Sh. Bilioni 13.9 kukarabati Bombardier nchini Canada

Sh. Bilioni 13.9 kukarabati Bombardier nchini Canada

Hizi bilioni kazaa zitatoka wapi? Ndo maana CAG akasema bunge ni dhaifu
 
Masikini JF...!
14JAN 2019...Bombardier kukarabatiwa 
Canada kwa bilioni 13.9/-!
SERIKALI imesema ndege mbili aina ya Bombardier Dash Q400 zilizonunuliwa mwaka 2016, zitapelekwa kufanyiwa ukarabati Canada mwezi ujao.
Imesema ukarabati huo unatarajiwa kugharimu Dola za Marekani milioni sita (Sh. bilioni 13.860).

Wow!
Detective J said:
Muwe mnasoma habari in deep. Sio zile mpya. Hii ni bomberdier Q300 ambayo iliharibika kitambo.. hii ilikuwepo zamani kabla ya hizi mpya kuja. Ndio ndege pekee atcl walibaki nayo.
Eti?
Acha uongo,hiyo ni ile ndege ya pekee ambayo atcl walikuwa nayo kabla Serikali haijaanza kununua zingne.usiwe unaongea kitu bila kuchunguza
Masikini wa Mungu!
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe, aliyasema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, wakati wa uzinduzi wa kozi ya wahudumu ndani ya ndege katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT).

Kumbe ni Waziri!
Kwa nini mnaaminisha umma mambo ya uongo?? Km huna jambo la kupost la maana si ukae kimya? Chombo chochote kufanyiwa ukarabati ni jambo la kawaida na wala siyo dhambi....kama mnadhani sisi tutarudi nyuma kwa maneno yenu ya kijinga mmekwama,MAGUFULI MBELE KWA MBELE hadi 2025 asiyetaka ruksa kuhama nchi
What?
Bombardier kukarabatiwa 
Canada kwa bilioni 13.9/-
Mtumba!
Hiyo heading imekaa kipropaganda
Kivipi?

“Bombadier mbili tulizozinunua tunatarajia kuzipeleka nchini Canada kwa ajili ya kufanyiwa 'service', na ndege moja itagharimu Dola za Marekani milioni tatu,” alisema Waziri Kamwelwe.

Serikali hiyo inaongea!
Inaelekea habari hii ina mawaa/uongo kwani Bombardier zimekuja juzi tu na kabla ya hapo ATCL hawakuwa na ndege aina ya Bombardier
Are you sure?
Waziri huyo alisema kuwa, baada ya kuletewa taarifa hiyo, alilazimika kumfuata Rais John Magufuli na kumshauri serikali ianze kufanya ukarabati kwa hanga lililopo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ili kupunguza gharama kubwa ambazo nchi inaingia katika kuzikarabati ndege.
Lo salaale!
Dudus said:
ukarabati unaogharimu 13.8b/- kwa ndege mbili ndogo yaani wastani wa 6.9b/- kwa ndege moja yenye umri usiozidi miaka mitatu halafu ni ukarabati wa kawaida? Sina hakika kama zimesharudisha japo 15% ya gharama iliyotumika kuzinunua.
Na bado
Inaitwa Remanufacturing. Yani ndege inabomolewa yote, wanaanza kurudishia kifaa kimoja kimoja. Vilivyozeeka vinawekwa pembeni na kufungwa vipya.
Remanufacturing? Kazi mbona ipo!
Habari nyeusi, sishangai Zitto alisema hizo ndege ni mitumba nikama kivuko cha MV Dar Es Salaam #2020 Lissu#
Ni kweli
Hizi ndege zimeanza kazi mwaka 2016, so ni kitu cha wazi kuwa zitakuwa zikihitaji ukarabati.
Nachokaa...!
 
Kwa nini mnaaminisha umma mambo ya uongo?? Km huna jambo la kupost la maana si ukae kimya? Chombo chochote kufanyiwa ukarabati ni jambo la kawaida na wala siyo dhambi....kama mnadhani sisi tutarudi nyuma kwa maneno yenu ya kijinga mmekwama,MAGUFULI MBELE KWA MBELE hadi 2025 asiyetaka ruksa kuhama nchi

Sent using Jamii Forums mobile app
Wahame nchi ni ya babu yako?
 
Ukarabati == Service , chombo chochote lazima kifanyiwe service kubwa kila baada ya kipindi fulani.
Watanzania sasa kila kitu tunafanya siasa.
 
Kwenye hili sidhani kama serikali ni wakweli ..bei za hiyo service imeongezwa kimkakati.haiwezekani service ya ndege ni nusu ya bei ya kununulia ndege!
Yani ununua gari jipya 80m halafu kama wanaovoiita service ya kawaida iwe 40m.
HUU NI WIZI.....! Hapo ndo napoamini hatuna viongozi Bali ni watawala kama wakoloni.....
 
sasa mkuu ukarabati kwa ndege iliyokuja juzi tu ! Duh !


Ndege inakarabatiwa hata baada ya miaka miwili, ulikuwa hulijuwi hili? Na kukarabati haimaanishi kama ndege mbovu ila ni routine maintenance tu kama gari ama chombo chochote kile cha moto. Watanzania jamani acheni ujinga, kwanini hampendi kujisomea ili muondokane na ujinga wa kujitakia? Siku hizi elimu bure na rais kafanya hivi makusudi tu ili afute ujinga uliokithiri hapa nchini. Na ndiyo maana nimesema kwa makusudi tu kuwa Zitto na Lissu wanapenda sana watu wasiojitambua na kuwachezea akili.
 
Ukarabati == Service , chombo chochote lazima kifanyiwe service kubwa kila baada ya kipindi fulani.
Watanzania sasa kila kitu tunafanya siasa.


Wengi ni wajinga wa kujitakia, hawapendi hata kujisomea ili wajuwe ukweli.....wao kila kitu ni kukashifu na kukariri tu.
 
What the f&&$&& Tuliwaambia mkasema tunatumwa na mabeberu. Mtachunwa pesa ya migodi ya dhahabu kupitia upumbavu wetu


Someone has to resign ASAP
 
Ndege inakarabatiwa hata baada ya miaka miwili, ulikuwa hulijuwi hili? Na kukarabati haimaanishi kama ndege mbovu ila ni routine maintenance tu kama gari ama chombo chochote kile cha moto. Watanzania jamani acheni ujinga, kwanini hampendi kujisomea ili muondokane na ujinga wa kujitakia? Siku hizi elimu bure na rais kafanya hivi makusudi tu ili afute ujinga uliokithiri hapa nchini. Na ndiyo maana nimesema kwa makusudi tu kuwa Zitto na Lissu wanapenda sana watu wasiojitambua na kuwachezea akili.
Iwe inafanyiwa baada ya miezi miwili mwaka mmoja haijalishi. Mlisaini mkataba nao matengenezo yoyote Canada wazungu waliona wajinga ndio waliwao. Mkiwavuruga na madini watasubiri ndege iende kwa service halafu wataishikilia END OF THE MOVIE
Acheni kujipa moyo mmelikoroga
Muwe mnasikiliza
 
Kaka ATCL kabla ya kununuliwa hizi ndege sita mpya za Magufuli walikuwa na Bombardier mbili zenye namba za usajili 5H-MWG, na 5H- MWF, tofauti ya hizo ndege za zamani na hizi bombardier mpya za Magufuli ni model, hizi mpya ni Q400 na zina speed kubwa na capicity ya abiria ni kubwa kidogo kuliko zile Bombadier zetu za zamani ambazo model yake ni DHC8 (kwa sasa ni mbovu na zinahitaji kufanyiwa matengenezo)

"Bombadier mbili tulizozinunua tunatarajia kuzipeleka nchini Canada kwa ajili ya kufanyiwa 'service', na ndege moja itagharimu Dola za Marekani milioni tatu,” alisema Waziri Kamwelwe.

 
Canada wanahitaji wakimbizi 1m hebu wajazeni humu angalau tupate wataalamu huko wa baadae

Sent from my SM using Tapatalk
 
Kwenye gharama kuna cha juu cha wajanja wachache waliotengeneza dili la kwenda kukarabati Canada

Pata picha unaambiwa mratibu wa zoezi ilo ni mh kiongozi chenge lazima utumbo ukucheze🤣🤣🤣[emoji1063]


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kwanza gharama ya kusafiri mpaka Canada nayo ni kubwa sana na kila ndege ikiwa inaenda kukarabatiwa Canada ni vigumu shirika la ndege kukua kwa kasi na kuendelea

Nadhan ingeenda na trip moja na watu ili kufidia cost kdg ngoja chenge watawapanga ye c ndo mratibu mpango wa service


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom