaona mzuka/mzimu unatisha umevalia mavazi meupe juu mpaka chini, nikasita kuendelea nikaanza kurudi nyuma, ghafla ukaanza kunifuata na kunifukuza ile nageuka ili nikimbie vizuri nikashtuka usingizini.

Alooh kuanzia ile siku nilikoma kwenda kufuata fimbo kwenye ule mti, nikawa nachukia ile kazi kadri siku zilivyosogea nikawa napeleka vifimbo vya hovyo na mwshowe nikaambiwa naona kazi imekushinda, akapewa mtu mwingine. Ile ndoto kuna namna ilikuwa na ujumbe maana ilinitisha kweli kweli.
 
Nikiwa primary school nilikuwa mpole na mkimya sana hali iliyopelekea kupendwa sana na baadhi ya walimu, ilifikia hatua nikawa miongoni mwa wanafunzi wanaoachwa kuadhibiwa hata likiadhibiwa darasa zima( wengine wanaachwa kwa sababu mbalimbali kama za kiafya). Darasa la 5 akahamia mwl mmoja wakike ana mwanae wakwanza wakiume mwenye jina kama langu, alikuwa mkali sana ila hakuwai kunipiga kabisa alikuwa ananipenda kwa sababu n mtulivu na nna jina kama la mwanae.

Nikawa siadhibiwi kazi yangu ni kuleta fimbo nzuri kwa ajili ya kuadhibu wengine na kwa akili za kitoto na nilivyokuwa mtiifu kufuata maelekezo nilikuwa naleta fimbo nzuri kweli kweli. Nilikuwa na chimbo langu mtoni kwenye mti mmoja ulikuwa umenyooka haswa na fimbo zake hazivunjiki haraka.

Hii ikanijengea chuki kwa baadhi ya wanafunzi wenzangu na ukizingatia mimi huwa siadhibiwi.
Usiku mmoja nimelala nikaota nimefuata fimbo kama kawaida, kabla sijafika kwenye ule mti nikaona mzuka/mzimu unatisha umevalia mavazi meupe juu mpaka chini, nikasita kuendelea nikaanza kurudi nyuma, ghafla ukaanza kunifuata na kunifukuza ile nageuka ili nikimbie vizuri nikashtuka usingizini.

Alooh kuanzia ile siku nilikoma kwenda kufuata fimbo kwenye ule mti, nikawa nachukia ile kazi kadri siku zilivyosogea nikawa napeleka vifimbo vya hovyo na mwshowe nikaambiwa naona kazi imekushinda, akapewa mtu mwingine. Ile ndoto kuna namna ilikuwa na ujumbe maana ilinitisha kweli kweli.
😂😂 oya usikute mule palikua na kitoto kimoja chakichawi
 
Nikiwa primary school nilikuwa mpole na mkimya sana hali iliyopelekea kupendwa sana na baadhi ya walimu, ilifikia hatua nikawa miongoni mwa wanafunzi wanaoachwa kuadhibiwa hata likiadhibiwa darasa zima( wengine wanaachwa kwa sababu mbalimbali kama za kiafya). Darasa la 5 akahamia mwl mmoja wakike ana mwanae wakwanza wakiume mwenye jina kama langu, alikuwa mkali sana ila hakuwai kunipiga kabisa alikuwa ananipenda kwa sababu n mtulivu na nna jina kama la mwanae.

Nikawa siadhibiwi kazi yangu ni kuleta fimbo nzuri kwa ajili ya kuadhibu wengine na kwa akili za kitoto na nilivyokuwa mtiifu kufuata maelekezo nilikuwa naleta fimbo nzuri kweli kweli. Nilikuwa na chimbo langu mtoni kwenye mti mmoja ulikuwa umenyooka haswa na fimbo zake hazivunjiki haraka.

Hii ikanijengea chuki kwa baadhi ya wanafunzi wenzangu na ukizingatia mimi huwa siadhibiwi.
Usiku mmoja nimelala nikaota nimefuata fimbo kama kawaida, kabla sijafika kwenye ule mti nikaona mzuka/mzimu unatisha umevalia mavazi meupe juu mpaka chini, nikasita kuendelea nikaanza kurudi nyuma, ghafla ukaanza kunifuata na kunifukuza ile nageuka ili nikimbie vizuri nikashtuka usingizini.

Alooh kuanzia ile siku nilikoma kwenda kufuata fimbo kwenye ule mti, nikawa nachukia ile kazi kadri siku zilivyosogea nikawa napeleka vifimbo vya hovyo na mwshowe nikaambiwa naona kazi imekushinda, akapewa mtu mwingine. Ile ndoto kuna namna ilikuwa na ujumbe maana ilinitisha kweli kweli.

Mh hadi mimi nmeogopa aloo
 
Mimi niliruhusiwa kuhudhuria mahafali muda wa kurudi niliambiwa ni saa 9 kamili niwe home nikachelewa nikafika home saa 10 nikajificha naogopa kipigo had saa 12,nasikia ndani wanavoulizana nimejibanza dirishani nimejificha baba akapata uoga akaenda had shule kuniulizia karudi namuona muda huo ni saa 1 usiku wamepika hawajala wanaulizana nawasikia, Mimi nikaanza kuzunguka nyumba natafuta pa kupitia nikakosa

Mama akaenda kuuliza Kwa majirani wakasema waliniona wakat narudi jioni inakuwaje nisiwepo wakaanza msako majirani wote na wazazi wangu, nikakimbia najificha kwenye miti eneo la jirani wakipita huku naelekea upande mwingine msako ulikuwa mkali had saa 5 usiku watu hawajalala 😃😃😃Mimi Sina nguvu ninauoga na njaa inaniuma balaa,mbu washaniuma wa kutosha 😂😂😂 walivoniona wakaanza kunikimbiza "huyo huyo" walinibeba juu juu kama mwizi,majirani wakamuwahi baba kumuomba anisamehe asinipige maana wanajua shughuli yake
 
Mimi niliruhusiwa kuhudhuria mahafali muda wa kurudi niliambiwa ni saa 9 kamili niwe home nikachelewa nikafika home saa 10 nikajificha naogopa kipigo had saa 12,nasikia ndani wanavoulizana nimejibanza dirishani nimejificha baba akapata uoga akaenda had shule kuniulizia karudi namuona muda huo ni saa 1 usiku wamepika hawajala wanaulizana nawasikia, Mimi nikaanza kuzunguka nyumba natafuta pa kupitia nikakosa

Mama akaenda kuuliza Kwa majirani wakasema waliniona wakat narudi jioni inakuwaje nisiwepo wakaanza msako majirani wote na wazazi wangu, nikakimbia najificha kwenye miti eneo la jirani wakipita huku naelekea upande mwingine msako ulikuwa mkali had saa 5 usiku watu hawajalala 😃😃😃Mimi Sina nguvu ninauoga na njaa inaniuma balaa,mbu washaniuma wa kutosha 😂😂😂 walivoniona wakaanza kunikimbiza "huyo huyo" walinibeba juu juu kama mwizi,majirani wakamuwahi baba kumuomba anisamehe asinipige maana wanajua shughuli yake
Yaani kujificha ndipo ulipoharibu wewe😂

Nmevuta picha ulivyobebwa!!
 
1. Mwalimu alikuwa anakaa kwenye koti na kukihamisha na kudondoka chini pwaa. Darasa zima lika Cheka. Ila Mungu c athumani adhabu alipewa mwingine . Maana nisogeza kiti na kusogea mbele.
Ilipogundulika ni mimi. Nikaambiwa nije na mzazi. Nilishambuliwa na ofisi nzima ya walimu. Na kurudi nyumba kama season nyingine ya adhabu.

2. Tupo na Wana Huwa tunatabia yankuchokoza mbwa wa geti Kali, tunachungulia kwenye upenyo tunabweka wuuu,wuuu, mbwa anabweka hatari, siku hazigandi tunaona Raha wenzangu wakawa wanapanda kwenye geti na kumfanya mbwa afyatuke kwenye mnyororo wake akaukata. Aloooo, bwana Yesu saidia nilikimbia kimya kimya niliposimama nikaamza kulia.
Jamaa yetu alipigwa bite za kutosha akalazwa na kuchomwa sindao za mbwa kichaaa.
Wengine ikawa adhabu mkienda kumwona fimbo 12.

3. Mechi za ndondo kapu kati ya mtaa na mtaa, Kuna watoto wa mabibo jeshin wakaja kucheza kwetu , tukafungwa tukaleta uhuni kuwa tupo mtaani kwetu tukachomoa goli ilikuwa matawi ya mnazi lilikuwa upande wetu tukarusha kwenye nyumba mojawapo ikaingia ndani, ugomv8 ugomvi jamaa yetu mmoja mjukuu wa Mary chipungahelo akagungulia mbwa wake wahuni wakakimbia woote, tukajua tumemaliza
Saa mbili usiku wakaja tena na brothers zao wengine walikiwa sijui MP wale waliangusha kichapo, kwa watu wengine sisi kwenye ugomvi tukampiga dogo mmoja baba yake.mjeshi nahisi aliumia vibaya jichoni. Mpaka sasa nichongo. Ulikuwa mzozo mkubwa sana. Lakini kesi sijui iliishaje .
4. Kuiba /kupora kofia ya police, akiwa anacheza kamali. Aisee cjawahi kuona police anakuwa mpole kiasi kile l, hii kesi yake tulipona kwa sababu aloyekuwa kwenye kesi alikuwa mjukuu wa Mkubwa.
5. Kesi zilivyokuwa nyingi nikapelekwa kijijini kama adhabu. Shule moja inaitwa igowole ipo mufindi. Mkataba wa kwenda Kule nikifanya ujinga wowote, mzazi hayupo na hakuna wa kunitetea, Kule nikakutana na watoto wanatoka morogoro wamepinda balaa, tunakumbuka shule ilikuwa na miradi tofauti, walimu wetu ndo walikiwa wanafaidi direct na ile.miraid, gafla wanafunzi wakagoma na maandano na mgomo mimi nikawa moja ya VIONGOZi wagomaji kwa stand 1. Migomo ya zamani ni kupasua vioo vya madarasani shuleni, nyumba za walimu, kubomoa ghala za misosi na pamoja na kuchoma mifugo na kuharibu mazao.. mishale ya saa 6 kwenda saa 7 fujo zimekolea kumbe FFU WALIKUJA KIMYA KIMYA C GIZANI. GAFLA UNASHANGAA MTU KAVAA KIOO KAMA ANAENDA KUVUA KAMBALE mabomu wa machozi mawili tumedakwa kama kuku wote. Wengine tukalal porini kwenye magogo baridi inatupiga... Aisee nimechoka kuandika

Ila Mungu alikuwa anasikikiza sana Sala za Mama, maana Kuna siku alikuwa anasali sitting room anasema Mungu huyu mtoto nakukabidhi wewe, ikiwezekana kama sio mpango wako asiwe wangu mpeleke Sehemu sahihi kama Yusuph. Alooooo
 
Mimi nilikua mpole sana kipindi cha primary tena nilikua mdogo ukilimganisha na wenzangu niliosoma nao kijijini enzi hizo.
Kuna wengine walikua wakubwa wananionea sasa mimi siwezi kupambana nao.
Hasira zangu ilikua navizia madaftari yao wakiacha darasani nayapiga nyembe tu. Hasira za kuonewa zinaniisha.
 
Mimi nilikua mpole sana kipindi cha primary tena nilikua mdogo ukilimganisha na wenzangu niliosoma nao kijijini enzi hizo.
Kuna wengine walikua wakubwa wananionea sasa mimi siwezi kupambana nao.
Hasira zangu ilikua navizia madaftari yao wakiacha darasani nayapiga nyembe tu. Hasira za kuonewa zinaniisha.
Mama alikuwa anasema roho za uharibifu... Unakula fimbo then anakuambia soma mithali ngapi ngapi' inasema usimnyime mtoto fimbo/mapigo maana hatayasahu hata atakapokuwa Mzee' ukimaliza kúsoma zinaanzia stick za maana
 
Kuna siku moja Mzee Alienda huko Akanunua Miche akaileta ili Aipande Basi Bana Akaipanda Ile Miche Asubuhi Yake Mimi na Upanga Wangu Hadi ilipo Ile Miche Nikaikata Kama Miwili hivi afu Nikaja Kushtuliwa na Mama Kua Ni Ya baba yako hiyo Miche.Daah Ile Siku Tumbo la ghafla Likanishika Mzee akarudi Akakuta ule Msala kuuliza Akaambiwa Ni Mimi Basi Bana Si Akaanza Kunikimbiza Akaja Akanishika Kwa bahati Nzurii Akawepo Mzee jirani Wanae heshimiana Akamwomba anisamehe!! Akawa ameniacha Sasa Usiku Wakati Wa chakula Kumbe Hasira Hazijaisha Kumtizama tu wakati Wa kula Nikala Bonge moja la Kofi eti Vibaya Kumtizama Wakti wa kula Nilienda na Kulala.
 
Primary darasa la tatu, siku darasani mwalimu ilikuwa aniadhibu kwa kosa sikulifanya mimi kabisa.
Nilisononeka sana Moroni kwa uonevu ule.
Kimoyomoyo nilimuomba Mungu atende lolote nisiadhibiwe.
Ghafla banda la mbuzi wa shule wakiwa ndani lililipuka moto.
Shule nzima wanafunzi walitoka madarasani, adhabu yangu ilipotea hapohapo.
Watakao sema ni coincidence sawa, lakini mimi hadi sasa naamini nilie muomba kwa dhati alinisaidia.
 
Eeeh mjjomba
1. Mwalimu alikuwa anakaa kwenye koti na kukihamisha na kudondoka chini pwaa. Darasa zima lika Cheka. Ila Mungu c athumani adhabu alipewa mwingine . Maana nisogeza kiti na kusogea mbele.
Ilipogundulika ni mimi. Nikaambiwa nije na mzazi. Nilishambuliwa na ofisi nzima ya walimu. Na kurudi nyumba kama season nyingine ya adhabu.

2. Tupo na Wana Huwa tunatabia yankuchokoza mbwa wa geti Kali, tunachungulia kwenye upenyo tunabweka wuuu,wuuu, mbwa anabweka hatari, siku hazigandi tunaona Raha wenzangu wakawa wanapanda kwenye geti na kumfanya mbwa afyatuke kwenye mnyororo wake akaukata. Aloooo, bwana Yesu saidia nilikimbia kimya kimya niliposimama nikaamza kulia.
Jamaa yetu alipigwa bite za kutosha akalazwa na kuchomwa sindao za mbwa kichaaa.
Wengine ikawa adhabu mkienda kumwona fimbo 12.

3. Mechi za ndondo kapu kati ya mtaa na mtaa, Kuna watoto wa mabibo jeshin wakaja kucheza kwetu , tukafungwa tukaleta uhuni kuwa tupo mtaani kwetu tukachomoa goli ilikuwa matawi ya mnazi lilikuwa upande wetu tukarusha kwenye nyumba mojawapo ikaingia ndani, ugomv8 ugomvi jamaa yetu mmoja mjukuu wa Mary chipungahelo akagungulia mbwa wake wahuni wakakimbia woote, tukajua tumemaliza
Saa mbili usiku wakaja tena na brothers zao wengine walikiwa sijui MP wale waliangusha kichapo, kwa watu wengine sisi kwenye ugomvi tukampiga dogo mmoja baba yake.mjeshi nahisi aliumia vibaya jichoni. Mpaka sasa nichongo. Ulikuwa mzozo mkubwa sana. Lakini kesi sijui iliishaje .
4. Kuiba /kupora kofia ya police, akiwa anacheza kamali. Aisee cjawahi kuona police anakuwa mpole kiasi kile l, hii kesi yake tulipona kwa sababu aloyekuwa kwenye kesi alikuwa mjukuu wa Mkubwa.
5. Kesi zilivyokuwa nyingi nikapelekwa kijijini kama adhabu. Shule moja inaitwa igowole ipo mufindi. Mkataba wa kwenda Kule nikifanya ujinga wowote, mzazi hayupo na hakuna wa kunitetea, Kule nikakutana na watoto wanatoka morogoro wamepinda balaa, tunakumbuka shule ilikuwa na miradi tofauti, walimu wetu ndo walikiwa wanafaidi direct na ile.miraid, gafla wanafunzi wakagoma na maandano na mgomo mimi nikawa moja ya VIONGOZi wagomaji kwa stand 1. Migomo ya zamani ni kupasua vioo vya madarasani shuleni, nyumba za walimu, kubomoa ghala za misosi na pamoja na kuchoma mifugo na kuharibu mazao.. mishale ya saa 6 kwenda saa 7 fujo zimekolea kumbe FFU WALIKUJA KIMYA KIMYA C GIZANI. GAFLA UNASHANGAA MTU KAVAA KIOO KAMA ANAENDA KUVUA KAMBALE mabomu wa machozi mawili tumedakwa kama kuku wote. Wengine tukalal porini kwenye magogo baridi inatupiga... Aisee nimechoka kuandika

Ila Mungu alikuwa anasikikiza sana Sala za Mama, maana Kuna siku alikuwa anasali sitting room anasema Mungu huyu mtoto nakukabidhi wewe, ikiwezekana kama sio mpango wako asiwe wangu mpeleke Sehemu sahihi kama Yusuph. Alooooo
😂😂😂 bila shaka we ni mkulya mkuu
 
Mimi nilikua mpole sana kipindi cha primary tena nilikua mdogo ukilimganisha na wenzangu niliosoma nao kijijini enzi hizo.
Kuna wengine walikua wakubwa wananionea sasa mimi siwezi kupambana nao.
Hasira zangu ilikua navizia madaftari yao wakiacha darasani nayapiga nyembe tu. Hasira za kuonewa zinaniisha.
Nyembe kwa kwenda mbele
 
Kuna siku moja Mzee Alienda huko Akanunua Miche akaileta ili Aipande Basi Bana Akaipanda Ile Miche Asubuhi Yake Mimi na Upanga Wangu Hadi ilipo Ile Miche Nikaikata Kama Miwili hivi afu Nikaja Kushtuliwa na Mama Kua Ni Ya baba yako hiyo Miche.Daah Ile Siku Tumbo la ghafla Likanishika Mzee akarudi Akakuta ule Msala kuuliza Akaambiwa Ni Mimi Basi Bana Si Akaanza Kunikimbiza Akaja Akanishika Kwa bahati Nzurii Akawepo Mzee jirani Wanae heshimiana Akamwomba anisamehe!! Akawa ameniacha Sasa Usiku Wakati Wa chakula Kumbe Hasira Hazijaisha Kumtizama tu wakati Wa kula Nikala Bonge moja la Kofi eti Vibaya Kumtizama Wakti wa kula Nilienda na Kulala.
😅😅mzee baba alikutunzia tu
 
Back
Top Bottom