1. Mwalimu alikuwa anakaa kwenye koti na kukihamisha na kudondoka chini pwaa. Darasa zima lika Cheka. Ila Mungu c athumani adhabu alipewa mwingine . Maana nisogeza kiti na kusogea mbele.
Ilipogundulika ni mimi. Nikaambiwa nije na mzazi. Nilishambuliwa na ofisi nzima ya walimu. Na kurudi nyumba kama season nyingine ya adhabu.
2. Tupo na Wana Huwa tunatabia yankuchokoza mbwa wa geti Kali, tunachungulia kwenye upenyo tunabweka wuuu,wuuu, mbwa anabweka hatari, siku hazigandi tunaona Raha wenzangu wakawa wanapanda kwenye geti na kumfanya mbwa afyatuke kwenye mnyororo wake akaukata. Aloooo, bwana Yesu saidia nilikimbia kimya kimya niliposimama nikaamza kulia.
Jamaa yetu alipigwa bite za kutosha akalazwa na kuchomwa sindao za mbwa kichaaa.
Wengine ikawa adhabu mkienda kumwona fimbo 12.
3. Mechi za ndondo kapu kati ya mtaa na mtaa, Kuna watoto wa mabibo jeshin wakaja kucheza kwetu , tukafungwa tukaleta uhuni kuwa tupo mtaani kwetu tukachomoa goli ilikuwa matawi ya mnazi lilikuwa upande wetu tukarusha kwenye nyumba mojawapo ikaingia ndani, ugomv8 ugomvi jamaa yetu mmoja mjukuu wa Mary chipungahelo akagungulia mbwa wake wahuni wakakimbia woote, tukajua tumemaliza
Saa mbili usiku wakaja tena na brothers zao wengine walikiwa sijui MP wale waliangusha kichapo, kwa watu wengine sisi kwenye ugomvi tukampiga dogo mmoja baba yake.mjeshi nahisi aliumia vibaya jichoni. Mpaka sasa nichongo. Ulikuwa mzozo mkubwa sana. Lakini kesi sijui iliishaje .
4. Kuiba /kupora kofia ya police, akiwa anacheza kamali. Aisee cjawahi kuona police anakuwa mpole kiasi kile l, hii kesi yake tulipona kwa sababu aloyekuwa kwenye kesi alikuwa mjukuu wa Mkubwa.
5. Kesi zilivyokuwa nyingi nikapelekwa kijijini kama adhabu. Shule moja inaitwa igowole ipo mufindi. Mkataba wa kwenda Kule nikifanya ujinga wowote, mzazi hayupo na hakuna wa kunitetea, Kule nikakutana na watoto wanatoka morogoro wamepinda balaa, tunakumbuka shule ilikuwa na miradi tofauti, walimu wetu ndo walikiwa wanafaidi direct na ile.miraid, gafla wanafunzi wakagoma na maandano na mgomo mimi nikawa moja ya VIONGOZi wagomaji kwa stand 1. Migomo ya zamani ni kupasua vioo vya madarasani shuleni, nyumba za walimu, kubomoa ghala za misosi na pamoja na kuchoma mifugo na kuharibu mazao.. mishale ya saa 6 kwenda saa 7 fujo zimekolea kumbe FFU WALIKUJA KIMYA KIMYA C GIZANI. GAFLA UNASHANGAA MTU KAVAA KIOO KAMA ANAENDA KUVUA KAMBALE mabomu wa machozi mawili tumedakwa kama kuku wote. Wengine tukalal porini kwenye magogo baridi inatupiga... Aisee nimechoka kuandika
Ila Mungu alikuwa anasikikiza sana Sala za Mama, maana Kuna siku alikuwa anasali sitting room anasema Mungu huyu mtoto nakukabidhi wewe, ikiwezekana kama sio mpango wako asiwe wangu mpeleke Sehemu sahihi kama Yusuph. Alooooo