Sh. Bilioni 13.9 kukarabati Bombardier nchini Canada

Sh. Bilioni 13.9 kukarabati Bombardier nchini Canada

Mkuu Kiswila ukitaka kusema uongo jitahidi kuuelewa hata wewe huo uongo. Fastjet anadiawa au ana deni la USD 200 milioni. Faida yake iko wapi? Pamoja na ukweli kuwa comments za hapa sio za kitaalamu bali siasa naona nichangie kidogo kuwapa mwanga maana ndege na biashara yake naijua, kidogo!. CEO wa ATCL kakwepa asubuhihii akiwa TBC1 kuhusu gharama aliyosema Waziri na kudai hilo ni swala la uendeshaji, kwa maana halisi, amejitenga na maneno na takwimu za Waziri. Hata hivyo katoa shule ambayo inauhalisia wa nini kinafanyika. Kasema sio matengenezo ya ubovu bali uchunguzi na matengenezo yaliyopangwa (scheduled maintenance au check C kwa kitaalamu) baada ya ndege kufikisha masaa 4,000 ya kuruka. Miaka miwili kwa ndege zinazofanya kazi kama inavyotakiwa ni muda tosha na huenda zikawa zimechelewa kufikisha masaa hayo kutokana na kutotumika sana. Ukichukua wastani wa masaa 12 ya kuruka kwa siku, ingewachukua ATCL mwaka mmoja tu kufikisha masaa 4,000. Kwa mwenye uelewa wa maswala ya ndege hili la masaa lina uhalisia ukiacha wapiga porojo wa JF ambao hutafuta ncha ya kushika na kuifanya issue hata kama ni butu. Tatizo lililopo, kwa uelewa nilionao, ni hiyo hesabu aliyotoa huyo Mh Waziri. Nafikiri ni siasa bila kujua madhara yake ili aonakane kasema na kuonyesha pesa ipo. Kwa uzoefu wangu Check C inaweza kufanyika hapa Tanzania na kama itabidi iende nje basi Addis Ababa ndio rahisi zaidi na siyo Canada kama huyu Mheshimiwa anavyojitapa. Hajui hata gharama za hayo matengenezo zinatokana na nini. Kuipeleka ndege Canada ni kuongeza gharama zisizo za lazima maana utahitajika kulipia mafuta, vibali vya kuruka katika anga ya nchi unazopita na kutua, na gharama ya crew (marubani na mafundi). Kama ndege zitafanyiwa matengenezo hapa Tanzania, nina hakika kwa ndege moja haitazidi USD 135,000 karibu shilingi 300,000,000. Magufuli bado yuko sahihi kununua ndege aangalie tu nidhamu ya utendaji hasa ya wanasiasa nje ya ATCL ambao watatafuta kiki kwa kujifanya wanajua kumbe wanaharibu! Wawaachie ATCL ambao wameonyesha uwezo mkubwa wafanyekazi yao bila wkuingiliwa na wanasiasa.

Ndege zinaendeshwa kwa Ruzuku kila mwaka Fastjet kila mwaka walikua wakitengeza faida na bei zao ziko chini sana zinashindana na mabasi ATCL, pamoja na kubaki wenyewe, Fastjet kunyimwa vibali nakubaki wenyewe bado wanaomba Ruzuku Serekalini Watanzania tusikubali kufuka jini ATCL ni jini,Watu wanaziogopa kuzipanda Kitwanga ali hoji ubora wa hizo ndege wakampuuza na kumuita mlevi akiwa wazi na mwana ccm, #2020 Lissu # tuzipige mnada zote tujenge shule na miundombinu mbali mbali nchini
 
hIzi ndege zitapunguza kura nyingi sana kwa bwana mtukufu hapo 2020.
kwani kwa mpinzani wake akitoa ahadi ya kuziuza na Kujenga zahanati na shule lazima achukue point
Hiyo shughuli ya kujenga zahanati inafanywa na mtu mmoja anaitwa Jaffo, anazijenga huko mikoani kila kukicha.
 
Mara hii speedometer zimeshasoma? Ila kama umenunua chombo mpya,mtengenezaji angetufanyia bure gharama za ukarabati.Je tumepata faida kiasi gani kusudi tutoe gharama za ukarabati? Nisaidieni wenye vikikokotoo
 
Mbona juzi tu tulikuwa tunashangilia kuwa tumerudishiwa senti kadhaa na hao Waliotuuzia Ndege, sasa tena leo tunarudisha mabilioni huko huko.

Sielewi, labda kwa sababu mimi ni Mwananchi wa kawaida.
 
Ndege
Hata kama tusipotoboa wee Ndege zetu zinakuhusu nini? Ndege tununue sisi usingizi ukose wewe wapi na wapi? Unaacha kukosa usingizi na Mbowe ananyea debe miezi sasa unakuja kukosa usingizi na ndege zetu?
Ndege ni za Serikali/ATC sasa za kwako na akina nani? labda uwe Abiria utashukuru kwa kuletewa usafiri kupitia Kodi zetu..
 
Mbona juzi tu tulikuwa tunashangilia kuwa tumerudishiwa senti kadhaa na hao Waliotuuzia Ndege, sasa tena leo tunarudisha mabilioni huko huko.

Sielewi, labda kwa sababu mimi ni Mwananchi wa kawaida.
Waliotuuzia au walioiuzia Serikali ndege?
 
Kama services za kawaida tu inamaana south Africa au Ethiopia hawawezi tengeneza kuna jamaa aliniambiaga hizo bombadia zinakwenda service kila baada ya masaa 400 mpaka 700 ni ila kama kuna upigaji vile

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha uongo,hiyo ni ile ndege ya pekee ambayo atcl walikuwa nayo kabla Serikali haijaanza kununua zingne.usiwe unaongea kitu bila kuchunguza

Sent using Jamii Forums mobile app

#HABARI Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Izack Kamwelwe amesema ndege mbili aina ya Bombardier Dash Q400 zilizonunuliwa mwaka 2016, zitapelekwa nchini Canada mwezi ujao kwa ajili ya kufanyiwa ukarabati, kwa gharama ya shilingi bilioni 13.860.
 
Kenya na Ethiopia wapo jirani ni kwa nini wasipeleke hapo? Tatizo la ATC ni wajanja wachache kujinufaisha kupitia visingizio kama hivyo
Siamini kama kuna mjanja ATCL wakutaka kujinufaisha kwa visingizio,ninachokiona hapo wanajitoa kwenye lawama,wameshajua ndege hizi zina hali gani na ni bora apelekewe mwenyewe mtengenezaji kuliko upeleke kwa wakenya au waethiopia halafu baada ya hapo litokee la kutokea waliotoa hilo wazo la kupeleka huko kwa bei nafuu wataliwa nyama.kwa maoni yao nimewaelewa ATCL,wamenawa mikono.
 
Hadi hapa nilivyofuatialia uzi huu,zaidi 85% ya wachangiaji hawajasoma content yote ya habari ya mleta uzi
Wanauliza maswali yaliomo Tena wazi kwenye habari hapo juu.....

Na hii inanyeosha Ni namna gani hata kwenye mada zingne humu jukwaani kwa Great Thinkers ambavyo watu huwa wanachangia "just by reading the thread title " kinachofata Ni kusifia/kusupport au kupinga/kutusi na kukashifu

Mkuu wengi tulichangia wakati mleta Mada bado hajaweka maelezo ya kutosha. Aliweka picha ya gazeti la nipashe tu. Haya maelezo mengine ameyaongeza baadae wakati wengine tuliisha changia tayari.

Tiba


Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu kilichomo ndani kimepakwa pakwa mafuta tu lakini ukweli ndio huo, tulichagua koroma.

hiyo gharama ya matengenezo imezidi income iliyotokana na ndege hizo, hata hivyo bado ni mapema mno.
Ipo kazi
 
swali tu.la kijiuliza itafikaje huko garage Canada.maana kama ni.mbovu haziwezi safiri safari ndefu zinahitaji kuvutwa na Breakdown
 
Ni ile ndege mpya iliyonunuliwa hivi karibuni na kupokelewa kifalmeView attachment 993742

14JAN 2019

Bombardier kukarabatiwa 
Canada kwa bilioni 13.9/-

SERIKALI imesema ndege mbili aina ya Bombardier Dash Q400 zilizonunuliwa mwaka 2016, zitapelekwa kufanyiwa ukarabati Canada mwezi ujao.
Imesema ukarabati huo unatarajiwa kugharimu Dola za Marekani milioni sita (Sh. bilioni 13.860).


WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO, ISACK KAMWELWE, PICHA MTANDAO
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe, aliyasema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, wakati wa uzinduzi wa kozi ya wahudumu ndani ya ndege katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT).
Ndege hizo zilinunuliwa na serikali zikiwa na uwezo wa kubeba abiria 76 kila moja na zimekuwa msaada mkubwa kwa wananchi wanaozitumia kwa safari za ndani ya nchi.


“Bombadier mbili tulizozinunua tunatarajia kuzipeleka nchini Canada kwa ajili ya kufanyiwa 'service', na ndege moja itagharimu Dola za Marekani milioni tatu,” alisema Waziri Kamwelwe.


Waziri huyo alisema kuwa, baada ya kuletewa taarifa hiyo, alilazimika kumfuata Rais John Magufuli na kumshauri serikali ianze kufanya ukarabati kwa hanga lililopo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ili kupunguza gharama kubwa ambazo nchi inaingia katika kuzikarabati ndege.


Alisema katika kulitekeleza hilo, serikali imeshaanza kuchukua hatua kwa kuanza kukarabati hanga hilo kwa kuweka taa na kwamba serikali imeshaingia mikataba mitatu, mmojawapo utakuwa wa kununua vifaa vya matengenezo.
Alisema Rais Magufuli ameshakubali kutoa pesa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vitakavyotumika katika hanga hilo.


“Kwa hiyo, ndugu zangu tutaanza kukarabati ndege sisi wenyewe, nimeamua kusimamia 'industry' inadumu na hakuna kurudi nyuma,” alisema Waziri Kamwelwe.


Kuhusu mafunzo ya uhudumu ndani ya ndege yaliyoanzishwa na NIT, Waziri Kamwelwe, alisema yatasaidia kupata Watanzania wakaohudumia ndege zilizonunuliwa na serikali.




Aliutaka uongozi wa NIT kuhakikisha mafunzo ya kozi hiyo yanakidhi viwango vya kimataifa.
Mkuu wa NIT, Prof. Zacharia Mganilwa, alisema idadi ya wahandisi wa ndege nchini inaendelea kushuka, akibainisha kuwa mwaka 2012 kulikuwa na wahandisi 172, mwaka 2016 walikuwa 74, huku asilimia 69 kati yao, wakiwa ni raia wa kigeni.


Prof. Mganiliwa pia alisema zaidi ya asilimia 70 ya matengenezo ya ndege yanafanyika nje ya nchi.
“Tulikuwa na upungufu wa marubani kwa asilimia 60, mwaka 2017, idadi yao ilikuwa 743 kati ya hao 317 walikuwa ni wazawa na 425 ni raia wa kigeni,” alisema Prof. Mganilwa.


Alisema idadi ya wahudumu wa ndege waliosajiliwa nchini imekuwa ikiongezeka tangu serikali ilipoanza kununua ndege.
Alisema mwaka 2013/14, idadi yao ilikuwa 43, mwaka 2014/15 walikuwa 42, mwaka 2015/16 walikuwa 50, mwaka 2016/17 walikuwa 96, mwaka 2017/18 walikuwa 143 na mwaka 2019 waliopo katika mafunzo ni 61.


Alisema kuwa mwaka 2015, NIT ilianzisha shule kuu ya usafiri wa anga ikiwa na idara mbili ya uhandisi wa ndege na wahudumu wa ndege.


Alisema NIT ilipewa ithibati ya kutoa mafunzo ya uhudumu ndani ya ndege Aprili 25, mwaka jana na ithibati ya utengenezaji wa ndege na urubani bado hawajapewa. Alisema kuwa kwa sasa wapo katika hatua ya nne ya kukamilisha matakwa ya kupewa ithibati hiyo.

range inatoka mkoa kufanya service dar na wakati mkoa wanaweza kuweka service.shikamoo tanzania
 
Ni ile ndege mpya iliyonunuliwa hivi karibuni na kupokelewa kifalmeView attachment 993742

14JAN 2019

Bombardier kukarabatiwa 
Canada kwa bilioni 13.9/-

SERIKALI imesema ndege mbili aina ya Bombardier Dash Q400 zilizonunuliwa mwaka 2016, zitapelekwa kufanyiwa ukarabati Canada mwezi ujao.
Imesema ukarabati huo unatarajiwa kugharimu Dola za Marekani milioni sita (Sh. bilioni 13.860).


WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO, ISACK KAMWELWE, PICHA MTANDAO
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe, aliyasema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, wakati wa uzinduzi wa kozi ya wahudumu ndani ya ndege katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT).
Ndege hizo zilinunuliwa na serikali zikiwa na uwezo wa kubeba abiria 76 kila moja na zimekuwa msaada mkubwa kwa wananchi wanaozitumia kwa safari za ndani ya nchi.


“Bombadier mbili tulizozinunua tunatarajia kuzipeleka nchini Canada kwa ajili ya kufanyiwa 'service', na ndege moja itagharimu Dola za Marekani milioni tatu,” alisema Waziri Kamwelwe.


Waziri huyo alisema kuwa, baada ya kuletewa taarifa hiyo, alilazimika kumfuata Rais John Magufuli na kumshauri serikali ianze kufanya ukarabati kwa hanga lililopo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ili kupunguza gharama kubwa ambazo nchi inaingia katika kuzikarabati ndege.


Alisema katika kulitekeleza hilo, serikali imeshaanza kuchukua hatua kwa kuanza kukarabati hanga hilo kwa kuweka taa na kwamba serikali imeshaingia mikataba mitatu, mmojawapo utakuwa wa kununua vifaa vya matengenezo.
Alisema Rais Magufuli ameshakubali kutoa pesa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vitakavyotumika katika hanga hilo.


“Kwa hiyo, ndugu zangu tutaanza kukarabati ndege sisi wenyewe, nimeamua kusimamia 'industry' inadumu na hakuna kurudi nyuma,” alisema Waziri Kamwelwe.


Kuhusu mafunzo ya uhudumu ndani ya ndege yaliyoanzishwa na NIT, Waziri Kamwelwe, alisema yatasaidia kupata Watanzania wakaohudumia ndege zilizonunuliwa na serikali.




Aliutaka uongozi wa NIT kuhakikisha mafunzo ya kozi hiyo yanakidhi viwango vya kimataifa.
Mkuu wa NIT, Prof. Zacharia Mganilwa, alisema idadi ya wahandisi wa ndege nchini inaendelea kushuka, akibainisha kuwa mwaka 2012 kulikuwa na wahandisi 172, mwaka 2016 walikuwa 74, huku asilimia 69 kati yao, wakiwa ni raia wa kigeni.


Prof. Mganiliwa pia alisema zaidi ya asilimia 70 ya matengenezo ya ndege yanafanyika nje ya nchi.
“Tulikuwa na upungufu wa marubani kwa asilimia 60, mwaka 2017, idadi yao ilikuwa 743 kati ya hao 317 walikuwa ni wazawa na 425 ni raia wa kigeni,” alisema Prof. Mganilwa.


Alisema idadi ya wahudumu wa ndege waliosajiliwa nchini imekuwa ikiongezeka tangu serikali ilipoanza kununua ndege.
Alisema mwaka 2013/14, idadi yao ilikuwa 43, mwaka 2014/15 walikuwa 42, mwaka 2015/16 walikuwa 50, mwaka 2016/17 walikuwa 96, mwaka 2017/18 walikuwa 143 na mwaka 2019 waliopo katika mafunzo ni 61.


Alisema kuwa mwaka 2015, NIT ilianzisha shule kuu ya usafiri wa anga ikiwa na idara mbili ya uhandisi wa ndege na wahudumu wa ndege.


Alisema NIT ilipewa ithibati ya kutoa mafunzo ya uhudumu ndani ya ndege Aprili 25, mwaka jana na ithibati ya utengenezaji wa ndege na urubani bado hawajapewa. Alisema kuwa kwa sasa wapo katika hatua ya nne ya kukamilisha matakwa ya kupewa ithibati hiyo.
Hakuna cha ajabu hapo,

Hio haina tofauti na scheduled maintenance ya gari kwa authorised dealership. Kwa kutegemea aina ya gari kawaida ilifika kilometa kadhaa (kwa mfano 15,000 au miezi 12) ni lazima gari ipelekwe garage wakafanye checkup, na kubadili filters, oil etc...

Sasa kwa ndege ambazo zilinunuliwa 2016 tayari hayo masaa ya kuruka yameshafika hakuna ujanjaujanja hapo ni lazima ziende kufanyiwa checkup makini sio gereji bubu....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba, kwa niaba ya wazalendo wenzangu wa Isansa Mbozi nitoe ufafanuzi kuhusu na kilichoandikwa na gazeti la *NIPASHE* la leo tarehe 14 January 2019, kwenye kichwa cha habari _"Bil 13.9 kukarabati Bombadier Canada"_

Ni kwamba tarehe 10 mwezi huu, mh waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano *Mhandidi Isack Kamwele* , alialikwa kama mgeni rasmi katika chuo cha usafirishaji( NIT) katika uzinduzi wa kozi ya wahudumu ndani ya ndege

Katika hotuba yake, alieleza changamoto katika sekta hii ya usafiri wa anga hapa nchini, mojawapo ya changamoto aliosema, ni ukosefu wa karakana( Hanga) za kukarabati ndege zenye ubora na ukubwa wa kutosha hapa nchini

Hivyo akasema kwa mfano mwakani wanapaswa kupeleka ndege zetu 2 za bombadier kwa ajili ya kuzifanyia service( Schedule service), kwa kawaida kila ndege ina muda wake maalumu wa kufanyiwa service kutokana na flying hours, ambapo kwa bombadier Q 400 hufanyiwa service kila baada ya masaa( Flying hours) 600 ya kuwa angani

Na akasema, kama watapeleka ndege hizo nchini Canada kwa ajili ya service itawagharimu serikali takribani $ 3m kwa ndege moja na $ 6m kwa ndege zote mbili

Lakini akasema, baada ya kuambiwa hilo, alimfuata mh Rais na kumuomba apewe fedha kwa ajili ya ukarabati wa hanga yetu, iliyopo katika uwanja wa kimataifa wa Kilimanjaro( KIA) ambapo kimsingi ombi lake lilikubaliwa na mh Rais, na serikali wameshaanza ukarabati mkubwa katika hanga hiyo na pia wameshaingia mikataba 3, ikiwemo ya kununua vifaa vya kisasa kwa ajili ya ukarabati wa ndege zetu

Na yote hii, inafanyika ili tuweze kuokoa fedha nyingi za kupeleka ndege Canada kwa ajili ya service

Binafsi kama mzalendo nitoe wito, hasa kwa vyombo vya hsbari kama magazeti, kujiepusha kuwa na vichwa vya habari vyenye kuweza kupotosha umma,

Nadhani kwa hili la NIPASHE, nina imani mamlaka husika zitachukua hatua stahiki juu ya jambo hilo

Mzalendo
_Ngamanya Kitangalala_
Kwa hiyo kwa mujibu wa aya ya nne kwenye hii post yako ndege zitakuwa zimefikisha 600 flight hours na kupelekwa service mwaka ujao 2020 na siyo mwezi ujao (February, 2019) kama ilivyoripotiwa gazetini?
 
Back
Top Bottom